Category Archives: Teknolojia

Jinsi ya kupata Namba zilizofutika kwenye Simu

Kwenye simu huwa tunatuza namba na siku hizi Smartphone huturuhusu kutunza katika Email mbali na kuzitunza katika Laini na Simu yenyewe. Mara nyingi mtu unashariwa utunze namba za simu kwenye simu yako katika Email. Email ni sehemu nzuri ya kutunza namba zako maana huwa Inazitunza namba in cloud na kuzifanya iwe rahisi kuzipata hata utakapo ibiwa au kupoteza simu. Yani hata kama umeibiwa simu, ukiwa na taalifa za Email yako uliotunzia namba tu, unaweza ingiza email hiyo kwenye simu yako nyingine na ukapata namba za simu ulizotunza. Taalifa za Email tunazoziongelea ni Email yenyewe na Password yake tu.

Ukiona dalili hizi ujue akaunti yako ya Facebook si salama BONYEZA HAPA>>>


Katika ukurasa huu wa The bestgalaxy, hatuta zungumzia kuhusu utunzaji wa namba za simu zaidi ya hapa. Ila tunaenda kueleza jinsi ya kupata Namba za simu zilizofutika.

Jinsi ya kupata Namba za simu zilizofutika

Ikiwa umefuta namba yoyote kwenye simu yako na haipo tena kwenye Lain, Email na hata katika simu yenyewe, tambua bado unanafasi ya kuipata namba hiyo. Namba iliofutika kwenye simu inaweza kuwa katika akaunti yako ya Facebook iliopo kwenye app ya Facebook ya simu yako.

Ukiwa na app ya Facebook kwenye simu yako, huwa wanaomba ruhusa ya kuchukua namba za simu ulizotunza kwenye simu yako ili wazitumie kuiweka akaunti yako ya Facebook karibu na watu unaowajua. Hii ni moja ya sababu ambazo hupelekea kuwaona watu unaowajua kwenye Facebook.
Ukiruhusu ruhusu Facebook ichukue namba za simu kwenye simu yako, hata zikifutika kwenye simu, bado zitakuepo ndani ya akaunti yako ya Facebook. Kama uliiruhusu Facebook kuchukua namba za simu, unaweza fuata yafuatayo ili kupata Namba zilizofutika kwenye Simu yako.

  • Ingia katika Facebook na ubonyeze vimistari vitatu gusa “Settings”
  • Ingia kwenye settings alafu nenda kwenye “Accounts center”.
  • Ingia kwenye “Your Information and permissions” na ubonyeze kwenye “Upload contacts”
  • Chagua account yako ya Facebook utakayoiona Pele alafu utapelekwa kwenye ukurasa uliona orodha ya majina ya namba ambazo Facebook imeyatunza.
  • Baada ya hapo utakua ukigusa tu majina ili kuona namba. Kwenye orodha ya namba hizo unaweza kuziona namba ya simu iliofutika kwenye simu yako.

Kama haukuiruhusu Facebook kuchukua namba za simu kwenye simu yako, unaweza usiikute namba ambayo unaihitaji. Ni hayo tu tulio kuandalia hapa ila usiache kutembea The bestgalaxy.

WOWCube: Ni kifaa gani hiki na kinatumikaje?

Kama umewahi chezea “Rubik’s Cube” basi unaweza kuielewa zaidi WOWCube. “Rubik’s Cube” ni kifaa kilichoundwa na Ernő Rubik mnamo mwaka 1974. Ni kifaa chenye puzzle au fumbo ambalo linajumuisha kurejesha sura sita za maraba katika usawa baada ya kuvurugwa. Kuna Cube nyingine zanaubo mbali na mraba. Rubik’s Cube imekuwa maarufu zaidi ulimwenguni na inachezwa na mamilioni ya watu ulimwenguni.

Sasa WOWCube(WOWCUBE® Entertainment System) ni kifaa ambacho ni kama “Rubik’s Cube” lakini kipo kidigitali zaidi. WOWCube ipo kisasa zaidi kiasi ambacho inaitwa kifaa cha kucheza games. Kina kuruhusu kucheza games nyingi na unakua unacheza kwa kukizungusha, kukitikisa na kugusa screen. Kifaa hiki kina screen ndogo 24 ambazo zinakufanya uone vitu au games unachocheza.
Unakua unakichaji kama unavyochaji vifaa vingine vya kuchaji vya kidigitali alafu unaweza kukiunganisha na simu ya smartphone kwakutumia Bluetooth. Haijali ni simu ya Android au iOS, zote zinaweza kufanya kazi na hiki kifaa.


