Tag Archives: swahili funny stories

Vichekesho vya kiswahili vunja mbavu




Karibu kwenye makala hii yenye vichekesho vya kusoma vinavyofurahisha! Katika ulimwengu wa hadithi za kuchekesha, tunakuletea mkusanyiko wa visa vya kufurahisha na kukuvunja mbavu. Kupitia makala hii, utaweza kufurahia na kucheka kwa kujitupa katika hadithi fupi zilizojaa kujifunza na kuchekesha pia.

Hadithi hizi za kuchekesha zimeandikwa na watu kwa ustadi na kubuniwa kwa kina ili kukuvutia wewe msomaji lakini hapa the bestgalaxy, zimekusanyawa tu. Hadithi inaweza kuja na mchanganyiko wa utani, kujikosoa, na vituko, kikubwa usiwe serious sana, lengo kubwa ni kucheka kufurahi hivyo jiachie.


Kucheka ni moja ya mambo muhimu katika maisha yetu ya kila siku. Kwanza kabisa, kucheka husaidia mtu kupunguza msongo wa mawazo na hali ya wasiwasi. Unapocheka, mwili wako huzalisha homoni za furaha kama vile endorphins, ambazo husaidia kupunguza mkazo na kuongeza hisia za nzuri.

Vichekesho vya kiswahili vunja mbavu

MUOKOTA MAKOPO:

Tamaa mbaya! Muokota makopo katika uokotaji wake wa makopo akaona chupa ambayo ndani kuna kikaratasi, alipoifungua chupa likatoka jitu la ajabu lisilo onekana na watu wengine. Lilikua likitetemeka na lilimwambia “kijana asante sana kwa kuniokoa omba vitu viwili sasa hivi”. Kijana kwa hofu akaomba pesa za kumiliki magari na majumba ya kifahari. Ghafla fuko liliojaa hela na pete ya dhahabu ya bahati vikadondoka mbele yake. Akaambiwa aseme ombi la pili, akasema “Nibadilishe niwe kivutio ili nipendwe sana nakina dada wazuri” Hapohapo jamaa akageuzwa akawa chipsi yai.!!

MTOTO MDOGO KATULIA NA BABA:

MTOTO: Hivi Baba ivi wewe umezaliwa wapi?
BABA: Nimezaliwa Mbeya
MTOTO: Mama nae kazaliwa Mbeya?
BABA: Hapana, amezaliwa Tanga
MTOTO: Na Mimi jee?
BABA: Dar
MTOTO: Mh Sasa tulikutanaje????
Baba akaangua kicheko

JAMAA BAADA YA KUCHELEWA KAZINI:

Boss: kwa nini umechelewa kazini

Juma: kuna mtu njiani alidondosha 5000 boss

Boss: anha kwahiyo ulikua unamsaidia kuitafuta

Juma: Hapana, bahati nzuri niliikanyaga nikawa nasuri aondoke.

MAWAZO YA VIKOBA:

(Mdada baada ya kufika kwa mpenzi wake akiwa na Mawazo mengi ya vikoba)

Mdada: Baby, naomba shilingi elufu kumi na tano nilipie taxi niliokua nayo.

(Mkaka kaingiza mkono mfukoni kutoa pesa lakini ghafla alipomuangalia mpenzi wake vizuri akashtuka!)

Mkaka: Unasema umekuja na Taxi? Mbona umejisahau umekuja na helmet ya Bodaboda?

Katika ukurasa huu, tuliokuandalia ni hayo tu lakini Kuna vichekesho vingi ndani ya The bestgalaxy ambayo unaweza furahia kuvisoma. Endelea kuwa karibu na sisi kwenye mambo mbalimbali tunayojihusisha nayo.

Stori za vichekesho vya kuvunja mbavu BONYEZA HAPA>>>

Vunja mbavu sms za vichekesho (soma hapa)

BANGE SIO CHAI..

Siku moja Nyani alikuwa kakaa kijiweni anavuta bangi,Mjusi(lizard) akaja akampa “Hi” akajiunga na kumuomba puff.

Nyani akamuonya kuwa ile bangi ilikuwa ni kali sana,ni kipisi cha kutoka Milimani huko. Mjusi akapokea wakaanza kuvuta bangi kwa raha zao…baada ya muda mjusi akawa hoi kwa stimu akamuambia nyani “Duh nasikia koo langu limekauka acha niende mtoni nikanywe maji!”

