Tag Archives: Mkopo

Jinsi ya kukopa Pesa katika Mixx by yas (Kwenye simu)

Watu wengi wanaotuma na kupokea pesa kwenye simu zao hapa Tanzania huwa wanatumia huduma za kifedha za mitandao ya simu ikiwemo Mixx by yas kutoka Yas(Tigo).
Mixx by yas imekua moja ya njia nzuri za kutuma na kupokea pesa toka miaka nyuma ambayo ilikua inaitwa “Tigo Pesa”.


Mbali na kutumika kutuma na kupokea pesa, Mixx by yas huwa ina huduma nyingine ndani yake zinahusisha fedha. Katika huduma hizo, kuna huduma ambazo zimelenga kumsaidia au kumuwezesha mtumiaji wao.
Katika Makala hii, tutajikita katika huduma yao ya mikopo inayomuwezesha mtu kukopa pesa zinazoweza kumsaidia kwenye mambo mbalimbali. Ikiwa unahitaji kujua namna ya kukopa pesa katika akaunti yako ya Mixx by yas, basi hapa ndio mahali pake.

Mambo ya kuzingatia unapochukua Mkopo kwenye app za mikopo BONYEZA HAPA>>>

Kukopa Pesa katika akaunti ya Mixx by yas

Kama unahitaji kukopa pesa katika akaunti ya Mixx by yas na uwe huru kuitumia kwenye mambo mbalimbali basi utatakiwa kutumia huduma yao ya “Nivushe plus“. Nivushe plus ni huduma ya Mixx by yas inayokuwezesha mtumiaji kukopa kiwango flani cha pesa na kukilipa katika muda uliochagua kurejesha. Unapewa uhuru wa kuchagua ni muda gani utarejesha(inaweza kuwa baada ya wiki kadha au mwezi mmoja kabisa).

Kama ilivyo mikopo mingine, Nivushe plus pia huwa ina riba ingawa ni kiwango kidogo sana ukilinganisha na baadhi ya huduma za mikopo. Ukiachilia mbali kuwa na riba kidogo, Nivushe plus ni huduma ya haraka sana ya Mkopo kwa watumiaji wa Yas (Tigo).

Jinsi ya kukopa pesa Nivushe plus

Njia rahisi ya kukopa pesa katika Nivushe plus ni kupitia app ya “Mixx by yas“. Kama una app hii kwenye simu yako, fanya yafuatayo:

  • Fungua app ya Mixx by yas
  • Chagua kipengele Cha “Mikopo” kinachoandikwa “Loans” kwa lugha ya kiingereza.
  • Baada ya hapo, chagua “Nivushe plus” kwenye chaguzi zitakazokuja.
  • Ukishachagua, utapelekwa kwenye ukurasa maalum wa kuchukua, kuangalia na kurejesha mikopo.
Ukurasa wa Nivushe plus katika app ya Mixx by yas

Kwenye ukurasa huo unaweza kukopa Mkopo na kuangalia taalifa nyingi za mikopo. Taalifa hizo ni pamoja na Salio la deni, kiwango chako Cha kukopa na hata historia ya malipo yako.

Kiwango unachoweza kukopa katika Nivushe plus huwa kinaongezeka kutoka na mambo kama miamala unavyofanya kwenye akaunti yako na uaminifu katika kurejesha mikopo. Mara nyingi mtu muaminifu na mwenye miamala mikubwa huwa anakua na kiwango kikubwa cha kukopa. Lakini kitu muhimu zaidi ni uaminifu. Ukiwa vizuri unaweza kukopa hadi milioni 2 (Tsh 2,000,000)

Epuka kukopa pesa kama unatabia hizi ndani yako

Kuna uwezekanao wa kuwa na mambo mengi sana yanayoweza kusukuma mtu kukopa pesa za watu wengine au taasisi mbali mbali za kifedha. Na kukupa ni jambo zuri sana maana kuna muda mtu unaweza kukwama kifedha kwa kukumbana na jambo linalohitaji pesa ambayo hauna lakini ukalimudu kupitia mkopo.

Kuna watu hukopa pesa ili kurekebisha mambo yao yalioenda vibaya na kuna hata ambao hukopa ili kulifanikisha jambo lisilo na ulamazima sana. Kukopa kwasababu yoyote ile ni uamuzi mzuri lakini itakua uamuzi mzuri zaidi kama umefanikiwa kwenye jambo lako na kuulipa mkopo wako. Kama haujakamilisha jambo lako au umefanikisha lakini haujafanikiwa kulipa deni la mkopo wako, uamuzi wa kukopa unaweza kuwa mbaya kwako. Na endapo hali yakushindwa kulipa itakua inakuandama kila mara unapokopa ni vema ukaanza kujiweka mbali kidogo na mikopo.

Hapa The bestgalaxy tunakupa tabia ambazo mara nyingi zikiwa ndani yako basi mikopo huwa karibu sana na pia huwa ni ngumu kuilipa. Sio kila mtu mwenye madeni au anaeangukia kwenye madeni anatabia hizi. Ni baadhi ya watu tu ndio huwa na tabia tunazoenda kuzielezea hapa. Niwesema hivyo maana wengine husukumwana na vitu vilivyo nje kabisa na uwezo wao  au sababu myingine mabali na tabisa hizi.

Mambo unayotakiwa kujua kuhusu simu za mkopo BONYEZA HAPA>>>

Epuka kukopa pesa kama unatabia hizi ndani yako

Kushindwa kuzirudisha pesa zako mwenyewe

Kama ni mtu mwenye malengo na huwa unajiwekea pesa kwaajili ya mambo mbalimbali basi kuna muda unaweza kuwa unajikopa mwenyewe. Yani unachukia pesa ulizojiwekea kwaajili ya jambo flani na kuzitumia kwenye jambo lingine tu huku ukiwaza kichwani “Nitazirudisha”. Ikiwa unatabia hiii na unakua na msimamo wa kuzirudisha tena hizo pesa basi unaweza usiteseke sana kulipa hata ukikopa kwa watu wengine. Lakini kama huwa haurudishi pesa hizo na ni tabia yako, kunaweza kuwa na ugumu pia unapokopa kwa wengine. Ni vema ukajaribu kujiimarisha ndani yako kabla ya kukopa kwa wengine. Hakikisha unapambana sana kurudishia pesa sehemu zako za dani ukichukua pesa.

Jinsi ya kupata Mkopo kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Kuhairisha mipango yako ulioianza

Kuna baadhi ya watu huwa na mipango ya biashara na Mambo mengine yanayoweza kuhitaji pesa ili kuingiza pesa. Kukopa kunaweza kuwa ni wazo la haraka kwa mtu mwenye mipango ya namna hii lakini hana mtaji au pesa inayohitajika.
Kukopa sio kitu kibaya kama umekusudia kuanza kupambana kutimiza mpango uliojiwekea. Lakini kama ni mtu unaempenda kuhairisha mipango ulioianza, kukopa kunaweza kuumiza.
Ukichukua Mkopo kwaajili ya mpango flani lakini ukahairisha na kwenda tofauti na mpango huo, kunakua na hatari kubwa ya kupoteza pesa hiyo. Pesa ikiisha bila kufanya kitu kilichosababisha ukope, unaweza jilaumu kuliko ungefanya na kushindwa.
Kama haujaweka vizuri mipango yako au haupo tayari kuipambania kwa asilimia 100, basi usikope pesa kwanza.

Kusahau shinda unapokamata pesa yoyote

Hali yako huwa inakua vipi muda ambao hauna pesa? Na hua inakua vipi ukipata pesa? Kama ukipata pesa yoyote mkononi mwako shida huwa unazisahau, unafanya matumizi na kuacha kabisa kutafuta pesa basi kukopa kunaweza kuwa kubaya kwako. Ukikopa pesa na kuishika mkononi pesa hiyo inabidi iwe kichwani kwako kuwa sio pesa yako na unahitajika kulipa. Hii inaweza kukusaidia kupata mpango wa kuilipa na kuwa makini unapozitumia pesa hizo za mkopo.
Ikiwa utaruhusu pesa hiyo ikusahaulishe shida na kuichukulia ni yako, basi unaweza kuwa ndio mwanzo wa kupuuza deni lako, kuridhika na kuanza ikiutumia pesa.
Usiache kuiona pesa ya Mkopo kuwa ni Mkopo hata ikiwa na mamilioni ya pesa.

Haupendi kudaiwa.

Kutopenda kudaiwa ni jambo zuri sana ila linakua zuri kama utakua na uwezo wa kujikumbusha mwenyewe kulipa pesa kabla haujadaiwa. Mbali na hapo ukiwa haupendi kudaiwa itabidi uanze kuepuka kukopa pesa maana kudaiwa ni lazima na ukichukia au kumfanyia vibaya anaekudai itakua ni kosa kwako tu kivyovyote maana umeshindwa kutimiza makubaliano. Wengine hufikia mpaka hatua ya kupambana kukata kulipa Kwasababu ya kudaiwa vibaya lakini hawajihukumu kwa kuchelewesha pesa muda mrefu kinyume na makubaliano.

Natumaini umesoma na kuelewa makala hii na inaweza kuwa msaada katika Maisha yako kwenye upande wa kukopa. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi.

Jinsi ya kupata mkopo kwa njia ya simu tanzania (Watu Million 10+ wanaitumia njia hii halali ya kukopa)

Unaambiwa, zaidi ya watu milioni 100 duniani wanatumia simu zao kupata mkopo kwa haraka. Na Kwa hapa Tanzania kuna watu wengi sana ambao tayari wanatumia simu zao kupata mikopo inayowazaidia kuwasukuma katika mambo mbali mbali kimaisha.
Kutumia simu kupata mkopo ni moja ya matumizi chanya ya simu hizi za Smartphone. Ni matumizi chanya kwasababu mkopo ambao watu hupata kupita simu zao, unawasaidia katika maisha halisi. Maana wanaweza kupata mkopo ili kurekebisha mambo yanapoenda vibaya katika biashara and maisha Kwa ujumla.


Kwa mfano; Kuna dada flani mzuri sana sitomtaja jina. alikua anasafiri alipanda gari alafu alipokua ndani ya gari na wakati gari limeanza safari akagundua sehemu alioweka pesa zake ikiwemo nauli ipowazi na hakuna pesa… Basi moja Kwa moja akajua ameibiwa pesa na hana pesa yoyote. Dada yele alikua mpole kama amemwagiwa maji ya baridi kwenye gari hilo huku akiwaza ni jinsi gani konda atamuelewa, ukizingatia maneno ya makonda wengi huwa ni mabaya kwenye maswala ya hela.
Lakini Kwa bahati nzuri alikumbuka kuwa kwenye simu yake huwa anatumia huduma flani inayo mruhusu kukopa hadi 100,000 ndani ya dakika 5 tano tu. Alikua hadaiwi kwenye hiyo huduma na alikua ni Moja ya watu wanalipa mikopo Kwa wakati ndio maana alipewa uwezo wa kukopa kiasi kikubwa kidogo.


Basi bila kupoteza muda yule dada akatumia huduma hiyo kukopa kiasi cha pesa Cha kutosha nauli na mambo mengine. Pesa aliokopa ilitumwa kwenye laini yake ya simu (Tsh 70,000). Alipoingia tu kwenye simu akapatanguvu, akamuita konda na kumwambia “Samahani kaka, nimedondosha pesa ya nauli lakini ninapesa kwenye simu naomba uniruhusu nikutumie nauli kwenye simu yako au nikifika stendi tukatoe Kwa wakala…”. Konda akampa pole yele dada kisha akamwambia atume tu kwenye simu ila utume na yakutotea. Basi yele dada alipona kiivyo.

Sasa huo ni kama mfano mzuri unaoonesha umuhimu wa watu kujua na kua na huduma za kukopa kwenye simu. Ikiwa wewe ni moja wa watu wanaohitaji kuwa na huduma za kukopa kwenye simu basi hapa tunakujuza juu ya njia moja ya haraka na halali ya kupata mkopo kwenye simu Tanzania. Soma maelezo yafuatayo hadi mwisho ili kuelewa zaidi njia hii.

Jinsi ya kupata mkopo kwa njia ya simu tanzania.

Kama unahitaji kupata huduma ya mkopo kwa njia ya simu, basi tumia app iitwayo Branch. App ya branch ni moja ya app halali ambayo ukiwanayo kwenye simu yako inakupa uwezo wa kukopa Tsh 5,000 na kuandelea ndani ya dakika chache tu. Tena mkopo unatumwa kwenye laini yako hapo hapo na utakuja kulipa kwa gharama nafuu.
App ya Branch unaweza kuipata na kuiingiza kwenye simu yako kirahisi kwa kugusa HAPA. Lakini kabla haujaiingiza kwenye simu yako ningepeda ufahamu mambo ya fuatayo;

Ukishaiingiza app hii kwenye simu yako, jisajili na ujaze taalifa zako za ukweli kabisa alafu ndio uombe mkopo. Na kwa mara ya kwanza unavyokopa, kopa kiasi kidogo tu (Tsh 5000) na urudishe kwa wakati. Kurudisha kwa wakati kutafanya wakuamini na upadate uwezo wa kukopa kiasi kikubwa kirahisi mbeleni. Unapokopa Kwa mara ya kwanza wanaweza wakachelewa kidogo kukupa. Ila mkopo utakao omba baadaya kurudisha mkopo wa kwanza unaweza upata hata ndani ya dakika moja. Maana wanakua wanajua wewe ni mwaminifu.

Zawadi ya Tsh 5750 BURE Utayopewa na Branch (USISAHAU HII)

App ya Branch pia huwa wanatoa Zawadi ya Tsh ,5750 BURE unaporudisha mkopo wa kwanza. Lakini ni lazima uwe umeandika namba za mualiko. Hii ni kwaajili ya uaminifu wako maana wanaotangulia kukupa pesa ni mwenye.


Kama unahitaji kupata zawadi hiyo basi ingize app kwenye simu yako Kisha jisajili. Ukijisajili Gusa sehemu ilioandikwa “Alika” alafu chagua “Ingiza Nambari ya promosheni” kama unavyoona hapa chini.

Baada ya hapo, unaletewa kibox, jaza nano hili “””elia04c93“”” katika kibox kama inavyo onekana katika picha ya hapa chini. Usisahau kunandika namba hiyo ya mualiko ili upate zawadi.

Ukishajaza tu na kugusa kitufe cha blue, siku yoyoye utakayoomba mkopo alfu ukarejesha, utapata Tsh 5750 BURE.

Kama utakua na tatizo, njoo uulize maswali WhatsApp kwa kugusa HAPA>>>

App hii itakusaidia kuomba mkopo kwa Simu Tanzania. Na ukiwa mwaminifu basi unaweza kuitumia kupata mikopo ya haraka kupitia simu yako Kila unapohitaji. Utakuaunaomba mkopo online kirahisi sana.

Fanya haya kabla simu yako haijaibiwa ili kuipata ikiibiwa GUSA HAPA>>>