Tag Archives: usafiri wa anga

Usifanye mambo haya ukiwa Dubai

Dubai ni mji maarufu duniani unaovutia watalii kutoka kila pembe ya dunia. Una mandhari za kuvutia, teknolojia ya kisasa, utajiri na ni mahali panapopendwa sana na watu. Lakini, kama ilivyo kwa miji mingine mikubwa, kuna sheria, desturi, na kanuni za kipekee ambazo wageni wanapaswa kuziheshimu. Kutozingatia mambo kama hayo ukiwa Dubai, kunaweza kusababisha usumbufu au matatizo makubwa hatakama ni mgeni.

Kama mgeni unayeitembelea Dubai kwa mara ya kwanza, ni muhimu kujua mambo unayotakiwa kujiepusha nayo ili kuhakikisha safari yako ni ya kufurahisha na sio matatizo. Mji huu una mchanganyiko wa mila za Kiislamu na tamaduni za kisasa, ambazo zote zinahitaji heshima kutoka kwa wageni wake. Kutokujua sheria za msingi kunaweza kusababishia migogoro isiyo ya lazima.

Katika makala hii, tutakupa mwongozo wa mambo unayopaswa kuepuka unapokuwa Dubai. Kwa kuzingatia mwongozo huu, utakuwa na fursa ya kufurahia safari yako bila wasiwasi na kuonyesha heshima kwa wenyeji wa mji huu wa kuvutia.

Jinsi ya kupata Ticket za ndege za bei rahisi BONYEZA HAPA>>>

Mambo Usiotakiwa Kufanya Ukiwa Dubai

Usile hadharani kipindi cha Ramadan


Kipindi cha Ramadan ni takatifu kwa Waislamu, na kula, kunywa, au kuvuta sigara hadharani wakati wa mchana ni marufuku kwa wote, wakiwemo wageni. Ni muhimu kujizuia na kuheshimu ibada ya kufunga kwa wenyeji. Kama ukiwa katika mji huo kipindi cha Ramadan, basi kuwa mtulivu na ufuate utaratibu wao.

Usilale na mpenzi wako chumba kimoja kwenye baadhi ya hoteli

Hoteli nyingi katika Dubai zina sera zinazofuata sheria za Kiislamu, na wanandoa wasiooana hawaruhusiwi kulala chumba kimoja. Hakikisha unafahamu sera za hoteli kabla ya kufanya malipo. Kuna hotel nyingine huruhusu wageni kulala pamoja hatakama hawajaoana na ndio unapaswa kuzitumia ili kuepuka usumbufu.

Kunywa pombe hadharani

Ingawa pombe inaruhusiwa lakini ni kwenye maeneo maalum kama baa na hoteli zinazoiruhusu. Kujiachia na kunywa au kuionyesha hadharani kunaweza kusababisha matatizo makubwa, ikiwa ni pamoja na faini au kifungo. Swala hili linatakiwa kuzingatiwa kila siku na sio siku za Ramadan tu kama ilivyokua kwenye kula.

Kusalimia kwa kutumia mkono wa kushoto

Katika tamaduni za Kiarabu, mkono wa kushoto unachukuliwa kama mchafu, na hivyo ni vyema kutumia mkono wa kulia unapotoa au kupokea kitu, au hata kusalimiana. Fanya havyo maana Dubai ina utamaduni wa kiarabu na nivema ukauheshimu unapokuna wenyeji.

Hatumaini hayo wamekupa mwanga na mwongozo juu ya jinsi gani unatakiwa kuwa au kufanya huko Dubai. Mbali na kuyajua hayo, ni vema ukawa chini ya mtu mwenyeji atakea kusaidia kujua zaidi mambo ya kufanya katika mji huo ili kuhakikisha haukosei.

Jinsi ya kupata Tiketi za Ndege za bei rahisi

Unapokua na mpango wa safari mbele yako, unaweza kuwa na uwanja mkubwa wa kuchangua ni usafiri gani utaoutumia kwenye hiyo safari. Lakini hiyo safari ikiwa ni ndefu, usafiri wa anga ndio unaweza kuwa ni chaguo sahihi kwako. Katika usafiri wa anga, kupanda ndege kutaokoa sana muda wako ambao ungeupoteza kwenye vyombo vingine vya usafiri kama vile Gari au Meli. Kwa mfano; Ukiwa na safari inayokuchukua masaa mengi au siku nzima kwenye gari, katika ndege safari hiyo inaweza kukuchukua Dakika au masaa machache sana.

Kwaiyo, pamoja na kwamba kusafiri kwa ndege huonekana kama ni gharama sana, Bado ni chaguo zuri kwasababu huokoa muda. Ndani ya dakika au saa unaweza kuwa umefika katika sehemu unayohitaji kuwa. Na hii ndio Sababu kubwa ya watu kutumia njia ya anga katika safari zao ukiondoa Sababu zao nyingine binafsi.


Sasa hapa chini kwenye ukurasa huu, tunaenda kufungua ubongo wako juu ya jinsi gani wanaweza pata ticket za ndege za bei rahisi ili usafiri bila kutumia Pesa nyingi.

Tunazungumzia hilo kwasababu watu hupata ticket za ndege kwa bei tofauti tofauti. Kuna watu hulipia pesa nyingi kupata au kubook Ticket na pia Kuna watu hupata ticket hizo kwa bei rahisi. Na ikiwa wewe unahitaji kupata Ticket za ndege kwa bei rahisi, tumia njia hizi chini.

