Tag Archives: mpira

Njia 3 za kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu yako

Kama ni shabiki mzuri wa mpira wa miguu unaweza kua ni mmoja wa watu wanopenda kufuatilia matokeo ya mechi mbalimbali katika ulimwengu wa kabumbu. Teknolojia imeisharahisisha mambo mengi sana katika soka. Kupitia simu yako ya mkononi unaweza kuangalia mechi live na ukafurahia, kiganjani pako!.. Mbali na nakushuhudia mechi live kiganjani pako, unaweza pia kuangalia matokeo ya mechi zilizochezwa au zinazoendelea kuchezwa hapo hapo kiganjani pako. Hii inasadia sana maana unaweza kua hauna muda wa kutulia na kuangalia mechi lakini lakini ukawa unajua mechi katika upende wa scoles ziko vipi.

Kuna njia zaidi ya moja zinaweza kutumika kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu na watu huzitumia kila siku yaani kuangalia matokeo ya mechi za leo, jana na siku zaidi hiyo. Hapa The bestgalaxy tunaweka wazi njia 3 unazoweza kuzitumia kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu yako ya mkononi.

Njia 3 za kuangalia matokeo ya mechi za mpira kwenye simu

1. App na site/tuvuti maalum kwaajili ya kuangalia matokeo

Unapotaka kujua matokeo ya mechi mbalimbali kwenye simu yako, tambua kuna app za simu ambazo ni maalum kaajili ya matokeo ya mechi za mpira wa miguu na michezo mingine. Unaweza ingiza moja ya app za muundo huu kwenye simu yako na ukawa unatumia kuangalia matokeo ya mechi unazozihitaji kwenye simu. Uzuri wa app hizi ni kwamba nyingi huwa zinakua zinatoa huduma ya kukupatia matokeo bure kabisa japo kila utakapotaka kuzitumia utatakiwa kutumia internet. Mfano wa app hizi ni app iitwayo “LiveScore” na pia hii nyingine inaitwa “GOAL Live Scores”. Mbali na app izo kuna App ningine nyingi sana unaweza tumia kuangalia Scores. kwenyewe app hizi unaweza pia kufurahia vipengele vingine kama vile habari za michezo na ratiba za michezo.

Ukiachana na uwepo wa app, pia kuna websites/tuvuti unaweza tumia kuangalia matokeo ya mechi. App nyingi zinazojihusisha a matokeo ya mechi huwa ni za websites. mfano mzuri ni hii appp ya LiveScore; kuna website inatwa “LifeScore” na hiyo website ndio inaapp iitwayo “LiveScore”. kwahiyo hapo unakua uamuzi wako kuangalia matokeo mechi zako kupitia website au app.

2. Angalia matokeo ya mpira kupitia Google search

watu wengi hutumia google search kupata taharifa mbalimbali kwa haraka. Kunavitu ukivitafuta google unawezeza kuvipata kwa shida lakini sio matokeo ya mechi(hasa kama mechi inatambulika). Google inaweza kukupa matokeo moja kwa moja ya mechi ilioisha unayoihitaji bila mizungusho mingi. Na kitu kizuri ni kwamba kupitia Google unaweza pata taalifa nyingine kuhusu mechi kirahisi sana na bila kupoteza muda wala kutumia bando sana kama baadhi ya njia nyingine. Unaweza tumia njia hii kuangalia matokeo ya mechi za simba na yanga bila utata.

3. Angalia scores kwenye app au tuvuti za kubeti

Ukiachana na njia hizo mbili ambazo unaweza tumia kuangalia scores, njia ya tatu ni kucheki scores kupitia app au tuvuti za kubeti. Kama wewe ni mtu unaebeti kupitia simu, hainaaja ya kujitesa kuangalia matokeo ya mechi zinanoendelea kuchezwa. Unaweza kuangalia kirahisi kupitia kipengele cha “LIVE” katika website au app ambayo unaitumia kubeti. Kipengele hiki huwa kinakupa taalifa za mechi zinazochezwa muda huo na Moja ya taalifa utakazo zipata ni pamoja na magoli. Kipengele hiki ni kwaajili ya kubeti lakini unaweza kukitumia kuangalia scores za mechi unazozijitaji.

Jinsi ya kuangalia mechi za Tanzania kwenye simu

Kama ni shabiki mzuri wa soka la ndani basi bilashaka ninahakika unijiskia Vizuri sana pale unapotazama mechi zinazohusishia timu za bongo kama vile Azam fc, Simba, yanga na nyinginezo.


Tulishazungunzia katika makala iliopita jinsi unavyoweza cheki ama kuangalia mpira wa nje kwenye simu. Kama ni mfuatiliaji wetu mzuri utakua tayari umelijua hilo. Kwenye makala hii tunakujuza jinsi ya kuangalia mechi za Tanzania kwenye simu(online). Yaani namba unavyoweza kuangalia mechi zote zinazohusishia soka la bongo/Tanzania.

