Category Archives: Uncategorized

Jinsi ya kutengeneza au kurekodi Nyimbo kwa kutumia Simu

Kutengeneza nyimbo kwa kutumia simu inawezekana? Ndio, inawezekana na nyimbo unayotengeneza kwa kutumia simu inaweza kuwa na mafanikio makubwa tu kama nyimbo za Studio rasmi. Kipindi cha nyuma, ukiwa kama msanii wa Muziki ilikua ni lazima uhusishe vyumba vya Studio rasmi vinavyomilikiwa na maproduser ili kufanya mazoezi ya nyimbo na kurekodi nyimbo zako. Lakini kwa sasa, hakuna ulazima sana wa kwenda huko kama hauna uwezo. Unaweza tumia simu yako ya mkononi kufanya mazoezi ya kurekodi nyimbo zako na hata kurekodi kabisa ukiwa nyumbani tu.

Jinsi ya kutengeneza au kurekodi nyimbo kwa kutumia simu

Unaweza tengeneza au kurekodi nyimbo iliokamilika kwenye simu ila utatakiwa kuwa na app maalumu kwa kazi hiyo. App zipo nyingi na kati ya app hizo kuna app ngumu kutumia, pia kuna app rahisi kidogo zisizo hitaji mambo mengi kwenye kuzitumia. Moja ya app ambazo ni rahisi kutumia ni app iitwayo “Voloco”. Inapatikana katika Playstore kwa simu za Android na hata Appstore kwaajili ya watu wa iPhone au vifaa vya iOS kwa ujumla.

App ya Voloco inahusiana zaidi na kuweka Voco kwenye Beat. Unaweza ingiza Beat lako mwenyewe au ukadownload humo humo ndani Beat zilizotengenezwa na watu wengine. Ni ngumu kukuelezea kila kipengele cha app hii kwa maandishi ili uweze kuitumia ila tumejaribu kukuelezea hapa chini kwa msaada wa picha vitu vya muhimu kuvijua utakapo fungua app hii.

Kutengeneza nyimbo ni project na kwenye app hii kitu cha kwanza utakachotakiwa kukifanya ni kutengeneza au kufungua project mpya. Ukisha fungua project mpya unaweza weka Beat unalotaka kuliimbia kwenye project hiyo alafu ukaanza kurekodi sauti au voco zako. Uzuri ni kwamba Ina Autotune hivyo kunajinsi sauti au voco zako zinaboreshwa.

Unashauriwa kuvaa Earphone unaporekodi voco zako. Baada ya kumaliza kila kitu kwenye project hiyo, unaweza itunza project yako kwenye app hiyo.


Ukihitaji kuitoka kama audio za kawaida unaweza ingia kwenye project ulizo tunza alafu ukabonyeza vidoti vitatu vilivyo kwenye project yoyote unayoyahitaji alafu ukaugusa “Download” ili kuidownload nyimbo uliotengeneza iwe kwenye simu yako. Utakua na chaguo la kutunza iyo nyimbo kama Audio au video. Nyimbo yoko itakua tayari lkuisikiliza japo unaweza pia kuipitisha kwenye software nyingine ili kuiweka kwenye ubora zaidi au kuibadilisha kuwa mp3 kama utahitaji.

Ujumbe wa siku ya kuzaliwa kwa Mpenzi au Rafiki

Moja ya siku au tarehe ambazo watu wanaweza ya ona zina umuhimu sana kuzijua kwenye maisha yao ni siku ya kuzaliwa. Na ni kweli zina umuhimu maana katika mambo mengi huwa watu wanahitajika kutaja siku au tarehe ya kuzaliwa. Mara nyingi hii inaweza kuwa ni kwaajili ya kudhibitisha umri maana mtu anaweza kujua umri wako kwa kujua siku uliozaliwa(tarehe,mwezi au mwaka). Umri wa mtu ni tofauti kati ya siku mtu aliozaliwa na siku aliopo.
Katika jamii zetu siku ya kuzaliwa imewekwa mbele sana kwa baadhi ya watu kiasi kwamba inakua inakumbukwa kila mwaka na kusherehekewa. Sio jambo la ajabu na sio jambo la lazima pia.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>

Kama unampenzi au rafiki anaejali siku yake ya kuzaliwa, unaweza mfanyia jambo lolote la furaha katika siku yake ya kuzaliwa na akafurahi. Na inasemekana hata ambao hawazisherehekei na kuzijali siku zao za kuzaliwa, wanajiskia vizuri sana wakifanyiwa jambo lolote la furaha kuhusu siku yao hiyo. Hivyo ukiwa na rafiki au mpenzi hata ambae hajali kuhusu siku yake ya kuzaliwa, unaweza mfurahisha kwa kuonesha unaijali siku yake.

Katika birthday au siku ya kuzaliwa ya mtu, unaweza fanya mambo mengi kumfurahisha ikiwemo kumpa zawadi au kumtumia ujumbe kwenye simu. Hapa chini tumeweka baadhi ya jumbe au sms za kumtumia mpenzi au rafiki katika siku ya kuzaliwa.

