Tag Archives: Love

SMS za kumiss Mpenzi wako (Mwanamke au Mwanaume)

Katika maisha ya mahusiano ya kimapenzi, kuna nyakati ambapo hisia za kumkumbuka mpenzi wako zinakuwa nyingi sana. Hali hii hutokea pale mnapokuwa mbali au hata wakati mnakuwa karibu lakini shughuli za kila siku zinawazuia kuwa pamoja. Kumkosa mtu unayempenda kwa muda ni huleta hali ngumu sana hata mnapokua na mapenzi ya dhati. Lakini ni jambo zuri ni kwamba, kuieleza hali hiyo kwa mpenzi wako hufanya ajue umuhimu wake kwako na hata kukupenda zaidi. Yani unaweza kumtumia hata ujumbe wa sms mzuri wa kumueleza jinsi gani umemiss na akafurahi na kujua unamuhitaji.

Mfano; Ujumbe mdogo wa “Nimekukumbuka mpenzi wangu, natamani niwe karibu na wewe” unaweza kubeba uzito wa hisia zako zote na kuonyesha jinsi gani unamuhitaji mpenzi wako. Wakati mwingine, huenda mpenzi wako anajihisi mpweke au hana uhakika wa hisia zako ila akiwa anapata ujumbe wako wa kummiss, anaweza kuwa ni faraja anayoihitaji. Ni jambo dogo kulifanya lakini lenye nguvu ya kuimarisha uhusiano na kuonyesha kwamba unamjali.

Mambo yasiofaa kuwambia marafiki kuhusu Mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Katika makala hii, tumekusanya orodha ya SMS bora ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako kumjulisha jinsi unavyomkumbuka. Unaweza zitumia bura kuleta furaha kwenye mahusiano wako.

SMS za kumiss mpenzi wako

  • Nipo hapa nimetulia ila kila nikifikilia jinsi nafurahia nikiwa karibu yako, natamani nikufuate ulipo. Nakumiss sana mpenzi, natamani niwepo ulipo.
  • We ni ile tamu waliosema “haionjwi” kwasababu mtu akionja hunogewa. Tangu nilipo onja ukaribu wako, nautamani kila mara. Nakumiss sana.
  • Upo mbali mpenzi wangu, lakini moyo haujawahi punguza upendo wako. Bado nahitaji wewe uwe wangu, na Bado nahitaji niendelee kuwa wako.
  • Unauzuri wa kushangaza kama nyota angani. Nikiangalia nyota na vitu vingine vyenye uzuri wa kushangaza, huwa nakukumbuka sana wewe.
  • Kuna muda unaweza waza eti nitakuacha na maumivu niende mbali. Huko mbali nafika vipi bila wewe? Moyo unakuhitaji kila dakika. Hata sasa nimekumiss nakuwaza wewe…
  • Nakupenda sana. Tafadhali njoo unijaze furaha ya uwepo wako Kipenzi. Moyo wangu umemiss zile hisia za kuwa karibu yako.
  • Huku Moyo uliokupenda unanisumbua kuhusu wewe. Umekukumbuka sana mpenzi wangu, natamani uje useme nao kwa ukaribu. Umechoka, uhitaji kukuona wewe Tabibu.
  • Njoo niyaone yale macho yako mazuri Mpenzi. Njoo unilishe kile chakula mimi hupenda. Nimekumiss mpaka onaona giza, siioni furaha bila ya wewe ninaekupenda.
  • Kile na hitaji nikiwa na huzuni, ni wewe. Na hata kile nile nahitaji nikiwa na furaha, ni wewe. Kiufupi, maisha yangu nayaona ni mzuri nikiwa na wewe. Nimekumiss mpenzi wangu.
  • Nakupenda na ninakutaka karibu nami zaidi ya kitu chochote ulimwenguni. Nakuhitaji zaidi ya chupa ya maji jangwani. Uko wapi mpenzi?

Sms hizi za kumiss ni nzuri kwa walio kwenye ndoa (Mume au mke) na hata kwa wasio kwenye ndoa (Wapenzi). Kikubwa unatakiwa kuchagua sms au ujumbe unapenda na hali yenu. Na pia ni muhimu kujua ni wakati gani wa kumtumia sms huyo umpendae.

Mambo yasiofaa kuwaambia Rafiki zako kuhusu Mpenzi wako

Katika Urafiki na Mahusiano ya kimapenzi, ni muhimu sana kujua mipaka ya mazungumzo na jinsi ya kuhifadhi baadhi ya mambo. Kuna wakati urafiki unaweza kuwa na umuhimu mkubwa katika kupeana mawazo lakini si kila kitu kinachohusiana na mpenzi wako kinapaswa kuwa sehemu ya mazungumzo na marafiki. Urafiki na mahusiano ya mapenzi, yote ni mahusiano lakini katika baadhi ya mambo, unatakiwa kutenganisha kabisa.

Kuna baadhi ya watu hupuuza kutenganisha mahusiano haya na mwisho wa siku hujikuta wanagombana na rafiki zao au wapenzi wao. Usipoweka mipaka katikati ya mahusiano haya, kunakua na asilimia kubwa ya kuingia kwenye ugomvi na marafiki au mpenzi wako. Na hakuana anaetaka jambo hilo litokee katika Maisha yake. Wengi tunapenda tuwe na amani na wapenzi wetu, na vile vile kwa marafiki zetu.

Kujua ni nini cha kusema na nini cha kuhifadhi ni Jambo muhimu katika kudumisha uhusiano na Marafiki zako huku ukiwa na uhusiano mzuri wa kimapenzi na wenza wako. Kuna baadhi ya mambo ukiepuka kuwaambia marafiki zako kuhusu Mpenzi wako, utakuwa unalinda sio tu heshima ya mpenzi wako bali pia uhusiano wako na watu wa karibu.

Kuchepuka kuna faida lakini hizi ni hasara zake BONYEZA HAPA>>>

Mambo yasiofaa kuwaambia Rafiki zako kuhusu Mpenzi wako

Mipango yenu ya baadae

Kama mmeongea mipango mingi na mpenzi wako, hakikisha unakua makini katika mazungumzo yako na marafiki ili usitoe mambo yote muliopanga. Inaweza kuwa ngumu kuwaficha marafiki zako kuhusu mambo mazuri muliopanga na mpenzi wako lakini ni vema kuwa hivyo ili kulinda mahusiano yako.
Marafiki wengi sana wanaweza kukuzunguka lakini sio kila Rafiki anaweza kuwa anania njema na mahusiano yenu. Na mtu asie na nia njema akiambiwa mipango yenu, inaweza kuwa rahisi sana kuharibu mahusiano yenu.

