Tag Archives: Vunjambavu

Vichekesho vya Maandishi unavyoweza kusoma

Kucheka ni njia bora ya kupunguza mawazo yanayotukumba kila siku. Katika maisha haya yenye changamoto nyingi, kila mtu anahitaji muda wa kupumzika na kufurahia vitu vidogo vinavyoweza kuleta tabasamu. Hakuna njia bora ya kufurahia muda wako wa kupumzika kama kuangalia video au kusoma vichekesho vya maandishi, vinavyoweza kukuchekesha na kukufanya usahau magumu ya maisha kwa muda.

Utafiti unaonyesha kwamba kucheka kuna faida kubwa kiafya, kama vile kupunguza msongo wa mawazo, kuongeza kinga ya mwili, na kuboresha hali ya moyo. Kicheko pia huimarisha mahusiano ya kijamii kwa sababu huleta furaha na mshikamano miongoni mwa watu unaocheka nao. Kwa hivyo, kama unatafuta kitu cha kukuchekesha na kukupa muda wa kuburudika, basi uko mahali sahihi.

Katika makala hii, tumekusanya orodha ya vichekesho vya maandishi vinavyovutia na kuchekesha, ambavyo unaweza kusoma popote ulipo. Jiandae kwa kucheka kupitia vichekesho hivi vya maandishi!

Soma Vunjambavu za vichekesho BONYEZA HAPA>>>

Vichekesho vya Maandishi vya kuvunja mbavu

  1. Mtoto katika maombi

Kila mara mtoto alikua akiambiwa kuwa anaeleta au kuwapa chakula ni Mungu. Siku moja, Mama yake alimwambia huyo mtoto aombee chakula kabla ya kula. Mtoto akaanza:
“Mungu, tunashukuru kwa chakula hiki. Naomba pia ulete chips na soda kesho maana ugali na mboga za majani kila siku zinachosha!”
Watu wote mezani walicheka sana.

  1. Mtoto na Mwalimu

Mwalimu alianza kuuliza kila mwanafuzi darasani “Kwa nini unahitaji kujifunza hesabu?”
Mtoto mmoja akajibu “Ili mama yangu asitumie hela zangu vibaya nikimpa anishikie”
Darasa zima likacheka

  1. Bibi na TikTok

Bibi Fatuma alikuwa sio mjanja na hakuielewa teknolojia ya TikTok. Wajukuu wake walimshawishi ajaribu. Alianza na video kutaka kutengeneza video akiwa anacheza live. Badala ya kubonyeza kitufe cha kuanza kurekodi, aliweka simu mfukoni na kuanza kucheza peke yake huku akipiga makelele ya nyimbo za zamani.
Baada ya muda mrefu, aliwauliza wajukuu:
“Mbona hakuna mtu ana-like video yangu?”
Wajukuu alipo fikilia kuwa bibi yake alichofanya, alicheka sana.

  1. Mtu na mpenzi wake wanaoongea kwenye simu

MKAKA: Hi uwapi swity?
MDADA: Niko home
MKAKA: Unafanya nini?
MDADA: Nakula
MKAKA: Unakula nini?
MDADA: Mama katengeneza macaroni, ambayo kanyunyizia chiizi na sausage fulani imported ambazo baba amenunua supermaketi Masaki, na saladi, kisha ntateremsha na Epo juisi…

Mara ghafla ikasikika sauti ya mama yake “Hivi we Gulo kaka yako atakula nini na we umemaliza ugali na maharage yote?”

  1. Ndoa nyingine

Mtaani kwetu kuna jamaa mmoja anaitwa chogo, ana mtoto mmoja anaitwa “emma” pamoja na mke wake.. leo bwana katoa kali; Alikua amekaa nje ya nyumba yake kwenye kibalaza, alikua ameshikilia cheti cha ndoa yake.. akanza kukitazama sana, ikafika kipindi mke wake ikabidi avunje ukimya na kumuuliza “Baba emma, mbona unakitazama sana hicho cheti..?” bwana chogo akajibu huku akilia, akitoa sauti ya upole “NATAFUTA EXPIRE DATE YA HIKI CHETI CHETU..” Mke wake hoi akazimia…!

Soma Stori 2 Fupi za Vichekisho (Vunjambavu)

KIKUNDI CHA WATALII kilitembelea mto wa kufugia mamba na walikuwa wakielea kwenye meli ndogo katikati ya mamba wenye njaa. Ikasikika sauti ya mmiliki wa eneo hilo ikisema: “Atakaye ruka kwenye maji na kuogelea kutoka nje atazawadiwa dola milioni 10”. Kila mtu kimya, ghafla mwanaume mmoja akajirusha majini. Alikimbizwa na mamba kwa bahati nzuri alitoka salama. Akatangazwa mshindi. Wakati anarudi hotelini na mkewe akamwambia mkewe “Aisee sijajirusha mwenyewe majini, kuna mtu alinisukuma nikapambana niokoe maisha yangu”. Mke wake akatabasamu na kusema “Ni mie ndio nilikusukuma”. Wewe ungemfanyaje kama ni mkeo? Anyway, “Nyuma ya kila mwanaume mwenye mafanikio kuna mwanamke anayemsukuma kufikia mafanikio”.🤣🤣🤣

UMEMUAGA mkeo unaenda kazini, ukapita kwa mchepuko wako, wakati unajimwaya-mwaya na mchepuko, mume wa mchepuko akagonga mlango, ikabidi ufichwe uvunguni mwa kitanda.
Wakati bado upo uvunguni ka mchepuko kakamuaga mume wake kwamba, kanaenda saloon, mume wa ka-mchepuko naye akaona ndo muda wa kuita mchepuko wake, akauita ukaja, wakajimwayamwaya kwa sana muda huo wee bado upo uvunguni. Mara mchepuko wako akarudi kutoka saloon, akagonga mlango, ikabidi mume wa mchepuko wako aufiche uvunguni mchepuko wake.
Kucheki hivi kumbe mchepuko wenyewe ndo mke wako uliyemuaga unaenda kazini, kwa hiyo wewe na mke wako wote mkawa mmefichwa uvunguni…Ukisikia vita ya tatu ya dunia, ndo hii sasa.