SMS za kumbembeleza mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Sms au Ujumbe wa siku ya kuzaliwa kwa mpenzi na rafiki

  • Mtu ambea ni mwanga wa maisha kwangu ni wewe. Napenda kila wakati ukumbuke kuwa furaha ya moyo wangu ni wewe. Nakutakia siku ya kuzaliwa yenye baraka tele.
  • Happy birthday rafiki yangu. Nakutakia maisha marefu na yenye furaha. Baraka na mafanikio ziwe katika Maisha yako na kila jema lisiache kukufuata.
  • Heri ya siku ya kuzaliwa rafiki yangu kipenzi. Natumai siku yako itakua nzuri na furaha. Napenda kukuona na furaha hivyo napenda kuona ukifurahia siku hii muhimu kipenzi.
  • Mpenzi wangu, Kuzaliwa kwako ni siku muhimu kwangu. Maana huo ni wakati zawadi yangu nzuri ililetwa toka kwa mungu. Nakupenda sana zawadi yangu, pia nakutakia maisha marefu yenye afya njema na furaha.
  • Happy birthday rafiki mpendwa! Nakutakia kila wakati kupata nguvu na msukumo wa kutimiza matamanio yako hapa Dunia. Maisha ni safari na nakutakia kila jema kwenye safari yako rafiki yangu.
  • Ninafuraha sana Leo maana ni siku mbayo malaika wangu ulizaliwa ili uje kuangaza maisha yangu. Kuwa na wewe na Raha sikufichi. Happy birthday my queen.
  • Nakupenda sana. Napenda jinsi unavyonifanyia katika Upendo na maisha kiujumla. Nafurahi kuwa na wewe. Tunapitia mengi ila daima nitakupenda wewe. Hicho ndio kitu natamani ujue katika siku hii, happy birthday mpenzi!
  • Nakutakia siku njema ya kuzaliwa rafiki yangu. Wewe ni mtu ambaye anamaanisha mengi kwangu na ambaye ninathamini sana wepo wako. Uishi maisha marefu rafiki yangu.
  • Kila siku ninapokuwa nawe ni zawadi kubwa. Siku ya kuzaliwa yako ni fursa kwangu ya kusherehekea upendo wetu. Heri ya siku ya kuzaliwa, mpenzi!
  • Upendo wangu kwako hauwezi kuelezwa kwa maneno yakatosha. Lakini katika siku hii ya kuzaliwa nataka nijaribu tu kwa kumwambia Nakupenda sana na uishi maisha marefu kipenzi changu. Happy birthday!
  • Ningekua na uwezo ningeiweka siku yako ya leo iwe ni siku ya kitaifa my love. Natamani Kila mtu ajue siku ya leo ndio siku mtu alieuweza mayo wangu na kunipa furaha maishani amezaliwa. Nakutakia siku njema na maisha marefu.

Sms hizi au jumbe hizi zina maneno mazuri ya siku ya kuzaliwa kwa rafiki na hata mpenzi. Unaweza zitumia bure kwa mpenzi wako mwanaume au mwanamke au rafiki. Kikubwa uchague ipi ni sahihi kuitumia kwa upande wako.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook.

Mambo 5 ya kujua kuhusu Tattoo

Pamoja na kwamba watu wengi wanaonekana wanachora tottoo kipindi hiki, lakini mabaki ya binadamu walioishi miaka iliopita yanaonesha kwamba tattoo hazijaanza kuchorwa miaka hii. Totoo zilianza kuchorwa toka zamani na mpaka sasa binadamu wameendelea kuzichora.


Kwasasa tottoo huchorwa kwa kifaa maalumu kinacho tumia sindano kuingiza wino katika ngozi. Hii inaweza kuwa ni tofauti na zamani kutokana na utofauti wa kiteknolojia.
Watu ambao huusika na kuchora tatoo kwa kiingereza huitwa “tattoo artists, tattooer au tattooist”. Kuchora tattoo ni sanaa kama sanaa nyingine lakini kuchora tattoo kumekua na mitazamo mingi sana kwenye jamii.
Hapa The he bestgalaxy, tunakupa mambo machache kuhusu Tattoo au uchoraji wa tattoo. Tende pamoja kuangalia mambo haya pengine lakini utapenda kuyajua.

Mambo 5 ya kujua kuhusu Tattoo

Wino mweusi

Katika kuchora tattoo, wino wa rangi nyeusi ni wino ambao ukichorea tattoo kwenye mwili, unakua ni rahisi ukuuondoa unapoifuta. Tattoo zinaweza kufutika kwa kutumia kifaa kinachotumia mionzi kinachoitwa Laser. Lakini kufuta Tattoo huambatana na maumivu. Wino mweusi unaweza kufutika kirahisi zaidi kama itakua ni ya wino mweusi.

Sindano huchoma ngozi mara 50 hadi 3000 kwa dakika

Mashine ya kuchorea tattoo Ina sindano ambayo hutumia kuingiza wino katika ngozi. Sindano hii unapoiweka katika ngozi ili kuingiza wino, huichoma ngozi kwa haraka mara 50 hadi 3000 kwa dakika moja. Jambo hili ndio huleta maumivu flani mtu anapochora tattoo. Lakini sindano hii huishia kwenye ngozi tu, haitakiwi kuchoma zaidi mpaka ndani kabisa ya mwili.

Asilimia 23 ya watu hujutia kuchora tattoo na hujutia zaidi majina.

Katika tafiti inaonekana kuwa baadhi ya watu hujutia maamuzi yao ya kuchora tattoo. Asilimia 23 ya watu waliochora tattoo imeonekana kujutia maamuzi yao ya kuchora tattoo hasa tattoo za majina. Na hii, kama utakua ni mfuatiliaji wa watu maalufu mtandaoni, unaweza kuwa tayari umeisha kutana taharifa za wasanii au watu maharufu wakijutia maamuzi ya kuchora tattoo kama hizo.

Tattoo ya thamani kubwa kuwahi kuchorwa.

Katika historia ya kuchora tattoo, tattoo ya thamani kuwahi kuchorwa ni yenye thamani ya Dola 924,000 za kimarekani. Hii ilikua ni tattoo ya muda mfupi iliochorwa kwa kujumuisha vipande vya almasi. Lakini tattoo hii iliochorwa kwa lengo la kuwa kama tangazo. Kampuni ya Shimansky ndio ilihusika na jambo hilo na aliechorwa tattoo hii alikua ni mwanamke model aitwae Minki van der Westhuizen.