Mjusi kufika mtoni kwa kuwa alikuwa na stimu nyingi akatumbukia mtoni. Bahati nzuri Mamba alikuwa pembeni, akawahi kumuokoa mjusi na kumtoa nje ya maji.

Baada ya kumuokoa, Mamba akamuuliza mjusi “Ina kuwaje bro mbona umetumbukia mtoni kipuuzi vile?” Mjusi akajibu “Nilikuwa na nyani tunavuta bangi nikasikia kiu ya ajabu nikajikuta kwenye maji bila kujua!” Mamba akasema “Aaah wacha niende huko kwa nyani nikamuone.”

Mamba kufika akamkuta nyani ndo anamalizia kipisi chake,kazidiwa hata macho ni tabu kufungua. Mamba akamuita “Oya” Nyani akafungua macho,kumuona Mamba akashtuka Et”Duh! Mshikaji kwani umekunywa maji yote mtoni! Mbona umerudi mkubwa hivyo!!”

SIPATI PICHA INGEKUAJE…

Jamaa yangu mmoja alikuja kunitembelea kule Mburahati Madoto. Sasa wakati namsindikiza tukafika kituo cha madoto mwisho

kusubiri daladala. Mara jamaa yangu akanyewa na kunguru kichwani. Jamaa akaangalia juu alivyogundua amenyewa akamuona

kungulu usawa wake, jamaa akaangua kicheko sana yaani. Mi nilikuwa naona yote yanayotokea nikamuuliza “sasa unacheka nini

ndugu yangu wakati umenyewa?” Jamaa akajibu “We acha tu, afadhali bata hawapai angani kama kunguru”

AMRI KUMI KWA WAPENDAO OFA

  1. Muheshimu anayekununulia
  2. Muamkie mtoa ofa kabla hujakaa kitini
  3. Uwe ndie mchekeshaji wa kikao, lakini usimkatishe mazungumzo anaetoa ofa
    . Mtoa ofa akikutuma popote usikatae
  4. Mtoa ofa akiupenda muziki fulani, we anza kucheza kwa bidii kabisa
  5. Usinywe kwa pupa, kunywa mafunda madogomadogo
  6. Mtoa ofa akitoa kichekesho cheka sana hata kama hakichekeshi

Soma Stori 2 Fupi za Vichekisho (Vunjambavu)

KIKUNDI CHA WATALII kilitembelea mto wa kufugia mamba na walikuwa wakielea kwenye meli ndogo katikati ya mamba wenye njaa. Ikasikika sauti ya mmiliki wa eneo hilo ikisema: “Atakaye ruka kwenye maji na kuogelea kutoka nje atazawadiwa dola milioni 10”. Kila mtu kimya, ghafla mwanaume mmoja akajirusha majini. Alikimbizwa na mamba kwa bahati nzuri alitoka salama. Akatangazwa mshindi. Wakati anarudi hotelini na mkewe akamwambia mkewe “Aisee sijajirusha mwenyewe majini, kuna mtu alinisukuma nikapambana niokoe maisha yangu”. Mke wake akatabasamu na kusema “Ni mie ndio nilikusukuma”. Wewe ungemfanyaje kama ni mkeo? Anyway, “Nyuma ya kila mwanaume mwenye mafanikio kuna mwanamke anayemsukuma kufikia mafanikio”.🤣🤣🤣

UMEMUAGA mkeo unaenda kazini, ukapita kwa mchepuko wako, wakati unajimwaya-mwaya na mchepuko, mume wa mchepuko akagonga mlango, ikabidi ufichwe uvunguni mwa kitanda.
Wakati bado upo uvunguni ka mchepuko kakamuaga mume wake kwamba, kanaenda saloon, mume wa ka-mchepuko naye akaona ndo muda wa kuita mchepuko wake, akauita ukaja, wakajimwayamwaya kwa sana muda huo wee bado upo uvunguni. Mara mchepuko wako akarudi kutoka saloon, akagonga mlango, ikabidi mume wa mchepuko wako aufiche uvunguni mchepuko wake.
Kucheki hivi kumbe mchepuko wenyewe ndo mke wako uliyemuaga unaenda kazini, kwa hiyo wewe na mke wako wote mkawa mmefichwa uvunguni…Ukisikia vita ya tatu ya dunia, ndo hii sasa.

SOMA STORI HIZI UVUNJE MBAVU

Dogo kakamatwa na polisi akiwa na
bangi mfukoni;
POLISI: Kijana unatembea na bangi
hili ni kosa la jinai
DOGO: Afande mi naona kama nimelogwa
hiyo bangi kila nikiitupa chooni unakuta imerudi mfukoni mwangu
POLISI: Acha kunifanya mie fala
twende kituoni
DOGO: Kama huniamini afande na wewe tumbukiza chooni utaona imerudi
mfukoni mwangu toka jana inanisumbua sana ….
POLISI: Natumbukiza tuone na
ukinidanganya ndipo utakapojua
Dola maana yake nini ……afande
akatumbukiza bangi chooni
POLISI: Haya hebu toa hiyo bangi sasa mfukoni mwako
DOGO: Bangi bangi gani?
POLISI: Si ile uliyosema inarudi
mfukoni mwako
DOGO: Afande mi sikuelewi kabisaa,
mi na wewe tulizungumza wapi kuhusu bangi Mimi hiyo bangi naijua wapi
bangi hata kuishika sijawahi Au unataka kunibambikizia
kesi ya bangi afande?

😂😂😂

Gusa hapa>> USOME JAMBO ZURI ZAIDI KWAAJILI YAKO

Dah soma hii👇👇

Ni majira ya saa 11 jioni nikitoka zangu Morogoro kwenye usaili narudi zangu Dar ninapoishi.. Kutokana na ugumu wa maisha, nimebakiwa na shilingi 3000 tu mfukoni hapo nikiwaza chakula cha jioni pamoja na nauli ya daladala..tena ukizingatia Mbagala ilivyo mbali.. Nikajipa moyo siku itapita.
Tulipofika Chalinze, basi lilisimama na akapanda mrembo mmoja matata sana, umri kati ya miaka 24 hadi 26, mwenye urefu wa wastani, mweupe, mwembamba kiasi huku akiwa ametupia suruali ya jinsi pamoja na t shirt iliyomkaa vizuri na kuonesha umbo lake maridhawa la namba nane. Akaja akaketi kwenye siti iliyopo pembeni mwangu kwa kuwa kabla ya kufika chalinze, abiria aliyekuwa amekaa jirani yangu alishuka.. Basi tukasalimiana na safari ikaendelea.
Akajitambulisha anaitwa Karishma.. Na Mimi nikamwambia naitwa Abdulghan nilichukua jina la mdogo wangu abdulghanim ilimradi tu nikaeka zile za kihindi fulani ilimladi mambo yaende sawa. Basi tukapiga stori nyingi sana.. Tulipokaribia kufika Mbezi akaniaga akasema atashuka kituo cha mbezi mwisho kwani ndipo anapoishi. Basi nikamuaga..tukabadilishana namba za simu.. Kwa kweli alikuwa mcheshi sana na nilifurahi mno kupata namba zake nikijua nishapata bint mrembo mwenye asili ya kihindi.. Basi baada ya kufika Ubungo wakati natoa mizigo yangu sehemu ya kuhifadhia, nikaona pochi ya kike.
Nikakumbuka karishma nae aliweka mizigo yake pale..nikasema hebu nifungue niangalie ndani.. Heeeeh nikakuta pesa nyingi sana za kitanzania pamoja na Dola za marekani nyingi sana pamoja na vitambulisho vya karishma. Nikajiuliza, je nimpigie au nipotezee niondoke na pesa?? Wakati nawaza hayo ghafla nikaona simu inaita..Jina ni karishma. Dah..nikawazaaa nikiwazu huku simu inaita..nikaamua tu kupokea,
“Hallo, samahani Abdulghan eti umeona pochi yangu hapo hata sijui nimeipoteza wapi”
Nikamjibu ” Yah karishma ndio nimeiona sasa hivi nashuka Ubungo hapa nikawa nataka nikupigie simu”
“Ooooh thanks God! Yaan you can keep hizo hela but please naomba unisubiri nijekuchukua passport na visa yangu vitambulisho hivyo ni muhimu mno yani”
“Whaaat?? Mbona usiku sana! Are you serious?”
Ilikuwa inakaribia saa 6 usiku.
“Yah, why not? Sawa Nakusubiri Karishma.”
“ahsantee akasema Karishma”
“Usijali.. Nikiwa nafijiria sasa akifika usiku huu atarudi kweli kwao ama itakuwaje”.
Mawazo yakanijia nitaenda kulala nae kama atakubali.
Dah, ni kama nilichanganyikiwa ghafla.. Nikaona gari aina ya BMW X6 ikiingia langoni Mara nikamuona Karishma akishuka akiwa peke yake.
Nikawa nawaza, sijui itakuwaje huko ndani kama akikubali kwenda kulala na mimi ? Wakati nawaza hayo, mara nasikia Abdulghan nashukuru kwa kunihifadhia vitu vyangu mi siwezi kurudi nyumbani mana nimewaaga nitalala kwa rafiki yangu.
Sasa unaonaje tuende Landmark hotel tukalale pale mpaka asubuhi.
Mimi tena bila ya hiyana nikakubali kinyonge huku nikijua ataingia tu kwenye mtego.
Abdulghan mbona umeitikia kiunyonge au mi stahili kulala na wewe?.
Uzalengo ukanishinda usiseme hivyo Karishma kwanini usistahili?.
Nikapanda kwenye gari mpaka Landmark Hotel tukachukua chumba kimoja nikamuliza Mimi nitalala wapi choon au? Akanijibu utalala kitandani na Mimi.
Hivi naota ama kweli nikasema kimoyoni.
Abdulghan naenda kuoga nawe pia ujiadae nikirudi uende.
Mara akatoka choon akiwa na nightdress hee! Mtoto kajazia nyuma utasema body ya Nissan morano.
Salale! Anakuja kitandani nilipo.
“Unajua nini kilichotoea”
“We Abdulaziz Umejilaza tu hapo kwenye mkeka mbona hao samaki hivi umeongeza mkaa kweli? Na wakiungua hawo utakula wali na chumvi…”
Dah, mama yangu kaniamsha nilikuwa ndotoni, tena usingizi wa mchana..Duuh!!!
Dah! Hizi ndoto nyengine

Gusa hapa>> USOME JAMBO ZURI ZAIDI KWAAJILI YAKO

VICHEKESHO VYA KUVUNJA MBAVU ZAKO

Kuna vichaa walitolewa hospitali moja kwenda nyingne asa wakiwa njiani wakaambiwa wakachimbe dawa(wajisaidie) alafu safari iendelee waliposhuka kila mtu na njia yake wakakimbia dereva kuona hivyo akamwambia konda tutafanyaje sasa? Konda akajibu niachie mimi nitaliweka sawa hilo wakaondoka wakafika stend wakakuta abiria kibao wakashusha nauli watu wakajazana konda akasema dereva haina kituo hiyo mojakwa moja mpaka hospital,.

Gusa hapa ujiunge>> VICHEKESHO KUMU VYA KUVUNJAMBAVU 2022


MKE: vipi leo mbona mapema na mpole?
MUME: ofisi yetu imeungua na watu wote wamekufa,
MKE: ilikuwaje wewe ukapona?
MUME: nilikuwa chooni, jirani na ofisi najisaidia.
MKE: Loh masikini familia zao itakuwaje?
MUME: watalipwa milioni 100 kila mfiwa.
MKE KWA HASIRA: ona sasa na wewe kunya kunya kwako umetukosesha mihela..ungeenda kunya akhera……
Ungekuwa Mwanaume Ungejibu Vip


Mlevi kakutwa akikojoa eneo la
shule, Mwalimu mkuu akamuuliza,
hilo bango hapo limeandikwaje?
Mlevi akajibu ‘USIKOJOE HAPA’.
Mwl: Kwahiyo unafanya nini
hapo?
Mlevi kwa makini na upole
akajibu: HAKI YA MUNGU NILIJUA
NDIO JINA LA SHULE!!


STORI ZA VICHEKESHO VYA KUVUNJA MBAVU

mke; mme wangu ungekuwa tajiri ningefurahi
mimi; kwa nini?
mke; ungekuta na sisi tuna gari nzuri hatutembeu kwa mguu
mimi; ah wap,unadhani ningekuwa tajiri ningekuwa na wewe?ungekuta natoka na kina wema,zari…

Gusa hapa jiunge>> VICHEKESHO YA MWEZI HUU TAFUTA HAPA (MPYA)

Mlevi katuma meseji kwa mke wake; “Darling nipo bar napata mbili tatu,nitaludi nyumbani ndani ya dakika hamsini zijazo,ukiona kimya tafadhari soma tena hii meseji”. mke wake akakaa dakika hamsini kimya,kaisoma tena meseji inamwambia Nitarudi nyumbani ndani ya dakika hamsini zijazo ukiona kimya tafadhari soma tena hii meseji.
hahahahaaaa…………kumbe kila akirudia mesejiinamwambia vilevile ila inamuongezea dakika hamsini..jamaa akarudi kesho yake asubuhi mkewe alichoka ile mbaya…

Magemu mazuri ya kucheza kwenye Simu


Mwalimu aliingia darasani na kuwauliza wanafunzi juu ya ndoto zao za baadae.
MWAL: John we unataka ukiwa mkubwa uwe nani?
JOHN: Nataka niwe daktari wa moyo niwasaidie watanzania wanaougua magonjwa ya moyo.
MWAL: vizuri. Na wewe Rose unataka kuwa nani?
ROSE: Nataka kuwa rubani, niweze kusaidia watu wanapenda kusafiri kw anga.
MWAL: Safi sana Rose. Utakua utakua mfano kwa wasichana wenzio kuwa na bidii kwenye masomo ya sayansi.
MWAL: Na wewe James??
JAMES: mimi nataka kuwa tajiri mkubwa sana. Niwe na nyumba Tanzania, S.Africa, Marekani na Dubai. Niwe na gari 7 za kutembelea. Kila siku nabadilisha. Leo nikipanda hii, siirudii hadi week iishe. Nataka niwe namiliki viwanda, Makampuni, ndege binafsi na mashamba makubwa. Nataka niwe na nguvu serikalini ya kuamua nani awe Rais na nani asiwe……”
Akameza mate kisha akaendelea….
“Nataka kuwa na walinzi 20 wenye silaha nzito wakinizunguka, na watumishi wakininyenyekea. Nataka kuwa bilionea ninayeogopwa. Lakini pia nataka kuwa na mke mzuuuri sana ambaye nitakuwa natembea nae kila mahali.”
MWAL: ndoto nzuri sn lakini unahitaji bidii sana kutimiza. Haya na wewe Jenny tueleze unataka kuwa nani??
JENNY: Nataka kuwa mke wa James.!!

Gusa hapa>> USOME JAMBO ZURI ZAIDI KWAAJILI YAKO


WALEVI WAWILI KATIKA MAZUNGUMZO YAO
MLEVI 1 hivi rafiki yangu china ni mbali kweli
MLEVI 2 sidhani mbona pale kazin kuna mchina anakuja na baiskeli
😆😆😆😆😆

😂😂 😂


STORI MPYA ZA VICHEKESHO

🙊🙈✍️
JAMAA KATOKA CHURCH KAFIKA HOME KWAKE, AKAMKUMBATIA MKEWE NA KUMBEBA JUU JUU KWA HAMAKI… 😴😴

MKE; KWANI VP LEO MUMEWANGU MAPENZI YAMEONGEZEKA MPK UNAYAFANYA HAYA MPK NASHANGAA.. !!!!🙄🙄

MUME: AKAMJIBU MKEWE KUWA CHURCH WAMEAMBIWA WAYANYANYUE MATATIZO Yao JUU MUNGU AYAONE… 🙆🙆🙆🏃🏃🙆🐼/span>

Gusa hapa>> USOME JAMBO ZURI ZAIDI KWAAJILI YAKO

Binti;;

Binti alipokea txt kwny cm yake “Hi,mremb una boyfriend?” BINTI:Ndio, ninae kwan we nan?? “Mimi ni baba yako naomb nkukute hapo nyumbn unielez vzuri” Baad ya mda kidog akapokea text nyingn “Hlw!,una boyfriend?” BINTI:Cna kabixaa! Bt u nan tena?? “Mi ni boyfriend wako nlitak kujua unavyojicfia kuw na mm, kwl nimegundua hunipend” BINTI:Oh,sorr bby nlijua baba ang mana ametok kuniulza swl iloilo! “Yes,ndio mm baba yako yan leo utantambua nkirud uko shenz ww!!!!”..


Gusa hapa>> USOME JAMBO ZURI ZAIDI KWAAJILI YAKO

MUELEVU NA MJINGA
Mwelevu na Mjinga walienda ktk usaili, walipofika kabla hawajaingia wakakubaliana aanze Mwerevu kisha akitoka ampe majibu Mjinga ili wote wapate kazi.*
*Basi Mwerevu akaingia na maswali yakawa hivi:-*
*Msaili:- Tanzania ilipata Uhuru mwaka gani?*
*Mwerevu:- ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mpaka 1961 kutokana na sababu mbalimbali..*
*Msaili:- Nani hasa alihusika na upatikanaji wa Uhuru huo?*
*Mwerevu:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J.K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia.*
*Msaili:- Inasemekana katika sayari ya Mars kuna viumbe wanaishi, je ni Kweli?*
*Mwerevu:- Watu wengi wanasema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi.*
*Baada ya Mwerevu kutoka basi Mjinga akapewa majibu yote..*
*Kuingia ktk usaili maswali yakawa hivi:-*
*Msaili:- Tuambie ulizaliwa mwaka gani?*
*Mjinga:- Ilitakiwa iwe mwaka 1960 ila ikasogezwa mbele mpaka mwaka 1961 kutokana na sababu mbali mbali.*
*Msaili:- Mungu Wangu, BABA yako anaitwa nani?*
*Mjinga:- Kuna watu wengi walihusika ila Mwl. J. K. Nyerere ndiye alikuja kumalizia .*
*Msaili:- Hivi wewe ni chizi?*
*Mjinga:- watu wengi husema hivyo lakini haijathibitishwa na wanasayansi*😂😂😂😂😂😂


Gusa hapa>> USOME JAMBO ZURI ZAIDI KWAAJILI YAKO

STORI YA KUSIKITISHA
majamaa watatu walikodi chumba katika hoteli moja hapa mjini, wakawa wamepata chumba cha mwisho kabixa ambacho kipo ghorofa ya hamsini (50), walipotoka walirudi wakakuta umeme umekatika, hvyo iliwabidi kupanda ngazi ili waeze kufika kwny chumba chao, hivyo walikubaliana wakwanza atapiga stori ya kuchekesha, wapili atapiga stori za kutisha na watatu atawapigia stori za kuhuzunisha, wa kwanza alpiga ctor za kuchekesa mpk walpo fika ghorofa ya 15, akafata yule wa pili akawapigia ctori za kutisha mpk walipofika ghorofa ya 30, akapokea yule watatu akawapigia story za kuhuzunisha. walipofika ghorofa ya 50 aliwageukia wenzake na kuwaambia na hii ndo yakuhuzunisha zaidi, TUMESAHAU KUCHUKUA UFUNGUO PALE MAPOKEZI…


STORI ZA VICHEKESHO ZINAZOWEZA KUKU VUNJA MBAVU


STESHENI YA TRENI

Jamaa wawili walifika stesheni wakakuta tren ndo kwanza inaondoka. Wakaanza kuikimbiza. Mmoja akafanikiwa kupanda akaondoka…

Yule Aliye baki akaanza kucheka sanaa
Mpaka machozi yakamtuka. Watu wakamuuliza, unacheka nini sasa wakati umeachwa? Akawajibu:
“Kinacho nichekesha , yule aliye panda alikuwa ananisindikiza.

GUSA HAPA>> KUPATA VITU VIZURI ZAIDI KWAAJILI YAKO SASA


NDEGE ILIOPATA AJALI

Ndege ilipata hitilafu angani Ndipo rubani akatoa taarifa kwamba ndege imepata hitilafu na itadondoka baada ya dakika 10. Ndani ya ndege kulikuwa na watu watano Lakini maparashuti yalikuwa manne tu.
Watu hao ni mchungaji, waziri, mwanajeshi, Msukuma na mwanafunzi wa chekechea, Mchungaji akasema yeye anategemewa na kanisa hivyo hapaswi kufa. Akachukua parachute akaruka. Waziri akasema wananchi wanamtegemea alete maendeleo, Akachukua parachute akaruka. Msukuma akasema familia inamtegamea akachukua parachute akaruka faster.
Wakabaki mwanajeshi na mwanafunzi wa chekechea. Yule mjeshi akamtazama mwanafunzi akamuonea huruma kisha akasema. Mimi najitolea kufa kwa ajili yako, we chukua hilo parachute lililobaki ujiokoe halafu mi ntakufa na hii ndege.
Yule mwanafunzi akajibu “usijali yamebaki maparashuti mawili” yule mjeshi akashangaa akauliza mawili kivipi.? Mwanafunzi akasema YULE MSUKUMA KACHUKUA BEGI LANGU LA SHULE ALIDHANI NI PARASHUTI


NAMBA MPYA

Mke wangu alisajili line mpya jina la Jenifer Godson bila mimi kujua.
Jana usiku nimerudi home akaniomba elfu 10 akasuke.
Nikajibu sina elfu 10 nikampa buku 4
Wakati tumelala, Mara Paa msg katika simu yangu

“HI MY LOVE”.

Kidume nikatoka nje nikaenda toilet, nikaijibu:
“we nani”

MSG: ni mimi Jane Msambwanda”.

Kusikia Msambwanda, mshipa wa ubongo ukanicheza.
MIMI: Jane Msambwanda wa wapi tena?”

MSG: Bwana baby nawe, si pale unapokulaga kila siku?”

MIMI: “ooh, kumbe unaitwaga Jenifer, namba yangu umeipata wapi?

MSG: “nimepewa na rafiki yako DJ Tipwil, nakupenda sana handsome, sema huwa naogopaga kukwambia, ila mi sijiwez juu yako, yaani kila ukija kula, natamani usiondoke, nikwambie yaliyomo moyoni mwangu, nateseka sana mwenzio”

MIMI: Jamani pole mpenzi, hata mimi nilikuwa nakupenda, yaan kila nikiona huo msambwanda nahisi mzunguko wa damu kubadilika, I love you too honey.

MSG: Basi mpenzi ,nikuombe kitu

MIMI: aah, sema tu

MSG: naomba elfu 50

MIMI: nakutumia sasa ivi”
(NIKATUMA)

MSG: Waaoo asante mume wangu, haya rudi ndani tulale, mi mkeo MAMA KIDUKU hapa..

🙆‍♂🙆‍♂🙆‍♂

🎼_hapo ndo utaukumbuka wimbo wa dunia Lukumba lukumba🎼


KITOTO KIJINGA

WAGOGO watatu walisafiri, walipofika kwa ndugu yao mjini wakapewa soda wakasemezana GALIMUZINZI, Yaani tamu, walipoondoka mmoja alitia kizibo(cha kisoda) mfukon badae walipotoka nje akamnong’oneza mwenzie MUYANGU NASOLA MBEYU! Yaani, mwenzio nimechukua mbegu nikapande.


HUU NDIO UBAYA WA KUWA NA MWALIMU MKUU ALIESOMEA SAYANSI

*MWALIMU: Nani alimuuwa Chifu Mkwawa?
Mwanafunzi 1; Sio mimi
Mwanafunzi 2: Jana sikuja shule
Mwanafunzi 3:Mwalimu kwa kweli sie unatuonea….baada ya mwalimu kuona darasa zima ni vilaza akaamua kumtaarifu mwalimu mkuu, ambaye naye akaja kwa ukali
MWALIMU MKUU: Nani aliyemuua Chifu Mkwawa? Msipojibu humu ndani patawaka moto…darasa zima wakaanza kulia
Darasa:Mwalimu sio sisi
Mwalimu Mkuu akamgeukia mwalimu wake akamuuliza, “Mwalimu una uhakika huyo muuwaji yuko darasa hili?” 😂😂😂😂


KITAMBULISHO CHANGU

NLKUA NATEMBEA NKAONA MWENDAWAZIMU AKIOKOTA NOTI YA KSH.1000 MBELE YANGU.
MIMI: samahani sana boss, hio uliookota hapo ni kitambulisho changu.
MWENDAWAZIMU: hatakama cjui kitambulisho lakini hiki si kitambulisho, OK Kama ni kitambulisho chako kweli nambie waitwa Nani? Na umezaliwa mwaka gani
MIMI: naitwa JAMHURI KUU YA KENYA na nimezaliwa mwaka wa 1000.
MWENDAWAZIMU: oh Pole boss kwa kukupotezea wakati shika kitambulisho chako, lakini mbona uko na vitambulisho vingi na unavibwagabwaga ovyoovyo? Nko na vyengine ishirini hapa acha nkupe mwenyewe.
MIMI: asante sana kwa kuniokotea izo ni photocopy na nimuhimu sana kwangu. Zilipotea tangu mwakajana zinanpatia shida sana.