Tag Archives: mapenzi

Mambo ya kuzungumza na Mpenzi ili kudumisha Furaha kati yenu



Katika mahusiano, mawasiliano si jambo la hiari bali ni msingi wa kudumu kwa furaha kati ya wapenzi. Wapenzi wengi hushindwa kudumisha ukaribu wao wa furaha kwa sababu hawajui ni mazungumzo gani yanayoweza kuimarisha uhusiano. Hapa tumekusogezea mambo muhimu ambayo unaweza kuzungumza na mpenzi wako mara kwa mara ili kuongeza furaha kati yenu.

Mambo ya Kuzungumza na Mpenzi Ili Kudumisha Furaha kati yenu



1. Malengo Yenu na Mipango Ijayo



Kuzungumza kuhusu malengo ya maisha ni njia nzuri ya kuonyesha kwamba mna ndoto za pamoja. Waweza kuzungumzia mambo kama kujenga nyumba, kuanzisha biashara, au hata ndoto za kusafiri sehemu fulani siku moja. Mazungumzo haya humjengea kila mmoja matumaini kwamba uhusiano huu unaelekea mbali na si wa muda mfupi. Hii pia huimarisha mshikamano na kuonyesha kwamba kila mmoja anathamini uwepo wa mwenzake kwenye maisha.


2. Kusifiana



Kila mtu hupenda kusifiwa, na jambo hili linapokuja kwa mpenzi wako linakuwa na nguvu kubwa zaidi. Usisubiri matukio makubwa ili kumsifia, hata mambo madogo kama alivyojitahidi kupika chakula kizuri, jinsi alivyoonekana vizuri, au bidii yake wenye kazi. Maneno ya kusifia hufanya mpenzi ajisikie kupendwa na kuthaminiwa, na huongeza furaha katika kila siku mnayoshirikiana.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako kwa sms BONYEZA HAPA>>>



3. Kukumbushana kuwa Mnapendana



Wengi hudhani kwamba kusema “Nakupenda” mara kwa mara hupoteza maana yake, lakini ukweli ni kinyume. Kila unapomwambia mpenzi wako maneno haya, unamjengea ujasiri na kuondoa mashaka moyoni.
Hata katika nyakati ngumu za mahusiano, kukumbushana mapenzi yenu huleta nguvu ya kumaliza matatizo yalio kati yenu. Haya ni maneno rahisi, lakini yana nguvu kubwa sana.



4. Ahadi za Kuwa Pamoja



Kila uhusiano unahitaji imani kama nguzo, na ngozo hii huletwa zaidi ahadi. Ahadi ndogo ndogo kama “Nitakuwa nawe maishani mwangu” au “Sitakuacha hata siku moja” hubeba maana kubwa. Kuzungumza kuhusu ahadi na kuzitekeleza hufanya kila mmoja ajihisi salama na hufurahia penzi bila woga wa kuachwa.



5. Mambo ya Utani



Utani mzuri ni kama sukari kwenye kikombe cha chai; huwa unafanya kila kitu kiwe kitamu zaidi. Mahusiano bila vicheko huwa ni magumu. Utani unaoaidia kuleta furaha, kucheka pamoja na michezo kidogo midogo hufanya mapenzi yawe mazuri zaidi. Jihadharini tu usitumie utani unaoweza kumkera mwenzako ila hakikisha kuna hali ya ucheshi inayowafanya muwe na furaha.



Mwisho nikukumbushe tu kuwa mahusiano mazuri ni yenye chembe za urahiki wa kweli na furaha kati yenu. Ni hayo tu katika Makala hii ya The Bestgalaxy. Endelea kuwa karibu nasi kwa mambo mazuri zaidi.

Sms 10 za kiingereza kwaajili ya mpenzi wako

Kila maneno yanayotamkwa kwa makini yanaweza kuwa kioo cha kumwambia mpenzi wako, “Nakupenda, nakutamani, na wewe ni muhimu kwangu.” Katika dunia inayozunguka kwa simu, hata kama muko mbali na mpenzi wako, lakini maneno machache ya mapenzi kupitia SMS, yanaweza kuvunja umbali na kuwaweka pamoja kihisia.

Katika kutuma SMS za mapenzi, Lugha ya Kiingereza inaweza kuwa na ule mkuki wa kupenya roho kwa njia isiyotarajiwa. Sio kwa kuwa ni ya kigeni, bali kwa kuwa ina mafumbo yake yenye kugusa hisia. Kitu kikubwa hapa ni unaemtumia awe anaelewa.

Zingatia haya ili usichokwe na mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Sms 10 za kiingereza kwaajili ya mpenzi wako


Hapa chini, utapata orodha ya SMS za kiingereza chache unazoweza tumia kuweka wazi hisia zako kwa mwanamke au mwanaume umpendae. Ziangalie vizuri kwa lugha ya kiingereza(English )na kiswahili ili kujua kama zinaenda na hali ya mahusiano yako kabla haujazitumia.

  1. English:
    “Every morning I wake up, my first thought is of you. You are the reason my days feel brighter and my heart feels lighter.”
    Kiswahili:
    “Kilina asubuhi ninapoamka, wazo langu la kwanza ni wewe. Wewe ndio sababu siku zangu zina mwanga na moyo wangu mwepesi.”
  2. English:
    “Your smile is my favorite sight in this world.”
    Kiswahili:
    “Tabasamu lako ndio mandhari niipendayo zaidi hapa ulimwenguni.”
  3. English:
    “No matter where I am, you’re always on my mind and in my heart. Distance means nothing when you mean everything.”
    Kiswahili:
    “Haijalishi niko wapi, daima uko kwenye akili na moyo wangu. Umbali hauna maana wakati wewe ni kila kitu.”
  4. English:
    “Loving you is the easiest and most natural thing I’ve ever done.”
    Kiswahili:
    “Kukupenda ni jambo rahisi na la asili zaidi nimefanya.”
  5. English:
    “You turned my life into a beautiful poem, every line speaks of you.”
    Kiswahili:
    “Umebadilisha maisha yang kuwa shairi zuri, kila mstari unazungumzia wewe.”
  6. English:
    “I never believed in magic until I met you. Now, every day feels like a wonderful spell.”
    Kiswahili:
    “Sikuwahi amini uchawi mpaka nakutana nawe. Sasa, kila siku inahisi nzuri ya kustaajabisha.”
  7. English:
    “You are my today, my tomorrow, and all the days I hope to see.”
    Kiswahili:
    “Wewe ni leo yangu, kesho yangu, na siku zote ninazotumaini kuziona.”
  8. English:
    “Your love is my anchor, it grounds me when I feel lost and lifts me when I feel low.”
    Kiswahili:
    “Upendo wako ni nanga yangu, hutua nikihisi kupotea na kuniinua nikihisi nipo chini.”
  9. English:
    “I cherish the way you love me, the way you understand me, and the way you make ordinary moments extraordinary.”
    Kiswahili:
    “Nathamini vile unavyonipenda, unavyonielewa, na unavyofanya muda wa kawaida uwe wa kipekee.”
  10. English:
    “With you, I’ve found a home that isn’t a place, it’s a feeling. A feeling I never want to lose.”
    Kiswahili:
    “Pamoja nawe, nimepata nyumba ambayo sio mahali, ni hisia. Hisia ambayo sitaki kamwe kuipoteza.”

