Hapa chini The bestgalaxy nimekuandalia orodha ya app chache ambazo zinaweza kupa zawadi ya pesa kwa kufanya jambo flani dogo linaloweza kuwa jepesi kwako. Lakini kabla ya yote ufahamu kuwa pesa hizi ni ndogo sana na haziwezi kukufanya upate utajiri. Pia fahamu kuwa hizi app ni app ambazo hutoa pesa kama zawadi lakini sio app rasim kwenye upande huo. Hizi ni app rasmi katika upande wa kurahisisha upatikanaji wa huduma au mahitaji kirahisi. Yawezekana unazitumia kila siku. Kuna wakati tutazungumzia kuhusu platform rasimi kwa kutengeneza pesa nyingi.
Tunaweka app kwenye simu zetu kwasababu mbalimbali na moja kati ya sababu ya kuweka baadhi ya app ni kupata huduma au amahitaji kirahisi kwa kutumia simu. Mfano, kuna app ambazo tunaweka kwenye simu ili tuweze kupata huduma za kifedha kihisi kwenye simu zetu na pia kuna app hurahisisha manunuzi ya vitu kwa kutusogezea bidhaa tunazoweza nunua kwenye simu zetu.
App zinazo kupa pesa kwa kufanya kitu kidogo kwako (Android)
Farasi
Farasi ni moja ya app ambazo zinajihusisha na maswala ya usafili. Kwakutumia app hii unaweza pata usafiri wa kukutoa ulipo mpaka mahali unapotaka kwenda kirahisi. App hii inakutumika na watu wengi tu katika maswala ya usafiri. App hii hua inatoa zawadi kwa watumiaji wake pale wanapoitumia kupata usafiri. Kwasasa unapoanza kuitumia unapata Tsh 3000 mbali na zawadi nyingine utazopata unapotumia. Angalia app kwa KUBONEZA HAPA alafu kama utakua unajiunga usisahau kujaza namba 715233405 kwenye kibox cha referral code.
Branch app
App ya Branch ni app ya mikopo. Ni moja kati ya app nzuri sana katika upande wa app zinazokuwezesha kupata mikopo kwenye simu Tanzania. App hii inaweza kukupa zawadi ya pesa pele unaporudisha pesa kwa mara ya kwanza baada ya kuazima ila kupata zawadi hii ni lazimu uwe umealikwa. BONYEZA HAPA kupata maelezo zaidi ya app hii na zawadi zake
Tigo pesa app
App ya Tigo pesa ni app ambayo hurahisisha zaidi maswala ya kufanya miamala kwa watumiaji wa Tigo. App hii huwa anatoa kiasi kido cha pesa kama zawadi pale unapomualika rafiki yako. Kama unarafiki ambae anatumia mtandapo wa Tigo lakini ana app, unaweza mualika huyo rafiki alafu akapatiwa zawadi ya pesa kwenye akaunti yako ya Tigo pesa. Kama hauna app ya Tigo pesa, INGIA HAPA kuipakua.
Mwisho ningependa kukukumbusa tu kuwa app hizi sio app rasimi kwa kutengeneza pesa, zinatoa pesa kama zawadi TU.
Hapa The bestgalaxy, tunakufungua kidogo juu ya namna gani unaweza tumia mitandao ya kijamii vizuri. Mitandao ya kijamii imekua na mchango mkubwa katika mambo mbalimbali kwa binadamu wa sasa. Moja ya vitu vikubwa Teknolojia kupia mitandao ya kijamii imefanya ni kutuweka binaadamu pamoja na kutufanya tuwe na uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii kufanya au kupata vitu mbalimbali kirahisi. Zifuatazo na namna tatu za kutumia mitando ya kijamii vizuri.
Namna 3 za kutumia mitandao ya kijamii vizuri
Kupata burudani
Kama unapenda burudani basi Mitandao ya kijamii ndio sehemu ambayo inaweza ukukupa vitu vingi unavyoweza hitaji kuburudika. mitandao ya kijamii imekusanya vitu vingi sana ambavyo huburudisha na kufanya mtu apunguze msomgo wa mawazo. Ikiwa unataka kutumia mitandao ya kijamii kujiburudisha fanya kuingia kwenye vikundi vya burudani au kuzifuata kurasa zinanzo jihusisha na burudani ili kupata burudani toka kwenye kurasa hizo kirahisi. Pia usiache kutoa maoni na kuonesha umependezwa na vitu vinavyokuburudisha ili mitandao hiyo ya kijamii iwe inakuonesha mambo yatakayokuburudisha zaidi.
kujifunza vitu vipya
Kwenye mitandao ya kijamii unaweza jifunza vitu vipya pia. Kuna vikundi na kurasa ambazo hufundisha mambo mbali mbali kama vile, Ujasiliamali, Afya na Teknolojia. Endapo utakua ni mfutatiliaji mzuri wa vikundi na kurasa za namna hii, unaweza kuwa unajifunza vitu vipya vinavyo weza kuwa na msaada kwenye hata maisha yako. Katika matumizi yako ya mitandao ya kijamii, kwa na muda wa kufuatilia mambo yatakayokujenga na kukufungua ufahamu wa mambo mbalimbali ya msingi katika maisha yako.