Kuchangia damu.

Kuchora Tattoo hakukuzuii kuchangia damu kama utakua umekidhi vigezo vya kuchangia damu. Kumekua na baadhi ya watu wamekua wakijua kuwa ukichora tattoo hautaweza changia damu maishani mwako. Jambo hilo sio kweli, unaweza kuchangia damu bila shida kama utakua umekidhi vigezo vya kiafya vinavyohitajika kuchangia damu. Ila ukichora tattoo unatakiwa kukaa kwa miezi 3 au 6 ndipo ufanyiwe vipimo, uchangie damu.

Kuchora Tattoo sio jambo lisilo hitaji utaalamu. Kama umefikia uamuzi wa kuchora tattoo, unashauriwa kuwatumia wataalamu wa jambo hilo na sio kuchora hovyo tu. Hii ni Kwasababu kunavitu muhimu visipo zingatiwa unaweza jiwekea kwenye hatari zaidi kiafya kuliko tattoo yenyewe. Usalama usipo zingatiwa kwenye sindano, unaweza ambukizwa magonjwa. Pia Kuna wino wa tattoo huwa unapigwa marufuku kwasababu za kiafya lakini mtu asie mtaalamu wa mambo ya tattoo anaweza tumia wino huo kisa sio gharama kwake. Ukiachana na uliopigwa marufuku, wino mwekundu wa tattoo sio mzuri sana maana unaweza sababisha upere japo sio kwa wote. Nafikili umefurahia kujua mambo haya, usiache kufuatilia The bestgalaxy.

Jinsi ya kujiondoa kwenye post mbaya ulizoshirikishwa Facebook

Facebook inaruhusu kushirikisha mtu kwenye picha au post yako na huwa tunaita ku “Tag”. Mtu unaemshirikisha kwenye post yako anatakiwa kuwa ni rafiki yako wa Facebook. Kumshirikisha mtu ambae hamna urafiki kwenye Facebook haiwezekani kwa kumtag ila unaweza tumia kipengele cha kutaja (mention) kama njia ya kumshirikisha mtu.


Mtu unapo shirikishwa kwenye post kwa kipengele cha “Tag” na rafiki yako mmoja, marafiki zako wengine wanaweza pata taharifa kuwa umeshirikishwa kwenye post hiyo. Na endapo picha ulioshirikishwa itakua ni picha mbaya au usio taka kushirikiswa, Bado unauwezo wa kujiondoa.

Jinsi ya kujua kama akaunti yako ya Facebook ni Salama BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kujiondoa kwenye post mbaya ulizoshirikishwa Facebook

Hapa chini tunaenda kukuelekeza hatua kwa hatua jinsi ya kujiondoa kwenye post waliokutag katika Facebook lakini hautaki kuhusishwa. Jambo zuri ni kwamba ukijiondoa, aliekutag hawezi pokea taharifa kuwa umejiondoa.
Ili mtu kugundua kuwa umejiondoa kwenye post aliokushirikisha itambidi azingatie vitu viwili. Cha kwanza ni idadi ya watu aliowashirikisha na Cha pili ni kuzingatia uwepo wa jina lako kwenye orodha ya watu aliowashirikisha. Watu wengi hawazingati jambo hili wanapo post picha na kushirikisha wengine katika Facebook japo.
Unaweza fuata hatua hii kuondoa Tag

  • Ingia katika Facebook na uende Katika post waliokutag
  • Bonyeza vidoti vitatu vilivyo upande wa pembeni katika post hiyo.
  • Chagua “Remove Tag” kwenye orodha ya chaguzi utazoziona.
  • Bonyeza”CONFIRM” ili kuthibitisha maamuzi yako ya kujiondoa kwenye post hiyo.

Ukisha fanya hivyo tu, post itakua uhusiano na wewe tena. Utakua umefanikiwa kujiondoa kwenye post hiyo na kama ilikua inaonekana kwenye orodha ya post zako, itaondolewa. Lakini kama ikitokea watu wengine au post mpya unaweza shirikishwa tena kama kawaida.

Mambo muhimu kufanya kwa mpenzi mwenye hasira au ukorofi

Mkiwa kwenye mahusiano na mtu, inaweza kutokea mpenzi wako akawa na hasira kuhusu jambo flani au akaleta ukorofi tu. Kuna watu wanaweza kuwa na hali hiyo mara chache sana kiasi ambacho hatuwezi sema “Wana hasira sana” au ni “Wakorofi”.

Ukiachana na watu hao, kuna watu wengine hali ya kuwa na hasira au ukorofi ipo kwenye maisha yao kwa kiasi kikubwa. Watu Hawa wanaweza kuwa na hasira au ukorofi ambao hata wenyewe tu hawaupendi. Inaweza kuwa ngumu sana kuishi nao au kuwa nao kwenye mahusiano kama haujajua kuwa ni watu wenye hasira au ukorofi sana.

The bestgalaxy katika upande huu, tunakupa mwanga juu ya Mambo muhimu kufanya kwa mpenzi mwenye hasira au ukorofi. Mambo ya yanaweza saidia pale mpenzi wako asie na hasira anapopata hasira au kukusaidia katika kuishi na mpenzi mwenye hasira na ukorofi sana.

Lakini kabla ya yote, fahamu kuwa hasira au ukorofi inaweza kuwa ni hali ya mwanamke au mwanaume kwenye mahusiano. Hali hii haina jinsia na inaweza kuwa tatizo kubwa zadi kiasi ambacho muhusika mwenyewe haipendi, kutokana na kumsukuma kufanya vitu ambavyo hakusudii.