Kuna app yake unatakiwa uiingize kwenye simu ya smartphone unayoiunganisha nacho. App hiyo inaitwa WOWCube connect na kazi yake kubwa ni kukupa uwezo wa kuendesha kifaa cha WOWCube. Kupitia app hiyo unaweza ingiza games pamoja na app mpya kwenye kifaa cha WOWCube na kurekebisha vitu kama mwanga ili kuwa vile wewe unapenda.

Mbali na hayo, WOWCube pia inauwezo wa kuonesha notifications za kwenye simu ukiunganisha, tarehe (kalenda kwa ujumla), unaweza soma comics na kujifunza mambo mengine. Ni kifaa kizuri kwa watoto na wakubwa pia. Pre order kwenye website ya WOWCube, imeandikwa unaweza pata kwa kama dora 549 za kimalekani hivi. Hiyo ni pre-order.

Moja ya stori kuhusu jina lake lilivyotokea; wanasema kabla hakijaitwa WOWCube, watu alipokua wakioneshwa walikua wanamshangao wa “Wow”. Basi baada ya mishangao hiyo kuwa mingi, wakaamua kukiita “WOWCube”.

Jinsi ya kutumia bando kidogo unapokua Instagram

Mtandao wa instagram ni moja ya mitandao huwa inatajwa sana katika upande wa mitandao yenye kutumia sana data au bando la internet kwenye simu. Katika uzoefu wako wa kutumia mtandao huu kutoka Meta, unahisi unatumia sana bando la internet? Mh sijui kwa upande wako unawazo gani lakini ukweli ni kwamba mitandao ukiwemo instagarm ambayo hujihusisha na video huwa inatumia sana bando.

Instagram ina video ambazo hua zinajiplay bila hata uamuzi wa mtumiaji na video hizi hua zinachukua bando zinapojiplay. Mbali na video, picha zenye ubora pia zipo katika Instagram na picha zenye ubora hua zinachukua bando kuliko zisizo na ubora. Lakini hatuwezi sema mambo hayo kwenye instagram ni mabaya maana ndio kati ya mambo hufanya mtu ufurahie kutumia mtandao huu. Kama jambo la bando linakuumiza sana unawezafanya yafuatayo kutumia bando kidogo unapokua Instagram.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kutumia bando kidogo unapokua Instagram

Njia rahisi na rasmi ya kupunguza matumizi ya data au bando lako la internet ni kutumia App ya Instagram Lite. App ya Instagam Lite ni app ambayo imeundwa tofauti na jinsi ilivyo App ya Instagram ya kawaida. App hii ni ndogo kuliko app ya kawaida na imepunguzwa baadhi ya mambo au vipengele ambavyo hutumia bando lako ikiwemo ubora wa picha na video . Hivyo, unapoitumia app ya  Instagram Lite unakua unatumia bando kidogo kuliko ambavyo ungetumia app ya Instagram ya kawaida. Haitumi bando lako sana app hii na inaweza fanya vizuri hata kama mtandao wa internet kwenye simu yako haupo vizuri.

Kama hautataka kutumia app ya Instagram lite basi ni unaweza punguza matumizi ya data kwa kuwasha kipengele cha Data saver ambacho hupatika kwenye app ya Instagram ya kawaida. Kuwasha kipengele hiki, gusa vimistari vitatu vilivyo juu upande wa profile yako ya Instagram. Baada ya hapo ingia kwenye “Data usage and media quality” na uwase sehemu ya Data saver utakayoiona hapo.

Mbali na njia hiyo, unaweza punguza pia idadi ya video unazoangalia au ukapunguza muda unaotumia katika mtandao huu ili kupunguza matumizi ya bando lako.

Katika matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi GUSA HAPA>>>

Matumizi ya simu ya zamani unaponunua mpya (usiiuze au kuidharau)

Mara nyingi watu, hutumia simu walizonunua alafu hununua nyingine mpya baada ya muda flani. Sababu za kununua hutofautiana maana kila mtu huwa na jambo lake liliomsukuma kutoa pesa yake na kunua simu mpya. Kuna watu hununua simu mpya baada ya kuona simu ya zamani imeharibika kabisa, wengine hununua baada ya kupoteza simu, pia kuna wengine huwa wananuanua simu mpya kutokana na kuichoka simu ya zamani au kutamani kubadilisha simu tu.