kufanya biashara au kuingiza pesa
Ukiachana na kupata burudani na kujifunza vitu vipya, mitandao ya kijamii pia inaweza kutumika kufanya biashara au kuingiza pesa kiujumla. Hii ni mada pana sana maana kunanjia njingi za kufanya hayo na huwa zinatofautiana kutokana na mitandao kuwa tofauti pia. lakini kifupi sana ni kwamba unaweza tumia mitandao ya kijamii kuonesha biashara yako ili kuwafikia watu wengi wanaoweza hitaji huduma yako. Ukiachana na biashara, mitandao ya kijamii mingine huwa inatoa nafasi kwa content creators kuingiza pesa.
Angalizo: kufanya biashara au kuingiza pesa kwenye mitandao kuweza kuwa sio rahisi kama baadhi ya watu wanavyofikilia. Mara nyingi huwa kunahitaji uwekeze Akili, Pesa au Muda ili kufika unapo hitaji. Ukiingia kichwa kichwa unaweza poteza pesa na muda.
Whatsapp ni mtandao mkubwa ulimwenguni ambao watu huutumia sana katika mawasiliano. Unaweza kuwa ni mtandao wako pendwa katika mawasilioano ndio maana upo hapa… Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy, utajifunza vingi kuhusu mtandao huu.
Whatsapp ni mtandao mzuri kuutuumia katika kuwatumia watu Picha, Video, Audio au ujumbe wa maneno lakini unapofanya hivyo tambua kuwa kunajinsi ambavyo mtu mwingine anaweza kuona vitu vyote hivyo kwenye simu au kifaa chake bila wewe kutambua(kisiri). Kuna njia ambazo hata mtu asiebobea sana katika maswala ya Teknolojia anaweza tumia kuona sms au vitu unavyofanya kwenye Whatsapp. Lakini jambo hili lisikutishe maana hapa chini tunakwenda kukujuza jinsi ya kuangalia kama upo salama na jinsi ya kujilinda pia… Kwaiyo ondoa hofu na endelea kutumia Whatsapp yako kama kawaida.
Jinsi ya kujua mtu mwingine anaona sms na vitu unavyofanya WhatsApp kisiri
Whatsapp kwa sasa inakuruhusu mtumiaji wake kuunganisha akaunti yako moja ya Whatsapp kwenye kifaa zaidi ya kimoja. Unaweza fannya akaunti yako moja ya WhatsApp iwe inatumika kwenye simu mbili mpaka 4 na namba ikawa hiyo hiyo moja. Mtu mingine anaweza kuitumia hii kunganisha akauti yako kwenye simu yake au kifaa chake na kuanza kukuchunguza unachofanya bila wewe kujua. Na mtu akitumia ataweza kusoma sms zako, kujibu, kuona na kuchua audio,video na vitu vingine unavyotuma na kutumiwa bila wewe kujua.
Ukitaka kujua kama akaunti yako ya Whatsapp imeunganishwa fanya yafuatayo:
Fungua Whatsapp yako na uguse Vidoti Vitatu
Ukifanya hivyo, Chagua “Linked divices”
Baada ya kufanya hivyo utatupwa kwenye ukurasa ambao ukikuta kuna kifaa chochote kiorodheshwa basi jua whatsapp yako sio salama. Na kama hamna kifaa basi yawezekana upo salama. Unaweza angalia picha hapa chinikuelewa zaidi.
Endapo utakuta akaunti yako ya Whatsapp sio salama(hacked) unaweza gusa kifaa kilicho orodheshwa kwenye kwenye ukurasa huo alafu ukagusa vidoti vitatu itakavyoonekana juu kulia kisha utachagua “Remove device”.
Ili kuhakikisha kuwa WhatsApp yako iko salama kila mara, hakikisha unafanya kuangalia kama akaunti yako ya WhatsApp imeunganishwa mara kwa mara hasa baada ya kumruhusu mtu mwingine aishike simu yako bila uangalizi wako.
Katika ulimwengu wa sasa unaweza angalia movie kwenye simu yako ya kiganjani ukiwa popote ulimwenguni. Mara nyingi watu wakitaka kuangalia movie huwa wanatembelea website/tuvuti zinajihusisha na movie/filamu au hutumia app zinazojihusisha na filamu ili kupata huduma ya movies. Kuna baadhi ya tuvuti au app hukuwezesha kupata huduma ya movie bure na nyingine huwa zinakuhitaji ulipie. Huduma za kulipia huwa ni bora zaidi na zinausalama zaidi ukilinganisha na baadhi ya huduma za bure japo zote ni nzuri.
Hapa Tha bestgalaxy leo tunakupa orodha ya app chache kati ya app nyingi unazoweza tumia kuangalia movie kwenye simu yako mtandaoni(online).
App za kuangalia movies online(mtandaoni)
Netflix
Hii ni app ya kampuni ya kimalekni, Netflix ambayo inayotoa huduma ya kuangalia movies/filamu kupitia Internet. Unaweza ingiza kwenye simu yako ya mkononi na kuanza kufurahia filamu kiganjani pako. Unaweza kuangalia filamu nyingi nzuri na maalufu duniani kupitia app hii. Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba app hii ya netflix huwa haitoi huduma bure. Inaweza kukugharimu Tsh 7000 mpaka 23000(Makadilio).
ShowMax
ShowMax ni app inayotoa huduma ya kuangalia movies(filamu), michezo, vipindi vya TV na mambo mengine mengi, kiganjani pako. App hii inaweza kutumika kuangalia movie katika simu ya mkononi lakini sio bure pia. kufurahia huduma za app ya ShowMax utatakiwa kulipia kila mwezi. Kuna filamu nyingi unaweza angalia na pia kama ni mdau wa michezo, unaweza furahia michezo katika app hii. Kifurushi vyake vinaweza kugharimu Tsh 7800 mpaka 46000 kwa mwezi(Makadilio).
Youtube
Youtube ni app ambayo watu hutumia kuangalia video mbalimbali ambazo huwa zinapostiwa kwenye channel. Katika Youtube kuna channel ambazo hutuma filamu na unaweza angalia filamu hizo bure kabisa. Ukiachana na channel za filamu pia kuna kipengele cha Youtube kinachojihusisha na filamu tu(filamu za bure na kununua}. Kipengele hicho cha Youtube hakipatikani katika baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania kwa sasa ila unaweza soma maelezo ya kukuiona hapa chini.
App hii inaitwa “Amazon Prime Video” lakini kwa kifupi unaweza kuiita “Prime Video”. Ni moja ya app zinazoweza kukufanya ufurahie kuangalia movies na hata vipindi vya Tv pia kiganyani pako. Prime Video sio app ya bure lakini inakupa uwanja mpana unaofanana kiasi na netflix hivi katika filamu, unaweza angalia filamu nyingi maaalufu. Maelezo ya kiasi utakachotakiwa kulipa kwa mwezi yaliopo katika tuvuti yao yametaja kiasi kuwa ni USD 5.99 ambayo ni kama Tsh 14000 ivi…
~Viasi vya malipo vilivyo tajwa kwenye makala hii ni makadilio tu.
Whatsapp ni mtandao unaotumiwa na watu wengi sana na umekua na msaada mkubwa kwa watu katika swala la mawasiliano. Katika kutumia mtandao huu unaweza kupambana na changamoto au vitatizo vidogo vidogo, hasa katika app za simu. Changamoto au matatizo huwa hayatokei mara kwa mara lakini hapa The bestgalaxy tumekuandalia orodha ya matatizo au changamoto unazoweza kutananazo katika kutumia whatsapp na maelezo ya jisi ya kutatua. Hii inaweza kuwa msaada pindi mtu unapokumbana na changamoto hizo. Pia usisahau kuungana nasi kwenye WhatsApp namba 0622586399.
Changamoto au Matatizo kwenye kutumia Whatsapp na jinsi ya kutatua
Whatsapp ban
Kama upo banned/umezuiwa kwenye WhatsApp unaweza kuona hivi
Mtandao wa whatsapp unasheria zake ambazo ukikiuka katika kutuumia mtandao huu, wanazuia akaunti yako. Kutumia app za whatsapp zisizo rasimi ni moja ya jambo linaloweza kufanya akaunti yako izuiliwe Whatsapp. Nikizungumzia “Whatsapp zisizo rasmi” namaanisha app kama vile OG Whatsapp, GB Whatsapp au FM whatsapp. Mtandao wa Whatsapp una app rasmi mbili tu. App ya kwanza inaitwa “Whatsapp messenger” na ya pili inaitwa “Whatsapp business”… App yoyote mbali na hizo ni app isio rasmi na inaweza kufanya akaunti yako izuiwe/ifungwe na mtandao wa Whatsapp.
Ukiachana na kutumia app zisizo rasmi, unaweza fungiwa au kuzuiwa akaunti baada ya kufanya mambo mengine yasio faa katika Whatsapp au watu kutoa taarifa kwa Whatsapp kuhusu akaunti yako kujihusisha na jambo flani lisilo ruhusiwa kwenye Whatsapp.
kuna namna mbali za kuzuiwa; unaweza zuiwa na whatsapp kwa muda mfupi au kwa muda mrefu. Ukizuiwa kwa muda mfupi, baada ya muda flani akaunti yako itaondolewa kizuizi na mara nyingi huwa app inaonesha kabisa muda ambao akaunti itaachiliwa. Lakini ikizuiwa kwa muda mrefu huwa inachukua muda mrefu sana kuachiliwa… ukikumbana na kizuizi hiki unashauriwa kufungua akauti nyingine ya whatsapp kwa namba nyingine au kama unahisi wamekuonea, wasiliana nao kupitia Support@whatsapp.com tuma ujumbe wa kuelezea tatizo lako ili wakusaidie.
Backup katika whatsapp ni kipengele kinachokuwezesha kutunza sms za whatsapp na vitu vingine kwenye akaunti yako ya google drive ili iwe rahisi kupata au kurudisha sms na vitu hivyo pindi simu yako inapopotea au ukifuta app kwa bahati mbaya. Unaweza fungua whatsapp ukuta ghala tu wahatsapp imekuletea ujumbe unaoziba kioo kizima umeandikwa “Backup to Google drive” na kuna orodha ya chaguzi unazotakiwa kuzichagua pale. Kama hauelewi lolote kuhusu backup basi umaweza changua “Never” tu ili kuokeo muda na kuendelea kuitumia app yako ya Whatsapp.
Whatsapp kumaliza bando
Whatsapp ni moja ya app zisizotumia bando la internet sana ila kama wewe ni mtu unaetumia Whatsapp kwenye upande wa video sana basi app hii inaweza kutumia bando zaidi. Nikisema upande wa video namaanisha kutuma au kupokea video nyingi kwenye vikundi au watu wa kawaida, kutumia video call sana, kuangalia status za watu wengi wilio weka video kwenye status zao. Kuacha au kupunguza mambo hayo kutafanya Whatsapp isile bando lako sana.
Whatsapp inajaza picha na video nisizozitaka kwenye simu
Whatsapp inaweza kuwa inajaza picha na video usizozijua au usizozipenda kwenye simu yako. Kama hili ni tatizo, unaweza tatua tatizo hili kwa kuzima kipengele cha whatsapp kinacho iruhusu app ya whatsapp kuingiza kwenye simu video au picha zinazotumwa kwenye magroup au unazotumiwa. hii itafaya kila video au picha unayotumiwa kutojiingiza kwenye simu yako mpaka utakapo gusa kuidownload.
jinsi ya kufanya hivyo; fungua app yako ya whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” kisha gusa “Storage and Data” alafu baada ya hapo ingia walipo andika “When using mobile data” na uondoe alama ya tiki kwenye vibox vyote au cha video na Photos tu. baada ya kufanya hivyo, bonyeza “Ok” na rudi nyuma kidogo kisha uingie kwenye “When connected on WiFi” alafu uondoe alama ya tiki katika vibox vyote au vibox vya “Photos” na “Videos” tu.
kama umekua unajikuta umeingizwa kwenye magroup ya Whatsapp na watu usio wajua bila hata taharifa na haupendi hali hiyo basi kunakitu unaweza fanya hapa. Kwenye Whatsapp kunakipengele kinakuruhusu kuzuia mtu ambae hauna namba yake kukuingiza kwenye group. Unaweza kutumia kipengele hiki kuzuia watu ambao hauna namba zao wasikuingize kwenye group lolote bila kukutaharifu.
jinsi ya kufanya hivi; Fungua Whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” kisha gusa “Privacy”. Baada ya hapo, nenda eneo la chini kidogo uingie walipoandika “Groups” kisha chagua “My Contacts” alafu rudi nyumbani na uendelee kutumia app yako.
Nasumbuliwa na simu za watu nisio wajua
Whatsapp pia inakipengele cha kufanya watu watu ambano nambazao hazijawekwa kwenye simu yako wakikupigia usipate usumbufu. Mtu yoyote ambae anakupigia kwenye Whatsapp kwa namba ngeni, simu yako haita, itakua kimya tu bila kukusumbua. Kama ni mtu amabae huwa unapata simu nyingi kwenye Whatsapp toka kwa watu usio wajua na haupendi swala hiilo basi unaweza kutumia kipengele hicho kuondokana na jambo hilo.
Jinsi ya kufanya hivi; Fungua app yako ya Whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” alafu bofya “Privacy”. Baada ya hapo, nenda chini kidogo uingie katika “Call” alafu washa palipo andikwa “Silence unknown callers”.
Katika matumizi yako ya simu za Smartphone unatakiwa kuelewa kwamba vifaa hivi vinaweza kudukuliwa na mtu mwingine na kufanya mdukuzi au huyo mtu apate uwezo wa kuona vitu vilivyomo au vitu unavyofanya kwenye simu yako bila yeye kuigusa simu yako. Mbali na kuona vitu unavyofanya au ulivyohifadhi, Mtu aliedukua simu yako pia anaweza kuwa na uwezo wa kuitumia simu yako bila kuigusa… Mfano wa vitu anavyoweza kuvifanya ni kuitumia simu yako kutuma sms kwa mtu mwengine, kuitumia camera yako kuangalia unachokifanya, kuvujisha vitu vyako au kukuzuia kufanya baadhi ya vitu kwenye simu yako.
Lakini ukiwa kama mtumiaji wa smartphone wa miaka hii, hutakiwi kuwa na hofu sana juu ya hili kwani kunaviashilia vya kuangalia kwenye simu yako ili kujua upo salama au vipi. Hapa The beestgalaxy tutakupa mwanga juu ya jinsi ya kuangalia simu yako ya Android kama imedukuliwa na inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine.
Jinsi ya kuangalia kama simu yako inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine
katika matumizi ya simu watu huwa wanapenda kuingiza apps nyingine mbali mbali ukiachana na zile ambazo huwa wanazikuta tayari zipo kwenye simu. Kitu unachotakiwa kujua hapa ni kwamba kuna Program au apps ambazo unaweza kuingiza kwa bahati mbaya au ukaingiziwa kwenye simu yako na zikiwa kwenye simu yako zinakua zinatumika na mtu mwingine huona au kufanya vitu kwenye simu yako bila kuigusa.
Endapo katika simu yako kutaingizwa apps hizi kwa makusudi au bahati mbaya, simu yako itakua sio salama tena maana vitu. Lakini kitu kizuri ni kwamba kwenye sikuizi kwenye simu za Android kuna program inaitwa “Google play protect”. Program hii inamilikiwa na google na kazi yake kubwa kwenye simu ni kukulinda dhizi ya apps hatari unazoziingiza kwenye simu yako. Kama kuna app yoyote inayoweza kuwa hatari umeiingiza, Google play protect huwa inatoa taharifa na kukushari cha kuifanya. Unaweza kuitumia Google play protect kuangalia kama angalia kama simu yako ni salama au si salama. Unachotakiwa kufanya ni kufuata hatua hizi chini.
Chukua simu yako na uingie katika app ya Play store
Baada ya hapo, gusa kiduara cha profile yako na uchague “Play protect“
Bonyeza kitufe kilichoandikwa “Scan” na baada ya hapo Google play protect itaanza kuangalia kama kuna app zozote hatari kwenye simu yako alafu itakupa majibu.
Kama kutapatikana app yoyote hatari utaonyenshwa app hiyo alafu utashauriwa kuiondoa kwenye simu yako kwa kugusa kitufe cha “Uninstall“.
Google play protect ni njia nzuri na rahisi ya kuangalia kama simu iko salama ukiwa kama mtumiaji wa kawaida lakini huwa haikuhakikishii usalama kwa 100%.
Google play protect ikiwa “Active” kwenye simu yako huwa inatafuta na kulinda hii ya app hatari. Na endapo itakuta app harari imeingizwa au unataka kuiingiza kwenye simu yako, itakupa taharifa.
Mbali nna kutumia Google play protect kuangalia kama simu yako iko salama unaweza pia kujua kuwa simu kwa kuangangalia kama kwenye simu yako kuna vitu vifuatavyo.
Angalia orodha ya app zinazotumia sana internet na kama utakuta app ambayo haieleweki na hauitumi lakini ipo juu kwenye matumizi ya bando, inawezakua ni app hatari. Kama kamera ya simu yako ukiifungua inakuandikia “Camera is being used by another application” au “You cannot use more than one application that uses camera” au “Camera may be in use by another application” hiyo inaweza kuwa ni ishara ya kwamba simu yako sio salama. Mbali na hayo, kukuta vitu ambanyo haujavifanya lakini vimefanyika kunaweza kuwa kiashiria cha hatari pia.
Magemu ya mabasi yamekua ni kati ya magemu pendwa sana kipindi hiki. Magemu haya yapo mengi sana na watu huyacheza kupitia simu, pc na baadhi ya vifaa vingine kama hivyo vinavyo tuwezesha kucheza magemu. Katika makala hii tunazungumzia magemu mazuri ya mabasi lakini tutajikita katika upande wa simu za Android hivyo kama wewe ni mtumiaji wa simu yoyote ya Android, unapenda na kutaka magemu mazuri ya mabasi, hii ni kwaajili yako.
Kutokana na wingi wa magemu ya mabasi kwa simu za Android, inaweza kuwa ngumu kwa mtu kujaribu kila gemu ili kujua lipi ni zuri na lipi ni baya kwake ingawa unaweza fanya hivyo pia. Hapa sisi tunakupa orodha ya magemu macheche ya mabasi ambayo ni mazuri unayoweza kuyacheza katika simu yako na yanachezwa na watu wengi duniani. nafikili hii inaweza kukusaidia katika utafutaji wa gemu zuri kwako.
Katika magemu ya Android mazuri ya nayohusiana na uendeshaji wa mabasi, kunage hili linaitwa “Bus simulator 2023”.Bus simulator 2023 ni gemu la mabasi lililotoewa na Ovidiu Pop kwa simu za Android pamoja na iOS. Lilinakutupa katika ulimwengu ambao unakua ni deleva wa mabasi na kuna modes nyingi unaweza kuwa unafurahia humu ndani. Unaweza kucheza na marafiki aua watu wengine online na pia kwenye upande wa muonekano uko poa. Asilimia kubwa ya watu waliolicheza gemu hili,wamelipenda kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo muonekano.
Kama ni mfuatiliaji mzuri wa The bestgalaxy unawezakuwa umegundua kuwa gemu la Bus Simulator Indonesia tumeliongelea zaidi ya hapa. Hii ni kwasababu nigemu zuri sana na usioweza kuyaacha unapozungumzia magemu ya simu ya kuendesha mabasi. kwasasa gemu la Bus simulator indonesia imeishaingizwa kwenye simu na watu zaidi ya milioni 100 kutoka sehemu mbalimbali za dunuia. Mazingira na mabasi ya katika gemu hili ya yanaendana na mabasi na maingira halisi ya huko Indonesia. Muonekano wa gemu hili ni mzuri na pia uzuri mwingine wa gemu hili ni hutohitaji kutumia data/internet katika kulicheza ingawa ukihitaji kucheza na watu au marafiki, utahitaji kuwa na muunganiko wa internet(data).
Hili ni gemu la mabasi ambalo mpaka sasa watu zaidi ya milioni 10 wamelipakua katika vifaa vyao vya Android OS. Ndani ya gemu hili mchezaji unaendesha mbasi ya abilia ya masafa kuwatoa sehem moja kwanda nyingine. Na ukiwa kama dereva wa mbasi unakumbana na changamoto mbalimbali katika kazi yako unapokua barabaradi. Linamuonekano mzuri. Ovidiu Pop ndio waliotoa gemu hili na linapatikana bure kabisa kwa watu wote wanaohitaji kulicheza katika Android. Unaweza kulipakua kupitia Playstore na ukaanza kufurahia kulicheza kila siku bila kutumia data(Ni gemu la Offline).
Katika mwaka 2019 “Zuuks Games” walitoa gemu la Bus Simulator Ultimate na toka hapo mpaka sasa kuna mamilioni ya watu wamepakua gemu hili na wanaendelea kulicheza. Zuuks Games walisema gemu lao la bus simhlator limekua ni miongoni mwa magemu ya mabasi yaliopakuliwa na watu wengi… limeshafikisha zaidi ya watu milioni 200. idadi hiyo ya watu inajumuisha watu kutoka US,UK,Canada na sehemu nyingine yingine nyingi za dunia, ikiwemo Tanzania. Unaweza kulidowmload au kulipakua gemu hili bure ila kulicheza utahitaji kutumia data(internet).
Gemu jingine zuri la mabasi kwa upande wa Android ni hili linaitwa Public Transport Simulator C. 2019 ndio mwaka SkisoSoft walilitoa na tokalitolewe mpaka sasa limechezwa na zaidi ya watu milioni 50. Kutokaa na uzuri wake asilimia kubwa ya watu wanaolidownload na kulicheza wanalipenda na hii imeionesha kupita reviews ambazo zimekua zikitolewa na wachezaji wa game hili katika Playstore. Pamoja na kwamba gemu hili limetolewa mwaka 2019 lakini bado linaendelea kuboreshwa na hupata updates kila baada ya muda flani… Lakini jambo hili halifanywi kwenye gemu hili tu, hufanywa kwenye mgemu mengine. Kiufupi ni kwamba magemu yanaboreshwa Kila siku na Unaweza ona Gemu ni baya Leo lakini baada ya mwaka likawa limeboreshwa na kuwa zuri.
Mbali na magemu haya unafikili ni gemu gani lingine zuri kwa upande wako? Huu ni mwisho wa orodha yetu,, usiache kuwa kalibu nasi…
Kama ni mmoja kati ya watu wanaotafuta nafasi za kazi basi hapa kunakitu kidogo unahitaji kuwanacho kichwani katika miaka hii ukiwa katika mchakato wa kutafuta ajira. Unachotakiwa kujua ni kwamba teknolojia kupitia internet/mtandao imerahisisha mchakato wa kutafuta ajira na kuufanya uweze kufanyika katika kiganja chako kwa kutumia simu yako(Smartphone).
Unaweza tumia simu yako kuangalia nafasi za ajira unayoihitaji zilizojitokeza katika sehemu mbalimbali za dunia (Ndani na nje ya nchi). Na kama utapply au kufuata maelezo ya kuipata iyo nafasi na kubahatika kuipata, utakua ni mmoja wa mamilioni ya watu waliopata na wanaoendelea kupata nafasi za kazi kwa msaada wa internet. Kama unataka kutafuta nafasi za ajira/kazi kwa kutumia simu mtandaoni lakini haufahamu ni jinsi gani unaeza fanya hivyo, basi hapa chini nakupa mwanga juu ya hili kwa njia 3. Lakini kabla ya yote ni vema ukajua kwamba kunabaadhi ya nafasi za kazi au ajira ziwekwa na matapeli mtandaoni na maranyingi humuitaji mtaka nafasi atoe pesa ili kupata nafasi ya ajira… kuwa makini ni ajira za mtindo huo ili usije tapeliwa.
Njia za kutafuta nafasi za ajira/kazi zilizojitokeza kwa kutumia simu mtandaoni
Tafuta nafasi za kazi kupitia Google search
Watu tu hutumia google search kutafuta vitu mbalimbali kirahisi mtandaoni na imekua msaada mkubwa kwa watu wengi, nafikili hata wewe unaweza kuwa mmoja wa watumiaji wake mzuri. Mtu unaweza tumia Google kupata vitu vinavyokufurahisha, vitu vitakavyo kuelimisha na vitu vingine muhimu ikiwemo nafasi za ajira zilizojitokeza sehemu mbalimbali (Ndani na nje ya Tzanzania). Na nirahisi sana… kiufupi utatakiwa kuandika maneno yanayomaanisha nafasi za kazi, aina ya kazi na mahali(kwa kingereza ili kupata matokeo mazuri). Yaani unawezakwenda Google na kuandika “””””Aina ya kazi unayoitaka + jobs in + sehemu“”””” kisha ukitafuta na kwenye matokeo utapata orodha ya nafasi za kazi kulingana ulichokiandika. Kwamfano ukiwa unataka kazi ya “Customer care service” hapa Tanzania, utaandika “Customer care service jobs in Tanzania” kwenye matokeo utapata orodha ya nafasi za kazi za customer care zilizojitokeza Tanzania. Baada ya google ikukupa nafasi za kazi itakua ni kazi kwako kusoma maelezo ya kazi hizo ili kuzielewa zaidi na kuapply ikiezekana. Lakini unapotumia njia hii inatakiwa kufahamu kuwa Google ni search engine tu, hivyo huwa haina nafasi za kazi, inakupeleaka sehemu ilipopostiwa kazi…
Jiunganishe na blog zinazohusiana na mambo ya nafasi za ajira
Kuna blog ambazo hujihusisha zaidi na kutoa tahalifa kwa watu juu ya nafasi za ajira zilizojitokeza. Maranyingi huwa zinapost tahalifa za nafasi za ajira au habari zinazohusiana na mambo hayo hayo. Mfano mzuri ni Ajiraleo.com au Ajirampya360.com. Sasa kwakua na wewe unahitaji nafasi za kazi basi unaweza anza kuwa karibu na blog za mtindo huu ili wakitoa tu tahalifa za nafasi za ajira zilizojitokeza, zikupate kwa wakati na kuanza mchakato wa kuzichangamkia. Unaweza kuwa nazo karibu kwa kuzifuata blog hizo au kurasa zao katika mitandao ya kijamii ili kupata vitu wanavyopost.
Tumia LinkedIn
Linkedin ni mtandao kama vile Facebook au twitter lakini mtandao huu unakusanya wataalamu wa mambo mbalimbali na umejikitia katika zaidi maswala ya biashara na ajira. jiunga kwenye mtandao Linkedin bure kabisa na kwenye profile yako utatakiwa kujaza taalifa sahihi kuhusu wewe na utaalamu wako. Mambo unayotakiwa kuyafanya ndani ya mtandao huu ni vema yakawa yanaendana na utaalamu wako na jambo zuri ni kwamba unaweza kupata ajira kupitia mtandao huu… kurahisisha zaidi mchakato wa kutafuta nafazi za kazi, kunakipengele cha mtandao huu kinauruhusu kutafuta nafasi za kazi zilizojitokeza kulingana na uhitaji wako na kuapply.
Mbali na njia hizo tatu, kuna njia au vitu vingine zaidi unaweza fanya kupata taalifa za nafasi za kazi zilizojitokeza lakini huenda tutazungumzia katika sehemu nyingine, hapa tumekupa mwanga kwa hayo machache. Na ni vema kuendelea kutafuta nafasi za kazi nje ya mtandaoni pia. Ishi kwa kutangaza utaalamu wako. Endelea kufuatilia The bestgalaxy.
Kama ni shabiki mzuri wa mpira wa miguu unaweza kua ni mmoja wa watu wanopenda kufuatilia matokeo ya mechi mbalimbali katika ulimwengu wa kabumbu. Teknolojia imeisharahisisha mambo mengi sana katika soka. Kupitia simu yako ya mkononi unaweza kuangalia mechi live na ukafurahia, kiganjani pako!.. Mbali na nakushuhudia mechi live kiganjani pako, unaweza pia kuangalia matokeo ya mechi zilizochezwa au zinazoendelea kuchezwa hapo hapo kiganjani pako. Hii inasadia sana maana unaweza kua hauna muda wa kutulia na kuangalia mechi lakini lakini ukawa unajua mechi katika upende wa scoles ziko vipi.
Kuna njia zaidi ya moja zinaweza kutumika kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu na watu huzitumia kila siku yaani kuangalia matokeo ya mechi za leo, jana na siku zaidi hiyo. Hapa The bestgalaxy tunaweka wazi njia 3 unazoweza kuzitumia kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu yako ya mkononi.
Njia 3 za kuangalia matokeo ya mechi za mpira kwenye simu
1. App na site/tuvuti maalum kwaajili ya kuangalia matokeo
Unapotaka kujua matokeo ya mechi mbalimbali kwenye simu yako, tambua kuna app za simu ambazo ni maalum kaajili ya matokeo ya mechi za mpira wa miguu na michezo mingine. Unaweza ingiza moja ya app za muundo huu kwenye simu yako na ukawa unatumia kuangalia matokeo ya mechi unazozihitaji kwenye simu. Uzuri wa app hizi ni kwamba nyingi huwa zinakua zinatoa huduma ya kukupatia matokeo bure kabisa japo kila utakapotaka kuzitumia utatakiwa kutumia internet. Mfano wa app hizi ni app iitwayo “LiveScore” na pia hii nyingine inaitwa “GOAL Live Scores”. Mbali na app izo kuna App ningine nyingi sana unaweza tumia kuangalia Scores. kwenyewe app hizi unaweza pia kufurahia vipengele vingine kama vile habari za michezo na ratiba za michezo.
Ukiachana na uwepo wa app, pia kuna websites/tuvuti unaweza tumia kuangalia matokeo ya mechi. App nyingi zinazojihusisha a matokeo ya mechi huwa ni za websites. mfano mzuri ni hii appp ya LiveScore; kuna website inatwa “LifeScore” na hiyo website ndio inaapp iitwayo “LiveScore”. kwahiyo hapo unakua uamuzi wako kuangalia matokeo mechi zako kupitia website au app.
2. Angalia matokeo ya mpira kupitia Google search
watu wengi hutumia google search kupata taharifa mbalimbali kwa haraka. Kunavitu ukivitafuta google unawezeza kuvipata kwa shida lakini sio matokeo ya mechi(hasa kama mechi inatambulika). Google inaweza kukupa matokeo moja kwa moja ya mechi ilioisha unayoihitaji bila mizungusho mingi. Na kitu kizuri ni kwamba kupitia Google unaweza pata taalifa nyingine kuhusu mechi kirahisi sana na bila kupoteza muda wala kutumia bando sana kama baadhi ya njia nyingine. Unaweza tumia njia hii kuangalia matokeo ya mechi za simba na yanga bila utata.
3. Angalia scores kwenye app au tuvuti za kubeti
Ukiachana na njia hizo mbili ambazo unaweza tumia kuangalia scores, njia ya tatu ni kucheki scores kupitia app au tuvuti za kubeti. Kama wewe ni mtu unaebeti kupitia simu, hainaaja ya kujitesa kuangalia matokeo ya mechi zinanoendelea kuchezwa. Unaweza kuangalia kirahisi kupitia kipengele cha “LIVE” katika website au app ambayo unaitumia kubeti. Kipengele hiki huwa kinakupa taalifa za mechi zinazochezwa muda huo na Moja ya taalifa utakazo zipata ni pamoja na magoli. Kipengele hiki ni kwaajili ya kubeti lakini unaweza kukitumia kuangalia scores za mechi unazozijitaji.
Kama huwa unaambiwa umuweke status kitu lakini unashindwa kwasababu mbalimbali na kupelekea kutoelewana kati yenu au unakitu unahitaji kuiweka status bila watu au mtu flani kujua basi leo nakufundisha jinsi ya kufanya hivyo.
WhatsApp status ni kipengele cha WhatsApp ambacho mtu hutumia kupost vitu mbalimbali ambayo huonwa na watu wengine walio na namba yake kwenye simu kama alivyo nazo zao yeye kwenye simu yake. Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba katika kipengele hiki unauhuru wa kuchagua mtu au watu gani waone status yako na watu gani wasione… Hii inamaanisha unaweza chagua watu au mtu pekee unahitaji aone status yako kisha ukapost kitu kwenye status yako na akakina yeyetu.
Unaweza fanya hivyo kwa kufunya yafuatayo;
Fungua app ya WhatsApp kisha gusa vidoti vitatu vilivyo juu kulia.
Utakuta orodha ya maneno machache, Chagua “Settings” Kwakuigusa.
Katika settings utakuta orodha pia, Chagua “Account” Kwakuigusa na itakuletea orodha tena chagua “privacy”
Ukisha chagua privacy, utakuta orodha tena,Chagua neno “Status” Kwakuigusa Hapo utaletewa orodha hii:
My Contact My Contact except.. Only share with…
orodha hii inakidoti ambacho wewe unachagua kiwe katika nenolipi kati ya hayo.Na kidoti hicho utakikua kwenye “My Contact” wewe inabidi upeleke kwenye “Only shere with..” ukikipeleka hapo itakuletea namba za watu wako kwenye simu,inabidi umchague yule unaetaka aione hiyo status alafu gusa “Ok” kisha “Done” ukisha maliza nenda kaposti hiyo status, nenda kapost kitu anachotaka kwenye status yako na atakiona yeye tu!