Magemu ya mpira ya kucheza kwenye simu GUSA HAPA>>>

jinsi ya kuangalia mechi za Tanzania kwenye simu

Njia rahisi ya kuangalia mechi za Tanzania kwenye simu yako ni kutumia app iitwayo AzamTv Max. Unaweza gusa HAPA>>> kuipakua.

App hii imejaa channel ambazo huusika na mechi saka za Tanzania. Lakini app hiii sio ya bure. Utahijika kulipia ili kufurahia unachokipenda kiganjani kwako.


Mbali na app Azam Max, Kuna baadhi ya app pia huwa zinakupa uwezo wa kuangalia mechi za soka la bongo Kwa Bei nafuu ila huwezi fananisha huduma zake na huduma za Azam Max. AzamTv Max ni Moja ya app bora.

Jinsi ya kupata mkopo kwenye simu GUSA HAPA>>>>

Magroup ya WhatsApp ya kujiunga bure GUSA HAPA>>>

Unapotaka kuangalia soka kwenye simu inatakiwa kuwa na internet yenye kasi na iliotulia ili kufurahia zaidi kuangalia soka kiganjani mwako. Kama unajua kabisa internet yako haipo sawa, ni vema ukaangalia tu kwenye TV maana utainjoi zaidi kuliko kwenye simu. Mara nyingi Sana unapokua unatuzama soka kwenye simu ilio na muunganiko wa internet unaosumbua kunakua na matatizo ya kuganda ganda kwa video.

Jinsi ya kuangalia mpira live kwenye simu (Bure)

Kama ni mpenzi wa muda wa kuangalia mpira wa miguu wa nje ya nchi, nadhani umeshawahi kosa kuangalia  mechi ulioipania kwasababu mbalimbali ikiwemo kuwa mbali na Tv. Teknolojia inazidi kukua kila siku na kuturahisishia mambo. Sasa unaweza angalia mechi Kali za mpira wa miguu kupitia simu yako mubashara(Live) ukiwa popote. hapa tutakujuza jinsi ya kuangalia mpira wa nje karibu mechi zote kwenye simu yako BURE.

Simu ikiingia maji unatakiwa kufanya nini? GUSA HAPA>>>

Ikiwa unahitaji kuangalia mpira live kwenye simu yako, utahitajika kuwa na app maalumu kwaajili ya kuangalizia mpira. App hizi zipo nyingi sana katika playstore(Android) lakini mimi nakushauri uchukue app nyepesi na isiokula sana Mbs iitwayo Live Football Tv.

App ya Live Football Tv ni app ya kuangalia mpira live kwenye simu yako. Mpaka Sasa inatumiwa na zaidi ya watu Milioni ulimwenguni na wanaisifu kwa kuonesha mipira mingi bila matatizo. Mbali na kukuonesha mechi live(mubashara), huwa inakupa matokeo na video za matukio muhimu ya mechi zilizomalizika kwaiyo Kama haukua na bando la kutosha kuangalia mpira mzima, unaweza angalia video ya goli lilivyofungwa tu. Pia inakupa nafasi ya kuangalia vipindi vingine vya kimichezo bure toka Ptv sports. 

App hii ya kuangalia mpira live haipatikani Playstore kwasasa ila unaweza kitafuta Google na kuipakua. Pia Unaweza ipakua kirahisi kwa kugusa hapa>>> INSTALL. Na baada ya kuipakua, hauitajiki kujisajili au kufanya Jambo lolote la kujiunga ili kuitumia. Ni kuifungua na kuinjoi…

Fahamu kuwa: App nyingi zinazowezesha kuangalia mpira bure huendelewa Playstore kutokana na Kuvunja sheria za Playstore. Ikiwa app nilioitaja nayo itaondelewa basi unaweza ipakua app nyingine nje ya Playstore Kwa kugusa HAPA>>>

Jinsi ya kuangalia mechi za Tanzania kwenye simu GUSA HAPA>>>

Je, ni Mbs ngapi zinahitajika kuangalia mpira mzima(Dk90) kwenye simu?

Hili ni swali ambalo wengi hujiuliza, wanapohitaji kuanza kuangalia mpira kupitia simu. Ukweli ni kwamba, kadri video inavyokua na muonekao mzuri ndivyo Mbs huwa zinalika nyingi. Itakua ni vizuri zaidi Kama hautakua na chini ya Mb900 ili kutokua na wasiwasi wa bando kuisha.

Magemu ya Mpira ya kucheza kwenye simu GUSA HAPA>>>

{“remix_data”:[],”remix_entry_point”:”challenges”,”source_tags”:[“local”],”origin”:”unknown”,”total_draw_time”:0,”total_draw_actions”:0,”layers_used”:0,”brushes_used”:0,”photos_added”:0,”total_editor_actions”:{},”tools_used”:{“ai_enhance”:2,”square_fit”:1,”transform”:1},”is_sticker”:false,”edited_since_last_sticker_save”:true,”containsFTESticker”:false}