Nikatoka pale dirishani nikakaa kitandani nawaza “Dah ila huyu mwanamke mzuri… ila simuelewi, inamaana yeye ndio Tausi kweli? na mambo yaliokua yanaendelea hapo ni mambo gani sasa?”.
Nilikaa kama dakika 30 mule ndani nikiwa nimeduwaa nawaza lakini ghafla nikasikia mlio wa ndoo kama zimegongana hivi pale nje. Nikachungulia dirishani nikamuona Salma amevaa khanga ametoka kuoga alikua anaweka ndoo ya kuogea pale nje na baada ya kuweka nikakuta kama anatembea anakuja kama kwenye chumba changu hivi. Nilishtuka sana, nikatoka pale dirishani alafu nikakaa haraka huku nikiwa nawaza “Anakuja huku au?” huku nimetega sikio zote mbili mlangoni. Nikasikia visauti vya mlango ukigongwa kidogo pamoja na sauti ndogo ya Salma “Hodi”.
Mimi moyo ukadunda “Duh!” nikaitikia “Karibu” huku nikiweka akili na macho yangu yote mlangoni kuona kama anataka mimi niende mlangoni nikamsikilize au ataingia ndani maana mlango nilikua sijaufunga, Niilikua kama nimeufunga hivi ila niliacha kinafasi kidogo. Baada ya sekunde chache nikaona mlango unasukumwa, Salma huyo anaingia ndani. Mtoto alikua kajifunga khanga na haijafika hata magotini. Paja zilikua nene na kwakua alitoka kuoga kwenye ngozi yake nyeupe kulikua kama kuna vitone vidogo vidogo sana vya maji. Sura yake ilikua nzuri lakini kwa muda huo macho yake yalikua yamevimba alafu mekundu kutokana na kulia. Hata nilivyokua nikimuangalia muda huo alikua ni mtu ambae anataka kulia lakini anajikaza. Laikini bado alikua ni mzuri sana.
Basi akasimama mbele yangu alafu akaniangalia usoni kidogo na akaniambia “Mambo” kisha akaangalia chini kwa aibu huku akijiminya minya vidole vya mikono. Mimi nikamwambia “Fresh Salma, Niambie” akajibu “Safi” huku akiwa anaendelea kuangalia chini mara ajikune shingo kidogo. Mimi nilikua sijajua amefuata nini hapo muda huo maana sikumuita hivyo nikataka kumuuliza alichofuata lakini kabla sijamuulliza nikakuta anaanza kusema “Sa… Samahani… nilikua naomba unisaidie ile hela nilio irudisha. Sasa hivi nipo tayari kukupa ulichokua unahitaji”.
Mh mimi kusikia hivyo nikashtuka sana maana pamoja nakwamba nilikua nasikia watu wanasema yeye ni Tausi na kazi yake ni kujiuza nilikua bado siamini sana maana nilikua nampenda sana na sikuzani kuwa ni mtu wa hivyo kabla ya kuuweka moyo wangu kwake. Sikumbuki nilitaka neseme nini baada ya kuambiwa hivyo ila nakumbuka jasho la ajabu lilinishuka ghafla. Nahisi Salma aliona hali yangu maana nikakuta tu kabla sijaongea chochote, Salma akaanza kudondosha mimachozi huku akisema “Ila mimi ngoja nikwambie tu ukweli… Mimi sasa ivi sipo kama watu wanavyonifikilia… Kuna sehemu ya maisha yangu natamani niibadilishe ila sijui pakuanzia maana hata nikiikimbia naona inanikimbilia. Kuna muda naona hata nikiielezea kwa watu hakuna atakae nisaidia ila naona bora nikwambiie tu wewe maana ndio mtu ambae nimekupenda kwa sasa japo sijui utakavyo nichukulia”
Alivyokua akiongea hivyo niliganda nilikuwa namsikiliza kwa makini kweli maana alikua anaonekana anatoa maneno toka moyoni mwake kabisa yani. Salma aliendelea kuongea, akasema “Mimi naitwa Salma na hilo ni jina langu kabisa japo wengi hunijua kwa jina la Tausi hapa mjini. Nilipewa jina la Tausi na dada mmoja ambae alinileta hapa mjini toka kwa bibi yangu huko Tanga. Huyu dada alikua anaitwa Mariam na kwasasa hayupo hapa Dar, alipata fulsa ya kwenda kufanya kazi Kanada na sina mawasiliano nae toka aende huko. Alinitoa kule Tanga kuja huku Dar akidai kuna kazi nzuri anaifanya na atanifundisha maana yeye kule alikua anakuja kusalimia wazazi wake tu na hao wazazi walikua wanaishi karibu na bibi yangu. Mimi nilikua nakaa kwa bibi kwasababu wazazi wangu walifariki kwa ajari ya gari wakati hawana hata nyumba na ndugu wengine hawakua na msaada kwangu kiasi kwamba nilishindwa kumaliza hata shule ya sekondari.
Huyo dada ni kama alikua ananisaidia hivi kidogo niwe na uwezo wa kujitegemea maana nilifika kwenye umri ambao nilitakiwa nijipende, niwe na muonekano msafi lakini sina pesa hata ya kununua mahitaji yangu. Alivyonileta hapa mjini akanifundisha kazi aliokua akiifanya ambayo nikuuza mwili. Nilikua naogopa sana pindi alipokua akinifundisha maana kilikua ni kitu cha ajabu sana kwangu ila mazingira alioniweka yaliniondoa hofu kidogo maana jirani zetu na marafiki zetu walikua wanafanya kazi hiyo hiyo. Baadae niliingia mpaka kwenye makundi ya watu wanaofanya kazi hiyo na makundi hayo yalikua yana utaratibu wa kuchangisha pesa kwa kila mwanakikundi na kununuliana vitu. Usipokua unapeleka pesa kwa muda mrefu inakua kama unadaiwa hivi, wanakuja kuchukua vyombo au vitu vyako na kukutoa katika kikundi. Njia kuu ya kupata pesa za kupeleka kwenye kikundi ni kujiuza tu, wanakikundi wote wanajua hilo.
Mimi kiukweli kazi hii niliifanya kwa miezi michache sana na moyo ukaanza kukataa kuendelea lakini nilikua naogopa kuacha kila nikiwaangalia watu walionizunguka au nikifikilia pesa ninazotakiwa kutoa ili mambo yangu yaende vizuri. Ikafika wakati watu wengi wanajua najiuza na wananiita majina ya hovyo na kunisema vibaya karibu kila kona ninayofahamika. Watu wengine wananisema vibaya ila hawajawahi uona mwili wangu.
Nilichoshwa na hayo mambo, nikaamua toka moyoni kuiacha hiyo kazi. Nilijaribu kutafuta mtu ambae atanioa ili nitulie lakini kila nikikutana na mwanaume anakua ananichukulia mimi ni mtu ninaejiuza hivyo anakua hana mpango na mimi. Wengine wanaweka mipango lakini inaharibika kutokana na watu kuwambia kuwa najiuza wakati mimi nataka kuacha.
Nina miezi sasa nimejitenga na marafiki wanaojiuza, nimepanga chumba huku ambako watu hawanijui sana na nilianza mpaka kuuza nguo za watoto ili kuondokana na kazi ya kujiuza lakini leo mambo yamebadilikatena. Rafiki zangu wamekuja kubeba vitu walivyoninunulia na mbaya zaidi wameondoka mpaka na nguo ninazouza. Hapa sina kitu cha maana kwenye chumba changu, sina hela na sielewi pakuipata kwa haraka zaidi ya kuingia tena kwenye biashara ya kujiuza na ndio maana nimekuja kwako hivi.
Samahani kama unanipenda kweli, najua utakua umeumia kujua mambo yangu ila naomba utambue kuwa na mimi nakupenda sana lakini maisha yangu mimi siyaelewi. Natamani kutoka kwenye maisha haya na kuwa na mwanaume mmoja maishani atakae nielewa lakini kila nikijaribu, vitu vinaingilia kati, nadondoka tena kwenye kazi ya kujiuza. Nikifanikiwa kutoka kwenye maisha haya mabaya, sitatamani kurudi tena. Natamani kuitwa mke, natamani kuheshimiwa kama watu wengine na natamani nifute vitu vyote vibaya nilivyowahi fanya lakini nashindwa.”
INAENDELEA…
Tag Archives: simulizi za mapenzi
UTAMU WA JUMLA 07 (Simulizi ya Maandishi)
Nilikaa kitandani nikaanza kuwaza “Yaani inamaana Tausi ndio huyu Salma?… Na inamaana wale madada ulioniamsha nikiwa nimelala walikua wanamtaka Salma ambae ndie huyo Tausi?… alafu huyo tausi anajiuza?… Ah hapana, Mpenzi wangu Salma sio huyo Tausi wao”
Lakini nikaanza kufikilia tena “Au kweli anaitwa Tausi na anajiuza ndio maana kila nikimtaka tulale wote anakataa? huenda anataka hela huyu…. Dah ila ananiumiza moyo huyu mwanamke. Sijui kwasababu nampenda?… Mbona moyo wangu unaumia hivi nikiwaza kuwa ni kweli anajiuza?… Mh Ila kama ni kweli Salma anajiuza basi siku zote hizi alikua ananiona mshamba na mapenzi yangu ya maneno haya… Yani nabembeleza na kuogopa kabisa kumbe mtu mwenyewe anataka hela na sio maneno” nilpokua nafikilia hivyo moyo ulikua unaumia na nikaanza kuona mpaka kizungu zungu. Nikalala kitandani huku nikijiona mshamba kweli. Siku hiyo nilikua humo ndani mpaka Salma akarudi. Salma alivyorudi alisalimiana na mimi nikiwa ndani huku yeye akiwa nje.
Sikutaka kupiga nae stori kabisa siku hiyo. usiku ulipoingia alikua akinitumia ujumbe kwenye simu lakini sikua na jibu maana nilikua na mawazo alafu nahisi kama Salma ananiona mshamba na vitu vyote anavyofanya ni kama ananiigizia hivi. Nilikua nazisoma kabisa ila sijibu na alivyona sijibu nikakuta amenitumia sms akisema “Njoo tulale wote” lakini nikaipuuzia. Nikakuta tena akasema “Njoo basi, nakusubiri hapa mlangoni kwangu”. Mh mimi kuona hivyo tamaa ikaniingia kidogo nikawaza “Mh ngoja niende tu na nikipata nafasi ya kula tunda ntakula tu maana pamoja nakwamba anajiuza bado namtamani… Ngoja nikamkunje mpaka hasira ziishe, huenda naweza punguza hata mawazo kwa kufanya hivyo”. Nikatoka pale kitandani nilipo jilaza ili nitoke nje niende kwa Salma lakini kabla sijaenda kwa Salma, akili ikaniambia “Nenda na hela maana anauza huyo… Usije ukaumbuka huko”. Na mimi kweli nikachukua hela za kutosha na kutoka nje kuelekea mlangoni kwa Salma.
Nilipofika mlangoni kwake tu nikakuta mlango wake unafunguliwa ili niingie lakini kabla sijaingia alinisimamisha pale pale kwa mapozi ya kimahaba hivi akiwa amevaa kinguo kimoja chepesi kilichokua kimeacha aslimia kubwa mikate yake nje. Nikakuta ananiambia kwa sauti ya upole “Kwanini haujibu sms zangu?… nimekukosea nini?” basi mimi nilivyo muona anaongea hivyo nikaona ndio ananiona mshamba kabisa yani maana nimeambiwa yeye anaangalia hela tu. Sikupoteza muda kumjibu, nikachukua hela nilizokujanazo nikamshikisha mkononi mwake alafu nikamwambia “Samahani, unaweza kunihudumia usiku wa leo mpaka asubui?”. Nikakuta kashtuka, kaiangalia ile hela kisha kaniangalia mimi husoni kwa sekunde chache alafu akafunga mlango wake na kuniacha nimesimama pale mlangoni.
