Category Archives: Teknolojia

Jinsi ya kujua kama simu inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine(anaona bila kuigusa)

Katika matumizi yako ya simu za Smartphone unatakiwa kuelewa kwamba vifaa hivi vinaweza kudukuliwa na mtu mwingine na kufanya mdukuzi au huyo mtu apate uwezo wa kuona vitu vilivyomo au vitu unavyofanya kwenye simu yako bila yeye kuigusa simu yako. Mbali na kuona vitu unavyofanya au ulivyohifadhi, Mtu aliedukua simu yako pia anaweza kuwa na uwezo wa kuitumia simu yako bila kuigusa… Mfano wa vitu anavyoweza kuvifanya ni kuitumia simu yako kutuma sms kwa mtu mwengine, kuitumia camera yako kuangalia unachokifanya, kuvujisha vitu vyako au kukuzuia kufanya baadhi ya vitu kwenye simu yako.

Lakini ukiwa kama mtumiaji wa smartphone wa miaka hii, hutakiwi kuwa na hofu sana juu ya hili kwani kunaviashilia vya kuangalia kwenye simu yako ili kujua upo salama au vipi. Hapa The beestgalaxy tutakupa mwanga juu ya jinsi ya kuangalia simu yako ya Android kama imedukuliwa na inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kuangalia kama simu yako inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine

katika matumizi ya simu watu huwa wanapenda kuingiza apps nyingine mbali mbali ukiachana na zile ambazo huwa wanazikuta tayari zipo kwenye simu. Kitu unachotakiwa kujua hapa ni kwamba kuna Program au apps ambazo unaweza kuingiza kwa bahati mbaya au ukaingiziwa kwenye simu yako na zikiwa kwenye simu yako zinakua zinatumika na mtu mwingine huona au kufanya vitu kwenye simu yako bila kuigusa.

Endapo katika simu yako kutaingizwa apps hizi kwa makusudi au bahati mbaya, simu yako itakua sio salama tena maana vitu. Lakini kitu kizuri ni kwamba kwenye sikuizi kwenye simu za Android kuna program inaitwa “Google play protect”. Program hii inamilikiwa na google na kazi yake kubwa kwenye simu ni kukulinda dhizi ya apps hatari unazoziingiza kwenye simu yako. Kama kuna app yoyote inayoweza kuwa hatari umeiingiza, Google play protect huwa inatoa taharifa na kukushari cha kuifanya. Unaweza kuitumia Google play protect kuangalia kama angalia kama simu yako ni salama au si salama. Unachotakiwa kufanya ni kufuata hatua hizi chini.

  • Chukua simu yako na uingie katika app ya Play store
  • Baada ya hapo, gusa kiduara cha profile yako na uchague “Play protect
  • Bonyeza kitufe kilichoandikwa “Scan” na baada ya hapo Google play protect itaanza kuangalia kama kuna app zozote hatari kwenye simu yako alafu itakupa majibu.
  • Kama kutapatikana app yoyote hatari utaonyenshwa app hiyo alafu utashauriwa kuiondoa kwenye simu yako kwa kugusa kitufe cha “Uninstall“.

Google play protect ni njia nzuri na rahisi ya kuangalia kama simu iko salama ukiwa kama mtumiaji wa kawaida lakini huwa haikuhakikishii usalama kwa 100%.

Google play protect ikiwa “Active” kwenye simu yako huwa inatafuta na kulinda hii ya app hatari. Na endapo itakuta app harari imeingizwa au unataka kuiingiza kwenye simu yako, itakupa taharifa.

Mbali nna kutumia Google play protect kuangalia kama simu yako iko salama unaweza pia kujua kuwa simu kwa kuangangalia kama kwenye simu yako kuna vitu vifuatavyo.

Angalia orodha ya app zinazotumia sana internet na kama utakuta app ambayo haieleweki na hauitumi lakini ipo juu kwenye matumizi ya bando, inawezakua ni app hatari. Kama kamera ya simu yako ukiifungua inakuandikia “Camera is being used by another application” au “You cannot use more than one application that uses camera” au “Camera may be in use by another application” hiyo inaweza kuwa ni ishara ya kwamba simu yako sio salama. Mbali na hayo, kukuta vitu ambanyo haujavifanya lakini vimefanyika kunaweza kuwa kiashiria cha hatari pia.