Kama unatabia ya kununua simu mpaya ili kubadilisha simu au kwenda na wakati ni jambo zuri. Simu mpya huwa zinakuja na maboresho pamoja vitu vingine vizuri kwa huo wakati zinaotolewa. Hivyo kwenda na wakati katika upande wa simu ni jambo zuri. Lakini unaponunua simu, mpya simu ya zamani huwa unafanya nini?
Kama haujui matumizi ya simu yako ya zamani unapo nunua simu mpya, soma hapa chini ili kufahamu jinsi wanavyoweza itumia.

Matumizi ya simu ya zamani unapo nunua mpya

Badili kuwa kifaa cha games

Simu yako ya zamani kama ipo vizuri na inaweza kuwekwa games za kucheza, basi ibadili kuwa kifaa cha games. Kuna games nzuri sana ambazo unaweza zijaza kwenye simu hiyo alafu ukitulia ukawa unazicheza. Sio lazima iwe wewe tu unacheza, hata ukiwapa watoto inaweza kuwa vizuri pia.

Ifanye WiFi ya nyumbani

Simu za smartphone huwa zina WiFi ambayo unaweza unganisha vifaa vingine vinavyotumia internet alafu vikatumia internet kupitia simu hiyo. Sasa endapo itakua na simu ya zamani na laini ya simu usioitumia, unaweza weka bando la kutosha kwenye hiyo laini alafu ukiingiza kwenye simu kisha ukawa unaitumia iyo simu kama WiFi ya nyumbani kwako. Kama unatumia internet kwenye PC au simu yako, hii inaweza kuwa nzuri kwako maana utakua unaiunganisha kifaa chako kwenye simu hiyo ya zamani ili kupata internet.

Iweke kuwa simu ya nyumbani

Unasimu ambayo ukiwa mbali na nyumbani ukiipiga mtu yoyote aliopo nyumbani anaweza ipokea? Mh sawa. Ni vema kuwa na simu ya nyumbani ili ukipata dharura au wakipata dharaura watu alioko nyumbani muwasiliane. Kama hauna simu ya zamani, unaweza ibadili kuwa simu ya nyumbani kwa kuiwekea laini na kuwaambia wanaoshinda nyumbani waitumie kama simu ya nyumbani tu.

Badili kuwa kifaa Cha Muziki na video

Kama unapenda kusikiliza nyimbo na kuangalia filamu, basi simu yako ya zamani inaweza kukufurahisha kwenye hilo. Unaweza ijaza nyimbo zote ambazo huwa ukitulia unazisikiliza sana bila kuchoka au ukajaza filamu unazozipenda sana. Baada ya kufanya hivyo ukipata muda utakua unachukua iyo simu na kusikiliza nyimbo au filamu zako bila Kuigusa simu yako mpya na kumaliza betri.

Tunzia file usizotaka kutembea nazo au zipotee

Simu yako ya zamani pia inaweza tumika kama kifaa cha kuhifadhia vitu vyako. Unaweza ingiza mafaili ambayo hautaki yapotee au hautaki yawe kwenye simu yako mpya. Ukishaingiza, unaweza ficha hiyo simu sehemu ambayo unahisi ni salama. Kama ni mtu unaekumbuka password, basi unaweza weka na password kwenye simu hiyo.

Unaponunua simu mpya, usisahau kuwa thamani ya simu ya zamani bado ipo. Kikubwa ujue jinsi gani utaitumia simu ya zamani baada ya kupata simu hiyo maana usipojua hautaiona thamani yake.

Mbali na yote, kuiuza au kuigawa ni jambo zuri pia maana unakua ni kama unawasaidia watu wengine kupata simu na kuwaonesha upendo.

Jinsi ya kuona sms za WhatsApp kwenye simu nyingine (Bila Kuigusa)

WhatsApp inatuwezesha watu kuwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki mtandaoni. App hii ina vipegele vingi na moja kati ya vipengele vyake kuna kipengele kinaitwa “Link a device”. Kipengele hiki kinamuwezesha mtumiaji wa Whatsapp kuunganisha akaunti ya WhatsApp kwenye vifaa viwili mpaka vinne. Baada ya kuunganisha WhatsApp kwenye vifaa hivyo sms na vitu vingine vingi vitakua vinaonekana kwenye simu zote hata zikiwa mbali. Na kila kifaa kitakua na uwezo wa kutumika kujibu na hata kufuta sms.

Kama ni mtu mwenye simu mbili na unahitaji kuona sms zako za Whatsapp kwenye simu nyingine bila kuigusa unaweza fanya hivyo kwa kutumia kipengele cha Whatsapp kiitwacho “Link a devices”. Hapa chini tunakupa mwanga juu ya jinsi unavyoweza kufanya kuungalisha na kuanza kuona sms za Whatsapp kwenye simu nyingine bila kuigusa. Hakikisha hautumii kipengele hiki kialifu.