Baaada ya kuona hivyo mimi nikaona nirudi kwenye chumba changu tu na niliporudi nikakaa kama dakika moja hivi hali yangu nikiwa siielewi. Ghafla ikaingia SMS ya toka kwa Salma “Mimi sio mtu wa hivyo, kwanini unanichukulia hivyo?” mimi nikaona ananiigizia huyu, nikamjibu “We Tausi acha kunizungusha,mimi nipo tayari kulipia… si ndio kazi yako hiyo?” Yeye akasema “Nani Tausi? Mimi sio tausi” alafu hapo hapo kabla sijamjibu akasema “Njoo uchukue hela yako, nimeiweka chini mlangoni kwangu. wakiiba usinidai”. Mh mimi nikaona niangalie kama kweli ameiweka chini hela yangu, nikakuta kweli ipo chini pale mlangoni kwake. Nikaichukua ile hela pale mlangoni kwake alafu nikarudi kwenye chumba changu. Sikujibu SMS yoyote muda huo mpaka akapiga simu akawa anaongea mambo yasio eleweka kwa sauti kama ya kulia hivi eti “Wasikudanganye hao… nakupenda… mimi sio wa hivyo… Tausi sio jina langu, naitwa Salma… Watu wananiongelea vibaya. Mbona huongei sasa? wewe huongei?” mimi nilikua simjibu, alikata simu.
Sikutaka kumjibu chochote siku hiyo mpaka asubui ikafika, nikajiandaa kwenda kwenye mafunzo yalionileta mjini hapo alafu nikaondoka kwenda kwenye mafunzo. Nilivyokua naondoka niliacha mlango wa Salma haujafunguliwa na ulikua ukionekana kama Salma bado yupo ndani hajaamka. Sikua namjali sana Salma muda huo maana nilikua naona ananiumiza japo moyoni bado nampenda.
Kule kwenye mafunzo nilikua sijaenda siku za nyuma na nilivyoenda siku hiyo nilikuta kumbe katika siku ambazo sikwenda kampuni ilisema kila mtu anaetaka kuajiriwa pindi mafunzo yatakapoisha inatakiwa alipie Milioni 10 pindi mafunzo yatakapoisha ila watakao toa ndani ya wiki hiyo milioni 5 hawatatakiwa kulipa tena. Hiyo ni kama punguzo kwa watu watakaolipia mapema. Basi mimi nikaona imebaki siku moja tu ofa iishe na nilipokua narudi toka mafunzoni nikawa nawaza kwamba nikifika nyumbani nikawapigie simu wazazi na kuwajulisha juu ya hili. Nilipokua nafika kwenye nyumba niliokua nakaa nikakuta watu wengi kidogo maeneo yale na tena ni wanawake alafu wapo maeneo ya chumba cha Salma.
Nilikua sielewi wamefuata nini pale ingawa nilikua naona wanatoa kitanda na vitu vingine ndani ya chumba cha salma. Sikutaka kujihusisha nao, nikaelekea moja kwa moja kwenye chumba changu na kukaa humo ila nilipokua nimekaa nikawa nasikia uko nje watu wakitupa maneno kama “Tumekutafuta sana… Kwenye simu hupatikani una mwezi sasa… Kama yamekushinda yaache yaende na raha zake… mwanamke huna haya”. Nikaona ngoja nichungulie dirishani labla nitaona vizuri kinachoendelea, nikaona watu wanabeba vitu wanaondoka navyo na kumuacha Salma amekaa mlangoni kwake kama anajizuia kulia hivi ila machozi kiasi yana mdondoka. Watu hao walikua wakiondoka huku wakitupa maneno ya dharau sana na kulitaja jina la Tausi na sio Salma.
Nikatoka pale dirishani nikakaa kitandani nawaza “Dah ila huyu mwanamke mzuri… ila simuelewi, inamaana yeye ndio Tausi kweli? na mambo yaliokua yanaendelea hapo ni mambo gani sasa?”.
INAENDELEA…
UTAMU WA JUMLA 06 (Simulizi ya Maandishi)
Walivyoondoka tu nikajisemea “Bora wameniamsha maana simu nimeiweka pabaya kiasi kwamba mwizi angepita maeneo haya angechukua simu bila mimi kujua”. Baada ya hapo mawazo ya Salma yakaanza kuteka kichwa changu. Nikaanza kuwaza “Dah Salma nae sijui kaenda wapi?… Naanza mpaka kukosa raha yani. Na hii ndoto nilioiota hapa ni ukweli au imesababishwa na makelele ya waliokua wananiamsha tu? Itakua ni hawa mbwa wameniletea lindoto la ajabu… ila sasa mbona hayupo na hakuniambia jana kwamba hatokuepo leo?”Niliwaza mambo mengi sana hapo lakini kichwa kilikua hakinipi majibu ya moja kwa moja, nilikua najiuliza maswali yanayo zaa maswali tu.
Mida ya saa 7 mchana hivi nikiwa palepale mlangoni nilikuta Salma anarudi na anarudi na mzigo mkubwa kiasi kwenye pikipiki. Nilivyomuona Moyo ukadunda kwa furaha “Nduh” alafu nikaendelea kuwaangalia yeye na dereva wa pikipiki wakifika pale. Walipofika nikasalimiana na dereva wa pikipiki pamoja na Salma pia alafu nikasaidia kutua mzigo na kumuwekea mlangoni kwake maana alishakua malaika wangu muda huo, vitu vyake vigumu na vizito lazima nijihusishe navyo.
Baada ya hapo dereva wa pikipiki aliondoka na kutuacha pale na mimi hapo nilimuuliza alikua wapi akaniambia alikua kununua mzigo wa nguo za watoto anataka kuanza kuuza maana alikua hana kazi ya kufanya hapo mjini. Aliponijibu tu hivyo mimi sikumchimba sana kwenye mambo ya kazi huko, nikajikuta moyo umekua mwepesi alafu nikawa na furaha ya ajabu kumuona malaika wangu Salma amerudi.
Siku hiyo tukaendelea kuongea mambo ya mahusiano yetu na mambo mengine ya kijinga kijinga mpaka jua linazama. Usiku uliingia na katika kutumiana nae ujumbe usiku huo nilimuomba aje tulale wote lakini alikataa, nikamuomba nimfuate nikalale kwake lakini bado alikataa. Nikajua huenda ni mwanamke muoga na anaogopa kukubari kirahisi kuwa na mwanaume, hivyo nikamuacha siku hiyo, sikumsumbua sana. Na hata kulivyokucha niliendelea kuwa nae vizuri tu kimaongezi ila sikuingizia swala la yeye kukataa kulala na mimi usiku. Sikwenda kwenye mafunzo siku hiyo ili tu nibaki na yeye nyumbani.

Siku ya pili usiku katika kuchati nikaamua kujaribu tena kumshawishi tulale wote usiku huo chumbani kwangu ili angalau nipate nafasi ya kumkamata na kumgusa panapotakiwa. Nakumbuka nilimwambia “Salma, njoo ulale kwangu leo… Natamani tulale wote” lakini hakukubari, akajibu “Ah hapana, huko siji hahaha”. Nilijaribu pia kumwambia anifungulie mlango wa chumba chake ili niende nikalalale kwenye chumba chake lakini hakuniruhusu kufanya hivyo, alikataa. Siku hiyo nilijisikia vibaya kidogo maana ilikua ni mara ya pili kunigomea lakini nikajitahidi kupuuza alafu tukaendelea kuongelea mambo mengine. Kulivyokucha, tulikua tunaongea mambo ya mapenzi na vitu vingine kama kawaida lakini sikua naingizia mambo ya yeye kukataa kulala na mimi usiku. Na kiukweli nilikua siwezi muuliza “Kwanini hutaki kulala na mimi?” akiwa mbele ya macho yangu kwakua nilikua kwa kiasi flani namuogopa na pia kichwani nilikua nawaza “Nisiwe na haraka, huenda usiku unaofuata atakubari”. Jambo hili lilinipa mawazo sana mpaka nikashindwa tena kwenda kusoma mafunzo, nikabakia tu nyumbani na yeye.
Siku ya tatu usiku pia alinigomea na siku hiyo niliumia sana maana ilikua ni mara ya tatu hiyo najaribu kumshawishi na hanikubalii. Lakini usiku huo nilijikaza tena nikaendelea kuongeanae mambo mengine tu. Na baada ya kukucha nikakutananae kama kawaida na tulikua kama wapenzi kabisa katika kusalimiana na kuongea. Siku hiyo nilibaki nyumbani ili niongee nae tena kama kawaida lakini sikupata nafasi ya kukaa nae muda mrefu maana mida ya saa 3 asubui alikua anaenda kuuza nguo za watoto na aliniaga na aliniambia anaweza kurudi jioni.
Hiyo siku Salma alivyoondoka na kuniacha pale nyumbani nilikumbwa na mawazo mengi sana juu yake kwakua nilikua simuelewi kabisa. Nakumbuka niliingia ndani ya chumba changu nikakaa nikawanawaza “Huyu dada mbona ananitesa hivi? Au ndo ameanza mambo aliokua ananifanyia Zuu kipindi nipo chuo? yaani nashindwa kumuelewa maana mchana tukikutana anakua kama ni mpenzi wangu ambae anaweza kubali chochote ninachomwambia lakini nikimwambia usiku tulale wote anakataa… Inamaana na haelewi ninachomaanisha au? Mh itakua huyu Salma hanipendi ila ananiigizia… Itakua ananiigizia tu huyu maana pamoja nakwamba nashindwa kumwambia moja kwa moja ninachotaka lakini jinsi ninavyomwambia tulale wote, yeye ilibidi aelewe tu nataka nini. Au mimi ndio nakosea kumwambia? Mh labla ila bado nampenda acha anisumbue tu akili yangu… Kuna siku ataniruhusu tu kugusa mtunda wake ule… yani mdada mweupee, mzuri sura alafu kapewa umbo lenye mamizigo ya kutosha… mmh acha anitese tu ila nikikamata nitambana mpaka atafurahi”
Wakati nimo ndani mule naendela kuwaza nikasikia kama kunamtu nje anapiga hodi hivi, Nilipotoka nje nikakutana na majamaa watatu. Mmoja kati yao niliposalimiana nae akajitambulisha kuwa yeye ndie mwenye kile chumba ambacho nilikikuta kwenye nyumba hiyo wakasema mwenye nacho amesafiri. Alisema amekuja hapo kuchukua vyombo vyake na ameishaongea na mwenye nyumba. Mimi nikamkubalia na baada ya dakika chache nikawa nawashuhudia wakifungua mlango na kuanza kutoa vitu kuvipeleka kwenye gari ambalo lilisimama mbali kidogo na kwenye nyumba.
Baadae na mimi nikaona nisiishie kuwaangalia tu, nikajumuika nao kuwasaidia kutoa vyombo na kupeleka kwenye gari. Basi tukaanza kupiga stori huku tukifanya kazi kama ilivyo kawaida kwa wanaume kupiga stori nyingi hatakama hatujajuana sana. Tulifanikiwa kupakia kila kitu kwenye gari na jamaa akaanza kuniaga. Nakumbuka yule jamaa alisema “Asante sana, mimi nimehamia mtaa wa mbele hapo kunajumba linawapangaji wengi, Hiyo nyumba ni ya mama mmoja tajiri sana anafahamika kama Mama Suzi anakaa kwenye jumba lake huko… Ukiwa na muda unaweza ukanitembelea mzee” basi mimi nikaitikia “Anh sawa, usiwaze”. Baada ya mimi kusema hivyo akasema “Poa bwana, utaniagia huyu Tausi maana naona hayupo sjui kaenda kujiuza huko hahaha”.
Mh mimi nikashtuka, nikamuuliza “Tausi yupi huyo?” akasema “huyo dada mweupe mwenye chumba hicho”. Mh nilishangaa nikajikuta naropoka “Anaitwa Tausi huyo?”. Huyo jamaa akajibu “Ndio.. kwani vipi? si ndio jina lake ilo au?” Muda huo niliona niseme tu “Ndio” ili tukaete maengezi. Nikamsikia jamaa akisema huku akiondoka “Nasikia huyo dada ni hela yako tu… ukimpa hela, anakupa chungawa. Kuna mitaa niliwahi muona wanamjua sana ila sijui mitaa ya huku kaamia kufanya nini… Kwaheri bwana”. Mimi sikua na maneno mengi hapo nikajibu “Sa.. sawa” alafu nikaenda haraka ndani kupumzisha akili maana hali yangu iliishaanza kuwa mbaya. Nilikaa kitandani nikaanza kuwaza “Yaani inamaana Tausi ndio huyu Salma?… Na inamaana wale madada ulioniamsha nikiwa nimelala walikua wanamtaka Salma ambae ndie huyo Tausi?… alafu huyo tausi anajiuza?… Ah hapana, Mpenzi wangu Salma sio huyo Tausi wao”…
INAENDELEA….