Jinsi ya kutafuta nafasi za ajira/kazi kwa kutumia simu mtandaoni

Kama ni mmoja kati ya watu wanaotafuta nafasi za kazi basi hapa kunakitu kidogo unahitaji kuwanacho kichwani katika miaka hii ukiwa katika mchakato wa kutafuta ajira. Unachotakiwa kujua ni kwamba teknolojia kupitia internet/mtandao imerahisisha mchakato wa kutafuta ajira na kuufanya uweze kufanyika katika kiganja chako kwa kutumia simu yako(Smartphone).

Unaweza tumia simu yako kuangalia nafasi za ajira unayoihitaji zilizojitokeza katika sehemu mbalimbali za dunia (Ndani na nje ya nchi). Na kama utapply au kufuata maelezo ya kuipata iyo nafasi na kubahatika kuipata, utakua ni mmoja wa mamilioni ya watu waliopata na wanaoendelea kupata nafasi za kazi kwa msaada wa internet. Kama unataka kutafuta nafasi za ajira/kazi kwa kutumia simu mtandaoni lakini haufahamu ni jinsi gani unaeza fanya hivyo, basi hapa chini nakupa mwanga juu ya hili kwa njia 3. Lakini kabla ya yote ni vema ukajua kwamba kunabaadhi ya nafasi za kazi au ajira ziwekwa na matapeli mtandaoni na maranyingi humuitaji mtaka nafasi atoe pesa ili kupata nafasi ya ajira… kuwa makini ni ajira za mtindo huo ili usije tapeliwa.

Njia za kutafuta nafasi za ajira/kazi zilizojitokeza kwa kutumia simu mtandaoni

Tafuta nafasi za kazi kupitia Google search

Watu tu hutumia google search kutafuta vitu mbalimbali kirahisi mtandaoni na imekua msaada mkubwa kwa watu wengi, nafikili hata wewe unaweza kuwa mmoja wa watumiaji wake mzuri. Mtu unaweza tumia Google kupata vitu vinavyokufurahisha, vitu vitakavyo kuelimisha na vitu vingine muhimu ikiwemo nafasi za ajira zilizojitokeza sehemu mbalimbali (Ndani na nje ya Tzanzania). Na nirahisi sana… kiufupi utatakiwa kuandika maneno yanayomaanisha nafasi za kazi, aina ya kazi na mahali(kwa kingereza ili kupata matokeo mazuri). Yaani unawezakwenda Google na kuandika “””””Aina ya kazi unayoitaka + jobs in + sehemu“”””” kisha ukitafuta na kwenye matokeo utapata orodha ya nafasi za kazi kulingana ulichokiandika. Kwamfano ukiwa unataka kazi ya “Customer care service” hapa Tanzania, utaandika “Customer care service jobs in Tanzania” kwenye matokeo utapata orodha ya nafasi za kazi za customer care zilizojitokeza Tanzania. Baada ya google ikukupa nafasi za kazi itakua ni kazi kwako kusoma maelezo ya kazi hizo ili kuzielewa zaidi na kuapply ikiezekana. Lakini unapotumia njia hii inatakiwa kufahamu kuwa Google ni search engine tu, hivyo huwa haina nafasi za kazi, inakupeleaka sehemu ilipopostiwa kazi…

Jiunganishe na blog zinazohusiana na mambo ya nafasi za ajira

Kuna blog ambazo hujihusisha zaidi na kutoa tahalifa kwa watu juu ya nafasi za ajira zilizojitokeza. Maranyingi huwa zinapost tahalifa za nafasi za ajira au habari zinazohusiana na mambo hayo hayo. Mfano mzuri ni Ajiraleo.com au Ajirampya360.com. Sasa kwakua na wewe unahitaji nafasi za kazi basi unaweza anza kuwa karibu na blog za mtindo huu ili wakitoa tu tahalifa za nafasi za ajira zilizojitokeza, zikupate kwa wakati na kuanza mchakato wa kuzichangamkia. Unaweza kuwa nazo karibu kwa kuzifuata blog hizo au kurasa zao katika mitandao ya kijamii ili kupata vitu wanavyopost.