Kutokana na hili unashauriwa ukiwa kwenye mahusiano ujue mambo ya fuatayo ili usipateshida kuhusu hasira au ukorofi toka kwa mtu unaempenda.

SMS za kumbembeleza mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Mambo muhimu kufanya kwa mpenzi mwenye hasira au ukorofi(Wanaume na Wanawake)

Onyesha hali ya kumsikiliza

Unapoona mpenzi wako ana hasira kutokana na jambo flani au ameibua ukorofi na anaongea na wewe, onyesha hali ya kumsikiliza. Usioneshe hali ya kumpuuza anachoongea maana anaweza ongeza hasira au ukorofi na kufikia hali mbaya. Jaribu kuonesha hali ya kuwa unasikiliza anasema nini wakati anaongea na wewe ili uweze kupunguza hasira zake. Muache apunguze kilichopo kifuani pake kwa kutoa maneno.

Usibishane

Hatakama atakua anaongea kitu kisicho cha kweli au cha ajabu, jaribu kujizuia usibishane. Unaweza mwambia au kujieleza pale anapokupa nafasi lakini kuwa makini sana mmapofika hali ya kuanza kubishana. Kubishana kunaweza ibua ugomvi mwingine ambao hata yeye hakukusudia. Watu wengi wenye hasira wakibishiwa hutaka kuja juu zaidi kiasi ambacho baadhi yao huingia kupigana kimwili.
Kutombishia kunaweza kuwa ni jambo gumu lakini uzuri wake ni kwamba mambo yote ambayo anaongea kwa msukumo wa hasira alafu sio ya kweli yanaweza kumjia kichwani akitulia na kuona makosa yake yote.

Vitu vya kushangaza ambavyo hutokea ukimpenda mpenzi wako sana BONYEZA HAPA>>>

Chagua wakati sahihi wa mazungumzo nae

Kama mpenzi wako kuna kitu ameongea vibaya, amekukosea au unahitaji kumwambia, tulia na utafute muda mzuri kwaajili ya maongezi yenu. Usijaribu kumwambia mpenzi wako mambo hayo wakati unaona yupo kwenye hali ya hasira au ukorofi. Wewe fanya kutafuta muda ambao unaona kabisa hana na hawezi kuibua hasira kirahisi. Mbane kwenye muda huo kwa utulivu sana huku ukichanganya maneno yanayoweza ugusa moyo wake kwa upendo kwenye maongezi hayo.
Watu wengine wenye hasira wakifanyiwa hivi hufikia mpaka hatua ya kuomba msamaha kabisa na kukili. Wengine wanaweza kuwa wabishi kidogo ila dawa inakuwa imewaingia. Na wengine wanaweza anza tabia ya kuchunga asira zao ili wasirudie makosa.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Usiache kumuheshimu na kumuonesha upendo

Kama mpenzi wako mwanaume au mwanamke akiwa ana hasira na ukorofi lakini bado unaona mnapendanq, usiache kumuheshimu na kumuonesha. Kikubwa ni kumsoma tu tabia yake na kujua viwango vyake vya hasira kinafika wapi, anakua vipi na unatakiwa kufanya nini ili muwe na furaha. Upendo ni pamoja na kujuana pande zenu zote mbili, za furaha na hasira, hasa mukishaanza itana mume na mke.

Tafuta suluhisho na fanya mambo bila kukurupuka

Usije kukurupuka kufanya maamuzi pale unapoona wanaume au mwanamke wako ana hasira. Badala yake, tuliza kichwa na kufikilia nini ni suluhisho. Ukisha pata jibu kichwani, lifanyie kazi kwa utulivu ili kuweka mambo sawa. Kukurupuka kunaweza fanya na wewe ukafanya maamuzi mabaya ambayo baadae yanaweza kukujia kichwani na kugundua haukua sawa. Jitahidi usikasirike na kupandisha hasira pale mpenzi wako anapo waka. Tumia akili na usitumie hasira sana maana hasira zikikutana na hasira, hazizai kitu kizuri.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika tendo BONYEZA HAPA>>>

Mwisho; Hizi ni zama za kisasa na mambo ya ukatiri hayakubaliki karibu Duniani kote. Kama mpenzi wako wa kiume wa kike ana hasira au ukorofi unaomsukuma kukufanyia ukatiri, ni vema ukaachana nae au ukampeleka kwenye mamlaka husika hata kama tayari ni mume au mke wako.

Jinsi ya kucheza game la Call of Duty Mobile bila kudownload kwenye Simu

Call of Duty mobile ni moja ya zile games hupendwa na watu ambao hupendelea magame ya kupambania ufalme wa vita. Game hili ni game maalufu kutoka Activision na lilitengenezwa na TiMi Studio Group kwaajili ya simu.

Watu wanaolipenda gemu hili ulimwenguni ni wengi na baadhi yao huwa wanatamani kujua jinsi ya kulicheza kwenye simu bila kudownload. Hii ni kutokana na game hili kuwa kubwa au kuhitaji simu zenye uwezo kuliko simu zao. Hapa The bestgalaxy tunaweka wazi moja ya njia mtu anaweza cheza game hili bila kudownload. Kama unahitaji kujua hili, basi tuwe pamoja hapa chini.

Jinsi ya kucheza game la Call of duty mobile bila kudownload

Now.gg ni moja huduma za cloud gaming zinazokuwezesha mtu kucheza magame mtandaoni bila kudownload au kuyapakua. Mbali na magame, pia kua app nyingine unaweza tumia kupitia huduma hii bila kudownload kwenye simu yako. Huduma hii kwasasa ndani yake Ina app ya Aptoide ambayo ukifungua utakutana na magemu mengi ikiwemo Call of duty mobile na utaweza kulicheza bila kudownload.
Unataka kujaribu? Sawa, fuata hatua zifuatazo kucheza hili la Call of duty mobile ili kulipakua kwenye simu.