Ubaya wa mpenzi wako kimwili au kitabia

Hapa Duniani, wote tuna mabaya yetu na mazuri yetu. Inaweza kuwa sio ajabu kuona mabaya ya mpenzi wako kimwili au kitabia. Lakini mambo hayo hayatakiwi kuwa katika maongezi na rafiki zako. Kama kuna jambo lolote baya kuhusu mwenza wako na umeweza kulivumilia, basi fanya kumfichia Siri.


Unapotoa mabaya ya mpenzi wako kwa rafiki zako, kuna namna wote mnaweza shushwa thamani na watu wengine pindi mambo hayo yakisambaa. Yani unakua umeandika sifa mbaya kwa mdomo wako mwenyewe. Na kama umeshindwa tunza Siri ya mpenzi wako mwenyewe, usije walaumu watu wakiendelea kupeana Siri hiyo.

Matukio yake mabaya

Katika Maisha ya mahusiano kunaweza kuwa na matuko mabaya au ya aibu kuhusu Mpenzi wako ambayo umeyajua kwa kusimuliwa nae au kuyashuhudia. Mambo hayo ukiyaongelea kwa mtu mwingine zaidi yenu, jua kabisa kuna asilimia kubwa ya kuendelea kusambaza na kuwachafua wote.
Liwe ni tukio la kitandani au Maishani mwake, epuka kuliweka kuwa sehemu ya mazungumzo na marafiki zako.

Hali ya mpenzi wako kipesa Pesa

Mambo ya Pesa katika mahusiano yenu ni mambo yanayowahusu nyie na sio marafiki. Mpenzi wako akiwa na Hela au hana Hela, isiwe ni jambo la kuzungumza na marafiki zako. Mambo ya pesa husukuma watu wenye tamaa kufanya vitu vingi sana katika Maisha. Hapa Duniani kuna hata ndugu ambao hugeukana kisa pesa. Nadhani hata wewe umewahi sikia simulizi nyingine mbaya kama hizi zilizohushisha pesa.


Swala Mpenzi wako na Pesa linaweza kuwa jambo zuri kuliongelea lakini si vema kuliweka katika mazungumzo yenu ili kulinda urafiki wenu na vile vile kulinda mahusiano yako.

Ni hayo tu lakini kabla haujafika katika kituo cha mwisho wa makala hii, fahamu kuwa mambo tuliozungumza hapa hayatakiwi kukuzuia kuomba ushauri. Unaweza kuomba ushauri kwa rafiki zako unaowaamini Pele unapoona masaada kama huo unahitajika. Lakini kuwa makini sana na unachokiongea.

Mambo Wanawake hujutia kutoyajua Mapema

Katika maisha, kila mtu hupitia changamoto na maamuzi ambayo yanaweza kuleta furaha au kuleta majuto baadaye. Mwanamke, kama binadamu yeyote yule, anakutana na hali mbalimbali ambazo zinaweza kuathiri maisha yake kwa namna tofauti hapa Duniani. Kuna mambo mengi ambayo mwanamke anaweza kuyapitia lakini baadaye akaona kuwa yalikuwa na athari zisizo nzuri katika maisha yake.

The bestgalaxy hapa, tutajadili mambo machache ambayo wanawake wengi hupitia na kujutia kutoyajua baadae. Lengo si kumuhukumu mtu yeyote bali ni kutoa mwangaza na uelewa juu ya mambo ambayo yanaweza kuathiri maisha ya mwanamke. Mambo haya yanaweza kuwa yale ambayo yamepitia katika maisha yako, unayapitia au unayoiona kwa wengine .

Ukitambua mambo haya mapema, inaweza kusaidia mwanawake kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kufanya maamuzi bora na kuepuka majuto yanayoweza kuepukika. Tunatumaini kwamba, kupitia makala hii, utaweza kujifunza kitu.

Maneno Matamu kwa mpenzi wako wa kiume BONYEZA HAPA>>>

Mambo wanawake hujutia kutoyajua Mapema

Uzuri hauna mchango mkubwa sana kwenye ndoa

Mwanamke akiwa mzuri anaweza kuwa anajiamini sana na uzuri wake. Kuwa mzuri ni jambo zuri na hufanya wanaume wengi wazimike. Lakini katika ndoa, uzuri ni jambo lisilo na nguvu sana ikiwa mwanamke utashindwa kuwa na heshima pamoja na kutimiza wajibu wako.


Ndoa ni zaidi ya kuwa mzuri, ndoa ni maisha na haya maisha yana mambo mengi zaidi kuangaliana mwili. Kuna muda itakubidi utumie akili, kuna muda utatakiwa kuwa mjinga mwenye heshima pamoja na uzuri ulionao.

Upendo wa kweli sio pesa

Wakati baadhi ya wanawake wanaamini mwanaume anaewapa pesa sana ndie anae wapenda kwa dhati, Kuna wanaume wanaweza toa pesa sana kwa wanawake wasio wapenda. Baadhi ya wanaume hawa humwaga pesa kwa mwanamke kama malipo ya kumpeteza muda tu japo hawasemi kwa uwazi.
Kukimbiza pesa kwenye mapenzi hufanya wanawake kuingia kwenye majuto. Kuna watu hupata magonjwa na hata kuingia kwenye mahusiano yasio faa kisa pesa lakini hujutia mwishoni.

Kuwa katika familia ni Bora kuliko katikati ya marafiki

Mwanamke kuwa na marafiki ni jambo zuri lakini kila jambo huwa na wakati wake. Mwanamke akifikia wakati ambao maisha yake yanamvuta kujenga familia, ni vema akakubari kujiondoa katikati ya marafiki.


