Tag Archives: Games

Magame mazuri na rahisi kwa kila mtu unayoweza kucheza kwenye simu (Android)

Katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia, simu za mkononi zimekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunazitumia kwa mawasiliano, kuperuzi mitandao ya kijamii, na kwa burudani. Moja ya njia maarufu zaidi za kuburudika kwenye simu zetu ni kucheza magame mbalimbali. Magame kwa wengi ni njia ya kupumzika, kujifurahisha, na hata kujifunza mambo mapya maana kuna game zinazofunsha pia.

Ingawa kuna maelfu ya magame yanayopatikana kwenye internet, si magame yote yanakua yanaonekana mazuri kwa kila mtu. Kuna watu hawajajikita sana kwenye games na kama wakicheza game huwa wanapenda games zisizo na mambo mengi sana. Kwa bahati nzuri, kuna magame mazuri mengi rahisi ambayo yanaweza kuchezwa na watu wanamna hii, bila kujali umri au ujuzi wa teknolojia.

Magame ya mpira ya kucheza kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Katika makala hii, tutakuletea orodha ya magame mazuri na rahisi ambayo unaweza kucheza kwenye simu yako kama ni mtu wa namna hii. Kabla hatujaenda katika kuangalia games hizi, fahamu kuwa game zinaweza kusaidia kupunguza msongo wa mawazo na kuongeza furaha katika maisha yako ya kila siku.

Magame mazuri na rahisi kwa kila mtu unayoweza kucheza kwenye simu (Android)

Classic block falling

Hili game ni moja ya magame yenye muundo ambao baadhi watu husema ni “magame ya kupanga tofali”. Katika game hili unadondoshewa vitu kama tofali ambavyo huwa katika maumbo tofauti na utatakiwa kuyapanga vizuri. Unakua unapata score baada ya kufanikiwa kupanda vizuri tofari bila kuacha nafasi. Game kama hizi zipo nyingi na zinafahamika mno. Kucheza game la Classic block falling inaweza kuwa sio jambo gumu kulifanya kwa watu wengi.

Water color sort

Water color sort ni gemu lingine rahisi linaloweza kuchezwa na kila mtu. Kwenye game hili unapewa maji yenye rangi nyingi yaliowekwa kwenye chupa 2 au zaidi alafu utatakiwa kukusanya maji yenye rangi sawa na kuyaweka kwenye chupa zake. Water color sort linahitaji mchezaji atumie akili sana kabla ya kufanya maamuzi unapocheza. Kadri unavyoendelea kucheza na kushindwa ndivyo unaendelea kukutana na mafumbo yanayohitaji utumie akili zaidi. Ni game lisilo na mambo mengi kabisa na hufurahisha pia.

Bubble Shooter

Ukiwa umetulia na unahitaji game lisilo na mambo mengi kulicheza basi kumbuka kuna hili huitwa Bubble shooter. Hili game mchezaji unakua unatumia vimipira vyenye rangi kuvilenga vimipira vingine vinavyoning’inia juu. Ili kufanikiwa, unatakiwa kulenga vimipira vinavyo fanana rangi na ya mpira unaorengea. Yani kama umepewa mpira mwekundu wa kurengea basi utatakiwa kuulenga mpira wa rangi nyekundu pia.

Subway suffer

Subway suffer ni game maalufu sana ulimwenguni katika ulimwengu wa game ya simu za smartphone. Katika gemu hii, unacheza kama kijana anaekimbia ili kukwepa polisi anaemkimbiza baada ya kumkuta akichora maeneno ya treni. Unatakiwa kukimbia kwenye Barabara ya treni ili askari huyo asikukute. Katika kukimbia unakua unakutana na vitu mbalimbali unavyotakiwa kukwepa. Unakua unakimbia na kukwepa vitu kama ilivyo kwenye game kingine maalufu liitwalo Tempo run japo hayelekeani sana.

Racing in Car 2


Racing in Car 2 ni game la simu ambalo linakuweka kwenye ulimwengu wa kuendesha magari uwe kama Dereva. Game hili mchezaji anakua Dereva na anacheza kwa kuyumbisha simu ili kulielekeza gari upande wa kwenda pindi linapotembea barabarani. Katika barabara mchezaji anatakiwa kufanya vizuri kwa kupishana na magari mengine vizuri huku kuepuka ajali.

Huu ni mwisho wa orodha yetu lakini kuna game nyingine zaidi ya hizi tungeweza weka hapa. Lakini hatuwezi weka zote hivyo hizi zikikufaa, zijaribu na ufurahie.

