Tag Archives: Swahili

Mazoezi ya kupunguza tumbo au kitambi (rahisi unafanya hata nyumbani)

Tumbo au kitambi imekua ni tatizo ambalo baadhi ya wanaume na wanawake hukumbananalo katika miili yao. Tukitungunzia kitambi katika mwili wa mwanadamu ni mafuta ambayo hujikusanya katika maeneo ya tumbo na kulifanya tumbo kuonekana limeongezeka ukubwa. Mara nyingi kitambi huibuka katika mwili wa mtu kutokana na mlo wa mtu mwenyewe au staili ya maisha yake kiujumla. Mazoezi ni njia salama na ya bure ya kuepukana au kuondokana na kitambi.

Kunawatu huwa wanashindwa kutumia njia hii na kufanikiwa kupunguza kitambi kutokana na kutarajia matokeo ndani ya siku moja au mbili. Ukiwa na mawazo hiyo kichwani hautaweza kufanikiwa kupunguza kitambi kwa njia ya mzaoezi maana matokeo huwa yanachukua muda. Yanaweza kuaanza kuonekana zaidi baada ya siku 30(mwezi).

Ukitaka kufanikiwa kirahisi, kichwa chako kiwe kinaelewa kwamba mazoezi unayoanza kufanya hayapunguzi tumbo tu, yanakufanya uweunacheza mchezo wa kitandani vizuri na kwakuchangamka, utachangamka pia katika shughuli zako nyingine tena utaepukana baadhi ya magonjwa. Ukifanya mazoezi vizuri kwa siku 7 tu unaweza anza kuona faida hizo nyingine hatakama tumbo halijapungua. Ni vema ukafanya mazoezi kuwa ni tabia yako tu ili faida zake uwe unazifurahia kila siku katika maisha yako.

Hapa chini tunashusha mazoezi matatu tu ambayo unaweza kuanza kuyafanya kila siku ili kupunguza kitambi au tumbo. Mazoezi haya ni kwaajili ya wanawake na wanaume pia. Yanaweza fanyawa hata nyumbani tu na kama hauna muda maalum wa mazoezi unaweza tafutiza dakika chache kila siku kabla haujaingia kuoga, ukayafanya. kwasiku za mwanzo unaweza pata maumivu kutokana na mwili kutozoea mazoezi lakini usikate tamaa, endelea kufanya tu maana maumivu huisha na hukuacha ukiwa imara zaidi.

Mazoezi matatu ya kupunguza Tumbo au kitambi (Mwanawake na Mwanaume)

Zoezi la kwanza

Tafuta sehemu nzuri na safi ambayo itakuruhusu kulala chali bila tatizo. Nenda katika sehemu hiyo kisha ulale chali. Nikisema “kulala chali” namaanisha kulala kwa kuangalia juu. Baada ya kulala chali hapo chini, kishike kichwa chako kwa mikono yako yote miwili alafu ukiwa hivyo hivyo, anza kujinyanyua kiwiliwili na kichwa juu alafu unarudi chini. Endelea kwenda juu na chini, juu chini bila kuibandua miguu yakochini. Angalia mfano katika picha hii;

Image:Giphy

Zoezi la pili

Katika zoezi hili, hatua ya kwanza ni kuchuchumaa chini. Baada ya kuchuchumaa nyoosha mikono yako mbele alafu shika chini katika sakafu. Baada kufanya hivyo, anza kuitegua na kuivuta miguu yako yote miwili kwa nyuma bila kiwili wili kugusa chini alafu irudishe tena miguu kama ilivyokua. Endelea kuifanya hivyo miguu kama inavyoonekana katika picha hii.

Image:Giphy

Zoezi la tatu

Kwenye zoezi hili utatakiwa kuanza kwa kulala chali kama katika zoezi la kwanza. Lakini baada ya kulala chali utatakiwa kuwa unanyanyua miguu yako yote miwili, wa kushoto na wakulia na kulileta juu kwa pamoja alafu unairudisha Tena chini. Endelea kufanya hivyo kwa kurudia kwenda juu na chini. Unaweza angalia picha ili kuelewa zaidi.

Image:Giphy

Magemu mazuri ya mabasi kucheza kwa simu za Android

Magemu ya mabasi yamekua ni kati ya magemu pendwa sana kipindi hiki. Magemu haya yapo mengi sana na watu huyacheza kupitia simu, pc na baadhi ya vifaa vingine kama hivyo vinavyo tuwezesha kucheza magemu. Katika makala hii tunazungumzia magemu mazuri ya mabasi lakini tutajikita katika upande wa simu za Android hivyo kama wewe ni mtumiaji wa simu yoyote ya Android, unapenda na kutaka magemu mazuri ya mabasi, hii ni kwaajili yako.