UTAMU WA JUMLA 05 (Simulizi ya Maandishi)
Ila kama huyu ni mke wa mtu basi waliosema mke wa mtu mtamu hawajakosea kabisa… Ngoja nimuulize” nikaifuta ile SMS niliotaka kuituma. Nilivyofuta nikamwambia tu “Salma, nikuulize Swali?” alafu ikapita kama dakika moja nikakuta anajibu “Ah hapana usiniulize, nijibu kwanza swali langu”….
Basi mimi nikamwambia “Skia Salma, nijibu kwanza swali ntakalokuuliza alafu ndio nitakwambia” nikakuta tu kaniambia “Nina hamu” nilipo soma nikawa nawaza “Anamaanisha nini huyu? mbona kama ametangulia mbele sana huyu… Neno tata hili… Anamanisha nini kusema hivi usiku huu? Dah sijui nimjibu nini sasa hapa?” kabla sijapata cha kumjibu nikakuta ametuma SMS nyingine imeandikwa “Nina hamu ya kumjua huyo anaenipenda”. Nilipoona amesema hivyo, nikamuelewa alichokua akimaanisha ila alikua ameishaniingiza tamaa juu ya kumpata maana aliposema tu anahamu akili yangu ikawa inaniletea picha za jinsi alivyoumbika, Salma alikua ni dada flani mzuri wa sura na amebalikiwa umbo.
Nikajikuta nimetupia mbali wazo la kumuuliza mambo ya kuolewa, nikamwambia “Sawa, huyo mtu anaekupenda ni mimi”. Alikaa kama dakika 3 hivi bila kujibu mpaka nikaanza kuwaza “Au nimekosea kumwambia? Mbona hajibu? Au anaandika ujumbe mrefu huyu… Dah” lakini ghafla nikakuta kajibu “Mmh Haya, lakini samahani, sijakuelewa vizuri unanipenda kivipi yani?”. Mh alivyosema hivyo nikawanawaza mbona kama anataka kukataa huyu wakati alikua kama anaelewa ninachotaka kumwambia?… Kwamba hajaelewa kweli?… Dah liwalo na liwe, ngoja nimuelekeze tu”. Basi nikatulia nikaandika “Salma, nakupenda sana na upendo wangu kwako nashindwa hata niuelezee vipi kwako ila tambua tu nahitaji tuwe wapenzi. nimejikuta tu nakupenda Salma, nahitaji nafasi katika moyo wako maana moyo wangu umeishauteka.” alafu nikamtumia. Akatulia kama dakika 2 hivi bila kujibu na mimi nikawa nasubiri huku moyo wangu unadunda “Nduh Nduh Nduh”.
Nakumbuka baada ya ukimya wa dakika chache akasema “Kitu gani umependa kutoka kwangu?” nikafikilia ninavyompenda nikaona siwezi elezea kitu gani nampendea maana nimejikuta tu napenda jinsi alivyo hivyo nikamjibu “Nakupenda jinsi ulivyo tu”. Akakaa tena kama dakika 4 ivi alafu akasema “kwani nikoje?” mimi nikamwambia “Ni dada falni mzuri, msafi, unajielewa na mtulivu pia, nahisi ni mungu aliniumbia… Nimejikuta navutiwa kua na wewe ikiwezekana maishani Salma. Naona nakua na furaha nikiwa na wewe. Alafu sijaanza leo kukupenda, nakupenda tangu nakutia machoni siku ile tuliokutana hapo nje”. Nilivyo mwambia hivyo, akaniambia “Kwani siku ile tuliokutana hapo nje ilikua ndio siku yako ya kwanza kuniona?” nikamjibu “Ndio salma, nilipokuona nilihisi nimekutana na malaika”. Basi nikakuta kanijibu ujumbe wa kucheka “Hahahaha” mimi nikamwambia “Kweli tena, sitanii”
Akakaa tena kama dakika 4 hivi alafu akasema “Sawa, mimi mwenyewe nakupenda ila naogopa usijekua unanidanganya mwisho ukaniumiza” mimi kwa haraka haraka nikawa na furaha nikamwambia “Siwezi fanya huo ujinga, Nakupenda sana Salma”. Nikakuta kanijibu “Haya, Nakupenda pia” nilipata furaha ya ajabu mpaka nikataka nipige kelele usiku huo mule ndani. Niliona kama ni bahati kuwa na mahusiano na dada huyo maana alikua ni mzuri na anajipenda sana kiasi kwamba ukimuona barabarani huwezi zani anatokea kwenye nyumba za kupanga, unaweza hisi ni mke wa mtu mwenye pesa sana au ni wale wadada wazuri wa kwenye video.
Basi usiku huo ulikua wa furaha sana na nilikua na hamu tukutane pindi kutakapokucha maana muda huo mvua ilikua inanyesha sana na ulikua muda mbaya tayari. Na kweli kulikucha ila nilichelewa kidogo kuamka kutokana na kuchelewa kulala na kitu cha kwanza kukifanya kilikua ni kumtumia Salma SMS lakini ilionesha kuwa hapatikani kwa muda huo. Nilipotoka nje nikakuta mlango wa Salma unaonekana kama Salma hayupo ndani maana umefungwa kwa nje. Nilivyona hivyo nilikua na vimaswali kichwani mpaka nikaamua nisiende kwenye mafunzo ya kampuni siku hiyo. Nilikaa tu chumbani kwangu, ukafika muda wa kula chakula nikaenda kununua alafu nikarudi nikakaa mlangoni kwangu nikawa nacheza gemu kumsubiri. Kwenye mida ya kama saa 4 asubui hivi nilikua nimechoka kushika simu, niliegemea pembeni ya mlango pale nje, usingizi ukanichukua.
Huko usingizini nikaanza kuota nipo na Salma sehemu nisioijua hata vizuri napambana kumshika na kumkumbatia Salma lakini nashindwa sababu yeye ananisukuma huku akinifokea kama hanijui kwa kusema “Hebu niachie… Wewe Mkaka vipi!… We mkaka!”. Dah ndoto hiyo ilifanya nishtuke toka usingizini na nilipofungua macho mbele yangu nikakuta Madada wawili wamesimama mbele yangu pale mbele ya mlango wangu wananiangalia huku wakiniamsha kwa kusema “Wewe kaka… Wewe kaka”. Basi mimi nikasema “Naam” huku nikiwa najaribu kuyaweka macho vizuri ili niwaone vizuri maana macho yangu yalikua usingizini na hao madada sikujua watakuwepo mbele yangu. Nikawaangalia sura zao haraka haraka nikakuta sura zao ni ngeni.
Basi nikakuta wananisalimia na mimi nikaitikia alafu wakauliza “Samahani kaka, tulikua tunaulizia anapokaa dada mmoja hivi anaitwa Tausi… tunasikia anakaa mitaa hii”. Mimi kwakua nilikua mgeni kidogo kwenye maeneo hayo na nilikua sijafahamiana sana na watu wa mtaa huo, sikuweza mtambua mtu wanaemuulizia hivyo nikawaambia “Ah mimi sijui watu wengi mtaa huu ila hapa hakuna mtu anaitwa tausi” wakanishukuru alafu wakawa wanaondoka. Madada hao walikua wasafi na wamevaa vinguo vifupi vinavyotega macho ya wanaume. Mimi kwa haraka haraka nilivyoona muonekano wao nilihisi huenda wanafanya kazi ya kuuza miili yao maana walikua wameanika vitu nje nje alafu hawajiwazii.
Walivyoondoka tu nikajisemea “Bora wameniamsha maana simu nimeiweka pabaya kiasi kwamba mwizi angepita maeneo haya angechukua simu bila mimi kujua”. Baada ya hapo mawazo ya Salma yakaanza kuteka kichwa changu. Nikaanza kuwaza “Dah Salma nae sijui kaenda wapi?… Naanza mpaka kukosa raha yani. Na hii ndoto nilioiota hapa ni ukweli au imesababishwa na makelele ya waliokua wananiamsha tu? Itakua ni hawa mbwa wameniletea lindoto la ajabu… ila sasa mbona hayupo na hakuniambia jana kwamba hatakuepo leo?”
INAENDELEA….
UTAMU WA JUMLA 04 (Simulizi ya Maandishi)
Mh alikua amejisogeza karibu yangu na tulikua tumegusana kabisa kiasi kwamba nilikua najikuta nahisi vitu tofauti na kitu ninachokifanya muda huo. Mwili wake mlaini ulileta joto la ajabu mwilini mwangu alipokua karibu yangu maaana alikua ni mwanamke mwenye kila sifa ya kuamsha hisia kwa mwanaume. Ukiachana na hayo yote, alikua ananukia vizuri.
Basi siku hiyo nilifanikiwa kumrushia nyimbo kwenye simu yake na tulipeana hata namba za simu ili tuweze kuwasiliana kwenye simu. Baada ya hapo tulikua tunaurafiki nae na urafiki huo ulikua kama unaelekea kuwa wa kimapenzi hivi japo nilikua sijawahi mwambia nampenda wala yeye hajawahi niambia hivyo.
Kuna siku tulikua tumekaa sehemu moja tunaongea pale nje mlangoni kwangu mida ya jioni… Nakumbuka tulikua tunapiga stori za kawaida huku mimi nimeshika simu yangu naangalia video za vichekesho. Salma alikua pembeni yangu kidogo upande wa kulia. Niliona video moja ikanichekesha sana mpaka nikasema “Hahah angalia video hii” Salma akasogea zaidi kwangu ili aone lakini katika kusogea kwake aliingia mpaka mwilini kabisa, mimi nikawa namuonesha video huku akili ikiwa imehama kutokana na yeye kuja mwilini mwangu. Nakumbuka aliangalia video ile alafu nikamuona akicheka “Hahaha…. wasumbufu hawa” huku akiyatoa macho yake kwenye simu na akaniangalia usoni.
Kwakua mimi akili ilikua haipo tena kwenye video ipo kwake, tukajikuta tumekaa kimya kwa sekunde chache tunaangaliana alafu tunataka kama kusogezeana midomo yetu hivi. Ilikua kama tunataka kuikutanisha midomo hivi lakini ghafla Salma akazuga kwa kushtuka na kusema “Ivi mziki huo unalia wapi?” huku akitoka mwilini mwangu. Na mimi nikajiweka vizuri na kusema “Mh Itakua huko nyuma” na baada ya hapo tukaendelea na stori nyingine ila kiukweli ilibaki kidogo sana kuanza kupimana joto la mwili.
Ukiachana na siku hiyo, kuna siku nyingine tulikaa pamoja sehemu na tulikua tumegusana miili yetu alafu alikua amevaa kinguo kilaini kifupi ambacho kinaonesha mpaka sehemu za juu ya magoti. Tulikua tunaongea mambo ya kawaida tu ila mimi mawazo yangu ya kahama kabisa maana alikua ananigusa gusa ila yeye yupo bize kuongea ongea.
Nilikua namuangalia anavyoongea alafu kichwani nawaza “mwanamke ananukia vizuri huyu… Midomo yake mizuriii… Dah… ananipa majaribu na mapaja yake… Sijui niyaguse? Mh ngoja nijifanye kama nayagusa bahati mbaya maana natamani balaa”. Uvumilivu ukanishinda, nikajikuta tu mkono wangu nimeuweka kwenye moja ya paja lake na lilikua limejaa sana nikaanza kulipapasa kama natafuta vitu hivi. Nakumbuka muda huo alikua anataja nyimbo anazozipenda na kabla hajamaliza, nikauweka mkono wangu. Nilivyo fanya hivyo akaacha kuongea na alishtuka kidogo na akasema kwa kisauti cha chini “OOh.. iiii… Wewe… mkaka nini?… Mbona unafanya hivyo?” Mimi ujasiri ukanikimbia nikazuga nikasema “Ku… Kuna kitu nimeona kama kimedondokea hapa” huku nikiutoa mkono.
Basi aliniangalia usoni kidogo alafu akayatupa macho yake chini kwa aibu huku akiguna “MMh”. Mimi mwenyewe nilifanya kitendo hicho kwa msukumo wa hisia zangu juu yake tu hata sikujielewa, nilipoutoa tukakaa sekunde chache alafu tukaendelea kupiga stori kama kawaida. Salma alikua ni mwanamke mzuri na alikua ananivutia ila uzuri wake ulikua unaniogopesha mpaka kumwambia nakupenda maana alikua anateka hisia mpaka akili zangu zinahama, pia nilikua nahisi ni mke wa mtu na mme wake huenda amesafiri hivyo naweza kutwa nae muda wowote.
Nilikaa kama miezi miwili hivi nilikuwa naongea nae, ninamazoea nae lakini sijamwambia kama nampenda. Ila katika hiyo miezi miwili nilikua kunavitu sivielewi kabisa kwenye maisha yake. Nilikua namuona anaishi peke yake, Sijawahi muona na mwanaume na wala Hafanyi kazi yoyote inayoonekana na karibu kila siku anapika na kula. Nilikua najiuliza hela “Anatoa wapi?” maana hata kutoka nyumbani huwa hatoki mara kwa mara, anaweza kwa wiki akatoka mchana masaa mawili kwa siku moja au mbili tu akarudi nyumbani. Usiku pia huwa anatoka na anarudi asubuhi ila hii katika miezi hiyo miwili niliwahi muona akitoka usiku mara moja tu na alirudi na mchubuko kidogo kwenye paji lake la uso. Nikamuuliza aliniambia alikua kwenye sherehe na kuna mtu alimuumiza kwa bahati mbaya.
Siku moja katika mida ya saa 5 usiku hivi nilikua nikitumiana nae SMS kwenye simu yeye akiwa kwenye chumba chake alicho panga na mimi kwenye chumba changu. Kimvua kilikua kinanyesha siku hiyo nje na kilianza mida ya saa 4 usiku hivi. Nakumbuka katika kutumiana SMS Salma aliniambia “Yani mvua ya leo imeleta baridi hatari… yani nimejifunika shuka mbili nzito lakini bado nahisi baridi” mimi nikasema “Ah mimi huku nina shuka moja jepesiii, fikilia baridi ninayoihisi hapa ni kiasi gani” akasema “hahah wewe basi unatia huluma, Au nikupe shuka moja zito unipe lako jepesi?”. Basi mimi nikajibu “Njoo unipe utakua umenisaidia sana Salma” alafu nikawa nasubiri atakachojibu. Nikakuta anachelewa kujibu nikaanza kuwaza kichwani “Eh mbona anachelewa kujibu huyu, anakuja kweli nini?… Mh kwajinsi alivyoumbika sita mruhusu atoke… Mh na ile mizigo yake aliobeba nitakavyoifanya hata amini…. Mtoto msafi balaa”.

Wakati nikiwaza hayo nikakuta SMS toka kwa Salma imeingia, moyo wangu ukadunda pigo moja kubwa “Nduh” nilipoona SMS imeingia na nilipoifungua nikakuta amesema “Mh ningekuja kukupa ila naogopa”. Nikamjibu “Unaogopa nini sasa?” akajibu “nakuogopa wewe” mimi kama utani nikamwambia “Haha kwanini sasa unamuogopa anaekupenda?” akachelewa kidogo kunijibu alafu akaja kujibu “Mh wewe acha kunirusha roho bana… nani huyo ananipenda?”. Alivyosema hivyo mimi nikapumua kwa nguvu kama mara mbili hivi alafu nikatuliza kichwa nikaandika “Mimi hapa nakupenda. alafu nilitamani ujue hili toka nakuona kwa mara ya kwanza. Nakupenda sana Salma, umeukamata moyo wangu mpaka nashindwa elewa jinsi ya kuelezea upendo nilionao kwako, sitamani nikukose… Nataka uwe mpenzi wangu”. Baada ya kuiandika nikawa kama nimeituma hivi alafu nikaiweka simu pembeni ya kitanda changu kisha nikalala chali nikawanaangalia juu huku nikiwanawaza “Dah sijui atakubali huyu… Akikubali nitamfaidi kweli na ile mizigo ya nyuma alafu Kabinuka… Kifua chake tu kizuri sijui ndani atakuaje. Mtoto namuona mtamu kabla sijamla Dah… nilipanga kutokumpa moyo mwanamke ila huyu sjui kaniibia moyo?” alafu hapo hapo nikaanza kuwaza tena “Mh ila huyu mwanamke nikimtongoza na akikubali alafu baadae mtu akaja kusema natembea na mke wake si nitaharibu kilakitu nilichojia huku Dar?… Wazazi wangu wakisikia nimepata matatizo kwasababu ya kutembea na mke wa mtu watanionaje? wataendelea kutupa hela zao kwaajili yangu kweli? Mh sidhani”.
Nikakuta Ghafla SMS toka kwa Salma imeingia imeandikwa “Wewe, mbona kimya?” nikashtuka nikaangalia vizuri nikakuta SMS nilioiandika kumbe sikuituma, hivyo haikwenda. Nikajicheka kidogo huku nikijisemea “Bora hata haikwenda, ngoja nimuulize maswala ya kuolewa vizuri maana ananitamanisha lakini nikienda kichwa kichwa naweza umia mimi. Ila kama huyu ni mke wa mtu basi waliosema mke wa mtu mtamu hawajakosea kabisa… Ngoja nimuulize” nikaifuta ile SMS niliotaka kuituma. Nilivyofuta nikamwambia tu “Salma, nikuulize Swali?” alafu ikapita kama dakika moja nikakuta anajibu “Ah hapana usiniulize, nijibu kwanza swali langu”….
INAENDELEA….
UTAMU WA JUMLA 03 (Simulizi ya Maandishi)
Ujumbe huo niiliona kama fulsa hivi kwasababu ulikua unaeleza kwamba kuna kampuni inaenda kuanzishwa na
kabla ya kuanzishwa Dar inatoa mafunzo kama miezi sita hivi na waliopata mafunzo ndio wataajriiwa. Kulikua kuna
namba zao pale kwenye ujumbe ili kupata maelezo zaidi.
Basi mimi nikachangamkia fulsa bila kulaza damu. Nikawaambia wazazi wangu ingawa walikua wabishi sana
kukubali lakini niliwaelewesha mpaka wakaelewa wakanipa pesa za kutosha kuishi Dar na za kulipia mafunzo
yatakayoendeshwa na kampuni maana ilikua sio bure. Nikafungua akaunti yangu ya binafsi ya benki kisha nikaweka
hizo hela. Baada ya hapo nikaenda Dar, Nikapanga chumba kimoja kwenye nyumba iliokua inavyumba vitatu
ambapo viwili vilikua pia vinawapangaji ambao walipanga kabla yangu. Siku ya kwaanza nilifika katika chumba
nilichopanga nikaweka mabeigi yangu humo nikalala. Siku ya pili nikanunua kitanda na vitu vingine vya muhimu
kwenya maisha ya kusoma ambayo naenda kuyaishi. Siku ya tatu ilikua ni jumatatu nikaanza kwenda kwenye
sehemu ya mafunzo ya hiyo kampuni. Nilikua naenda asubui narudi mchana mida ya saa 8 hivi.
Siku kama tano ivi zilipita bila kuwaona wapangaji wenzangu. Nilikua naona makufuli yamefungwa tu kila siku
lakini baada ya siku kadhaa nilipotoka kwenye mafunzo nilimkuta dada mmoja mweupe mzuri sana anafua nguo
karibu na mlango wa chumba kimoja kwenye hiyo nyumba niliopanga, kilicho tazamana na chumba chamgu. Alikua
amefunga khanga tu kifuani na amejiachia sana mpaka sehemu za juu ya usawa wa magoti zinaonekana. Nikajua
huwenda ni mke wa mpangaji wa chumba hicho maana chumba hicho kilikua kipo wazi muda huo. Nikamsalimia
“Habari Shemeji” akawa kama amesimama kufua hivi alafu akaniangalia vizuri usoni kwa macho yake mazuri alafu
akasema kwa sauti tamu sana “Maambo”. Mh basi me nikamjibu “Fresh tu” nikiwa nataka kufungua mlango kuingia
ndani akaniuliza “Ah wewe ndio umepanga chumba hicho?” nikamwambia “Ndio… wakati nahamia mwenye
nyumba aliniambia kunawapangaji wengine lakini nikawa nashangaa siwaoni”. Nilivyosema hivyo yule dada
akasema “Hahaha mimi nipo hapa nina mwezi sasa ila siku hizi chache nilikua nalala kwa rafiki yangu.
Nikamwambia “Anh na huyo mpangaji mwingine vipi?” akasema “Huyo kasafiri, nilimkuta anakaa hapa pekeake na
mimi nilikua mgeni kwake maaana mimi nina mwezi mmoja tu katika chumba hiki yeye nahisi ni mtu wa muda
kidogo hapa ila kwa sasa kasafiri”,. Nikamuuliza “Kwenye hicho chumba uko peke yako?” akatabasamu alafu
akajibu “Ndio, nipo pekeangu tu hapa hahaha”. Cheko na tabasamu lake tu vilikua kama vimeupasua moyo wangu
kwa furaha na kuamsha vihisia vya mapenzi juu yake.
Nilivyoona hivyo mimi nikasema “Anh sawa, we endelea kufua mimi niingie ndani” ili nikatishe maongezi kidogo
maana alishaanza kunichanganya kichwa na nilikua nimechoka muda huo. Yeye akasema “Sawa, mimi nipo…
ukinihitaji naitwa Salma” mimi hapo nikakumbuka sijamwambia hata jina langu, Nikamwambia jina langu alafu
nikafungua mlango kisha nikaingia ndani. Baada ya kuingia ndani nikatua daftari zangu pale ndani Huku kichwani
nikiwa nawaza “Huyu mwanamke anadawa nini? mbona mzuri alafu nilipokutana nae nimejiskia tofauti? yaani
nakutanane mara yakwanza na ananichanganya hivi… Au kisa sija mzoea? Mh itakua sijamzoea tu, Hana maajabu!
Alafu anaonekana kama mke wa mtu ila ananificha… hawezi ishi pekeake na uzuri huo”.
Sikua na ratiba ya kula muda huo maana huwa nikitoka kwenye mafunzo napitia kula kwanza kwa mama ntilie ndio
nakuja nyumbani. Tangu nifike hapo nilikua sipiki, nilikua nanunua chakula tu maana pesa nilikuanayo ya kutosha
na hata ingeisha nyumbani wangetuma tu. Vitu vikubwa nilivyokua nafanya nikiwa naishi hapo ni kunununua
chakula, kusoma mafunzo na kucheza magemu au kusikiliza muziki kwenye simu yangu.
Salma nae alikua ameongeza kitu katika maisha yangu ya pale maana ilikua kama nimepata rafiki wa kupiganae
stori mara moja moja nikiwa nyumbani. Mara nyigi nilikua nikikosa cha kufanya ndani natoka nje nikimkuta yeye
amekaa, anapika au anafanya kazi nyingine nje, tunapiga stori mpaka basi. Ila kiukweli Salma alikua ananivutia sana
maana alikua mzuri kupita maelezo. Alikua mweupe sana mwenye kifua kilicho simama vema na nzigo wa nyuma wa kutosha. Ukimuangalia usoni macho yeke ni makubwa alafu mazuri sana, tabasamu lake nlilikua linanimaliza na
akicheka ndio kabisa. Kuna muda nikiwa naongea na yeye akili yangu ilikua inahama najikuta namuangalia sehemu
kama kifuani au midooni mpaka najishtukia na yeyepia akiona hivyo alikua anaona viaibu kidogo.
Siku ya kwanza kuongea nae sana ilikua ni baada ya siku kama mbili hivi toka nikutane nae mara ya kwanza. Ilikua ni
mida ya jioni nimetoka kuangalia mpira, nimepitia kula chakula kwa mama ntilie ndipo nikaenda nyubani. Nilipofika
nyumbani nikamkuta amekaa mlangoni pake, mbele yake kuna jiko anapika chakula. Nilimsalimia akaitikia alafu
nikenda ndani nikachukua simu yangu ambayo kwa muda wote ambao sikuepo ilikua kwenye chaji. Baada ya
kuchukua simu nikaanza kucheza gemu nikiwa nipo ndani ya chumba changu lakini baada ya Dakika chache
wakakata umeme kukawa na giza mule ndani. Nikaamua kutoka nje nikakaa kwenye mlango tukawa tunaangaliana
na Salma akiwa amekaa mlangoni kwake na kwa muda huo alikua ameshikilia sahani mkononi anaanza kula.
Nikiwa nakaa pale mlangoni ili nianze kucheza gemu nikamsikia anasema “karibu tule” mimi nikajibu “Ah mimi
nimeshakula, asante”. Tukakaa kama dakika mbili hivi bila kuongea alafu nikasikia akijisemesha “Umeme nao
umetuachia giza bora warudishe mapema kabla simu yangu haijaisha chaji” mimi nikasema “Hahaha mimi simu
yangu inachaji yakutosha, wakate mpaka kesho tu” kusikia hivyo akacheka “Hahahahaha” alafu nikaongeza kusema
“Simu yangu hata nicheze gemu au kusikiliza muziki, kesho itafika ikiwa na chaji”. Nilipogusia muziki nikakuta
ananiambia “Enhe alafu kunanyimbo naomba unirushie kama unazo maana simu yangu mimi ni batani, siwezi pata
nyimbo mpaka niingiziwe”.

Nikamuliza “Unataka nyimbo gani?” akanitajia na kwakua hizo nyimbo nilikua nazo
nikamwambia “lete simu nikurushie”.
Akachukua simu akanyanyuka na kuja kunipa huku akiwa ameshikilia sahani ya chakula mkononi. Mimi
nikachukua simu yake na kuanza kurusha nyimbo huku yeye akiwa hajarudi mlangoni kwake, alikua amesimama
pale karibu yangu akisubiri simu yake maana jambo la kurusha nyimbo si jambo la kuchukua muda mwingi.
Nilipokua nikirusha nyimbo nikakutana na kitatizo kidogo ambacho kilinifanya nichukue muda kidogo kuliko
kawaida. Yeye alivyoona nachelewa, akaamua kukaa na mimi pale mlangoni pangu akawa anaendelea kula huku
ananiangalia ninachokifanya kwenye simu na kuendelea kuongea na mimi. Mh alikua amejisogeza karibu yangu na
tulikua tumegusana kabisa kiasi kwamba nilikua najikuta nahisi vitu tofauti na kitu ninachokifanya muda huo. Mwili
wake mlaini ulileta joto la ajabu mwilini mwangu alipokua karibu yangu maaana alikua ni mwanamke mwenye kila
sifa ya kuamsha hisia kwa mwanaume. Ukiachana na hayo yote, alikua ananukia vizuri.
INAENDELEA…
Zingatia hii: Tafadhali fahamu kuwa hadithi hii ni mali ya mwandishi. Hairuhusiwi kunakili hadithi yote bila idhini. Unaweza kushiriki au kuchukua sehemu ndogo ya hadithi, lakini si kuichukua hadithi kamili. Asante kwa kuheshimu kazi ya mwandishi!
UTAMU WA JUMLA 02 (Simulizi ya Maandishi)
Wakati nakusanya nguo ghafla mlango ukagongwa “Ngo ngo ngo” na sauti ya Jimmy akisema “Oi wewe”.
Niligundua ni Jimmy nikasema “Oya… Umerudi sasa haha” akawa anasukuma malango huku anasema “Ahaha
nimekuja na shemeji yako huyu” huku akimruhusu mtu aingie. Mimi nikatupa macho kuangalia mtu anaeingia ni
nani, nikakuta ni Zuwena amevaa nguo nyeusi fupi alafu inaangaza kiasi ambacho baadhi ya sehemu zake za mwili
zinaonekana na Jimmy alikua anamshika kiuno alipokua akiingia ndani. Nilipomuona Moyo wangu ulidunda kwa
mshtuko “Nduh” na nikahisi kama kuishuwiwa nguvu hivi…
Nikaona bora nijikaze tu ila nisiwe na maneno mengi hapo maana nawezajikuta nimesema kitu kibaya. Nakumbuka
nilimsalimia Zuu kama ndio mara ya kwanza nakutana nae hapo. Na yeye alikua ananisalimia kama sijawahi ongea
nae kwa ukaribu. Baada ya kuwasalimia nikatoka nje na nguo nilizokusanya ili kuzifua na kuwaacha mule ndani.
Nilivyotoka tu, Jimmy aliufunga mlango ili mtu yoyote asiingie mule ndani na mimi sikua na hofu juu ya hilo
maana vitu vyote ambavyo vilikua vinahitajika ili nifue vilikua vinapatikana nje.
Nilichukua ndoo nikachota maji, nikavuta kiti pembeni ya chumba nilichukua nakaa alafu nikaanza kufua. Kichwa
changu muda huo kilikua hakipo sawa kabisa maana nilikua naona rafiki yangu Jimmy anaenda kula tunda la mtu
ninaempenda na kwakua sikumwambia basi nikaona acha niendelee kuumia moyoni tu kimya kimya huku nikifua
japo bado kichwani nilikua najiuliza “Amempataje huyu kiiumbe? Mbona sijawahi waona wakiwa karibu? Dah yani
Zuu nae inaonekana hanikubali kabisa maana aliponiona hata hakushtuka.ila namtamani sana huyu mwanamke”.
Wakati naendelea kufua ghafla nikaanza kusikia visauti toka ndani kupitia kidilisha kilichokua karibu na nilipokua
nafua. Mara ya kwanza nilikua nimevipuuza visauti hivyo nikawa nahisi ni Jimmy na Zuu wanaongea kawaida
kimahaba lakini baadae nikaanza kusikia sauti inaongezeka na inakua kama Zuu anabishana na Jimmy mule ndani.
Hali hiyo ilinifanya niache kufua nisogee zaidi kwenye dilisha nijue wanabishana nini humo ndani badala ya kuanza
mambo yao. Nilipotega sikio nikasikia Zuu akiwa na sauti kama amechukia hivi akisema “Usiniguse kwanza, Mimi
nataka uniambie ukweli kwanza… umesema hapa ni kwa nani?” Jimmy akawa anajibu “Kama nilivyokwambia
Zuwena, kwa rafiki yangu hapa… Kwanini unakua mgumu kunielewa” Zuu akajibu “We endelea kunidanganya tu, si
umeniona mimi mtoto mdogo? hiyo michezo naijua, usiniguse”. Nilimsikia Jimmy akisema “Tatizo huniamini…
Kama nilivyokwambia, mimi nakaa kule ila funguo kuna mtu ameondoka nayo ndio maana nimekuja kwa rafiki
yangu huku. Hata kodi ya hapa huwa nalipa mimi, huyo jamaa alietoka hapo nje huwa ni kama namsaidia tu maana
hayupo vizuri kipesa. Alafu nilishakwambia habari ya huyo jamaa hapo… Sasa kinachokufanya ubadilike sijui ni kitu
gani”. Nikakuta Zuu anamuuliza Jimmy “Yani umeniona mimi mjinga sana bora hata ungekua mkweli tu… Mimi
naona humu ndani kuna nguo zako ninazo zijua na hata viatu alafu bado unasema hapa sio pako. Sawa, kwasasa
naomba uniache niondoke maana nimekuchoka”. Mimi hadi hapo nikaanza kupata picha kidogo ya kinachoendelea
humondani. Kwa maongezi yale nilio yasikia nikajua tu huenda Jimmy hadi amemfikisha hapo huyo mwanamke ni
baada ya kumdanganya sana na muda huo uongo wake uligundulika na jambo hilo lilpelekea mpaka huyo
mwanamke kutaka kutoka humo ndani.
Basi nikatoka pale dilishani nikarudi nilipokua nafua ili kama wanatoka wasijenikuta pale na kugundua nilikua
nawasikiliza. Baada ya dakika kama tano hivi nikasikia mlango unafunguliwa, wakatoka kama wapo vizuri tu japo
Zuu alikua na sura inayoonesha amekasirika na Jimmy alikua ni kama anaaibu kiasi kutokana na kilicho mtokea.
Nakumbuka waliniaga pale alafu wakawa wanaondoka na kuniacha nikwa nafua. Kiukweli siku walivyokua
wanaondoka waliniacha nikiwa na furaha sana moyoni kwangu kutokana na kutofanikiwa kufanya mambo yao
humo ndani. Nilikua napenda sana Jimmy afanikiwe kwenye mipango yake kwasababu ni rafiki yangu lakini kwenye
Suala la kumkamata Zuu, sikulipenda maana mimi pia nilikua nampenda sana Zuu japo sikumwambia.
Nilipokua nikiendelea kufua na kufurahia tukio lililotokea, gafla nikaanza kufikilia tena yale maneno nilioyasikia
dilishani na kuanza kuwaza “Inamana Jimmy amemwambia Zuu mambo mengi kuhusu mimi alafu mimi sijui… Dah
na najua hawezi kuongea ukweli au jambo la kunisifu, lazima alikua ananiponda ili aonekane ni mtu wa juu”. Na kweli baada ya tukio hilo chuoni kulikua na watu wengi wajua juu ya Jimmy na Zuu. Zuu alimchafua sana jimmy
hapo chuoni kwa kuwaambia watu vitu alivyokua anaambiwa na Jimmy. Kulikua na maneno mengi ya Jimmy
kujigamba kwa Zuu ambayo yalienea kwa watu pale chuoni ila moja ya vitu nilivyosikia mwenyewe Jimmy
alimwambia Zuu ni kwamba ananilipia kodi tu lakini hakai na mimi. Jambo hili liliniumiza sana maana nilihisi
huenda ndio chanzo cha Zuwena kunipuuza nilipokua namtafuta. Lakini kwakua Jimmy alikua ni rafiki yangu,
nilipuuzia na tukaendelea kuwa pamoja hapo chuo.
Pamoja na yote yaliotokea, sikuwahi mtafuta tena Zuu. Nilikua nimetulia na mpenzi wangu sara na alikua anasema
ananipenda kweli. Niliweka moyo wangu wote hapo huku nikiwa na soma sana lakini nilivyozama sana katika penzi
lake, nikakuta Sara anaanza kunibadilikia tena. Ghafla tu alianza tabia ya kutonitafuta mpaka nimtafute na hata
nikimtafuta anaweza sema atanitafuta lakini hafanyi hivyo. Hali hii iliniumiza sana maana nilikua najua kwamba ni
dalili ya kuwa Sara amepata mwanaume mwingine. Nilichanganyikiwa sana kipindi hicho mpaka masomo nilikua
naona hayaeleweki. Hakuniambia kwamba tuachane ila tabia yake ilionesha kuwa tayari ameishaniacha ila ni mmi
tu ndio sijui. Nilifuatilia nikakuta kumbe kapata Mwanaume mfanyakazi na anamiliki mpaka gari. Niliwahi shuhudia
kwa macho yangu Sara akiingia kwenye gari baada ya kutoka chuoni. Niliumia sana na nikaamua kukubaliana na
uhalisia kuwa nimeachwa ila moyoni nikajisemea “Siku nikipata ajira na kuwa na hela nitawakamata sana
wanawake… yani nitawala sana. Ntanunua gari na ntakuwa na wanawake kila kona… Siwezi mpa moyo wangu
mwanamke auchezee kama hivi, ntakuwa nao wengi ili niwachezee wao… Pesa nyingine nitakua natumia na
marafiki tu maana ni bora marafiki kuliko kuwa na mpenzi”.

Basi siku zilisonga hapo chuo mpaka tukamaliza na kurudi nyumbani Tabora. Nakumbuka mimi na Jimmy tulirudi
nyumbani na tulikua tunaishi kwa wazazi wetu. Kwetu na kwakina Jimmy ni karibu sana. Kwao ni nyumba ya tatu
kutoka kwetu. Tulivyokua wadogo hatukua pamoja, familia yake ilihamia hapo kipindi nipo sekondari na yeye
alikua sekondari na tulipokutana tukawa marafiki mpaka tulipoenda chuo pamoja na kurudi pamoja. Tulivyorudi
tulikua mabishoo sana na tunapendeza juu mpaka chini kila muda na masimu yetu makubwa ya kupalasa.
Baada ya miezi kadhaa ishu ya chuo tukawa tumeimaliza kabisa tukawa tunamawazo ya kupata Ajira kichwani
mwetu kutokana na vyeti tulivyopata. Lakini tulianza kuona kama neno “ajira” linaongelewa kwenye ma TV alafu
hatuzioni mtaani na hata wakiziongelea kwenye TV mara nyingi wanasema “changamoto ya upungufu wa ajira”.
Jambo hili lilinifanya nijiulize “Inamaana pamoja nakuwa na vyeti Ajira naweza kupata au nisipate? Duh!”. Siku moja
nikakuta tu ghafla jamaa yangu Jimmy kasafili. Na hakuniambia kwamba anasafiri mpaka nilipomcheki kwenye simu
“Wewe uko wapi mwanangu, mbona haujaonekana leo” ndio akaniambia amerudi Dar. Mimi nikamuliza “Mbona
hukuniambia rafiki yangu?” akasema “Hahaha ilikua ni ghafla mzee, Nitakucheki tutaongea vizuri”. Mh Mimi
nikajua atanicheki kweli lakini haikua hivyo, siku zilizidi kusongea tu hanicheki na hata nikimcheki ananiambia
“ntakucheki”. Baadae nikakata tamaa kabisa ya kumtafuta maana nilikua najua nimuongo hivyo ukimsikiliza
unapoteza muda nikakata mawasiliano nae. Kiukweli baada ya Jimmy kuniacha kule Tabora nilianza kuwa na
mtizamo tofauti kidogo juu ya Marafiki, nilikua kama nimegundua kuwa marafiki hawajashikana na maisha yangu,
wanaweza ondoka muda wowote.
Nikaendelea kukaa pale nyumbani bila mafanikio ya kupata ajira na wazazi nilikua naona hawaniwazi tena kwenye
mambo ya pesa, wao walikua wapo tayari walipie mamilioni sehemu nisome au nipate kazi kuliko kunipa mimi pesa
ya hivi hivi tu. Kadri siku zilivyo zidi kusonga nilianza kuchakaa kimuonekano kutokana na kukosa hela. Wakati
nakuja kutoka chuo nilikua napendeza kiasi kwamba nikikutana na mtu ananiuliza “Hiyo sendo uliovaa mguuni
shingapi?” nikimwambia bei anasifia “Dah nzuri sana hiyo sendo!” lakini mambo yalibadilika kiasi kwamba
nakutana na mtu ananiangalia juu mpaka chini alafu anauliza “Hiyo gundi ni supagruu?” namuuliza “Wapi? hapa
kwenye sendo?” Anajibu ” ndio, hapo mguuni” namwambia “Ndio ni yenyewe” ananijibu “Gundi nzuri sana
hiyo!”. Kiukweli nilichakaa sana na hali hiyo ilinifanya niwe na kiu ya kufanya chochote nipate ajira na ilikua kama
bahati hivi nilikutana na tangazo ambalo liliingia kwenye simu yangu kama ujumbe. Ujumbe huo niiliona kama fulsa
hivi kwasababu ulikua unaeleza kwamba kuna kampuni inaenda kuanzishwa na kabla ya kuanzishwa Dar inatoa
mafunzo kama miezi sita hivi na waliopata mafunzo ndio wataajiriwa. Kulikua kuna namba zao pale kwenye ujumbe
ili kupata maelezo zaidi…
INAENDELEA….
Hii ni simulizi ya UTAMU WA JUMLA ilio katika maandishi. Ina uhusiano kidogo na Simulizi ya SUKARI YA DADA na MZIGO WA WAKUBWA. Inapatikana katika Sauti pia. Inavipande 11.
KUMBUKA: Hairuhusiwi kusomwa na mtu mwenye umri chini ya miaka 18.
Ukihitaji simulizi zote 3, Njoo WhatsApp
DAWA CHUNGU (Simulizi Fupi ya Kusoma)
Nina mke mzuri sana, na nampenda. Nina uhakika na yeye pia ananipenda. Tumebarikiwa na mtoto mdogo mmoja. Nafanya kazi, lakini kuna kipindi mambo yangu ya kikazi yalienda vibaya. Kipato kikawa kidogo sana. Mke wangu alianza kudai mahitaji ya nyumbani na mtoto kila wakati. Kila alivyodai, ndivyo nilivyoanza kumwona kama kero, maana hachoki kusema. Hali hii ilinipeleka kwenye uhusiano wa pembeni na binti mmoja mzuri, mdogo alafu mjanja mjanja, anayekaa mtaa wa tatu kutoka kwangu.
Nilikutana naye katika sehemu za starehe. Nilienda pale kupoteza mawazo kwa kunywa pombe kama wanavyoseoma. Tulipokutana huko, furaha yangu ilianza kufufuka hivi. Kila nilipopata pesa kidogo, badala ya kupeleka nyumbani, nilikua naenda kwenye sehemu za starehe, nampigia simu huyo binti aje tuwe wote. Yeye alinipa furaha zaidi kuliko mke wangu kwa kipindi hicho, maana tulilewa pamoja, tulikuatunacheka, na kufanya mambo mengi ambayo sikufanya na mke wangu. Mke wangu tukitulia alikua nawaza kunidai na kuniambie matatizo. Hali hii huwa inatesa sana.
Pamoja na yote hayo, bado nilimpenda sana mke wangu. Niliweka siri hiyo, sikutaka ajue chochote maana najua na yeye ananipenda sana ila maisha ndio yanatufanya tuwe kwenye hali hiyo. Mioyo yetu inapendana sana ila mifumo ya maisha ndio tatizo.
Siku moja kazini, mpango mmoja niliokuwa nao ulienda vizuri, nikapata pesa nyingi kiasi kwa mpigo. Nilikuwa na furaha kubwa, nikaingiziwa pesa kwenye simu. Badala ya kufikiria familia yangu au mke wangu, akili yangu ilikimbilia kwenye starehe maana ilikua ni kama nimezoea hivi. Mwanzo nilianza kwa lengo la kupoteza mawazo lakini mwisho ikawa tabia yangu bila kushtuka.
Sika hiyo nilipanga kujipongeza kwa kukutana na yule binti tufanye starehe. Nilifika kwenye sehemu ya starehe, nikapata chupa moja ya pombe na kuanza kunywa. Wakati nakunywa nikatuma ujumbe kwa yule binti “Njoo sasa, nina furaha sana kuliko siku zote, nataka uje tufurahi pamoja.” Siku jieleza sana maana niliongea nae kabla.
Kabla huyo binti hajajibu, nikakuta mke wangu anapiga simu. Siku taka kupokea, niliiacha ikiita huku nikiendelea kunywa pombe kidogo kidogo. Baada ya muda simu iliacha kuita, nikakuta ujumbe toka kwa mke wangu unaingipia. Sikutaka hata kufungua hivyo sikujua alichoniandikia. Baada ya dakika moja yule pinti alinijibu ujumbe niliomtumia.
Alinijibu kuwa alikuwa na matatizo yaliyohitaji kiasi fulani cha pesa. Alisema akiipata hiyo pesa popote, atakuja. Kwakua mimi nilikua na pesa, nikamwambia asiwe na wasiwasi, nitamtumia hiyo pesa ndani ya dakika tano.
Baada ya kumwambia hayo, nilianza mchakato wa kumtumia pesa yule binti. Nikachukua simu na kuandika kiasi cha pesa anachohitaji kisha nikatuma.
Baada ya kutuma tu, nikamuandikia yule binti ujumbe uliosemeka “Tayari nimeisha tuma. Itumie hiyo pesa kwenye hayo mambo yako yote alafu tufurahi wote maana ninafura na furaha yangu nataka nifurahi nikiwa na wewe mpenzi wangu” kisha nikautuma.
Lakini baada ya dakika nilishangaa kuona ujumbe wa shukrani kutoka kwa mke wangu. “Asante sana mume wangu. Sijui nikupe nini wewe mwanaume. Mungu akulinde na kukubariki sana pacha wangu. Najiona nina bahati kuwa na wewe”
Nilishangaa sana. Nilipochunguza, nikakumbuka kuwa sikuusoma ujumbe wa kwanza wa mke wangu. Nipousoma nikaona ulikuwa ni wamalalamiko mengi kuhusu mahitaji ya nyumbani na mtoto wetu.
Hapo akili yangu ilianza kukaa vizuri: kumbe pesa niliyotuma, nilimtumia mke wangu kimakosa badala ya yule binti! Mbaya zaidi, nilikuwa nimeandika kiasi kikubwa cha pesa kuliko nilivyokusudia. Sijui zilikua ni pombe au nini ila kukosea kuandika kiasi cha pesa kulifanya pesa nilioituma kuwa kubwa sana kuliko iliobaki kwenye simu yangu. Na kumbe hata ule ujumbe nilipotaka kumtaalifu yule binti,nimemtumia mke wangu pia.
Nilichanganyikiwa. Pombe kichwani ilikata ghafla. Nikabaki nimekaa pale, huku simu ya mke wangu ikiendelea kuingia na ujumbe wa shukrani ukija mmoja baada ya mwingine.
Hakukuwa na maneno mengi ya kumwambia. Nilijua ningesema jambo lolote, basi ningeharibu ndoa yangu. Ingenibidi nieleze hiyo pesa nyingi hivyo nilikua natuma wapi alafu pia ujumbe niliokosea kumtumia kwanini una neno “mpenzi”.
Nilijaribu kuwasiliana na watu wa mtandao kidogo ili warudishe ila nikaacha. Nikaona kama hiyo pesa imeokolewa na mungu maana kiasi kile cha pesa kingeenda kwa yule binti mjanja wa mjini, sidhani kama ningefaidika chochote. Bora mke wangu kaipata maana ni kama nimepunguza matatizo ya nyumbani kidogo.

Baade nilirudi nyumbani nikamkuta mke wangu anafuraha sana. Yani alikua ananiangalia hanimalizi maana hakutegemea jambo lile. Alikuwa amenipikia chakula kizuri, na kila kitu kilionekana kama sherehe humo ndani. Alinipongeza na kunishukuru kwa msaada wa kifedha ambao kimoyomoyo sikupanga kumpa. Akili yangu ilikuwa kwenye pesa yangu kuwa nimetuma kimakosa.
Sikuweza kurudisha pesa hiyo mikononi mwangu wala kuliongelea sana. Ila kufidia kidogo pesa yangu nilimkopa mke wangu kiasi kidogo baada ya wiki na akakubali bila kusita maana ananiamini. Hiyo pesa niliyokopa, sina mpango wa kuirudisha japo yeye anadhani nitarudisha.
Pamoja na yote siwezi jilaumu sana kuhusu tukio hilo maana lilimfanya mke wangu aanze kuelewa kidogo nikimwambia niko vibaya kwenye pesa. Alikua anaamini kuwa nikipata pesa huwa namkumbuka. Na kweli kwanzia tukio hilo limenitokea, huwa namkumbuka sana mke wangu. Ukimfanyia jambo lolote zuri la bila kutarajia huwa anachanganyikiwa kwa furaha.
Mwisho
UNANIITA? (Simulizi Fupi ya Kusoma)
Nilikua kijana mdogo tu niliyepambana kujenga maisha yangu. Kazi yangu ilikuwa ni kuendesha pikipiki, yaani nilikuwa bodaboda hapa mjini. Siku moja, nikiwa kazini, alinisimamisha dada mmoja ili nimpeleke kwake. Nilisimamisha pikipiki yangu, nikambeba na safari ikaaanza kuelekea kwake. Huyu dada alikuwa mweupe, mzuri sana, na ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona.
Njiani, alianza kulalamika kuhusu bodaboda wake wa kila siku; alisema amemchoka kwa sababu huwa anachelewa na hapendi muonekano wake maana hajipendi kabisa alafu akanisifia mimi kuwa ni asafi. Aliponisifia kwa usafi na jinsi nilivyopendeza, nilijisikia vizuri. Alisema anatamani bodaboda wake awe msafi kama mimi. Nilikuwa na tabia ya kujipenda na kujiweka safi kila siku, nikiamini kwamba kuwa hivyo kunaweza kufungua milango mingi maishani.
Tulipofika kwenye nyumba yake, niliona ni nyumba kubwa yenye wigo mrefu. Sikuingia ndani ya wigo, nilimshusha nje ya nyumba na akanilipa pesa yangu. Aliomba na namba yangu ya simu, akisema atakuwa akinipigia kila anapohitaji bodaboda. Nilijisikia vizuri kupata mteja mpya.
Siku iliyofuata, mchana, nikiwa kwenye kijiwe cha bodaboda, simu yangu iliita. Ilikuwa ni Zena, yule dada mzuri niliyembeba jana. Aliniomba nimfuate nyumbani kwake, alikuwa anaenda sehemu. Nilifika kwake na kumpigia honi nikiwa nje. Wakati nasubiri, nilitupia macho ndani ya wigo kupitia nafasi ndogo ya geti. Niliona gari moja kali sana likiwa ndani na nikajiwazia, “Hivi kwa nini hawa matajiri wanapanda bodaboda wakati wana magari ya kifahari? Ningekua mimi, Hilo gari lisingetulia hapo”
Baada ya dakika chache, Zena alitoka nje akiwa amependeza sana. Nilijiweka vizuri na kumkaribisha kwenye pikipiki. Tukiwa njiani, aliongea na simu kwa sauti ya upole, lakini niliweza kusikia sauti kubwa ya mwanaume akimjibu kwa hasira: “SIMESEMA NITAKUPIGIA! KWA SASA NINA KAZI NYINGI WE MWANAMKE! SIKU NIKIRUDI, TUTAONGEA VIZURI MAANA NINA KAZI ZA WATU HUKU. YANI KICHWA KINA MAMBO MENGI SANA” Huyo mwanaume alionekana kumuumiza Zena, na baada ya kukata simu, Zena alionekana kuwa na huzuni.
Nakumbuka akaniuliza, “Hivi nyie wanaume mnataka nini? Mwanamke anapokupenda mnamuona kama hana thamani.”
Mh mimi nikasema “Mh kwanini unasema hivyo?” akasema “Wanaume mnatesa sana mwanamke anaewapenda… Yani mwanamke akiwapenda na kuwa muwazi, huwa mnamuona mjinga sana”. Mimi nikasema “Hahaha hiyo inategemeana na Tabia ya mtu. Mwanaume wengine huwa wanawapenda wanaowapenda”. Niliposema hivyo yule dada akasema “Dah huyu mwanaume wangu ananiumiza sana mpaka naanza kuchoka”. Mimi nikacheka tu “hahaha” maana hayo ni mambo yake binafsi na hata sikutaka kumuuliza sana kuhusu huyo mwanaume.
Lakini yeye akaendelea kuongea kwa kusema “Yani Tangu amenioa, Hana muda wa kunizingatia. Anakua anazingatia kazi zake alafu ananiona mimi kama msela wake tu. Hana maneno mazuri ya kuongea ili hata nijisikie tupo kwenye mahusiano. Akiwa mbali na nyumbani huwa hajibu sms wala haniruhusu kuongea nae vizuri kwenye simu. Sijui anataka nini? Yani naona kabisa hanipendi huyu mwanaume maana ananitesa.”
Mh mimi hapo nikacheka tena tu “hahaha” maana hayo ni mambo yake binafsi lakini hakuishia hapo, akiniuliza “Wanaume wote ndio muko hivyo kweli?”. Mimi nikasema “Hapana ila unaweza kuta yupo na kazi nyingi ndio maana yupo hivyo. Hata mimi nikiwa naendesha pikipiki huwa nashindwa kuwasiliana sana na watu kwenye simu zaidi ya abilia wangu”.
Nilipo sema hivyo, akaniambia “Lakini si ukitulia hata mida ya usiku unamtafuta mpenzi wako, unaongea nae vizuri?”. Nikamjibu “Ndio, na sio lazima usiku. Nikipata muda hata huo huo mchana huwa naongea nae vizuri tu” Yule dada akajibu “Mimi huyu mwanaume hayupo hivyo. Akirudi nyumbani huwa anasema anachoka sana, nisimsumbue hata kwa kumgusa. Alafu akiwa kazini hataki kuongea sana kwenye simu”.
Mh mimi sikutegemea kabisa huyo dada mzuri kukutana na changamoto kama hizo. Mimi kwa uzoefu wangu nikiwa kama mwanaume nikamwambia “Jaribu kuwa una mtumia Ujumbe wa kuamsha hisia au kama unaongea nae uwe unaongea vitu vya kuamsha hisia. Mimi hata nikiwa kwenye kazi nikiona mpenzi wangu kaniletea hivyo vitu huwa najikuta namzingatia kuliko kazi hahaha”.
Huyo dada akajibu “Vitu vya kuamsha hisia kama Vipi sasa?” Nikaona aidu kumuelekezea moja kwa moja, nika mwambia tu “Hahaha Yani sijui nikuelezee vipi… Ila nyie wanamke ndio mnavijua sana hivyo vitu” akatulia sekunde chache alafu akasema “Anha sawa, nimekuelewa…. Nimewahi mfanyia lakini kwakua umeniambia, nitajiribu nione kama itasaidia”
Baada ya kumpeleka saluni kama alivyotaka, nilimuaga alafu nikaja kumrudusha nyumbani tena kisha kuendelea na kazi zangu. Zena alinilipa vizuri na nilirudi kijiweni. Siku mbili baadaye, usiku wa saa nne, nilipokea ujumbe kutoka kwa Zena: “Umelala?” Nilimjibu kwa kumwambia kuwa “Sijalala, Bado niko kazini na baada ya dakika chache nitakua nikiwa kwenye safari ya kumpeleka mteja sehemu flani hivi. Nikitoka huko ndio natarudi nyumbani kulala maana najisikia vibaya sana, Leo nitawahi kulala.”
Akaandika tena, “Pole, unajisikia vibaya, unaumwa nini?” Nikamwambia “Uchovu wa kawaida wa kazi ya bodaboda, ila Leo umezidi. Viungo vya mwili vyote vinauma”. Aliniambia, “Pole sana, lakini si una mpenzi wako akukande mwili?”
Nilicheka kidogo mwenyewe, maana ukweli ni kwamba sikuwa na mpenzi. Mpenzi wangu aliniacha mwezi uliopita bila sababu yoyote, lakini sikuwa na nia ya kumwambia hilo Zena maana hayamuhusu. Niligeuza mazungumzo na kuuliza kama alihitaji nikambebe tena kwa pikipiki. Akaniambia, “Hapana, mda huu niko tu peke yangu nyumbani, najihisi upweke mpaka nimeona nikujulie hali.”.
Kwakua muda huo mimi nilikua naenda kupeleka mteja sehemu na pikipiki, nilimwambia Zena “Sawa, ila sasaivi ndio naenda kumpeleka mteje hivyo nitakutumia ujumbe baada ya dakika chache ili tuendelee kuwasiliana” akajibu “Sawa, hapa silali, nitakusubiri mpaka unitumie ujumbe”. Mimi nikajibu “Hahaha Sawa, usijali”.
Basi nikaacha maongezi nae hapo alafu nikaenda kwenye kazi. Nilivyorudi nikapitiliza kulala tu bila hata kumtafuta kwenye simu.
Asubuhi ilipofika, nilikuta Zena amenitumia ujumbe mara nyingi sana usiku na hiyo asubuhi alinitumia tena ujumbe wa salamu za asubuhi. Nilipomjibu, alinipigia simu hapo hapo. Aliniuliza kwa kama kautani hivi kuwa “Mbona jana hukunitafuta tena? Au ulikuwa na mpenzi wako?”
Nilicheka na kumjibu, “Hapana, Samahani sana. Nilipotoka kule Uchovu ilizidi zaidi nikajikuta nimepitiliza kulala. Yani Uchovu ni mwingi mpaka muda huu bado najisikia vibaya na sijui nafanyeje.”
Akasema, “Mh kama bado unajisikia vibaya, njoo jioni kwangu nikupatie dawa” Nikamuulaza “dawa gani hiyo?” Akasema “Ni mafuta flani hivi unayapaka kwenye viungo vinavyouma huku unakanda mwili na maji ya moto. Utamwambia mpenzi wako aitumie kuviweka sawa viongo vyako.” Mh mimi kusikia mambo ya hayo na Sina hata huyo mpenzi, nikamwambia tu “Sawa, nakuja kuchukua jioni”
Baada ya kuongea hayo tulikata simu nikaenda na kazi za Kila siku. Lakini hiyo siku nilikua napokea sms nyingi toka kwa Zena. Na nilikua na jibu maana niligundua ni mtu mpweke sana na ameanza kama kunipenda hivi. Mimi kumpenda nilikua nampenda ila namuheshimu kidogo kama dada alafu pia ni mke wa mtu.
Jioni ilifika nikaenda kwake mpaka ndani. Nilikuta anaangalia TV na nilivyofika akanipa chakula. Baada ya kunipa chakula, nikiwa nakula, nikamuona kama anajiandaa kwenda kuoga hivi maana aliingia chumbani na kutoka na kinguo chepesi alafu kifupi sana. Kwa juu kilikua ni kama vikamba vimepita mabegani.
Nilivyomuona anatoka chumbani hivyo nilimtolea macho ya kutamani maana alikua na mwili mzuri. Moyo wangu ulidunda sana sana baada ya kuona kama anakuja kwangu hivi.
Kumbe kweli, yule dada alifikia mpaka nilipokaa huku akiwa naniangalia machoni toka mbali. Nakumbuka alipokuja karibu yangu akaniambia “Umeniita?”. Nilishangaa sana kusikia hivyo maana Sikua nimemuita hapo. Na moyo wangu ulikua unadunda kwa kasi sana kutokana na matamanio yangu muda huo. Macho yake yalikua yamelegea sana alafu asilimia kubwa ya sehemu za juu ya magoti zilikua zinaonekana.
Mdomo ulikua mzito sana muda huo. Jambo aliloniuliza nililikataa kwa kwa gigugumizi sana “hapana… Sija… Sija… Sijakuita mbona” nilivyosema hivyo, akaacha kusogea nilipo, akasema tu “anha sawa, labla nimesikia vibaya” kisha akaanza kwenda chumbani kwake tena.
Aliniacha pale moyo unadunda sana alafu nilikua sielewi maana sahihi ya jambo alilolifanya. Macho yake hayakuacha kuuangalia mwendo wake wa kujitikisa alipokua akielekea chumbani.
Yani hata chakula nilichokua nakula muda huo nilikiacha kwa muda, nikawa nimeganda nawaza maana ya tukio lile.
Baada ya kama ya dakika 3 hivi, Nikakuta kuna ujumbe mpya umeingia kwenye simu na mtumaji alikua ni Zena. Nilifungua huo ujumbe nikakuta umeandikwa “Njoo huku chumbani unisaidie kitu flani”. Mh nilishtuka nikajua tu kinachoendelea hapo ni kutegana na sio kingine. Nilimjibu “Kitu gani hicho?” Akajibu “We njoo basi, Acha woga”.
Basi sikua na jinsi, niliamua kunyanyuka na kuanza kuelekea kwenye hicho chumba. Nilopofika Mlangoni, nikapiga hodi, akaniambia “Sukuma tu mlango, ingia”. Na Mimi kweli nikafanya hiyo ili kuingia ndani.
Sikutarajia kuwa nitaingia kwenye mitego yake kirahisi hivyo. Ila ndio hivyo, nilishaingia tayari kwenye mtego na nilikua nimeisha tekwa hisia.
Humo ndani hatukua hata na cha maana cha kuongea. Tulikaa kwenye kitanda na sikumbuki tuliongea nini ila nakumbuka tulianza kurukiana rukiana humo ndani na yule dada.
Tukitumia muda mrefu sana humo ndani maana huyo dada alikua ni hatari sana. Nilijikuta silazi Damu kabisa.

Mwisho tulimaliza alafu akanilaza na kuanza kunikanda na maji viungo vilivyokua vinaniuma kama alavyokua akiongelea. Hicho kitu nilikua sijawahi fanyiwa. Huyo dada alifanya viungo viwe vizuri mpaka nikatamani ningekua ndio mume wake.
Siku hiyo nilitoka humo ndani nikiwa tayari nimeingia kwenye penzi na uyo Dada. Huyo dada alikua anasema ananipenda kuliko mume wake. Kwanzia hapo, tuliendelea kuwasilina kupitia simu na kuna muda tulikua tunakutana na kufurahia mambo yetu.
Tuliendelea kuwa na mawasiliano, na mara kadhaa tulikutana tena. Lakini mambo yote yalibadilika nilipopokea simu ya vitisho kutoka kwa mtu aliyedai kuwa ni mume wa Zena. Aliniambia ameunganisha simu ya mke wake na anaona ujumbe wote tunaotumiana. Alinipa onyo kali kwamba kama sitamuacha mke wake, atanichukulia hatua mbaya.
Niligundua kuwa nilikuwa kwenye hatari kubwa. Niliamua kumkwepa Zena, nikabadilisha hata namba yangu ya simu ili kuepuka mawasiliano naye. Japokuwa nilikuwa tayari nimempenda, nilijua kwamba kuendelea naye kutaharibu maisha yangu na ya kwake pia maana mume wake anapesa.
Mpaka sasa moyo yangu unampenda yule dada na natamani ajue hilo. Natamani ajue kuwa napenda kumuona na furaha, hata kama siyo nami.
Namfikiria na namuombea awe na furaha kwenye ndoa yake. Nilitamani sana kuwa naye, lakini niliamua kuheshimu ndoa yake. Hata sasa, bado sijapata njia ya kumsahau kabisa, lakini najua kuwa penzi letu haliwezi kuendelea.
Mwisho
NI UTELEZI (Simulizi Fupi ya Kusoma)
Nilihamia kwenye nyumba moja nzuri nikiwa napambana na maisha. Nilipata chumba kizuri sana, cha kisasa, lakini bei ya kulipia ilikuwa ndogo mno. Jambo Hilo ndio lililonivutia na nilivutiwa zaidi na utulivu wa nyumba yenyewe na upatikanaji wa huduma pia. Wenye nyumba walikuwa ni mume na mke, wakikaa peke yao bila mtoto yeyote. Kwa miezi michache, niliishi pale kwa amani bila shida yoyote, tukiheshimiana na wenye nyumba.
Siku moja, mtoto wao wa kike, Doris, alirudi kutoka masomoni. Hakuwa akiishi nao hapo muda mrefu kwa sababu alikuwa akisoma chuo, lakini alikuwa kwenye likizo kipindi hicho. Kabla hajaja nilikuwa nimesikia wazazi wake wakimzungumzia mara kadhaa, lakini sikuzingatia sana.
Aliporudi, mara ya kwanza kumwona nilishtuka kidogo. Doris alikuwa anamwili mdogo kiasi alafu mzuri wa kuvutia. Nilijikuta nashindwa kutomwangalia kila tulipokua tukipishana hapo nyumbani. Siku za mwanzo tulikuwa tukisalimiana tu kwa kifupi sana alafu bila mazungumzo hasa pale wazazi wake walipokuwapo karibu. Kuna wakati tulikuwa tunapitana kama hatuonani kabisa, kila mmoja anakua na mambo yake.
Siku moja, nilikuwa sokoni nikinunua mahitaji yangu ya kila siku. Wakati narudi, mvua ndogo ilianza kunyesha taratibu, lakini haikuchukua muda mvua ikaanza kuongezeka. Niliona ni heri nikimbilie nyumbani kabla haijawa kubwa kabisa. Wakati nakimbia, nilimuona Doris mbele yangu akitembea taratibu, akiwa amejifunika na mwamvuli. Bila kufikiria sana, niliamua kumkimbilia ili nijiunge naye chini ya mwamvuli wake.
Aliniona nikimkaribia, akaniangalia kwa haraka kisha akaniwekea mwamvuli vizuri ili utukinge wote. Nikiwa hapo, niliamua kufungua mazungumzo nea kwa kusema “Bora ulikuja na mwamvuli! Ulijuaje kama mvua itanyesha?” huku tukitembea.
Alitabasamu kisha akasema, “Niliona mawingu yanakusanyika, nikaona ni bora nijipange mapema kwa kuja na mwamvuli.” Sauti yake ilikua ya kuvutia sana. Nilijikuta nikiendelea kuongea nae kwa kumwambia, “Dah asante kwa kuniokoa. Huenda hua unaongea na Mungu wewe.”
Tulicheka pamoja, na mazungumzo yaliendelea kuwa mazuri sana. Safari ya kurudi nyumbani, ilionekana kama hitaisha haraka hivi… Na hatukutaka ifike mwisho. Doris alikuwa na harufu nzuri, na jinsi alivyoongea, nilivutiwa naye sana siku hiyo. Baada ya maongezi mazuri, alinionyesha kuwa anaweza kuwa rafiki na akanipa mpaka namba yake ya simu ili tuendelee kuchati kuwasiliana nae.
Tulipofika nyumbani, tulitengana kama hatukua wote. Kila mtu aliendelea na shughuli zake, lakini ndani yangu, moyo uliacha kuzingatia kazi yake ya kusukuma Damu, ukaanza kumpenda sana Doris.
Kwanzia siku hiyo, urafiki wetu uliendelea kukua. Nilianza kuwa mjanja, kila niliposikia wazazi wake wamemtuma sehemu fulani, nilihakikisha na mimi natoka kwa wakati huo ili tutoke pamoja. Hali ilifika mahali nilishindwa kuvumilia, nilimwambia kuwa na mpenda na nahitaji awe wangu.
Hakunisita hata kidogo, alikubali maana na yeye alikua ananipenda, na hapo uhusiano wetu wa siri ukaanza rasmi. Tuliendelea kuonana kisirisiri kila tulipopata nafasi. Tulikua tukitumia muda mwingi nje ya nyumbani ili kuepuka macho ya wazazi wake. Lakini kama unavyojua, hakuna siri inayodumu ikionwa na majirani. Majirani walianza kutusema, kwa wazazi wake Doris alafu wazazi walianza kututazama kwa macho ya mashaka. Walijaribu kutuchunguza lakini hawakuwa na ushahidi wa moja kwa moja, hivyo wakawa wanafikiria tu.
Siku moja, Mchana, Doris aliniambia usiku niache mlango wangu wazi, kuna jambo la kuniambia. Sikutaka kumuuliza sana, lakini nilihisi alitaka kufanya ninachokitamani kufanya nae lakini nakosa mbinu. Usiku ulipofika na watu wakiwa wamelala, nilihisi mlango wangu ukisukumwa, kisha nikaona anaingia Doris.
Basi utulipiga stori humo ndani kwa visauti flani ya chini chini mwisho tukaanza kutamani kushikana. Ndani ya muda mchache tukawa tayari tunaucheza mziki humo ndani. Huo mziki Doris alikua anataka sana na Kila nikibandika alikua analalamika lakini hataki nibandue. Doris alionekana kuwa na kiu ya kucheza na nami mziki mpaka ananivuta kwake. Niliendelea kufurahia kuwa naye huku nikiwa na hofu ya wazazi wake kujua. Nilikua najitahidi sana mziki usisikike nje usiku mpaka tukamaliza kucheza, akarudi kwao.
Hiyo ilikua ni siku ya Doris kutoroka kwao na kuja kwangu lakini hakuishia hapo, alikua akipata nafasi usiku anakuja kila mara.
Baada ya kuja mara kadhaa, wazazi wake walijua wazi kuwa kuna kitu kinachoendelea kati yetu. Walichukia sana na wakanipandishia bei ya chumba ghafla ili nihame. Walifikiri ningeshindwa kumudu kodi mpya na kuondoka, lakini mimi niliendelea kuishi pale…
Doris, kwa upande wake penzi lilimchanganya mpaka alifikia hatua ya kukataa kurudi chuo. Alianza kuwajibu wazazi wake vibaya kila walipomwonya kuhusu mimi na nilikua nasikia kabisa. Kila mara walipojaribu kunizungumzia vibaya, Doris alikuwa anatetea sana. Aliwahi hata kuwatishia kujiua kama watajaribu kututenganisha. Kwa kweli, nilianza kuwa na hofu kwa jinsi uhusiano wetu ulivyokuwa unazidi matarajio yangu. Mimi nilijua yatakuwa mahusiano ya kawaida tu alafu tutakuja kuachana baadae kama mahusiano yangu mengine ya huko nyuma.
Wakati hayo yote yakiendelea, siku moja Doris aliniambia kwamba ana ujauzito. Hapo ndipo moyo wangu ulianza kudunda kwa kasi sasa. Sikutarajia habari kama hizo kwa wakati ule alafu yeye alikua anataka azae kabisa. Nilihisi kama maisha yangu yakuwa yenye majukumu makubwa. Niliona kabisa kwenye maisha nitateleza na kuanguka na huyu Doris ni utelezi utakaoniangusha.
Katika hayo Mawazo, wazo la kumkimbia lilinijia maana niliona ndio njia sahihi ya kujiokoa muda huo. Nilianza kupanga kimya kimya jinsi nitakavyohama na kuanza maisha mapya sehemu nyingine. Nikapata chumba mbali na hapo alafu nikaanza kuhamisha vitu kwa Siri Kila usiku unapoingia.

Baada ya kuhamisha baadhi ya vitu vyangu muhimu kwa siri, niliondoka ghafla bila kumwambia. Nilihamia mbali ila sio sana. Nilikua nikifikiria kwamba pengine nikiwa huko nitakua na nguvu ya kumkataa Doris na ujauzito wake alafu nitaanza upya maisha yangu. Lakini usiku huo huo wa kwanza baada ya kuhama, nilikosa usingizi. Nilijikuta nikiwaza sana kuhusu Doris na jinsi alivyokuwa tayari kufanya kila kitu kwa ajili ya upendo wetu. Moyoni mwangu nilihisi kama nilikuwa napanga kufanya kosa kubwa.
Nilikua nikikumbuka jinsi alivyokua anavimba kwa wazazi wake kwaajili yangu, jinsi alivyonipenda, alivyoacha upendo wake kwangu umuendeshe bila kujali chochote kiasi kwamba wazazi wake walifikiri nimemloga. Moyoni mwangu, nilihisi kumwacha Doris kwa sababu ya ujauzito ingekuwa dhambi kubwa sana. Maumivu ambayo niliona naenda kumpa nilihisi kabisa hata mungu awezi nisamehe. Hivyo niliamua kupuuza maamuzi yangu.
Usiku huo huo nilimwandikia ujumbe Doris atoroke kwao aje sehemu niliopo. Baada ya kuja nilimshawishi tuanzishe maisha yetu pamoja. Na kweli, Doris alikubali japo alikua anaogopa kidogo. Tulikio yafanya sio mzuri sana lakini ndio tulianzakuishi pamoja kama mke na mume, ingawa hatukuwa tumehalalisha uhusiano wetu.
Wakati tuliendelea na maisha yetu, wazazi wake walianza kuachana na chuki zao kwangu. Waliniona nikijitahidi na kumtunza binti yao mpaka wanakosa sababu ya kunichukia . Hatimaye walinipa baraka zao, na nikamfanya Doris kuwa mke wangu rasmi.
Sasa tunaishi kwa furaha kama familia. Maisha ya kuishi pamoja Kuna muda yakuwa ni magumu kama haujajipanga lakini namshukuru mke wangu Doris kwa kuwa na mimi mpaka sasa tunamaisha mazuri kidogo.
Mwisho