Game zenye muonekano mzuri za Online battle Royale (simu)

Unatafuta magame mazuri ya kucheza? Hii ni moja ya makala usizotakiwa kukosa unapotaka magame ya kucheza kwenye simu. Kabla ya yote ningependa kukufahamisha hapa tunaenda kuangalia game nzuri zenye muonekano mzuri lakini game hizi ni game za Online battle loyale. Duniani kwasasa watu wengi hupenda kucheza game hizi kwa sasababu ni games zinazo jumuisha kushindana au kushirikiana na watu toka sehemu mbalimbali ulimwenguni.


Magame ya muundo huu husaidia watu kufahamiana au kupata marafiki. Kuna game za battle royal ukizicheza kwa muda wa saa moja unaweza kuwa umekutana na watu zaidi ya ishirini toka sehemu mbali za Dunia. Watu hao unaokutanana nao wanaweza kuwa marafiki zako japo haushauriwi sana kujenga urafiki na watu usio wajua tabia zao. Kuna watu huwa na tabia mbaya ambazo zinaweza kuwa ni wizi au utapeli mtandaoni, hivyo unatakiwa kuwa makini na watu unaokutana nao kwenye online games.

Game za mpira za kucheza kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Magame mazuri ya Battle Royale ya kucheza kwenye simu (Android na iOS)

Call of duty Warzone Mobile

Warzone Mobile ni moja games maarufu katika upande wa games za “Battle royale”. Game hili ni game la kivita ambalo ni FPS, yaani ni first person shooter ambalo lipo chini ya Activation kama games nyingine za Call of duty. Call of Duty: Warzone, ulioundwa kwa ajili ya vifaa vya simu na kutolewa mwaka 2024. Kabla ya hapo lilikua lipo lakini halikutolewa kwaajili ya simu.
Kwenye battle royal ya call of duty warzone Mobile mtu kwanza unafurahia graphics au muonekano mzuri. Mbali na Hilo Kuna mode zaidi ya moja unazoweza kuzifurahia.

Mambo ya kujua kuhusu game la Call of Duty warzone mobile BONYEZA HAPA>>>

PUBG mobile

PUBG mobile ni game lingine zuri katika upande wa battle royal. PUBG ni Third person shooter na vile vile ni First-Person Shooter. Ukitaka muonekano mzuri PUBG mobile ni chaguo sahihi lakini utatakiwa kujua kuwa Kuna “PUBG lite” ambayo hua ni game la PUBG lililopunguzwa ubora kwaajili ya simu zenye uwezo mdogo na kupunguza matumizi ya data. Ukitaka kufurahia ubora wa game la PUBG kwa asilimia 100, tumia PUBG mobile na sio PUBG lite.

Call of duty Mobile

Call of duty Mobile ni game lingine la Call of Duty lililoundwa kwaajili ya simu. Game hili lilikuepo kabla ya game la “Call of Duty warzone Mobile” halijatolewa kwaajili ya simu. Linawachezaji wengi na kitu kizuri ni kwamba linaweza chezwa kwenye simu zenye uwezo mdogo kidogo ukilinganisha ya Call of Duty warzone. Muonekano wake upo vizuri na katika modes lina mpaka mode ya zombies unayoweza furahia kucheza na marafiki.

Fortnite

Fortnite Mobile ni toleo la game maarufu la ” Fortnite battle royale” lililoundwa na Epic Games kwajili ya watu wanaotumia simu kucheza games. Game hili lilipititia matatizo ambayo huenda yangefanya game hili liwe limesahulika kwasasa lakini kutokana na ubora na kuwa game zuri mpaka Leo hawazisahau. Tatizo ambalo game la Fortnite battle royal mobile lilipitia ni kuondolewa kwenye platform kubwa ya Playstore. Jambo hili lilileta ugumu kwenye upatikanaji wa game hili kwenye simu.

Jinsi ya kucheza game la Fortnite kwenye simu bila kudownload BONYEZA HAPA>>>

Free Fire


Free Fire ni game la simu la aina ya “battle royale” lililotengenezwa na Garena. Katika game hili, wachezaji wanarushwa kwenye kisiwa ambapo wanapaswa kupambana na wachezaji wengine hadi awepo mshindi atakae simama hai. Hii ni kama battle royal za game nyingine ila lina mazuri yake tofauti. Free Fire ni game maalufu ulimwenguni na hukubali kuchezwa kwenye simu zenye uwezo mdogo kidogo ukilinganisha na baadhi ya game nyingine kubwa za battle royal.

Huo ndio mwisho wa orodha yetu katika ukurasa huu. Kama imekua msaada kwako, unaweza wajuza na rafiki zako juu game hizi. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Game nzuri za PSP za kucheza kwenye Simu na PC

Kampuni ya Sony ni kampuni kubwa sana katika upande wa games kutokana na sababu nyingi ikiwemo kuleta vifaa vya games vyenye mafanikio makubwa ulimwenguni. Katika Miaka ya nyuma Sony ilitengeneza kifaa kidogo cha mkononi kiitwacho PSP (PlayStation Portable) kama moja ya vifaa vya games ambacho kinamuwezesha mtu kucheza games popote kama vile inavyotumika simu siku hizi. Hii PSP ilitolewa rasmi na Sony mwaka 2005 na ilikua ni bidhaa iliopokelewa vizuri sana na watu.

Kulikua kuna magemu/gemes kama 1900 hivi na zaidi ambayo mtu ukinunua PSP, unaweza kuyacheza. Lakini Baada ya muda Sony walitangaza kusitisha projekti yao ya PSP. Baada ya Sony kufanya hivyo Games za PSP na vifaa vya PSP vikaacha kuzalishwa mpaka leo. Lakini kutokana na ubora wa vifaa vya PSP na game zake kwa kipindi kile, watu mpaka sasa hawajaisahau PSP. Kuna watu mpaka sasa wana vifaa vya PSP, wengine wanaiga kutengeneza vifaa vya PSP na wengine wametafuta njia ya kuyacheza magemu ya PSP kwenye PC na Simu.

Ukitaka kucheza magame ya PSP kwenye simu au PC, utahitajika kutumia app au software ziitwazo Emulators. Moja ya Emulators za magame ya psp zinazotumika sana inaitwa “PPSPPP PSP Emulator“. Hii inafanya mpaka baadhi ya watu kuyafahamu magame ya PSP kama “Magame ya PPSPP”.

Magame ya mpira ya kucheza kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Game nzuri za psp za kucheza kwenye simu au PC

GTA Liberty City Stories

GTA Liberty City Stories psp

Liberty City Stories ni sehemu ya mfululizo maarufu wa magame ya Grand Theft Auto ambayo yapo chini ya Rockstar. Game hili katika upande wa PSP, ni kati ya game zuri sana kucheza katika PC na Simu pia. Unapo cheza game hili unacheza kama jamaa mmoja muhuni au muhalifu aitwae Toni Cipriani, ambaye anarudi mjini baada ya kukaa mbali kwa muda. Unaingia katika ulimwengu wa uhalifu wa Liberty City na kupambana kuwa juu katika mji huo.

God of War chain of Olympus

God of War chain of Olympus PSP

Game hili pia ni mfululizo wa magame ya God of War ambayo ni maarufu pia kwenye ulimwengu wa games. Humu unacheza kama Kratos ukipigana na miungu pamoja kutatua changamoto mbali kwa mtiririko wa simulizi ya God of War. Liliundwa SCE Santa Monica Studio na kuchapishwa na Sony Computer Entertainment kwaajili ya vifaa vya PSP. Ni game la PSP zuri kulicheza mpaka sasa.

Assassin’s Creed bloodlines

Assassin’s Creed bloodlines

Assassin’s Creed: Bloodlines katika psp ni game ambalo ambao lilitoka mwaka 2009. Magemu ya Assassin’s Creed yapo mengi katika ulimwengu wa games na hili ni moja kati ya hayo. Katika Assassin’s Creed bloodlines hili unacheza kama mtu aitwae Altair Ibn-La’Ahad. Huyo ni muhusika mkuu katika game na yupo katika miji ya Kilatini wakati wa karne ya 12(Zamani). Game la Assassin’s Creed bloodlines bado linaweza kuwa chaguo zuri mpaka sasa unahitaji kucheza game za psp maana sina stori nzuri na muonekano mzuri pia.

NFS most wanted

Need For Speed Most wanted

Ukiwa unapenda magame ya magari na unataka kufurahia game hizi upande wa PSP, game NFS most wanted linaweza kuwa zuri kwako. Game hili linaitwa “Need For Speed Most” wanted lakini unaweza liita “NFS most wanted” kwa ufupi. Need For Speed ni moja majina makubwa kwenye video games na hili game tunaloliongelea hapa, lina jina hili Kwasababu ni sehemu ya game za Need For Speed. Lilichapishwa na Electronic Arts Katika PSP na unaweza furahia mpaka sasa maana bado lipo vizuri.

Spider man 3

Spider man 3 PSP

Hili game la Spider man 3 la PSP la Spider-Man 3 ni sehemu ya mfululizo wa magame ya Spider-Man. Kuna magemu mengi ya spider man na hili ni moja ya magemu hayo lilichapichwa kwaajili ya PSP ambalo linafurahisha mpaka sasa. Humu ndani ukiwa kama spider man utapambana na maadui kama Sandman, Venom, na New Goblin.

Hapo juu tumeweka games chache TU lakini games za psp zipo nyingi sana nzuri mbali na hizo. Lakini unapaswa kujua games za psp zilisimama kutolewa hivyo hakuna games mpya za psp ambazo ni rasmi. Ila u aweza kutana na game za zamani za psp zilizo boreshwa lakini sio rasmi. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo kuhusu games na mengine.

Jinsi ya kucheza game la Call of Duty Mobile bila kudownload kwenye Simu

Call of Duty mobile ni moja ya zile games hupendwa na watu ambao hupendelea magame ya kupambania ufalme wa vita. Game hili ni game maalufu kutoka Activision na lilitengenezwa na TiMi Studio Group kwaajili ya simu.

Watu wanaolipenda gemu hili ulimwenguni ni wengi na baadhi yao huwa wanatamani kujua jinsi ya kulicheza kwenye simu bila kudownload. Hii ni kutokana na game hili kuwa kubwa au kuhitaji simu zenye uwezo kuliko simu zao. Hapa The bestgalaxy tunaweka wazi moja ya njia mtu anaweza cheza game hili bila kudownload. Kama unahitaji kujua hili, basi tuwe pamoja hapa chini.

Jinsi ya kucheza game la Call of duty mobile bila kudownload

Now.gg ni moja huduma za cloud gaming zinazokuwezesha mtu kucheza magame mtandaoni bila kudownload au kuyapakua. Mbali na magame, pia kua app nyingine unaweza tumia kupitia huduma hii bila kudownload kwenye simu yako. Huduma hii kwasasa ndani yake Ina app ya Aptoide ambayo ukifungua utakutana na magemu mengi ikiwemo Call of duty mobile na utaweza kulicheza bila kudownload.
Unataka kujaribu? Sawa, fuata hatua zifuatazo kucheza hili la Call of duty mobile ili kulipakua kwenye simu.

  • Unanginisha vpn katika saver ya USA kama upo nje ya USA.
  • Ingia google na utafute “Call of duty mobile now gg” alafu chagua matokeo ya juu kutoka Now.gg
  • Baada ya hapo utaletewa ukurasa unaoionesha app ya Aptoide, bonyeza kitufe kilichoandikwa “Play in browser” ilicho chini ya Aptoide katika ukurasa huo.
  • Baada ya hapo utapelekwa katika ukurasa wa Aptoide na utatakiwa kutumia sehemu ya kutafuta kulitafuta game la “call of duty mobile” (Yani utaandika “call of duty mobile” kwenye kisehemu cha kutafuta cha Aptoide.
  • Ukishalipata, lichague kisha utabonyeza “INSTALL” na kuacha kwa muda mpaka utakapoona batani ya “OPEN” kwenye game hilo.
  • Ikisha tokea batani ya “OPEN” utalibonyeza ili kulifungua gemu na kuanza taratibu nyingine za ndani ya gemu pamoja na kulicheza.

Mwisho, unapotaka kucheza bila matatizo, hakikisha unazingatia muunganiko wako wa mtandao/internet. Inatakiwa uwe na mtandao wenye kasi na usio yumba maana huduma za cloud gaming huwa zinategemea internet zaidi.

Total Football: Fahamu kuhusu Game hili la mpira

Total football ni game la mpira ambalo unaweza cheza kwenye simu ya mkononi. Ni game la mpira wa miguu kama lilivyo game la eSports football, FIFA mobile (EA SPORTS FC) au Dream League soccer.


Game la Total football limetengenezwa na GALA Sports kisha kutolewa na Studio Vegas private Limited pamoja na GALA Sports pia. Limetolewa katika platform mbili tu kwasasa ambazo ni Android na iOS. Hiyo kwasasa watu wanaweza cheza kwenye simu za Android or iOS(iPhone). Ni game la Bure kabisa na lina mode zaidi ya moja unaweza furahia kucheza na kitu kizuri zaidi ni kwamba linaruhusu kucheza offline pamoja na online.


Yani ukiwa una data au bando unaweza cheza game hili online alafu ukiwa hauna data, unaweza cheza bila ya kuwa na muunganiko wa internet. Ukiachana na hayo, Total football lina muonekano au graphics nzuri japo linaeweza zidiwa na baadhi ya magemu mengine ya mpira, lakini bado lipo vizuri kimuonekano.

Linakuruhusu kuunda timu ya ndoto yako kutoka kwa machezaji zaidi ya 4000 ulimwenguni, kuitengenezea jezi na Logo kisha kuonesha jinsi gani timu yako ni Bora kwa kucheza na timu nyingine. Linakupeleka katika ulimwengu wa bosi halisi wa timu ya mpira wa mguu kama DSL na magemu mengine kama hilo.

Kudownload na kucheza game la Total football (Android)

Total football kabla ya kutolewa rasmi Kuna baadhi ya watu walikua wanacheza likiwa kwenye maboresho na lilikua likisubiriwa sana na watu litolewe rasimi. Katika kulitoa napo halikutoka katika nchi au maeneno yote. Baadhi ya nchi au maeneno, hauwezi kucheza game hili kirahisi maana bado halipo rasimi kwenye maneno hayo.


Kwa hizi pande zetu, ukiingia playstore kwenye game hili (Android) unaweza kuta ujumbe ulioandikwa “This item isn’t available in your country”. Ujumbe huu unamaana sehemu ulipo game hili halipatikani. Sijajua ni lini wanaweza fanya game hili kuwa rasimi katika pande za huku kwetu lakini nisieme tu kuwa ni muda wowote kwanzia sasa linaeweza patikana. Unaweza BONYEZA HAPA kuangalia muda huu katika playstore kama limeishaachiliwa rasimi lichezwe pande za huku kwetu au bado.

Kama Bado, basi jaribu kupakua au kudownload APK file yake nje ya playstore alafu install kwenye simu yako ya Android. Baada ya kuinstall kwenye simu yako, lifungue na uanze kulicheza. Ukitaka uianza safari ya Kudownload APK file ya game la Total football unaweza BONYEZA HAPA.

Call of Duty Warzone Mobile: Mambo ya kujua kuhusu game hili

Kuna muda Activision ilituacha na game moja tu zuri la Call of Duty ambalo tunaweza kulicheza kwenye simu. Game hilo linaitwa “Call of Duty mobile” na Activision walilitoa katika mwaka 2019. Katika mwaka wa 5 toka game hilo litoke na kuwa na mafanikio makubwa duniani, wakaamua kuongeza game lingine la Call of Duty iitwalo “Call of Duty warzone Mobile”. Game hili kilikua likisubiriwa na watu wengi sana maana lilikua linapatikana katika platform nyingine za game. Lilikua rasimu kwenye vifaa vingine vya games lakini halikua rasimi kwa simu/mobile. Activision walilitoa game hili rasimi tarehe 21 mwezi wa 3 mwaka 2024.

Call of Duty Warzone Mobile

Call of duty warzone Mobile ni First-person shooter game ambalo lina mode ya Battle Royale ambayo inawakusanya watu au wachezaji zaidi ya 120 katika eneo moja wapambane kubaki hai. Ni game la kivita la mtandaoni(online) unaloweza cheza kama timu au peke yako(solo). Kama ilivyo kwenye mechi za magame mengine ya Battle Royale, mshindi ni anaebaki hai peke yake au timu inayobaki hai pekee.

Sasa ukitaka kuona raha ya Mode hii, anza na kujiuliza kama unaweza kuwekwa sehemu moja na zaidi ya watu 120 wanaopambana alafu ukabaki mzima peke yako au na timu yako? Ukihisi unaweza, pakua na kujaribu katika game hili.

Kulipakua na kulicheza

Ili kulipakua/kudownload game la Call of Duty warzone Mobile kwenye simu yako ni lazima simu ikidhi vigezo. Simu inahitajika kuwa na GB 4 hadi 8 za RAM alafu pia Adreno 618 GPU au GPU nyenye uwezo zaidi ndio zanaweza kukuwezesha kulicheza. Hayo ni kwaajili ya simu za Android tu tena Android 13 na kuendelea.
Kwenye iOS huku, kifaa chako kinatakiwa kuwa na iOS 17.0 au zaidi na GB 3 za RAM.

Simu yako ikiwa na uwezo huo ndio utaweza kulipakua gemu la Call of Duty warzone Mobile na kulicheza. Linapatikana katika Play store kwaajili ya mtu wa Android na pia inapatika kwenye Appstore kwa watu wa iOS. Lakini kabla ya yote unakiwa kujua kuwa game hili linaweza kuchukua kama GB 5 hivi katika nafasi ya simu yako. Kwaiyo hakikisha unanafasi ya kutosha na hata kwenye internet pia uko vizuri.

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy na usisahau kusoma na kujifunza vitu vingine vingi katika sehemu hii.

Kutatua tatizo la “CONNECTING TO ONLINE SERVICES” kwenye Warzone mobile BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG Mobile

PUBG Mobile ni Game linalokutupa katika eneo moja uwe kati ya wachezaji 100 wanao pambana kubaki hai katika eneo hilo. Gemu hili linachezwa na watu wengi sana hapa Duniani pamoja na kuzuiliwa kwenye baadhi ya nchi.


Mechi moja ya PUBG inaweza kuwa ngumu au nyepesi kwako maana unacheza na watu halisi unaoweza kutana nao alafu ukawazidi uwezo au wakakuzidi uwezo. Kiufupi ni ngumu sana kuwa mtu unaweza kumzidi kila unaekutana nae kwenye mechi ya gemu la PUBG. Kuna muda ukiwa kama mchezaji unaweza jikuta umefanya vibaya kwenye mechi na kutolewa kwenye mechi mapema.


Kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG ni jambo muhumu sana na hutoa points za uhakika. Hata usipokua na Eliminations nyingi, ukiishi kwa muda mrefu kwenye mechi utapewa points.
Kama umekua na changamoto ya kutoishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG, yafuatayo ni mambo yanayoweza kukufanya ukishi muda mrefu kwa urahisi kidogo.

Mambo ya kuzingatia kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG

Chukua Level three helmet

Unapotua na kukusanya vitu katika mechi ya PUBG, huwa ni ngumu kupata kitu unacho hitaji maana vitu huwa haviwi kwenye mpangilio unaoeleweka. Lakini kama utabahatika kupata “Level three helmet” usiiache. Level three helmet katika mechi ya PUBG hulinda zaidi kichwa chako pindi kinapo pigwa na maandui. Level three helmet inaweza kulinda kichwa chako hata ukipigwa na M24 ambayo watu huiogopa pindi inapo nguruma katika eneo.

Usitembee kwenye sehemu za wazi

Hata sehemu iwe inaonekana salama kiasi gani, hakikisha haupiti bila kuwaza utajificha wapi pindi utakapo sikia mtu kaanza kukushambulia. Ukiwa unapita sehemu ya uwazi katika gemu la PUBG ni rahisi mtu usiemuona kukuona wewe na kuanza kukushambulia. Hivyo ni vema ukawa na tabia ya kupita sehemu zisizo na uwazi ili usipoteze maisha mapema. Pendelea kupita sehemu zenye mawe makubwa, miti, majani marefu au nyumba ili kuishi mda mrefu katika mechi ya game la PUBG.

Usikimbilie Eliminations kuliko kulinda uhai wako

Kutafuta Eliminations kwenye game la PUBG mobile ni kitu kizuri tu. Ila kama utakua unacheza ukiwa na tamaa ya kupata Eliminations nyingi alafu unasahau swala la kujilinda mwenyewe, utakua haudumu sana kwenye mechi. Kabla ya kufuata mtu kushambulia, hakikisha upo kwenye upo kwenye usalama na unauhakika wa kumuweza. Kama unaona upo kwenye hali mbaya, kujificha au kukimbia inaweza kuwa uamuzi mzuri pia.

Kuwa makini unapofuata Airdrops

Airdrops zinaposhuka huwa watu wengi wanaangalia juu ili wajue zinapotua. Zikishatua tu, kuna watu wengi wanakua tayari wapo njiani kuzifuata. Sasa ukiwa mmoja kati ya watu wanaozikimbilia Airdrops hakikisha unakua makini maana watu wengi wanaenda sehemu unayoenda. Mukikutana, wanaweza kukuzidi au ukawazidili lakini sehemu za Airdrops bado huwa ni hatari maana watu wengi hushindwa.

Usitue sehemu zenye majina makubwa mara kwa mara.

Kuna sehemu Katika ramani za game la PUBG mobile huwa zinafahamika sana. Watu wengi huwa wanapenda kushuka katika sehemu hizi kiasi kwamba unaweza tua na kupoteza maisha ndani ya sekunde chache tu. Sasa ukitaka kuishi mda mrefu katika mechi ya gemu la PUBG, usiwe na tabia ya kutua katika maneno haya. Tua katika maneno ambayo watu wengi hawatui ili upate hata muda wa kujiweka sawa.

Mwisho; Game la PUBG mobile ni gemu linalohitaji ujipe muda wa kujifunza pia. Jipe muda wa kucheza Kila mara ili upate uzoefu wa kulicheza na huu uzoefu unaweza kukufanya uwe na wezo wa kuishi mda mrefu katika mechi. Asante sana na endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Jinsi ya kucheza game za Xbox kwenye simu

Kama ni mpenzi wa magemu ya Xbox na una magemu yako pendwa ya xbox ambayo hua unayacheza kwenye vifaa vya xbox basi leo napenda kukufahamisha kuwa kuna uwezekano wa kuyacheza magemu hayo kwenye simu yako. Na hapa The Bestgalaxy tunaenda kukueleza njia ya kucheza game za xbox kwenye simu.

Haijalishi ni Simu ya Android au iOS(iPhone), njia inayoenda kuelezwa hapa inaweza tumika kwenye  simu hiyo vizuri tu ila inajumuisha malipo ya huduma.

Jinsi ya kucheza game za Xbox kwenye simu

Unaweza cheza magemu ya Xbox kwenye simu yako kwakutumia huduma ya Xbox cloud gaming. Huduma hii ni huduma ya Xbox inayowezesha watu kucheza magemu ya xbox na yasio ya Xbox kwenye simu kwa kutumia internet. Unaweza kucheza magemu hayo kwenye huduma hiyo bila kudownload. Kupitia huduma hii tunaweza sema sio lazima kununua kifaa cha xbox ndio ucheza magemu ya Xbox maana unaweza yacheza kwenye sumu yako kwakutumia internet kupitia huduma hiyo ya xbox cloud gaming..

Kujiunga na huduma ya Xbox cloud gaming ni bure kabisa ila baada ya kujiunga utakua na uwezo wa kucheza bure game la Fortine tu. Ili kucheza magemu mengine itabidi ulipie moja vifurushi vyao ambayo kwa mfumo wao huitwa “Xbox Game pass”. Kivurushi hivi huanza kwa bei ya ofa ya dola 1 tu kwa siku 14 alafu baada ya siku hizo kuisha utaendelea na malipo yao ya kawaida ya vifurushi.

Fuata hatua zifuatazo kucheza game za Xbox kwenye simu kwa huduma ya xbox cloud gaming.

  • Fungua VPN kisha uunganishe server ya USA kama haupo usa kwa sasa.
  • Ingia Google kwa web browser.
  • Tafuta “Xbox game pass” kisha ingia kwenye matokeo ya juu toka xbox.com
  • Baada ya kufanya hivyo, utatua kwenye ukarasa unaokukaribisha kujiunga kwa kuchukua moja ya vifurushi vyao kwa bei ya ofa. Bonyeza kitufe kilichoandikwa “JOIN FOR $1” kuanza taratibu za kujiunga.
  • Kabla ya kuendelea utapelekwa kwenye ukurasa wa kuingia na akaunti ya Microsoft au kutengeneza mpaya(kama hauna utatengeneza mpya na kama unayo utaiweka)
  • Chagua kifurushi chako cha “Ultimate” alafu bonyeza “Next” kuendelea mpaka kwenye ukurasa wa malipo kwaajili ya kulipia.
  • Ukisha lipia tu, utakua na uwezo wa kucheza magemu ya Xbox kwenye simu ndani ya hiyo huduma yao bila kudownload. Utakua unatumia mtandao tu.

Unapocheza magemu kwa njia ya cloud, ni vema ukawa na mtandao uliotulia sana maana hicho ndio kitu kikubwa kwenye kucheza magemu kwa njia hii. Endapo mtandao utakua haujatulia, game pia litakua linasumbua unapolicheza. Asante kwa muda wako, endelea kuwa na The bestgalaxy kwa mambo mengine mazuri.

Jinsi ya kufikia Ace kirahisi kwenye PUBG

PUBG mobile ni game lenye jina kubwa katika ulimwengu wa magemu ya simu ya Battle Royale. Gemu hili huwakutanisha watu toka pande mbali mbali za dunia kama wachezaji wanao pambania ufalme wa vita.
Unapocheza game hili huwa unapata points ambazo zinakusaidia kuongezewa PUBG Ranks kwenye gemu hilo. PUBG Ranks zimepangwa Toka chini kwenda juu na kadri unavyoongezewa rank ndio unakutanishwa na watu wengine wenye uwezo mzuri kwenye gemu hilo. Ukishindwa kufanya vizuri katika mechi, unakatwa points na kushushwa Rank pia. Ace ni moja ya PUBG Ranks ambazo baadhi ya watu hukumbana na ugumu kidogo katika kuifikia.

Ikiwa upo hapa na unashindwa kufikia Ace katika gemu la PUBG, hapa chini Kuna mbinu chache ya kukusaidia kufikia Ace kirahisi.

Mbinu za kufikia Ace kirahisi kwenye PUBG

Ishi muda mrefu

Watu wengi huwa wanapocheza gemu la PUBG mobile huwa wanatafuta Eliminations nyingi. Ni jambo zuri lakini ukiwa na Eliminations nyingi katika mechi alafu haujaishi kwa muda mrefu, hauwezi pata points zitakazo kufanya upande Rank. Kudumu muda mrefu kwenye gemu ndio kitu cha msingi zaidi kwenye gemu na hukupa point nyingi za uhakika zitakazo kufikisha kwa haraka kwenye Ace. Usishambulie kuliko kujilinda. Jilinde usipoteze maisha kwenye game kwa kutua kwenye sehemu ambazo watu wengi hawatui, kuwa makini unapofuata airdrops na pia usisahau kuchagua siraha nzuri. Usiogope kuwa “lone wolf”.

Cheza mara nyingi

Kwakua mechi za PUBG huwa zinakupa points, basi ni vema kucheza mara nyingi maana kadri unavyocheza ndio unajizolea points zaidi ambazo zitakufanya ufikie Ace. Ukiachilia mbali Points, kucheza mara nyingi au mara kwa mara huongeza uzoefu ambao utakufanya ufanye vizuri kwenye mechi unazocheza.

Chukulia Ace ni kitu cha kawaida alafu zingatia points

Ace ni kawaida sana na kinachokufanya ufikie ni points. Sasa ni vema ukazingatia kupata point nyingi kwenye mechi zako na kuacha kuiogopa. Usichukulia kama ni kitu kikubwa sana, zingatia kwenye kuwa mchezaji mzuri kwenye mechi zako na kupata points nyingi alafu hizo points ndio zitaifikia Ace.

Mwisho; Fahamu kwamba kupata Ranks kubwa kwenye game la PUBG inaweza kuwa ni ngumu kwa baadhi ya watu kwasababu ya uzoefu. Ni vema kujipa muda wa kujifunza kutokana na makosa unayofanya kwenye gemu ili kupata uzoefu utakao kufanya mchezaji Bora.

Jinsi ya kucheza game la Fortnite online kwenye simu (bila kudownload)

Fortnite ni game lililotolewa na Epic Games katika  mwaka 2017. Epic games ni kampuni inayojihusisha na Games na imetengeneza magemu mengi tu, ikiwemo hili game linaloitwa Fortnite. Tangu game hili limetoka mpaka sasa kuna mamilioni ya watu wanalicheza na baadhi ya watu wanaotumia simu za Android ni miongoni mwa watu hao.

Hapa chini The bestgalaxy tunatoa maelezo juu ya jinsi ya kulicheza gemu kwenye simu za Android online bila kudownload. Game la Fortnite halipatikani katika Playstore hii ni baada ya kuondolewa kwa kutofuata sheria za Google Play store. Liliondolewa mwisho wa mwaka 2020 na game nyingi zikikiondelewa katika Playstore huwa zinakufa lakini Fortnite ni game ambalo lipo hai mpaka leo na unaweza cheza kwenye simu yako ya Android kwa kudownload nje ya Playstore na hata kujeza bila kudownlod pia.

Magemu ya mpira ya kucheza kwenye simu GUSA HAPA>>>

Jinsi ya kucheza game la Fortnite online kwenye simu (bila kudownload)

Kucheza gemu hili kwenye simu bila kulidownload ni rahisi tu japo utakitaji kuwa na internet yenye kasi, VPN pamoja na Accounti ya Microsoft. Kama hauna akaunti ya microsoft usihofu maana unaweza tengeneza  katika ya safari ya kulicheza gemu hili. Fuata hatua zifuatazo kucheza game la fortnite online kwenye simu bila kudownload.

  • Unganisha VPN na iwe kwenye server ya USA
  • Tumia web browser yako kuingia katika Xbox.com/play
  • Bonyeza kiduara cha upande wa kulia juu ya ukurasa wa kwanza wa Xbox.com/play
  • Bonyeza batani ya kijani ilioandikwa “SIGN IN” alafu jaza taharifa za akaunti ya Microsoft. Kama hauna akaunti utabonyeza neno “Create One” utakaloliona baada ya bonyeza hiyo batani ya kijani.
  • Baada ya kuweka sawa akaunti ya Microsoft utarudishwa kwenye ukurasa wa Xbox
  • Utatakiwa kutumia kisehemu ya tafuta cha ukurasa huo kutafuta game la “fortnite” alafu kuliona utalichagua na kubonyeza “Play” ili kuanza kulicheza.

Unapocheza gemu hili, hakikisha internet yako iko vizuri maana ikiwa iko vibaya unaweza kutofurahia kucheza gemu la fortnite kwa njia hii. Njia hii ya kucheza gemu huwa inaitwa “Cloud gaming” na huduma ya” Xbox cloud gaming” ndio inayotumika maana inaruhusu kucheza gemu hili bure.

Kama wewe ni mtu uliekua USA na upo kwenye sehemu ambayo game hili halikupi nafasi ya kucheza basi hizo hatua juu ukizifuata utaweza kucheza gemu lako pendwa ukiwa nje ya USA.