Kutokana na wingi wa magemu ya mabasi kwa simu za Android, inaweza kuwa ngumu kwa mtu kujaribu kila gemu ili kujua lipi ni zuri na lipi ni baya kwake ingawa unaweza fanya hivyo pia. Hapa sisi tunakupa orodha ya magemu macheche ya mabasi ambayo ni mazuri unayoweza kuyacheza katika simu yako na yanachezwa na watu wengi duniani. nafikili hii inaweza kukusaidia katika utafutaji wa gemu zuri kwako.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Magemu ya mabasi za kucheza kwenye simu za Android(5)

1. Bus simulator 2023

Katika magemu ya Android mazuri ya nayohusiana na uendeshaji wa mabasi, kunage hili linaitwa “Bus simulator 2023”.Bus simulator 2023 ni gemu la mabasi lililotoewa na Ovidiu Pop kwa simu za Android pamoja na iOS. Lilinakutupa katika ulimwengu ambao unakua ni deleva wa mabasi na kuna modes nyingi unaweza kuwa unafurahia humu ndani. Unaweza kucheza na marafiki aua watu wengine online na pia kwenye upande wa muonekano uko poa. Asilimia kubwa ya watu waliolicheza gemu hili,wamelipenda kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo muonekano.

2. Bus simulator indonesia

Kama ni mfuatiliaji mzuri wa The bestgalaxy unawezakuwa umegundua kuwa gemu la Bus Simulator Indonesia tumeliongelea zaidi ya hapa. Hii ni kwasababu nigemu zuri sana na usioweza kuyaacha unapozungumzia magemu ya simu ya kuendesha mabasi. kwasasa gemu la Bus simulator indonesia imeishaingizwa kwenye simu na watu zaidi ya milioni 100 kutoka sehemu mbalimbali za dunuia. Mazingira na mabasi ya katika gemu hili ya yanaendana na mabasi na maingira halisi ya huko Indonesia. Muonekano wa gemu hili ni mzuri na pia uzuri mwingine wa gemu hili ni hutohitaji kutumia data/internet katika kulicheza ingawa ukihitaji kucheza na watu au marafiki, utahitaji kuwa na muunganiko wa internet(data).

3. Coach Bus Simulator

Hili ni gemu la mabasi ambalo mpaka sasa watu zaidi ya milioni 10 wamelipakua katika vifaa vyao vya Android OS. Ndani ya gemu hili mchezaji unaendesha mbasi ya abilia ya masafa kuwatoa sehem moja kwanda nyingine. Na ukiwa kama dereva wa mbasi unakumbana na changamoto mbalimbali katika kazi yako unapokua barabaradi. Linamuonekano mzuri. Ovidiu Pop ndio waliotoa gemu hili na linapatikana bure kabisa kwa watu wote wanaohitaji kulicheza katika Android. Unaweza kulipakua kupitia Playstore na ukaanza kufurahia kulicheza kila siku bila kutumia data(Ni gemu la Offline).

4. Bus simulator ultimate

Katika mwaka 2019 “Zuuks Games” walitoa gemu la Bus Simulator Ultimate na toka hapo mpaka sasa kuna mamilioni ya watu wamepakua gemu hili na wanaendelea kulicheza. Zuuks Games walisema gemu lao la bus simhlator limekua ni miongoni mwa magemu ya mabasi yaliopakuliwa na watu wengi… limeshafikisha zaidi ya watu milioni 200. idadi hiyo ya watu inajumuisha watu kutoka US,UK,Canada na sehemu nyingine yingine nyingi za dunia, ikiwemo Tanzania. Unaweza kulidowmload au kulipakua gemu hili bure ila kulicheza utahitaji kutumia data(internet).

5. Public Transport Simulator C

Gemu jingine zuri la mabasi kwa upande wa Android ni hili linaitwa Public Transport Simulator C. 2019 ndio mwaka SkisoSoft walilitoa na tokalitolewe mpaka sasa limechezwa na zaidi ya watu milioni 50. Kutokaa na uzuri wake asilimia kubwa ya watu wanaolidownload na kulicheza wanalipenda na hii imeionesha kupita reviews ambazo zimekua zikitolewa na wachezaji wa game hili katika Playstore. Pamoja na kwamba gemu hili limetolewa mwaka 2019 lakini bado linaendelea kuboreshwa na hupata updates kila baada ya muda flani… Lakini jambo hili halifanywi kwenye gemu hili tu, hufanywa kwenye mgemu mengine. Kiufupi ni kwamba magemu yanaboreshwa Kila siku na Unaweza ona Gemu ni baya Leo lakini baada ya mwaka likawa limeboreshwa na kuwa zuri.

Mbali na magemu haya unafikili ni gemu gani lingine zuri kwa upande wako? Huu ni mwisho wa orodha yetu,, usiache kuwa kalibu nasi…

SMS nzuri za kumtumia mpenzi wako asubuhi

Asubuhi ni mwanzo wa siku na kuianza siku vizuri kunaweza kuwa ni pamoja na kupokea sms ya maneno ya upendo toka kwa watu tunaowapenda. Kumpa maneno mazuri ya upendo mpenzi wako wa moyoni anaekupenda kunaweza kufanya aifurahie siku nzima na pengine kufanya aendele kukuamini kwamba unamjali, upo yupo kichwani mwako na unamuwaza huko uliko. Hivyo kama unataka kufanya jambo hili, tambua kuwa hizo ni kati ya faida zake katika mahusiano. Na kama unahitaji sms za maneno mazuri za asubuhi zitakazo mgusa roho mpenzi wako, unaweza ukoa muda kwa kuangalia sms fupi ziliopo hapa chini zitakazo endana na hali ya penzi lenu.

Mambo ya kuepuka katika mahusiano BONYEZA HAPA>>>

SMS za asubuhi njema kwa umpendae

Asubuhi njema… Natamani siku ya leo tungeamka kitanda kimoja na wewe. Tena sikufichi, huku niliko nakosa vitu vingi sana kwasababu niko mbali na wewe mpenzi wangu… Ila nikikumbuka kuwa unanipenda na pia nakupenda, moyo wangu unatulia kidogo na kusubilia siku tutakayoonana ingawa naona kama nachelewa kukutana na wewe malaika wangu, nakupenda sana.

Upendo ni zawadi ya pekee sana mungu aliyoiweka ndani ya mioyo yetu bure na mimi nimeitumia vema sasa zawadi hii kwa kukupenda wewe. Nakupenda sana na sijawahi jutia kukupenda mpenzi wangu. Asubuhi njema wangu.

Sms za kumfanya mpenzi wako afurahi BONYEZA HAPA>>>

Kuna mtu mmoja mzuri, anaakili sana, mkarimu na nampenda saaaana, yupo anaisoma sms hii niliomtumia pekeyake asubuhi hii. Ameuteka moyo wangu na sihitaji kuunasua maana anaupa raha kwa penzi lake, Asubuhi njema kwake.

Natumai ulikuwa na usingizi mzuri sana. Tafadhali amka sasa kwa sababu asubuhi yangu haiwezikamilika kujua hali yako wewe. Habari ya asubuhi mpenzi!

kila siku huwa nawaza kukusu wewe na mapenzi yetu kiujumla… nimegungua najifunza vitu vingi sana toka kwako, pia upendo wako unaboresha maisha yangu na kunifanya niishi kwa furaha sana. Asante kwa kuwa mimi, nimekuweka moyoni, nakupenda na nazidi kukupenda kila siku mpenzi wangu, Asubui njema kwako.

Natumai umelala kama malkia. Sasa tafadhali amka kama nyota na utawale ulimwengu wangu kwa siku ya leo tena. Habari za asubuhi!

Katika penzi letu kunamuda tunagombana alafu tunapatana. Hii isije kukufanya uamini kuwa sikupendi. Kama jinsi jua linavyo chomoza asubuhi hii na kuleta mwanga palipo na giza ndivyo uwepowako unaleta furaha kwenye maisha yangu. Nakupenda sana na najivunia kuwa na wewe…. Nakutakia asubuhi njema wangu.

Tunapitia vitu vingi katika penzi letu lakini sijawahi jutia kukupenda wala kuwa na wewe kwenye penzi. Mimi huwa naamini mimi ni Mfalme na wewe ni Malkia katika safari ya maisha na penzi letu, naamini unanipenda na nakupenda sana. Nakutakia asubuhi njema na siku yenye furaha.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>

Leo nimeamka nikiwa na mawazo yako tu akilini mwangu. Huwezi amini nilivyo kumiss hapa. Siezi kufurahia asubuhi hii nzuri bila wewe mpenzi wangu. Amka!

Najisikia kubarikiwa sana kila asubuhi ya maisha yangu ninapojua hali yako ni salama. Umeamka poa?

Jinsi ya kumueleza hisia zako Mwanaume bila kusema unampenda

Kuna mtaalam mmoja wa mambo haya alisema hivi…

Mara nyingi kuwa na aibu ndio chanzo cha wanawake wengi kushindwa kuwaeleza hisia zao kwa wanaume wanao wahitaji na kibaya zaidi wanawake tunaweza kutunza siri zetu kwa muda mrefu hivyo, hutunza pia hizo hisia kama siri nyingine japo hutuumiza sana pale wanaume tunaowapenda  wanapoenda kwa wanawake wengine.

Wapo baadhi ya wanawake ambao hawana uoga katika kueleza hisia zao kwa wanaume na pia huwa huru pindi wanapokuwa karibu na wanaume. Lakini wanawake wengi ni sisi ambao tunashindwa hata kuongea pindi tunapo wakaribia wanaume tunaowapenda.

Sio kwamba tunakosa ustadi wa kimapenzi wa kimapenzi au hatujui kutamka maneno ya kueleza hisia zetu ila ni tunasikia raha na furaha inayotuzidi mpaka tunaogopa maana mapigo ya moyo hupiga kwa kasi na maneno yote hupotea na hurejea baada ya mwanaume uondoka.

Kuwa na aibu hakupaswi kukuzuia kumueleza mwanaume unayempenda hisia zako. Kuna mambo madogo madogo ambayo unaweza kuyafanya na ukafanikiwa kufikisha ujumbe wa hisia zako kwa mwanaume unayempenda lakini kitu cha msingi inatakiwa kujiamini tu.

Badala ya kumfuata na kumwambia mwanaume vile unajiskia juu yake unaweza tumia njia ya vitendo itakayo mfanya kukuzingatia na kuelewa kuwa unamuhitaji na utamfanya akuhitaji pia.

1.Wasiliana nae kwa macho.

Kuwasiliana kwa macho ni moja wapo ya njia rahisi na ya hila zaidi ya kumruhusu mwanaume ajue kuwa unavutiwa naye. Wakati mwingine wazo la kuwasiliana na mtu usiempenda linaonekana kuwa la kichefuchefu, lakini ikiwa unafikiria ni mzuri, muangalie. Kama ni muoga sana basi jaribu kuangaliana na picha yake kwenye simu yako. Usimtazame kama wewe ni polisi na yuko kwenye orodha ya watu wanaotafutwa. Mtazamo mfupi ndio unahitajika yaani muangalia mpaka ugonganenae macho na agundue ulikua unamungalia kisha acha kumuangalia na uiangalie sehemu nyingine (ila usingalie chini kamwe) huku ukiendelea na shughuli zako. Kitendo hiki ukiwa unakifanya kitamfanya ahisi kitu juu yako na anaweza kuanza mawazo ya upendo juu yako.

Katika Matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi (Unaweza juta!) GUSA HAPA>>>

2. Weka tabasamu.

Pindi unapomuangalia hakikisha anakukuta na tabasamu zuri la kupendeza. Sio anakukuta unamuangalia huku umeweka sura ya kawaida tu utamfanya asihisi chochote juu yako na akakuona ni mtu unaemfuatilia mambo yake hivyo hakikisha unaweka tabasamu zuri litalomuonesha kufurahishwa na yeye. Akikukuta katika hali hii moja kwa moja atagundua umevutiwa nae.

3. Muulize swali kuhusu jambo flani.

Hii ni njia nzuri sana kwaajili ya kuanzisha mahusiano kati yenu.

Kuuliza swali kuhusu jambo flani au kuomba usaidizi juu ya jambo flani. Unaweza muuliza mwaswali ambayo yatamfanta ajibu kwa urefu au atumie muda wake kukuelekeza.

Mfano: Eliy, nimependa wallpaper ya simu yako, naomba nielekeze jinsi ya kuweka wallpaper kama yako?

Naomba nielekeze jinsi ya kufanya kitu hiki?

Njia hii pia utakusaidia kuanzisha mazungumzo nae yaani pale unapokosa neno la kuongea au kuanza mazungumzo basi unaweza uuliza kuhusu kitu flani.

Mbinu 6 zitakazo kusaidia katika mapishi yako GUSA HAPA>>

4. Mtege kwa kujichezesha.

Kila mwanamke anavitu ambavyo anajua vinamshawishi zaidi mwanaume katika mwili wake. Vitu hivi vinaweza kuwa ni lips nzuri, macho na vinginevyo. Vitu hivi unaweza vitumia pale ambapo unakuambele ya macho yake au unapogundua anakuangalia. Kuvitumia vitu hivi kunaweza kumchanganya mwanaume kisawa sawa mpaka akashindwa kuongea na kumfanya avutiwe na wewe zaidi.

 Mfano, unaweza zichezesha lips zako pindi anapokuangalia na kukuelekeza kitu fulani ulicho omba akuelekeze.

Kwakufanya vitendo Kama hivi kutachochea hisia zake kwako.

5. Toa maoni juu ya kile unachokiona kwake na pia usisahau kumsifia na kusifu anavyovipenda.

Kila mtu anapenda kusifiwa na  sikuzote watu huwapenda watu wanaowasifu pia unachotakiwa kujua ni kwamba  wanaume wengi huongeza juhudi katika jambo fulani pale wanaposifiwa yaani kama ni mchezaji mpira alafu ukawa unamwabia kuhusu uchezaji wake mzuri wa mpira basi utamfanya ajiskie vizuri mpaka ataanza kukualika mazoezini ili tu umuone anachokifanya na umsifie tena. Hivyo basi kumsifu inaweza kuwa njia nzuri ya kufanya avutiwe na wewe.

6. Usichukue vitu kibinafsi.

Ikiwa umemfanyia yote hayo na bado haoneshi matokeo mazuri juu yako, Usihisi kuwa wewe ni mbaya au hunamvuto. Huenda haoneshi dalili nzuri juu yako kwasababu hataki kukuchezea hivyo unapaswa kuheshimu pia mawazo yake na kuendelea na maisha yako huku ukimtafauta anaekupenda kwa dhati. 

”kwanini wanawake wazuri/warembo hawaolewi?” sababu zinaweza kuwa hizi

Mara nyingi wanawake warembo na wenye mvuto wa kumvutia kila mwanaume huishia kuzisikia ndoa kwa wenzao tu kutokana na sababu mbalimbali.

Wengi huwa na tabia ambazo huudhi na huwaogopesha wanaume wanaowahitaji bila wao wenyewe kujijua.

Ivi unaweza kuchagua kuwa na kitu chenye muonekano mzuri maishani mwako kitakachokupa shida na maumivu milele?

Ikiwa watu hushindwa kuvumilia kuishi na vidonda vinavyowapatia nyumba, magari na pesa, unafikiri urembo/uzuri unaweza kuwa na nini cha ajabu kwenye maisha?

Wanaume huwa sio wajinga na katika asilimia kubwa ya wanawake wanaoolewa huwa ni wanawake wa kawaida sana ukiwaangalia kwa macho jinsi walivyo, mpaka unakuta wengine wanajiuliza “mbona kamchagua mwanamke wa kawaida sana pamoja na malizote zile?”

Ukiwa mrembo/mzuri utapendwa na wanaume wengi ila watakupenda kwa lengo la kupata Penzi tu, baada ya hapo utakuwa wa kuchezewa na baadhi ya sababu zinazopelekea wanaume kufanya hivyo ni zifuatazo;

Tabia

Wanawake kama hao huwa na tabia mbaya na nikiongelea tabia mbaya basi najumuisha uvaaji, ukaaji, viwanja vya starehe, lugha zisizo nzuri na marafiki pia. Vitu hivyo humtenganisha mwanamke mzuri na wanaume wa oaji. Labla akutane na mtu wa tabia yake lakini asilimia kubwa ya wanaume wenye tabia hizo huwa wanatafuta wanawake waliotulia huku wakiendelea wanawake warembo wasio tulia. Wanaume wengi huwa hawapendezwi na tabia za aina hiyo hata mwanamke awemrembo kiasi gani.

Kuwa na maringo sana

Unakuta mwanamke ameweka kucha ndefu, nzuri,za kuvutia na anamaringo kiasi kwamba mwanaume mwenye mpango wa kuoa akimuona anajiuliza 

“Sasa kwa hizi kucha atanifuliaje nguo?… Anamaringo sana sijui itakuaje tukipishana?… Anaanzaje kuosha vyombo?… Ivi atakubali kutulia na kulea mtoto?.. Inaonekana hata kupika hajui”

Mwisho mwanaume anaona hafai wala haoneshi tabia zozote za mwanamke ambae anatakiwa kukaa katika nyumba.

Katika Matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi (Unaweza juta!) GUSA HAPA>>>

Ghali kuwatunza

Wanawake warembo huwa ghali kuwatunza kwa sababu wamejiwekea dhana kuwa wanafaa kupelekwa katika hoteli kubwa kubwa na maeneo yaliyo na bidhaa ghali. Huwa hawalegezi msimamo hasa kuhusu mahitaji yao na wanakotaka kwenda kununua bidhaa.

Mwanaume akipiga hesabu za haraka haraka kuhusu ghalama ambazo anatumia kipindi cha ambacho yupo na mwanamke mrembo anaependa kulidhishwa kwa kufanyiwa mambo makubwa huwa anagundua kumuoa ni sawa na kubeba mzigo mzito sana kichwani.

Ni wabinafsi

Wanawake wa aina hiyo huishi wakifikiria dunia ni yao na kwamba wanafaa kuabudiwa na kila mwanamume. Wanaume wengi hupenda kuwa katika mahusiano nao na hii ndio sababu kubwa ya wanawake hawa kujiona wa hali ya juu sana.

Wasichojua ni kuwa wanaume huwatumia tu na kuwaacha kutokana na tabia zao ili kutafuta mwanamke mzuri wa kuoa. Kibaya zaidi ni kwamba, wanawake hawa huendelea kutiwa moyo na uzuri wao huku wakisahau kuwa umri walionao hauwasubiri.

Hawataki kuwa wazazi

Wanawake hao hupenda kusalia wakiwa wanapendeza, hivyo huwa wanaogopa kuzaa wasipate mikunjo, wasinenepe au kuwa na matiti kulegea. Kwa kawaida, hakuna mwanamume anayependa kuoa mwanamke ambaye hawezi kumzalia, hasa kwa sababu ya utamaduni wa Kiafrika. 

wavivu kutatua changamoto za mahusiano

Kuna wanawake ni warembo na wazuri sana kiasi ambacho wanaume huwafananisha au huwasifu kuwa ni kama malaika. Kutokana na kusifiwa sana hujiona wazuri sana na hupenda kuwa kama yai kwenye mahusiano. Ukweli ni kwamba hata uwe mzuri vipi, kuna changamoto utakutananazo kwenye mahusiano. Nikizungumzia changamoto inaweza kuwa umekuta mweza wako kabadilika ghafla au kunajambo limetokea katiyenu na linafanya musielewane. Wanawake wazuri wanapokutana changamoto hizi huwa hawajisumbui kutatua changamoto…. Wanaona bora kubadilisha mwanaume kuliko kutafuta njia inayoweza rekebisha mahusiano yao hatakama wao ndio chanzo cha kuyumbisha mahusiano. Hali hii inawafanya wawewanabadilisha tu wanaume na hawafikii hatua ya ndoa… Na hata wakiingia kwenye ndoa huwa sio wavumilivu maana ndoa inachangamoto nyingi zaidi.

Sasa kama una sifa za aina hiyo, huenda ni wakati wako kubadilika ikiwa unataka kupata mume. 

Fanya haya baada ya kondomu kupasuka katika tendo

Mpira wa kondomu hutumika katika tendo la kujamiiana ili kuzuia mimba na vile vile hutumika kwa lengo la kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi na magonjwa mengine ya zinaa. 

Katika utumiaji wa mipira ya kondomu kupasuka kwa kondomu hutokea mara nyingi Sana bila kutarajiwa. Mara nyingi kitendo hiki husababisha mimba zisizotarajiwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa. Hapa kuna hatua nne unazoshauriwa kuzifuata iwapo kondomu imepasuka:

1. Kuwa mtulivu na tafuta kondomu hiyo iliopasuka.



Mara nyengine kwa mwanamke vipande vya mpira huo wa kondomu vinaweza kuingia ndani ya mwili.

Ingiza vidole vyako ndani ya mwili, vishike na kuvitoa nje.

Mipira ama vipande vya kondomu vinavyosalia ndani ya mwili wa binadamu vinaweza kusababisha hasara hivyobasi ni muhimu kuangalia na kuhakikisha kuwa umetoa kondomu yote.

2. Tumia dawa za kuzuia kushika mimba iwapo hamjakubaliana kupata mtoto(Kwa mwanamke)



Dawa hizi zinapaswa kutumiwa katika kipindi cha saa 72 tu. Zinauzwa madukani yaani zinapatikana katika maduka ya dawa.

Iwapo huna mpango mbadala unaweza kutumia dawa za kupanga uzazi.



3. Kupimwa magonjwa ya zinaa hususan HIV iwapo hujui hali ya mwenzako




Nenda katika kituo cha dharura karibu nawe na umwambie daktari yaliofanyika.

Pia unaweza kuchukua dawa aina ya Post Exposure Prophylaxis (PEP) katika kipindi cha saa 72.

PEP ni mchanganyiko wa dawa za kukabiliana dhidi ya virusi vya ukimwi ambazo zinakuzuiwa kutoambukizwa HIV iwapo mwenzako ni mwathiriwa.

Kumbuka kwamba kila ugonjwa wa zinaa una muda wake wakati unapoambukizwa na wakati utakapoonyesha unapopimwa.

Unashauriwa kufanyiwa vipimo zaidi vya vya magonjwa ya zinaa baada ya mwezi na baada ya miezi sita ili kujua hali yako.



4. Jiulize kuhusu kilichosababisha na usirudie kosa.





Wapenzi wengi huruka hatua hii bila kujua kuwa hayo ni makosa makubwa, kwa sababu utakapoelewa ni kwa nini mpira huo ulipasuka ndipo unaweza kujiweka vizuri katika mchezo mwingine. Hivyobasi jiulize kuhusu hilo.

Vunja mbavu sms za vichekesho (soma hapa)

BANGE SIO CHAI..

Siku moja Nyani alikuwa kakaa kijiweni anavuta bangi,Mjusi(lizard) akaja akampa “Hi” akajiunga na kumuomba puff.

Nyani akamuonya kuwa ile bangi ilikuwa ni kali sana,ni kipisi cha kutoka Milimani huko. Mjusi akapokea wakaanza kuvuta bangi kwa raha zao…baada ya muda mjusi akawa hoi kwa stimu akamuambia nyani “Duh nasikia koo langu limekauka acha niende mtoni nikanywe maji!”

Mjusi kufika mtoni kwa kuwa alikuwa na stimu nyingi akatumbukia mtoni. Bahati nzuri Mamba alikuwa pembeni, akawahi kumuokoa mjusi na kumtoa nje ya maji.

Baada ya kumuokoa, Mamba akamuuliza mjusi “Ina kuwaje bro mbona umetumbukia mtoni kipuuzi vile?” Mjusi akajibu “Nilikuwa na nyani tunavuta bangi nikasikia kiu ya ajabu nikajikuta kwenye maji bila kujua!” Mamba akasema “Aaah wacha niende huko kwa nyani nikamuone.”

Mamba kufika akamkuta nyani ndo anamalizia kipisi chake,kazidiwa hata macho ni tabu kufungua. Mamba akamuita “Oya” Nyani akafungua macho,kumuona Mamba akashtuka Et”Duh! Mshikaji kwani umekunywa maji yote mtoni! Mbona umerudi mkubwa hivyo!!”

SIPATI PICHA INGEKUAJE…

Jamaa yangu mmoja alikuja kunitembelea kule Mburahati Madoto. Sasa wakati namsindikiza tukafika kituo cha madoto mwisho

kusubiri daladala. Mara jamaa yangu akanyewa na kunguru kichwani. Jamaa akaangalia juu alivyogundua amenyewa akamuona

kungulu usawa wake, jamaa akaangua kicheko sana yaani. Mi nilikuwa naona yote yanayotokea nikamuuliza “sasa unacheka nini

ndugu yangu wakati umenyewa?” Jamaa akajibu “We acha tu, afadhali bata hawapai angani kama kunguru”

AMRI KUMI KWA WAPENDAO OFA

  1. Muheshimu anayekununulia
  2. Muamkie mtoa ofa kabla hujakaa kitini
  3. Uwe ndie mchekeshaji wa kikao, lakini usimkatishe mazungumzo anaetoa ofa
    . Mtoa ofa akikutuma popote usikatae
  4. Mtoa ofa akiupenda muziki fulani, we anza kucheza kwa bidii kabisa
  5. Usinywe kwa pupa, kunywa mafunda madogomadogo
  6. Mtoa ofa akitoa kichekesho cheka sana hata kama hakichekeshi

Magroup ya WhatsApp ya kujiunga BURE

Hapa tutaangalia vikundi vya WhatsApp ambavyo unaweza kujiunga. Sote tunajua kuwa vikundi vya WhatsApp ni muhimu sana kwa sababu watu huvitumia kuungana na wengine na kushiriki habari fulani au kujadili mambo mengi. Lakini unahitaji kujua kwamba kila mtumiaji wa WhatsApp anaweza kuunda kikundi cha WhatsApp na kuongeza watumiaji wengine kwenye kikundi. Hii inamaanisha kuwa unaweza pia kuwa na kikundi chako mwenyewe cha WhatsApp na kukifanya kama Msimamizi.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kuunda kikundi chako cha WhatsApp?


Ni rahisi sana, unachohitaji kufanya ni kufungua programu yako ya WhatsApp kisha uguse nukta tatu. Baada ya kugonga nukta Tatu, utapata orodha ya chaguo chache. Chagua “New group” ili kuanza kuunda kikundi chako mwenyewe. Kwenye kuliunda utatakiwa kuwachagua watu watu unaotaka wawe kwenye group. Unaweza kuchagua wale watu wote unahitaji wawekwenye group lako lakini tambua kuwa sio mtu anapenda kuungwa kwenye group bila tahalifa. Hivyo ni vema ukawatahalifu watu unaotaka kuwaweka kwenye group juu ya group unalotaka kuwaweka kwanza.

Yafuatayo ni magroup ya WhatsApp ambayo unaweza kujiunga nayo

Hapa nakupa orodha za vikundi vya WhatsApp ambavyo unaweza kujiunga badala ya kuunda kikundi chako cha WhatsApp. Hivi ni vikundi ambavyo unaweza kujiunga na kutumia lugha ya Kiswahili katika kuchati.

Magroup ya Marafiki/Mahusiano

Magroup ya Biashara

Magroup ya Ajira/Kazi

Magroup ya Michezo & Burudani

Unapaswa kujua kuwa, vikundi vyote vilivyoorodheshwa hapa vina watu kutoka sehemu tofauti na hatuna uhusiano wowote nao. Kwa hivyo hakikisha kuwa kila wakati unakuwa mwangalifu na walaghai au wanachama wengine ambao wanaweza kukosa nidhamu.

Njia 3 za kutumia intaneti bila malipo kwenye simu ya Android au iPhone

Katika mabilioni ya watu wanaotumia internet ama mtandao kila mwaka na watu wengi kati yao wanaotumia Simu. Na siku hizi, watumiaji wengi wa simu wanatumia simu za Android na iOS. Mambo mengi ambayo watumiaji wa simu za Android au iOS wanapenda kufanya kwenye simu zao yanahusisha kutumia intaneti.

Wanatumia intaneti kwenye mambo kama vile kushiriki habari, kujifunza, kuendesha biashara zao, kupata burudani na zaidi. Kwa vile sote tunajua kwamba mtandao sio bure, inagharimu watumiaji kiasi cha pesa kununua bando za internet au kulipia huduma za internet. Lakini bado kuna nini cha kufanya ili kutumia wa internet bure kwenye simu.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>

Pata BAND0 kubwa la internet Kwa Bei rahisi GUSA HAPA>>>

Ikiwa wewe ni mmoja wa watu wanaotumia simu yoyote ya Android au iPhone na unahitaji kutumia intaneti bila malipo basi hapa chini kuna kinachoweza kufanya ili kupata intaneti bila malipo.

Njia za kupata intaneti ya Bure kwenye simu ya Android na iPhone


  1. Unaweza unganisha simu yako Kwenye huduma za Wifi za bure zinazopatikana kwenye mazingira yako… unaweza tafuta sehemu zilizio na huduma ya WiFi kitahisi kwa kutumia App yako ya Facebook. App ya Facebook inakipengele kinachokuonesha maeneo yenye huduma za WiFi katika eneo ulilopo.
  2. Unaweza pata ofa au zawadi za interneti ambazo hutolewa bure na kampuni inayokupatia huduma ya internet (mfano Tigo: Ukituma neno “BURE” au “Social bonus” kwenda Namba 15166 unaweza zawadiwa Mb za internet BURE..
  3. VPN pia inaweza tumika kupata internet bila malipo… lakini njia hii imewekwa hapa Kwa lengo la elimu tu na si vinginenyo. Unaweza soma moja ya makala zetu zinazohusisha njia hii HAPA>>>>>

Magroup ya WhatsApp ya kujiunga bure GUSA HAPA>>>

Maneno ambayo hautakiwi kusema kwa mwenza wako

Endapo umekwisha ingia katika mahusiano au unatarajia kuingia katika mahusiano ya kimapenzi, yapo mambo yanyofaa ambayo unaweza kumwambia mpenzi wako naye akafurahi, lakini yapo mambo ambayo kimsingi hupaswi kabisa kumwambia mpenzi wako. Kwani endapo utaamua kumwambia utatengeneza njia ambayo itawafanya mahusiono yenu yafe mara moja.
Maneno yafuatayo ni hatari kwa kuwa yanaleta madhara makubwa moyoni mwa mlengwa na ni vyema kuzuia kuyatamka kwa namna yoyote ile.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze Kila mara BONYEZA HAPA>>>

Maneno ambayo hutakiwi kuyasema kwa mwenza wako


1. Nakuchukia

Chuki ni kitu kikubwa sana, kwa kweli huwezi kuishi na mtu ambaye unamchukia. Hutakiwi kumtamkia mwenza wako neno hili. Unaweza kuchukia tabia yake lakini si yeye mwenyewe. Njia nzuri ni kusema kuwa “Nachukia au sipendi tabia yako ya kuchelewa kurudi nyumbani” au maneno yanayofanana na hayo.


2. Maneno ya matusi

Maneno kama “mjinga” au “mpumbavu” yasitumike kwa mwenza wako hata kama yana ukweli ndani yake. Japo ujinga ni kutofahamu kitu fulani lakini neno hili linaleta majeraha kama likitoka kwa mwenza. Hasa kama linatoka wakati wa ugomvi au kutofautiana.
Usiseme maneno mabaya yanayomshusha mweza wako mfano kuhusu mwonekano mbaya wa mwenza wako kama “sura mbaya”,”Mnene kama nguruwe” na maneno mengine kama hayo.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>


3. Kumfananisha tabia mbaya mwezi wako na wazazi wake.

“Tabia zako kama mama yako”, au “..kama baba yako” maneno yanayomfananisha mwenza wako na wazazi au familia anakotoka yanachokoza sana na huweka vidonga kwa muda mrefu moyoni na yaepukwe.


4. Acha! nitafanya mwenyewe

Katika mahusiano kusaidiana ni jambo la kawaida na muhimu, maneno mabaya ya namna hii yanamvunja moyo mweza wako kutaka kufanya jambo kwako siku nyingine na linaleta utengano na kuvunjika kwa upendo.


5. Maneno mabaya ya kukatisha tamaa

“Hutaweza” ,”Hutafanikiwa” n.k yanavunja moyo kwa mwenza wako na kurudisha nyuma maendeleo. Ni muhimu kwa wenza kupeana moyo na kusaidiana ili wote muende mbele kwa pamoja. Umoja ni nguvu.
Hivyo nikusihi ya kwamba kama kweli unataka kudumu katika mahusiano acha mara moja kumwambia maneno hayo, bali unatakiwa kumfariji kwa maneno mazuri yenye kuleta upendo wa kweli na kujenga hamasa ya kudumu

Magroup ya WhatsApp ya kujiunga bure GUSA HAPA>>>