Tag Archives: Love

Jinsi ya kuwa mtu wa thamani kwa mpenzi wako

Karibu kila mtu anatamani kuwa mtu wa thamani kwa mpenzi wake. Katika makala hii, tutaorodhesha mambo muhimu yanayoweza msaidia mtu kuwa mpenzi bora na kuongeza thamani katika uhusiano. Unaweza fanya mambo ya kwenye makala hii ili kumfanya mpenzi wako anaekupenda akupende zaidi. Lakini pia Mahusiano ya mapenzi yakiwa hayapo sawa na unaona thamani yako kwa mpenzi wako imeshuka, unaweza jaribu mambo ya kwenye makala hii.

Ikiwa unataka kujua jinsi ya kuwa mtu wa thamani zaidi kwa mpenzi wako, endelea kusoma makala hii mpaka mwisho. Lakini tambua kuwa kupambana kuwa mtu wa thamani kwa mtu asiyekupenda kunaweza pelekea kuumizwa na kujishusha thamani yako pia. Kwaiyo ni vema kutotumia nguvu kubwa kutaka kuwa mtu wa thamani kwa mtu asiekupenda. Kuna muda mtu huvipa thamani vitu anavyo vipenda.

Sms za kumsifia mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Fanya haya kuwa mtu wa thamani kwa mpenzi wako

Kuwa upande wake na msaada kwenye matatizo au shida zake

Watu wa thamani sana katika Maisha ni watu wanaokua upande wako unapokua na shida. Watu wengi hukimbia linapokuja swala la shida na wanaobaki hua ni watu wa thamani sana katika Maisha. Sasa kama unataka kuwa mtu wa thamani kwa mpenzi wako, unaweza fanya hivyo kwakua na tabia ya kuwa upande wake na msaada kwenye matatizo au shida.
Unaweza kumsaidia ushauri au pesa kidogo kwenye matatizo au shida na akakuona wa thamani sana.

Kuwa muaminifu katika Mahusiano

Watu wengi hua wanatamani kuwa na wapenzi waaminifu kwenye mahusiano ili mioyo yao iwe na amani. Ukikutana na watu hawa ambao ni waaminifu na ukawa muaminifu kwao, unaweza kuwa mtu wa thamani sana. Uaminifu hutuliza moyo wa mpendwa wako na kufanya afurahie mapenzi kwa amani.

Weka nae malengo ya wazi

Watu wengi huona mtu wa thamani kwenye mahusiano ni yule mwenye malengo ya kuwa pamoja maishani. Ukiwa mtu unaeyaweka wazi malengo ya kuwa pamoja nae kwa mpenzi wako, utakua na thamani tofauti na watu wengine kwenye maisha yake. Ukifanya hivi kama mpenzi wako ana mapenzi ya dhati, anawezakuona unamalengo ya kuwa nae maishani na sio kumpotezea muda. Hii inaweza pelekea akuone wathamani sana kwenye maisha yake akiwa mwanamke au mwanaume.


Ni hayo tu katika ukurasa huu, The bestgalaxy tumekuandalia machache haya lakini Kuna mengi unaweza jifunza kupitia sisi. Kikubwa usiache kufuatilia The bestgalaxy.

Michezo ya kuchati na Mpenzi wako kurefusha maongezi BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kujua mpenzi ulienae anakupotezea muda

Katika safari ya mapenzi, ni muhimu kujua kama mpenzi ulienae anakufaa kwa muda mrefu au anakupotezea muda. Wengi tunajua mahusiano ya mapenzi yanaweza anza popote na yanapoelekea inabidi yawe ni mahusiano ya kuwa pamoja katika Maisha. Hata dini huwa zinasimamia juu ya hili ndio maana watu wanaopendana kidini wanatakiwa waingie katika ndoa na kuishi pamoja.


Katika kutafuta mpenzi ambae utakua nae kwenye maisha, unaweza kutana na watu wengi, ukaingia nao kwenye mahusiano na musifanikiwe kuwa pamoja maishani. Endapo utatumia muda mrefu kuwa na mtu au mpenzi ambae hawazi kuwa nawewe maishani unaweza jilaumu baadae kwa kupotezewa muda. Jambo hili ni baya kwa mwanamke na hata mwanaume.

Bahati mbaya ni kwamba inaweza kuwa ngumu kujua moja kwa moja mtu ambae hatafika na wewe mbali. Lakini uzuri ni kuna ishara unawezeza kuziona zinaweza kuwa ni ishara za mpenzi ulienae kukupotezea muda. Ishara hizi The Bestgalaxy tumeziweka hapa chini.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kujua mpenzi ulienae anakupotezea muda

Kufanya mahusiano yenu siri.

Ukiwa kwenye mahusiano ya dhati mara nyingi huwa manashindwa kujizuia kuyaonesha kwa watu wengine. Lakini kama utakua kwenye mahusiano na mtu anekupotezea muda atakua makini sana kufanya mahusiano yenu yasijulikane na wengine. Anaweza hata kukuambia usimwambie mtu kuhusu mahusiano yenu ili mue kwenye mahusiano ya Siri. Sasa swali hapa ni “kitu gani kina mfanya awe makini na usiri?”. Mara nyingi inakua ni kwasababu anampenzi mwingine anaemuheshimu kuliko wewe. Kama ni mwanaume anaweza kukupa pesa na kila kitu cha gharama ili mladi mahusiano yawe Siri. Hii inaweza kuwa ni ishara kuwa hana mpango na wewe na anakupotezea muda.

Mnatafutana kwa haja za mwili au pesa.

Sawa mnaweza kuwa kwenye mahusiano ya mapenzi na mnaambiana “nakupenda” kila mara lakini kitu gani kikubwa huwakutanisha na kufanya mkumbukane? Kama ni shida za pesa au shida za mwili basi hizo ni dalili mbaya. Mapenzi kuwa pamoja maishani ni zaidi ya pesa na tamaa za mwili. Kama hakuna kitu kinachowaweka pamoja mkakumbukana mbali pesa au shida za mwili basi mnaweza kosa hata uwezo wa kuwa pamoja maishani. Ukiona dalili hii kwa mpenzi wako, kuwa makini maana si nzuri.

Mambo ya kuepuka katika Mahusiano BONYEZA HAPA>>>

Huficha mambo yake na hataki kujua sana kuhusu wewe.