  • Unanginisha vpn katika saver ya USA kama upo nje ya USA.
  • Ingia google na utafute “Call of duty mobile now gg” alafu chagua matokeo ya juu kutoka Now.gg
  • Baada ya hapo utaletewa ukurasa unaoionesha app ya Aptoide, bonyeza kitufe kilichoandikwa “Play in browser” ilicho chini ya Aptoide katika ukurasa huo.
  • Baada ya hapo utapelekwa katika ukurasa wa Aptoide na utatakiwa kutumia sehemu ya kutafuta kulitafuta game la “call of duty mobile” (Yani utaandika “call of duty mobile” kwenye kisehemu cha kutafuta cha Aptoide.
  • Ukishalipata, lichague kisha utabonyeza “INSTALL” na kuacha kwa muda mpaka utakapoona batani ya “OPEN” kwenye game hilo.
  • Ikisha tokea batani ya “OPEN” utalibonyeza ili kulifungua gemu na kuanza taratibu nyingine za ndani ya gemu pamoja na kulicheza.

Mwisho, unapotaka kucheza bila matatizo, hakikisha unazingatia muunganiko wako wa mtandao/internet. Inatakiwa uwe na mtandao wenye kasi na usio yumba maana huduma za cloud gaming huwa zinategemea internet zaidi.

Mwanaume kuogopa wanawake wazuri kupita kiasi (Fahamu kuhusu hii)

Kuna wanaume huwa wanaogopa wanawake wazuri kwao. Kuogopa huku tunakozungumzia sio kuogopa kuwaoa. Yani unakuta mwanaume akimuona mwanamke mzuri wa sura, muonekano au msafi sana, akili huwa inamuhama. Na haimuami kwa matamanio, inamuhama kwa woga.

Kwenye kuongoza ndio muoga kabisa kiasi cha kutojaribu. Anaweza kuwa anaogopa na kuona kwamba mwanamke huyo mzuri ni kiumbe ambacho hawezi hata kukigusa. Anaweza kujiona yupo kwenye wakati mgumu sana endapo atakua kwenye mazingira ambayo amezungukwa na wanawake wazuri. Hatakama atatakiwa kuongea na mwanamke mzuri kuhusu mambo yasio husiana na mapenzi, bado huwa ni mthihani kwake. Katika maisha ya mahusiano, ameisha jiwekea mipaka ya mwanamke wazuri asio weza kuwao nao kwenye mahusiano maana hua wanamchanganya hata akiwa nao karibu tu. Kiufupi ni mwanaume anaeogopa wanawake wazuri.


Kwanza kabisa ni vema kujua kuwa ni kawaida kwa wanaume kuogopa au kuwa na wasiwasi mbele ya wanawake wazuri. Ila kama hali hii imezidi sana inaitwa gynophobia. Gynophobia ni hali ya kuogopa wanawake kiujumla.

Katika upande wa wanawake wazuri, unaweza jaribu kuelewa na kufanya yafuatayo ili kuondoa au kupunguza uoga.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika tendo BONYEZA HAPA>>>

Sababu za Mwanaume kuogopa wanawake wazuri na jinsi ya kujiweka sawa

Mambo unayotarajia

Kuna watu hua wanaingiwa na woga au wasiwasi wanapokua mbele ya mwanamke wazuri. Kuna vitu huwa vinawajia kichwani mara tu ya kuwaona. Yani anaweza kuwa amemuona mwanamke mzuri lakini akili yake imempeleka mbele kiasi kwamba anapoteza umakini katika wakati aliopo. Mfano; anaweza kuwa ameonana ya mwanamke mzuri na anataka kumsalimia lakini kichwani ameisha waza kuwa “Huyu mwanamke mzuri sana. Huenda nikimsalimia hata jibu… Asipojibu itakuaje?”. Kwa kuwaza hayo tu unaweza poteza umakini na kuingiwa na woga.


Kama unajiona unaogopa wanawake wazuri kwasababu hii, jaribu kupunguza matarajio mbaya. Fanya kitu unachoona ni sahihi bila kujali atafikiliaje au kitakutokea kitu gani kibaya. Ukifanya kitu kizuri alafu akakutukana, akakuonesha dharau au kitu chochote kibaya, tatizo litakua kwake na sio kwako.


Pia tabia ya kuangalia video za ngono na kujichua inaweza fanya unapokutana na mwanamke mzuri ufikilie vitu vingi kichwani na kuingiwa na woga au wasiwasi kupita kiasi mbele yake. Kama unajihusisha na tabia hizi, unaweza ziacha au kupunguza ili kujiweka sawa.

Uzoefu

Kuna baadhi ya wanaume hawana mazoea ya kuwa karibu na wanawake wazuri na ndio sababu ya kuwaogopa. Hii inaweza kuwa ni kutokana na mazingira mwanaume uliokulia au aliopo.
Kama unahisi hili inaweza kuwa sababu ya kuogopa wanawake wazuri na unataka kubadilika, anza kwa kujizoesha kuwa nao karibu.

Unaweza anza na kujisukuma kuwasalimia unapokutana nao. Unapojiwekea uzoefu huu, usiwe unawaza kuwaweka kuwa wapenzi wako. Jizoeshe kuwa nao karibu tu na usiwe na lengo la moja kwa moja la kuingia nao kwenye mahusiano. Liweke pembeni kidogo wazo la kuwa nao kwenye mahusiano. Unapo msalimia, anapokuita, unapomuita, unapokua mbele yake au kongea nae, usifikilie moja kwa moja mambo ya mahusiano ya mapenzi.
Kwa kufanya hivyo unaweza zoea na kuwachukulia wanawake wazuri ni wakawaida kwenye maisha yako alafu baada ya hapo, maamuzi ya kuingia nao kwenye mahusiano yatakua ni yako sasa.