Tumia LinkedIn

Linkedin ni mtandao kama vile Facebook au twitter lakini mtandao huu unakusanya wataalamu wa mambo mbalimbali na umejikitia katika zaidi maswala ya biashara na ajira. jiunga kwenye mtandao Linkedin bure kabisa na kwenye profile yako utatakiwa kujaza taalifa sahihi kuhusu wewe na utaalamu wako. Mambo unayotakiwa kuyafanya ndani ya mtandao huu ni vema yakawa yanaendana na utaalamu wako na jambo zuri ni kwamba unaweza kupata ajira kupitia mtandao huu… kurahisisha zaidi mchakato wa kutafuta nafazi za kazi, kunakipengele cha mtandao huu kinauruhusu kutafuta nafasi za kazi zilizojitokeza kulingana na uhitaji wako na kuapply.

Mbali na njia hizo tatu, kuna njia au vitu vingine zaidi unaweza fanya kupata taalifa za nafasi za kazi zilizojitokeza lakini huenda tutazungumzia katika sehemu nyingine, hapa tumekupa mwanga kwa hayo machache. Na ni vema kuendelea kutafuta nafasi za kazi nje ya mtandaoni pia. Ishi kwa kutangaza utaalamu wako. Endelea kufuatilia The bestgalaxy.

Njia 3 za kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu yako

Kama ni shabiki mzuri wa mpira wa miguu unaweza kua ni mmoja wa watu wanopenda kufuatilia matokeo ya mechi mbalimbali katika ulimwengu wa kabumbu. Teknolojia imeisharahisisha mambo mengi sana katika soka. Kupitia simu yako ya mkononi unaweza kuangalia mechi live na ukafurahia, kiganjani pako!.. Mbali na nakushuhudia mechi live kiganjani pako, unaweza pia kuangalia matokeo ya mechi zilizochezwa au zinazoendelea kuchezwa hapo hapo kiganjani pako. Hii inasadia sana maana unaweza kua hauna muda wa kutulia na kuangalia mechi lakini lakini ukawa unajua mechi katika upende wa scoles ziko vipi.

Kuna njia zaidi ya moja zinaweza kutumika kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu na watu huzitumia kila siku yaani kuangalia matokeo ya mechi za leo, jana na siku zaidi hiyo. Hapa The bestgalaxy tunaweka wazi njia 3 unazoweza kuzitumia kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu yako ya mkononi.

Njia 3 za kuangalia matokeo ya mechi za mpira kwenye simu

1. App na site/tuvuti maalum kwaajili ya kuangalia matokeo

Unapotaka kujua matokeo ya mechi mbalimbali kwenye simu yako, tambua kuna app za simu ambazo ni maalum kaajili ya matokeo ya mechi za mpira wa miguu na michezo mingine. Unaweza ingiza moja ya app za muundo huu kwenye simu yako na ukawa unatumia kuangalia matokeo ya mechi unazozihitaji kwenye simu. Uzuri wa app hizi ni kwamba nyingi huwa zinakua zinatoa huduma ya kukupatia matokeo bure kabisa japo kila utakapotaka kuzitumia utatakiwa kutumia internet. Mfano wa app hizi ni app iitwayo “LiveScore” na pia hii nyingine inaitwa “GOAL Live Scores”. Mbali na app izo kuna App ningine nyingi sana unaweza tumia kuangalia Scores. kwenyewe app hizi unaweza pia kufurahia vipengele vingine kama vile habari za michezo na ratiba za michezo.

Ukiachana na uwepo wa app, pia kuna websites/tuvuti unaweza tumia kuangalia matokeo ya mechi. App nyingi zinazojihusisha a matokeo ya mechi huwa ni za websites. mfano mzuri ni hii appp ya LiveScore; kuna website inatwa “LifeScore” na hiyo website ndio inaapp iitwayo “LiveScore”. kwahiyo hapo unakua uamuzi wako kuangalia matokeo mechi zako kupitia website au app.

2. Angalia matokeo ya mpira kupitia Google search

watu wengi hutumia google search kupata taharifa mbalimbali kwa haraka. Kunavitu ukivitafuta google unawezeza kuvipata kwa shida lakini sio matokeo ya mechi(hasa kama mechi inatambulika). Google inaweza kukupa matokeo moja kwa moja ya mechi ilioisha unayoihitaji bila mizungusho mingi. Na kitu kizuri ni kwamba kupitia Google unaweza pata taalifa nyingine kuhusu mechi kirahisi sana na bila kupoteza muda wala kutumia bando sana kama baadhi ya njia nyingine. Unaweza tumia njia hii kuangalia matokeo ya mechi za simba na yanga bila utata.

3. Angalia scores kwenye app au tuvuti za kubeti

Ukiachana na njia hizo mbili ambazo unaweza tumia kuangalia scores, njia ya tatu ni kucheki scores kupitia app au tuvuti za kubeti. Kama wewe ni mtu unaebeti kupitia simu, hainaaja ya kujitesa kuangalia matokeo ya mechi zinanoendelea kuchezwa. Unaweza kuangalia kirahisi kupitia kipengele cha “LIVE” katika website au app ambayo unaitumia kubeti. Kipengele hiki huwa kinakupa taalifa za mechi zinazochezwa muda huo na Moja ya taalifa utakazo zipata ni pamoja na magoli. Kipengele hiki ni kwaajili ya kubeti lakini unaweza kukitumia kuangalia scores za mechi unazozijitaji.

Jinsi ya kuweka kitu WhatsApp status bila mtu au watu flani kukiona

Kama huwa unaambiwa umuweke status kitu lakini unashindwa kwasababu mbalimbali na kupelekea kutoelewana kati yenu au unakitu unahitaji kuiweka status bila watu au mtu flani kujua basi leo nakufundisha jinsi ya kufanya hivyo.

WhatsApp status ni kipengele cha WhatsApp ambacho mtu hutumia kupost vitu mbalimbali ambayo huonwa na watu wengine walio na namba yake kwenye simu kama alivyo nazo zao yeye kwenye simu yake. Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba katika kipengele hiki unauhuru wa kuchagua mtu au watu gani waone status yako na watu gani wasione… Hii inamaanisha unaweza chagua watu au mtu pekee unahitaji aone status yako kisha ukapost kitu kwenye status yako na akakina yeyetu.

Unaweza fanya hivyo kwa kufunya yafuatayo;

  1. Fungua app ya WhatsApp kisha gusa vidoti vitatu vilivyo juu kulia.
  2. Utakuta orodha ya maneno machache, Chagua “Settings” Kwakuigusa.
  3. Katika settings utakuta orodha pia, Chagua “Account” Kwakuigusa na itakuletea orodha tena chagua “privacy”
  4. Ukisha chagua privacy, utakuta orodha tena,Chagua neno “Status” Kwakuigusa
    Hapo utaletewa orodha hii:

My Contact
My Contact except..
Only share with…


orodha hii inakidoti ambacho wewe unachagua kiwe katika nenolipi kati ya hayo.Na kidoti hicho utakikua kwenye “My Contact” wewe inabidi upeleke kwenye “Only shere with..”
ukikipeleka hapo itakuletea namba za watu wako kwenye simu,inabidi umchague yule unaetaka aione hiyo status alafu gusa “Ok” kisha “Done”
ukisha maliza nenda kaposti hiyo status, nenda kapost kitu anachotaka kwenye status yako na atakiona yeye tu!

Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kuongeza speed ya internet kwenye simu

Unasumbuliwa na speed ndogo ya internet? Usiwe na wasi tena! Hapa The Bestgalaxy tunakufungua juu ya nini unachoweza kukifanya kufurahia internet nyenye kasi kwenye simu yako ya smartphone.


Moja ya vitu ambavyo huudhi katika katika matumizi ya internet ni speed/ kasi ndogo. Speed ndogo ya internet sio tu huudhi bali pia hupoteza muda wa mtu anaetumia internet kwasababu kitu ambacho alitaka kukifanya kwa dakika 1 kwenye internet kinaweza mchukua mpaka dakika 5 ikiwa speed ya internet itakua ni ndogo. Watu wengi wanao thamini muda huchukizwa na swala hili.