Kwenye mahusiano mtu anaekupotezea muda huwa hataki ujue vitu vingi kuhusu yeye. Anaweza kukuficha kuhusu ndugu zake, sehemu anayotoka na hata jina lake kamili. Mbali na hayo hata ikija kwa upande wake utaona hajishughulishi kujua kuhusu wewe sana. Anaweza asitake kujua kitu zaidi ya jina lako na namba ya simu. Hataki kukuingiza sana kwenye maisha yake na pia hataki ingia sana kwenye maisha yako kwasababu anajijua kuwa kwako si wakudumu.

Hajali kuhusu wewe kwenye vitu muhumu.

Unaweza umwa au kuwa na jambo la muhimu lakini asijishughulishe kwa chochote. Kiufupi unaweza kuwa nae kwenye mahusiano lakini haoni kama mambo yako yanamuhusu sana. Anaweza kuwa Hana wivu kabisa na wewe.
Hii ni dalili ya kuwa yupo kukupotezea muda na anajiona kabisa hayupo karibu na wewe hivyo kuwa makini.

Ni hayo tu katika ukurasa huu. Natumaini yanaweza kuwa msaada kwa mwanamke au mwanaume yoyote ambae yupo kwenye safari ya kutafuta mtu wa Maisha. Endelea kuwa karibu na ulimwengu wa The bestgalaxy.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kum-surprise/kumshangaza mpenzi wako bila kutumia Pesa


Katika maisha ya mahusiano na mtu kunakua na vitu vingi ambavyo mnaweza fanyiana ili kufurahishana mkiwa kama wapenzi. Maisha ya upendo yanakua na mambo mengi ya kufurahisha kiasi ambacho ukikaa na kuyafikilia, tabasamu linaweza kukujia tu. Matukio muliofanyiana kwa msukumo wa upendo mukiwa kama wapenzi ndio mara nyingi hubakia akilini na kufurahisha moyo kila mkiyakumbuka au kufikilia. Lakini pia Matukio haya huwa yanaumiza pindi mtakapoachana au mkishindwa kutimiza ahadi zenu za kuwa pamoja mlizojiwekea.



Kumfanyia surprise mpenzi wako ni jambo zuri la kumfurahisha mapenzi wako na pia hutengeneza kumbukumbu nzuri katika safari ya mahusiano. Watu wengi wanapotaka kuwafanyia surprise wapendwa wao huwaza mambo yanayohusisha pesa tu na kusahau kuwa surprise sio lazima iwe hivyo.


Kum-surprise mpenzi wako ni kufanya jambo au kitu cha upendo cha kumshangaza na kumuacha na furaha. Unaweza fanya jambo linalo husisha pesa kum-surprise lakini kuna mambo yasio husisha pesa unaweza yafanya pia na akafurahi. Hapa chini The bestgalaxy tumejaribu kukufungua kidogo kwa kukupa matokio au mambo ambayo unaweza fanya kumshangaza mpenzi bila kutumia Pesa.

Zawadi za kumpa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kum-surprise/kumshangaza mpenzi wako yasio husisha Pesa

Kumpiga simu usiku sana kumwambia umemkumbuka



Ikiwa mkombali na sio kawaida wewe na yeye kuongea kwa simu usiku, njia hii inaweza kuwa nzuri na itamshangaza zaidi. Subiri usiku ufike kisha jaribu kumpiga simu itakayo muamsha usingizini. Inaweza kwa sio rahisi kumuamsha kwa simu lakini kama ukifanikiwa akapokea basi atakua ameshangazwa na simu yako. Akili itakua inatamani kujua nini kimekufanya upige simu usiku na bila kusita unaweza kumwambia sababu ni kumkumbuka, yaani umemiss. Unaweza isindikiza sababu hiyo na maneno matamu kuonesha moyo wako ulikua unatamani sana kusikia sauti yake usiku huo mpaka ukashindwa vumilia kukuche.

Kumsaidia au kufanya kazi ambazo kikawaida hufanya yeye



Kama kuna kazi au mambo ambayo kikawaida mpenzi wako huwa anafanya yeye unaweza afanya wewe ili kumshangaza. Kama ni mwanaume unaweza mkupikia mwanamke wako au ukamsaidia kupika huku ukipiganae stori kama rafiki tu. Mbali na kupika unaweza msaidia kufanya usafi wa nyumbani ambayo kikawaida hufanya yeye. Jambo hili linaweza mshangaza sana mpaka akakuuliza. Unaweza mjibu kuwa “nimeamua kukusaidia tu mpenzi wangu, nakupenda sana” au maneno mengine kama hayo.

Kumuandikia barua ya karatasi ya kawaida kwa mkono wako



Kutokana na Teknolojia watu tunatumia sana simu katika kuwatumia maneno mazuri tunao wapenda. Lakini ukihitaji kumshangaza mpenzi wako kwa sasa, mfikishie ujumbe huo kwa karatasi ya kawaida. Hakikisha unaiandika kwa mkono wako mwenyewe na unaiandika kwenye karatasi ya kawaida tu na sio karatasi maalumu. Hatakama unapesa za kununua zile kadi za upendo zenye maneno ya mapenzi, fahamu kuwa njia ya kuandika mwenyewe ni yakushangaza zaidi. Kunajinsi mpenzi wako anaweza hisi unampenda mno na yupo kichwani mwako sana. Mbali na hayo utakua umeweka kumbukumbu isio sahaulika kirahisi akili mwake.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Kumuimbia wimbo mzuri wa mapenzi



Ninapoongelea kuimba simaanishi uwe msanii alafu umtolee nyimbo ambayo atakua anasikiza kwenye Redio. Na maanisha kuimba mbele yake nyimbo yoyote ya msanii iliobeba ujumbe wa mapenzi kuhusu nyinyi. Sio lazima uwe na sauti nzuri, kikubwa ni umshangaze tu. Unaweza jitoa ufahamu kidogo ukamwambia akuangalie na kukusikiliza mpaka mwisho bila kukukatisha. Jambo hili ninaweza mshangaza sana kama sio kawaida yako na litatengeneza kumbukumbu nzuri kati yenu wapenzi.



Mambo tuliozungumzia hapo juu ni machache kati ya mengi unayoweza kufanya kumshangaza mtu wako bila pesa. Mambo madogo madogo kama haya kwenye mapenzi huwa yanaunda historia nzuri isioweza futwa kirahisi. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy, tunaenda kujifunza mambo mengine zaidi.

SMS za kumsifia mpenzi wako (Mwanamke au Mwanaume)

Karibu the bestgalaxy na hapa katika makala tunaenda kuangalia SMS za kumsifia mpenzi wako. Hakuna raha kama kusifiwa na mtu unaempenda. Mtu ukisifiwa na unaempenda toka moyoni unaweza hisi Duniani upo juu na wathamani sana. Kiufupi maneno mazuri ya kusifu yakitoka kwa wapenzi au watu tunao wapenda huwa yanaupasua moyo kwa furaha na kufanya tuhisi kuwa tunathamani. Hivyo ukitaka kuugusa moyo wa mpenzi wako kwa kiasi hicho si vibaya ukatumia sms nzuri za mapenzi za kumsifia mpenzi wako. Hii inaweza kufanya awe na furaha, aione thamani yake na kujua umetambua thamani yake pia.


Kupitia ujumbe mfupi wa SMS, unaweza kumwambia mpenzi wako jinsi unavyomheshimu, kumjali, kumkumbuka na kwanini upo hivyo kwake. Unaweza fungua moyo wako kwake na kumwagia sifa zake zote nzuri.
Makala hii imekukusanyia ujumbe au sms ambazo unaweza kutumia kumsifia mpenzi wako mwanaume au mwanamke ili ajisikie vizuri na kujua jinsi unavyomthamini. Kama utahitaji unaweza ziangalia hapa sms chini

Zawadi za kumpa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

SMS za kumsifia mpenzi wako (mwanaume au mwanamke)

  • Ninafuraha kwakua nina Bahati sana. Bahati ya kwanza ni kufikia siku ya Leo na bahati ya pili ni kuwa na wewe mpaka leo. Nitakupenda Milele mpenzi wangu, wewe ni mtu muhimu kwangu.
  • Ivi ni nani alikufundisha Mapenzi? Yani hata kukuchiti siwezi, naona ushenzi. Nanenepa kwa Mahaba yako na chini ya shuka nakula mpaka mfupa, sitemi.
  • Najua huwenda kunasiku unahisi umewahi niudhi na kuna pia siku unahisi unanifurahisha. Lakini ukweli ni kwamba nazifurahia siku zote nilizokua na ntazokua na wewe. Nakupenda sana furaha yangu.
  • Hapo zamani nilikua naomba mungu nikutane na mwanaume jasiri, anaenipenda, anae nijali na kunithamini. Nashukuru mungu kwa kunileta karibu nawe. Mwanaume upo moyoni, unazunguka kwenye damu mpaka akilini. Nakupenda honey.
  • Wanasema “mapenzi ni matamu” ni kweli, umenipa nikaamini. Wanasema “Raha ya mapenzi umpate anae kupenda na kuyajua” hata siwezi pinga maana Raha naiona tangu ulivyoungana na mimi. Nakupenda na sihitaji kutoka penzini.
  • Mapenzi unayonipa yamenifanya nione maajabu. Siku hizi nikifumba macho sioni giza, nakuona wewe. Moyo unajawa na furaha, najikuta natabasamu kila nikikuwaza wewe. Yani naishi maisha ya furaha kwasababu nimekuchagua wewe.
  • Kila siku nikikutazama nakuona mpya katika uzuri wako. Na unanivutia kiasi ambacho tukiwa karibu natamani kugusisha moyo wangu na wako. Nimeisha kuwa teja wa penzi lako.
  • Nilikua natamani kupata na kumpenda mtu mwenyewe sifa nyingi nzuri. Nashukuru mungu kunikutanisha na wewe. Nimekupata sasa, nakupenda na napenda jinsi ulivyo.
  • Nilipokua mdogo nilikua napenda sana kuangalia mwezi na nyota angani. Zilikua zinanivutia sana kila nikizitizama. Siku hizi napenda kuangalia macho yako. Ni mazuri zaidi sana.
  • Lips tu ni tamu zaidi ya pipi, na vingine vitamu havielezeki, nitavitoa wapi kama si kwako? Huniishi hamu na wala wewe si bigG, hivyo sahau swala la mimi kuondoa moyo wangu kwako.
  • Huwa napenda vile unavyo vaa, unajipatia wewe malaika. Ni msafi unaependeza. Unakua kama nyota inayong’aa angani ambayo mungu ameichukua amenipa.
  • Ndoto yangu ya kuwa na mtu ninaempenda maishani, ilianza kutimia nilipokutana na wewe kipenzi changu. Kwasasa nipo pamoja na wewe, najiona naishi kwenye ndoto yangu, Nakupenda sana.
  • Macho yangu yakikutana na yako, moyo wangu hulipuka kwa furaha. Wewe ni mzuri kama malaika ulieshushwa kwangu, namuomba mungu, usiote mbawa.
  • Hakuna njia ya kuachana na mimi isio niumiza. Siwezi kukupoteza alafu nikwa na furaha au bila kuumia. Nimekuweka moyoni mpenzi, wewe ni muhimu kwangu . Nahisi nakupenda.
  • Mambo mazuri yote nilianza kuyaona maishani nilipokupata wewe. Umekua ni mwanamke mzuri unaevutia mambo mazuri kama ulivyo wewe.
  • Maua hufanya bustani ipendeze na kuvutia. Upendo wako wewe, hufanya nijione wa thamani kwenye hii Duniani. Nakupenda sana.
  • Uwezo wako wa kunitambua na kuelewa ninachohitaji bila kusemwa, hufanya mahusiano yetu kuwa ya kipekee sana. Unanipenda sana, najua. Na Mimi nakupenda kuliko unanyojua. Nitaishi nikiwa nawe moyoni mpaka mwisho wa Dunia.
  • Unajua kupenda malaika wangu. Penzi lako hufanya nione bahati kuwa na wewe. Sauti yako, hunibembeleza. Najihisi kuishi mbingu ya saba na upendo wako ndio umenileta.

Sms hizi zimewekwa hapa kwaajili ya watu wa Jinsi zote. Kama ni mwanaume unataka kumtumia mwanamke/mke unaempenda, unaweza pata sms inayofaa. Na hata ukiwa mwanamke pia unaweza pata sms kwaajili ya Mwanaume/mme. Wakati ukifurahia hayo, endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Vitu vya kushangaza ambavyo hutokea ukimpenda mpenzi wako sana

Mahusiano ya mapenzi ni jambo la asili ambalo binadamu tunajihusisha nalo katika maisha yetu. Naweza sema mahusiano ya mapenzi ni jambo linaloweza fanya binadamu afurahie maisha yake. Ingawa kwa wengine wanaweza pitia maumivu kwenye maisha kwasababu ya mpenzi, lakini bado mahusiano ya mapenzi ni jambo la kumfurahisha katika maisha yake.

Ila hii haimaanishi kuwa ukiwa kwenye mahusiano yenye maumivu, haupo kwenye mahusiano sahihi kwenye maisha yako. Maumivu yanawezakua ni mapito tu katika mahusiano yako. Na mahusiano ya mapenzi ni zaidi ya kuishi mukiwa na raha au furaha ndio maana watu wanaopendana wanaapishwa kuendelea kuwa pamoja kwenye shida na Raha. Hapo hapo tena mahusiano yanaweza sababisha upate furaha na faraja kwenye shida.

Hapa the bestgalaxy leo tunaenda kuangalia mambo ya kushangaza ambayo watu husema yanawatokea wanapo mpenda sana mtu kwenye mahusiano. Bila kupoteza muda, hebu tuangalie mambo haya.

Vitu vya kushangaza ambavyo hutokea ukimpenda mpenzi wako sana

Unasukumwa kukutananae au kuongeanae bila sababu

Inasemekana ukimpenda mtu sana unaweza jikuta mara nyingi unatamani kuongea nae lakini hauna cha kuongea. Yani unaweza piga simu ili tu muongee na mpenzi wako au ukakutananae lakini jambo kuu la kufanya hivyo usilijue. Unakua ni msukumo tu usioelezaka unaotoka moyoni kutaka ufanaye hivyo bila sababu ya msingi ila upendo tu.

Unaweza waza mpenzi wako na akatokea mazingira uliopo

Kuna watu husema kwamba walikua kwenye mazingira falani wakiwaza kuhusu mpenzi wanaempenda alafu akatokea katika mazingira hayo. Linaweza kuwa ni jambo ambalo halimtokei kila mtu au mara kwa mara lakini baadhi ya watu wana sema wamewahi patwa na jambo hili kwa wapenzi wao wanaowapenda mara moja au zaidi. Wanasema unaweza kuwa katika mazingira kama sokoni ukamuwaza mpenzi wako alafu ghafla ukamuona anapita maeneo hayo.

Unaweza muita mtu jina lake

Kumuita mtu kwa jina la mpenzi wako unaempenda, nalo ni jambo la kushangaza. Kuna watu wengi wanakumbana na hili jambo wanapokua wamempenda sana mtu. Unaweza ukawa ni mwanaume au mwanamke mwenye mpenzi mwenye jina lililo kukaa kichwani sana mpaka unajisahau mara chache unawaita watu jina la lake kimakosa.

Ukiona dalili hizi ujue akaunti yako ya Facebook si salama BONYEZA HAPA>>>

Ukisikia jina lake moyo unadunda

Unaweza mpenda sana mtu kiasi ambacho moyo unakua ni kama umeshikana na jina la huyo unaempenda. Yani ukisikia tu jina la mpenzi wako kitu cha kwanza kukushtua kwenye mwili wako ni moyo. Moyo unaweza dunda pigo moja kuwa nguvu “Pah” baada ya jina hilo kuingia masikioni mwako. Wengine hata wakisoma tu jina la mpenzi huwa moyo hautulii.

Ni hayo tu katika ukurasa huu wa The bestgalaxy, Ni jambo gani kati ya haya limewahi kukutokea katika safari yako ya mahusiano? Watu wengi huona mambo haya wanapopenda mtu, hivyo kama umeyaona, hauko peke yako.

Mwanaume kuogopa wanawake wazuri kupita kiasi (Fahamu kuhusu hii)

Kuna wanaume huwa wanaogopa wanawake wazuri kwao. Kuogopa huku tunakozungumzia sio kuogopa kuwaoa. Yani unakuta mwanaume akimuona mwanamke mzuri wa sura, muonekano au msafi sana, akili huwa inamuhama. Na haimuami kwa matamanio, inamuhama kwa woga.

Kwenye kuongoza ndio muoga kabisa kiasi cha kutojaribu. Anaweza kuwa anaogopa na kuona kwamba mwanamke huyo mzuri ni kiumbe ambacho hawezi hata kukigusa. Anaweza kujiona yupo kwenye wakati mgumu sana endapo atakua kwenye mazingira ambayo amezungukwa na wanawake wazuri. Hatakama atatakiwa kuongea na mwanamke mzuri kuhusu mambo yasio husiana na mapenzi, bado huwa ni mthihani kwake. Katika maisha ya mahusiano, ameisha jiwekea mipaka ya mwanamke wazuri asio weza kuwao nao kwenye mahusiano maana hua wanamchanganya hata akiwa nao karibu tu. Kiufupi ni mwanaume anaeogopa wanawake wazuri.


Kwanza kabisa ni vema kujua kuwa ni kawaida kwa wanaume kuogopa au kuwa na wasiwasi mbele ya wanawake wazuri. Ila kama hali hii imezidi sana inaitwa gynophobia. Gynophobia ni hali ya kuogopa wanawake kiujumla.

Katika upande wa wanawake wazuri, unaweza jaribu kuelewa na kufanya yafuatayo ili kuondoa au kupunguza uoga.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika tendo BONYEZA HAPA>>>

Sababu za Mwanaume kuogopa wanawake wazuri na jinsi ya kujiweka sawa

Mambo unayotarajia

Kuna watu hua wanaingiwa na woga au wasiwasi wanapokua mbele ya mwanamke wazuri. Kuna vitu huwa vinawajia kichwani mara tu ya kuwaona. Yani anaweza kuwa amemuona mwanamke mzuri lakini akili yake imempeleka mbele kiasi kwamba anapoteza umakini katika wakati aliopo. Mfano; anaweza kuwa ameonana ya mwanamke mzuri na anataka kumsalimia lakini kichwani ameisha waza kuwa “Huyu mwanamke mzuri sana. Huenda nikimsalimia hata jibu… Asipojibu itakuaje?”. Kwa kuwaza hayo tu unaweza poteza umakini na kuingiwa na woga.


Kama unajiona unaogopa wanawake wazuri kwasababu hii, jaribu kupunguza matarajio mbaya. Fanya kitu unachoona ni sahihi bila kujali atafikiliaje au kitakutokea kitu gani kibaya. Ukifanya kitu kizuri alafu akakutukana, akakuonesha dharau au kitu chochote kibaya, tatizo litakua kwake na sio kwako.


Pia tabia ya kuangalia video za ngono na kujichua inaweza fanya unapokutana na mwanamke mzuri ufikilie vitu vingi kichwani na kuingiwa na woga au wasiwasi kupita kiasi mbele yake. Kama unajihusisha na tabia hizi, unaweza ziacha au kupunguza ili kujiweka sawa.

Uzoefu

Kuna baadhi ya wanaume hawana mazoea ya kuwa karibu na wanawake wazuri na ndio sababu ya kuwaogopa. Hii inaweza kuwa ni kutokana na mazingira mwanaume uliokulia au aliopo.
Kama unahisi hili inaweza kuwa sababu ya kuogopa wanawake wazuri na unataka kubadilika, anza kwa kujizoesha kuwa nao karibu.

Unaweza anza na kujisukuma kuwasalimia unapokutana nao. Unapojiwekea uzoefu huu, usiwe unawaza kuwaweka kuwa wapenzi wako. Jizoeshe kuwa nao karibu tu na usiwe na lengo la moja kwa moja la kuingia nao kwenye mahusiano. Liweke pembeni kidogo wazo la kuwa nao kwenye mahusiano. Unapo msalimia, anapokuita, unapomuita, unapokua mbele yake au kongea nae, usifikilie moja kwa moja mambo ya mahusiano ya mapenzi.
Kwa kufanya hivyo unaweza zoea na kuwachukulia wanawake wazuri ni wakawaida kwenye maisha yako alafu baada ya hapo, maamuzi ya kuingia nao kwenye mahusiano yatakua ni yako sasa.

Kujiamini na kuijua thamani yako

Kuna watu huwa wanaogopa wanawake na tatizo kubwa ni kushindwa kujiamini tu. Yani wanajiona hawana thamani mbele ya mwanamke wazuri kwao.
Kujiamini sio lazima uwe na pesa. Kujithamini au kutambua thamani yako sio lazima uwe na pesa. Kuna mpka watu kwenye maisha waliaza kujiamini au kujithamini ndipo wakapata pesa.
Popote ulipo kama mwanaume, jiamini na kujithamini pia. Usiionee aibu kazi yako, nguo zako, sura yako, sauti yako, mwendo wako au vitu unavyofanya hata kama unahisi mwanamke mzuri atakidharau. Ukifanya hivyo hata kama hauna pesa, unaweza mtetemesha mwanamke wazuri wenye pesa.

Asante kwa muda wako ndani ya The bestgalaxy. La kuongezea hapa mwisho ni kwamba mtazamo wako juu ya wanawake wazuri ni muhimu kuuweka vizuri ili usiwaogope. Watazame wanawake wazuri kama binadamu wa kawaida na sio malaika kama jinsi tunavyowasifu au wanavyojisifia. Na pia fahamu kuwa uzuri wa mwanamke au urembo anaoweka ni kwaajili yako wewe mwanaume hivyo hauna haja ya kuogopa, furahia kuwaona.

Dalili za mahusiano ya mapenzi yanayo taka kuvunjika na jinsi ya kuokoa

Tulisha angalia vitu au mambo muhimu katika mahusiano ya mbali yanayoweza pelekea mahusiano ya mapenzi kudumu. Kama haukusoma, unaweza BONYEZA HAPA kusoma juu ya hili.
Hapa the bestgalaxy, tunaenda kukujuza juu ya dalili za mahusiano ya mapenzi yanayo taka kuvunjika bila kujali ni ya mbali au karibu. Inaweza kuwa ni ngumu moja kwa moja kueleza mambo yanayo ashiria kuwa mahusiano ya mapenzi yanataka kuvunjika maana kuna mahusiano ya mapenzi hupitia vitu vingi vibaya na bado hudumu. Mahusiano haya ya mapenzi huwa yanafikia hatua ambayo unaweza sema yanaenda kuvunjika lakini yanarudi katika mstari na kuwa poa tena.


Lakini mbali na yote, sisi tumekukusanyia dalili ambazo mara nyingi huwa zinaashiria kuwa mahusiano yanaenda kuvunjika. Pia utapata na mwanga mdogo wa namna mtu unaweza fanya kuyarudisha mambo kwenye mstari.

Kama umeona dalili hizi kwenye mahusiano yako ni vema akazishughulikia maana hatakama mnapendana sana bado huwa zikionekana inamaana mahusiano yapo kwenye hali mbaya kidogo.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Dalili za mahusiano ya mapenzi yanayo taka kuvunjika na jinsi ya kuokoa

Kufifia kwa mawasiliano

Inaweza kuwa sio mara ya kwanza kuambiwa kuwa “Mawasiliano ni kitu cha msingi sana katika mahusiano”. Mawasiliano yakiwa sio mazuri au yamefifia kwenye mahusiano ya mapenzi ni jambo hatari sana maana huashilia mahusiano yanataka kuvunjika au yanaweza kuvunjika kirahisi.

Hali hii inaweza kuwa ni hamuwasiliani kwenye simu au muko sehemu moja lakini hamna muda mnakaa na kuzungumza vizuri.
Ukikusa mahusiano yako yapo kwenye hali hii jaribu kumgeukia mpenzi wako na kutengeneza muda mtaokaa pamoja na kufanya mazungumzo. Usizidishe kuwa buzy kiasi cha kushindwa kumjulia hali mpenzi wako au kutenga muda wa kuongea nae ujue anataka nini, anawaza nini au amepanga kufanya nini.

Mara nyingi ukipambana na kuanza kuongea na mtu, hatakama alikua hataki inaweza fika wakati mnajikuta mnapenda kuwasiliana tena.

Kutojali

Ikifika wakati wapenzi mupo kwenye mahusiano na hakuna tena kujaliana au mmepenguza kujaliana inaweza kuwa ishara mbaya. Katika mahusiano kila mmoja anatakiwa kumjali mwenza wake. Mwanaume anatakiwa kumjali mwanamke na mwanamke pia anatakiwa kumjali mwanaume.

Endapo kujali kutapungua katika upande mmoja au pande zote inaweza kuwa ndio mwanzo wa mahusiano kuvunjika. Hali hii inaweza weka hata urahisi wa mtu kuanzisha mahusiano mengine mapya na mtu ambae anaona atamjali zaidi.
Unapona hali hii katika mahusiano ni vema kumgeukia mwenza wako na kuonesha jinsi gani unamjali. Usiishie kuongea, uoneshe kwa vitendo pia kuwa yeye ana umuhimu kwako, unampenda na unapenda anavyokupenda. Usisahau kujali hisia zake, kumsikiliza, kumsaidia kwenye shida na kuwa upande wake unapoona anakuhitaji.

Mambo muhimu kufanya kwa mpenzi mwenye hasira au ukorofI BONYEZA HAPA>>>

Kupungua kwa hisia au msukumo wa kuwa pamoja

Hisia za upendo na msukumo wa kuwa pamoja ndio mara nyingi hutuendesha kwenye mahusiano. Hisia na misukumo hii huwafanya watu waingie kwenye mahusiano ya mapenzi bila hata ya kuambiana neno “Nakupenda”. Lakini msukumo wa kuwa pamoja na hisia hizi zinaweza pungua watu wakishaingia kwenye mahusiano. Hili hii inaweza pelekea mahusiano kuyumba au kuvunjika kabisa.


Kuna mambo mengi hupelekea jambo hili na kabla ya kuangalia utaokoa vipi, ni vema ukajiuliza chanzo ni kipi. Hili ya kukosa msukumo wa kuwa pamoja au hisia za upendo inaweza tokea kutokana na mambo kama Msongo wa mawazo, mazoea au kukosa malengo na mtu ulienae kwenye mahusiano.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze Kila mala BONYEZA HAPA>>>

Malumbano ya mara kwa mara

Mahusiano nyenye Malumbano ya mara kwa mara yanaweza kuwa ndio yanatoa ishara ya kufikia mwisho japo mengine huendelea. Baadhi ya mahusiano hupitia kwenye malumbano na misukosuko kibao lakini huendelea kusonga. Lakini bado malumbano katika mahusiano yakizidi ni jambo baya linaloweza pelekea mahusiano kuvunjika.


Mukiwa kama wapenzi mukiona malumbano yamezidi inafaa mbanane, mkae pamoja, muweke hasira pembani na kuulizana “kwanini muko hivyo? Na unatakiwa kufanya nini ili kuyashinda kisha muendelee kuwa pamoja kwa amani?”.

Kupotea kwa malengo yenu ya pamoja

Mahusiano bila malengo ya pamoja tunaweza sema ni safari bila muelekeo. Mnapokua kwenye mahusiano, kuongelea mambo yenu ya mbele mtayofanya pamoja au kutimiza ni jambo muhimu. Ni muhimu kuwa na vitu ambavyo hata mkikosana mkikumbuka kuwa mmepanga kuvitimiza kwa pamoja, inakua rahisi kupatana. Endapo mambo au malengo yenu ya pamoja yataanza kukosa uzito kwenu au yatapotea kabisa, inaweza kuwa dalili ya kuwa mahusiano pia yanaenda kupotea.

Ukiona dalili hii ni vema ukazidisha upendo na kuwa karibu na mwenza wako sana alafu mkiongea, mazungumzo yenu yawe yanajumuisha malengo au vitu vya kufanya pamoja.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>

Usianze na mambo makubwa kama ndoa, Anza na madogo ambayo unaweza mtimizia au mkafanya pamoja baada ya wiki toka muongee tu. Mfano; kwenda nae sehemu nzuri, kununuliana vitu au kusaidiana mambo mengine yajayo.

Ni hayo tu katika ukurasa huu tumekuandalia. Lakini kabla ya kuondoka nakukumbusha kuwa mambo haya yanaweza tokea kwenye mahusiano na bado safari ya mapenzi ikaendelea japo mara nyingi huashiria mahusiano yanataka kuvunjika.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Mambo ya kuepuka baada ya kuachana na Mpenzi wako

Muhusiano ya mapenzi yanaweza kuanza vizuri, yakakua, na watu wanaopendana wakawa na ndoto kubwa kwenye mahusiano hayo. Lakini katika safari ya kuelekea kutimiza ndoto zao katika upendo au maisha ya kua pamoja, kuna mambo mengi hutokea na kuyumbisha mahusiano ya mapenzi. Baadhi ya mahusiano huwa yanadumu na kuendelea kusonga mbele pamoja na mambo mengi yanayoyumbisha.


Lakini pia Kuna mahusiano huwa yanavunjika na kushindwa kuendelea kusonga mbele kabisa. Kuvunjika kwa mahusiano huwa kunazalisha watu wenye mitazamo tofauti juu ya mapenzi na tabia tofauti pia. Hapa ndio utasikia “mapenzi ya kweli hamna… siji kupenda tena” na mambo mengine kama hayo. Mitazamo hiyo mara nyingi huja baada ya maumivu yaliosababishwa na kuachana. Maumivu baada ya kuvunjika kwa mahusiano yanaweza kukusukuma ufanye vitu vingi sana.

Japo kuachana na mpenzi hufanya mtu awe na maumivu lakini kuna vitu au mambo ambayo ni vema kuyaepuka.

Mambo ya kuepuka baada ya kuachana na Mpenzi wako

Kufanya vitu ili kumuumiza

Baada ya kuachana, kunaweza kuwa na mawazo mengi sana ya kukusukuma kufanya vitu vitakavyo muumiza mtu ulieachananae. Msukumo huu unaweza kukufanya usiwe makini na kupelekea ufanye maamuzi mabaya ambayo utayaona kama yanamuumiza lakini kwa upande mwingine yana haribu maisha yako wewe. Mfano mzuri ni kujihusisha na wapenzi wengi baada ya kuachana na Mpenzi uliempeda; unaweza hisi unamuumiza ulieachana nae kwa kumuonesha kuwa watu wengi wanakuhitaji lakini kwa upande mwingine ni maamuzi hatari kwako na sio kwake. Unaweza pata magonjwa, unaweza poteza muda wako na vuruga vitu vingine ulivyopanga kufanya maishani.

Kujilaumu au kumlaumu

Baada ya kuachana na Mpenzi wako unaweza kuwa ni mtu wa kujilaumu sana au kumlaumu ulieachana nae. Lakini kujilaumu au kumlaumu hakuwezi fanya kitu zaidi ya kukuletea maumivu pindi unapofikilia. Ni vema kujisamehe wewe na yeye pia alafu ukakubali hali na kuendeleza maisha yako. Chukulia kama yaliopita yote yalipangwa kuwa hivyo kwenye maisha yako na mambo mengi mazuri yanakuja mbele ya maisha yako. Usijishushe thamani kwaajili ya mtu asiyeona thamani yako. Wewe bado ni wathamani na unapaswa kujipenda na kujithamini hata kama umeachana na mtu unaempenda.

Kufuatilia mambo yake

Kufuatilia mambo ya mtu ulieachana nae, kunaweza fanya ukawa unaumia zaidi. Ni vema kama umeachana na mtu, ukaacha kumfuatilia mambo yake maana utakua unaumia pindi atakapokua anafanya vitu vinavyo uumiza moyo wako. Epuka kumfuatilia kwa siri maana utakua unatumia kwa siri hivyo hivyo.

Uamuzi mzuri wa kufanya baada ya kuachana na Mpenzi wako na kuona hakuna uwezo wa kurudiana ni kukubaliana na hali halisi, kujipenda na kuendelea na maisha yako mpaka utakapo taka kuingia kwenye mahusiano tena. Asante kwa muda uliotumia kusoma makala hii na natumaini umejifunza kitu. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi ya tuliozungumzia hapa.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Sms za kubembeleza mpenzi wako

Kubembeleza mpenzi wako sio kuwa mjinga. Ni moja katika ya mambo muhimu kufanya unapokua kwenye mahusiano ya mapenzi na mtu anaekupenda. Na kubembeleza hua kuna nyakati zake na sio kila wakati. Unaweza hitajika kumbembeleza mpenzi wako baada ya tukio lililomuumiza hisia zake, baada ya kuchukizwa, kuonesha hali ya kukataa jambo unalohitaji au unapohitaji kumtuliza moyo wake na kumuweka sawa katika penzi lenu.
Kuna baadhi ya watu husema “mimi sjui kubembeleza kwenye mapenzi” au “mimi siwezi kubembeleza kwenye mapenzi” lakini unapaswa kufahamu kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kubembeleza hawaujui.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>


Kubembeleza mpenzi wako huonyesha upendo na kujali kwako kwake. Yani kunajinsi anahisi unamjali. Kubembeleza mpenzi wako pia kunaweza kuimarisha uhusiano wenu kwa kufanya muwe na maelewano ya amani. Kubembeleza mpenzi wako kunaweza kusaidia kukuza uhusiano wa kimwili na kihisia kati ya wewe na mpenzi wako. Kubembeleza mpenzi wako kunaweza kusaidia kujenga imani kati yenu pia.
Huo ni muhimu wa kubembeleza katika mahusiano ya mapenzi ila kabla hatujaendelea, ukizidi sana kubembeleza inaweza kuwa sio jambo zuri tena. Lakini katika ukurasa huu tunaenda kuangalia sms za kubembeleza mpenzi.
Kutokana na utandawazi, watu hutumia sms kuwasiliana na wapenzi wao. Sasa ukiwa mmoja wa watu hawa, kuna sms ambazo mtu unaweza mtumia mpenzi kubembeleza kwenye mambo mbali mbali kwenye mahusiano yenu. Sms hizo unaweza tulia na kuziandika mwenyewe au unaweza angalia sms zitakazo kufaa hapa chini na kuzitumia.

Maneno ambayo hautakiwi kusema kwa mwenza wako BONYEZA HAPA>>>

Sms za kubembeleza mpenzi wako

  • Wewe ndiye wangu mahabuba unaejua kunipa huba. Mwanamke ambae moyo umeushika. Nitabaki na wewe milele, sitochoka kukupenda malaika.
  • Kuna muda nakaa nawaza jinsi gani naweza fanya ili nioneshe moyo wangu unakupenda kiasi gani ili tu uondoe mashaka juu ya upendo wangu kwako kipenzi. Natamani hata kukupeleka kwa wangu wazazi. Nakupenda sana mpenzi.
  • Usije choka kunipenda honey. Na mimi siwezi choka kukupenda pia. Siwezi hata kuelezea jinsi nafurahi kuwa na wewe dear. Ninapokwambia “nakupenda” moyo wangu ndio unanituma kukuambia.
  • Amini kuwa mimi nakupenda wewe japo wanaonitamani ni wengi. Moyoni mwangu kuna chumba chako wewe, sina vyumba vya wengi na humo upo wewe tu mpenzi.
  • Tumekua hatuelewani sana katika siku hizi. Yawezekana ni shetani amekuja kutuchezea. Hebu tumshinde kwa kuanza siku ya leo vizuri kipenzi. Pamoja na yote tunayopitia, tambua sitamani kukupoteza. Moyo wangu bado unakupenda.
  • Nisikupende wewe ili nimpende nani kwenye hii Dunia? Kuwa na wewe ni ndoto niliokua nasubiri kutimiza hapa chini ya jua. Hakuna anaeweza kuniamsha kwenye ndoto hii zaidi yako. Na sitamani itokee maana nakupenda sana.
  • Ivi katika maisha yako umewahi ona penzi lililodumu kwa kusikiliza sana maneno ya watu? Mimi sijawahi, ila nimeona watu wanaodumu kwa kusikilizana tu. Hebu tupuuze ya watu twende mbele mpenzi wangu, nakupenda wewe tu.
  • Nyakati za usiku wewe hua mwezi na wakati wa mchana wewe unakua jua langu. Kiufupi umekua msaada kila wakati ili nisipote kwenye giza. Nakupenda sana mpenzi.
  • Wewe ni wapeke maishani na ninakupenda, sifikirii kukusaliti na wala sifikirii kukutenda. Nakuomba tuendelee kupendana kila siku siku habbity wangu.
  • Unataka kuondoka kwenda wapi? Unataka kunicha na nani mwenzio? Unataka kuniumiza kweli? Atatibu nani majeraha unayota kuniachia? Hebu tumia dakika chache kufikilia tulipotokea. Kumbuka kuwa nakupenda sana mpenzi wangu.

Mwisho; Sms hizi zinaweza tumika na wanawake au wanaume. Kikubwa unapotumia, hakikisha inaendana na hali yenu ya mahusiano au mazungumzo.

Siku hizi Mapenzi ni Pesa au bado Upendo wa kweli upo?

Uhusiano wa pesa na mahusiano ya mapenzi umekua ukifanya watu wa wawe na imani tofauti kuhusu mapenzi ya sasa. Kuna watu wanaamini kuwa kwasasa mapenzi bila pesa ni hayapo. Na pia Kuna watu wanaamini kuwa mapenzi bila pesa yapo.


Ukweli usio fichika ni kwamba pesa imekua na umuhimu mkubwa sana katika maisha ya binadamu katika kipindi hiki. Japo sio yote, lakini mambo mengi katika maisha ya binadamu huwa yahitaji pesa ukilinganisha na kipindi cha nyuma.

Mapenzi na Pesa

Pesa juu ya Upendo wa kweli


Katika mapenzi, mara nyingi pesa inaanza kuwa juu ya upendo wa kweli kutokana na uhitaji wa vitu au maisha yanayo hitaji pesa. Pesa haiwezi kuendesha au kuvuruga mahusiano ya mapenzi kama watu au wapenzi watakua hawahitaji kufuata maisha au vitu vinavyo hitaji pesa nje ya upendo au mahusiano yao.

Kwa watu ambao huingia kwenye mahusiano yenye upendo wa kweli lakini wanahitaji sana vitu au maisha ya juu yalio nje ya upendo wao au mahusiano walionayo, ni rahisi kutupa chini ndoa au mahusiano walionayo na kuanzisha mahusiano na mtu mwenye pesa au maisha wanayohitaji.


Kuna wanaume wapo tayari kuacha mahusiano yao na kufuata mwanamke mwenye pesa na pia kuna wanawake wapo tayari kuacha mahusiano na kufuata mwanaume mwenye pesa. Hii haipo kijinsia kwa sasa.

Watu hawa wanaweza kuwa hivi kutokana na mazingira waliokulia, hali ya Maisha walionayo, tamaa au mitazamo yao juu ya mapenzi na pesa. Ukizungukwa au ukikutana na watu kama hawa kwenye mahusiano, inaweza kuwa ngumu kuamini kuwa kuna upendo wa kweli tena.

Upendo wa kweli upo

Mapenzi ya kweli yapo na yataendelea kuwepo japo watu hutoa hoja nyingi za kwamba mapenzi ni pesa kwa sasa, hasa katika mitandao ya kijamii. Lakini tukienda kwenye uhalisia, kuna watu wengi tu walipendana na wanapendana bila kuzingatia maswala ya pesa. Kuna watu wengi pia ambao wanapesa nyingi lakini upendo haupo kati yao kiasi kwamba wanaanza kutafuta watu wengine hata wasio na pesa ili kufurahia upendo. Kuna watu mpaka ambao hukataliwa na watu wanaowataka pamoja na kutanguliza pesa zao mbele, yani mtu anachukiwa yeye na pesa zake. Mbali na hayo, Kuna watu wengine hupendwa bila kuwa na pesa.


Ni ngumu kuuteka moyo wa mwanamke au mwanaume mwenye pesa kwa kumpa pesa ila kuna watu huuteka moyo wa mwanamke au mwanaume mwenye pesa kwa mapenzi.

Mambo hayo yanaweza kuwa yanaashiria nini? Hii ni ishara ya kwamba Mapenzi sio pesa japo pesa inaweza athiri upendo wa baadhi ya watu wanaokimbiza zaidi vitu vinavyo hitaji pesa au maisha yanayo hitaji pesa.

Mpenzi kuomba pesa

Jambo la muhimu la kujua hapa ni kwamba maisha ya sasa ya binadamu yanahitaji pesa ili kufanya baadhi ya mambo. Mukiwa kwenye mahusiano, ukiachana na Magari, maisha ya juu na zawadi za gharama, mpenzi wako anaweza kuwa na shinda au mahitaji ya muhimu yanayohitaji pesa. Kuombwa pesa za vitu kama hivyo na mpenzi wako haina maana mbaya na kumpa ni kumsaidia tu, sio ujinga.


Akikuomba pesa kwanini usimpe kama ipo ndani ya uwezo wako? Unaweza kumsaidia vipi hiyo shida yake bila kutumia pesa? Kuna sehemu nyingine unayohisi anaweza chukua pesa?

Kama unajua kabisa wewe ndie mtu wa karibu na jambo lake lipo ndani ya uwezo wako, shughulikia shinda yake maana upendo ni pamoja na kusaidiana kwenye vitu hivyo ukiwa ni mwanaume au mwanamke.

Usipoonesha msaada kwa mpenzi wako mwanamke kwenye vitu vidogo vidogo vya muhimu vinavyo hitaji pesa, unaweza kumuweka kwenye hatari ya kushawishika na kuanza kukimbilia pesa nje ya penzi lenu. Ukiona anashida nyingi muanzishie hata biashara au michezo ya pesa ili asiwe anakuomba omba pesa moja kwa moja na wewe uwe unasehemu ya kumfukuzia.

Mwisho; Upendo wa kweli upo na kama mahusiano yenu yametawaliwa na upendo wa kweli ni jambo zuri. Uvumilivu ni jambo la msingi sana ili kudumisha penzi lenu pale mnapokua na hamna pesa. Tambua kuwa hakuna alie kamilika. Kuacha upendo na kuikimbiza pesa kunaweza kukufanya uangukie sehemu nzuri au sehemu mbaya. Unaweza fanikiwa kupata pesa na vitu vyote ulivyo hitaji lakini ukakosa upendo wa kweli maana upendo sio pesa wala mali. Ukiachilia mbali kukosa furaha au upendo wa kweli, unaweza angukia kwenye magonjwa au kupotezewa muda kisha kuachwa.

Pamoja na yote, hatuwezi zuia mitazamo. Mtazamo wako ni upi kuhusu Pesa na mapenzi?