Huu ni mwisho wa Makala hii lakini ningependa ufahamu kwa sio kila mtu hufurahia kusoma sms za kiingereza kwenye mahusiano. Baadhi ya watu huwa wanafurahia maneno ya kiswahili hata kama wanajua vizuri lugha ya kiingereza. Kwaiyo ni vema ukasoma akili ya mwenza wako vizuri kabla haujazitumia. Na kama unazitumia, usizitumie mara kwa mara.

RAHA ZA MSAADA (Simulizi fupi ya Kusoma)

Baada ya kuoa nilijua nimepata mke wa kuishi naye na ambaye angeweza kunifanya nipate amani na nilidhike kila ninapomhitaji. Naweza kusema ilianza hivyo, lakini haikuishia hivyo. Mambo yalikuwa hivi;

Baada ya ndoa, nilianza kuishi na mke wangu Neriah kwa furaha kubwa. Alikuwa mwanamke mzuri sana na nilijivunia kumuweka ndani. Ilikuwa ndoto yangu siku zote kumwoa, na japo watu wengi walimuwinda, mimi ndiye nilibahatika. Haikuwa rahisi, kwa sababu hali yangu ya kifedha haikuwa kubwa sanaa, lakini nilijitahidi hata kumwaga pesa kiasi fulani ili anielewe.

Tulipoanza maisha, kila siku nilitoka kazini asubuhi na kurudi mchana, naye akibaki nyumbani kufanya shughuli za ndani. Baada ya muda alianza kuleta marafiki zake wengi nyumbani. Niliporudi kazini mara nyingi niliwakuta, jambo lililonifanya nisiwe huru sana. Nilimueleza juu ya hili, akapunguza kidogo, lakini tabia ikaendelea.

Kadri muda ulivyopita, nilianza hata kuzoeana na baadhi ya marafiki zake. Hata barabarani walinisalimia na wengine walikuwa wakinionesha wanapokaa, wakinikaribisha kwa kusema: “Shemeji karibu, mimi nakaa hapa.” Kwa sababu nilimpenda mke wangu, nilichukulia wote kama mashemeji.

Baada ya miaka miwili, ndoa yangu ikaanza kubadilika. Mke wangu alianza kuwa na makasiriko ambayo mara nyingi yalitokana na ndugu zake. Kwa kuwa sisi ndiyo tulikuwa na uwezo kiasi katika ukoo, alianza kuwasaidia. Mwanzoni alikuwa akiniambia kabla ya kufanya chochote, lakini baadaye akaanza kufanya maamuzi bila kunishirikisha. Alifikia hata kuuza vitu vyetu au kugawa bila ruhusa yangu. Nilijaribu kumkalisha tuzungumze, lakini akawa mkali sana, kama ilivyo tabia ya baadhi ya wanawake wanapokomaa kwenye ndoa.

Wakati huo huo, mambo yangu ya kazi yalikwama. Niliyumba kiuchumi, japo sikupungukiwa chakula. Lakini tabia yake ya kufanya mambo pasipo kuniambia ilinipa mawazo makubwa. Nilivumilia sana, lakini alikuwa haambiliki. Sio kwamba hakunipenda, alinipenda, ila vitendo vyake vilinifanya nisimwelewe. Nilihisi pengine tatizo letu lilikuwa kuchelewa kupata mtoto.

Misukosuko ikaendelea, na hali yangu kifedha ikazidi kuwa mbaya. Kila mara tulipogombana, mke wangu alikuwa akirudi kwao. Nilikua naomba sana ndio anarudi. Nilimweleza mara nyingi atulie ili nipate nafasi ya kutafuta kupambana mambo ya kimaisha vizuri, lakini hakunielewa.

Katika hali hiyo, nilijikuta nikiwa na mawasiliano ya karibu na rafiki zake, hasa mmoja aitwaye Julieth. Wakati mwingine nilimhitaji anisaidie kuniunganisha na mke wangu pale ambapo mke wangu hakuwa tayari kunisikiliza. Hali hii ikatufanya tuzoeane sana.

Julieth alikuwa mwanamke mzuri, mwenye mvuto, lakini kwa kuwa nilimheshimu kama rafiki wa mke wangu, tulidumisha heshima. Lakini, kutokana na ukosefu wa amani katika ndoa yangu, nilijikuta nikiingia kwenye penzi zito naye. Julieth alikuwa single mother akiishi na mtoto wake, na alijipenda sana. Alikua na mwili ulioja kidogo ila ni mzuri utafikili hana mtoto.

Tulipoanza uhusiano, maisha yangu yalianza kuwa na mwanga tena. Nilipata furaha, mambo ya kazini yalienda vizuri kwenye upande WA uchumi na niliweza kuvumilia vituko vya mke wangu bila maumivu makubwa. Mapenzi ya Julieth yalikuwa matamu, hasa kwa kuwa yalikuwa ya siri. Nilikua nikienda kwake nasahua maudhi yote ya mke wangu. Na kwakua alikua anajua kitu gani kina nisumbua kwenye ndoa yangu, alikua hanipi nafasi ya kuwaza.


Lakini Pamoja na kwamba tulikua na mahusiano na Julieth, Bado mke wangu tulikua tuna muheshimu sana. Nakumbuka hata Julieth alikua anasema yupo na mimi kwasababu ya ninayopitia na ukaribu tulioujenga kati yetu. Alikua ananikumbusha mpaka kurudi nyumbani nikiwa nae kwa muda mrefu. Aliwahi pia kuniambia kwa haamini sana kwenye mapenzi kwasababu mtu aliemzalisha wanawasiliana ila anamsumbua sana. Na hakunificha, aliniambia anampenda ila ndio hivyo tu hawapo sawa.
Alikua unaurusha moyo wangu kwa furaha tukiwa kwenye uwanja wetu. Yani nilikua nikizidisha makofi, yeye anakua mtu wa viitikio tu “ooh.. shem” mpaka nachanganyikiwa.

Tuliendelea na mahusiano ya Siri kwa muda flani japo lilikua sio jambo zuri. Lakini baada ya muda, mke wangu alipata ujauzito wangu. Ujio wa mtoto ulikuwa jambo kubwa sana kwenye familia yetu. Kuanzia hapo niliacha kabisa uhusiano na Julieth na kuelekeza nguvu zangu kwa mke wangu. Hatimaye alijifungua na akawa mwanamke wa heshima tena kwangu. Hali hii ilinishangaza ila nikaichukulia kama ilivyo.