Lakini tukirudi kufikilia kahusu historia ya internet utagundua internet imebadilika Sana na huwezi fanananisha na kipindi cha nyuma. Hata internet ya sasa isumbue vipi kwenye speed lakini huwezi ilinganisha na zamani maana huko nyuma internet ilikua haina kasi kabisa kama ya sasa. Kudownload nyimbo Moja tu yenye Mb 5 ilikua inaweza kukuchukua mpaka saa 1. Kama ni mtumiaji wa muda mrefu wa internet unaweza kuwa unajua kuhusu hili.

Yafuatayo ni mambo ambavyo Unaweza fanya kuongeza speed ya internet kwenye simu yako (hayahusishi matumizi ya WiFi)

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Namna ya kuongeza speed ya internet kwenye simu

1. Hakikisha unatumia laini ya 4G au 5G na Simu 4G au 5G

Kwasasa ukitaka kufurahia kasi nzuri ya internet basi inatakiwa iwe ni kuanzia kasi ya 4G. Ukitaka kufurahia kasi hii ya internet kwenye simu yako ya smartphone inatakiwa iwe na laini ya 4G na pia simu yako iwe ni ya 4G au 5G. Mbali na havyo pia ni vema “preferred network type” yako ikaiseti kwenye “Auto“. Kuiset preferred network type kwenye simu yako nenda kwenye “settings” ingia kwenye na uende katika “Network & internet” alafu ingia kwenye “SIM cards” kisha ingia kwenye “Mobile network“. Baada ya hapo gusa “Preferred network type” na uchague “Auto“.

2. Hamia kwenye mtandao wa simu wenye huduma ya internet yenye kasi.

Kuna muda mtu anaweza kuwa unakumbana na changamoto ya kasi ndogo ya internet katika matumizi ya internet kutokana na mtandao wa simu unaokupa huduma ya internet kutokua vizuri katika maeneo uliopo. Jaribu kufanya utafiti kwa watu uwalio kuzunguka ili kujua mtandao wanotumia kupata internet na speed yake ya internet iko vipi. Unaweza tu kuwaambia watu “Mimi ninatumia mtandao flani kupata huduma ya internet lakini naona Kama haupo vizuri Sana katika speed kwenye maeneo haya… Ivi ni mtandao gani nyinyi mnautumia na upo vizuri?”

Fanya haya kabla simu yako haijaibiwa ili kuipata ikiibiwa GUSA HAPA>>>


Kama kutakua na mtandao wanao sema upo vizuri basi jaribu na uangalie kama utakua vizuri kwako pia. Unaweza pia wasiana na watu wanao husika na mtandao wako wa simu na kuwataalifu kuhusu Jambo unalopitia kwenye eneo lako ili warekebishe. Tena bahati nzuri ni kwamba sikuizi makampuni ya mitandao ya simu ina kurasa zake katika mitandao ya kijamii na Unaweza watumia ujumbe kule na wakakujibu.

3. Boost speed ya internet kwa kuwasha “Flight mode” na kuizima.

Kama speed yako ya internet inasubua subua wakati unaitumia unaweza kuwa unaiboost kwa kuwasha “Flight mode” na kuizima. Flight mode huwakilishwa na kialama Cha “ndege ya usafiri” na hupatikana katika kisehemu Cha simu unachokifuata pindi unapo washa Data kwaajili ya kuanzia kutumia internet.

4. Tumia app zinaweza ongeza Speed ya internet.

Kuna baadhi ya app za VPN zinaweza ongeza speed ya internet. Hii inaweza onekana zaidi unapo download vitu au ku-stream vitu online ukiwa unatumia VPN. Lakini app za VPN zipo maalum kwaajili ya kuufanya muunganiko wako wa internet uwe salama na si kuongeza speed. Na pia sio kila unapotumia VPN utapata internet yenye kasi, VPN zinaweza pia kupunguza kasi kabisaa.

Mbali na app za VPN pia Kuna app zinazohusisha zaidi DNS zinaweza kuongeza kikasi Cha internet unapotumia. Mfano mzuri ni app iitwayo WARP… Unaweza ijaribu kwuingiza kwenye simu yako ya Android kwa lugusa hapa au iPhone kwa kugusa hapa

Magroup ya WhatsApp ya kujiunga BURE

Hapa tutaangalia vikundi vya WhatsApp ambavyo unaweza kujiunga. Sote tunajua kuwa vikundi vya WhatsApp ni muhimu sana kwa sababu watu huvitumia kuungana na wengine na kushiriki habari fulani au kujadili mambo mengi. Lakini unahitaji kujua kwamba kila mtumiaji wa WhatsApp anaweza kuunda kikundi cha WhatsApp na kuongeza watumiaji wengine kwenye kikundi. Hii inamaanisha kuwa unaweza pia kuwa na kikundi chako mwenyewe cha WhatsApp na kukifanya kama Msimamizi.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kuunda kikundi chako cha WhatsApp?


Ni rahisi sana, unachohitaji kufanya ni kufungua programu yako ya WhatsApp kisha uguse nukta tatu. Baada ya kugonga nukta Tatu, utapata orodha ya chaguo chache. Chagua “New group” ili kuanza kuunda kikundi chako mwenyewe. Kwenye kuliunda utatakiwa kuwachagua watu watu unaotaka wawe kwenye group. Unaweza kuchagua wale watu wote unahitaji wawekwenye group lako lakini tambua kuwa sio mtu anapenda kuungwa kwenye group bila tahalifa. Hivyo ni vema ukawatahalifu watu unaotaka kuwaweka kwenye group juu ya group unalotaka kuwaweka kwanza.

Yafuatayo ni magroup ya WhatsApp ambayo unaweza kujiunga nayo

Hapa nakupa orodha za vikundi vya WhatsApp ambavyo unaweza kujiunga badala ya kuunda kikundi chako cha WhatsApp. Hivi ni vikundi ambavyo unaweza kujiunga na kutumia lugha ya Kiswahili katika kuchati.

Magroup ya Marafiki/Mahusiano

Magroup ya Biashara

Magroup ya Ajira/Kazi

Magroup ya Michezo & Burudani

Unapaswa kujua kuwa, vikundi vyote vilivyoorodheshwa hapa vina watu kutoka sehemu tofauti na hatuna uhusiano wowote nao. Kwa hivyo hakikisha kuwa kila wakati unakuwa mwangalifu na walaghai au wanachama wengine ambao wanaweza kukosa nidhamu.

Njia 3 za kutumia intaneti bila malipo kwenye simu ya Android au iPhone

Katika mabilioni ya watu wanaotumia internet ama mtandao kila mwaka na watu wengi kati yao wanaotumia Simu. Na siku hizi, watumiaji wengi wa simu wanatumia simu za Android na iOS. Mambo mengi ambayo watumiaji wa simu za Android au iOS wanapenda kufanya kwenye simu zao yanahusisha kutumia intaneti.

Wanatumia intaneti kwenye mambo kama vile kushiriki habari, kujifunza, kuendesha biashara zao, kupata burudani na zaidi. Kwa vile sote tunajua kwamba mtandao sio bure, inagharimu watumiaji kiasi cha pesa kununua bando za internet au kulipia huduma za internet. Lakini bado kuna nini cha kufanya ili kutumia wa internet bure kwenye simu.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>

Pata BAND0 kubwa la internet Kwa Bei rahisi GUSA HAPA>>>

Ikiwa wewe ni mmoja wa watu wanaotumia simu yoyote ya Android au iPhone na unahitaji kutumia intaneti bila malipo basi hapa chini kuna kinachoweza kufanya ili kupata intaneti bila malipo.

Njia za kupata intaneti ya Bure kwenye simu ya Android na iPhone


  1. Unaweza unganisha simu yako Kwenye huduma za Wifi za bure zinazopatikana kwenye mazingira yako… unaweza tafuta sehemu zilizio na huduma ya WiFi kitahisi kwa kutumia App yako ya Facebook. App ya Facebook inakipengele kinachokuonesha maeneo yenye huduma za WiFi katika eneo ulilopo.
  2. Unaweza pata ofa au zawadi za interneti ambazo hutolewa bure na kampuni inayokupatia huduma ya internet (mfano Tigo: Ukituma neno “BURE” au “Social bonus” kwenda Namba 15166 unaweza zawadiwa Mb za internet BURE..
  3. VPN pia inaweza tumika kupata internet bila malipo… lakini njia hii imewekwa hapa Kwa lengo la elimu tu na si vinginenyo. Unaweza soma moja ya makala zetu zinazohusisha njia hii HAPA>>>>>

Magroup ya WhatsApp ya kujiunga bure GUSA HAPA>>>

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook imedukuliwa na si salama (hacked)

Account za mitandao ya kijamii huwa zinawindwa na kudukuliwa na hackers. Katika Facebook muda mwingine unawezakua unatumia account iliodukuliwa na haujui kuwa imedukuliwa. Madhara ya kutumia account ya Facebook iliodukuliwa ni kwamba hacker anaweza itumia account yako ya Facebook kufanya uhalifu kwa watu Wengine na hao watu wakajua wewe ndiye umewafanyia hivyo. Kwaiyo ni muhimu kujua hali ya account yako ya Facebook ili kuepukana na mambo kama hayo.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Kwenye audio nimezungunzia jinsi unavyoweza tambua kama account yako ya Facebook imedukuliwa/hakiwa na hackers. Kama imekufungua wewe basi usiache kuwa kuwajulisha na watu wako wengine wa karibu juu ya hili ili waweke account zao salama sisijetumika kukutapeli na vitu vingine kama hivyo. Unaweza gusa kitufe cha kijani hapo chini kuwasamazia watu ujumbe huu kwenye WhatsApp.

Kuangalia vifaa vilivyotumika kuingia kwenye Akaunti yako ya Facebook

  • Ingia kwenye account yako ya Facebook na uguse vimistari vitatu(menu)
  • Baada ya hapo chagua “Settings” ingia kwenye “Security and Login
  • Ukisha fanya hivyo utatupwa kwenye ukulasa ambao unakipengele kilichoandiwa “Where you Logged in“. Kwenye kipengele hiki unakutana na list ya vifaa ulivyotumia kuingilia kwenye account yako ya na taalifa nyingine kuhusiana uingiaji.

Jinsi ya kufanya simu isiishe chaji haraka

Hapa tumeelezea vitu vichache unavyoweza kufanya kwenye simu yako ya Smartphone (Android) ku refusha maisha ya chaji. Hii inaweza kuwa msaada mkubwa Kwa watu wenye simu zinazowahi kuisha chaji.

Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba vitu vinne tulivyotaja katika Audio si vitu pekee vinavyorefusha maisha ya chaji. Kama utaka kaelezo zaidi ya kufanya vitu hivi kuandika ujumbe wako na kutumia Kwa njia ya WhatsApp kwa kugusa kitufe kilicho andikwa “Chati nasi WhatsApp” kwenye Home Page yetu.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>

Magroup ya WhatsApp ya kujiunga bure GUSA HAPA>>>

Fanya haya kabla simu yako haijaibiwa ili kuipata ikiibiwa

Kuibiwa simu(Smartphone) ni Jambo ambalo karibia kila mtu hapendi limtoke lakini huwa linamtokea tu pasipo kutarajia. Ukiwa bado upo na simu yako unatakiwa kuandaa mazingira ya kuipata kirahisi pindi itakapoibiwa. Ili kuipata simu iliobiwa unatakiwa kuwa na taalifa ambazo zitatumika katika kufanikisha zoezi la kuitafuta simu yako. Taalifa hizo ni pamoja na namba za IMEI za simu.

Jinsi ya kufanya simu isiishe chaji haraka GUSA HAPA>>>


Kila simu huwa na namba zake za IMEI na endapo utaenda polisi ili wakusaidie kutafuta simu yako basi utahitajika kuwapa namba za IMEI za simu ilioibiwa ili kufanikisha upatikanaji wake. Hivyo ni muhimu kuwa na namba za IMEI za simu zetu ili tukipoteza tuzipate kirahisi. 


Sasa unachotakiwa kufanya kabla simu yako haijaibiwa ni kwenda katika sehemu ya kupiga simu alafu piga namba  *#06#  Kisha zinakili katika karatasi namba(IMEI) utakazoletewa na utunze karatasi hilo kwenye vitu vya muhimu ili lisipotee kirahisi.

Kama utakuja kupapoteza simu yako, namba hizo zitatumika kuipata simu yako pindi utakapo peleka swala lako polisi. Pia kumbuka kutunza na lisiti ya ununuzi wa simu.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>