Tag Archives: WhatsApp

Mtu akiku “Block” WhatsApp unaweza fanya hivi kuchati nae

Je, ungependa kujua mbinu za kuchati na mtu aliyekuzuia (Block) kwenye WhatsApp? Usijali, katika makala hii tutazungumzia kuhusu hilo.
Watu huzuiwa kwenye WhatsApp kwa sababu tofauti kama vile migogoro ya uhusiano na vitu vingine. Na hakuna njia ya kujitoa block mtu akiku block kwenye WhatsApp. Lakini hapo tutakupa njia za kuchati tu na mtu aliyekuzuia kwenye WhatsApp.
Kabla ya kwenda moja kwa moja kwa uhakika wa makala hii, hebu tuangalie vitu vinavyoashiria kwamba mtu amekublock kwenye WhatsApp.

Ni nini kinaonyesha kuwa mtu amekublock kwenye WhatsApp?

Huwezi kumuona yupo Online, muda wote unaoneshwa mara yake ya mwisho kuonekana Online/mtandaoni. Na pia huwezi ona profile picha.
Si hivyo tu, bali hata jumbe unazotuma kwake zinaonesha alama ya tiki moja tu wakati wote.
Ukiachana na hiyo, huwezi kufanikiwa kupiga simu ya sauti au ya video (voice call & video call) mtu aliekublock kwenye WhatsApp alafu akapokea.

Katika Matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi (Unaweza juta!) GUSA HAPA>>>

Jinsi ya kuzungumza na mtu aliyekuzuia kwenye WhatsApp

1. Chati naye kupitia group la WhatsApp.

Kama alie kubook ni mpenzi wako au marafiki, basi mwambie rafiki yako mwingine atengeneze group la WhatsApp kisha akuweke wewe na mtu aliekublock kwenye hilo group. Baada ya rafiki yako kukuweka kwenye kikundi/group hilo, utaweza kuchati nea ndani ya hilo group.
Rafiki aliyeunda group anaweza kuondoka kwenye hilo group na kuwaacha nyie.
Baada ya hapo, utakua Ukituma meseji zako kwenye group kisha rafiki au mpenzi wako aliekublock atapokea ujumbe wako kupitia group hilo. Pia atakuwa na uwezo wa kujibu ujumbe wako.

Tumia hii kama nafasi ya kutatua migogoro kati yako na mpenzi wako au rafiki aliyekuzuia/kublock.

2. Tumia app nyingine anazotumia kuchati.

Ikiwa hutafaulu kuzungumza nae kupitia group la WhatsApp, jaribu kuzungumza na mtu huyo kupitia app nyingine za kuchati ambazo yeye hutumia. Unaweza kumpata kwenye Facebook messenger, Telegram, Signal na app nyingine zingine unazofikiri mtu huyo anatumia. Lakini unapaswa kukumbuka kuwa anaweza kublock pia kwenye app hizo, kwa hivyo ukipata nafasi ya kuchati na mtu huyo, itumie vizuri.

3. Tumia app za nambari ya pili (Vitural number apps)

Movies za kutafsiliwa GUSA HAPA>>>>

Hizi ni app zinazokupa nambari ya pili na unaweza kuitumia kutuma ujumbe mfupi au kumpigia mtu yeyote kama nambari yako ya kawaida ya simu. Mfano wa app hizi ni app iiitwayo “TextMe
Ikiwa haukufanikiwa kwa njia zilizo hapo juu, unaweza kupagua app moja ya nambari ya pili. Kisha chagua nambari na uitumie kutuma ujumbe au kumpigia simu aliyekuzuia. Tumia hii kama nafasi ya kutatua tatizo lililo kati ya wewe na aliyekuzuia.

Huu ndio mwisho wa makala hii Lakini ningepeda kukujuza kuwa hapa ndipo maunja yote ya teknolojia unaweza kuyapata. Kikubwa ni usisahau kutembelea mahali hapa Kila mara ili usikose vitu vipya.

Unasumbuliwa na kelele za sms za Magroup ya WhatsApp? Fanya hivi

Wengi tumekua tukitumia WhatsApp katika kuwasiliana na ndugu na jamaa zetu kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Pia tumekua tukijiunga katika Magroup (Vikundi) ambavyo nia na madhumini yake ni kutujumuisha kwa pamoja ili tuweze kujadili au kubadilishana mambo mbalimbali. 
Kuwa na group si tatizo ila tatizo huja pale group linapokuwa na watu wengi wanaochati kipindi wewe hauna muda wa kuchati kutokana na sababu mbalimbali na kukupelekea kuona sms za wengine kuwa kero kwakua huingia kwa kelele mfululizo.
Kama unagroup ambalo husababisha kelele kutokana na message zake, unaweza lifanya yafuatayo ili kulifanya liingize message kimya kimya;

  • Nenda katika ukarasa wako wa WhatsApp kisha lishikilie group lenye kelele kwa muda usiopungua sekunde tatu Kama inavyooneshwa hapo chini.
  • Ukishikilia kwa muda wa sekunde tatu group litajipiga tiki na maeneo ya juu ya WhatsApp kutatokea chaguzi: katika chaguzi hizo utaona alama ya spika iliokatwa. Alama hii inamaanisha kulikarisha kimya group hivyo utaigusa alama hiyo kama picha inavyokuonesha hapa chini. 
  • Baada ya kuigusa alama hiyo utaletewa chaguzi uchague group hilo liwekimya kwa muda gani kwaiyo utachagua masaa8, wiki 1 au milele kisha utagusa neno “Ok” kama inavyooneshwa katika picha.

Baada ya kufanya hayo utakua umetatua tatizo la kelele maana sms za group hilo zitakua zinaingia kimya kimya. Na unachotakiwa kujua ni kwamba kama utachagua masaa8 basi baada ya masaa8 group litakua linaingiza sms kwa kelele kama kawaida na hata ukichagua wiki, wiki likiisha kelele zitakua palepale ila ukichagua milele hutaskia kelele za group hilo mpaka utakapo lishikilia tena group hilo na kugusa kialama cha sipika isiokatwa ili kuliweka huru.
Kama ni mtu ambae unamagroup mengi au unamagroup ya ajabu ajabu unaweza tumia njia hii kuepuka kelele na kulifanya group lisije kuleta taalifa za sms za ajabu ajabu.