Tag Archives: Mahusiano

Kutongoza: Jinsi ya kumpata Mwanamke unaempenda 2026

Katika kipindi hiki wanaume huongea sana kuhusu wanawake na mahusiano lakini hii haimaanishi swala la “Kutongoza” linawezwa na kila mtu. Swala hili bado ni gumu kwa vijana wengi na ugumu wake huwa unawapelekea kupata wanamke wanaojitokeza kirahisi tu, na sio wanaowataka au kuwapenda.


Kwa wasio jua vizuri ulimwengu huu, Makala hii ina hatua ambazo mwanaume unaweza fuata kumpata kila mwanamke unaemuhitaji.


Kuna umuhimu mkubwa wa kijana kujua namna ya kutongoza mwanamke anaemtaka. Huwa kunasaidia hata kupata mwanamke sahihi maishani maana mtu usipojua kuwakamana, itakua ngumu kupata mwanamke unaemuona ni sahihi.

Maswali ya kumuuliza mpenzi wako mpya BONYEZA HAPA>>>

Hatua za kumpata Mwanamke yoyote unaempenda 2026

1. Mchunguze ni mtu wa namna gani na anapenda nini

  • Kabla ya kuwa na ukaribu na mwanamke unaemtaka, hakikisha unamchunguza kwanza. Hapa nazunguzia kuangalia yeye ni mtu wa namna gani na anapenda nini katika mahusiano au maisha yake kwa ujumla.
  • Hatua hii itakusaidia kujua unaingia vipi kwenye maisha yake. Kama anapenda pesa sana na unataka kuingia kwa namna hiyo, basi utajua hapa. Kama unaweza kukuelewa bila pesa, unona kwenye hatua hii pia.

2. Tengeneza ukaribu kupitia unachokijua kwake

  • Ukishajua mambo flani kuhusu yeye, inaweza kuwa ni rahisi sasa kuanzisha ukaribu nae. Unaweza anza ukaribu kwa kuongea nae kidogo kuhusu mambo ambayo ni mbali kabisa na mahusiano. Hii inaweza kuwa ni kuongea vitu kuhusu biashara anayoifanya, kumuomba msaada kwenye kitu flani anachokiweza au onyesha kumjalia na hata ukimtania tu kwenye vitu vitakavyo mfurahisha sio mbaya.
  • Kiufupi unakua ni kama unaingia kwenye maisha yake kiasi cha kuanza kumzingatia na kuwasilinana kwenye simu kuhusu jambo flani au kuongea nae tu pale mnapokutana. Lakini wakati unajisogeza kwake kutengeneza ukaribu, hakikisha haujengi mazoea nae sana. Fanya kila kitu unachokifanya ili kuwa karibu nae lakini mazoea yawe kwa kiasi tu.

3. Angalia muitikio wake juu ya ukaribu wako

  • Ukishaweka ukaribu nae, anza kuangalia muitikio wake juu ya ukaribu wako. Yani angalia kama anafurahia au amekubali kirahisi wewe kuwa karibu yake.
  • Unaweza ona mambo haya kwenye namna anavyo jibu ujumbe wa simu, namna anavyokuzingatia mkikutana na hata jinsi anavyoongea na wewe.
  • Kupitia muitikio wake juu yako, unaweza hata kuona dalili za mapema za kufanikiwa kwenye jambo lako.

4. Tafuta muda mzuri wa kumwambia kuwa unampenda na umwambie

  • Baada ya kujiweka karibu na akaonesha muelekeo wa kutambua ukaribu wako kwake, basi ni muda wa kumwambia ukweli. Kupitia ukaribu mulionao, tafuta wakati mzuri ambao utaanzisha mazungumzo ya kueleza hisia zako. Hii inaweza kuwa kwenye simu au kwa kuonanae kabisa.
  • Kama ni kwenye simu, unaweza anzisha mazungumzo yako muda ambao unajua atakua ametulia(mfano; usiku, muda wa kulala). Kama ni ana kwa ana, unaweza muita au kukutananae mahali ili kumwambia hisia zako.

Wakati kufanya hayo yote, zingatia heshima. Baadhi ya wanawake unaweza kuwakosa kwasababu tu umewavunjia heshima. Wanawake huwa wanajali na kuangalia vitu vidogo vidogo alafu wanakuweka kwenye makundi. Kwaiyo unaweza kuwa na kila ushawishi lakini ukatupwa mbali au kuchezewa akili kwasababu ya mambo madogo kama dharau.

SMS za kumtakia Mpenzi Asubuhi njema 2026

Ndani ya mahusiano mazuri ya mapenzi, huwa wapenzi wanapeana maneno mazuri. Maneno mzuri yanaweza kudharaulika na watu wengi kwenye mahusiano lakini nguvu yake ni kubwa mno. Huwa yana nguvu ya kugusa moyo wa mpenzi na kurekebisha pale ambapo haupo sawa.

Ukiwa kama mtu unaempenda mwenza wako, ni muhimu kutoa maneno mazuri kwake. Usiishie kusema “Nakupenda” siku ya kwanza kisha ukaacha kumpa maneno mazuri kwasababu tu amekukubalia kuwa kwenye mahusiano. Ndani ya mahusiano unatakiwa kutoa maneno mazuri katika mazungumzo yako ya simu au ana kwa ana.

Hapa chini, The Bestgalaxy tumeandaa ujumbe/Sms za kumtakia mpenzi asubuhi njema ambazo ni mpya katika mwaka 2026. Hii ni kwaajili ya watu wanao tumia sms kutoa maneno kwa wapendwa wao lakini wanahitaji kuandika ujumbe bila kuumiza kichwa sana.

Mambo ya kuzungumza na mpenzi wako ili kudumisha mahusiano BONYEZA HAPA>>

Sms za kumtakia asubuhi njema mpenzi wako 2026

Japo sipo hapo ulipo ila matumaini umeamka salama. Ni asubuhi nyingine hii mpenzi wangu, nimeaka nikiwa nakupenda kuliko jana.

Mapenzi yako nayaota mpaka ndotoni maana umekua ndio furaha yangu kubwa kwenye maisha. Amka siku yangu iwe poa wewe Malaika.

Uwe na siku njema kipenzi. Chochote utakachofanya kwenye siku yako, usisahau kuwa nafasi ya kupenda ya moyo wangu ilikua inakusubiri wewe tu. Umeipata sana na nakupenda sana.

Kuna muda tukiwa mbali, moyo wangu hupata maumivu na mashaka. Lakini maumivu na mashaka hupotea ninapokumbuka kuwa wewe ni wangu, na mimi ni wako. Nakutakia asubuhi njema mpenzi wangu.

Kila asubuhi inapofika huwa napata wazo la kumjulia hali mtu nnaempenda hapa Duniani. Ndio maana kila asubuhi nakusumbua wewe. Vipi, umeamka salama mpenzi?

Nakutakia siku nzuri kama ulivyo, huo moyo wako uendelee kunipenda kama ninavyokupenda. Na hata tusipoelewana, naomba Mungu atukumbushe kuwa tunapendana.

Sihitaji kuona Nyota njema asubuhi ili kuwa na siku njema. Mimi huwa nakuhitaji wewe tu kipenzi. Umeamka salama kweli?

Kila siku ninapoamka, unaekuaja akilini ni wewe mpenzi. Nahisi kukuhitaji kama pumzi yangu, unanivutia kuwa karibu yako na nakuona ni kila kitu kwangu.

Hizo zote ni sms nzuri za asubuhi njema kwa mpenzi wako. Unaweza chagua ujumbe mzuri unaoona atafurahia zaidi ndio ukatumia kama salamu ya asubuhi. Lakini epuka kutumia sms moja kwa kurudia kila mara maana utazoeleka na kuonekana hauna jipya kwa mwanamke au mwanaume wako.

Ishara 5 za Mwanamke Anaekuchukia kwenye Mahusiano

Mwanamke anaweza kukupenda na mukaingia kwenye mahusiano ya furaha sana. Lakini katika mahusiano yoyote, mambo yanaweza kubadilika na akaanza kukuchukia au kutokukupenda tena. Hii hutokea pia kwa wanaume, lakini kwa sababu tunazungumzia mwanamke, hebu tuchimbe zaidi.

Mwanamke kukuchukia katika mahusiano huwa kunakuwa na sababu. Inaweza kuwa umemkosea, amepata mtu mwingine, au ameona mahusiano hayo hayamfaidi kutokana na matarajio yake. Mara nyingi ni vigumu kwa mwanamke kusema moja kwa moja kuwa hakupendi tena, lakini kuna ishara ambazo ukiziona, unajua kabisa kuna kitu kimebadilika.

Jinsi ya kupata Mpenzi mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Ishara 5 za mwanamke anaekuchukia kwenye mahusiano

1. Hajibu SMS wala kupokea simu zako

Kama mwanamke anakupenda, ni lazima azingatie mawasiliano. Atapokea simu zako na kujibu ujumbe wako hata akiwa busy.
Lakini akiwa anakuchukia, hupuuza sana simu na ujumbe wako. Simu zako huwa kama usumbufu kwake, ujumbe wako unaweza kusomwa lakini usijibiwe. Hii ni ishara kuwa upendo umepungua au haupo kabisa.

2. Anasema yupo busy kila mara

Ni kweli binadamu anaweza kuwa busy sana, lakini si kwenye vitu anavyovipenda. Mara nyingi tunapata muda kwa watu tunaowapenda hata tukiwa na shughuli nyingi kuliko muda. Ni ngumu mtu kuwa busy kiasi cha kukosa muda kabisa kwa mtu anayempenda, hasa kwa wanawake.

Lakini mwanamke akikuchukia, atakuwa busy kila mara. Hatakupa muda wake, wala hatataka umpe muda wako.

3. Hataki mkutane tena

Kama mwanamke mlikuwa mnapanga kukutana na mnatimiza, lakini ghafla hataki tena, hiyo ni ishara mbaya. Mwanamke asiyekupenda anaweza kuanza kukukwepa kila linapokuja suala la kuonana.

Anaweza kuweka mgomo wa kukutana kimwili na hata kuonana kwa maongezi ya kawaida. Anaweza kutafuta kila sababu ya kutokua huku akikupa ahadi hewa za kuonana mfululizo mpaka pale utakapogundua mwenyewe kuwa hataki.

4. Mengi unayofanya yanakuwa mabaya kwake

Mwanamke anaekuchukia huwa anaona mabaya yako tu hata ukijitahidi kuwa mzuri kwake. Unaweza kufanya mambo mazuri ili kuugusa moyo wake, lakini ukaambulia dharau na lawama.

Yani unaweza kujikuta unakosea kila unachofanya, hata kama makosa hayo hayakuhusu.

5. Hakutambulishi kwa watu wake wa karibu

Mwanamke akikupenda kweli huwa ni ngumu kuwaficha watu wake wa karibu kuhusu wewe. Anaweza kuwaambia marafiki zake kuwa yupo kwenye mahusiano, na hata kukutambulisha kwa ndugu zake.

Lakini kama anakuchukia, ni ngumu sana kukutambulisha kwa watu wake au kuwaambia wale walio karibu naye kuhusu uhusiano wenu.

Maneno ya kumsifia mwanamke wako kwa kiingereza/English

Kuna njia nyingi za kumfurahisha mpenzi wako bila gharama yoyote. Njia moja muhimu ni kumsifia. Wanawake wengi wanapenda kusifiwa, si tu kwa muonekano bali pia kwa mambo wanayofanya vizuri. Kumsifia mwanamke kunaweza kumfanya akuzingatie zaidi na kuimarisha uhusiano wenu. Hakuna mtu asiyependa kusifiwa, lakini wanawake hupenda zaidi hisia hii.

Kama mwanaume unaempenda mwanamke wako, ni vyema kuwa na tabia ya kumsifia kimuonekano au kwa mambo mazuri anayofanya. Hakuna haja ya kuzidisha sifa, lakini kumsifia pale anapoonekana vizuri au anapofanya mambo vizuri kunamfurahisha, kumongeza ujasiri, na kumhamasisha kufanya vyema zaidi. Yaani kumsifia kwenye upande wa mapenzi, biashara au kazi, kutamfanya ajiamini kwenye mambo hayo na azidi kufanya vizuri zaidi.

Katika upande huu wa kumsifia mwanamke, katika makala hii ya The Bestgalaxy, tumekuwekea maneno mazuri ya kiingereza ya kumsifia mwanamke. Ikiwa unamtu anayeweza kufurahia kusifiwa kwa lugha ya kiingereza (English), unaweza yatumia. Ikiwa ni kama sms za mapenzi au ukamwambia mukiwa pamoja, yote sawa.

Sms za kumwambia mpenzi wako kuwa unampenda BONYEZA HAPA>>>

Maneno ya kumsifia mwanamke kwa kiingereza/English

  1. You have a beautiful energy that lights up every room you enter. Your calm confidence and warmth make everything around you feel brighter. You make my heart feel alive every time you’re near.
    (Una nguvu nzuri inayong’aa kila unapofika, ujasiri na upole wako huleta mwanga kila mahali, unanifanya moyo wangu uwe hai kila ninapokuwa karibu nawe.)
  2. Your confidence and elegance make you stand out beautifully. You move and speak with such grace, it’s natural and real. Every time I look at you, I fall in love all over again.
    (Ujasiri na ustaarabu wako vinakufanya uwe tofauti. Unaongea na kutembea kwa upole wa kuvutia, kila nikikuangalia nahisi kama nimenivutia upya.)
  3. I admire how strong and independent you are. You face challenges bravely and grow stronger each time. You inspire me to be better, and I’m proud to love someone like you.
    (Ninavutiwa na nguvu zako, unakabiliana na changamoto kwa ujasiri na kuwa imara zaidi kila siku. Unanitia moyo kuwa bora zaidi, na najivunia kukupenda wewe.)
  4. You have a kind heart that shows in how you treat others. You care and give without expecting anything back. Your heart is the reason I believe in true love.
    (Una moyo mwema unaoonekana kwa jinsi unavyowajali watu. Unatoa bila kutarajia chochote. Moyo wako ndio sababu naamini upendo wa kweli upo.)
  5. Your smile is so genuine, it brightens everything. One smile from you can change the whole mood. Your smile melts my heart every single time.
    (Tabasamu lako ni la kweli, linaweza kubadilisha hali nzima ya siku. Tabasamu lako huyeyusha moyo wangu kila wakati.)
  6. There’s something special about your presence. Even in silence, you attract people effortlessly. When you’re near, I feel peace like nowhere else.
    (Uwepo wako una mvuto wa kipekee. Hata kimya chako kinavutia watu. Ninapokuwa karibu nawe nahisi utulivu wa kipekee.)
  7. I love how you stay true to yourself. You don’t change to please others, you just grow better. That’s what makes me love you even more every day.
    (Ninapenda jinsi unavyobaki kuwa wewe. Hubadiliki kuwafurahisha wengine bali unakua vizuri, hilo ndilo linanifanya nikupende zaidi kila siku.)
  8. Your intelligence and the way you express yourself are beautiful. Talking to you always leaves meaning behind. You make my mind and heart fall for you together.
    (Uelewa wako na jinsi unavyoongea ni wa kuvutia. Mazungumzo nawe huleta maana. Unanifanya nipende akili yako na moyo wako kwa pamoja.)
  9. You have a rare mix of beauty, class, and depth. You win hearts with your soul, not just your looks. You’re the kind of woman I prayed for all my life.
    (Una mchanganyiko wa uzuri, heshima, na undani. Hugusa mioyo kwa roho yako, si mwonekano tu, wewe ni mwanamke niliyekuwa nakuomba maisha yangu yote.)
  10. Every time I talk to you, I feel peace and joy. You leave memories that never fade. You’re my peace, my happiness, and my forever.
    (Kila nikiongea nawe, nahisi furaha na utulivu. Kumbukumbu zako hubaki moyoni daima, wewe ni utulivu wangu, furaha yangu, na wa milele wangu.)

Ni maneno hayo tu ndio tumekuwekea hapa lakini fahamu kuwa upo huru kumsifia mpenzi wako kwa lugha ya kiswahili pia. Mara nyingi watu waswahili huguswa zaidi wanaposikia maneno mazuri kwa lugha ya kiswahili, lakini kiingereza pia inaweza kuwa vizuri katika siku moja moja. Kikubwa awe anajua maana ya kilichoandikwa.

Mambo ya kuzingatia katika kuwasiliana na mpenzi aliye mbali BONYEZA HAPA>>>

MAPENZI NA MBWA (Simulizi fupi ya Kusoma)

Kulikuwa na binti mmoja aliyeishi maisha ya peke yake kwenye chumba kimoja alichokuwa amepanga. Alikuwa binti mdogo aliyeanza kuishi maisha hayo baada ya kumaliza chuo, lakini hakupata kazi wala mpenzi wa kumuoa. Maisha yake ya mahusiano hayakuwa mazuri, maana alikuwa ametendwa mara nyingi mpaka kufikia hapo.

Kwenye upande wa kazi, alikuwa anafanya kazi ya kuuza duka ambalo halikuwa lake. Yaani, yeye alikuwa mtu anayekwenda kuuza duka asubuhi na kurudi usiku, lakini duka na vilivyomo vilikuwa si vyake. Kupitia kazi hiyo ya kuuza duka, alikuwa akipata pesa kidogo ya kulipa chumba anachoishi na chakula cha kawaida.

Kila mara mwanamke huyo alionekana kutoamini wanaume, kiasi cha kuchukia kuwa nao kabisa. Hii ilitokana na mahusiano kadhaa aliyopitia na kuvunjwa moyo huko nyuma. Wanaume wengi waliokuwa wanahitaji kuwa naye hawakupata nafasi, na hata waliopata, waliishia kuachwa kila alipokumbuka jinsi wanaume walivyomuumiza kwenye mahusiano ya nyuma. Hii ilimfanya mara nyingi awe anatembea peke yake. Alikuwa haongozani na mtu anapotoka kazini kwake au kurudi. Kulikuwa na umbali kiasi kutoka anapouzia duka hadi kwake, lakini alikuwa anatembea kwa miguu kwa sababu umbali haukumchosha. Hata hivyo, katika kutembea kwake, changamoto kubwa aliyokuwa anakutana nayo ilikuwa ni mbwa.

Mbwa walikuwa wengi njiani alipokuwa akirudi kwake, hasa akichelewa usiku. Pamoja na kupita mara nyingi, alikuwa anaogopa sana mbwa. Tangu utotoni, alikuwa mtu anayewaogopa sana mbwa na kuwachukia, kwa sababu mbwa wa jirani yao alimng’ata akiwa na umri wa miaka 8. Tukio hilo lilimfanya aogope sana mbwa katika maisha yake yote.

Siku moja, katika njia ya kurudi nyumbani, alikutana na mbwa mmoja mdogo. Mbwa huyo alikuwa mbele yake, na alipomuona tu, alipunguza mwendo ili wapishane kwa tahadhari. Wakati wakipishana, mbwa akabweka ghafla, “Wouh!” Yule dada akaanza kukimbia kuelekea kwake. Mbwa kuona hivyo, akaanza kumkimbiza mpaka akaanguka chini baada ya hatua chache huku mbwa akiwa nyuma yake.
Baada ya kuanguka, mbwa alifika pale alipokuwa yule dada, lakini hakufanya chochote zaidi ya kumnusa na kuanza kurudi nyuma. Dada alipomuona mbwa anarudi, alinyanyuka haraka na kuendelea na safari ya kurudi nyumbani kwa haraka, akitembea huku akijipangusa vumbi kwenye nguo na kuangalia kama bado anafuatwa. Mbwa alibaki kusimama mbali, akimuangalia kwa umbali.

Baada ya hatua nyingi za kutembea, yule dada aliangalia nyuma na kukuta mbwa yule anamfuata taratibu. Hilo lilimshangaza sana, likamfanya aongeze mwendo mpaka akafika nyumbani bila matatizo, ingawa nguo zake zilikuwa zimechafuka kwa vumbi. Ilikuwa kawaida kwake kukimbizwa na mbwa, hivyo hakuchukulia kama jambo kubwa sana.

Lakini baada ya siku hiyo, alianza kushangazwa na jambo ambalo halijawahi kumtokea maishani. Mbwa yule alianza kumfuata kila mara na kujipitisha karibu na nyumbani kwake. Kila alipokuwa akitoka au kurudi, alikuwa akimuona mbwa huyo akiwa karibu naye au akimfuatilia kwa umbali.

Hili lilikuwa jambo geni kwake, maana hajawahi kuwa na urafiki na mbwa. Wakati mwingine alikuwa akimtupia mawe, lakini mbwa hakuwahi kuacha kumfuata kwa upole uleule. Alijaribu kumfanyia ubaya mara kadhaa, lakini mbwa hakukoma kuhitaji kuwa karibu naye. Wakati mwingine alikuta amelala mlangoni kwake.

Baada ya matukio mengi, yule dada aliamua kuanza kumchukulia yule mbwa kama mbwa wake. Ingawa hakuwahi kufanya hivyo maishani mwake, aliamua kujaribu tu kumfuga. Alianza kumjali kwa kumpa chakula, hadi wakaanza kutembea pamoja kwenye baadhi ya safari zake. Alishangazwa sana na jinsi mbwa huyo alivyokuwa mwaminifu kwake, hasa alipokuwa anarudi nyumbani usiku. Alikuwa akitembea naye kwenye njia alizokuwa akiziogopa bila uoga. Mbali na hilo, alianza kukosa hofu hata alipokutana na mbwa wengine, maana sasa alikuwa ameelewa tabia zao kupitia mbwa wake.

Mwisho wa yote, hakujutia kabisa kumfuga mbwa huyo, ingawa baada ya mwaka mmoja alikufa kwa kugongwa na gari akiwa kwenye mizunguko yake. Lakini aliacha funzo kubwa kwa yule dada juu ya kutoa nafasi ya upendo kwa watu au vitu anavyoviogopa, kwa sababu hajavijua vizuri. Alifanikiwa mpaka kupata mtu anaempenda sana na kuishi nae kwa uaminifu maishani.

Kutokana na mambo aliopitia, Kila mara alikua akishuhudia watu kuwa kuna wanawake hupitia mahusiano kadhaa yanayovunja moyo, kiasi cha kufanya wasihitaji ukaribu wa mapenzi ya kweli kwa wanaume. Wengine hawapiti huko, lakini kutokana na matukio au simulizi mbalimbali, wanashindwa kuamini wanaume. Kuna ambao husema hata “Wanaume wote ni mbwa,” na kuzingatia pesa. Wanafanya hayo wakisahau kwamba hata huyo Mbwa anaweza kuwa wao, akawapenda, kuwafurahisha, na kuwalinda Kila siku. Kikubwa ni uwe tayari kumpa nafasi, huku na yeye akiwa tayari kuwa wako.

Mukijua mambo haya hamuwezi kuachana na Mpenzi wako kirahisi BONYEZA HAPA>>>

Ishara 5 za Mwanaume kuwa na Wanawake wengi

Kwenye mahusiano, karibu watu wote huwa wanasema maneno ya kuaminisha kama “wanakupenda” na “upo peke yako,” lakini sio kila mtu humaanisha. Baadhi ya watu wanaweza kusema “Nakupenda” au “Upo peke yako,” lakini wakawa na wapenzi wengi wanaowaambia hivyo kila siku. Mtu muaminifu akiingia kwenye mahusiano na watu wa namna hii, kuna hatari kubwa ya kupata hata magonjwa ya moyo kwa mshtuko. Ukiacha mishtuko, mawazo pia huwa hayapingiki mnapoendelea kuwa pamoja.

Lakini uzuri ni kwamba kuna namna ya kujua mtu ambaye ana wapenzi wengi. Njia hii ni ya kuangalia ishara kwenye matendo yake na sio maneno yake. Kwenye makala hii naenda kuzungumzia ishara hizi, ila ni kwa upande wa mwanaume. Kwa hiyo kama unahitaji kujua ishara za mwanaume kuwa na wanawake wengi, basi hapa ni sehemu sahihi.

Maswali ya kumuuliza mpenzi wako mpya BONYEZA HAPA>>>

Ishara 5 za Mwanaume Kuwa na Wanawake Wengi

1. Simu yake na yaliomo ni siri

Simu yake inaweza kuwa inalindwa kama imeficha siri ambayo hautakiwi kuijua kabisa. Anaweza kuwa hawezi kukupa uitumie, na hata akikupa, haupati uhuru. Hii inaweza kuwa ni kwasababu ya kuficha mambo yanayoendelea kuhusu wanawake wengine.


Kuna wakati mtu anaweza kuwa hataki simu yake iwe mikononi mwa mtu mwingine kwa sababu tofauti na hiyo, lakini wanaume wasiotulia kwenye mahusiano huwa wanakuwa hivi pia ili kuficha wanayofanya.

2. Hakupi muda wa uhakika

Mwanaume mwenye wanawake wengi huwa hatabiriki kwenye suala la kukupa muda wa kuwa naye. Anaweza kuwa anatumia muda mdogo sana na wewe, na muda huo si wa uhakika. Muda mwingi husema yupo “busy” na hataki umfuate sehemu kukutana naye bila taarifa.

Wengine huwa wanakutafuta wanapokutana na hitaji la kimwili tu. Hapo ndio wanakupa muda sana na wakifanikisha wanachokitaka kutoka kwako, hurudi kwenye hali ya kutokua na muda.

3. Haongelei maisha yake wala muelekeo wenu

Mnaweza kuongea vitu vingi vya kufurahisha na mwanaume huyu, lakini hauwezi kugusa  kuongelea maisha yake sana au maisha yenu ya baadaye. Wengine huwa maongezi yao makubwa ni starehe na kukutana kimwili.

Kiufupi, hataki umjue sana na hata ukimjua, hataki kukupa matumaini ya kuwa utakuwa naye kwa muda mrefu. Anakua kwenye mahusiano lakini haingii sana ndani maana yupo na wanawake wengi kwenye mahusiano.

4. Hujionesha lakini bila wewe

Mwanaume mwenye wanawake wengi anaweza kuwa na tabia ya kutotaka kuonekana na wewe sana kwenye maisha ya mitandao au maisha halisi. Kutokana na watu kutumia zaidi mitandao ya kijamii, basi naweza kusema upande wa mitandao ya kijamii ndio wa kuzingatia zaidi.


Mwanaume huyu huwa hawezi kuonesha picha ambayo inaonesha kujihusisha nawe. Hii inaweza kuwa ni kwa sababu anaogopa kuwashtua wanawake wengine aliowakamata.

5. Hana wivu wa kweli

Mwanaume mwenye wanawake wengi huwa hana wivu wa kweli pale anapokuona upo na wanaume wengine. Yaani, akiona umeanza kuonesha tabia ya kumsaliti, huwa haumsumbui kichwa kabisa. Anaweza hata kujua kabisa una mwanaume mwingine lakini asichukulie kama ni kitu kikubwa sana kiasi cha kuvunja mahusiano.


Kiufupi, wanakuwa kama ni wavumilivu sana kwenye mahusiano hata ukiwafanyia vitu vikubwa, lakini ukweli ni kwamba hawana wivu.

Uzuri wa hizo ishara 5 za mwanaume kuwa na wanawake wengi ni kwamba unaweza kuziangalia hata kwenye mahusiano machanga. Baadhi ya wanaume wenye wapenzi wengi huwa hawawezi kuzificha kabisa. Ndani ya mwezi mmoja tu katika mahusiano, unaweza kugundua ishara 2 au mpaka 4.

Mambo 3 niliojifunza baada ya kusoma SUKARI YA DADA, UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA (Simulizi)

Baada ya kuzisoma simulizi tatu nzuri; Sukari ya Dada, Utamu wa Jumla na Mzigo wa Wakubwa, nimegundua funzo kubwa kuhusu maisha halisi ambalo hapa nitaweka wazi.

Simulizi hizi tatu ni miongoni mwa simulizi nzuri sana ambazo zimesimulia maisha ya watu tofauti wanaoishi katika ulimwengu mmoja.
Kila simulizi lina hadithi yake tofauti, lakini unaposoma zote kwa pamoja, unagundua zinaunda picha moja kubwa inayogusa maisha ya vijana, mapenzi, na changamoto nyingine katika jamii.

Baada ya kuzisoma kwa makini, haya ndiyo mambo matatu kati ya mengi muhimu niliyojifunza;

Mambo 3 Niliojifunza Baada ya Kusoma simulizi

1. Usifanye Usichopenda Kufanyiwa

Hili limejitokeza sana katika simulizi ya Mzigo wa Wakubwa.
Mhusika mkuu alijikuta akimfanyia rafiki yake jambo baya; kuchukua pesa zake ili kuokoa hali yake binafsi. Lakini muda haukupita, naye akajikuta akifanyiwa jambo lilelile na mtu mwingine wa karibu sana.

Maumivu aliyoyapata yalikuwa makubwa, lakini hakuweza kulalamika kwa sababu alitambua kwamba naye aliwahi kufanya kosa hilo.
Hapa kuna somo moja kubwa:

“Ukifanya ubaya, ujue ipo siku utaukuta uso kwa uso… Inaweza kuwa si leo, lakini ipo siku.”

2. Huwezi Kumpima Mtu kwa Kuangalia Tu

Hili nimejifunza kupitia simulizi mbili; Sukari ya Dada na Utamu wa Jumla.
Mwisho wa Sukari ya Dada, muhusika mkuu anakutana na Tausi na kuhisi kuwa anaishi na virusi vya UKIMWI.
Lakini unaposoma Utamu wa Jumla, unakuja kugundua kuwa Tausi hana virusi kabisa!

Hii imenifunza kitu kimoja muhimu sana:

“Usihukumu mtu kwa muonekano wake wa nje au mazingira yake. Ni ngumu kujua hata vita gani anaipigana ndani yake.”

3. Kila Mtu Ana Njia Yake ya Mafanikio

Katika simulizi zote tatu, wahusika walionesha njia tofauti za kupambana na maisha.
Wote walikuwa vijana waliokataa kukata tamaa. Yani kila mmoja alipambana kwa namna yake hadi kufikia mafanikio ambayo anayahitaji. Hakuna aliekubali kushindwa, wote walikubali kusonga mbele kutafuta ushindi kwenye njia zao.

Simulizi hizi zimenikumbusha kuwa:

“Hakuna njia moja sahihi ya kufanikiwa. Kila mtu ana wakati wake, njia yake, na changamoto zake za kipekee.”

Kwa ujumla, simulizi hizi tatu zimebeba uhalisia wa maisha ya sasa kwa upande wa vijana. Kwaiyo nilioyaongelea tu, utaona zinatuonesha kuwa dunia ni duara unachokifanya leo, kinaweza kukurudia kesho. Zinatusukuma pia kuwa waangalifu, wenye huruma, na wenye subira katika safari zetu za mafanikio.

KWENYE KAGIZA (Simulizi fupi ya Kusoma)

Nilikua nimeolewa na ninaishi na mume wangu kwa amani sana. Katika miaka yetu michache ya ndoa, kulikua na changamoto moja tuliyopitia na siwezi sema wazi niliimaliza vipi sasaivi, lakini acha nifafanue mambo yalivyokua.

Mme wangu alikua na rafiki yake mmoja anaitwa Mambe; Aliekua kama ndugu kwake. Kabla ya mume wangu kukutana na mimi, alikua na huyo rafiki yake, hivyo mimi ndio nilikua mgeni kwenye urafiki wao.
Urafiki wao haukua wa kuitana rafiki tu, walikua wameungana pamoja hata kwenye kazi. Walikua wanafanya kazi sehemu moja na wanashirikiana kwenye mambo mbalimbali ikiwemo ya kiuchumi.
Huko kazini, nilikua nasikia huyu rafiki ndio mwenye cheo kikubwa na pia anaundugu na bosi wao mkubwa kabisa. Mme wangu alikua ananisimulia mambo mengi mazuri anayofanya huyo rafiki yake. Alikua anasema “Huyu Mambe ni ndugu yangu” kila mara tunapomuongelea.
Na ukweli huyo rafiki yake alikua anaonekana mstaarabu sana, lakini siku moja kwenye kupiga stori na mmoja wa marafiki zangu alinieleza mambo ambayo sikuamini kuhusu yeye. Huyu rafiki yangu alikua anaitwa Lisah na alikua ananisuka nywele huku akinipa stori za huyo mwanaume.
Nakumbuka alisema huyo Mambe ni mwanaume mpole, anaishi peke yake, lakini anawanawake wengi sana hapo mjini anao wahudumia na hawajijui. Ilikua ni kawaida sana kusema watu tukiwa na rafiki yangu, maana ni mtu anayejihusisha na kusuka nywele huku akiongea sana. Lisah liniambia pia kuwa amewahi kupewa pesa akawa nae pamoja usiku mmoja kipindi cha nyuma ila hawakua wapenzi.

Baada ya kama mwaka hivi, nilikua nimesikia mambo mengi sana kuhusu yeye, na ilionekana ni kweli yupo hivyo hata akisimama mbele ya macho yangu.
Hii haikua tatizo kwangu, lakini tatizo langu lilianza kuwa ni ukaribu wake na mume wangu, maana wanasema ndege wanaofanana huruka pamoja.

Nilipomaliza kuchunguza marafiki wa mume na kukuta yupo hivyo, nikajikuta nimeingiwa na mashaka na mume wangu pia. Hali hii ilikua kama utani ilipoanza, lakini baada ya muda ikawa ni tatizo hata kwangu, maana nilikua nakosa amani. Nilishindwa kumuamini moja kwa moja hata akisema anaenda kazini.
Kiufupi, nilikua najiona kama na mimi nasalitiwa na mwanaume wangu, kwa sababu niliona jinsi rafiki zake wanavyochezea wanawake huku wakiwa nao. Nilijikuta nipo kwenye ndoa ambayo sikujiona kama niko salama kabisa. Moyo wangu ulikua unawasiwasi sana, na huo wasiwasi niliufanya siri. Ndoa yangu ilikua kama inapita KWENYE KAGIZA.

Huo wasiwasi niliokua nao ulianza kunisukuma kufanya mambo ya ajabu kwa mme wangu. Yaani nilikua kila mara namfuatilia kama namchunga, halafu akifanya jambo nisilolielewa namtukana sana kuwa anawanawake nje ya ndoa.
Mme wangu alikua anakataa, ila nilikua namtupia maneno mengi sana hata akichelewa kurudi nyumbani kidogo tu.
Ilikua ni kawaida sana kumwambia “Rudi kwa wanawake zako, kalale huko huko!!! Mbwa wewe.”
Mwanaume wangu alikua ananiangalia na kunionya kuhusu maneno yangu, japokuwa alikua ananiacha niongee mpaka hasira ziishe.

Nilijaribu kuchunguza sana kama na yeye ana tabia hizo, lakini sikupata ushahidi wowote. Mwisho nikaamua kupanga siku ya kumuuliza mme yangu juu ya tabia mbaya za rafiki Mambe, maana yeye huongelea tabia nzuri tu.
Siku moja katika stori za hapa na pale tukiwa chumbani, nikaingizia hizo habari za rafiki yake. Nilishangaa kuona na yeye anakubali kuwa rafiki yake anafanya mambo hayo hapo mjini.
Ikabidi nimuulize, “Sasa kama rafiki yako yupo hivyo, inamaanisha na wewe upo hivyo?”
Akanijibu, “Hapana, mimi huwa namshauri aoe na kuwa na mwanamke mmoja.”
Pia alisema kuwa wanaume wanaweza kuwa marafiki sana lakini wakawa na tabia tofauti kwa wanawake. Mwanaume mmoja anaweza kumtesa mke wake lakini rafiki zake hawatesi wake zao. Hivyo nisiwe na wasiwasi.

Kiukweli moyo wangu haukuwa na chochote zaidi ya kumuamini, maana ushahidi wa yeye kunisaliti nilikua sina kabisa. Lakini nilijifunza kutochunguza sana marafiki wa mwanaume, maana walinifanya niwaze sana na kukosa amani kwenye ndoa yangu.
Unaweza kujikuta unaumiza moyo wako na kumhukumu mpenzi wako kwa sababu ya kuwachunguza rafiki zake….

Baada ya muda mingi kupitia walianza kutengana maana naskia tabia ya Rafiki yake ilizidi kuwa mbaya mpaka akawa anafumaniwa na wake za watu. Hii ilimfanya mme wangu kuwa mbali nae maana ananipenda sana. Alianza kunikataza mpaka mazoea nae.

Yote kwangu yalikua ni furaha maana nilipata amani ya moyo.

MWISHO

Mambo 5 Mwanaume hapendi kuona kwa Mwanamke katika Mahusiano

Kwenye mahusiano, watu wengi huingia wakiwa wamependana kwa dhati, ingawa siku hizi wapo wanaoingia kwa matamanio au tamaa tu. Na Katika maisha ya mahusiano ya mapenzi, kuna mambo ambayo mwanaume au mwanamke huyaona na kuyapenda, jambo linalowafanya waendelee kubaki pamoja hata kama mwanzo haukuwa na nia ya kweli.

Lakini pia, yapo mambo mengine ambayo mtu akikumbana nayo, huweza kuyachukia kiasi cha kuamua kuondoka kabisa kwenye uhusiano. Makala hii itazungumzia zaidi upande wa mwanaume, kwa kuangazia mambo machache muhimu ambayo kwa kawaida mwanaume hapendi kuyaona kwa mwanamke wake katika mahusiano.

Maswali ya kumuuliza Mpenzi wako Mpya BONYEZA HAPA>>>

Mambo 5 Mwanaume hapendi kutoka kwa Mwanamke

  1. Kukosa Uaminifu

Uaminifu ndio nguzo kuu ya uhusiano wowote. Mwanaume hapendi mwanamke asiyeaminika kwasababu akihisi kwa hutoa siri zake au ana tabia za usaliti, moyo wake huhisi hayupo sehemu salama. Hata kama atabaki kwenye uhusiano kwa muda, mara nyingi itakuwa kwa sababu ya tamaa tu, si kwa upendo wa kweli. Mwanamke anapokuwa mwaminifu, hujenga heshima na kumfanya mwanaume ajisikie yuko na mtu sahihi wa maisha yake.

  1. Dharau

Heshima ni kitu kikubwa kwa mwanaume. Haijalishi mwanamke ni mrembo kiasi gani, mwanaume hatavumilia dharau. Anapenda kujisikia kama kiongozi na mtu muhimu ndani ya uhusiano. Maneno ya kejeli, kutojali maamuzi yake, au kumdharau mbele za watu huumiza moyo wake na kumfanya ajiulize kama kweli yupo sehemu sahihi. Mwanamke anapompa heshima mpenzi wake, hujenga hata misingi ya mapenzi ya muda mrefu.

  1. Uchafu au Kutokujipenda

Mwanaume hupenda mwanamke msafi na anayejipenda. Uchafu au kutojijali kunamfanya mwanaume akose kabisa hamu ya kuwa na mwanamke, hata kama alikuwa amempenda sana. Kujipenda si lazima uwe na nguo za gharama kubwa; hata nguo za kawaida zikivaliwa kwa usafi na mpangilio mzuri humfanya mwanamke avutie. Mwanamke anapojitunza kimwili na kihisia, humvutia zaidi mwanaume na kuimarisha heshima yake.

  1. Kulinganishwa na Wanaume Wengine

Hakuna mwanaume anayependa kulinganishwa na mwingine. Kauli kama, “Mbona fulani kafanya vile alafu wewe umefanya hivi?” ni sumu kubwa kwa mapenzi. Kila mwanaume anapenda kujiona wa kipekee machoni pa mwanamke wake. Kumlazimisha ajione wa hali ya chini kwa kumlinganisha na wengine humfanya ajisikie hafai na kupoteza nguvu ya kupigania uhusiano wengu.

  1. Kutokuwa na Shukrani

Shukrani ni jambo dogo linalobeba uzito mkubwa. Wanaume wengi hujitahidi sana kuhakikisha wapenzi wao wanapata furaha na amani, hata kwa njia ndogo ndogo. Kukosa shukrani au kuchukulia kila kitu kawaida humvunja moyo mwanaume. Neno rahisi kama “asante” linamfanya ajisikie kuthaminiwa na linazidisha upendo ndani ya uhusiano. Akikosa neno hili ndani ya mahusiano, Kuna hatari kubwa ya kuhamia popote atakapolipata nje ya mahusiano.

Mapenzi ya kudumu yanahitaji uaminifu, heshima, kujali na kushukuru. Mwanamke akijitahidi kuepuka mambo haya matano ( kutokuwa mwaminifu, dharau, uchafu, kulinganisha wanaume na kukosa shukrani) anakuwa ameweka msingi mzuri katika mahusiano.

Kwanini Wanawake wanawapenda Wanaume Warefu?

“Yule mkaka ni mrefu Hadi raha, natamani angekuwa wangu…”
“Alafu hata mimi napenda mwanaume mrefu alafu akiwa mweusi ndio nachanganyikiwa kabisa.”

Haya ni mazungumzo unayoweza kusikia kwenye daladala, mitandaoni au hata mitaani. Lakini swali kubwa ni: kwanini wanawake wengi wanawapenda wanaume warefu?

Je, hii ni kwa sababu ya hisia za kweli, mitazamo wa mtu au ni matokeo ya mila na tamaduni zilizojengeka kwa muda mrefu?

Ukifuatila kidogo; Wengine wanasema ni sayansi ya mwili, huku wengine wakiamini ni ushawishi wa mitindo ya maisha ya kisasa ulioletwa na filamu au mitandao ya kijamii.

Katika makala hii ya The Bestgalaxy, tutachunguza kwa undani sababu kuu zinazofanya wanaume warefu wavutie zaidi kwa wanawake, huku tukikukumbusha kuwa mapenzi ya kweli hayapimwi kwa futi wala sentimita, bali kwa moyo.

Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Sababu za Wanawake kupenda Wanaume Warefu

  1. Hisia za kujihisi salama

Wanawake wengi husema mwanaume mrefu huwapa hali ya kujiamini na kujisikia salama. Wanaume warefu mara nyingi huonekana kuwa na nguvu zaidi kimwili, jambo linalomfanya mwanamke ahisi kwamba yuko na mtu anayeweza kumlinda kwenye hatari. Hata kama si lazima awe na nguvu nyingi, urefu pekee unaleta hisia za usalama kichwani mwa mwanamke.

  1. Mvuto katika Jamii

Jamii nyingi zimekuwa zikiwapa nafasi kubwa wanaume warefu. Wakati mwingine wanaonekana kama viongozi wa kikundi toka wakiwa wadogo. Mfano, kwenye mikusanyiko hata wa wakubwa, mwanaume mrefu mara nyingi husimama na kuonekana kwa urahisi, kitu kinachoongeza mvuto wake bila hata kusema chochote. Kwa wanawake wengi, hii ni ishara ya hadhi, utawala na mamlaka.

  1. Sayansi

Watafiti wa saikolojia ya mwili (evolutionary psychology) wanaeleza kuwa urefu ni moja ya sifa ambazo ubongo hutafsiri kama ishara ya afya njema na vinasaba (genes) bora. Mwanamke anaweza asijue, lakini hali yake ya ndani humwambia mwanaume mrefu ana uwezo mkubwa wa kulinda na kuendeleza familia yenye afya. Hii inatokana hata na historia ya nyuma ya kibinadamu ambapo urefu na nguvu vilihusishwa na afya njema.

  1. Utamaduni na Mitindo

Filamu, muziki, na mitandao ya kijamii zimechangia pakubwa kuunda picha kwamba mwanaume mrefu ndiye “Handsome” Ukifuatilia sinema/movie nyingi, uhusika wakuu wa kiume mara nyingi holewa kwa waigizaji warefu. Hii hujenga taswira akilini mwa watu kwamba urefu ni moja ya vigezo vya mwanaume anayependeza. Kwa hiyo, hata kama mwanamke hakuwahi kufikiria hivyo awali, mazingira na utamaduni hujenga mtazamo huu taratibu.

Jinsi ya kupata Mpenzi mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Mwisho: Si wanawake wote hufuata dhana hii juu ya wanaume warefu. Wengi huweka kipaumbele zaidi kwenye tabia, mawasiliano, na heshima kuliko urefu. Kuna wanaume wafupi lakini wenye mvuto mkubwa kutokana na jinsi wanavyojiamini na jinsi wanavyowajali wapenzi wao. Mapenzi ya kweli hujengwa kwenye uaminifu, mawasiliano, na upendo wa dhati; mambo ambayo hayawezi kupimwa kwa sentimita.