Jinsi ya kuunganisha na kuona sms za WhatsApp kwenye simu nyingine bila kuigusa

Chukua simu zote mbili za smartphone na uziunganishe kwenye internet(ziwe na bando). Simu yenyewe unataka kuangalizia sms tutaiita simu ya pili, simu ambayo ina sms unazotaka uwe unaziona tutaiita simu ya kwanza. Baada ya kuziweka sawa simu hizo, fuata yafuatayo:

  • Chukua simu yenyewe unataka kuangalizia sms kwenye simu nyingine(simu ya pili) alafu ufungue web browser (Chrome) na kwenda katika website ya WhatsApp web ambayo ni https://web.whatsapp.com/
  • Baada ya kufanya hivyo, washa “Desktop site” kwenye hiyo web browser.
  • Baada ya kufanya hivyo, refresh ukurasa wa WhatsApp web alafu utaona kibox Cha QR code kimetokea kwenye ukurasa huo.
  • Baada ya kufanya hayo kwenye simu yako ya pili, sasa uchukue simu yenyewe itakua na sms unazotaka kuziona(simu ya kwanza) kisha fungua app ya WhatsApp.
  • Ukishafungua app ya WhatsApp, bonyeza vidoti vitatu vilivyo upande wa juu alafu chagua “Linked devices”.
  • Baada ya hapo utatupwa kwenye ukurasa wenye kitufe kilichoandikwa “Link a device”. Kibonyeze hicho kitufe alafu kamera ya simu hiyo itafunguka na utatakiwa kuitumia kamera hiyo kuscan QR code zinazooneshwa kwenye kile kibox kwenye simu nyingine. Ninaposema kuscan nnamaana elekeza hiyo kamera kwenye kibox kilichopo kwenye ukurasa wa WhatsApp web uliufungua kwenye ile simu nyingine.
  • Ukisha scan itaunganisha akaunti hiyo ya Whatsapp alafu utaandika jina lolote la kwenye sehemu ya device name itakayo jitokeza uijaze na kusave.
  • Baada ya hapo, utaanza kuona sms za Whatsapp kwenye simu zote mbili hata ukiwa mbali. Kiufupi utakua umefanikiwa kuziunganisha na utakua na uwezo wa kuangalia sms za Whatsapp za simu ya kwanza kwenye simu ya pili kupitia https://web.whatsapp.com/ ambayo ambayo inaitwa “WhatsApp web”.
  • Yani ukitaka kuangalia sms za WhatsApp za simu nyingine bila kuigusa, utaingia https://web.whatsapp.com/ kupitia Web browser yako na kuwasha “Desktop site” kwenye hiyo web browser ( Chrome) bila kuscan tena mara ya pili.
  • Ukifanya hivyo tu, moja kwa moja sms za simu ya kwanza utaziona kwenye simu ya pili kwa muonekano huu chini.

Hatua hizi zinaweza kuwa ngumu kama sio mtu unaejua sana vipengele vya simu. Lakini nadhani wengi wanaekewa vipengele vyote nilivyoelezea.


Mwisho; muunganiko huo utakatika endapo simu ya kwanza yenye sms itakua haijawa online kwa siku ya 14, ambazo ni sawa na wiki mbili.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Apple vision pro: Fahamu kuhusu Miwani hii ya Apple

Miwani ya VR(VR headsets) ni vifaa vya kisasa ambayo huvaliwa na watu na hufanya watu kuanza kuona mazingira ya kisasa au yalioundwa tofauti na mazingira ya ulimwengu halisi. Ukivaa Miwani hii unaweza kuona upo kwenye ulimwengu mwingine kabisa na ulimwengu ulio uzoea alafu utakua na uwezo wa kufanya vitu katika ulimwengu huo.


Makampuni mengi hujihusisha na utengenezaji wa Miwani hii ya VR ikiwemo kampuni ya Apple inayotoa simu za iPhone. Katika February 2, 2024 huko US, kampuni ya Apple ilitoa Miwani ya VR itwayo Apple vision pro. Miwani hii ilikua ikisubiriwa sana na watu wanaofuatilia mambo ya VR maana ilikua ikiongelewa sifa na mambo ambayo itakua nayo kabla Apple hawajaitoa.

Mambo kuhusu Apple vision pro

Apple vision pro imebeba vingi vizuri

Kwasasa Miwani hii imeisha toka na unaweza ipata kama bidhaa nyingine za Apple tunazozifahamu kutoka kampuni Apple. Baada ya Miwani ya Apple vision pro kutoka kumekua na mambo mengine yameongelewa kuhusu badhaa hii ya Apple. Machache kati ya mambo hayo ni yafuatayo.

Apple vision pro Ina vitu vingi vizuri tunavyoweza viongelea. Kwanza kabisa Miwani hii ina “eye and hand tracking”. Kupitia hii unaweza ivaa na kugusa au kuchagua vitu unavyooneshwa na Miwani hiyo bila kutumia kifaa kingine. Unaweza kuchagua au kugusa vitu kwakutumia macho tu au mikono yako bila kuwa na kifaa kingine chochote mkononi.

Kwenye kioo, Apple vision pro Iko na micro-OLED displays zenye pixels milioni 23, ambazo zitafanya ufurahie ubora wa picha za 4k kwenye Kila jicho.
Kwa usaidizi wa kamera, Apple Vision Pro inaweza kuunda Avatar ambae ataonekana unapowapigia kupiga video call watu wengine kupitia Miwani hiyo.

Kiufupi, Apple vision pro ni bidhaa nzuri sana toka kampuni ya Apple na imetikisa ulimwengu wa bidhaa za VR katika mwanzo wa mwaka 2024. Angalia video hii hapa chini.

Video ya Apple vision pro

Bei


Moja katika ya vitu watu wameongelea sana baada ya Apple vision pro kutoka ni bei yake. Ukihitaji kununua bidhaa hii kutoka kampuni ya Apple kwasasa itakuhitaji uwe na $3,499. Hiyo ndio bei yake katika Dola za kimalekani, ukiigeuza kibongo bongo(Tsh) inaweza kuwa kama milioni 8 na laki 9 hivi.

Kuna baadhi ya watu ikiwemo CEO wa kampuni ya Meta, Mark Zuckerberg wamezungumza kuwa ni ghalama sana kuliko Miwani ya Meta Quest 3 inayofanya baadhi ya vitu kama Apple vision pro japo haina ubora sana kwenye baadhi ya vitu pia. Miwani ya Meta Quest 3 inapatikana kwa Dola 499.99 za kimalekani.

Lakini Kuna waataalamu wameeleza kuwa Apple vision pro imeundwa nah baadhi ya vitu vyenye gharama kuliko Meta Quest 3, hivyo inaweza kuwa ni sawa kuwa na gharama kubwa.

Credit: Apple

Haipo vizuri kwenye games

Baadhi ya watu wanonunua miwani ya VR huwa wanapenda kutumia zaidi upande wa games. Kucheza VR Games kwenye Miwani ya VR kunaweza huwa kunafurahisha sana. Sasa Apple vision pro bado haiko sawa katika upande huu.

Hand tracking yake haiko vizuri sana ukilinganisha na Meta Quest 3 na haina game nyingi za VR unazoweza furahia kuzicheza. Pia hand tracking haiko vizuri sana kiasi cha kukufanya ufurahie zaidi kucheza game za VR. Ila Meta Quest 3 ndio imetajwa kuwa vizuri katika upande huu wa games kuliko Apple vision pro.

Inaendelea kuboreshwa

Apple vision pro ni bidhaa nzuri Toka apple lakini ni toleo la kwanza, yani “first-generation product”. Mara nyingi bidhaa toleo la kwanza huwa zinakuja na matatizo na madogo madogo madogo ambayo kampuni huwa inaangalia namna ya kutatua na kuboreshwa bidhaa yao hiyo au zijazo. Apple vision pro nayo ipo kuboreshwa na kampuni ya Apple ili iweze kuwa bora zaidi.

Ni hayo TU katika ukurasa huu, usiache kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi.

Image credit: Apple

Mambo ya kuzingatia katika kununua bidhaa Mtandaoni (Online)

Kufanya manunuzi mtandaoni ni jambo watu hufanya sana katika miaka hii. Watu hununua vitu kwenye kwenye platfom maalumu za kuuza badhaa mtandaoni au kwenye mitandao ya kijamii.
Kununua vitu mtandaoni au online ni jambo zuri na huweza kufanyika kupitia vifaa kama simu au PC. Faida moja ya kununua vitu mtandaoni ni kuokoa pesa yako maana kuna bidhaa ambazo hupatikana kwa bei ya chini huku mtandaoni.

Ukiachilia mbali faida, kunachanga moto unaweza kutana nazo katika kufanya manunuzi mitandaoni. Hapa hatutazungumzia moja kwa moja changamoto hizi ila tunakupa mambo ya kuzingatia katika kununua bidhaa Mtandaoni. Mambo haya yanaweza kusaidia katika baadhi ya changamoto.

Mambo 5 ya kuzingatia katika kununua bidhaa Mtandaoni

Maelezo kuhusu badhaa

Bidhaa zinazouzwa mitandaoni huwa mara nyingi zinawekwa maelezo ambayo ukiwa kama mnunuzi unatakiwa kuyasoma ili kuielewa bidhaa. Unatakiwa usiishie kuangalia picha na bei tu, hakikisha unasoma na maelezo yaliowekwa kwenye hiyo bidhaa pia. Alafu usisahau kulisoma jina la hiyo bidhaa mara mbili mbili.
Ukiwa na tabia ya kununua vitu mtandaoni bila kusoma maelezo unaweza nunua kitu tofauti na ulichokusudia. Yani badala ya kununua simu, unaweza jikuta umelipia kupata kava la simu.

Angalia maoni toka kwa walionunua

Kabla ya kununua bidhaa Mtandaoni inashauriwa kuangalia maoni kabla ya kufanya maamuzi ya kununua. Mara nyingi watu huwa wanatoa maoni juu ya bidhaa walizonunua mtandaoni na kama bidhaa mbaya au nzuri huwa wanaweka wazi ili wengine wajue. Unaweza ingia YouTube, Facebook au ndani ya platfom unayotumia kununua bidhaa alafu ukaangalia maoni toka kwa walionunua katika kipengele cha “Reviews”.
Hii itakusaidia kujua kitu unachotaka kununua ni vizuri au kibaya. Ila unatakiwa kuwa makini na maoni ya uongo pia. Na fahamu kuwa baadhi ya vitu huwa vinakua vibaya kwa wengine ila ni vizuri kwako.

Utaratibu wa kurudisha bidhaa

Mambo mengi yanaweza tokea baada ya kulipia na kuletewa bidhaa ulioiona mtandaoni. Unaweza letewa bidhaa ikawa haina tatizo, ukaendelea kutumia au ikawa na tatizo, ukataka kurudisha.
Bidhaa ikiwa vizuri ni jambo zuri lakini ukiwa na matatizo alafu ukataka kuirudisha unapaswa kujua kuwa sio kila huduma huwa zinakuruhusu kurudisha bidhaa. Sasa ukiwa kama mnunuzi ambae unaona unaweza chukua bidhaa yenye matatizo kwa bahati mbaya, ni vema ukaangalia utaratibu wa kurudisha bidhaa zenye matatizo kabla hauja nunua hiyo bidhaa Mtandaoni.

Linganisha bei

Badhaa za mtandaoni huwa zinatofautiana bei. Unaweza kuta sehemu flani bidhaa inauzwa kwa bei kubwa kuliko sehemu nyinge lakini ni bidhaa moja. Kutokana na hili, inashauriwa kuwa mtu ambae ukiwa unataka bidhaa mtandaoni, uangalie hiyo badhaa katika sehemu tofauti tofauti na kulinganisha bei. Kwa kufanya hivyo, utapata sehemu ambazo bidhaa unayoihitaji inaizwa kwa bei rahisi.

Usalama wa pesa zako

Unapofanya manunuzi mitandaoni, usisahau kuzilinda pesa zako. Hakikisha unanunua bidhaa mtandaoni katika sehemu inayoaminika ili usiibiwe pesa zako. Hakikisha unajaza taalifa za malipo vizuri ili usije kosea kulipia. Hakikisha haudanganyiki katika kutoa taalifa za akaunti yako ya pesa.

Kama unatumia credit card katika kulipia, epuka kujaza taalifa za Credit card ukiwa umeunganisha kifaa chako na public WiFi bila VPN.

Mambo hayo machache yanaweza kusaidia katika kuepuka baadhi ya changamoto ambazo watu hukutana nazo. Hii inaweza kuwa kwenye platfom za kununua bidhaa kama; Alibaba, kikuu, Jiji na nyinginezo au mitandao ya jamii kama; Facebook na Instagram.

Tofauti kati ya Facebook Lite na Facebook ya kawaida kwenye simu yako

Ukihitaji kutumia mtandao wa kijamii wa Facebook kwenye simu, unaweza tumia kupitia njia mbili. Njia ya kwanza kabisa ni kutumia mtandao wa Facebook moja kwa moja katika tuvuti/website ya facebook. Njia ya pili ni kutumia Facebook kupitia app maalumu ambazo ni “Facebook lite” and “Facebook ya kawaida”.
Njia nzuri na rahisi ya kutumia mtandao wa Facebook ni njia ya app. App rasmi za Facebook zipo mbili, unaweza tumia app ya kawaida ya Facebook au ukatumia app ya Facebook lite ila kikubwa ni utambue tofauti ya app hizi. App hizi zinautofauti na hapa chini tumeweka tofauti chache kati ya Facebook lite na Facebook ya kawaida.