Mwanamke anaweza kuwa ameolewa(kapata mume), amepata mtoto na muda mwingi anahitajika kuwa katika familia sio kuzungukwa na marafiki. Kuacha kutumia muda mwingi mukifurahi na marafiki sehemu mbalimbali ni jambo gumu lakini sio muhimu kuliko kuijali ndoa, watoto au familia kiujumla.
Hii haimaanishi usiwe na marafiki, unaweza kuwa nao ila itakua vizuri kama utakua na wale wanao heshimu hali yako ya ndoa au familia. Yani wale wanoweza kukupa ushauri chanya kuhusu mtoto, ndoa na hata kuwa upande wako pale unapopitia magumu.

Mambo mengi ya mitandao si mazuri katika uhalisia

Utakutana video nyingi sana kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mahusiano au maisha. Lakini tambua asilimia kubwa ya mambo yaliyo kwenye hizo video, yanaweza kuwa hatari kuyafuata kwenye maisha au mahusiano ya uhalisia. Ni vema ukiwa kama Mwanamke wa kipindi hiki ukawa na uwezo wa kufikilia na kuchuja kila unachokiona kwenye mitandao hatakama kimetoka kwa watu maalufu.

Kutumia na akili yako na mafuzo uliyoyachukua kwa wazazi wako ni muhimu zaidi kuliko kupelekwa na upepo wa mitandao maana kwa asilimia kubwa upepo huo huwa ni Burudani tu. Ukifuata upepo wa mitandao unaweza kukuweka kwenye mtindo wa Maisha na mitazamo mibaya utakayoijutia baadae.

Ni hayo tu katika The bestgalaxy na itakua vizuri kama utatufuta katika mitandao ya kijamii ili kuwa mwana familia.

Sababu 5 za kukataliwa na Wanawake

Kukataliwa na wanawake ni jambo linaloweza kumkuta mwanaume yeyote, na mara nyingi linaweza leta huzuni na kuchanganyikiwa kabisa. Katika mambo mwanaume huogopa katika Maisha yake, kukataliwa na mwanamke ni moja wapo. Mwanaume anaweza mzawadia zawadi ya thamani mwanamke bila kumwambia anampenda kwasababu ya woga wa kukataliwa tu.


Kipindi cha nyuma baadhi ya wanaume wasio amini kuwa kuna maisha ya furaha baada ya kukataliwa na mwanamke, walikua wanajitupa hata kwenye maamuzi mabaya baada ya kukataliwa. Lakini kwa sasa watu wengi wameelimika na wanaamini kuna maisha yanaendelea baada ya kukataliwa na mwanamke.


Sababu za mwanaume kukataliwa ni nyingi na huwa tofauti. Na sio kila mwanamke husema Sababu ya kumkataa mtu, wengine huficha.
Katika Sababu hizo tofauti, kuna mambo au sababu huwa zinajirudia na wanaume wengi hukataliwa kwasababu hizo. Kama ni mtu ambae upo katika kipindi cha kutafuta mwenza wako, itakua vizuri kuzihafamu sababu hizi.


Kuzifahamu au kuzijua hizi sababu kunaweza kusaidia kuboresha mbinu zako za kumpata mwanamke unaempenda maishani. Katika makala hii ya The bestgalaxy, tunaenda zungumzia baadhi ya sababu zinaweza kusababisha mwanaume kukataliwa.

Sababu 5 za kukataliwa na Wanawake

Usafi au kutojipenda

Inasemekana kuna wanawake wengi wanavutiwa na mwanaume msafi anaejipenda. Kati yao, wanawake wengine huwa wanafikili mwanaume msafi ana anaejipenda anaweza kuwajali kama anavyojijali. Hapa ndio mara nyingi wanaume wanaoitwa “Mabishoo” huwa juu.


Usipo kuwa msafi na unaejipenda, unaweza kukumbana na changamoto za kukataliwa sana na wanawake. Mwanamke anaweza asikwambie moja kwa moja, lakini tatizo au sababu ya kukataa ikawa ni hiyo.

Kumuhitaji sana


Mwanamke anaweza sema anamtaka mwanaume anaempenda na kumjali lakini akawa na Wanaume wengi wanaomkata na wanapambana kumpata kwa kumfanyia vitu vingi vya kumjali ili awakubalie lakini anawakataa. Cha kushangaza, mwanaume ambae anaweza uteka moyo wa mwanamke wa namna hii anaweza kuwa ni mwanaume asieonesha kumuhitaji sana kama wengine.


Kiufupi baadhi ya wanawake hawataki mwanaume aoneshe uhitaji sana. Wanataka mwanaume anaewapa muda, anaewapa vimashaka mashaka kidogo lakini anaupendo wa kweli.
Kuonesha kumuhitaji sana mwanamke, kunaweza kufanya uonekane mjinga kwake na ukakataliwa.

Kutokujiamini

Wanawake wengi huvutiwa na mwanaume anaejiamni. Kujiamini kwenye maisha na mambo yako ukiwa kama mwanaume, kunaweza fanya wanawake wengi kuvutiwa na wewe alafu wakakukabari.
Usiwe ni mtu unaeonesha kutokujiami mbele ya wanawake. Kuna wanawake huchukizwa sana na mwanaume ambae hajiamni hata kwakuongea kinyonge tu kunaweza mchukiza.


Ukiwa ni mwanaume unaejiamni, mwanamke anaweza kukukubali na kuamini katika wewe. Kiufupi ukijiamni, wanawake watakuamni. Lakini katika kujiamni kwako hakikisha unaepuka kujisifu sana kwake.

Muelekeo wa maisha

Mwanaume anaweza mtongoza mwanamke bila kufikilia mbali kuhusu mahusiano na maisha. Lakini mwanamke anaweza mkubali mwanaume baada ya kufikilia mbali sana kuhusu maisha na mahusiano.


Mwanaume mwenye maisha mazuri au anaeweza kupambana kupata maisha mazuri anakua na nafasi kubwa ya kukubaliwa na wanawake. Unaweza mwanaume usiwe na pesa nyingi lakini upambanaji wako wa Maisha na muelekeo wako ukawa ni mzuri kiasi, utakubaliwa kirahisi.

Kukata Tamaa ya jibu zuri


Kuna wanaume hukata tamaa ya kuendelea kumfuata mwanamke ambae amekataa kuwa nae mara moja tu. Ukiwa ukiwa Mwanaume unaekata tamaa kwa kukataliwa mara moja, utakosa wanawake wengi sana wanaokupenda kwa dhati.