Kujiamini na kuijua thamani yako

Kuna watu huwa wanaogopa wanawake na tatizo kubwa ni kushindwa kujiamini tu. Yani wanajiona hawana thamani mbele ya mwanamke wazuri kwao.
Kujiamini sio lazima uwe na pesa. Kujithamini au kutambua thamani yako sio lazima uwe na pesa. Kuna mpka watu kwenye maisha waliaza kujiamini au kujithamini ndipo wakapata pesa.
Popote ulipo kama mwanaume, jiamini na kujithamini pia. Usiionee aibu kazi yako, nguo zako, sura yako, sauti yako, mwendo wako au vitu unavyofanya hata kama unahisi mwanamke mzuri atakidharau. Ukifanya hivyo hata kama hauna pesa, unaweza mtetemesha mwanamke wazuri wenye pesa.

Asante kwa muda wako ndani ya The bestgalaxy. La kuongezea hapa mwisho ni kwamba mtazamo wako juu ya wanawake wazuri ni muhimu kuuweka vizuri ili usiwaogope. Watazame wanawake wazuri kama binadamu wa kawaida na sio malaika kama jinsi tunavyowasifu au wanavyojisifia. Na pia fahamu kuwa uzuri wa mwanamke au urembo anaoweka ni kwaajili yako wewe mwanaume hivyo hauna haja ya kuogopa, furahia kuwaona.

Total Football: Fahamu kuhusu Game hili la mpira

Total football ni game la mpira ambalo unaweza cheza kwenye simu ya mkononi. Ni game la mpira wa miguu kama lilivyo game la eSports football, FIFA mobile (EA SPORTS FC) au Dream League soccer.


Game la Total football limetengenezwa na GALA Sports kisha kutolewa na Studio Vegas private Limited pamoja na GALA Sports pia. Limetolewa katika platform mbili tu kwasasa ambazo ni Android na iOS. Hiyo kwasasa watu wanaweza cheza kwenye simu za Android or iOS(iPhone). Ni game la Bure kabisa na lina mode zaidi ya moja unaweza furahia kucheza na kitu kizuri zaidi ni kwamba linaruhusu kucheza offline pamoja na online.


Yani ukiwa una data au bando unaweza cheza game hili online alafu ukiwa hauna data, unaweza cheza bila ya kuwa na muunganiko wa internet. Ukiachana na hayo, Total football lina muonekano au graphics nzuri japo linaeweza zidiwa na baadhi ya magemu mengine ya mpira, lakini bado lipo vizuri kimuonekano.

Linakuruhusu kuunda timu ya ndoto yako kutoka kwa machezaji zaidi ya 4000 ulimwenguni, kuitengenezea jezi na Logo kisha kuonesha jinsi gani timu yako ni Bora kwa kucheza na timu nyingine. Linakupeleka katika ulimwengu wa bosi halisi wa timu ya mpira wa mguu kama DSL na magemu mengine kama hilo.

Kudownload na kucheza game la Total football (Android)

Total football kabla ya kutolewa rasmi Kuna baadhi ya watu walikua wanacheza likiwa kwenye maboresho na lilikua likisubiriwa sana na watu litolewe rasimi. Katika kulitoa napo halikutoka katika nchi au maeneno yote. Baadhi ya nchi au maeneno, hauwezi kucheza game hili kirahisi maana bado halipo rasimi kwenye maneno hayo.


Kwa hizi pande zetu, ukiingia playstore kwenye game hili (Android) unaweza kuta ujumbe ulioandikwa “This item isn’t available in your country”. Ujumbe huu unamaana sehemu ulipo game hili halipatikani. Sijajua ni lini wanaweza fanya game hili kuwa rasimi katika pande za huku kwetu lakini nisieme tu kuwa ni muda wowote kwanzia sasa linaeweza patikana. Unaweza BONYEZA HAPA kuangalia muda huu katika playstore kama limeishaachiliwa rasimi lichezwe pande za huku kwetu au bado.

Kama Bado, basi jaribu kupakua au kudownload APK file yake nje ya playstore alafu install kwenye simu yako ya Android. Baada ya kuinstall kwenye simu yako, lifungue na uanze kulicheza. Ukitaka uianza safari ya Kudownload APK file ya game la Total football unaweza BONYEZA HAPA.

Dalili za mahusiano ya mapenzi yanayo taka kuvunjika na jinsi ya kuokoa

Tulisha angalia vitu au mambo muhimu katika mahusiano ya mbali yanayoweza pelekea mahusiano ya mapenzi kudumu. Kama haukusoma, unaweza BONYEZA HAPA kusoma juu ya hili.
Hapa the bestgalaxy, tunaenda kukujuza juu ya dalili za mahusiano ya mapenzi yanayo taka kuvunjika bila kujali ni ya mbali au karibu. Inaweza kuwa ni ngumu moja kwa moja kueleza mambo yanayo ashiria kuwa mahusiano ya mapenzi yanataka kuvunjika maana kuna mahusiano ya mapenzi hupitia vitu vingi vibaya na bado hudumu. Mahusiano haya ya mapenzi huwa yanafikia hatua ambayo unaweza sema yanaenda kuvunjika lakini yanarudi katika mstari na kuwa poa tena.


Lakini mbali na yote, sisi tumekukusanyia dalili ambazo mara nyingi huwa zinaashiria kuwa mahusiano yanaenda kuvunjika. Pia utapata na mwanga mdogo wa namna mtu unaweza fanya kuyarudisha mambo kwenye mstari.

