Tag Archives: simu

Katika Matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi (Unaweza juta!)

Kama ni mtumiaji wa simu za smartphone unatakiwa kuwa makini sana katika matumizi yako ya smartphone maana ukiitumia smartphone yako vibaya unaweza kujikuta jela au unaweza kuwa kwenye wakati mgumu kwa kupoteza vitu vyako vya msingi na heshima kwa jamii. Leo nimekuandalia baadhi ya vitu ambavyo unapaswa kuvizingalia katika kutumia smartphone yako. Tutazungumzia vitu vichacheche tu, vingine tutaangalia katika makala nyingine. Lakini Kabla ya yote ningependa kukushukuru Kwa kufuatilia “The Bestgalaxy” na nakusihi usiache kufuatilia ili kujifunza vitu vingi zaidi.

Jinsi ya kupata mkopo kwenye simu GUSA HAPA>>>>

Bila kupoteza muda hebu tuangalie ni vitu gani usifanye katika matumizi ya simu yako…

1. Usijichukue picha za utupu na kutunza kwenye simu yako.

Kama ni mtu unaependelea kujichukua picha za utupu kwa makusudi na kuzitunza basi hakikisha unajiweka tayari kiakili kuwa hata zikivuja hazita kushtua wala kukuumiza. Kumekua na uvujaji mkubwa wa picha/video za utupu na ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya watu wenye picha au video hizo hawajui ni kwanini picha hizo zimetoka nje ya simu zao. Kitu muhimu kukijua ni kwamba si vizuri kuweka picha au video hizo kwenye simu maana kunavitu vingi sana ambavyo vinaweza pelekea kuvuja kwa vitu vyako.

2. Usiingize app nje playstore hovyo hovyo.

Wengi tumezoea kuingiza app tunazozipenda kupitia playstore lakini kuna baadhi huwa tunaingiza tu yaani mtu katuma kwenye group la WhatsApp, basi unajaribu kuiingiza au umesearch Google bila kuangalia ata site inaaminika vipi, unaiingiza kwenye simu yako.
Kitu muhimu cha kujua ni kwamba kuna app ambazo ukiingiza kwenye simu yako tu huwa zinabeba taarifa zako kwenye simu na kuzituma kwa huyo mtaka taharifa za watu tena kwa kutumia bando lako bila wewe kujua. App hizi hupatikana nje ya Playstore hivyo basi katika kuingiza app nje ya Playstore hakikisha sehemu unayotoa app unaiamini na inaaminika pia.

Jinsi ya kufanya simu ijinunulie bando la internet (usichome pesa zako kununua bando) GUSA HAPA>>>

3. Usisambaze taarifa au link usizozijua kiundani.

Kama ni mtumiaji mzuri wa simu na mitandao nadhani umewahi fanya kitendo cha kusambaza link au ujumbe flani ili upata kituflani lakini mwisho ukagundua ni uongo. Sasa unadhani uliowasambazia walikuchukuliaje? na ulichokisambaza kingekua kinahusisha utapeli, unadhani tapeli wa hao uliowasambazia angekua ni nani kama si wewe?
Usipendelee kusambaza ujumbe au tahalifa usizo na uhakikanazo na wala usiwe na tamaa na vitu vya bure mitandaoni, utaibiwa alafu unaonekana wewe ndio mwizi.

4. Usisahau taarifa za Email yako wala kuzigawa.


Wewe ni mmoja kati ya watu wasio jua Email zao au password zakuingilia katika email zao?
Naweza kusema, kwasasa Email ni kitu cha msingi kuliko simu unayotumia. Email yako ni utambulisho wako katika sehemu mbalimbali pia email husaidia kupata vitu vyako vya msingi vilivyopo kwenye simu endapo simu yako itaibiwa au kuhalibika ghafla. Kwakutumia email yako utaweza itafuta simu yako ikipotea na kutambua mahali ilipo.
Email hurahisisha sana mambo maana unaweza ukawa umeibiwa simu au imezimwa ghafla lakini ukawa unavitu vyote muhimu kama picha zako,video na majina ya simu kwa kushika Email yako na password yake kichwani mwako (Kama uliseti hivyo).

Tambua kuwa ni muhimu kujua Email yako na password yake na kamwe usimpatie mtu password maana utakua umempa tahalifa zako na akiwa mjanja atakupekua mpaka vitu unavyo search Google na kujua uwezo wako unaishia wapi.

Download na kuangalia movie zote bure kwenye simu GUSA HAPA>>>

Simu ikiingia maji unatakiwa kufanya nini?

Simu kuingia maji Ni moja ya mambo ambayo hutokea katika shughuli zetu za Kila siku. Jambo hili huogopesha sana maana husababisha mpaka baadhi ya simu kupata matazizo au kutowaka kabisa. Hatuwezi zuia simu zetu kuingia katika maji maana hutokea Kama ajali, lakini tunaweza zuia simu zibaki salama yaani zisiwe na matatizo yoyote baada ya kuingia kwenye maji.Kama simu yako imeingia maji na unahitaji iwesalama basi fanya mambo yafuatayo;

Jinsi ya kupata mkopo kwenye simu GUSA HAPA>>>>

1. Zima simu

Baada ya simu kuingia maji unatakiwa kuhakikisha aiendelei kuwaka. Izime bila kupoteza muda maana ikiendelea kuwaka maji yalioingia yatasababisha vitu vya ndani ya simu hiyo kuharibika.


2. Chomoa betri



Kama simu yako inachomoka betri hakikisha unachomoa betri na kuliweka pembeni ya simu ila kama simu yako si ya kuchomoka betri, Fanya kuichoma line au memory Kisha kimbia moja kwa moja kwa fundi ili aifungue na kutenganisha vitu ili ikauke Kwa uhakika.

Download na kuangalia movie zote bure kwenye simu GUSA HAPA>>>


3. Iachewazi katika sehemu kavu

Chomoa line ya simu,Memoy na ikiwezekana nenda kwa fundi aliopo karibu na wewe ili aifungue ibaki wazi na kukauka kirahisi. Baada ya kuiweka wazi unatakiwa kuiweka sehemu kavu kwa muda mrefu mpaka itakapokauka kabisa.

Zingatiausijaribu kuiwasha simu kwa kuijaribu kabla ya kufuata hatua hizi!

Ukweli kuhusu mcheleWatu wengi huweka simu zao katika mchele wakiamini simu zao zitapona lakini kitu cha muhimu kukijua ni kwamba, mchele ni unaweza kukausha maji lakini Kuna uwekano wa asilimia 4 hadi 1 ya maji yalioingia kubaki ndani ya simu na kuleta matatizo ambayo yatakuja kuonekana mbeleni. hivyo kabala ya kuweka huko unatakiwa kufuata hatua hizi pia.

Mtu akiku “Block” WhatsApp unaweza fanya hivi kuchati nae GUSA HAPA>>>

Kama itakua si maji ila vimiminika vinginekama simu itangia katika pombe,Maji ya chumvi na vimiminika vingine, utatakiwa kuzima na kutoa betri kisha Kifungua nakuisafisha au kuifuta na kitambaa maana usipofanya hivyo baadhi ya vimiminika vikikaukia ndani ya simu, huozesha baadhi ya vitu vilivyo ndani ya simu (ukishindwa ni bora upeleke kwa fundi).

Nyongeza: Kuna baadhi ya simu zimeundwa kutoathiliwa na maji kabisa(Water proof). Yani hata ikidumbukia kwenye maji huwa maji hayaingii ndani ya simu. Lakini pia kunasimu ambazo zimeundwa kuzuia maji Kwa muda flani au maji ya joto flani(water resistant) lakini hazuii Kwa asilimia 100%. Simu hizi unaweza zidumbukiza kwenye maji dakika Moja au mbili na kuzitoa bila tatizo. Mara nyingi masharti yake ni maji yasiwe joto na usizidishe muda.

Endelea kuwa nasi kujifunza vitu vingi zaidi.

Jinsi ya kuangalia mpira live kwenye simu (Bure)

Kama ni mpenzi wa muda wa kuangalia mpira wa miguu wa nje ya nchi, nadhani umeshawahi kosa kuangalia  mechi ulioipania kwasababu mbalimbali ikiwemo kuwa mbali na Tv. Teknolojia inazidi kukua kila siku na kuturahisishia mambo. Sasa unaweza angalia mechi Kali za mpira wa miguu kupitia simu yako mubashara(Live) ukiwa popote. hapa tutakujuza jinsi ya kuangalia mpira wa nje karibu mechi zote kwenye simu yako BURE.

Simu ikiingia maji unatakiwa kufanya nini? GUSA HAPA>>>

Ikiwa unahitaji kuangalia mpira live kwenye simu yako, utahitajika kuwa na app maalumu kwaajili ya kuangalizia mpira. App hizi zipo nyingi sana katika playstore(Android) lakini mimi nakushauri uchukue app nyepesi na isiokula sana Mbs iitwayo Live Football Tv.

App ya Live Football Tv ni app ya kuangalia mpira live kwenye simu yako. Mpaka Sasa inatumiwa na zaidi ya watu Milioni ulimwenguni na wanaisifu kwa kuonesha mipira mingi bila matatizo. Mbali na kukuonesha mechi live(mubashara), huwa inakupa matokeo na video za matukio muhimu ya mechi zilizomalizika kwaiyo Kama haukua na bando la kutosha kuangalia mpira mzima, unaweza angalia video ya goli lilivyofungwa tu. Pia inakupa nafasi ya kuangalia vipindi vingine vya kimichezo bure toka Ptv sports. 

App hii ya kuangalia mpira live haipatikani Playstore kwasasa ila unaweza kitafuta Google na kuipakua. Pia Unaweza ipakua kirahisi kwa kugusa hapa>>> INSTALL. Na baada ya kuipakua, hauitajiki kujisajili au kufanya Jambo lolote la kujiunga ili kuitumia. Ni kuifungua na kuinjoi…

Fahamu kuwa: App nyingi zinazowezesha kuangalia mpira bure huendelewa Playstore kutokana na Kuvunja sheria za Playstore. Ikiwa app nilioitaja nayo itaondelewa basi unaweza ipakua app nyingine nje ya Playstore Kwa kugusa HAPA>>>

Jinsi ya kuangalia mechi za Tanzania kwenye simu GUSA HAPA>>>

Je, ni Mbs ngapi zinahitajika kuangalia mpira mzima(Dk90) kwenye simu?

Hili ni swali ambalo wengi hujiuliza, wanapohitaji kuanza kuangalia mpira kupitia simu. Ukweli ni kwamba, kadri video inavyokua na muonekao mzuri ndivyo Mbs huwa zinalika nyingi. Itakua ni vizuri zaidi Kama hautakua na chini ya Mb900 ili kutokua na wasiwasi wa bando kuisha.

Magemu ya Mpira ya kucheza kwenye simu GUSA HAPA>>>

{“remix_data”:[],”remix_entry_point”:”challenges”,”source_tags”:[“local”],”origin”:”unknown”,”total_draw_time”:0,”total_draw_actions”:0,”layers_used”:0,”brushes_used”:0,”photos_added”:0,”total_editor_actions”:{},”tools_used”:{“ai_enhance”:2,”square_fit”:1,”transform”:1},”is_sticker”:false,”edited_since_last_sticker_save”:true,”containsFTESticker”:false}