Baadhi ya wanawake hukataa unapowajia mara ya kwanza na kuwaambia hisia zako lakini moyoni mwao wanakupenda. Huwa wanakataa ili kukupima tu kama unaupendo wa kweli au unawajaribu. Yani wanawake wengine wanaweza kukubali baada ya kuwaelezea zaidi ya mara tatu.

Michezo ya kuchati na Mpenzi wako (Hufurahisha na kurefusha Maongezi)

Kuchati na mpenzi kwenye simu ni njia nzuri ya kuimarisha uhusiano na kujenga hisia za ukaribu kati yenu. Katika ukurasa huu, The bestgalaxy inaenda kukupa michezo michache ambayo mnaweza kucheza pamoja katika kuchati na Mpenzi. Michezo hii itasaidia kurefusha maongezi, kuburudisha na kuongeza furaha katika uhusiano wenu.

Kuna muda wapenzi mnaweza kosa kabisa mambo ya kuchati na hii hutokea mara nyingi. Lakini kama mmoja kati yenu atakua anauelewa juu ya michezo ya kuchati, mnaweza ianzisha na kufanya maongezi yaendele katika kuchati kwenu. Michezo hii ya kuchati ni mbinu nzuri ya kufanya maongezi yaendele katika kuchati kwa wapenzi. Kwa kiingereza michezo hii inaitwa “Texting Games” na ipo mingi sana japo hapa tutaangalia michezo michache tu.

Michezo hii michache ni rahisi na inahitaji muda mchache kumuelewesha mpenzi wako kama haijui unapotaka mcheze. Haina haja ya kuwa na vifaa maalum au kuwa pamoja kimwili ili kueleweshana. Endelea kusoma ili kuijuia na kuielewa michezo hii ya kuchati.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Michezo ya kuchati na Mpenzi wako wa kiume au wakike

Kwasababu nakupenda

Mchezo huu unachezwa na wapenzi ambao mnapendana alafu mmetulia mnachati kwa sms. Wapenzi mnatakiwa kuwa mnatumiana sms zenye ujumbe unaojumuisha maneno “Kwasababu nakupenda”.

Kwamfano; unaweza mwambia mpenzi wako “Nimekupa moyo wangu wote kwasababu nakupenda”. Huu ni mfano tu lakini mnatakiwa kutumiana sms za muundo huo zinazogusa mioyo yenu na kuelezea hisia zenu. Mchezo wa “Kwasababu nakupenda” unaweza kuwafurahisha na vilevile mtakua mnajenga mahusiano yenu kwa kuambiana mambo mazuri mnayoweza kufanya,mlio yafanya na mnayotaka kufanya Kwasababu ya upendo.

Maliza au taja wimbo

Mchezo mwingine ni huu unaitwa “Maliza au Taja wimbo”. Wapenzi katika mchezo huu mnakua manatajiana mistari ya nyimbo za mapenzi alafu kila anaetajiwa atatakiwa kumalizia mstari au kutaja jina la nyimbo aliotajiwa.

Kutuma mistari mitamu ya kisisimua, kutamfurahisha zaidi mpenzi unaechati nae kwenye mchezo huu.
Kwenye mchezo huu mnatakiwa kuwa ni watu mnaosikiliza na kufuatilia nyimbo za mapenzi. Kama ni watu wa namna hiyo, basi mnaweza furahia zaidi mchezo.

Jinsi ya kulinda Ndoto zako Maishani zisife BONYEZA HAPA>>

Kisia nilipo

Mchezo huu unachezwa na wapenzi na wanaucheza kwa kukisia mazingira ambayo wapo. Yani unaweza anza kwa kukisia sehemu alipo, anachokifanya na hata vitu vilivyo mzunguka. Yeye atakua anakwambia kama umekosea au umepatia.

Mtakua mnapokezana pale mmoja wenu anapopatia kukisia. Mchezo huu wa kukisia unakua mzuri zaidi kama watu wote ni wakweli alafu mnapendana kiasi cha kuweza kuumiza kichwa kufikilia na sio kutaja tu mnachojiskia. Kila mchezaji anatakiwa kufikilia jibu kulingana na anavyomjua mwenza wake.

Nishawishi tulale

Katika michezo, mchezo mzuri sana wa mapenzi katika kuchati ni huu. Mchezo wa “Nishawishi tulale” ni mchezo unachezwa wakati wa usiku unapochati na mpenzi.
Unachezwa kwa kuahidiana kuwa hamtalala na mtachati pamoja mpaka asubuhi. Kama mmoja anataka kulala kabla ya asubuhi, tatatakiwa kumshawishi mweza wake walale kwa kufanya au kumwambia jambo lolote litakalomshawishi mwenza wake.
Mtu anaetaka kulala aweza ahidi zawadi, akatoa maneno mtamu au jambo lolote litakalo mfanya mpenzi asietaka kulala, alale. Wachezaji wote mnatakiwa kujali sheria za mchezo na kutimiza ahadi zenu.

Mpelelezi

Machezo wa “Mpelelezi” ni mchezo wa kuchati ambao unahusu kuulizana maswali. Wapenzi mnakua mnapeana maswali kwa kupokezana na kila swali linatakiwa kujibiwa.

Idadi ya maswali inaweza kuwa 5 kwa kila mtu na hata 20 mkipenda. Kikubwa hapa ni kuulizana maswali mazuri yatakayo wafurahisha wote wawili.
Mchezo huu wa kuchati unaweza fanya watu mnaopendana mjuane zaidi ya mnavyojuana kwenye mambo mbalimbali. Ukipata nafasi ya kucheza mchezo huu, kuuliza maswali ya kusisimua na kujenga mahusiano yenu ni muhimu sana.

Michezo yote hii tulioiweka hapa ni rahisi sana kumfurahisha mpenzi wako wa mwanamke au mwanaume. Na huwa inafaida kubwa kwenye kujenga umahusiano ya wapenzi wanapenda kuchati. Unaweza ucheza na mume wako, mke wako bila tatizo lolote. Unaweza pia mtumia mwenza wako makala hii ili kuokoa muda wa kumulelezae ingawa ni vizuri kumuelekeza mwenyewe.

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy!

Unajuaje kama Ex wako anakupenda? Dalili ni hizi

Mahusiano ya mapenzi yanaweza kuwafanya watu waamini kuwa watakua pamoja milele lakini sio kila mahusiano hufikia huko. Baadhi ya watu hushindwa kufikia malengo ya mahusiano yao baada ya kukumbana na mambo ambayo hutikisa au kuvunja mahusiano. Lakini pia sio kwamba Mahusiano yanayodumu huwa hayapitii mambo kama hayo, hupitia mambo magumu. Kuna watu huvunja mahusiano kabisa na kuitana “ex” lakini baada ya muda hurudiana tena na kuendelea kuwa pamoja. Kiufupi kurudiana na mpenzi wa zamani ni jambo la kawaida ambalo watu hufanya.

Kama bado mpenzi wako wa zamani unampenda, kujaribu kumuelewa mpenzi wako wa zamani inaweza kuwa ni changamoto. Wakati mwingine, mpenzi wako wa zamani anaweza kutoa dalili za kukupenda lakini kichwani kwako ukawa unawasiwasi na hauzielewi. Hapa katika The bestgalaxy, tutazungumzia kuhusu dalili za mpenzi wa zamani(ex wako) kukupenda. Kujua dalili hizi husaidia kumuelewa au kujua kama bado mpenzi wako anakupenda na kuna nafasi ya kurudisha upendo wenu ikiwa na wewe Bado unampenda.

Kujua dalili hizi kunaweza kukupa uwezo wa kujua hisia zake na kusaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu kurudisha uhusiano wenu. Wakati ukifanya hayo, ni vema kufahamu kuwa maamuzi ya kurudisha na mpenzi wa zamani yanaweza kuwa maamuzi mabaya pia kama hautafanya utafiti vizuri juu ya lengo lake kwako.

Mambo ya kuepuka baada ya kuachana na mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Dalili za mpenzi wa zamani kukupenda

Kuweka ugumu katika mawasiliano

Kuna watu mkiachana huwa wanakata njia za mawasiliano haraka na kukuwekea ugumu wa kuwapata lakini moyoni wanaokua bado wanakupenda. Mtu hufanya hivyo kwa msukumo wa hasira tu au ili aone unamtafuta na ajiridhishe kuwa anamuhitaji. Anaweza kublock kwenye simu na kukuwekea ugumu wa kukutananae lakini siku akiona umepambana na kukutananae mkaogea, atajisikia vizuri kuliko kawaida.

Mara nyingi hii hutokea endapo wewe ndio chanzo cha mahusiano kuvunjika. Adhabu anayokupa ni kuwa mbali na wewe kwa kukata ukaribu ili angalau uone umuhimu wake na kutambua makosa yako. Kupambana kumtafuta kunaweza fanikisha kurudisha uhusiano wenu.

Kukutafuta au kufungua njia za mazungumzo

Mpenzi wa zamani anaweza kuwa anakutafuta kwa njia mbalimbali na kufungua njia za mazungumzo kati yenu. Hii inaweza kuwa dalili ya mpenzi wa zamani kutamani murudiane. Anaweza kuwa anafanya hivi baada ya kukumbuka ukaribu wako na Mapenzi yenu kwa ujumla.


Kukupigia simu, kukutumia sms, kukuondolea block kwenye simu au kutafuta vinjia vingine vya kufanya maongezi na wewe ni ishara za kutaka murudiane. Wengine huwa wanashindwa kuficha kabisa hisia zao na kutaka mzungumzie mambo ya mahusiano yenu. Hapa ndio utasikia akisema mambo kama “Ulienae kwa sasa anafaidi… Umenifanya mapenzi niyaogope… Msalimie mpenzi wako” ili tu muongelee mahusiano yenu.

Wivu unapokua karibu na watu wengine

Njia rahisi ya kujua ex wako anakupenda au hakupendi ni wivu. Ni ngumu sana kwa mpenzi wa zamani kukuficha wivu wake anapo kuona na watu wengine. Kama hakupendi, anaweza asiwe na wivu ila kama anakupenda, moyo wake hauwezi muacha salama pindi unapooneka upo karibu na watu wengine. Anaweza kukosa amani au kufanya jambo lingine linaloonesha anawivu na wewe. Kama ni mtu wa “WhatsApp Status” basi wivu juu ya jambo aliloliona kwako atauweka kwenye Status yake kwa maneno ya kukuumiza au kuonesha ameumizwa.

Yupo makini sana na wewe au mambo yako

Ex anaekupenda anaweza igiza kukupuuza lakini hawezi kukupuuza kirahisi. Unapoongea nae anaweza igiza kukupuuza lakini huwa anazingatia kila neno. Mkiwa sehemu moja anaweza igiza kutokukuzingatia lakini macho na akili yake inakua kwako. Kuna muda unaweza gongana nae macho akiwa anakuangalia alafu akazuga kufanya mambo mengine. Yote ni kwasababu anakupenda na upo kwenye akili yake.

Ni hayo tu katika makala hii ya The bestgalaxy, kama utapenda unaweza Endelea kusoma makala nyingine. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi huku ukijiunga nasi kwenye mitandao ya kijamii.

Maswali ya mwanamke yanayohitaji umakini kujibu (Fikilia kwanza)

Mwanamke anaweza kuwa na maswali mengi ukiwa nae kwenye mahusiano. Maswali haya yanaweza kutokea kutokana na hali mbalimbali zinazomkabili, ikiwa ni pamoja na masuala ya afya, mahusiano, kazi, na hata utani tu. Sio kila swali analouliza mwanamke ulienae kwenye mahusiano lina umuhimu au linahitaji umakini. Laini baadhi ya maswali hayo yanahitaji kufikiriwa kwa kina ili kutoa majibu yanayofaa.

Ukiwa kama mwanaume ni muhimu kuwa na uelewa wa kutambua maswali muhimu toka kwa mwanamke. Mwanamke ulienae kwenye mahusiano akikuuliza maswali usijibu vyovyote unavyojisikia tu, jaribu kufikilia kabla haujajibu. Baadhi ya maswali yanaweza kuwa kama mepesi lakini ndio yakawa ni mazito kuliko mahusiano yenyewe.

Mwanamke anaweza kukuwinda mwezi mzima ili akuulize swali dogo sana kwako lakini jibu lako linaweza kuwa na maana kubwa kwake. Usipo mridhisha na majibu yako anaweza kukujia tena na swali hilo hilo au akaliuliza kwa mtindo mwingine.

Katika makala hii, tumechambua maswali machache ambayo mwanamke anaweza kuwa nayo, maswali ambayo yanahitaji umakini katika kuyajibu. Kujua haya inaweza kukusaidia mwanaume kijana katika mahusiano ya mapenzi na mwanamke.

Jinsi ya kujua mpenzi ulienae anakupotezea muda BONYEZA HAPA>>>

Maswali ya mwanamke yanayohitaji umakini kuyajibu

Unamalengo gani na mimi?



Mara nyingi wanawake ukiwanao kwenye mahusiano wanaweza uliza Swahili na huwa zito sana japo ni kama jepesi. Mwanamke mpaka kafikia hatua ya kukuuliza swali hili tambua amejiuliza vitu vingi sana kichwani kuhusu mahusiano yenu na anataka uyajibu wewe kwa hilo jibu utakalo litoa. Ukijibu jibu ambalo litamuonesha hauna mpango mzuri nae basi mahusiano kwanzia hapo yanaweza anza kukata muda wowote.


Huwa mara nyingi wanauliza swali hilo ili kujua mahusiano mulioyaanzisha ni yakudumu au laa. Kama ataona umejibu kama hauna mpango nae basi anaweza anzisha mahusiano yoyote mapya muda huo. Unaweza kuta tu hata ameolewa ghafla na hajakwambia.

Unafanya kazi gani?



Wanaume wengi huwa wanajibu swali hili kirahisi lakini ni swali ambalo ukikosea kujibu mahusiano yako yanaweza kuwa magumu. Mwanamke ambae hajui kazi yako akikuuliza kuhusu kazi unayoifanya, usikurupuke kutaja kazi nzuri sana ili tu akupende. Ni bora utaje ya kawaida au usitaje kabisa.


Unapomwambia mwanamke kazi yako kuna jinsi kichwani anafikilia atakavyoishi na wewe na maisha yatakuaje. Ukiwa mtu mwenye kipato kidogo na anakupenda basi kunajinsi anaweza kuwa anajibana kimatumizi na kukuomba pesa ndogo kwenye shida.


Ukimwambia unafanya kazi nzuri na ina pesa, usishangae akianza kukuomba viasi vikubwa vya pesa na kukuletea matatizo yanayohitaji pesa nyingi. Sio wanawake wapo hivi ila wengi baada ya kujua kazi huwa hivyo. Kiufupi huwa wanapenda kuwa wanawake wa kiwango chako na ukidanganya kiwango, kunajinsi uweza shindwa kufurahia mahusiano maana atakua amejiweka kwenye kiwango kisicho chako.

Unanipenda kweli?



Hata ukiamshwa usingizi na mpenzi wako unaempenda, hakikisha unajibu vizuri hili swali. Mara nyingi mwanamke akikuuliza “Unanipenda kweli?” Anaweza kuwa anataka kuondoa wasiwasi moyoni mwake juu ya upendo wako kwake.

Inaweza kuwa sio kila anapokuuliza swali hili anawasiwasi ila kumjibu huwa kunaufanya moyo wake ujimwage zaidi kwako.
Kuna muda swali hili pia huwa na jambo kubwa nyuma yake. Lakini uzuri ni kwamba sura yake inaweza kukuambia kama ni jambo baya au zuri.

Umenipendea nini?



Mwanamke kukwambia “Umenipendea nini?” ni jambo la kawaida sana na mwanaume wengi husema “Nakupenda jinsi ulivyo tu”. Mwanaume ni bora ujibu hivyo kuliko kujibu vingine ukajichanganya.


Kuna wanawake huwa wanatafuta mwanaume anaewapenda kweli jinsi walivyo na sio kuwatamani. Ukikutana na mwanamke ambae yupo hivi alafu akajibu mambo kama “Shepu” au “Macho” na vingine bila kumwambia kwanza umempenda jinsi alivyo, anaweza kuweka kwenye kundi la waliomtamani.
Ni vema ukamwambia kwanza umempenda jinsi alivyo alafu akataja na vitu vingine vinavyokuvutia zaidi au unavyo vitamani.



Maswali haya machache ni ya msingi na mara nyingi yanakua na machango mkubwa kwenye kuimarisha mahusiano. Kila swali lina maana yake na uzito wake, na unatakiwa kuyajibu kwa uangalifu. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Jinsi ya kumtuliza mpenzi wako mkikosana au kutoelewana

Kutokuelewana na kufanyiana makosa ni mambo ya kawaida na hutokea mara nyingi sana. Hakuna anaependa mambo hayo yatokee lakini mara nyingi hutokea bila kutarajia.


Kutokuelewana au kufanyiana makosa kunaweza fanya mahusiano ya mapenzi kutikisika na hata kuvunjika kabisa. Lakini hii inategemeana na jambo lililofanya wapenzi mufikie hatua mbaya na maamuzi au hatua muliochukua baada ya kukoseana au kutoelewana.


Katika mambo muhimu kujua katika Mahusiano ni jinsi ya kufanya mnapokoseana au kutoelewana na mpenzi wako. Ni muhimu Kwasababu kukosana na kutoelewana ni kama hakupingiki kwenye mahusiano, hutokea tu. Lakini ukiwa na ufahamu wa jinsi gani ufanye, itakusaidia kwenye kuweka sawa mahusiano kwenye hali hiyo.

Katika makala hii, tutajadili jinsi ya kumtuliza mpenzi wako mnapokosana au kutoelewana. Kwa kuelewa na kufuata mbinu sahihi, unaweza kusaidia kurejesha amani na kuimarisha uhusiano wenu bila shida.

SMS za kumfanya mpenzi wako afurahi BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kufanya kumtuliza mpenzi wako mkikosana au kutoelewana

Muombe msamaha

Baada ya kukosana au kutokuelewana kulikosababishwa na wewe ni vema ukamuomba msamaha mpenzi wako. Neno “Samahani” linaweza muweka sawa mpenzi wako na kumrudishia katika hali ya kwaida. Neno hili ni moja ya maneno yenye nguvu za kurekebisha hisia za mtu na kumuweka sawa mnapokua mmekosana.
Ukimkosea mtu bila kumuomba msahama anaweza kuwa na mawazo mengi sana. Wengine usipo waomba msamaha huwa wanakupangia vitu vingi kichwani ili kukulipizia. Lakini ukiomba msamaha baada ya kukosea inaweza fanya mwenza wako asifike mbali sana kimawazo.

Muache peke yake kwa muda

Kuna baadhi ya watu wakikosewa au wakitokewa na kutokuelewana huwa wanahitaji kuwa peke yao kwa muda ndipo watarudi sawa. Usipo mpa muda wa kuwa peke yake hata msamaha wako hawezi kuuelewa.
Sio kila mtu yupo hivyo ila kama ukiwa kwenye mahusiano na watu wa namna hii basi uwe unaheshimu muda wake wa kuwa peke yake pale ambapo hamuelewani au mmekosana. Unaweza ukamuacha peke yake wa muda alafu ukaanza kujisogeza tena kidogo kidogo.
Hii inaweza kuwa sio njia ambayo mtu unaweza fikili kuitumia kwa haraka haraka ila ni njia muhumu ya kuweka sawa kiakili baadhi ya watu mnapokosana.

Mzawadie kitu anachokipenda

Baada ya kukosana au kutokuelewana unaweza muweka mpenzi wako kwenye hali ya furaha kwa kumpa zawadi. Tafuta zawadi nzuri unayohisi anaweza ifurahia alafu mpatie.
Wote tunajua hakuna asiependa au kufurahia kupewa zawadi za gharama Duniani, lakini zawadi sio lazima iwe ya gharama. Zawadi nzuri inaweza kuwa kitu chochote kizuri kinachoweza ugusa moyo wa mtu. Kwaiyo jaribu kufikilia kitu chochote kizuri kitakacho ugusa moyo wa mwanamke au mwanaume umpendae. Kama ukikipata cha bei ndogo au kubwa, fanya kumpatia ili kumtuliza au kumuweka sawa.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Mwambie maneno mazuri ya upendo

Kwenye mahusiano ya mapenzi maneno ya upendo huwa yananguvu sana. Neno moja au mawili mazuri ya upendo yanaweza upasua moyo kwa furaha. Hasira na makasiriko baada ya kutoelewana au kukosana, vinaweza tulizwa na maneno matamu ya upendo.
Ukikosana na mpenzi wako au kutoelewana nae, unaweza tumia maneno mazuri au matamu kumuweka sawa. Unaweza mkumbusha jinsi gani unampenda, umuhimu wake kwako, uzuri wake na mambo mengine ya kuvutia au kugusa moyo.

Ni hayo tu katika makala hii, natumai unaweza kuwa umeelewa jinsi gani unaweza mtuliza mtu wako mnapokua hamko sawa. Napenda kusisitiza kwamba watu tupo tofauti hivyo ni vema kufikilia kidogo kama njia unayataka kuitumia inamfaa mwanamke au mwanaume umpendae.

Mwanaume usimfanyie mwanamke mambo haya katika Mahusiano (Fikilia kwanza)

Ni muhimu kuzingatia na kuheshimu hisia na mahitaji ya mwenzi wako. Hili lina umuhimu mkubwa zaidi kwa wanawake, ambao mara nyingi wanahitaji uangalifu maalum ili kuhisi kuthaminiwa na kuungwa mkono ndani ya mahusiano na hata maisha kiujumla. Hapa The bestgalaxy ukurasa huu unaenda kukujuza mambo ambayo si vema ukayafanya kwa mwanamke unapokua nae kwenye mahusiano. Makala hii inaweza onekana imelenga mwanaume lakini kila mtu anaweza isoma. Mbali na hayo kuna makala nyingine tutakuja lenga wanawake pia na itaweza somwa na yoyote.

Katika Mahusiano mnaweza kutana na watu wenye tabia tofauti, mkaelewana na kuwa pamoja. Kuwa pamoja kama wapenzi kunaweza kuwa na mambo mengi sana mnafanya au kufanyiana. Mambo mengine yanaweza onekana mazuri na mengine yakaonekana wazi kuwa mabaya. Mengine yanaweza kuonekana mazuri au ya kawaida lakini ni mabaya baada ya muda.

Jinsi ya kumfurahisha mwanamke katika Mahusiano BONYEZA HAPA>>>

Mambo mwanaume kumfanyia mwanamke si vizuri

Usitoe siri au mambo mabaya ya mwanamke wako kwa wengine

Unaweza ukawa na mpenzi mwanamke mwenye mambo ambayo si vema kuyaonglelea kwa watu. Yanaweza kuwa ni mambo yanayofanya mtu amshushe thamani na kumchulikia vibaya.

Ikiwa unatabia ya kuongea mambo hayo kwa watu na bado upo nae kwenye mahusiano hata wewe unaemuongelea unakua unajichafua pia. Itakua ni vizuri kama utakua unatabia ya kutomuongelea vizuri mwanamke wako maana thamani yake ikiwa kubwa kwa watu na wewe unaonekana wathamani pia. Ni bora usimuongelee kabisa kuliko toa Siri au kumuongelea vibaya mtu ulienae kwenye mahusiano.

Usimshawishi kufanya mambo hatari kupinga ujauzito

Kama unampenzi na hamjafikia hatua ya kukubaliana kuzaa, basi hakikisha ukiwa kama mwanaume unakua mungalifu pia kwenye kuzuia ujauzito. Usiwe ni mtu ambae unaenda mara kwa kama hauoni au kuelewa mwanamke anatumia njia zipi alafu anakua makini kusisitiza mwanamke atumie njia hatari kuzuia matokeo ya uzembe.

Njia hatari zikizidi zinaweza msababishia mwanamke matatizo ya kizazi. Sasa unaweza muelewa kirahisi pindi atakapo patwa na matatizo hayo na kushindwa kupata ujauzito?


Ukiona mwanamke wako haelewi au anatumia sana njia za hatari bila kukushirikisha, hakikisha unamsaidia na kumuelimisha. Sio Kila mwanamke anaufahamu mzuri juu ya mambo ya uzazi. Fanya hivyo ili muuzuie ujauzito kwa njia salama na awe vizuri mpaka mtakapo amua kupata mtoto.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Usimpuuze bila kumsifia au kumpa maneno mazuri baada ya tendo

Baada tu ya tendo hasa la mara ya kwanza kwa mwanamke anaweza kuwa na mawazo mengi ya kutaka kujua kama yupo vizuri kwako au laa. Ukiendelea na mambo yako na kuondoa ukaribu baada ya tendo Hilo unaweza kumfanya mwanamke ahisi vibaya juu yake mwenyewe.

Kama ni mpenzi wako, hakikisha haumuachi kwenye Mawazo hayo kila mara. Jitahidi kukumbuka kumtafuta na kumpa maneno mzuri juu ya alicho kufanya na wewe. Hii pia inaweza kumfanya ajiamini au kuwa huru anapokutana na wewe tena kwenye tendo.

Epuka mahusiano ya muda marefu kama haunampango wa kumuoa

Kati ya mwanamke na mwanaume, mahusiano yakianza mara nyingi anaewaza mbali kuhusu mahusiano ni mwanamke. Anaweza waza kuhusu familia na hata watoto kipindi mahusiano hayajafikia hata kuishi pamoja. Hili sio jambo baya maana ni moja ya ndoto zao.


Unapokua na mwanamke kwenye mahusiano ya muda mrefu anaweza kuwa anawekeza sana akili yake kwako na kufanya amini utakua nae milele. Sasa kama hauna mpango wa kumuoa au kuwa nae maishani basi ni wazi mahusiano ya muda marefu ni maandalizi ya kumuumiza tu. Ikiwa hautaki kumuumiza mwanamke usie na mpango nae, mahusiano ya muda mrefu ni yakuyaepuka sana ili usimuuze. Usipofanya hivyo unaweza uumiza na kumpotezea muda wa kumtafuta atakae mpenda milele au kumuoa.


Mambo tuliozungumzia hapo juu yanaweza kuwa marahisi kusahau au kupuuza lakini ni mambo muhimu. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy na useache kuwa nasi.

Sms za kumwambia mpenzi wako kuwa unampenda

SMS inaweza kuwa njia nzuri ya kueleza hisia za upendo na mapenzi kwa mwanamke au mwanaume umpendae. Sms kama sms zinamchango mkubwa katika mahusiano ya sasa maana ndio mara nyingi huunganisha wapenzi wakiwa mbali.

Katika makala hii, tumekuangalia jumbe mbalimbali za SMS ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako kumwambia kuwa unampenda. Kuonyesha upendo kupitia maneno kunaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha uhusiano na kuongeza ukaribu kati yenu. Kunaweza mkumbusha jinsi gani unampenda na unahitaji.

Kwenye mahusiano ya mapenzi, maneno ni kitu kikubwa sana. Maneno yanaweza yumbisha mapenzi na hata kuyaweka sawa pia. Soto tunajua kwamba wakati mwingine mnaweza kuwa kwenye mahusiano lakini yakawa yanayumba. Kumwambia maneno mpenzi wako ya jinsi gani unampenda kunaweza mkumbusha mpenzi wako kushikamana na kuwa pamoja kwenye mahusiano. Na pia kuna muda mpenzi anaweza kuwa na kiu ya maneno mazuri toka kwako lakini akashindwa kusema maana na yeye haelewi.

SMS za kumsifia mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Sms za kumwambia mpenzi mwanamke/mwanaume unampenda

  • Yule mtu anaeweza ufurahisha au kuuvunja moyo wangu ni wewe. Kuwa nawe ni furaha ya moyo wangu, sitamani kuwa mbali na wewe.
  • Kama kukupenda ni ujinga basi nakubari kuwa hivyo. Penzi lako limeushika moyo wangu mpaka naogopa. Ukiona chozi langu la maumivu ya mapenzi limenidondoka jua ni wewe. Na ikitokea hivyo naomba usije sahau kuwa hata wakulifuta pia ni wewe. Nakupenda sana.
  • Nakupenda Toka moyoni, Ukaribu wako huichemsha damu. Kuwa na Wewe ni Ndoto yangu tamu, staki kukatishwa mpenzi maana hainiishi hamu.
  • Penzi lako limenipeleka kwenye ulimwengu wa mapenzi ambao sikuwahi jua upo. Unanipa Raha, nakua na furaha kama mtoto.
  • Zawadi kubwa ninayotamani kuendelea kupata toka kwako ni upendo wako. Moyo wangu umeisha lidhia kuwa na wewe maishani, na wewe ukibadilika tu, jua unaniumiza mwanzako.
  • Duniani karibu kila mtu ana anae mpenda kwa dhati toka moyoni na yupo akili kila mara. Katika Maisha yangu mtu huyo ni wewe!
  • Wanaweza kuwa wamekwambia au umesikia maneno mengi kuhusu mimi. Ila naomba upuuze na usikilize moyo wangu unasema nini sasaivi. Moyo wangu usema unakupenda wewe!
  • Nimekua nikipenda kuangalia vitu vizuri na vyakupendeza ili nifurahi. Tangu nilipokutia machoni sina haja ya kuangalia chochote kizuri mbali na wewe ili nifurahi. Macho na kila kitu toka kwako hunivutia.
  • Ninapomaliza kuongea na wewe kwenye simu hua nakata simu lakini natamani kuendelea kuisikia sauti yako tena. Sijawahi kuichoka sauti yako maana ni faraja ya moyo wangu. Nakupenda sana.
  • Sijawahi jihisi mpweke nikiwa karibu na wewe mpenzi. Naweza umia kwa kupoteza vingi maishani ila nitaumia zaidi nikikupoteza wewe kipenzi. Maana nanipa sababu ya kufurahia maisha.
  • Moyo wangu hupitia mambo mengi maishani. Lakini dawa yake kila mara huwa ni wewe. Unajua jua kuugusa bila kuushika. Unagusa sehemu wajinga hawawezi fika. Nitakupenda mpaka mwisho wa Maisha.
  • Siri ya furaha yangu ni kuwa na wewe. Najiona wa thamani kwasababu yako. Moyo wangu umenitoraka, upo kwako. Umeuvuta kwa Raha za penzi lako. Nakupenda sana Mpenzi.

SMS hizi ni nzuri kwako? Kama ni nzuri unaweza tumia Bure kwa unaempenda. Usisahau kuangalia sms nyingine za mapenzi ndani ya The bestgalaxy na useache kuifuatilia pia. Asante sana kwa muda wako ulioutoa kusoma makala hii.