Kama umeona dalili hizi kwenye mahusiano yako ni vema akazishughulikia maana hatakama mnapendana sana bado huwa zikionekana inamaana mahusiano yapo kwenye hali mbaya kidogo.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Dalili za mahusiano ya mapenzi yanayo taka kuvunjika na jinsi ya kuokoa

Kufifia kwa mawasiliano

Inaweza kuwa sio mara ya kwanza kuambiwa kuwa “Mawasiliano ni kitu cha msingi sana katika mahusiano”. Mawasiliano yakiwa sio mazuri au yamefifia kwenye mahusiano ya mapenzi ni jambo hatari sana maana huashilia mahusiano yanataka kuvunjika au yanaweza kuvunjika kirahisi.

Hali hii inaweza kuwa ni hamuwasiliani kwenye simu au muko sehemu moja lakini hamna muda mnakaa na kuzungumza vizuri.
Ukikusa mahusiano yako yapo kwenye hali hii jaribu kumgeukia mpenzi wako na kutengeneza muda mtaokaa pamoja na kufanya mazungumzo. Usizidishe kuwa buzy kiasi cha kushindwa kumjulia hali mpenzi wako au kutenga muda wa kuongea nae ujue anataka nini, anawaza nini au amepanga kufanya nini.

Mara nyingi ukipambana na kuanza kuongea na mtu, hatakama alikua hataki inaweza fika wakati mnajikuta mnapenda kuwasiliana tena.

Kutojali

Ikifika wakati wapenzi mupo kwenye mahusiano na hakuna tena kujaliana au mmepenguza kujaliana inaweza kuwa ishara mbaya. Katika mahusiano kila mmoja anatakiwa kumjali mwenza wake. Mwanaume anatakiwa kumjali mwanamke na mwanamke pia anatakiwa kumjali mwanaume.

Endapo kujali kutapungua katika upande mmoja au pande zote inaweza kuwa ndio mwanzo wa mahusiano kuvunjika. Hali hii inaweza weka hata urahisi wa mtu kuanzisha mahusiano mengine mapya na mtu ambae anaona atamjali zaidi.
Unapona hali hii katika mahusiano ni vema kumgeukia mwenza wako na kuonesha jinsi gani unamjali. Usiishie kuongea, uoneshe kwa vitendo pia kuwa yeye ana umuhimu kwako, unampenda na unapenda anavyokupenda. Usisahau kujali hisia zake, kumsikiliza, kumsaidia kwenye shida na kuwa upande wake unapoona anakuhitaji.

Mambo muhimu kufanya kwa mpenzi mwenye hasira au ukorofI BONYEZA HAPA>>>

Kupungua kwa hisia au msukumo wa kuwa pamoja

Hisia za upendo na msukumo wa kuwa pamoja ndio mara nyingi hutuendesha kwenye mahusiano. Hisia na misukumo hii huwafanya watu waingie kwenye mahusiano ya mapenzi bila hata ya kuambiana neno “Nakupenda”. Lakini msukumo wa kuwa pamoja na hisia hizi zinaweza pungua watu wakishaingia kwenye mahusiano. Hili hii inaweza pelekea mahusiano kuyumba au kuvunjika kabisa.


Kuna mambo mengi hupelekea jambo hili na kabla ya kuangalia utaokoa vipi, ni vema ukajiuliza chanzo ni kipi. Hili ya kukosa msukumo wa kuwa pamoja au hisia za upendo inaweza tokea kutokana na mambo kama Msongo wa mawazo, mazoea au kukosa malengo na mtu ulienae kwenye mahusiano.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze Kila mala BONYEZA HAPA>>>

Malumbano ya mara kwa mara

Mahusiano nyenye Malumbano ya mara kwa mara yanaweza kuwa ndio yanatoa ishara ya kufikia mwisho japo mengine huendelea. Baadhi ya mahusiano hupitia kwenye malumbano na misukosuko kibao lakini huendelea kusonga. Lakini bado malumbano katika mahusiano yakizidi ni jambo baya linaloweza pelekea mahusiano kuvunjika.


Mukiwa kama wapenzi mukiona malumbano yamezidi inafaa mbanane, mkae pamoja, muweke hasira pembani na kuulizana “kwanini muko hivyo? Na unatakiwa kufanya nini ili kuyashinda kisha muendelee kuwa pamoja kwa amani?”.

Kupotea kwa malengo yenu ya pamoja

Mahusiano bila malengo ya pamoja tunaweza sema ni safari bila muelekeo. Mnapokua kwenye mahusiano, kuongelea mambo yenu ya mbele mtayofanya pamoja au kutimiza ni jambo muhimu. Ni muhimu kuwa na vitu ambavyo hata mkikosana mkikumbuka kuwa mmepanga kuvitimiza kwa pamoja, inakua rahisi kupatana. Endapo mambo au malengo yenu ya pamoja yataanza kukosa uzito kwenu au yatapotea kabisa, inaweza kuwa dalili ya kuwa mahusiano pia yanaenda kupotea.

Ukiona dalili hii ni vema ukazidisha upendo na kuwa karibu na mwenza wako sana alafu mkiongea, mazungumzo yenu yawe yanajumuisha malengo au vitu vya kufanya pamoja.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>

Usianze na mambo makubwa kama ndoa, Anza na madogo ambayo unaweza mtimizia au mkafanya pamoja baada ya wiki toka muongee tu. Mfano; kwenda nae sehemu nzuri, kununuliana vitu au kusaidiana mambo mengine yajayo.