Unaweza kubook ndege kwa App ya M-Pesa BONYEZA HAPA>>>

Njia ya kupata Tiketi za ndege za bei rahisi

Tafuta Tiketi Mapema

Ukihitaji Tiketi za ndege za bei rahisi, njia moja ya kuzipata ni kuwahi kuzitafuta. Yani tafuta Tiketi za ndege angalau hata mwezi 1 kabla ya safari yako. Mara nyingi Tiketi za ndege huwa zinakua bei rahisi kama siku ya kusafiri ipo mbali. Alafu tena bei huwa inapanda kadri siku ya kusafiri inapokaribia.

Kwaiyo kuwahi kuzitafuta tiketi kunaweza kukusaidia wewe kulipia pesa kidogo. Hii itakusaidia kuokoa pesa zako hasa kwenye zile safari zisizo za dharura.

Linganishia Bei za Ticket

Kama unasafari ya kwenda mahali flani, fahamu kuwa una uwanja mpana wa kuchagua ndege utayoitumia iwe ya shirika gani na hata ticket utaipata sehemu gani. Mashirika ya ndege yanaweza tofautiana bei na hata sehemu unazoweza pata Tiketi zinaweza tofautiana bei pia.


Kwaiyo ni vema ukawa na tabia ya kuangalia Tiketi unayohitaji inapatikana katika sehemu ngapi na tofauti ya bei Iko vipi. Alafu baadae uchague ambayo ni bei rahisi kwako na ulipie.

Kwasasa mtandaoni kuna tuvuti nyingi za kulinganisha bei za Ticket za ndege kwa wanao book ticket mtandaoni. Mfano mzuri ni hii iitwayo Skyscanner

Tumia Ofa au Punguzo

Kuzingatia Ofa au Punguzo kunaweza kukufanya upate ticket za ndege kwa bei rahisi pia. Punguzo la bei au Ofa zinaweza tokea kwenye mashirika ya ndege au tuvuti za ticket kwaajili ya kuvutia wateja wao.

Ukizingatia mambo kama hayo, unaweza kujikuta unaokoa pesa yako kwenye baadhi ya safari zako za ndege. Nasema hivyo kwasababu Ofa na Punguzo, mara nyingi hufanya ulipie pesa kiasi kidogo kuliko ambayo unapaswa kulipia kikawaida.

Safari siku au misimu isio na mambo mengi

Kama ulikua haujui, basi leo fahamu kuwa Bei za tiketi huwa juu wakati wa likizo, mwisho wa wiki, na kipindi cha msimu wa sikukuu. Kwaiyo ukihitaji kupata Tiketi za ndege zinazosafiri katika wakati huo, utalipia kiasi cha pesa kinachoweza kuwa cha juu kuliko kawaida.

Kusafiri siku za katikati ya wiki na vipindi vingine mbali na msimu wa sikukuu, kutakufanya upate ticket za ndege kwa bei rahisi. Hii ni kwasababu muda huo Tiketi huwa katika bei ya kawaida.

Natumaini mambo au njia hizi zitakusaidia katika kupata Tiketi bila kutumia Pesa nyingi. Kikubwa unatakiwa kuwa makini sana unapokata Tiketi ili kuepuka usumbufu unapotaka kukamilisha safari ulioipanga.

Unaweza book ndege kwa app ya MPesa?

Moja ya app zinazotupa uwezo wa kufanya miamala ya kifedha katika viganja vyetu ni app ya Mpesa. App hii ni kwaajili ya watumiaji wa Vodacom. Moja ya faida za kutumia app ya Mpesa kwa mtumiaji wa Vodacom ni kwamba hata laini voda ikiwa haipo hewani au imepotea, unakua umebaki na uwezo wa kufanya miamala kwenye app hiyo kwa kutumia internet ambayo haihusiani na laini yako ya voda.  

Kuna baadhi ya watu wamekua wakiuliza juu ya kubook ndege za usafiri kwenye app ya Mpesa na hapa tunaenda kuangalia kuhusu hilo. Kama na wewe unahitaji kujua juu ya hili basi hapa unaweza pata mwanga.

Kubook ndege kwa app ya MPesa

Unaweza book ndege kwa app ya MPesa?

Ndio, inawezekana. Precision Air na Vodacom waliungana na kukuletea uwezo wa kubook ndege kwenye simu yako kupitia app ya Mpesa. Kwa sasa app ya Mpesa inavipengele vingi ikiwemo kipengele cha kubook ndege za usafiri. Precision Air wamekiri kuwa huduma ya kubook ndege kwa app ya Mpesa ni huduma rahisi na haraka kwa watumiaji. Na pia moja ya kitu kizuri kuhusu kubook ndege kupitia app ya Mpesa ni kwamba unapata punguzo la asilimia 20  ambayo inaokoa karibu robo ya pesa yako. Kwaiyo tunaweza sema pia hii ni njia ya kupata tiketi za ndege kwa bei rahisi.

Kipengele cha kubook ndege kwenye app ya MPesa

Ukifungua app ya Mpesa unaweza kiona kipengele cha kubook ndege maeneo ya chini kikiwa kimeandikwa “Book Flights”. Kama umeangalia chini na haujakiona, mbonyeza sehemu ilioandikwa “Services” alafu ukisha fanya hivyo utapelekwa kwenye orodha ya huduma na utaona kipengele kinachoitwa Book Flights kwenye orodha hiyo. Ukifungua kipengele hicho utakutana na ukurasa huu chini kwaajili ya kutafuta na kubook ndege itakayofanikisha safari yako.

Asante kwa muda wako, Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy na usisahau kutembelea kila mara kupata vitu vipya.