Kuna uwezekanao wa kuwa na mambo mengi sana yanayoweza kusukuma mtu kukopa pesa za watu wengine au taasisi mbali mbali za kifedha. Na kukupa ni jambo zuri sana maana kuna muda mtu unaweza kukwama kifedha kwa kukumbana na jambo linalohitaji pesa ambayo hauna lakini ukalimudu kupitia mkopo.
Kuna watu hukopa pesa ili kurekebisha mambo yao yalioenda vibaya na kuna hata ambao hukopa ili kulifanikisha jambo lisilo na ulamazima sana. Kukopa kwasababu yoyote ile ni uamuzi mzuri lakini itakua uamuzi mzuri zaidi kama umefanikiwa kwenye jambo lako na kuulipa mkopo wako. Kama haujakamilisha jambo lako au umefanikisha lakini haujafanikiwa kulipa deni la mkopo wako, uamuzi wa kukopa unaweza kuwa mbaya kwako. Na endapo hali yakushindwa kulipa itakua inakuandama kila mara unapokopa ni vema ukaanza kujiweka mbali kidogo na mikopo.
Hapa The bestgalaxy tunakupa tabia ambazo mara nyingi zikiwa ndani yako basi mikopo huwa karibu sana na pia huwa ni ngumu kuilipa. Sio kila mtu mwenye madeni au anaeangukia kwenye madeni anatabia hizi. Ni baadhi ya watu tu ndio huwa na tabia tunazoenda kuzielezea hapa. Niwesema hivyo maana wengine husukumwana na vitu vilivyo nje kabisa na uwezo wao au sababu myingine mabali na tabisa hizi.
Mambo unayotakiwa kujua kuhusu simu za mkopo BONYEZA HAPA>>>
Epuka kukopa pesa kama unatabia hizi ndani yako
Kushindwa kuzirudisha pesa zako mwenyewe
Kama ni mtu mwenye malengo na huwa unajiwekea pesa kwaajili ya mambo mbalimbali basi kuna muda unaweza kuwa unajikopa mwenyewe. Yani unachukia pesa ulizojiwekea kwaajili ya jambo flani na kuzitumia kwenye jambo lingine tu huku ukiwaza kichwani “Nitazirudisha”. Ikiwa unatabia hiii na unakua na msimamo wa kuzirudisha tena hizo pesa basi unaweza usiteseke sana kulipa hata ukikopa kwa watu wengine. Lakini kama huwa haurudishi pesa hizo na ni tabia yako, kunaweza kuwa na ugumu pia unapokopa kwa wengine. Ni vema ukajaribu kujiimarisha ndani yako kabla ya kukopa kwa wengine. Hakikisha unapambana sana kurudishia pesa sehemu zako za dani ukichukua pesa.
Jinsi ya kupata Mkopo kwenye simu BONYEZA HAPA>>>
Kuhairisha mipango yako ulioianza
Kuna baadhi ya watu huwa na mipango ya biashara na Mambo mengine yanayoweza kuhitaji pesa ili kuingiza pesa. Kukopa kunaweza kuwa ni wazo la haraka kwa mtu mwenye mipango ya namna hii lakini hana mtaji au pesa inayohitajika.
Kukopa sio kitu kibaya kama umekusudia kuanza kupambana kutimiza mpango uliojiwekea. Lakini kama ni mtu unaempenda kuhairisha mipango ulioianza, kukopa kunaweza kuumiza.
Ukichukua Mkopo kwaajili ya mpango flani lakini ukahairisha na kwenda tofauti na mpango huo, kunakua na hatari kubwa ya kupoteza pesa hiyo. Pesa ikiisha bila kufanya kitu kilichosababisha ukope, unaweza jilaumu kuliko ungefanya na kushindwa.
Kama haujaweka vizuri mipango yako au haupo tayari kuipambania kwa asilimia 100, basi usikope pesa kwanza.
Kusahau shinda unapokamata pesa yoyote
Hali yako huwa inakua vipi muda ambao hauna pesa? Na hua inakua vipi ukipata pesa? Kama ukipata pesa yoyote mkononi mwako shida huwa unazisahau, unafanya matumizi na kuacha kabisa kutafuta pesa basi kukopa kunaweza kuwa kubaya kwako. Ukikopa pesa na kuishika mkononi pesa hiyo inabidi iwe kichwani kwako kuwa sio pesa yako na unahitajika kulipa. Hii inaweza kukusaidia kupata mpango wa kuilipa na kuwa makini unapozitumia pesa hizo za mkopo.
Ikiwa utaruhusu pesa hiyo ikusahaulishe shida na kuichukulia ni yako, basi unaweza kuwa ndio mwanzo wa kupuuza deni lako, kuridhika na kuanza ikiutumia pesa.
Usiache kuiona pesa ya Mkopo kuwa ni Mkopo hata ikiwa na mamilioni ya pesa.
Haupendi kudaiwa.
Kutopenda kudaiwa ni jambo zuri sana ila linakua zuri kama utakua na uwezo wa kujikumbusha mwenyewe kulipa pesa kabla haujadaiwa. Mbali na hapo ukiwa haupendi kudaiwa itabidi uanze kuepuka kukopa pesa maana kudaiwa ni lazima na ukichukia au kumfanyia vibaya anaekudai itakua ni kosa kwako tu kivyovyote maana umeshindwa kutimiza makubaliano. Wengine hufikia mpaka hatua ya kupambana kukata kulipa Kwasababu ya kudaiwa vibaya lakini hawajihukumu kwa kuchelewesha pesa muda mrefu kinyume na makubaliano.
Natumaini umesoma na kuelewa makala hii na inaweza kuwa msaada katika Maisha yako kwenye upande wa kukopa. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi.