Ni hayo tu katika ukurasa huu tumekuandalia. Lakini kabla ya kuondoka nakukumbusha kuwa mambo haya yanaweza tokea kwenye mahusiano na bado safari ya mapenzi ikaendelea japo mara nyingi huashiria mahusiano yanataka kuvunjika.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Kwanini haufanikiwi kimaisha? Sababu hizi hapa

Kila mtu unaweza kumsikia akiongelea kuhusu mafanikio lakini unapaswa kujua kuwa watu hawana maana sawa ya mafanikio. Hata ukiwauliza “Mafanikio ya kimaisha ni nini kwako?” watu huwaza vitu ambavyo hutegemeana na jinsi mafanikio yana maana gani kwao.

Kiufupi Mafanikio ya kimaisha tunaweza sema ni hali au matokeo ya kuweza kufikia lengo au malengo fulani maishani. Tunaweza pia kusema mafanikio ni kufikia au kuzidi matarajio, malengo, au viwango fulani vya utendaji katika maeneo mbalimbali ya maisha kama vile kazi, elimu, biashara, mahusiano au maendeleo binafsi.

Watu hukutana na changamoto nyingi katika kuyakimbiza mafanikio ya kimaisha. Hapa The bestgalaxy tumeisha zungumzia kuhusu mambo muhimu ili kufanikiwa pamoja na changamoto nyingi njiani. Katika ukurasa huu tunaenda kuangalia upande mwingine ambao ni mambo yanayoweza fanya mtu asifanikiwe.

Mambo yanayoweza fanya usifanikiwe

Kutojua mafanikio kwako ni nini na yanapatikana upande gani

Kama tulivyoeleza hapo juu, Kila mtu kuna jinsi ambayo mafanikio yanaonekana kwake. Sasa unapaswa kwanza kujiuliza wewe unahisi mafanikio ni nini kwako. Ni elimu ambayo itakupatia kazi? Ni biashara ambayo itafanya vizuri mpaka itabadili maisha yako? Usiwe na vitu vingi kichwani, fahamu mafanikio unayoyataka hapa Duniani na fikilia utayapata upande gani.


Kuna mtu aliulizwa “Unata kufanikiwa kivipi?” Akajibu “Kama msanii diamond… Yani nyumba kali, gari Kali na watoto wazuri kama wote… Alafu navimba kama kwenye nyimbo yake moja hivi. Yani nikisimama watu wote shangwe” akaulizwa “kwani wewe ni msanii?” Akajibu “hapana” akaulizwa tena “Unaimba mziki?” Akajibu “ah amna hata siwezi. Na sijikufanya kabisa hizo mambo”
Huyu jamaa kitu anachotamani maishani au mafanikio anayoyatamani ni ya mtu ambae ni msanii. Sio kitu baya, lakini yanaweza timia vipi ikiwa haupo kwenye upande ambao yanapatikana?. Hapa ukizidi kutamani, utapata msongo wa mawazo.


Ni vema kujua mafanikio kwako ni nini na yanapatikana upande gani. Kama mafanikio yako unahisi yatapatikana kwenye biashara, kuwa upande wa biashara, bana upande huo ata uwe msaidizi tu. Tambua kitu unachokihitaji alafu usicheze nacho mbali, pambana kukisogelea.

kubadirisha au kuyakatia tamaa malengo yako

Kujiweka malengo ni hatua nzuri ya kuanza safari ya mafanikio. Lakini mara nyingi malengo huwa na changamoto zake katika kuyatimiza. Unaweza kukumbana na vitu vingi sana katika safari ya kuyatimiza. Lakini unatakiwa kuwa makini sana linapokuja wazo la kubadirisha au kuyakatia tamaa malengo uliojiwekea. kubadirisha au kuyakatia tamaa malengo uliojiwekea inaweza kuwa ndio mwanzo wa kupotea na kushindwa kufikia mafanikio unayoyahitaji. Ni vema kupambana na kuwa msimamo wa kutimiza malengo yako ili uweze pata mafanikio unayoyahitaji.

Kukosa utayari wa kuwa unaetakiwa kuwa au kuacha vinavyo rudisha nyuma.

Inasemekana kwamba kunawatu huwa wana mipango mikubwa kwenye vichwa vyao, tena inayoweza kuwatoa waliopo. Watu hawa wanajua kila kitu kinachohitajika kufikia pale wanapotamani kuwa kimaisha. Sio hayo tu, wanajua mpaka kinachowafanya wasifikie mafanikio lakini hawapotayari kubadirika au kuacha vinavyo zuia kufanikiwa.


Ukitaka kufanikiwa mara nyingi inabidi uwe ni mtu unaweza badirika, kujifunza vitu vipya na kuwa na utayari wa kuacha mambo unayoona kabisa yanakuzuia. Usipo chukua hatua kwenye kufanya mambo hayo, unaweza jikuta unayaona mafanikio unayoyataka mbele yako lakini huyafikii.

Woga wa kushindwa au kuwa tofauti

Kama mafanikio unayoyataka yanahitaji ufanye kitu ili kuyafikia lakini unahisi woga basi tambua kwamba baada ya miaka kadhaa unaweza jutia kuogopa kwako. Wengi tukitaka kufanya bishara au vitu vya maandeleo vitakavyo boresha maisha yetu, huwa tunaogopa kudondoka au kuogopa ndugu, majirani, marafiki na watu wengine waliotuzunguka. Lakini jambo hili watu hujutia baada ya kutambua kuwa walitaka kufanya vitu vizuri ila walishindwa kutokana na kuogopa au kuwawaza watu ambao hawajaungana na maisha yao. Kama umefuatilia simulizi ya utamu wa jumla unaweza nielewa zaidi hapa.


Njia rahisi ya kuondoa woga wakufanya kitu unachotaka kukifanya ni kuingia wenye mazingira yanayohusiana na unachokitaka kukifanya. Kama unataka kuwa mfanya biashara wa samaki, Tafuta marafiki wanaojihusisha na mambo hayo, au naenda kwenye mazingira ya hayo mambo.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook