Tag Archives: simulizi za mapenzi

MAPENZI NA MBWA (Simulizi fupi ya Kusoma)

Kulikuwa na binti mmoja aliyeishi maisha ya peke yake kwenye chumba kimoja alichokuwa amepanga. Alikuwa binti mdogo aliyeanza kuishi maisha hayo baada ya kumaliza chuo, lakini hakupata kazi wala mpenzi wa kumuoa. Maisha yake ya mahusiano hayakuwa mazuri, maana alikuwa ametendwa mara nyingi mpaka kufikia hapo.

Kwenye upande wa kazi, alikuwa anafanya kazi ya kuuza duka ambalo halikuwa lake. Yaani, yeye alikuwa mtu anayekwenda kuuza duka asubuhi na kurudi usiku, lakini duka na vilivyomo vilikuwa si vyake. Kupitia kazi hiyo ya kuuza duka, alikuwa akipata pesa kidogo ya kulipa chumba anachoishi na chakula cha kawaida.

Kila mara mwanamke huyo alionekana kutoamini wanaume, kiasi cha kuchukia kuwa nao kabisa. Hii ilitokana na mahusiano kadhaa aliyopitia na kuvunjwa moyo huko nyuma. Wanaume wengi waliokuwa wanahitaji kuwa naye hawakupata nafasi, na hata waliopata, waliishia kuachwa kila alipokumbuka jinsi wanaume walivyomuumiza kwenye mahusiano ya nyuma. Hii ilimfanya mara nyingi awe anatembea peke yake. Alikuwa haongozani na mtu anapotoka kazini kwake au kurudi. Kulikuwa na umbali kiasi kutoka anapouzia duka hadi kwake, lakini alikuwa anatembea kwa miguu kwa sababu umbali haukumchosha. Hata hivyo, katika kutembea kwake, changamoto kubwa aliyokuwa anakutana nayo ilikuwa ni mbwa.

Mbwa walikuwa wengi njiani alipokuwa akirudi kwake, hasa akichelewa usiku. Pamoja na kupita mara nyingi, alikuwa anaogopa sana mbwa. Tangu utotoni, alikuwa mtu anayewaogopa sana mbwa na kuwachukia, kwa sababu mbwa wa jirani yao alimng’ata akiwa na umri wa miaka 8. Tukio hilo lilimfanya aogope sana mbwa katika maisha yake yote.

Siku moja, katika njia ya kurudi nyumbani, alikutana na mbwa mmoja mdogo. Mbwa huyo alikuwa mbele yake, na alipomuona tu, alipunguza mwendo ili wapishane kwa tahadhari. Wakati wakipishana, mbwa akabweka ghafla, “Wouh!” Yule dada akaanza kukimbia kuelekea kwake. Mbwa kuona hivyo, akaanza kumkimbiza mpaka akaanguka chini baada ya hatua chache huku mbwa akiwa nyuma yake.
Baada ya kuanguka, mbwa alifika pale alipokuwa yule dada, lakini hakufanya chochote zaidi ya kumnusa na kuanza kurudi nyuma. Dada alipomuona mbwa anarudi, alinyanyuka haraka na kuendelea na safari ya kurudi nyumbani kwa haraka, akitembea huku akijipangusa vumbi kwenye nguo na kuangalia kama bado anafuatwa. Mbwa alibaki kusimama mbali, akimuangalia kwa umbali.

Baada ya hatua nyingi za kutembea, yule dada aliangalia nyuma na kukuta mbwa yule anamfuata taratibu. Hilo lilimshangaza sana, likamfanya aongeze mwendo mpaka akafika nyumbani bila matatizo, ingawa nguo zake zilikuwa zimechafuka kwa vumbi. Ilikuwa kawaida kwake kukimbizwa na mbwa, hivyo hakuchukulia kama jambo kubwa sana.

Lakini baada ya siku hiyo, alianza kushangazwa na jambo ambalo halijawahi kumtokea maishani. Mbwa yule alianza kumfuata kila mara na kujipitisha karibu na nyumbani kwake. Kila alipokuwa akitoka au kurudi, alikuwa akimuona mbwa huyo akiwa karibu naye au akimfuatilia kwa umbali.

Hili lilikuwa jambo geni kwake, maana hajawahi kuwa na urafiki na mbwa. Wakati mwingine alikuwa akimtupia mawe, lakini mbwa hakuwahi kuacha kumfuata kwa upole uleule. Alijaribu kumfanyia ubaya mara kadhaa, lakini mbwa hakukoma kuhitaji kuwa karibu naye. Wakati mwingine alikuta amelala mlangoni kwake.

Baada ya matukio mengi, yule dada aliamua kuanza kumchukulia yule mbwa kama mbwa wake. Ingawa hakuwahi kufanya hivyo maishani mwake, aliamua kujaribu tu kumfuga. Alianza kumjali kwa kumpa chakula, hadi wakaanza kutembea pamoja kwenye baadhi ya safari zake. Alishangazwa sana na jinsi mbwa huyo alivyokuwa mwaminifu kwake, hasa alipokuwa anarudi nyumbani usiku. Alikuwa akitembea naye kwenye njia alizokuwa akiziogopa bila uoga. Mbali na hilo, alianza kukosa hofu hata alipokutana na mbwa wengine, maana sasa alikuwa ameelewa tabia zao kupitia mbwa wake.

Mwisho wa yote, hakujutia kabisa kumfuga mbwa huyo, ingawa baada ya mwaka mmoja alikufa kwa kugongwa na gari akiwa kwenye mizunguko yake. Lakini aliacha funzo kubwa kwa yule dada juu ya kutoa nafasi ya upendo kwa watu au vitu anavyoviogopa, kwa sababu hajavijua vizuri. Alifanikiwa mpaka kupata mtu anaempenda sana na kuishi nae kwa uaminifu maishani.

Kutokana na mambo aliopitia, Kila mara alikua akishuhudia watu kuwa kuna wanawake hupitia mahusiano kadhaa yanayovunja moyo, kiasi cha kufanya wasihitaji ukaribu wa mapenzi ya kweli kwa wanaume. Wengine hawapiti huko, lakini kutokana na matukio au simulizi mbalimbali, wanashindwa kuamini wanaume. Kuna ambao husema hata “Wanaume wote ni mbwa,” na kuzingatia pesa. Wanafanya hayo wakisahau kwamba hata huyo Mbwa anaweza kuwa wao, akawapenda, kuwafurahisha, na kuwalinda Kila siku. Kikubwa ni uwe tayari kumpa nafasi, huku na yeye akiwa tayari kuwa wako.

Mukijua mambo haya hamuwezi kuachana na Mpenzi wako kirahisi BONYEZA HAPA>>>

Mambo 3 niliojifunza baada ya kusoma SUKARI YA DADA, UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA (Simulizi)

Baada ya kuzisoma simulizi tatu nzuri; Sukari ya Dada, Utamu wa Jumla na Mzigo wa Wakubwa, nimegundua funzo kubwa kuhusu maisha halisi ambalo hapa nitaweka wazi.

Simulizi hizi tatu ni miongoni mwa simulizi nzuri sana ambazo zimesimulia maisha ya watu tofauti wanaoishi katika ulimwengu mmoja.
Kila simulizi lina hadithi yake tofauti, lakini unaposoma zote kwa pamoja, unagundua zinaunda picha moja kubwa inayogusa maisha ya vijana, mapenzi, na changamoto nyingine katika jamii.

Baada ya kuzisoma kwa makini, haya ndiyo mambo matatu kati ya mengi muhimu niliyojifunza;

Mambo 3 Niliojifunza Baada ya Kusoma simulizi

1. Usifanye Usichopenda Kufanyiwa

Hili limejitokeza sana katika simulizi ya Mzigo wa Wakubwa.
Mhusika mkuu alijikuta akimfanyia rafiki yake jambo baya; kuchukua pesa zake ili kuokoa hali yake binafsi. Lakini muda haukupita, naye akajikuta akifanyiwa jambo lilelile na mtu mwingine wa karibu sana.

Maumivu aliyoyapata yalikuwa makubwa, lakini hakuweza kulalamika kwa sababu alitambua kwamba naye aliwahi kufanya kosa hilo.
Hapa kuna somo moja kubwa:

“Ukifanya ubaya, ujue ipo siku utaukuta uso kwa uso… Inaweza kuwa si leo, lakini ipo siku.”

2. Huwezi Kumpima Mtu kwa Kuangalia Tu

Hili nimejifunza kupitia simulizi mbili; Sukari ya Dada na Utamu wa Jumla.
Mwisho wa Sukari ya Dada, muhusika mkuu anakutana na Tausi na kuhisi kuwa anaishi na virusi vya UKIMWI.
Lakini unaposoma Utamu wa Jumla, unakuja kugundua kuwa Tausi hana virusi kabisa!

Hii imenifunza kitu kimoja muhimu sana:

“Usihukumu mtu kwa muonekano wake wa nje au mazingira yake. Ni ngumu kujua hata vita gani anaipigana ndani yake.”

3. Kila Mtu Ana Njia Yake ya Mafanikio

Katika simulizi zote tatu, wahusika walionesha njia tofauti za kupambana na maisha.
Wote walikuwa vijana waliokataa kukata tamaa. Yani kila mmoja alipambana kwa namna yake hadi kufikia mafanikio ambayo anayahitaji. Hakuna aliekubali kushindwa, wote walikubali kusonga mbele kutafuta ushindi kwenye njia zao.

Simulizi hizi zimenikumbusha kuwa:

“Hakuna njia moja sahihi ya kufanikiwa. Kila mtu ana wakati wake, njia yake, na changamoto zake za kipekee.”

Kwa ujumla, simulizi hizi tatu zimebeba uhalisia wa maisha ya sasa kwa upande wa vijana. Kwaiyo nilioyaongelea tu, utaona zinatuonesha kuwa dunia ni duara unachokifanya leo, kinaweza kukurudia kesho. Zinatusukuma pia kuwa waangalifu, wenye huruma, na wenye subira katika safari zetu za mafanikio.

KWENYE KAGIZA (Simulizi fupi ya Kusoma)

Nilikua nimeolewa na ninaishi na mume wangu kwa amani sana. Katika miaka yetu michache ya ndoa, kulikua na changamoto moja tuliyopitia na siwezi sema wazi niliimaliza vipi sasaivi, lakini acha nifafanue mambo yalivyokua.

Mme wangu alikua na rafiki yake mmoja anaitwa Mambe; Aliekua kama ndugu kwake. Kabla ya mume wangu kukutana na mimi, alikua na huyo rafiki yake, hivyo mimi ndio nilikua mgeni kwenye urafiki wao.
Urafiki wao haukua wa kuitana rafiki tu, walikua wameungana pamoja hata kwenye kazi. Walikua wanafanya kazi sehemu moja na wanashirikiana kwenye mambo mbalimbali ikiwemo ya kiuchumi.
Huko kazini, nilikua nasikia huyu rafiki ndio mwenye cheo kikubwa na pia anaundugu na bosi wao mkubwa kabisa. Mme wangu alikua ananisimulia mambo mengi mazuri anayofanya huyo rafiki yake. Alikua anasema “Huyu Mambe ni ndugu yangu” kila mara tunapomuongelea.
Na ukweli huyo rafiki yake alikua anaonekana mstaarabu sana, lakini siku moja kwenye kupiga stori na mmoja wa marafiki zangu alinieleza mambo ambayo sikuamini kuhusu yeye. Huyu rafiki yangu alikua anaitwa Lisah na alikua ananisuka nywele huku akinipa stori za huyo mwanaume.
Nakumbuka alisema huyo Mambe ni mwanaume mpole, anaishi peke yake, lakini anawanawake wengi sana hapo mjini anao wahudumia na hawajijui. Ilikua ni kawaida sana kusema watu tukiwa na rafiki yangu, maana ni mtu anayejihusisha na kusuka nywele huku akiongea sana. Lisah liniambia pia kuwa amewahi kupewa pesa akawa nae pamoja usiku mmoja kipindi cha nyuma ila hawakua wapenzi.

Baada ya kama mwaka hivi, nilikua nimesikia mambo mengi sana kuhusu yeye, na ilionekana ni kweli yupo hivyo hata akisimama mbele ya macho yangu.
Hii haikua tatizo kwangu, lakini tatizo langu lilianza kuwa ni ukaribu wake na mume wangu, maana wanasema ndege wanaofanana huruka pamoja.

Nilipomaliza kuchunguza marafiki wa mume na kukuta yupo hivyo, nikajikuta nimeingiwa na mashaka na mume wangu pia. Hali hii ilikua kama utani ilipoanza, lakini baada ya muda ikawa ni tatizo hata kwangu, maana nilikua nakosa amani. Nilishindwa kumuamini moja kwa moja hata akisema anaenda kazini.
Kiufupi, nilikua najiona kama na mimi nasalitiwa na mwanaume wangu, kwa sababu niliona jinsi rafiki zake wanavyochezea wanawake huku wakiwa nao. Nilijikuta nipo kwenye ndoa ambayo sikujiona kama niko salama kabisa. Moyo wangu ulikua unawasiwasi sana, na huo wasiwasi niliufanya siri. Ndoa yangu ilikua kama inapita KWENYE KAGIZA.

Huo wasiwasi niliokua nao ulianza kunisukuma kufanya mambo ya ajabu kwa mme wangu. Yaani nilikua kila mara namfuatilia kama namchunga, halafu akifanya jambo nisilolielewa namtukana sana kuwa anawanawake nje ya ndoa.
Mme wangu alikua anakataa, ila nilikua namtupia maneno mengi sana hata akichelewa kurudi nyumbani kidogo tu.
Ilikua ni kawaida sana kumwambia “Rudi kwa wanawake zako, kalale huko huko!!! Mbwa wewe.”
Mwanaume wangu alikua ananiangalia na kunionya kuhusu maneno yangu, japokuwa alikua ananiacha niongee mpaka hasira ziishe.

Nilijaribu kuchunguza sana kama na yeye ana tabia hizo, lakini sikupata ushahidi wowote. Mwisho nikaamua kupanga siku ya kumuuliza mme yangu juu ya tabia mbaya za rafiki Mambe, maana yeye huongelea tabia nzuri tu.
Siku moja katika stori za hapa na pale tukiwa chumbani, nikaingizia hizo habari za rafiki yake. Nilishangaa kuona na yeye anakubali kuwa rafiki yake anafanya mambo hayo hapo mjini.
Ikabidi nimuulize, “Sasa kama rafiki yako yupo hivyo, inamaanisha na wewe upo hivyo?”
Akanijibu, “Hapana, mimi huwa namshauri aoe na kuwa na mwanamke mmoja.”
Pia alisema kuwa wanaume wanaweza kuwa marafiki sana lakini wakawa na tabia tofauti kwa wanawake. Mwanaume mmoja anaweza kumtesa mke wake lakini rafiki zake hawatesi wake zao. Hivyo nisiwe na wasiwasi.

Kiukweli moyo wangu haukuwa na chochote zaidi ya kumuamini, maana ushahidi wa yeye kunisaliti nilikua sina kabisa. Lakini nilijifunza kutochunguza sana marafiki wa mwanaume, maana walinifanya niwaze sana na kukosa amani kwenye ndoa yangu.
Unaweza kujikuta unaumiza moyo wako na kumhukumu mpenzi wako kwa sababu ya kuwachunguza rafiki zake….

Baada ya muda mingi kupitia walianza kutengana maana naskia tabia ya Rafiki yake ilizidi kuwa mbaya mpaka akawa anafumaniwa na wake za watu. Hii ilimfanya mme wangu kuwa mbali nae maana ananipenda sana. Alianza kunikataza mpaka mazoea nae.

Yote kwangu yalikua ni furaha maana nilipata amani ya moyo.

MWISHO

RAHA ZA MSAADA (Simulizi fupi ya Kusoma)

Baada ya kuoa nilijua nimepata mke wa kuishi naye na ambaye angeweza kunifanya nipate amani na nilidhike kila ninapomhitaji. Naweza kusema ilianza hivyo, lakini haikuishia hivyo. Mambo yalikuwa hivi;

Baada ya ndoa, nilianza kuishi na mke wangu Neriah kwa furaha kubwa. Alikuwa mwanamke mzuri sana na nilijivunia kumuweka ndani. Ilikuwa ndoto yangu siku zote kumwoa, na japo watu wengi walimuwinda, mimi ndiye nilibahatika. Haikuwa rahisi, kwa sababu hali yangu ya kifedha haikuwa kubwa sanaa, lakini nilijitahidi hata kumwaga pesa kiasi fulani ili anielewe.

Tulipoanza maisha, kila siku nilitoka kazini asubuhi na kurudi mchana, naye akibaki nyumbani kufanya shughuli za ndani. Baada ya muda alianza kuleta marafiki zake wengi nyumbani. Niliporudi kazini mara nyingi niliwakuta, jambo lililonifanya nisiwe huru sana. Nilimueleza juu ya hili, akapunguza kidogo, lakini tabia ikaendelea.

Kadri muda ulivyopita, nilianza hata kuzoeana na baadhi ya marafiki zake. Hata barabarani walinisalimia na wengine walikuwa wakinionesha wanapokaa, wakinikaribisha kwa kusema: “Shemeji karibu, mimi nakaa hapa.” Kwa sababu nilimpenda mke wangu, nilichukulia wote kama mashemeji.

Baada ya miaka miwili, ndoa yangu ikaanza kubadilika. Mke wangu alianza kuwa na makasiriko ambayo mara nyingi yalitokana na ndugu zake. Kwa kuwa sisi ndiyo tulikuwa na uwezo kiasi katika ukoo, alianza kuwasaidia. Mwanzoni alikuwa akiniambia kabla ya kufanya chochote, lakini baadaye akaanza kufanya maamuzi bila kunishirikisha. Alifikia hata kuuza vitu vyetu au kugawa bila ruhusa yangu. Nilijaribu kumkalisha tuzungumze, lakini akawa mkali sana, kama ilivyo tabia ya baadhi ya wanawake wanapokomaa kwenye ndoa.

Wakati huo huo, mambo yangu ya kazi yalikwama. Niliyumba kiuchumi, japo sikupungukiwa chakula. Lakini tabia yake ya kufanya mambo pasipo kuniambia ilinipa mawazo makubwa. Nilivumilia sana, lakini alikuwa haambiliki. Sio kwamba hakunipenda, alinipenda, ila vitendo vyake vilinifanya nisimwelewe. Nilihisi pengine tatizo letu lilikuwa kuchelewa kupata mtoto.

Misukosuko ikaendelea, na hali yangu kifedha ikazidi kuwa mbaya. Kila mara tulipogombana, mke wangu alikuwa akirudi kwao. Nilikua naomba sana ndio anarudi. Nilimweleza mara nyingi atulie ili nipate nafasi ya kutafuta kupambana mambo ya kimaisha vizuri, lakini hakunielewa.

Katika hali hiyo, nilijikuta nikiwa na mawasiliano ya karibu na rafiki zake, hasa mmoja aitwaye Julieth. Wakati mwingine nilimhitaji anisaidie kuniunganisha na mke wangu pale ambapo mke wangu hakuwa tayari kunisikiliza. Hali hii ikatufanya tuzoeane sana.

Julieth alikuwa mwanamke mzuri, mwenye mvuto, lakini kwa kuwa nilimheshimu kama rafiki wa mke wangu, tulidumisha heshima. Lakini, kutokana na ukosefu wa amani katika ndoa yangu, nilijikuta nikiingia kwenye penzi zito naye. Julieth alikuwa single mother akiishi na mtoto wake, na alijipenda sana. Alikua na mwili ulioja kidogo ila ni mzuri utafikili hana mtoto.

Tulipoanza uhusiano, maisha yangu yalianza kuwa na mwanga tena. Nilipata furaha, mambo ya kazini yalienda vizuri kwenye upande WA uchumi na niliweza kuvumilia vituko vya mke wangu bila maumivu makubwa. Mapenzi ya Julieth yalikuwa matamu, hasa kwa kuwa yalikuwa ya siri. Nilikua nikienda kwake nasahua maudhi yote ya mke wangu. Na kwakua alikua anajua kitu gani kina nisumbua kwenye ndoa yangu, alikua hanipi nafasi ya kuwaza.


Lakini Pamoja na kwamba tulikua na mahusiano na Julieth, Bado mke wangu tulikua tuna muheshimu sana. Nakumbuka hata Julieth alikua anasema yupo na mimi kwasababu ya ninayopitia na ukaribu tulioujenga kati yetu. Alikua ananikumbusha mpaka kurudi nyumbani nikiwa nae kwa muda mrefu. Aliwahi pia kuniambia kwa haamini sana kwenye mapenzi kwasababu mtu aliemzalisha wanawasiliana ila anamsumbua sana. Na hakunificha, aliniambia anampenda ila ndio hivyo tu hawapo sawa.
Alikua unaurusha moyo wangu kwa furaha tukiwa kwenye uwanja wetu. Yani nilikua nikizidisha makofi, yeye anakua mtu wa viitikio tu “ooh.. shem” mpaka nachanganyikiwa.

Tuliendelea na mahusiano ya Siri kwa muda flani japo lilikua sio jambo zuri. Lakini baada ya muda, mke wangu alipata ujauzito wangu. Ujio wa mtoto ulikuwa jambo kubwa sana kwenye familia yetu. Kuanzia hapo niliacha kabisa uhusiano na Julieth na kuelekeza nguvu zangu kwa mke wangu. Hatimaye alijifungua na akawa mwanamke wa heshima tena kwangu. Hali hii ilinishangaza ila nikaichukulia kama ilivyo.

Mapenzi kati yangu na Julieth yalikoma, na tukabaki kuheshimiana kwa umbali ghafla tu. Baadaye nikasikia ameolewa na baba wa mtoto wake. Hii ilikua ni habari nje kwangu maana mapenzi yote yalikua kwa mwanamke wangu na mtoto wangu.

Maisha yaliendelea, lakini kipande hiki cha safari ya maisha yangu kilinifundisha mambo makubwa sana. Wewe umejinza nini kwenye sehemu hii ya maisha yangu? Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy!

MWISHO

UTAMU WA JUMLA 11 (Simulizi ya Maandishi)

Au nimwambie asitume alafu nimwambie kilichotokea?… Hapana, kwasasa siwezi hata kumwambia, ngoja nimtumie namba yangu ya benki ili atume hela humo”. Basi nikafanya hivyo na kabla sijafika nyumbani hela ziliingia alafu nikamshukuru. Ila mawazo hayakuisha kichwani na kiukweli dunia nilikua naiona mbaya sana muda huo.

Nilirudi kwenye chumba nilichopanga nikakuta Salma yupo pale na nikakuta amepika chakula. Nilipofika Salma aliniuliza mbona kama umewahi kurudi, nikamwambia mafunzo yamewahi kuisha. Nilimficha kuhusu mambo yaliotokea na nilikua najaribu kujifanya niko sawa. Alinikaribisha kula chakula alichopika akaniambia hela niliompa ndio ametumia kukiandaa chakula hicho na amenibakizia pia. Nakumbuka nilikaa kama wiki hivi nikijaribu kumficha Salma kilichonikuta lakini sikuweza. kunasiku nilikua nimekaa njee yeye yupo ndani, nikakuta tu ameniita ndani na mimi bila kusita nikaenda ndani. Nikamkuta amekaa kitandani na nilipoingia tu nikamwambia “Unaniitia nini Salma?” akaniambia “Kaa hapa mpenzi wangu” huku akigusa kitandani anapotaka nikae. Mimi nikafanya alichosema, nikakaa nae pale kitandani alafu nikamwambia “Niambie”.

Nikakuta ananishika mkono mmoja alafu anaviingiza vidole vya mikono yake milaini kwenye nafasi ya vidole vya mkono wangu kisha akaniambia “Mpenzi wangu sasahivi umebadilika mpaka najihisi kama nimekukosea hivi… Ila nawaza nimekukosea nini lakini sipati jibu… Unaonekana ni mtu mwenye mawazo sana alafu hata kule unakosema kuna mafunzo unajifunza naona huendi.. Kula nako nakuona hukuzingatii na hata nikipika huwa nakulazimisha sana kula”. Mimi kusikia hivyo, nikafikilia nikaona anachosema ni kweli kabisa nimebadilika maana hata mwili wangu tu kuna jinsi ulianza kupungua kutokana na mawazo lakini nikajaribu kumficha kwa kusema “Ah mbona nipo vizuri tu Salma…Haujanikosea wala nini. Bado nakupenda malaika wangu, usiumize kichwa” nikakuta kasema “Haupo sawa… acha kichwa changu kiumie tu kwaajili yako maana nakupenda. mimi nipo kwenye mahusiano na wewe kwa muda mfupi lakini jinsi ulivyo nijaa kichwani mwangu ni kama nimekaa na wewe muda mrefu… Kuna vitu sivijui toka kwako lakini huwezi nificha hali yako, nakuona kabisa haupo vizuri. Niambie nini tatizo mpenzi wangu”. Bado nilikua mbishi kufunguka kinacho nisumbua mbele yake, nikasema “salma, ondoa hofu niko sawa… Kuna vitu tu vinanisumbua ila haviusiani na mapenzi yetu” akaniambia “Wewe unanificha tu ila tambua kuwa mtu akiwa anamchukia mtu, anakua anajisikia vizuri akiwa na hali mbaya lakini akiwa anampenda hujisikia vibaya kuona yupo kwenye hali mbaya…. sasa mimi ninavyokupenda hivi unafikili nakua kwenye hali gani ukiwa kwenye hali hiyo? Au unataka niondoke ila hutaki kuniambia?”.

Mh mimi mwanzo nilikua naona huenda nikimwambia ataanza kunizarau na kuniacha kwa kuona sina muelekeo ila muda huo mimi nikaona nifunguke tu maana kilikua ni kitu ambacho kinanisumbua akili mpaka nilianza kutamani kifo japo nilikua najaribu kuficha sana. Nilivyomwambia nikakuta ananipa pole na kuanza kunipa naneno mazuri ambayo kiukweli yalinisaidia. Aliniadithia mpaka hadithi za watu ambao anasikia walipitia sehemu ngumu sana katika maisha yao lakini walipambana bila kukata tamaa na mwisho maisha yao yalikua mazuri.

Nashukuru Mungu Salma alikuepo pale na kujaribu kuirudisha akili yangu kwenye mstari kidogo maana kabla ya kufunguka nilikua nahisi niko pekeangu. Tatizo lililonikuta alilichukulia kama limemkuta yeye na alikua upande wangu kwa kunitia moyo. Huenda tatizo hilo lingenikuta wakati salma hayupo maishani mwangu, ningefanya maamuzi mabaya sana kuhusu maisha yangu maana moyo na akili yangu vilikua havitoshi kuvumilia. Kwanzia hapo niliona Salma ni mmoja ya wanawake wenye akili sana. Na baada ya hapo nilijihisi ninanguvu sana tofauti na nilivokua. Nakumbuka baada ya siku mbili nilianza kupanga mipango ya kuanza biashara maana niliona kwakua nimesomea mambo ya biashara bila kupata ajira, huenda nikitumia elimu yangu kufanya biashara zangu naweza nikafika mbali.
Baada ya kupanga mipango, nikaingia kwenye vitendo kwakutumia hela niliotumiwa na wazazi wangu kwaajili ya kupata kazi kwenye yale mafunzo na kuna pesa nyingine niliokuanayo benki kwaajili ya kula nilikua nikiitumia kwaajili ya chakula nyumbani. Wazazi wangu niliwajulisha mambo yalionikuta alafu nikawaambia kwa sasa napambana kwanye biashara tu huku mjini.

Mwanzoni maisha yaliyumba sana na tulichakaa sana ila Salma alikua bado yupo upande wangu. Yani kuna muda nilikua nikimuangalia najisikia vibaya kumchakaza vile mtoto wa watu lakini yeye alikua bado yupo upande wangu na ananionesha upendo na kunishauri ninapotaka anishauri. Nilimshukuru sana mungu kwa kunipa mwanamke wa namna hiyo maana ni wanawake wachache wanaweza fanya hivyo.

Katika kupambana na maisha, sikuwahi kutana na Zuu wala Sara ila niliwahi kutana na Jimmy. Alikua yupo kwenye gari moja kari sana na wala hatukukaa kuongea, alinipungia mkono tu akiwa anaendesha gari kama anawahi sehemu hivi. Aliniacha nafikilia “Sjui aliotea mchongo gani huko?… Dah mwanangu hata kunishtua na mimi niende aliona anachelewa yani… Ila kila mtu na maisha yake hapa duniani acha tu nipambane na maisha yangu”

Basi nikaendelea kupambana na maisha yangu na baada ya muda mambo yalianza kukubali na maisha yalianza kuwa mazuri sana. Mimi na Salma tulifanya utaratibu wa kuwa wanandoa rasmi, tukajenga nyumba nje ya dar na pia nilikua na biashara zenye mafanikio makubwa tu mpaka nikamuingiza Salma kwenye biashara pia.

Nilimshauri aanzishe biashara ya urembo maana alikua anajua sana mambo hayo na alikua anauwezo wa kuwashauri wanawake wenzake kwenye mambo ya urembo. Alikua anafanya vizuri sana upande wa urembo ingawa kipindi hicho alikua anavaa nguo za heshima sana tofauti na mwanzo ila alikua bado anavutia sana. Uzuri wake ulikua haujifichi na baadae tulipata mtoto wa kike alikua mzuri kama yeye. Wakati anamimba ilimllazimu akapime virusi vya UKIMWI na hii iliniogopesha sana kutokana na kazi aliokua anafanya kabla ya kukutana na mimi lakini hakukutwa na virusi vya UKIMWI. Tulienda kupima tena tukiwa wote lakini bado majibu yalikua vizuri. Tulifurahi sana japo ata tungepata isingekua mwisho wa maisha yetu au furaha yetu, ningeendelea kumpenda tu. Namshukuru mungu maisha yetu yanaendelea kuwa mazuri na furaha mpaka sasa. Pia nashukuru mungu kwa kunipa mke bora kwa maisha yangu, nampenda sana salma.

MWISHO

Imetolewa na : The Bestgalaxy

Mawasiliano : +255 715 233 405

Simulizi ya UTAMU WA JUMLA ilio katika maandishi. Ina uhusiano kidogo na Simulizi ya SUKARI YA DADA na MZIGO WA WAKUBWA. Inapatikana katika Sauti pia. Kwaiyo usiishie hapa, Endelea kusoma simulizi nyingine!

Unaweza piga namba +255 715 233 405 au Njoo WhatsApp kwa namba +255 622 586 399 ili kutoa maoni yako juu ya simulizi au kupata maelezo zaidi kuhusu simulizi!

ZINGATIA HII: Tafadhali fahamu kuwa hadithi hii ni mali ya mwandishi. Hairuhusiwi kunakili hadithi yote bila idhini. Unaweza kushiriki au kuchukua sehemu ndogo ya hadithi, lakini si kuichukua hadithi kamili. Asante kwa kuheshimu kazi ya mwandishi!

Simulizi Bora za kusoma au kufuatilia katika The bestgalaxy

Katika moja ya mambo watu hufurahia kwenye simu zao ni kufuatilia simulizi mbalimbali kwa kusoma au kusikiliza. Hili ni jambo zuri ambalo mtu anaweza kulifanya kwenye simu mbali na kuwasiliana na watu. Sio kila muda mtu anaposhika simu anawasiliana na watu, Kuna muda anawezakua anafuatilia simulizi anazozipenda toka The bestgalaxy au sehemu nyingine.

The bestgalaxy ni sehemu unayoweza kujifunza mambo mbalimbali kuhusu mahusiano, Teknolojia na mengineyo. Katika the Bestgalaxy mtu unaweza pata simulizi pia. Na simulizi nyingi za The Bestgalaxy zimejikita kwenye mahusiano kwasababu ya kuburudisha na kuelimisha kwenye upande huo.


Katika makala hii tumeorodhesha simulizi chache nzuri za kusoma unazoweza pata kutoka The bestgalaxy. Kama unapenda kusoma simulizi za mahusiano/Mapenzi, basi zingatia orodha hii.

Hizi ni Simulizi Bora za kusoma au kufuatilia (Mapenzi na Maisha)

SUKARI YA DADA

Sukari ya dada ni simulizi inayomuhusu Kijana ambae alienda Dar es salaam kwaajili ya kufanya kazi za ndani baada kutofanya vizuri kidato cha nne. Kwenda huko ilikua ni njia pekee alioiona itamsaidia maishani kwa wakati huo lakini katika kuelekea anapohitaji, anakutana na changamoto nyingi sana kutokana na ujana.
Unaposoma simulizi hii, unapelekwa moja kwa moja katika kuyaona maisha ya kijana huyo. Lakini katika kuisoma simulizi ya SUKARI YA DADA, unatakiwa kuwa ni mtu uliefikisha umri wa maika 18 au zaidi.
Ukimaliza kuisoma simulizi ya SUKARI YA DADA mpaka mwisho, unaweza soma pia simulizi nyingine 2 ambazo ni UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA kwasababu zinauhusiano. Tutafafanua zaidi kuhusu simulizi hizi huku tukiwa tunaendelea na orodha.

UNANIITA?

Simulizi hii ni fupi na inamhusu kijana mdogo ambaye kazi yake ni kuendesha bodaboda mjini. Siku moja, anakutana na mteja mpya aitwaye Zena, mwanamke mrembo anayekabiliwa na changamoto katika uhusiano wake wa ndoa. Kupitia safari zao pamoja, Zena anafunguka kuhusu matatizo anayopitia na jinsi anavyojisikia kupuuzwa na mume wake. Kijana huyu anajaribu kumpa ushauri wa kumsaidia kuboresha mawasiliano na mumewe.
Hii ni moja ya simulizi nzuri sana lakini ni fupi.

UTAMU WA JUMLA

Unaposoma simulizi hii, unafuatilia maisha kijana aliyekulia Tabora na baadaye kuhamia Dar es Salaam kwa ajili ya masomo ya biashara chuoni. Akiwa chuoni, anakuwa na urafiki na Jimmy. Unaangalia maisha yake na changamoto anazopitia akiwa kama kijana amambe amesoma chuo na akiwa na ndoto au matarajio ya kufanikiwa maishani.
Hii simulizi inahusiano na simulizi 2 ambazo ni SUKARI YA DADA na MZIGO WA WAKUBWA. Kama umeisoma simulizi nzima ya SUKARI YA DADA na unataka simulizi nyingine, basi soma simulizi hii. Lakini unapoisoma, umri wako uwe umefia miaka 18.

SIRI NA SHEMEJI

SIRI NA SHEMEJI ni simulizi fupi inayomfuata Anisa, mwanamke mwenye heshima na upendo kwa mume wake, Kevin. Wakati ndoa yao ni changa, Anisa anabeba siri nzito kuhusu uhusiano wake wa zamani. Jambo hilo linamletea Anisa wasiwasi na hatimaye kusababisha mgogoro mkubwa katika ndoa yake na Kevin. Simulizi hii inagusia mada za uaminifu, siri, na msamaha katika mahusiano ya ndoa.
Ni simulizi isio ndefu lakini ni nzuri na inaweza kukupa burudani bila kupoteza muda wako sana.

MZIGO WA WAKUBWA

Katika simulizi hii, unaingia katika Maisha ya kijana anaekua na kuanza kuyazingatia maisha huku akishikilia Mahusiano ya mapenzi. Kijana huyu katika simulizi, anafanya baadhi ya maamuzi ya kukimbia mizingo akihisi ni yawakubwa.
Kama umeisoma simulizi ya SUKARI YA DADA na UTAMU WA JUMLA, basi simulizi ya MZIGO WA WAKUBWA ni simulizi unayotakiwa kumalizia kuisoma. Simulizi hizo tatu zinauhusiano na msomaji anashauriwa kuzisoma zote Loki kupata mocha moja nzuri na yaajabu sana.

Unachotakiwa kujua kuhusu simulizi ya SUKARI YA DADA, UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA

Simulizi ya SUKARI YA DADA, UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA ni simulizi unazoweza zisima pamoja ili kupata picha nzuri. Zimesimuliwa na watu tofauti ila zinakupa picha moja nzuri sana inayohusu mahusiano(Mapenzi)na maisha kwa ujumla. Na katika upande wa majina, kila jina Lina maana katika simulizi. Mfano; jina la MZIGO WA WAKUBWA katika simulizi lina maana “Majukumu”.

MZIGO WA WAKUBWA 01  (Simulizi ya Kusoma)




Tulikua tupo mimi na rafiki yangu Samsoni kwenye chumba chetu tunacholala ambacho watu huita Geto. Ilikua mida ya kama saa moja au mbili usiku hivi alafu muda huo rafiki yangu alikua ananihadithia mechi ya mpira ambayo imetoka kumalizika saa 2 zilizo pita na sikwenda kuiangalia kwenye vibanda vya mpira siku hiyo kutokana na mawazo. Mawazo yalifanya kichwa changu kiwe vibaya sana muda huo kiasi kwamba nilikua naonekana kumsikiliza Samsoni lakini kiukweli nilikua hata simuelewi japo nilikua nacheka kila akicheka na kuitikia “Ebwana ee” ili asigundue kua akili yangu haipo kabisa kwenye anayonisimilia.

Katikati ya hadithi zake za mpira tukasikia simu imeanza kuita katika kisehemu tunachozichaji simu kilichokua pembeni kidogo ya dirisha la chumba hicho. Simu yangu na ya Rafiki yangu Samsoni, zote zilikua zipo chaji alafu simu yangu niliichomeka chaji ikiwa imezimwa. Hivyo simu iliokua ikiita muda huo ilikua ni ya rafiki yangu na tuliigeukia wote ilipokua inaita maana ilitushtua kwa kupiga kelele katikati ya maongezi. Baada ya hapo Samsoni  alinyanyuka huku akijisemesha “Sijui nani huyu… itakua watu wa mpira hawa” alafu akaenda kuichukua ile simu mimi nikiwa namuangalia tu. Alipoishika simu na kusoma jina, nilimsikia akasema “Ah wewe Mpenzi wako huyu ananipiga huku. Sijui umekifanya nini tena kitoto cha watu”

Mimi nikashtuka kidogo alafu nikamuuliza “Ni Sabrina?” Samsoni alijibu “Ndio” alafu akasema tena “Ngoja nipokee nimsikilize” huku akiipokea simu na kuiweka sikioni. Mimi muda huo nilitaka nimwambie asipoke ila alikua ameishapokea kabla hata sijanyanyua mdomo kumwambia. Baada ya Samsoni kupokea simu, nilimsikia akisema “Halo Dada… niambie” alafu nikasikia kisauti kidogo cha Sabrina akasema “mambo vipi?” Samsoni akaitikia “kama kawa, vipi huko?”  Sabrina akasema “safi. Mbona rafiki yako hapatikani kwenye simu? Upo nae hapo?”. Mimi kusikia hivyo nikashtuka, nikamwambia kwa ishara rafiki yangu Samsoni asiseme yupo na mimi.

Samsoni alinielewa akamjibu “Sipo nae. mimi niko mbali kidogo muda huu”. Sabrina alipoambiwa hivyo, akasema “Sawa, ukionana nae mwambie namtafuta” Samsoni akajibu “sawa” kisha simu ikakatwa. Baada ya hapo rafiki yangu alirudisha simu kwenye chaji huku akisema “Haya si umesikia? Eti anakutafuta. Sauti yake tu inaonekana mmezinguana nyie. Huu ugomvi siingilii” mimi nikacheka kwanza kidogo alafu nikasema “nitamcheki baadae”.

Baada ya hapo Samsoni aliniaga kuwa anatoka kidogo hivyo mimi nilibaki mule ndani nikiwa nimetulia tu ila kichwani kwangu mawazo ni mengi sana. Wakati akiondoka alisema pia “Alafu nilipokua anaangalia mpira, Tino alinipigia akaniambia amekutafuta hakupati hivyo umpigie” mimi nikaitikia “Ah sawa”.

Nilipokua pekeangu mule ndani, Mawazo yalinituma ninyanyue godolo tunalolatila maana Samsoni alikua anatabia ya kuweka pesa huko. Nilipofanya hivyo, nilizikuata pesa zake nyingi kiasi na nikazichukua maana niliona kama zinaweza nisaidia katika hali niliokuanayo kwenye wakati huo. Nilikua ni kama na muibia Rafiki yangu kabisa ili tu niweze kukimbia tatizo linalonipa Mawazo.


Mawazo niliokuanayo siku hiyo yalikua yamesababishwa na matokeo ya mimi kuanza kuzifungua kurasa za mapenzi katika maisha yangu. Nakumbuka miaka michache iliopita kambla ya siku hiyo nilikua nasoma sekondari kidato cha tatu na nilikua nasoma shule za kutokea nyumbani. 

Tangu nilipoanza sekondari nilikua sijawahi jihusisha au kuwaza kuwa na mpenzi shuleni japo nilikua natamani. Hii ilikua ni kutokana na mambo mengi ikiwemo sheria za shule zilizokua zikikumbushwa kila siku na walimu. Na pia nilikua nawaogopa wazazi wangu kuniona nimejiingiza kwenye maswala ya mapenzi. Mbali na hayo, nilikua naogopa sana jinsia tofauti. Kuwasogelea na kuongea nao kulikua ni mthihani mkubwa sana kwangu kipindi hicho, hasa akiwa ananivutia.

Kwenye mambo ya kufanya vizuri shuleni kwa bahati mbaya nilikua siko sana huko. Uwezo wangu katika madaftari na mithihani ulikua wa kawaida sana. Nakumbuka darasani nilikua nakaa viti vya nyuma sana. Huko nyuma nilikua nakaa na rafiki zangu wawili ambao mmoja wapo ndio huyo  anaitwa Samsoni, alafu kuna mwingine alikua anaitwa Tino. Kwaiyo tulikua kama tuna kikundi cha watu watatu nyuma ya Darasa. Darasa letu lilikua lina viti vinavyo ruhusu kukaa wawili na kiti nilichokua na kaa mimi, tulikua tunakaa mimi na Samsoni ila mwalimu akitoka tu, Tino alikua anakuja kwenye kiti kile, tunajibana watatu, tunapiga stori. Tino alikua anakaa kiti cha pembeni yetu ambacho kilikua karibu sana na sisi.

Tino alikua ni mwenzetu ila mambo yake yalikua mengi mno. Alikua ni msumbufu sana kiasi kwamba kila mtu alikua anamjua kwa usumbufu wake hapo shuleni. Watu walianza kumjua baada ya kuletwa na mzazi wake shuleni na kupigwa kutokana na kutolala kwao pamoja na kutokuja shule kwa siku 5 mfululizo katika kidato cha kwanza.

Tulikua tuna shirikiana sana Tino lakini usumbufu wangu haukufikia usumbufu wa Tino. Samsoni nae  alikua kama mimi tu, hakumfikia usumbufu Tino hata kidogo. Ila katika mambo ya kwenye vitabu, wote tulikua hatufanyi vizuri sana japo hatui wamwisho Darasani. 

Kuna siku asubuhi tulikua watatu Darasani kule nyuma ya Darasa tunapiga stori kwa kujiachia lakini ghafla akaingia mwalimu. Alivyoingia tu, tukafunga midomo alafu kila mtu kati yetu alikaa vizuri anapokaaga kisha watu wote darasani tukasimama kumsalimia Mwalimu. Baada ya kumsalimia, akaturuhusu tukae alafu nikakuta tu anasema “Nyie watatu uko nyuma hebu simameni”. Mh alivyosema hivyo nikawa nawaza “Anaongelea mimi na rafiki zangu au? Mbona anaangalia huku nyuma?” wakati najiuliza nikakuta mwalimu anasema tena “Nyie muliokua mnapiga kelele mpaka darasa zima mnasikika nyie huko nyuma simameni kabla sijawafuata.” Basi mimi nikaona huenda anatuongelea sisi, nikasimama na bada ya mimi kusimama, nikakuta na Rafiki zangu wawili wanasimama.


Baada ya hapo mwalimu akaanza kufoka “Hivi nyie mna matatizo gani? Inamana hapa shuleni mmekuja kupiga makelele au?” baada ya kusema hayo akaninyoshea mkono na kusema “Wewe hapo wewe inaonekana msumbufu maana hata Nywele haujanyoa. Hizo nywele ni siku ya ngapi nakwambia sitaki kuziona? Hebu sogea hapa mbele” mimi nikiwa mnyonge sana nilisogea taratibu pale mbele ya Darasa. Mwalimu aliniuliza “Unataka ni kupige ndio uanze unijibu?” mimi nikiwa naogopa sana nikamjibu “Hapana, samahani mwalimu nilitaka kunyoa jana ila umeme walikata”. Baada ya kumjibu mwalimu alifikilia alafu akasema “Kesho nisione hizo nywele, sawa!?” nikamjibu “Sawa” alafu nikakuta ananiambia “Na kule nyuma unakokaa, uhame. Kabebe madaftari yako kule nyuma uyalete hapa mbele kwenye hiki kiti ambacho hakina mtu”.

Baada ya mwalimu kusema hivyo nilishtuka maana nilikua sijazoea kukaa viti vya mbele ya Darasa, nikamwambia “Mwalimu hapo wanakaa watu wawili, itakua wameitwa nje”. Mwalimu akasema “Hatakama wakija hao wanao kaa hapa, waambie mimi ndio nimekuweka hapa. Kwanzia leo utakua unakaa hapa mbele. Nawakija hao, waambie wachukue kiti kingine wakae sehemu nyingine ila sio hapa”. Dah nilikua mnyonge sana siku hiyo, nikachukua vitu vyangu nyuma ya Darasa na kuhamia mbele ya darasa huku mwalimu akiniangalia.


Baada ya kukaa mbele mwalimu alianza kufundisha somo lake maana ndio ulikua muda wake huo. Mimi pele mbele nilikua sina amani kabisa maana sijazoea kukaa hapo alafu mbali na hilo, Daftari la mwalimu huyo nilikua sina. Lakini mwalimu alipoanza kufundisha nilichukua kidaftari flani cha ajabu, nikakiweka pale mbele ili kuzuga.

Nakumbuka baada ya kama dakika 10 hivi Mwalimu alipoanza kufundisha, alikuja mwalimu Mkuu akiwa ameambatana na wanafunzi kama watano hivi na mwanafunzi wa kike alikua mmoja. Darasa zima tulijikuta tunavutiwa kumuangalia yule mwanafuzi wa kike. Mwalimu mkuu alianza mazungumzo na Mwalimu aliekua Darasani na mazungumzo yao yalikua ni kwamba hao wanafunzi watano ni wageni na kwanzia siku hiyo watakua wanasoma humo Darasani. Walimu walipomaliza kuzungumza, wale wanafunzi wakaingia ndani ya Darasa alafu yule Mwalimu aliekua Darasani akawaambia watafute nafasi za kukaa mule Darasani. Kabla hata hawajapiga hatua sana, nikakuta mwalimu ghafla anamwambia yule mwanafuzi mgeni wa kike “Wewe usiende huko. Kaa hapa na huyu”. Mimi moyo ulishtuka sana maana alikua anamuelekeza yule Mwanafunzi wa kike akae na mimi kwenye kiti kimoja. Kiukweli mimi nilikua naogopa kukaa na jinsia tofauti hasa wakiwa wazuri ndio napoteza uhuru kabisa yani. Na Mwalimu alikua anamzingatia yule mwanafuzi wa kike kwa kiasi flani, kama ni ndugu yake hivi.

Nakumbuka yule mwanafunzi alikaa na mimi pele huku akiwa na viaibu aibu vya ugeni alafu na mimi wakati huo nina viaibu vya kumuogopa.  Tukiwa tumekaa  pale mwalimu aliwauliza jina wageni wote waliokuja na nilisikia yule Mwanafunzi wa kike akijitambulisha kuwa anaitwa Zuwena.  Basi baada ya hapo mwalimu aliendelea kufundisha na mimi nikawa kama namsikiliza  hivi ingawa akili yangu ilikua inahama. Yani nikua nikitupa jicho langu mara moja moja kwa yule Mwanafuzi wa kike kumuangalia jinsi alivyo. Japo nilikua naogopa, ila alikua anavutia sana kumuangali alafu alikua msafi sana. Kuna muda nilimtupia macho tukagongananae alafu akaona viaibu. Mimi nilipogongananae macho nilishtuka na nikaingiwa na woga zaidi ila woga ulipungua nipowaza “ Inamaana na yeye ananiogopa huyu. Dah ila mzuri mpaka raha. Ingawa naogopa ila hapa nijitahidi niwe hata rafiki yake tu. Sina hata rafiki wakike ujue”. Nakumbuka niliwaza mambo mengi sana kuhusu huyo mgeni bila kujua kuwa ndio namuingiza moyoni hivyo mtoto wa watu.

Baadae, mwisho wa kipindi cha mwalimu aliekua akifundisha ulifika na mwalimu alituachia maswali ya kufanya nyumbani tuyaandike alafu akasema anaondoka. Lakini kabla hajaondoka akasema “Nyie muliofika leo hakikisheni munaazima madaftari Kwa wenyeji ili muandike vitu vyote vya nyuma. Wewe Zuwena utachukua Daftari kwa huyo uliekaanae hapo, sawa!?”. Nikiwa pembeni ya Zuwena nikamsikia Zuwena akiitikia “Sawa” huku nikiwa nimeshtuka mno maana Daftari wanalo liongelea sina. Kichwani nikaanza kuwaza “Hapa mbona kama naenda kuumbuka kwa mgeni sasa. Huyu mwalimu na huyu mgeni wanajua Daftari ni hili lililopo Mezani lakini ukweli ni kwamba sina Daftari. Nikijieleza kwa huyu mgeni kuwa sina daftari, nitaonekana mjinga sana kwake na naweza shindwa kuwa rafiki yake. Dah tena anaonekana anaakili sana huyu, ntaumbuka leo.”



INAENDELEA…

UTAMU WA JUMLA 10 (Simulizi ya Maandishi)

Uvumilivu ukanishinda, nikaona amelala ameniachia mgongo nikatoa mkono wangu wa kushoto nje ya shuka langu taratibu nikawa kama nampapasa sehemu zake za juu kidogo ya magoti hivi. nikakuta kaganda tu na anakautulivu flani kama anakitaka ninachokiwaza. Mimi nikaendelea kumpapasa taratibu huku nalitoa shuka lake kidogo kidogo.

Wakati nafanya hivyo nikakuta ghafla ananigeukia na tukaangaliana uso kwa uso. Kumbe na yeye alikua anataka. Baada ya kunigeukia tukajikuta tu tumeanza kamatana ulimi na mikono yetu imeyatupa mashuka pembeni nakuanza kuvutana. Tulizianzisha vurugu pale kitandani mimi na Salma kiasikwamba Salma alikua anashindwa kupumua vizuri. Nilipitisha mkono wangu sehemu zote nilizokua natamani kuzishika kwenye gari yangu mpya hiyo. Ngozi ya viti ilikua laini na nikiwanaishika nahisi kuchanganyikiwa zaidi kwenye vurugu hizo. Alikua anaumbo zuri sana na nilipomkamatia panapotakiwa kuna muda nikawa naona kabisa kwa raha ninayoipata siwezi kumuacha nimwage maji nje. Pamoja na kwamba alikua anafanya kazi ya kuuza mwili wake lakini alikua hajachoka bado. Kama kuna mtu alikua dirishani muda huo basi angekua anasikia sauti za Salma akilia “Ohooh…. uwii… aaa.. aiissssssiiii… Oooohhh.. anha ooisshii” na kutaja jina langu kutokana na makofi ya mkono wa tatu niliokua nikimpa “Pah pah pah pah” katika mikunjo mbali mbali ya vurugu.

Nilitamani nimwage maji nje lakini nilishindwa kabisa, nilijikuta namaliza mchezo kwa kuguna na kutaja jina lake tu “Mhh mhh Sa… salma… Mhh” huku nikiendelea kumchapa makofi ya nguvu “Pah pah pah” kwa kasi ya ajabu na kuifanya mizigo yake iwe inacheza kama maji yanayotikisika kwenye rambo. Baada ya kumaliza mchezo tukaanza kuongea mambo ya mahusiano tena kama kawaida. Nilimwambia nampenda sana nae aliniambia ananipenda pia hatamani niondoke maishani mwake wala nimtoe maishani mwangu. Nilimuahidi kuwa haitatokea ila asirudie ile tabia yake mbaya hata iweje na yeye akasema haitakuja kutokea.

Asubui ilifika nikajiandaa kwenda kwenye mafunzo ila kabla sijaenda nikamuachia kiasi kidogo cha pesa ili anunue chakula ale alafu nikawapigia wazazi ili watume ile hela. Wakaniambia “Subiri kidogo tunatuma” lakini nikaona wanachelewa, nikaweka simu mfukoni nikaanza safari ya kwenda kwenye mafunzo. Siku hiyo ilikua ni jumamosi ila huwa tunaenda kwenye mafunzo. Nilipokua njiani nilikua na mawazo kidogo na nilikua nawaza “Duh inamaana mimi ndio nimeisha oa ivi au?… Kuishi na mwanamke ambae unamahusiano nae ya kimapenzi ni sawa na kuoa tu japo sio rasmi. Ivi nitaweza kuishi nae kweli? Alafu mwanamke ananguvu huyu maana nilisema sitakuja kupenda sana kama hivi lakini nimejikuta nampenda zaidi ya sana, nilikuwa nafikilia kuwa nikipata kazi nitakua na wanawake wengi lakini yeye saivi ni mmoja ila nikikosana nae tu hata mafunzo yatakayo nifanya niipate hiyo kazi nayaona hayana maana. Na sijui nitafanyaje nikikuta kaondoka na vitu vyote mule ndani maana kuna wanawake huwa wanafanya hivi ujue?… Ah wakati namkaribisha Salma sikuwaza kuwa litakua jambo kubwa hivi ila kwakua nampenda, acha tu nione itakuaje ila akiwa ni mwanamke alietulia kweli, simuachi maana nampenda. Alafu si nikimaliza mafunzo nitapata kazi? Ah kumbe haina haja ya kuwaza sana kuhusu maisha maana maisha yetu mimi na Salma nitayaendesha vizuri tu”.

Baada ya mawazo hayo nikaanza tena kuwaza “Ila mimi kuoa naona kama nimewahi hivi… Huyu salma japo nampenda ila baada ya kupata kazi tu nitamuacha. Kwanza nahisi nitakua nimeisha mchoka maana mapenzi kuna muda huwa yanaisha. Yeye mwenyewe sidhani kama atakua na hamu namimi… Kwamba katika wanaume wote, mimi tu ndio nimeuteka moyo wake kwa uzuri ule? Mh sijui… Au nitaangalia cha kufanya mbele kwa mbele”. Nikaendelea na safari mpaka nikafika sehemu ya mafunzo. Lakini sehemu hiyo nilikuta imefungwa na kunawatu wengi tu wapo nje wamezagaa na wengi wao wameshika vichwa wanalia. Nikasogea kwa watu na kuwauliza kinachoendelea hapo nikakuta wanasema kumbe hayo mambo yaliokua yanaendelea hapo muda wote ni utapeli. Eh nilishtuka nikawa nataka waniambie vizuri kivipi lakini nao wanasema hawaelewi ila tu kinachoendelea hapo ni kwamba watu waliokua wakiendesha jambo hilo kwa sasa wameisha kimbia mji na hela za watu wote walio lipia na hata kampuni lao halitambuliki kiselikari.

Mh kiukweli nilichanganyikiwa kweli kusikia hivyo. Nakumbuka tulikaa pale kwenye eneo la tukio tukiwa hatuelewi kinachoendelea na nilikua na mawazo sana muda huo. Kichwani nilikua nawaza “Inamaana nimepoteza muda kusubilia kitu ambacho hakipo? Mkosi gani huu? Nitawaambia nini wazazi wangu kuhusu jambo hili? Nitaishije na Salma bila kuwa na ajira? Maisha yangu yatakuaje?” nilikua sipati jibu kabisa na kulikua hakuna dalili nzuri mbele yangu. Niliamua kuanza safari ya kurudi kwenye chumba nilichopanga na wakati niponjiani mawazo hayakunipa muda wa kukiacha kichwa kipumzike, nikaanza kuwaza “Hii ni ndoto au?… Au huyu Salma amenipa mkosi? Dah Mbona sielewi”. Mara grafla ukaingia ujumbe kwenye simu yangu na nilipouangalia nikakuta umetoka kwa baba. Moyo ulidunda kwa hofu nikizani huenda baba amepata taarifa tayari ya kinachoendelea huku. Ila nilipoufungua na kusoma ujumbe huo nikakuta kumbe baba anataka nimtumie namba za akaunti ambayo nitapokelea hela tu. Mh mimi niliposoma ujumbe huo nikapumua kidogo na baada ya hapo nikaanza kuwaza “Ivi sasa hizi hela nazipeleka wapi?….Au nimwambie asitume alafu nimwambie kilichotokea?… Hapana, kwasasa siwezi hata kumwambia, ngoja nimtumie namba yangu ya benki ili atume hela humo”. Basi nikafanya hivyo na kabla sijafika nyumbani hela ziliingia alafu nikamshukuru. Ila mawazo hayakuisha kichwani na kiukweli dunia nilikua naiona mbaya sana muda huo…

INAENDELEA….

Utataka Tena Au (Simulizi ya Maandishi)

Nilihamia Dar es Salaam kutafuta maisha, nikitegemea msaada wa kaka yangu ambaye hakuwa ameoa. Nilipokaa kwake, sikutilia sana mkazo kujenga maisha yangu. Badala yake, niliweka nguvu kwenye starehe za usiku, yani nikifanya kumbi za burudani kuwa sehemu yangu ya nisioweza kukoswa.

Huko kwenye kumbi, nilikutana na Merry. Mwanamke wa kuvutia, mwenye mwili wa mzuri sana. Uhusiano wetu ulianza kama biashara. Yani nilimpa pesa, naye alinipa penzi. Lakini kadri tulivyozidi kuzoeana, pesa zikawa si muhimu tena. Tulianza kufurahia penzi letu bila malipo, lakini tulikua tunakutana tu katika kumbi za starehe. Hakukuwa na mipango ya zaidi ya starehe.

Baada ya muda, niliona kuwa maisha yangu hayakuwa na mwelekeo ninao uelewa. Nilirudi kijijini kujaribu kujijenga upya. Nilijihusisha na kilimo na nikapata pesa za kutosha. Nikiwa kijijini, nilisikia kwamba kaka yangu ameoa na sasa anaishi na mkewe. Habari hizo zilinipa furaha na msukumo wa kurudi mjini ili kuanza maisha yangu binafsi.

Nilipofika mjini, nilipanga nyumba yangu na kuanza kujitegemea. Kabla ya kumtembelea kaka, niliendelea na starehe zangu maana ndio kitu nilichukua nakupenda sana hapo mjini. Nakumbuka nilipofika tu, Nikawasiliana na Merry ili tukutane kwe starehe tufanye mambo yetu. Lakini Merry aliniambia kuwa ameacha mambo ya zamani na hafiki tena kwenye kumbi za starehe kwakua ameolewa. Nilisikitika, lakini nikajitahidi sana mkushawi ili nipate tu penzi lake mara moja au turudi kwenye penzi letu kabisa. Baada ya mazungumzo marefu, alikubali na akasema atanifuata nyumbani kwangu tu na sio kwenye kumbi za starare tena.
Nilimuelekeza sehemu ambayo anatakiwa aje alafu alipokuaja, nikachukua hapo na kumpeleka ndani kwangu. Alikua ameva nguo nyeusi alafu fupi kiasi cha kuonesha sehemu za juu kidogo ya miguu. Muonekano wake ulikua unavutia sana na mapigo yangu ya moyo yalikua yanaongezeka kwa tamaa tulipoingia ndani. Ni kawaida yake kunichemsha Damu kiivyo maana ni mwanamke mwenye umbo zuri la kuvutia Kila mwanaume.

Nakumbuka tulikaa dakika chache tukiongea mule ndani mwangu kisha tukaanza kufanya kilichotukutanisha. Sauti za Merry za kuimba “Aahh mmh aissh aishii” ndizo zilitawala humo ndani huku tukiwa tunacheza hiyo nyimbo kwa kunesanesa.
Alilala na mimi usiku mzima ili kunifurahisha. Raha za kucheza mziki zilizidi mpaka alipokua anaondoka asubuhi, nilimshawishi aje tena akipata muda na akakubari.

Uhusiano wetu wa kimapenzi uliendelea kwa siku kadhaa tukiwa tunafurahia sana. Lakini moja, niliona ni vyema kumtembelea kaka yangu baada ya kukaa bila kuonana toka niingie hapo mjini. Nilipofika kwake, nilipigwa na mshangao wa ghafla kwasababu nilimkuta Merry akiwa ndiye mke wa kaka yangu!

Macho yetu yalikutana kwa sekunde chache tukaona aibu, lakini tuliweka sura za kutojali kama hatujawahi kuonana. Aibu ilitawala mioyo yetu, lakini hakuna aliyeweza kusema neno. Kila mmoja wetu alijua kwamba siri hiyo haikustahili kufichuliwa. Tangu siku hiyo, ni kama tulikubaliana kuwa kimya na kuacha kila kitu kilichotokea nyuma yetu.
Kuna muda nilikua nawaza “Huyu mke wa kaka huenda sio mtu mzuri… Alikua anawezaje kulala na mimi usiku wakati kaolewa?” Lakini nilikua nikifikilia tena kwa Mimi ndio niliepambana sana kumshawishi aje kunipa penzi wakati ananiambia ameolewa, naamua kuendelea kuwa kimya tu.
Mwisho nilianza maisha mapya, nikijifunza kuwa baadhi ya siri ni lazima zibaki kuwa siri, hasa zinapogusa heshima na furaha ya wengine.

MWISHO

UTAMU WA JUMLA 09 (Simulizi ya Maandishi)





Samahani kama unanipenda kweli, najua utakua umeumia kujua mambo yangu ila naomba utambue kuwa na mimi nakupenda sana lakini maisha yangu mimi siyaelewi. Natamani kutoka kwenye maisha haya na kuwa na mwanaume mmoja maishani atakae nielewa lakini kila nikijaribu, vitu vinaingilia kati, nadondoka tena kwenye kazi ya kujiuza. Nikifanikiwa kutoka kwenye maisha haya mabaya, sitatamani kurudi tena. Natamani kuitwa mke, natamani kuheshimiwa kama watu wengine na natamani nifute vitu vyote vibaya nilivyowahi fanya lakini nashindwa.” 

Basi mimi baada ya kusikia hivyo nikajikuta naanza tu kumuonea huluma Salma. Machozi yalikua yakimtililika na mimi kumuona dada mzuri kama yule akilia mbele yangu bila kuchukua hatua ilikua ningumu sana. Nilimfuata pale alipokua akilia, nikamkumbatia nikamwambia “Nyamaza basi… Salma nyamaza basi… Nimekuelewa salma nyamaza basi nikwambie kitu”. Nikamkalisha kitandani kwangu tukatulia kama dakika 10 hivi kumuweka sawa maana alikua anadondosha machozi. Baada ya kunyamaza nikamwambia “Ivi kwamfano nikikupa hiyo hela utaenda kuifanyia nini? alafu nimeona wameondoka mpaka na kitanda, unasehemu hata ya kulala leo wewe?” akatulia kidogo alafu akakataa kwa kutikisa kichwa.


Nikamwambia “Kwaiyo hata nikikupa tu hiyo hela bado utaendelea kujiuza?” Salma akawa anajiminyaminya tu vidole vya mikono huku anaangalia chini.  Nikakaa kama dakika moja hivi nikifikilia jinsi ya kumsaidia alafu bila kufikilia mbali nikamwambia “Fanya hivi… nenda kachukue vitu vyako vilivyobaki kule ulete humu tukae”. Akashtuka kidogo alafu akawa ananiangalia usoni kama haamini nilichokisema. Mimi nikamwambia “Mimi nikotayari tukae wote humu… Au unampango mwingine unaokufaa mbali na huo?” Akauliza “Yani inamaana mimi na wewe tuwe tunakaa humu?” nikamwambia “Ndio kwani wewe unaonaje?” Nikakuta ananikumbatia alafu alivyonikumbatia machozi yake yalikua yananidondokea shingoni huku nikimsikia akinishukuru. Ila nilimwambia kuwa hatutaishi humo kama wapenzi, tuwe ni kama marafiki tu mpaka atakapoelewa maisha yake na asirudi kwenye ile kazi yake ya kujiuza.


Basi baada ya dakika chache alihamishia vitu kwangu ili tuanze kuishi mule na alikua hana vitu vingi. Alikua na nguo za kuvaa chache, vitu vichache vinavyohusika na chakula, shuka pamoja na vitu vya urembo. Jioni ilifika na ilitukuta tukiwa pamoja na salma. Nikanunua chakula tukala na baada ya kula nikakumbuka kuwapigia simu wazazi kuhusu hela inayohitajika kwenye mafunzo ili kupata kazi. Niliwapigia nikawaelekeza wakawa wagumu kunielewa lakini mwishoni wakakubali wakaniambia “Sawa ila kutuma hiyo hela sasaivi haitawezekana, utatumiwa kesho asubui ila hakikisha unafanya vizuri huko maana tunatupa hizi hela kwaajili ya maisha yako”. Mimi nikawambia “Sawa” nikawaelekeza na jinsi ya kutuma pesa ili inifikie mimi alafu ndipo nikalipie. Baada ya hapo tukaendelea kupiga stori na Salma mule kwenye chumba changu. Tulikua tumekula na tumeshiba hivyo stori zilikua nyingi sana humu ndani. Ila stori tulizokua tunapiga zilikua haihusiani na mapenzi kabisa maana tulikubaliana hatutakua wapenzi humo ndani.


Nakumbuka ulifika muda wa kulala na kwakua kitanda kilikua kimoja nilimwambia alale kwenye kitanda mimi nilale chini. Akakubali kulala kitandani na mimi nikalala chini lakini nilivyokua nalala tu nikakuta mvua nje imeanza. Kibaridi kilianza kunipiga pale chini nikawa najigeuza geuza nipate hata afazari maana hata usingizi ulikua unagoma kuja. Mara ghafla nikakuta Salma kaitajina langu kwa sauti ya chini kiasi. Basi na mimi kwakua nilikua macho, nikaitikia “Naam” akasema “Kunabaridi leo… hujiskiii baridi hapo chini?” nikawa nataka kukataa kuwa sijiskii baridi ila nikaona bora nikubari tu “Dah kunabaridi kweli” akaniambia “Njoo tu tulale wote tu hapa maana ukilala hapo mpaka kukuche utaumwa”. Basi mimi nikafikilia nikaona ni kweli nitaumwa maana hata usingizi uligoma pale. Nikapanda kitandani na shuka langu nikalala yeye akiwa upande wangu wa kushoto.

Tulivyolala kitandani wote bado usingizi ulikua hauji. Nilianza kujisogeza kwake kidogo maana ndiko kulikua kuna joto la kuvutia. Kila mtu alikua na shuka lake lakini mimi nilikua najikuta tu navutiwa kujibana kwake maana kulikua na joto kidogo. Na yeye pia nilianza kumuona kama ana sogea kwangu hivi. Mawazo yakaanza kunihama nikajikuta natamani nianze kumshika yule dada. Nilikua naogopa kumuanza maana mimi ndie nilikua nikisisitiza kuwa humo ndani tuishi bila kuwa wapenzi. Hapo kitandani mkono watatu ulikua umeisha amka na najigeuza mara kwa mara maana hali yangu ilikua mbaya. Uvumilivu ukanishinda, nikaona amelala ameniachia mgongo nikatoa mkono wangu wa kushoto nje ya shuka langu taratibu nikawa kama nampapasa sehemu zake za juu kidogo ya magoti hivi. nikakuta kaganda tu na anakautulivu flani kama anakitaka ninachokiwaza. Mimi nikaendelea kumpapasa taratibu huku nalitoa shuka lake kidogo kidogo.




INAENDELEA….