Mapenzi kati yangu na Julieth yalikoma, na tukabaki kuheshimiana kwa umbali ghafla tu. Baadaye nikasikia ameolewa na baba wa mtoto wake. Hii ilikua ni habari nje kwangu maana mapenzi yote yalikua kwa mwanamke wangu na mtoto wangu.

Maisha yaliendelea, lakini kipande hiki cha safari ya maisha yangu kilinifundisha mambo makubwa sana. Wewe umejinza nini kwenye sehemu hii ya maisha yangu? Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy!

MWISHO

Faida na Hasara za kuoa Mwanamke mzuri sana

Mwanamke mzuri huweza kuvutia kwa haraka na kumfanya mwanaume ahisi kuwa amekutana na ndoto zake za mahusiano. Uzuri wa nje huonekana kuvutia, huamsha hisia, na mara nyingine huweza hata kuendesha maamuzi ya mwanaume. Lakini je, uzuri huo wa macho una nafasi gani katika maisha ya ndoa ya muda mrefu?

Ndoa ni zaidi ya muonekano wa nje. Ni safari yenye changamoto, majaribu na mafanikio yanayohitaji uvumilivu, uaminifu na mawasiliano mazuri. Uzuri unaweza kufifia kwa muda, lakini tabia na maadili vina uwezo wa kudumu. Hivyo, kuoa mwanamke mzuri kunaweza kuwa na manufaa makubwa, lakini pia kuna changamoto zinazoweza kujificha nyuma ya tabasamu na mwonekano wa kuvutia.

Katika Makala hii, unaenda kukupata uelewa mpana kwa kuangazia kwa uhalisia faida na hasara zinazoweza kuambatana na uamuzi wa kuoa mwanamke mzuri. Bila kupoteza muda, hebu tuangalie faida na hasara hizo;

Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>


Faida na hasara za kuoa Mwanamke mzuri sana




Faida za kuoa Mwanamke mzuri sana



1. Kuuridhisha moyo wako: Mwanaume ukiwa umeoa mwanamke mzuri sana kwako, inamaana umeuridhisha moyo wako. Moyo wako unafurahi kumuangalia na kuwa nae kiujumla. Ukiachana na mambo yoyote yanayojitokeza ndani ya ndoa, kitendo cha kufanikiwa kuwa nae kwenye ndoa tu kinaweza kufanya moyo wako ufurahi na kuridhika. Kumuweka ndani mwanamke mzuri sana kwako ni hatua kubwa kwenye mahusiano ambayo wengi hushindwa. Hii ni sawa na kutimiza ndoto au lengo flani kwenye maisha.

2. Kupata heshima kwa watu wengine: Mwanamke mzuri huwa haishii kuwa mzuri yeye tu, anampa heshima na mwanaume wake. Waswahili waliosema “kaa karibu na waridi, unukie” hawakukosea maana ndio kinachotokea ukiwa na mwanamke mzuri. Uzuri wake unaweza kukupa heshima kwa watu wengine. Mwanaume anaemiliki mwanamke mzuri anaweza kuwavutia hata mwanamke wengine kuwa nae kwenye mahusiano.

3. Huongeza kujiamini kwa watu na mambo yako: Mwanaume nae miliki au kuoa mwanamke mzuri huwa na tabia ya kujiamini. Tabia hii inaanza kujionesha hata kwa kile kitendo cha kukubari kuwa na mwanamke huyo mzuri. Wengi wanashindwa kimiliki mwanamke mzuri lakini yeye ameweza kumuoa kabisa.


Ukiachana na hilo, kujiamini kunaweza kuongezeka zaidi anapokua kwenye mambo yake akijua kuwa ana mwanamke mzuri sana kwenye maisha yake. Mwanamke mzuri anaweza kuwa chanzo cha furaha na kujiamini kwa mwanaume anaepambana na maisha.

Hasara za kuoa Mwanamke mzuri sana





1. Mwanamke kutafutwa na mwanaume wengi: Mwanaume ukiwa umeoa mwanamke mzuri, fahamu kuwa umeweka ndani kitu kinachoweza kuwavutia mwanaume wengine wengi. Wanaume wengi huwa wanavutiwa na mwanamke mzuri na kumiliki au kumuoa, hakuondoi kabisa hali ya yeye kuwavutia wengine. Kwaiyo ukiwa unaishinae unaweza kutana na mambo mengi sana ya wanaume wenzako kumuwinda hatakama watakua hawafanikiwi kumkamata.


2. Hofu ya kusalitiwa au kumpoteza: Mwanamke mzuri anaweza kufanya upate hofu ya kusalitiwa au kumpoteza. Hali hii ya hofu inaweza kutokea endapo mwanaume akimpenda sana mwanamke mzuri na huyo mwanamke akaonesha muelekeo au dalili za kumsaliti. Katika kuishi na mwanamke mzuri, moja ya vitu hatari kwa mwanaume na maisha yake ni hiki.


Mwanaume akiwa na hofu ya kusalitiwa au kumpoteza mke wake mzuri, anaweza jikuta anafanya vitu vingi hata vilivyo nje ya uwezo wake ili kumtuliza mkewe. Wivu mwingi unaweza kuibuka hapa. Kama mwanamke huyo atakua na nia mbaya au tabia mbaya, basi muelekeo wa maisha ya mwanaume unaweza badilika kabisa.



3. Dharau na Kiburi cha uzuri: Wanawake wengi wazuri husumbuliwa na tabia ya kujiamini sana kupitia uzuri wao. Tabia hii inaweza pelekea mwanamke mzuri kuwa na dharau au kiburi ndani ya ndoa huku akijiamini sana kwenye upande wa uzuri wake. Anaweza hata kufanya mambo mabaya lakini asijishushe kwasababu anaamini yeye ni mzuri na wengi wanampenda nje ya ndoa.


Mwanaume akiingia kwenye ndoa na mwanamke mzuri sana alafu mwanamke huyo akashindwa kujiendesha kwenye swala la kiburi au dharau, inakua ni kama amekula hasara hivi. Yani mwanaume anaweza kuhisi kunyanyaswa kihisa na kupata msongo wa Mawazo kabisa.



Mwisho niseme; hayo yote mwanga wa kukusaidia kufikiri kwa kina kabla ya kuchukua hatua muhimu maishani. Tafakari kwa utulivu kila hoja, kisha jiulize – je, ni uzuri wa macho au uzuri wa moyo unaostahili kuwekwa kipaumbele kwa mwanamke wako?

Lakini kabla ya kuondoka hapa, fahamu kuwa wanawake wametofautiana tabia. Yani Kuna wanawake wazuri sana ambao hauwezi ona hasara za kuwa nao kabisa.

Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy!

Maneno mazuri ya kumwambia mpenzi wako ili akupende zaidi

Ingawa vitendo ni muhimu kwenye mahusiano, lakini maneno mazuri huweza kugusa moyo wa mtu wako kipekee na kuimarisha hisia kati ya wapenzi wote wawili. Kwa kutumia maneno sahihi, unaweza kumfanya mpenzi wako ahisi kuthaminiwa, kupendwa na kuwa salama katika penzi lenu.

Watu hutumia njia mbalimbali kuwafikishia wapenzi wao maneno haya ya mapenzi. Wengine huandika ujumbe mfupi (SMS), wengine hutumia sauti katika simu au hata kuandika barua za kimapenzi. Kuna pia wale wanaopendelea kusema uso kwa uso wakitumia sauti ya upole na macho ya upendo. Lakini kilicho muhimu si njia unayotumia, bali ujumbe wenyewe (iwe ni kwa kumwambia “nakupenda”, au kwa kutumia maneno)
Katika makala hii, tumekuandalia orodha ya maneno mazuri ya kumwambia mpenzi wako ili akupende zaidi. Fanya uyaangalie hapa chini;

Maneno mazuri ya kumwambia mpenzi wako ili akupende zaidi

Kila inapofika asubuhi kama hii, nakumbuka kuwa huu ni mwanzo wa siku, na siku yangu njema huanza kwa kujua hali yako kipenzi. Umeamka salama mpenzi wangu?

Kwangu “Maisha Mazuri” yana maana “Mimi kupendana na wewe”. Tukitengana, yatabaki “Maisha” tu alafu “Mazuri” utakua umeondokanayo wewe.

Nikiwa kama Binadamu, sijakamilika na nina nafasi kubwa ya kukosea hapa duniani. Lakini katika yote, naamini sikukosea kukuchangua wewe maishani. Nakupenda na unanipa furaha sana.

Mtu ukiingia kwenye mahusiano mazuri, karibu kila kitu kwenye Dunia kinakua kitumu. Mfano ni Mimi sasaivi; Maisha ni MATAMU, chakula nikila ni KITAMU na hata WEWE kwangu upo hivyo hivyo Mpenzi.

Nilipogundua kuna WEWE kwenye huu ulimwengu, moyo wangu haukua tena na chaguo la kupenda au kuto kupenda. Nilianza kukupenda moja kwa moja mpaka nikashindwa kuuficha ukweli.

Nikikutizama, nakuona kama malaika. Nikikusikiliza, nasikia sauti inayougusa moyo wangu. Nikikufikilia, napata furaha moyoni. Wewe ni Mwanamke ninakupenda na pia waajabu sana maishani mwangu.

Tabasamu lako ni kama humwangia furaha moyo wangu. Siwezi elezea sana ni jinsi gani nakupenda na napenda unapotabasamu, lakini fahamu tu kuwa Nakupenda sana.

Sjui nina mapenzi ya kizamani???… Kama ni hivyo, basi acha tu unione hivyo mpenzi wangu. Natamani tuishi pamoja, tuwalee watoto wetu. Na natamani sana tuendelee kuwa pamoja mpaka mwisho wa maisha yetu.

Kama maisha ni simulizi basi, natamani kuandika simulizi ya Mapenzi na wewe. Simulizi ya watu wawili wanaopenda kwenye kila hali, Wenye mapenzi ya dhati, kusameheana na kushikana mpaka wakafika mbali. Tunaweza iandika pamoja si ndio?

Nahisi umeniweza sasa. Siwezi fikilia maisha yangu bila wewe. Siwezi kuwa ninafuraha nikikukosa hata nikinywa nielewe.

Jambo la muhimu: Ikiwa unataka kuimarisha mahusiano yako, kuongeza ukaribu au kumfanya mpenzi wako aone kuwa yupo na mtu anayemjali kweli, basi maneno haya yatakusaidia sana. Chagua yanayokufaa kwa hali ya mahusiano ya sasa ndio uitumie.

Ujumbe mzuri wa Mke au Mume aliembali BONYEZA HAPA>>

Kutoka kimapenzi na Shemeji kuna Madhara gani?

Uhusiano wa kifamilia ni jambo la muhimu sana. Familia hujengwa kwa misingi ya upendo, heshima na uaminifu baina ya wanafamilia. Kila mtu anatarajiwa kulinda mipaka ya heshima ili kuhakikisha amani na mshikamano vinaendelea kudumu ndani ya familia.

Lakini, kuna wakati watu hujikuta wakivuka mipaka hiyo na kujihusisha kimapenzi na shemeji zao. Ingawa hali hii inaweza kuja kwa kushawishiwa, kulazimishwa au chukuliwa kama jambo la kawaida kwa baadhi ya watu, ukweli ni kwamba huleta athari kubwa sana kwa maisha ya mtu binafsi na kwa familia nzima.


Ni muhimu kuelewa kuwa matendo kama haya yanaweza kuathiri sio tu wahusika wawili, bali vizazi na familia yote kwa ujumla. Hivyo, kabla mtu hajachukua uamuzi wa kutoka na shemeji kimapenzi, ni muhimu kujua madhara yanayoweza kutokea. hapa chini kunakupa orodha ya madhara makubwa yanayoweza kukupata au kuikumba familia yako endapo utajihusisha na kitendo hicho.

Jinsi ya kutafuta mpenzi mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Madhara ya kutoka na shemeji kimapenzi

Kupata magonjwa

Mtu kuwa ni shemeji yako haimaanishi yupo salama kwenye upande wa afya. Shemeji yako anaweza kuwa na magonjwa ya kawaida ya zanaa au virusi vya ukimwi kabisa bila wewe kujua. Na endapo utajihusisha nae, unaweza kupata magonjwa hayo kwa urahisi kwakua na imani kuwa ni shemeji wako. Kuna mashemeji wengi wanaume na Wanawake hawapo salama kiafya. Hivyo kujiepusha nao ni kujilinda kiafya.

Kumpoteza mpenzi ulienae na kuvunja familia

Unapokua na mahusiano na shemeji, Kuna hatari kubwa sana ya mahusiano kugundulika. Mahusiano ya Mapenzi ni ngumu sana kuyaficha maana upendo ukizidi mnaweza kifika hatua ya kutojali sana waliowazunguka.


Endapo utagundulika kutoka na shemeji yako, unaweza poteza mpenzi wako(kama unae) na kunivunja familia. Hakuna ndugu anaeweza kukuchukulia vizuri kwa kitendo hicho na utakua umetikisa familia kwa kiasi kikubwa.

Kashfa na Aibu

Watu hawawaamini watu wenye matukio ya kutoka na mashemeji. Sidhani kama na wewe msomaji unaweza muamini mtu unaejua anaweza kutoka na mpenzi wako kwa siri.


Sasa ukitoka na shemeji na kugundulika, utapata kashfa ya “kutembea na mashemeji”. Kashfa hii itakufanya uone aibu na pia hautoaminika na watu kwenye jamii inayojua jambo hilo.

Msongo wa Mawazo

Kutoka na shemeji wa kike au wakiume kunaweza kukupatia msongo wa Mawazo pia. Watu wengi hujikuta kwenye msongo wa Mawazo baada ya kuingia kwenye mahusiano na shemeji zao. Na msongo wa mawazo huu unaweza kuwa unatokana na ujauzito wa Siri, manyanyaso ya kijinsia na vitu vingine kama hivyo.

Sasa kwanini kupitie hayo yote? Ni vema ukajiheshimu na kuheshimu mahusiano ya watu wengine ili kuyaepuka. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengi zaidi.

Sms za kulalamika kwa mpenzi wako (Mwanamke au Mwanaume)



Katika mahusiano ya mapenzi, si kila wakati mambo yanakwenda kama unavyotarajia. Kuna nyakati unaweza gundua kuwa mpenzi wako amebadilika, haonyeshi tena upendo na kujali kama zamani. Labda ameanza kuwa mbali, hajali hisia zako, au hata anaonyesha dalili za kuzingatia katika uhusiano wenu. Hali kama hizi zinaweza kuumiza moyo na kukufanya uhisi huzuni, mashaka, au hata hasira.

Pia, kuna wakati unaweza kugundua kuwa mpenzi wako amekusaliti kabisa. Hakuna kitu kinachouma kama kugundua kuwa mtu uliyempenda kwa dhati ana mtu mwingine au aheshimu uaminifu wenu. Usaliti unaweza kuleta maumivu makubwa na kukufanya ujihisi si wathamani.

Mtu unapopitia katika hali kama hizi, unaweza kuhitaji kumwandikia mpenzi wako ujumbe wa kulalamika, ili aelewe jinsi kitendo chake kilivyokuathiri na, pengine, abadilishe tabia yake , kiwezekana. Kutuma ujumbe wa kuelezea hisia zako kunaweza kuwa moja ya kutoa hisia zako na kufungua mzingo kifuani. Katika makala hii, tumekuandalia orodha ya sms za kulalamika ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ili kuelezea hisia zako kwa bila kupoteza muda.

Simulizi bora za kusoma katika The bestgalaxy BONYEZA HAPA>>>

Ujumbe wa kulalamika kwa mpenzi wako





Moyo wangu upo kwako ni vile tu Umeamua kuubuluza. Unayoyafanya yananiuza na Sina chakufanya kukukumbusha kuwa ulisema milele utanipenda. Ok, Fanya unachofanya ila milele usisahau ninakupenda!



Mimezikumbuka zile siku za furaha , zile siku tulikua tunatafutana kila mara na kuambiana hisia zetu. Na bado nakumbuka tuliambizana “unanipa furaha, sina mwingine, ni wewe tu”. Lakini sasaivi wewe sijui umepata mwingine kakubadilisha… eti ni umesahau???



Ulikuja kama mwanga kuyaangaza maisha yangu, ulileta matumaini na ndoto lakini ghafla unaniacha nikiwa nimevunjika moyo na kukata tamaa ya kupenda tena. Asante kwa yote lakini!



Natamani miaka ambayo nimekaa na wewe isingetokea katika Maisha yangu. Zile kumbukumbu nilizofurahia na wewe zinaniumiza kwasasa. Ninatamani kufuta kila kumbukumbu yako ila ndio hivyo uliniweza, nikakupenda kweli na sasa umenisaliti ninaumia.



Nitajuta milele vile nilikupenda bila kujua dhamira yako na kukuamini. Nilikupa kila kitu nilicho hisi kitakufurahisha; lakini katika malipo, umenitoa machozi kwa maumivu yasio isha.



Najitahidi kila mara kuwaza na kukufanyia mambo yatakayo kupa furaha lakini wewe umekua ukinilipa mambo yanayoniumiza. Najua hii inamaana; Pamoja na kukupenda, Bado haunipendi. Asante sana, naendelea kukupenda ila nimekuelewa!



Nilikupenda bila sharti lolote na bila kuuliza kurudishiwa ila ulichukulia upendo huo kuwa udhaifu wangu. Siwezi sema mengi ila umeniumiza vya kutosha sasa, niache niendelee na maisha yangu.



Nilikuamini kwa moyo wangu wote, lakini umeshindwa kuelewa hilo. Umenifanya nijifunze kuto kumuamini mtu hata nikimpenda sana. Ninakuchukia, lakini nashukuru kwa somo! Nashukuru kwa kunivunja moyo pia!

Huu ndio mwisho wa orodha yetu ila Kuna mambo mengi sana katika The bestgalaxy unaweza furahia. Kikubwa Endelea kuwa karibu nasi ili kujifunza mengi!

Kijana hizi ni athari za Wanawake wakubwa sana (Majimama/Mishangazi)




Wakati baadhi ya vijana Wakiume wanaongelea na hata kutafuta kabisa Majima au Mishangazi, hebu tunangalie athari zake. “Mishangazi” au “Majimama” ni majina ambayo kuna watu hutumia wakiwa na maana “Wanawake wakubwa wanaoingia kwenye mahusiano na vijana wadogo.” wanawake hawa wapo katika jamii zetu na kumekua na simulizi nyingi za vijana kujihusisha nao kimapenzi.

Mahusiano kati ya wanawake wakubwa na vijana yanaweza kuwa ni upendo toka moyoni kabisa. Yani wanaweza kuanza kwa mazoea ya kuwa karibu alafu mwisho, wakajikuta kwenye penzi zito. Ila kwakua wanasema, Mapenzi hayana umri, tunaweza sema ni jambo lisiloshangaza sana.

Lakini pia baadhi ya mahusiano ya namna hii huwa ni kama wanabadilishana pesa au maisha mzuri kwa mpenzi. Yani hapa Kijana wa kiume anawezakua anatoa mapenzi huku Mwanamke mkubwa akitoa pesa au maisha mzuri kwa Kijana. Kwaiyo Kuna namna Kijana wa kiume anaweza faidika hapa.

Pamoja na yote ambayo kijana wa kiume anaweza pata au kufaidika kwenye mahusiano ya namna hii, Bado sio Mahusiano salama. Kijana anaweza pata athari mbaya kubwa kwenye maisha yake anapokua na majimama au Mishangazi. Athari zinazo zungumziwa hapa ni zifuatazo:

Kijana hizi ni athari za Wanawake wakubwa sana (Majimama/Mishangazi)

Magonjwa



Kama tunavyo fahamu, magonjwa kama vile HIV huwa yanaweza ambukizwa kwa kushariki Ngono zembe. Ngono zembe ni kushiriki tendo la ndoa bila Kinga yoyote.

Kama upo kwenye mahusiano na mwanamke mkubwa, Tendo hili linaweza kuwa ni tendo la kawaida sana. Mnaweza zingatia kinga siku ya kwanza lakini ya pili mukazitupia mbali kwa kuamini haziwafurahishi kwenye tendo.

Sasa ikiwa mmeamua kutotumia Kinga Kuna hatari kubwa ya kuambukizana virusi ya ukimwi na magonjwa mengine.


Kuwachukulia poa wanawake wengine



Kijana wa kiume anapoingia kwenye mahusiano na mwanamke mkubwa anaweza jikuta anaanza kudharau mwanamke wa umri wake. Yani anaweza anza wachukulia poa sana mwanamke wa umri wake maana tayari anaoneshwa au kufanyiwa vitu vingi ambayo wanawake wengine hawafanyi.


Hali hii inaweza kumfanya huyo Kijana ajiamini sana anapokua na Mwanamke wengine. Lakini kujiamni huko ni matokeo ya kugundua kuwa mwanamke wengine hawajui mapenzi.

Kugeuka tegemezi


Kijana wa kiume akipata mwanamke mkubwa anaempa pesa kisa mapenzi, kuna hatari kubwa ya huyo Kijana kuwa tegemezi kwenye maisha yake. Anaweza fikia wakati hata akiachwa na jimama anaona maisha yake yameharibika.


Kwa kawaida mwanaume anatakiwa kubeba Majukumu, kujitegemea na kutegemewa. Huyo mwanaume akizoeshwa kutegemea mwanamke, inakua ni ngumu kwake kuchukua Majukumu, kujitegemea na kutegemewa tena. Huo kwake unakua ni mzigo mkubwa sana.

Kuingia kwenye migogoro



Baadhi ya wanawake wanaoitwa “Majimama” au “Mishangazi” ni wake za watu au Mama za watu. Kutokana na hili, pamoja na yote wanayofanya, Bado ni wanawake ambao wana ndungu na jamaa kwenye maisha yao.

Kijana anaweza ingia kwenye migogoro ya kifamilia bila kujua. Ukiwa kama kijana, unaweza kuwa chanzo cha mke na mume kukosana, unaweza chukiwa na watoto wake au ndungu. Mongogoro mingi inaweza kuibuka hapa.

MZIGO WA WAKUBWA 01  (Simulizi ya Kusoma)




Tulikua tupo mimi na rafiki yangu Samsoni kwenye chumba chetu tunacholala ambacho watu huita Geto. Ilikua mida ya kama saa moja au mbili usiku hivi alafu muda huo rafiki yangu alikua ananihadithia mechi ya mpira ambayo imetoka kumalizika saa 2 zilizo pita na sikwenda kuiangalia kwenye vibanda vya mpira siku hiyo kutokana na mawazo. Mawazo yalifanya kichwa changu kiwe vibaya sana muda huo kiasi kwamba nilikua naonekana kumsikiliza Samsoni lakini kiukweli nilikua hata simuelewi japo nilikua nacheka kila akicheka na kuitikia “Ebwana ee” ili asigundue kua akili yangu haipo kabisa kwenye anayonisimilia.

Katikati ya hadithi zake za mpira tukasikia simu imeanza kuita katika kisehemu tunachozichaji simu kilichokua pembeni kidogo ya dirisha la chumba hicho. Simu yangu na ya Rafiki yangu Samsoni, zote zilikua zipo chaji alafu simu yangu niliichomeka chaji ikiwa imezimwa. Hivyo simu iliokua ikiita muda huo ilikua ni ya rafiki yangu na tuliigeukia wote ilipokua inaita maana ilitushtua kwa kupiga kelele katikati ya maongezi. Baada ya hapo Samsoni  alinyanyuka huku akijisemesha “Sijui nani huyu… itakua watu wa mpira hawa” alafu akaenda kuichukua ile simu mimi nikiwa namuangalia tu. Alipoishika simu na kusoma jina, nilimsikia akasema “Ah wewe Mpenzi wako huyu ananipiga huku. Sijui umekifanya nini tena kitoto cha watu”

Mimi nikashtuka kidogo alafu nikamuuliza “Ni Sabrina?” Samsoni alijibu “Ndio” alafu akasema tena “Ngoja nipokee nimsikilize” huku akiipokea simu na kuiweka sikioni. Mimi muda huo nilitaka nimwambie asipoke ila alikua ameishapokea kabla hata sijanyanyua mdomo kumwambia. Baada ya Samsoni kupokea simu, nilimsikia akisema “Halo Dada… niambie” alafu nikasikia kisauti kidogo cha Sabrina akasema “mambo vipi?” Samsoni akaitikia “kama kawa, vipi huko?”  Sabrina akasema “safi. Mbona rafiki yako hapatikani kwenye simu? Upo nae hapo?”. Mimi kusikia hivyo nikashtuka, nikamwambia kwa ishara rafiki yangu Samsoni asiseme yupo na mimi.

Samsoni alinielewa akamjibu “Sipo nae. mimi niko mbali kidogo muda huu”. Sabrina alipoambiwa hivyo, akasema “Sawa, ukionana nae mwambie namtafuta” Samsoni akajibu “sawa” kisha simu ikakatwa. Baada ya hapo rafiki yangu alirudisha simu kwenye chaji huku akisema “Haya si umesikia? Eti anakutafuta. Sauti yake tu inaonekana mmezinguana nyie. Huu ugomvi siingilii” mimi nikacheka kwanza kidogo alafu nikasema “nitamcheki baadae”.

Baada ya hapo Samsoni aliniaga kuwa anatoka kidogo hivyo mimi nilibaki mule ndani nikiwa nimetulia tu ila kichwani kwangu mawazo ni mengi sana. Wakati akiondoka alisema pia “Alafu nilipokua anaangalia mpira, Tino alinipigia akaniambia amekutafuta hakupati hivyo umpigie” mimi nikaitikia “Ah sawa”.

Nilipokua pekeangu mule ndani, Mawazo yalinituma ninyanyue godolo tunalolatila maana Samsoni alikua anatabia ya kuweka pesa huko. Nilipofanya hivyo, nilizikuata pesa zake nyingi kiasi na nikazichukua maana niliona kama zinaweza nisaidia katika hali niliokuanayo kwenye wakati huo. Nilikua ni kama na muibia Rafiki yangu kabisa ili tu niweze kukimbia tatizo linalonipa Mawazo.


Mawazo niliokuanayo siku hiyo yalikua yamesababishwa na matokeo ya mimi kuanza kuzifungua kurasa za mapenzi katika maisha yangu. Nakumbuka miaka michache iliopita kambla ya siku hiyo nilikua nasoma sekondari kidato cha tatu na nilikua nasoma shule za kutokea nyumbani. 

Tangu nilipoanza sekondari nilikua sijawahi jihusisha au kuwaza kuwa na mpenzi shuleni japo nilikua natamani. Hii ilikua ni kutokana na mambo mengi ikiwemo sheria za shule zilizokua zikikumbushwa kila siku na walimu. Na pia nilikua nawaogopa wazazi wangu kuniona nimejiingiza kwenye maswala ya mapenzi. Mbali na hayo, nilikua naogopa sana jinsia tofauti. Kuwasogelea na kuongea nao kulikua ni mthihani mkubwa sana kwangu kipindi hicho, hasa akiwa ananivutia.

Kwenye mambo ya kufanya vizuri shuleni kwa bahati mbaya nilikua siko sana huko. Uwezo wangu katika madaftari na mithihani ulikua wa kawaida sana. Nakumbuka darasani nilikua nakaa viti vya nyuma sana. Huko nyuma nilikua nakaa na rafiki zangu wawili ambao mmoja wapo ndio huyo  anaitwa Samsoni, alafu kuna mwingine alikua anaitwa Tino. Kwaiyo tulikua kama tuna kikundi cha watu watatu nyuma ya Darasa. Darasa letu lilikua lina viti vinavyo ruhusu kukaa wawili na kiti nilichokua na kaa mimi, tulikua tunakaa mimi na Samsoni ila mwalimu akitoka tu, Tino alikua anakuja kwenye kiti kile, tunajibana watatu, tunapiga stori. Tino alikua anakaa kiti cha pembeni yetu ambacho kilikua karibu sana na sisi.

Tino alikua ni mwenzetu ila mambo yake yalikua mengi mno. Alikua ni msumbufu sana kiasi kwamba kila mtu alikua anamjua kwa usumbufu wake hapo shuleni. Watu walianza kumjua baada ya kuletwa na mzazi wake shuleni na kupigwa kutokana na kutolala kwao pamoja na kutokuja shule kwa siku 5 mfululizo katika kidato cha kwanza.

Tulikua tuna shirikiana sana Tino lakini usumbufu wangu haukufikia usumbufu wa Tino. Samsoni nae  alikua kama mimi tu, hakumfikia usumbufu Tino hata kidogo. Ila katika mambo ya kwenye vitabu, wote tulikua hatufanyi vizuri sana japo hatui wamwisho Darasani. 

Kuna siku asubuhi tulikua watatu Darasani kule nyuma ya Darasa tunapiga stori kwa kujiachia lakini ghafla akaingia mwalimu. Alivyoingia tu, tukafunga midomo alafu kila mtu kati yetu alikaa vizuri anapokaaga kisha watu wote darasani tukasimama kumsalimia Mwalimu. Baada ya kumsalimia, akaturuhusu tukae alafu nikakuta tu anasema “Nyie watatu uko nyuma hebu simameni”. Mh alivyosema hivyo nikawa nawaza “Anaongelea mimi na rafiki zangu au? Mbona anaangalia huku nyuma?” wakati najiuliza nikakuta mwalimu anasema tena “Nyie muliokua mnapiga kelele mpaka darasa zima mnasikika nyie huko nyuma simameni kabla sijawafuata.” Basi mimi nikaona huenda anatuongelea sisi, nikasimama na bada ya mimi kusimama, nikakuta na Rafiki zangu wawili wanasimama.


Baada ya hapo mwalimu akaanza kufoka “Hivi nyie mna matatizo gani? Inamana hapa shuleni mmekuja kupiga makelele au?” baada ya kusema hayo akaninyoshea mkono na kusema “Wewe hapo wewe inaonekana msumbufu maana hata Nywele haujanyoa. Hizo nywele ni siku ya ngapi nakwambia sitaki kuziona? Hebu sogea hapa mbele” mimi nikiwa mnyonge sana nilisogea taratibu pale mbele ya Darasa. Mwalimu aliniuliza “Unataka ni kupige ndio uanze unijibu?” mimi nikiwa naogopa sana nikamjibu “Hapana, samahani mwalimu nilitaka kunyoa jana ila umeme walikata”. Baada ya kumjibu mwalimu alifikilia alafu akasema “Kesho nisione hizo nywele, sawa!?” nikamjibu “Sawa” alafu nikakuta ananiambia “Na kule nyuma unakokaa, uhame. Kabebe madaftari yako kule nyuma uyalete hapa mbele kwenye hiki kiti ambacho hakina mtu”.

Baada ya mwalimu kusema hivyo nilishtuka maana nilikua sijazoea kukaa viti vya mbele ya Darasa, nikamwambia “Mwalimu hapo wanakaa watu wawili, itakua wameitwa nje”. Mwalimu akasema “Hatakama wakija hao wanao kaa hapa, waambie mimi ndio nimekuweka hapa. Kwanzia leo utakua unakaa hapa mbele. Nawakija hao, waambie wachukue kiti kingine wakae sehemu nyingine ila sio hapa”. Dah nilikua mnyonge sana siku hiyo, nikachukua vitu vyangu nyuma ya Darasa na kuhamia mbele ya darasa huku mwalimu akiniangalia.


Baada ya kukaa mbele mwalimu alianza kufundisha somo lake maana ndio ulikua muda wake huo. Mimi pele mbele nilikua sina amani kabisa maana sijazoea kukaa hapo alafu mbali na hilo, Daftari la mwalimu huyo nilikua sina. Lakini mwalimu alipoanza kufundisha nilichukua kidaftari flani cha ajabu, nikakiweka pale mbele ili kuzuga.

Nakumbuka baada ya kama dakika 10 hivi Mwalimu alipoanza kufundisha, alikuja mwalimu Mkuu akiwa ameambatana na wanafunzi kama watano hivi na mwanafunzi wa kike alikua mmoja. Darasa zima tulijikuta tunavutiwa kumuangalia yule mwanafuzi wa kike. Mwalimu mkuu alianza mazungumzo na Mwalimu aliekua Darasani na mazungumzo yao yalikua ni kwamba hao wanafunzi watano ni wageni na kwanzia siku hiyo watakua wanasoma humo Darasani. Walimu walipomaliza kuzungumza, wale wanafunzi wakaingia ndani ya Darasa alafu yule Mwalimu aliekua Darasani akawaambia watafute nafasi za kukaa mule Darasani. Kabla hata hawajapiga hatua sana, nikakuta mwalimu ghafla anamwambia yule mwanafuzi mgeni wa kike “Wewe usiende huko. Kaa hapa na huyu”. Mimi moyo ulishtuka sana maana alikua anamuelekeza yule Mwanafunzi wa kike akae na mimi kwenye kiti kimoja. Kiukweli mimi nilikua naogopa kukaa na jinsia tofauti hasa wakiwa wazuri ndio napoteza uhuru kabisa yani. Na Mwalimu alikua anamzingatia yule mwanafuzi wa kike kwa kiasi flani, kama ni ndugu yake hivi.

Nakumbuka yule mwanafunzi alikaa na mimi pele huku akiwa na viaibu aibu vya ugeni alafu na mimi wakati huo nina viaibu vya kumuogopa.  Tukiwa tumekaa  pale mwalimu aliwauliza jina wageni wote waliokuja na nilisikia yule Mwanafunzi wa kike akijitambulisha kuwa anaitwa Zuwena.  Basi baada ya hapo mwalimu aliendelea kufundisha na mimi nikawa kama namsikiliza  hivi ingawa akili yangu ilikua inahama. Yani nikua nikitupa jicho langu mara moja moja kwa yule Mwanafuzi wa kike kumuangalia jinsi alivyo. Japo nilikua naogopa, ila alikua anavutia sana kumuangali alafu alikua msafi sana. Kuna muda nilimtupia macho tukagongananae alafu akaona viaibu. Mimi nilipogongananae macho nilishtuka na nikaingiwa na woga zaidi ila woga ulipungua nipowaza “ Inamaana na yeye ananiogopa huyu. Dah ila mzuri mpaka raha. Ingawa naogopa ila hapa nijitahidi niwe hata rafiki yake tu. Sina hata rafiki wakike ujue”. Nakumbuka niliwaza mambo mengi sana kuhusu huyo mgeni bila kujua kuwa ndio namuingiza moyoni hivyo mtoto wa watu.

Baadae, mwisho wa kipindi cha mwalimu aliekua akifundisha ulifika na mwalimu alituachia maswali ya kufanya nyumbani tuyaandike alafu akasema anaondoka. Lakini kabla hajaondoka akasema “Nyie muliofika leo hakikisheni munaazima madaftari Kwa wenyeji ili muandike vitu vyote vya nyuma. Wewe Zuwena utachukua Daftari kwa huyo uliekaanae hapo, sawa!?”. Nikiwa pembeni ya Zuwena nikamsikia Zuwena akiitikia “Sawa” huku nikiwa nimeshtuka mno maana Daftari wanalo liongelea sina. Kichwani nikaanza kuwaza “Hapa mbona kama naenda kuumbuka kwa mgeni sasa. Huyu mwalimu na huyu mgeni wanajua Daftari ni hili lililopo Mezani lakini ukweli ni kwamba sina Daftari. Nikijieleza kwa huyu mgeni kuwa sina daftari, nitaonekana mjinga sana kwake na naweza shindwa kuwa rafiki yake. Dah tena anaonekana anaakili sana huyu, ntaumbuka leo.”



INAENDELEA…

Ujumbe mzuri kwa Mke au Mume aliye mbali na wewe

Katika maisha ya ndoa, kuna nyakati ambazo wanandoa wanalazimika kuwa mbali kwa sababu mbalimbali kama vile kazi, masomo, au majukumu mengine ya maisha. Ingawa umbali unaweza kuwa changamoto, ni muhimu kuendelea kudumisha mawasiliano na kuonyesha upendo na kujaliana hata mkiwa mbali. Kwa bahati nzuri, ujumbe wa maandishi ni njia rahisi na ya haraka ya kufikisha hisia kwa mke au Mume, huku ukimpa moyo na kumhakikishia kuwa yupo akilini kila wakati.

The Bestgalaxy, katika makala hii tumekusudia kutoa mifano ya ujumbe mzuri kwa mke au mume aliye mbali. Ujumbe huu unaweza kumtia moyo, kumfariji, au hata kumpongeza kwa kukuweka moyoni, bila kujali umbali uliowatenganisha. Maandishi haya madogo lakini yenye maana kubwa yanaweza kuimarisha uhusiano wenu na kumfanya mwenzako ajisikie kupendwa na kuthaminiwa hata akiwa maili nyingi kutoka kwako.

Mambo ya kuzingatia katika kuwasiliana na mpenzi aliye mbali BONYEZA HAPA>>>

Ujumbe mzuri kwa Mke au Mume aliye mbali na wewe

  • Tupo mbali ila unavyonionesha upendo ni kama nipo karibu na wewe. Nakupenda na sitoacha kukupenda maana nililiandika Jina lako kwenye moyo wangu kwa wino usiofutika milele.


  • Kwenye familia yangu wewe ni malkia, mama watoto wangu na ndio familia yangu kiufupi. Kila nikikumbuka unavyonipenda, kunipa furaha, kunisaidia na kusimama nami, najiona nimekupata kama bahati. Ni maisha tu yananiweka mbali nawe ila nakupenda na natamani nirudi.

  • Nipo mbali kwasasa ila tambua Moyo na Mawazo yangu vipo kwako. Kila siku yangu ya huku haiwezi kuwa sawa bila kajua hali yako. Nakupenda sana na nakuahaidi kutunza penzi letu mpaka tutakapo onana.


  • Wanasema “Umbali si kitu kwenye mapenzi ya kweli”. Umenifanya niamini hivyo kwasababu haujapunguza penzi lako kwangu. Umekua na mimi kwa simu kila moyo unapohitaji, tumekua wanandoa ambayo ni marafiki kwenye kila hali. Nakupenda sana na asante kwa kuwa nami.
  • Huwa nakuona kwenye ndoto zangu. Na hata nikifumbwa macho kwenye maisha siku hizi sioni giza, nakuona wewe mwanga wangu. Asante kwa kuwa rafiki na mshauri na mzuri kwangu. Usijesahau kuwa nipo mbali ila nakupenda sana.

  • Ni wanawake wengi huitaji mahusiano ila wachache hukubali kuwa Mama. Asante kwa kukubari kuwa mama watoto wangu. Pia ni wanawake wechache huvumilia mume anapokua mbali lakini wewe unafanya hivyo. Asante kwa kuniheshimisha na sichoke kuniheshimisha. Nakupenda sana mke wangu.


  • Mungu akulinde huko uliko mume wangu. Unapambana sana juu ya maisha yetu. Naweza kuwa sipo vizuri katika kukushukuru kwa kila jambo ila tambua nakupenda na kukuombea kwenye kila unalofanya. Nakupenda sana mme wangu.

  • Nakukumbuka kila mara Mme wangu. Siku ya kuonana na wewe naiona kama ipo mbali sana ila kamwe siwezi punguza upendo wako. Naomba kwa mungu nafasi zetu ziwe pamoja milele, na akusaide kwenye kila jambo lako kipenzi.

Unapomtumia ujumbe mzuri mke au mume wako aliye mbali unamkumbusha kuwa unampenda, unamjali na haujamsahau. Kwaiyo jambo hili ni muhimu sana katika Mahusiano.