Tofauti kati ya Facebook Lite na Facebook ya kawaida kwenye simu yako

Matangazo mengi

Mtu unapotumia mtandao wa Facebook kupitia app ya Facebook lite hua unaoneshwa matangazo machache kuliko akitumia Facebook ya kawaida.
Unapotumia mtandao wa Facebook huwa kuna matangazo ambayo hujitokeza. Matangazo haya huioneshwa na kampuni ya Meta kwa kila mtu anaetumia mtandao wa Facebook Bure. Kuna watu hua wanalipia pesa Facebook ili kuyaondoa matangazo haya kwenye akaunti zao.

Kutumia data sana


Katika mtandao wa Facebook, Kuna vitu vingi sana ambayo mtu unaweza tumia bando lako kuvifurahia. Lakini unapaswa kufahamu huwa unapotumia app ya Facebook lite bando lako litatumika kidogo ukilinganisha na ukitumia Facebook ya kawaida.
App ya Facebook lite imeundwa kutumia data kidogo na inafanya vizuri hata kama upo kwenye mazingira ambayo mtandao unasumbua.

Kuchukua nafasi kubwa kwenye simu


Ukiingiza Facebook ya kawaida pamoja na Facebook lite kwenye simu yako kisha ukaangalia nafasi zilizochukua kwenye simu yako, utagundua Facebook ya kawaida imechukua nafasi kubwa sana kwenye simu yako kuliko Facebook lite.
Facebook lite ni app ndogo isiochukua nafasi kubwa sana kwenye Storage ya simu yako.

Ubora wa picha na video


Facebook lite ni app inayoonesha ubora wa chini wa picha ukilinganisha na app ya Facebook ya kawaida. Ukihitaji kuona ubora katika video na picha katika mtandao wa Facebook, tumia Facebook ya kawaida na sio Facebook lite. Facebook lite inawezapunguza ubora wa picha au video unapoziingiza au unapozitoa mtandaoni.

Katika video na picha za 360°

Kama ni mpenzi wa video na picha za 360° unatakiwa kufahamu huwa huwezi angalia video na picha za 360° ukiwa unatumia Facebook lite. Video na picha za 360° zinapatikana katika mtandao wa Facebook lakini unahitaji kuwa na app ya Facebook ya kawaida ili kuangalia kwenye kifaa chako.

Ni vema kufahamu tofauti ya app ya Facebook lite na Facebook ya kawaida ili uweza chagua unahitaji kutumia ipi, kwanini na wakati gani. Endelea kuwa karibu zaidi na The bestgalaxy.

WhatsApp: kuview status ya mtu na isionekane umeona

WhatsApp ni app inayotumika na watu wengi na app hii inavipengele vingi ikiwemo kipengele cha status. Kipengele  cha status huwezesha watu kushiriki hali zao na watu wengine. Kuiona status ya mtu kwenye WhatsApp utatakiwa kuwa na namba ya huyo mtu na yeye kuwa na namba yako. Na endapo ukiiangalia/ukiview  status ya mtu, ataona kuwa umeangalia status yake.

Sasa Kuna baadhi ya watumiji wa WhatsApp huwa wanataka kujua jinsi ya kuview status ya mtu na isionekane kuwa wameona kwa aliepost. Hapa The bestgalaxy tunaenda kukufungua juu ya hili kwa kukupa njia nzuri na salama ya kuanaglia au kuview status ya mtu bila kuonekana umeona.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kuview Whatsapps status bila kuonekana umeona

Kuview Whatsapp status ya  mtu bila kuonekana kunawezekana kufanyika kwa njia zaidi ya moja lakini njia nyingi sio salama kwa akaunti yako ya WhatsApp maana zinaweza kufanya uzuiwe kutumia WhatsApp. Njia salama ya kuview Whatsapp status ya  mtu bila kuonekana ni kuzima “Read receipts” kwenye app yako rasimi ya whatsApp. Fuata hatua zifuatazo kufanya hivyo.

  • Fungua App yako ya WhatsApp na uguse vidoti vitatu vilivyo juu kulia.
  • Chagua “Settings” kwenye orodha ya chaguzi zitakazo jitokeza.
  • Baada ya hapo ingia katika sehemu ilioandikwa “Privacy” na uzime kipengele kilichoandikwa“Read receipts
  • Baada ya kuzima kipengele cha hicho utakua na uwezo wa kungalia status za watu bila wenyenazo kujua. Kwaiyo ukizima, unaweza kuview status bila kuacha nyayo.

Kipengele hiki ni kipengele salama na hakiwezi pelekea akaunti yako ya Whatsapp kufungwa na Whatsapp. Lakini ubaya wake ni kwamba ukikizima huwa kinafanya usijue watu wanapoangalia status zako au kujua kuwa wamesoma sms ulizowatumia. Na wala wewe hautaweza kuonekana kama umesoma sms zao.

Kutokana na jambo hili unashauriwa; ukisha maliza kuangalia status ya mtu ambae hutaki ajue umeangalia, kiwashe tena hicho kipengele cha “Read receipts”.

Njia hii ni njia nzuri kuliko kutumia app za WhatsApp zisizo rasimi zilioweka urahisi katika kuangalia status bila kuacha nyayo. App hizo zinazoweza pelekea WhatsApp kuzuia akauti yako na ndio maana hatupendekezi japo unaweza tumia pia.

Magari ya Umeme: Fahamu mambo 5 kuhusu magari haya

Magari ya umeme yameonekana kuwa ni future katika teknolojia ya magari.

Kumekua na mipango mikubwa ya kuwezesha magari kuifikia sehemu ambayo magari ya diesel na petrol yameifikia. Na sio kuyafikia tu, Magari ya umeme yaenda kuwa mbadala wa Magari hayo ili kusimamisha uchafuzi wa hali ya hewa unaotokana na uchomaji wa diesel na petrol hapa Duniani.

Hapa The bestgalaxy tumekuandalia mambo matano kuhusu magari haya ya umeme. Kama wewe ni mtu unaependa kujua mambo kuhusu magari ya umeme, basi chukua muda wako kuyasoma hapa chini.

Mambo 5 kuhusu magari ya umeme

Betri ni moja ya vitu vya gharama sana kwenye magari haya

Kama tunavyo fahamu, magari huwa yananunuliwa, yatumika na katika kutumika huwa tunabadilisha sehemu za magari zilizochoka na kuweka mpya. Karibu kila sehemu tunayobadilisha kwenye gari hughalimu pesa.  Sasa katika magari ya umeme ukihitaji kubadili betri, huwa inagharimu pesa nyingi kuliko sehemu zote. Betri ya sehemu ya gharama sana katika magari ya umeme.

Unashauriwa kuangalia vituo vya kuchaji kabla haujanunua

Kutokana na magari haya kuonekana future, unaweza kuwa na shauku ya kufanya kila liwezekanano ili kununua. Lakini unapaswa kujua kuwa, kumiliki magari haya ya umeme katika sehemu iso na miundombinu mizuri kwajili ya magari ya umeme ni kitu unachoweza jutia. Unashariwa kuangalia zaidi upatikanaji wa vituo vya kuchaji katika mazingira yako kabla ya kuchaji magari haya ili usiteseke kupata chaji unapoishiwa ukiwa njiani.

Unaweza kuyachaji magari ya umeme nyumbani

Kutokana na Magari haya kutumia umeme, kunauwezekano wa kuyachaji nyumbani tu kwa umeme wa nyumbani. Lakini unapaswa kufahamu kuwa chaji zinazoweza kuwekwa nyumbani huwa hazina nguvu ya kujaza betri kwa haraka ukilinganisha na chaji zinazopatikana kwenye vituo maalum. Hivyo umuhimu wa vituo vya kuchajia upo pale pale.

Wamiliki wameonekana kupata changamoto katika baridi

Katika msimu wa baridi,  watu wanaomiliki magari ya umeme waishio nchi ambazo hukumbwa na theluji wamekumbana na changamoto katika kutumia magari haya. Changamoto hizi ni pamoja na kuchelewa kujaa kwa betri za magari na kupungua kwa “Range” (Umbali ambao gari linaweza kutembea kabla haujalipeleka kuchaji tena).

Yanaendelea kushuka bei

Watu wengi wanaotupia macho magari ya umeme huwa wanaishia kuyatupia macho magari ya kifahari au Luxuly cars zinazouzwa ghari sana na kusahau kuwa kuna magari ya umeme ya kawaida yasio na bei ya juu sana japo ni bado inaweza kuwa dharama sana kwa baadhi ya watu. Ujio wa magari ya umeme ni mapinduzi yanayogusa watu wote na kila siku zinavyozidi kwenda kunajisi bei zinaenda kuwa rafiki.

Unawazo gani kuhusu mapinduzi haya ya magari? Sawa, asante sana kwa muda wako. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine.