Tag Archives: mafanikio

Mambo yanayokwamisha Watu kukimbiza Ndoto zao



Ikiwa wewe ni kijana mwenye miaka 20 na kuendelea, kuna mambo muhimu sana unatakiwa kujua kuhusu safari ya kufikia ndoto zako.
Kila mtu huwa na ndoto kubwa maishani, lakini ni wachache sana wanaoweza kuzitimiza.


Sababu kubwa inayofanya wengi washindwe si kwa sababu hawana uwezo, bali ni kutokana na kutoanza kuzikimbiza kabisa. Hapa chini tunakupa baadhi ya mambo yanayokwamisha watu wengi kukimbiza ndoto zao. Unaweza kuyapitia ili kuwa na kuelewa kwenye mapambano ya kukimbiza ndoto zako.

Jinsi ya kulinda ndoto zako zisife maishani BONYEZA HAPA>>>

Mambo yanayokwamisha Watu kukimbiza Ndoto zao



1. Kusubiri Wapate Kitu cha Kuanzia

Watu wengi wana mawazo makubwa ya biashara, miradi au mipango ya kubadilisha maisha yao, lakini hawachukui hatua kwa sababu wanasubiri kupata mtaji au kusaidiwa na mtu mwingine ili waanze.
Hii ni moja ya sababu zinazowafanya watu wengi wabaki pale pale walipo kwa miaka mingi, wengine mpaka wanazeeka bila kufanikisha kitu.

Ukweli ni kwamba, ni nadra sana kuona mtu kakupa mkono wa kukuanzishia. Badala ya kusubiri, tafuta njia zako mwenyewe za kuanza hata kidogo.

Usiseme “Nahitaji mtu anipatie milioni 1 ili nifike mbali kibiashara” alafu ukatulia. Bali sema “Nipo napambana kupata pesa kidogo kidogo mpaka nifike kwenye hiyo milioni 1 ili nifike mbali kabisa kibiashara” huku ukifanya hivyo kweli.

Matendo madogo yanayoanza leo, yanaweza kuwa mwanzo wa mafanikio makubwa kesho.




2. Kubadilisha Malengo Mara kwa Mara

Watu wengi huanza mwaka wakiwa na lengo moja, lakini wakifika katikati ya mwaka wanakuwa tayari wamebadilisha mawazo mara kadhaa.
Ni vizuri kuwa na mawazo mapya, lakini kama kila wazo linakufanya usimalize uliloanza, unakuwa unajizungusha pale pale tu bila hatua yoyote.

Kila ndoto inahitaji msimamo na umakini. Usiruhusu malengo mapya yakupotezee mwelekeo wa lengo kuu ulilojiwekea.
Tambua unachokitaka, kisha kifuate bila kuyumbishwa na vitu vidogo vidogo njiani.



3. Kutaka Kuelewa Sana Kabla ya Kuanza Kufanya

Kuna watu hutumia muda mwingi sana kufikiri na kupanga, badala ya kuchukua hatua.
Wanataka kuelewa kila kitu kabla ya kuanza, na matokeo yake wanabaki kufikiri tu bila kufanya chochote cha maana. Kwenye hili; wataalam huwa wanasema “Overthinking Kills Success“, wakiwa na maana “Kufikilia Sana Kunaua Mafanikio”.

Mfano: Wakati wewe unawaza kuanzisha biashara kubwa ya kuuza samaki nchi nzima bila matendo yoyote, mtu mwingine anaamua kuanza kuuza samaki mtaani kwake tu kisha anaanza kuingiza pesa kila siku huku akikua taratibu kibiashara.

Mipango ni mizuri, lakini matendo ndio yanayoleta mabadiliko kwenye maisha.



4. Kutoamini Kwenye Mawazo Yao

Watu wengi wana mawazo mazuri sana, lakini tatizo ni kwamba hawaamini ndani yao kuwa mawazo hayo yanaweza kuleta mafanikio.
Kukosa imani kunazalisha hofu, na hofu inaua ndoto.

Kama huwezi kuamini unachokiwaza, hutachukua hatua, na hutawahi kujua mwisho wake hata kama ni mzuri.


Ndoto hazitimii kwa miujiza, bali kwa hatua ndogo zinazochukuliwa kila siku. Maisha yanabadilika pale unapochukua hatua.

Simulizi ya “Punda” ni mfano mzuri wa kutosikiliza watu katika Maisha

Moja kati ya simulizi ambayo huongelewa sana katika mifano ya maisha ni hii simulizi ya Mume, Mke, na Punda. Kama uijui vizuri simulizi hii, tulia uisome hapa chini;

Kulikuwa na mume na mke waliokuwa wakisafiri kijijini kwao wakiwa na punda. Njiani, walikutana na watu wa aina mbalimbali waliokuwa na maoni yao kuhusu safari yao.

Mume na mke walitembea kwa mguu huku wakiwa wamechukua punda wao akiwa amefungwa kwa kamba shingoni. Walionekana wamechoka, lakini walikuwa wakifurahia mazungumzo yao. Walipokutana na kundi la watu wa kijiji flani, walihisi macho yakiwatazama sana.

“Mna akili kweli? Mna punda lakini mnatembea kwa miguu! Kwa nini msimpande?” mmoja wa watu akasema huku akicheka.

Mume akatazama mke wake na akasema, “Labda wana ongea cha maana hawa. Hebu tubadilike.”

Mume alipanda punda huku mke akitembea pembeni. Baada ya muda, wakakutana na kundi jingine la watu.

“Angalia huyu mwanaume! Anawezaje kumpanda punda huku mke wake maskini anatembea? Hana hata huruma!” mmoja wa wanawake akasema kwa sauti ya lawama.

Mume aliona haya na kushuka. “Basi wewe panda sasa,” alimwambia mkewe.

Mke akapanda punda, alafu mume akaanza kutembea kwa miguu. Njiani, wakakutana na kundi jingine la watu waliokuwa wakifanya kazi shambani.

“Jamani! Angalia huyu mwanamke hana hata aibu. Anampanda punda huku mume wake mzee anatoka jasho akitembea!” mmoja wa wanaume akasema kwa dhihaka.

Mume na mke walitazamana na kuamua wote wapande punda.

Wote wawili walipanda punda na kuendelea na safari yao. Hawakufika mbali, wakaanza kusikia watu wakiwazungumzia tena.

“Hawa watu hawana huruma! Wote wawili wanampanda punda huyu mdogo. Wanataka kumuua kwa uzito wao?” mmoja wa wazee akasema huku akitikisa kichwa chake.

Mume na mke vichwa kikawaka moto, waliona bora wambebe huyo punda mgongoni ili wasisemewe tena. Wakafunga miguu ya punda kwa kamba vizuri na kumbeba kama mzingo. Walipokuwa wakivuka daraja, watu waliwaangalia kwa mshangao na kucheka sana.

“Jamani, angalia hawa wajinga! Wamegeuza mambo. Badala ya punda kuwabeba wao, wao ndio wanambeba punda!”

Kwa aibu, waliishiwa nguvu, punda akaanguka mtoni. Mume na mke wakakaa kimya huku wakitazama punda akizama majini…

Simulizi hii inamaana gani kwenye Maisha?

Simulizi hii inakumbusha kuwa katika Maisha, Haijalishi unafanya nini, watu watasema tu. Unaweza kufanya jambo kwasababu zako nzuri tu lakini wakaangaliwa kwa ubaya. Kiufupi, unapokua na ndoto au mambo mbalimbali unayotaka maishani, maneno ya watu usiruhusu yakuyumbishe au kukupoteza kama ilivyokua kwa wenye Punda.

Ushauri kwa aliesema pesa zake hazioni BONYEZA HAPA>>>

Huu ni ushauri kwa mtu anaesema “Naipata pesa lakini siioni” katika Maisha

Ikiwa unapambana kupata pesa na unapata lakini hauioni, hii makala ni ya kwako.


Kwanza unatakiwa kujua kuwa watu wengi wapo kwenye hali hiyo kwa sasa. Yani unaweza kuwa na pesa ndogo au nyingi zinazoingia lakini zinapita mkononi mwako tu na hazituli.

Pamoja na kwamba watu husema “Pesa sio Kila kitu” lakini unatakiwa kuelewa kuwa maisha ya sasa yanahitaji pesa. Hii ni kwasababu asilimia kubwa ya vitu vilivyopo kwenye maisha yetu, vinatumia pesa na vinadai pesa kabisa Yani.

Mfano; ukiwa umepanga nyumba unayolipa elufu 50 kwa mwezi inamaana katika Maisha yako Kila baada ya siku 30 unalipia elufu 50. Sasa hapo Ukijumlasha na mambo ya chakula, umeme na mambo mengine yanayojitokeza kwenye mwezi unaweza jikuta Kila mwezi unatakiwa kwenye mikono yako utoe pesa nyingi sana. Na hizo pesa zote unazotumia kwa ujumla wanaita “Gharama za maisha”. Hii inamaana maisha yana “Gharama”.

Mbinu za kutimiza malengo yako ya Mwaka BONYEZA HAPA>>>

Gharama za maisha na kiasi cha pesa unachoingiza

Gharama za maisha yako zikiwa ni kubwa kuliko kiasi cha pesa unachoingiza, unawezakuwa ni mtu unaeshika pesa lakini huzioni na unaangukia kwenye madeni. Yani unakua ni mtu unaetumia pesa nyingi kuliko unazoingiza.

Kujitoa kwenye hali hiyo unatakiwa kwanza kumuomba mungu akusaidie badala ya kukimbilia kwenye vitu kama pombe ili kumpunguza Mawazo.


Hatua ya pili, unatakiwa kutulia na kuiweka akili yako kwenye matumizi yako ili kuelewa kiasi gani unatumia kwa siku, mwezi na hata mwaka. Hapa utatakiwa kujua pesa kiasi gani unatakiwa kuwa nayo kwa mwezi ili uwe na mahitaji muhumu yote(Kodi, chakula n.k). Na pia unatakiwa kujua pesa kiasi gani huwa zinatoka mikononi mwako na kwenda kwenye vitu visivyo vya muhimu. Kiufupi unatakiwa kuzingatia pesa zinatokaje mikononi mwako.

Baada kujua pesa zinatokaje mikononi mwako, utatakiwa kuanza kuzizuia baadhi ya pesa zinazokwenda kwenye mambo yasio ya muhimu. Ni ngumu sana maana pesa nyingine unaweza gundua zinatoka mikononi mwako ili kuifurahisha Roho na imekua ni kama Tabia tayari kufanya hivyo. Lakini pambana sana kuzuia kwa kubadilisha tabia na kuepuka utoaji wa pesa usio wa muhimu sana.

Wakati ukiendelea kupambana kuzuia pesa zisitoke mikononi mwako kizembe, unaweza kuwa na hasira sana kuhusu pesa maana utakua unaona baadhi ya pesa zinaendelea kutoka mikononi mwako bila umuhimu na unashindwa kuzizuia. Lakini usikate tamaa maana jambo hili litakukumbusha kujiuliza “Nitarudisha vipi pesa zilizotoka mikononi mwangu bila umuhimu?”, Pia utajiuliza “Nifanye nini ili hizi pesa zinazokuja zisiwe zinatoka mikononi mwangu?”.

Unarudisha vipi pesa zilizotoka mikononi mwako?

Ni ngumu kurudisha pesa zinazotoka mikononi mwako ila unaweza anza kuzingatia utengenezaji wa pesa nyingi nyingine zitakazokuja mikononi. Yani hapa naongelea kuongeza kipato chako.

Mfano: kama ni mfanya biashara, basi unatakiwa kufanya bashara yako ikuingizie pesa nyingi zaidi. Na njia rahisi ya kufungua ubongo wako kwenye upande wakuongeza kipato ni kujifunza toka kwenye vitabu au watu wengine wanaoingiza pesa zaidi. Au unaweza anza kujaribu vitu mbalimbali ili kuitanua biashara yako iweze kuingizia pesa zaidi.

Kiufupi ni unatakiwa kutafuta njia za kuongeza kipato au pesa zinazokuja mikononi mwako huku ukiendelea kuzuia matumizi yasio na maana. Na ukifanikiwa kuingiza pesa nyingi kuliko unazotumia, utakua ni kama umefanikiwa kuzirudisha pesa zinazotoka mikononi mwako huku ukipata na nyingine za juu kwaajili ya mambo mengine.

Nini cha kufanya ili pesa zisiwe zinatoka mikononi mwako?

Kufanikisha hilo unatakiwa uwe unaweka pesa yako kwenye sehemu isiopungua thamani yake au uwe unaiweka pesa yako kwenye sehemu inayofanya pesa yako izalishe pesa nyingine.

Kiufupi ni utanatakiwa uwe unatuza pesa yako kwa kuweka kwenye akaunti au michezo ya kutuziana pesa. Wengine huwa wananunua mpaka viwanja ili kuitunza pesa tu isishuke thamani. Na pia unaweza iweka pesa yako kwenye biashara inayozalisha pesa zaidi ya ulioiweka.

Katika safari ya kuelekea mafanikio. Usisahau kuwa mungu atakusaidia ukijituma, na pia karamu na daftari ni muhumu kuvitumia kwenye mahebu yako ya kimaisha.

Mbali na hayo; kujiweka katikati ya watu wanapenda mafanikio ni muhimu. Hakikisha unakua na watu wanaopenda mafanikio kwenye maisha na sio waliokata tamaa. Ukishindwa kabisa kupata watu, wafuate wanao hamasisha kujituma na mafanikio kwenye maisha waliopo mtandaoni. Kama wewe ni kijana wa kiume unapenda kutiwa hasira sana za kutoka ulipo, unaweza wafuata hata wakina Chiefgodlove au Chimakeke. Pamoja na mabaya yao, hiyo ni moja ya kazi yao.

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy!

Wanasema “Ukitaka Kufanikiwa, Kuwa Kama Tai” kwasababu hizi

Tai au Eagle ni ndege maarufu kwa uwezo wake kwenye mambo mbalimbali na amekua akiongelewa sana. Baadhi ya watu hutumia ndege huyu kama alama za kuonesha ujasiri, nguvu na ubora. Lakini pia kunawatu humtumia ndege huyu kama mfano katika Maisha na mafanikio.


Kutumia mfano wa tai kama alama ya mafanikio ni njia bora ya kuelewa mambo muhimu yanayoweza kutusaidia kufikia sehemu flani maishani. Ili kufanikiwa, Kuna muda ni kweli tunahitaji kuiga tabia na sifa fulani za tai ambazo ni zenye thamani na zinazoweza kutupeleka mbali. Kati ya sifa hizo ni hizi hapa chini.

Jinsi ya kulinda ndoto zako zisife maishani BONYEZA HAPA>>>

Sifa za kumuiga Tai ili kufanikiwa kwenye maisha

Kuwa na Maono na Mtazamo wa Mbali

Tai ana uwezo wa kuona mbali sana, hadi kilomita 5! Hii inampa nafasi ya kuona mlo wake au adui akiwa mbali. Ili kufanikiwa, ni muhimu kuwa na maono ya mbali na kutazama mambo kwa upana. Jiulize: unataka kufikia nini maishani, na ni vikwazo gani vinaweza kujitokeza? Kama tai, kila mara angalia mbali zaidi ya hali ya sasa, na ujipange kulingana na unachokiona mbele.

Kuanza upya

Kuna wakati Tai hutenga muda kujibadilisha kwa kung’oa manyoya yake ili kufanya manyoya mengine mapya yaote. Hii ni muhimu kwetu pia; wakati mwingine ni lazima tuondoe tabia, mahusiano, au mawazo ambayo yanatuzuia kusonga mbele. Wakati mwingine, uamuzi wa kuacha kile kinachoturudisha nyuma, ndicho kinachoweza kutupeleka mbali zaidi. Hivyo tunapaswa kuishi kwa mfano huu katika mambo yetu ya kila siku.

Kukabiliana na Changamoto

Tai huwinda nyoka kwa kuruka chini na kuwashika kwa makucha yao, kisha kuruka juu huku nyoka akihangaika. Kisha tai wanaweza kuponda au kung’oa kichwa cha nyoka huyo na kukimeza kizima wakiwa bado wanaruka.

Tai huenda juu kwasababu ndio sehemu ambayo anaijua vizuri lakini nyoka hawezi kuhimiri. Tunawezasema Tai huwa anampeleka nyoka sehemu ambayo anaijua vizuri na ile inaruhusu yeye kushinda vita kirahisi.

Hii katika maisha inatukumbusha kuwa bora katika upande wetu na kutumia tulichonacho kuzishinda changamoto zinazokuja bila kuogopa. Tumia ulichonacho kuwa unapohitaji kuwa, au nenda katika sehemu inayoruhusu kupata unachohitaji. Na pia ondoka sehemu inayosababisha ushindwe.

Kwahivyo, ukitaka kufanikiwa, kuwa kama tai: mtazamaji wa mbali, mwenye moyo usiotetereka, na mwepesi wa kubadilika.

Picha za maneno ya hekima na misemo ya maisha

Kama huwa unapenda kusoma au kufuatilia maneno ya busara au maisha, hapa tunajambo lako. Laini kabla hatuja enda moja kwa moja kwenye jambo au lengo letu, ni vema ukatambua kuwa unachokifanya ni kitu kizuri.

Inasemekana kwamba mtu anapopenda kufuatilia vitu flani kwa kuangalia au kusoma, maisha yake yanaweza anza kuendana na mambo anayofuatilia. Japo sio watu wote lakini inasemekana kuwa maisha ya mtu yanaweza badilika kwa kufuatilia mambo flani kwa kusikiliza, kusoma au kuangalia.

Hiyo ndio sababu unaweza ona watu mpaka sasa wanasoma vitabu alafu utawasikia wakisema “Kitabu hiki kimebadilisha maisha yangu”. Ukiachila mbali kusoma, kuna watu huwa wanasikiliza vitu au kuangalia alafu mwisho, maisha yao yanabadilika kutokana hilo jambo alilokua analifuatilia.

Kiufupi vitu unavyofuatilia kwa kusoma, kusikiliza au kuangalia vinaweza kukutuia moyo usikate tamaa, kukuburudiasha ukafurahi na hata kukuelimisha ukabadirika.

Hapa chini tumekuandalia picha chache ambazo zina ujumbe kuhusu maswalia ya maisha kiujumla. Unaweza pitia moja baada ya nyingine kuangalia itajkayokufaa. Kama utataka download pia itakua sio jambo baya kwetu The bestgalaxy, unaweza fanya tu.

Mambo 5 husaidia kukimbiza mafanikio katika miaka 25 mpaka 38 BONYEZA HAPA>>>

Picha za maneno ya hekima na misemo ya maisha

Kwa kumalizia, “picha zenye ujumbe kuhusu maisha” ni njia bora ya kuwasilisha ujumbe muhimu kuhusu maisha kwa ujumla. Picha hizi, zimebeba ujumbe wa kweli kuhusu maisha na ujumbe huu unaweza kuendanda na hali za maisha ya watu wengi.

Unaweza wasambazia marafiki na ndugu unaowapenda picha hizi kupitia WhatsApp, Facebook na mitandao mingine. Ukishindwa kuzidownload, zipige screenshot.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Mbinu za Kutimiza Malengo yako ya Mwaka

Wanasema mwaka mpya huja na mambo mapya. Unapoanza mwaka, watu wengi hujiwekea malengo wanayotaka kutimiza ndani ya mwaka huo. Jambo hili huwa linafanywa na watu wengi sana Duniani lakini kufikia malengo hayo mara nyingi inakua sio rahisi kama wanavyotarajia. Katika mambo mapya mwaka mpya unayokujanayo huwa unajumuisha na changamoto mpya zinazoweza kuweka ugumu kutimiza malengo.

Lakini Swala la watu kushindwa kutimiza malengo ya mwaka, lisiwe chanzo cha kushindwa kuipamga au kuendelea kuipambania mipango yako ya mwaka. Jambo hili linatakiwa kuwa ni chanzo cha kuweka umakini katika mipango ya mwaka na kuhakikisha unapambana sana kuiitimiza.

Ni muhimu kuwa na mbinu sahihi za kuhakikisha kwamba malengo yako ya mwaka hayabaki kuwa ndoto tu, bali yanakuwa uhalisia. Katika kurasa hii ya The bestgalaxy, tutajikita kwenye mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kusaidia kutimiza malengo yako ya mwaka. Mbinu hizi zimewekwa hapa ili kukupa mwanga utakaokisaidia katika safari yako ya kufikia mafanikio unayoitaka kuyapata ndani ya mwaka. Kila mbinu itakusaidia kuweka malengo yako kwenye mstari sahihi kama utaitumia kwenye safari yako.

Jinsi ya kuzilinda ndoto zako Maishani zisife BONYEZA HAPA>>>

Mbinu za kutimiza Malengo yako ya Mwaka

Kuandika mipango yako na hatua


Watu wachache sana wanauwezo wa kukamilisha mipango ya muda mrefu bila kuandika. Wengi wasio andika huwa na malengo yanayo badilika badilika mpaka mwaka unaisha hawajui jambo gani walilopanga mwanzo wa mwaka.
Kitendo cha kuandika malengo yako huwa kinasaidia kutosahau kirahisi ulichokusudia kukifanya katika mwaka. Na hata ukisahau unaweza kumbuka picha nzima ya lengo lako kwa kusoma ulipoandika.


Ukishaandika hakikisha unakua na tabia ya kuandika mambo yako kwenye kila hatua unayopiga. Jambo hili litakusaidia kutimiza malengo yako ya Mwaka na hata usipotimiza utakua na mambo ya muhimu sana ulioyaandika kwaajili ya maisha yako ya Mwaka mwingine.

Kiufupi usiache kutumia karamu na karatasi kwenye maisha yako maana kichwa unachotegemea kukutunzia vitu vyako kinaweza kumbana na mambo mengi maishani. Mambo ya mitandao, matatizo ya familia na changamoto nyingine zote zinasubiri kuingia kichwani mwako.

Kuweka malengo chini ya miezi mitatu

Unataka kukifika mwezi wa 12 ndio uanze kufikilia kama mwaka huu umezembea au vipi? Acha hiyo tabia. Anza kujiweka malengo madogo ya miezi mitatu yatakayokua yakuonesha kama umezembea kabla haijafika mwezi wa 12. Yani gawanya lengo lako la mwaka kwenye miezi mitatu mitatu alafu kila mwizi mitatu ikifika unatulia unajiuliza “Nipo ninapotakiwa kuwa au nimezembea? Nifanye nini?”. Kufanya hivi kutakufanya uongeze umakini kabla ya mwaka haujaisha. Kama malengo yako yanaruhusu, unaweza weka hata miezi miwili na ikawa msaada kwako.

Fanya mambo kwa kasi kabla ya muda

Ikiwa unamipango migumu uliopanga na unatamani kuzitimiza, njia nzuri ya kuzitimiza ni kuanza kuipambania kwa kasi mapema. Yani kama kunajambo unatakiwa kulifanya kila siku ndani ya siku Saba(7) ndio ulitimize, Anza siku ya kwanza kwa kufanya kazi ya siku tatu. Kama ni kuweka pesa kiasi flani kila siku, Anza kwa kuweka pesa nyingi zaidi ya hiyo ya siku moja.

Kiufupi ukipata nafasi ya kufanya vitu vya kesho au kesho kutwa katika siku ya Leo, basi fanya Leo maana kesho kunaweza kuwa na changamoto ambayo bado haujaijua.
Kufanya hivi kutafanya uweze kupambana na changamoto katika safari yako bila kuiathiri sana safari uliojiwekea. Na vile vile tabia hii inaweza kukujenga ukawa mtu makini sana kwenye mambo yako.

Ahadi ya kubeba kila changamoto bila kukata tamaa

Usije msingizia mtu tena kuhusu wewe kushindwa kutimiza malengo yako. Jitahidi kubeba kila kitu kigumu utakachokutana nacho bila kutaka tamaa.

Tambua kuwa hakuna mwaka ambao hautakuja na changamoto. Hata waliofanikiwa wamefanikiwa lakini bado wanapambana na changamoto. Adui mkubwa wa malengo ya mwaka ni muda. Uheshimu muda maana ukizembea alafu muda wa mwaka uliojiwekea ukiisha, utakua umepunguza mwaka moja kwenye maisha yako ya Duniani lakini haujafanikiwa kukifanya unachokitaka. Sasa upo tayari kupoteza mwaka mwingine wa Maisha yako kumlaumu mtu au watu?

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kama makala kama hizi zinakua msaada kwako. Usisahau kuwa karibu nasi kwenye mambo mengine na kwenye mitandao ya kijamii pia.

Jinsi ya kutengeneza Logo ya biashara au binafsi BONYEZA HAPA>>>

Badilisha maisha yako kwa kubadilisha vitu hivi vidogo

Sote tunafahamu kuwa Maisha yanaweza kuwa na changamoto nyingi, lakini mara nyingi mabadiliko madogo yanaweza kuleta tofauti kubwa. Kila mmoja wetu anajitahidi kufikia sehemu anayohitaji au mafanikio. Lakini katika safari ya kufikia hayo, changamoto zinaweza kuwa zinaonekana nyingi na kubwa kiasi ambacho watu huona kabisa hawawezi kutimiza wanayo yahitaji. Watu hufikia kwenye hali hii baada ya kufikia hatua ya kuona wapo mbali sana na wanachokihitaji. Yani kunaweza kuwa na umbali mkubwa sana kati ya sehemu mtu anahitaji kuwa na sehemu alipo. Au umbali kati ya mtu anaehitaji kuwa na mtu aliopo.

Makala hii itakupa mwongozo juu ya mambo madogo muhimu ambayo, ukiyabadilisha, yanaweza kubadilisha Maisha yako. Mambo haya ni mambo madogo sana lakini yakibadilishwa yanaweza kukufanya uwe mtu unaetaka kuwa au kukufikisha sehemu unayoitaka kuwa.

Ukiyajua mambo haya, utapata mwanga na njia za kuboresha maisha yako kwa kubadilisha Maisha yako kuwa vile unahitaji.

Jinsi ya kulinda Ndoto zako Maishani zisife BONYEZA HAPA>>>

Badilisha maisha yako kwa kubadilisha vitu hivi vidogo

Mambo unayofuatilia

Mambo tunayofuatilia huwa yana athari kubwa kwenye maisha yako. Mambo haya yanaweza kuwa ni vitu tunavyosikiliza, tunavyoangalia na hata tunavyosoma.


Mfano; kunamtu alianza kufuatilia mpira kwa kuangalia kwenye Tv, kwenye simu alafu akaanza kwenda mpaka uwanjani kushapikia na sasa amepewa nafasi za juu katika timu ya mpira anayoishabikia. Sehemu aliopo ni zao la vitu anavyo fuatilia.


Sasa huo ni mfano tu lakini unaonesha jinsi gani kitendo cha kufuatilia vitu kwa kusoma, kusikia au kuangalia kunaweza ingilia maisha yako.
Kama wewe ni mtu unaependa mafanikio ya jambo flani basi usisahau kufuatilia vitu kuhusu jambo hilo kwenye maisha yako. Yani unaweza jifunza toka kwa watu unapotaka kuwa kama wao, soma au angalia video zinazohusu jambo unalohitaji na hata kusikiliza pia.

Mawazo unayowaza au mtazamo wako

Unawaza nini? Ni kibaya au kizuri? Kama ni kibaya, tafuta njia ya kuanza kuwaza vitu vizuri maana Mawazo yanaweza athiri maisha yako. Anza kwakuto jiwazia vibaya wewe, kisha usiwawazie vibaya watu wengine alafu usiwaze vibaya kuhusu vitu unavyohitaji.


Ukiwaza vibaya kuhusu kitu unachotaka kukifanya au kukipata hautaweza weka nguvu ya kutosha kukipata au kukifanya. Mfano ukitaka kuanza biashara huku unawaza “Biashara hii hailipi. Inaowalipa wote itakua wanatumia dawa, sio bure” basi kunajinsi unaweza kuwa hautumii akili yako sana kwenye kufanikiwa kwenye biashara mbali na kuwaza kupata dawa ya biashara.


Usiwe na mawazo ya kushindwa kwenye kichwa chako. Na ili usiwe na mawazo ya kushindwa mara kwa mara, unatakiwa uwe na mtazamo mzuri juu ya jambo lako alafu amini kuwa upo kujifunza.


Mfano; Ukiwa unataka kufanya biashara anza na “Biashara hii watu wengi haiwalipi lakini nataka kuwa kati ya wale inaowalipa. Ngoja nianze kujifunza kwa kuifanya huku nikiwaangalia waliofanikiwa wanafanya nini”. Kwa kuwaza hayo, unaweza kuwa mmoja wa waliofanikiwa maana utajifunza kitu sahihi wanachokifanya mbali na kuhisi tu kichwani mwako.

Ukiachana na upande huo, epuka mawazo yoyote mabaya maana huwa na athari kwenye maisha halisi. Yaelekeze Mawazo yako kwenye vitu vya msingi unavyovihitaji. Tenga muda wa kutulia na kuwaza kwa upana kuhusu maisha yako na vitu unavyo hitaji.


Tofautisha kati ya kuwaza kuhusu mambo yako na kupata “Msongo wa Mawazo”. Baadhi ya watu hawajipi muda wa kuwaza mambo yako wakiamini kuwa huo ndio msongo wa Mawazo. Waza kuhusu maisha yako, vya kubadilisha vibadilishe na vya kukubaliana navyo, vikubali. Jifunze kutoka kwa muhusika mkuu kwenye simulizi ya SUKARI YA DADA alivyokua akitulia kufikilia maisha yake.

Mambo unayoongelea sana

Unapenda kuongea kuhusu nini? Unapenda kuongea na nani? Mambo hayo yanaweza kuwa na mchango mzuri kwenye maisha yako? Kama hakuna basi kunajinsi unatakiwa kubadilika.
Baada ya kuongea na mtu, akili yako inaweza kuwa imeongeza vitu na huyo mtu anaweza kuwa ameongeza kitu kwenye akili yake pia. Vitu hivyo vinaweza kuwa na athari kwenye maisha yenu wote.


Mfano; Mkikutana mmnao penda vilevi na kuongelea vilevi, mnaweza ondoka mmejuzana kuhusu vilevi msivyovijua alafu kichwani mkawa na mawazo ya kuvijaribu vilevi hivyo. Na mnaweza hata kujaribu kweli mkija kuviona.


Lakini watu wa biashara mkiongelea mambo ya mafanikio ya biashara, mnaweza kuwa mmeondoka na mbinu au taalifa muhimu kuhusu biashara. Na pia mnaweza tumia mambo hayo kwenye harakati za kibiashara.
Unapoongea na watu, pata muda wa kusikiliza, uliza maswali na utoe baadhi ya mambo unayoyajua pia.

Ni vema ukawa na maongezi ya vitu vitakavyo kujenga na ili kumpata mtu anaeongea mambo hayo inabidi uwe na tabia ya kuongea mambo hayo. Hii inaweza kukufungulia hata fulsa mbalimbali zinazoweza badilisha maisha yako.

Huu ndio mwisho wa makala hii. Kiufupi ni vitu huonekana vidogo kwenye maisha ya binadamu lakini ni vitu vyenye matokeo makubwa kwenye maisha yake. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Mambo 5 husaidia kukimbiza mafanikio katika miaka 25 mpaka 38

Katika safari ya maisha hapa Duniani, kuna vipindi ambavyo vinaweza kubadilisha mwelekeo wa mtu mwenye ndoto na malengo makubwa kwenye maisha yake. Kipindi cha umri wa miaka 25 hadi 38 ni moja wapo ya nyakati hizo muhimu sana katika Maisha ya mtu. Katika kipindi hiki, watu wengi wanakuwa na nguvu za ujana, mawazo mapya, na hamasa ya kutimiza malengo. Kipindi hiki mtu anaweza tengeneza maisha anayohitaji kuyaishi. Lakini hiki sio kipindi rahisi, ni kipindi kigumu kinachoweza kukufanya upoteze muelekeo wa Maisha kabisa na kupoteza mambo mengi uliopanga Maishani.

Kunaweza kuwa na mambo mengi sana magumu yanayoendelea kichwani kwa mtu katika kipindi cha miaka 25 mpaka 38 yanayohusu maisha yake. Mambo hayo yanaweza kuwa ni kutokana na taaluma zao, familia, au hata kufuatilia ndoto za muda mrefu ambazo zimekuwa zikisubiri utekelezaji.

Kutokana na ugumu wa kipindi hiki baadhi ya watu hukata tamaa katika kukimbiza mafanikio. Katika makala hii, tunaangalia mambo matano ya kuyaelewa ili kuendelea kukimbiza mafanikio au ndoto katika miaka 25 mpaka 38. Haya mambo matano yanaweza kuwa mwongozo wako wa kukusaidia kupitia changamoto na kufurahia matunda ya juhudi zako.

Fahamu kuhusu AI kuchukua Ajira za watu BONYEZA HAPA>>>

Mambo 5 husaidia kukimbiza mafanikio katika miaka 25 mpaka 38

Kuelewa kipindi ulichopo na game yako

Kipindi cha miaka 25 mpaka 38 ni kipindi ambacho mara nyingi huwa kigumu sana katika Maisha ya mwanadamu. Ni kipindi ambacho mtu anatakiwa kufanya mambo yatakayo tengeneza maisha yake huku akipitia changamoto mbalimbali. Kwaiyo ukiwa kwenye kipindi hiki na unapitia magumu na mawazo mengi juu ya maisha yako, fahamu ni kipindi sahihi mtu kufanya hivyo. Pamoja na yote unayopitia, ielewe game ya maisha yako iko vipi alafu usichoke kuicheza mpaka utakapofika unapotaka. Ninaposema “Ielewe game” namaanisha jielewe wewe ni nani, unakumbana na changamoto gani, utafanya nini ili uwe unapohitaji kisha fanya kinachotakiwa kufanywa kuwa unapotaka kuwa. Kila mtu anacheza game yake duniani na sio rahisi.

Kujisamehe makosa

Katika umri huu unaweza fanya makosa mengi sana na kichwa kinaweza kukuletea Mawazo mengi yanayohusisha neno “Ninge”. Fahamu kuwa unapaswa kujisamehe mambo yote unayohisi ulifanya makosa kwenye maisha yako ili uweze kusonga mbele. Achana na mambo yote ya nyuma Kisha igeukie sehemu unayoenda. Mtu ukiwa unakimbia alafu ukajigonga kidogo na jiwe kwenye mguu lakini ukaendelea kukimbia ukiangalia mbele unaweza fikia sehemu unayoenda. Ila ukiendelea kukimbia huku umegeukia jiwe lililokugonga, unaweza anguka kabisa.

Pesa sio kila kitu ila ni kitu muhimu kuwa nacho

Kama mafanikio kwako yanamaana inayojumuisha pesa elewa kwanza pesa sio kila kitu hapa Duniani lakini ukishaelewa usiache kutafuta pesa. Mambo mengi hapa Duniani yanahitaji pesa na ukiwa hauna pesa hauwezi yapata kirahisi. Pesa usiiweke mbele ila iweke kwenye vitu muhumu maana usipoiweka kwenye vitu muhumu unaweza ukakosa nguvu ya kuitafuta alafu utaanza kusukumwa kukitafuta pesa kwasababu ya shida ulizonazo. Penda kutengeneza pesa hata bila kusukumwa na shida. Jifunze mambo mbalimbali yanayohusiana na kuweka uchumi wako vizuri au kujiimarisha kwenye mambo ya pesa. Usiogope kuchukua Daftari na kuandika mambo yako na mahesabu ya pesa au mipango yako ya uchumi.

Muda haukusubiri na hakuna mzuri zaidi wa kukimbiza mafanikio

Fahamu kuwa kadri dakika zinavyozidi kwenda, watoto wanaenda kuwa vijana, vijana wanaenda kuwa watu wazima na wanaenda kuwa wazee. Kuna siku unaweza amka unaitwa “Babu” au “Bibi” na watoto wadogo. Hiyo sio tatizo ila kujua hili inaweza kuwa ni chanzo cha kupata nguvu ya kuchukua maamuzi ya kupambania mambo yako katika muda huu wa maika 25 mpaka 38. Ni muda mzuri sana wa kupambania maisha unayohitaji maana unakua na nguvu ya kutosha kuliko utakavyokua Mzee. Pamoja na Mambo mengi unayopitia usikate tamaa katika kipindi hiki, tafuta njia yakuwa unapopataka bila kuchoka.

Yaamini Mawazo yako

Watu wanamawazo mengi mazuri kuhusu maisha yao lakini hawayaamini kiasi ambacho wanashindwa kuyafanyia kazi. Kama una Mawazo mazuri juu ya jambo flani muhimu kuhusu maisha yako, sio lazima ukamueleweshe mtu mwingine aelewe ndio ujiamini. Unaweza fanya utafiti wako binafsi, unachukua hatua na ukuwaachia watu matokeo. Amini unachowaza maana wazo moja dogo sana linaweza badilisha maisha na kukuweka unapo hitaji. Lakini wazo hilo linaweza kuwa ujinga ghafla baada ya kulitoa kwa watu wasio sahihi.

Ni hayo tu katika The bestgalaxy na natumaini yanaweza kuwa msaada kwa watu wenye miaka iliotajwa. Hakikisha haukai mbali na sisi kwa mambo mengine zaidi.

Jinsi ya kulinda Ndoto zako Maishani zisife

Katika maisha, kila mtu ana ndoto ambazo anatarajia kutimiza akiwa hai. Ndoto hizi zinaweza kuwa kuhusu elimu, familia, au mambo mengine . Mara nyingi, safari ya kuelekea kutimiza ndoto inaweza kuwa na changamoto nyingi zinazohitaji uvumilivu na mapambano ili kuzitimiza. Wengi hukata tamaa na kushindwa timiza ndoto zao wakiwa bado waopo hai. Ni muhimu kufahamu mambo ya kufanya ili kulinda ndoto zako na kuhakikisha unafanikiwa kutimiza pamoja na changamoto nyingi utakazopitia njiani.

Kuna muda mtu unapokimbiza ndoto zako unakua na nguvu ya kuendelea kuzifuata. Lakini katika safari hiyo, Kuna muda mtu unaweza fikia hauna nguvu tena ya kuendelea kuikimbiza ndoto kutokana na mambo unayokutana nayo safarini. Inaweza fikia wakati mtu unaamu kupuuza ndoto yako kwa kuamini kuwa “haiwezi kuwa kweli” na kujiona mjinga kwa hatua zote ulizopiga ili kufikia.

Kama unandoto na unahitaji kutimiza, Hapa The bestgalaxy tunaenda kukupa mambo machache muhimu yatakayo ilinda ndoto yako isife kama ndoto za watu wengine.

Mambo matano yanayoweza kukusaidia kufanikiwa Maishani BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kulinda ndoto zako Maishani zisife

Vutiwa na mafanikio ya wengine bila kuchukia


Unapokimbiza ndoto yako unaweza kuwa unaona watu wengi wakitimiza ndoto zao wakati wewe bado. Kushuhudia wengine wakipata unachokosa inaweza kuwa ni jambo gumu kwa moyo. Unaweza jihisi vibaya na hata kuanza kuwachukia waliofanikiwa kwenye jambo ambalo wewe linakuumiza na haufanikiwi.
Ili kuzilinda ndoto zako ni vema ukavutiwa na kufurahia mafanikio ya wengine. Ukifanya hivyo itakua rahisi hata kujifunza mambo ambayo waliofanikiwa wameyafanya ili kufanikiwa. Lakini ukiwachukia utakua huoni la kujifunza na ukionawanaendelea kufanikiwa, utaumia na kupoteza muelekeo wako.

Unayoyapitia yanakuandaa kwa yajayo

Kila magumu unayopitia kwenye kuikimbiza ndoto yako, yanakuandaa kwaajili ya kutimiza ndoto unayoikimbilia. Hivyo haina haja ya kukata tamaa unapopitia magumu. Ukidondoka au kuumizwa, nyanyuka futa machozi, jiulize jambo hilo limekufunza nini kisha songa mbele. Kuna watu wanasema “hauwezi kuiona thamani ya kitu muhimu maishani ulichopata kama haujapata shida kukitafuta”. Vitu vingi vya thamani vinakua na ugumu kuvipata na huo ugumu ndio thamani yake.

Chagua mtazamo mzuri juu ya kifo

Upande wa kifo ni upande ambao watu wachache huuongelea linapokuja swala la kutimiza ndoto maishani. Watu wengi wanapokua wanaona Matukio kuhusu kifo katika mazingira yaliowazunguka, ndoto zao huyeyuka. Huwa wanakosa nguvu ya kuendelea kukimbilia ndoto zao huku moyoni wakijisemea “Duniani Tunapitia”. Hatugusii upande wa kidini ila Kama unandoto na upo hai jambo hilo lisiwe kisingizio cha kutotimiza ndoto yako. Amini vyovyote ila usitupe ndoto zako ukiwa hai maana ndoto zako zinaweza kuwa ni zaidi ya uhai wako. Mungu anaweza kuwa anataka hata kizazi chako kukibadilisha ila ni baada ya wewe kutimiza ndoto. Ndoto ya mtu inaweza kuwa ni kubwa kuliko hata Dunia ndio maana kuna ndoto watu walizikimiza wakajikuta wamebadilisha Dunia.

Kuwa na Sababu kubwa kuliko wewe ya kutimiza ndoto zako

Ili ndoto yako iwe imara na isije kufa kizembe, unganisha ndoto hiyo na mambo makubwa kuliko wewe. Unapofikilia Sababu za kuikimbiza ndoto yako, weka sababu kubwa ya kutimiza ndoto yako na sio vitu vidogo kama gari au nyumba. Fikilia kuhusu maisha ya watoto wako, familia yako na vitu vingine vikubwa na vya muhimu kama hivyo.

Fahamu hakuna binadamu anaona ndoto yako kama uionavyo

Hakuna binadamu anaeona vitu unavyoona au kufikilia. Hivyo hivyo hakuna mtu anaeona ndoto unayoikimbiza kama jinsi unavyoona wewe. Hivyo ukimuona mtu anakucheka, anakukatisha tamaa au kukudharau, usikate tamaa maana hakuna analojua kuhusu wewe na ndoto yako. Ndoto yako inakuhusu wewe hivyo unaiona wewe pekeako alafu watu wengine wanaona matokeo tu. Usihangaike na watu wanaokudharau, kuogopesha au kukukatisha tamaa, wewe endelea kufanywa kinachotakiwa kufanywa ili uwe unapotakiwa kuwa kwenye maisha yako.

Natumaini makala hii itakua msaada katika Maisha yako na huu ndio mwisho lakini The bestgalaxy inavitu vingi kwaajili yako. Endelea kuwa karibu nayo kwa mengine zaidi.

Kwanini haufanikiwi kimaisha? Sababu hizi hapa

Kila mtu unaweza kumsikia akiongelea kuhusu mafanikio lakini unapaswa kujua kuwa watu hawana maana sawa ya mafanikio. Hata ukiwauliza “Mafanikio ya kimaisha ni nini kwako?” watu huwaza vitu ambavyo hutegemeana na jinsi mafanikio yana maana gani kwao.

Kiufupi Mafanikio ya kimaisha tunaweza sema ni hali au matokeo ya kuweza kufikia lengo au malengo fulani maishani. Tunaweza pia kusema mafanikio ni kufikia au kuzidi matarajio, malengo, au viwango fulani vya utendaji katika maeneo mbalimbali ya maisha kama vile kazi, elimu, biashara, mahusiano au maendeleo binafsi.

Watu hukutana na changamoto nyingi katika kuyakimbiza mafanikio ya kimaisha. Hapa The bestgalaxy tumeisha zungumzia kuhusu mambo muhimu ili kufanikiwa pamoja na changamoto nyingi njiani. Katika ukurasa huu tunaenda kuangalia upande mwingine ambao ni mambo yanayoweza fanya mtu asifanikiwe.

Mambo yanayoweza fanya usifanikiwe

Kutojua mafanikio kwako ni nini na yanapatikana upande gani

Kama tulivyoeleza hapo juu, Kila mtu kuna jinsi ambayo mafanikio yanaonekana kwake. Sasa unapaswa kwanza kujiuliza wewe unahisi mafanikio ni nini kwako. Ni elimu ambayo itakupatia kazi? Ni biashara ambayo itafanya vizuri mpaka itabadili maisha yako? Usiwe na vitu vingi kichwani, fahamu mafanikio unayoyataka hapa Duniani na fikilia utayapata upande gani.


Kuna mtu aliulizwa “Unata kufanikiwa kivipi?” Akajibu “Kama msanii diamond… Yani nyumba kali, gari Kali na watoto wazuri kama wote… Alafu navimba kama kwenye nyimbo yake moja hivi. Yani nikisimama watu wote shangwe” akaulizwa “kwani wewe ni msanii?” Akajibu “hapana” akaulizwa tena “Unaimba mziki?” Akajibu “ah amna hata siwezi. Na sijikufanya kabisa hizo mambo”
Huyu jamaa kitu anachotamani maishani au mafanikio anayoyatamani ni ya mtu ambae ni msanii. Sio kitu baya, lakini yanaweza timia vipi ikiwa haupo kwenye upande ambao yanapatikana?. Hapa ukizidi kutamani, utapata msongo wa mawazo.


Ni vema kujua mafanikio kwako ni nini na yanapatikana upande gani. Kama mafanikio yako unahisi yatapatikana kwenye biashara, kuwa upande wa biashara, bana upande huo ata uwe msaidizi tu. Tambua kitu unachokihitaji alafu usicheze nacho mbali, pambana kukisogelea.

kubadirisha au kuyakatia tamaa malengo yako

Kujiweka malengo ni hatua nzuri ya kuanza safari ya mafanikio. Lakini mara nyingi malengo huwa na changamoto zake katika kuyatimiza. Unaweza kukumbana na vitu vingi sana katika safari ya kuyatimiza. Lakini unatakiwa kuwa makini sana linapokuja wazo la kubadirisha au kuyakatia tamaa malengo uliojiwekea. kubadirisha au kuyakatia tamaa malengo uliojiwekea inaweza kuwa ndio mwanzo wa kupotea na kushindwa kufikia mafanikio unayoyahitaji. Ni vema kupambana na kuwa msimamo wa kutimiza malengo yako ili uweze pata mafanikio unayoyahitaji.

Kukosa utayari wa kuwa unaetakiwa kuwa au kuacha vinavyo rudisha nyuma.

Inasemekana kwamba kunawatu huwa wana mipango mikubwa kwenye vichwa vyao, tena inayoweza kuwatoa waliopo. Watu hawa wanajua kila kitu kinachohitajika kufikia pale wanapotamani kuwa kimaisha. Sio hayo tu, wanajua mpaka kinachowafanya wasifikie mafanikio lakini hawapotayari kubadirika au kuacha vinavyo zuia kufanikiwa.


Ukitaka kufanikiwa mara nyingi inabidi uwe ni mtu unaweza badirika, kujifunza vitu vipya na kuwa na utayari wa kuacha mambo unayoona kabisa yanakuzuia. Usipo chukua hatua kwenye kufanya mambo hayo, unaweza jikuta unayaona mafanikio unayoyataka mbele yako lakini huyafikii.

Woga wa kushindwa au kuwa tofauti

Kama mafanikio unayoyataka yanahitaji ufanye kitu ili kuyafikia lakini unahisi woga basi tambua kwamba baada ya miaka kadhaa unaweza jutia kuogopa kwako. Wengi tukitaka kufanya bishara au vitu vya maandeleo vitakavyo boresha maisha yetu, huwa tunaogopa kudondoka au kuogopa ndugu, majirani, marafiki na watu wengine waliotuzunguka. Lakini jambo hili watu hujutia baada ya kutambua kuwa walitaka kufanya vitu vizuri ila walishindwa kutokana na kuogopa au kuwawaza watu ambao hawajaungana na maisha yao. Kama umefuatilia simulizi ya utamu wa jumla unaweza nielewa zaidi hapa.


Njia rahisi ya kuondoa woga wakufanya kitu unachotaka kukifanya ni kuingia wenye mazingira yanayohusiana na unachokitaka kukifanya. Kama unataka kuwa mfanya biashara wa samaki, Tafuta marafiki wanaojihusisha na mambo hayo, au naenda kwenye mazingira ya hayo mambo.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook