Tag Archives: iphone

Hizi ni Website nzuri kwa watumiaji wa iPhone

Ukiangalia ulimwengu wa teknolojia ya sasa, unaona iPhone inabaki kuwa moja ya vifaa maarufu na vyenye ushawishi mkubwa. Kutokana na muundo wake wa kifahari na uwezo wake, iPhone imekuwa chaguo la kwanza kwa mamilioni ya watu duniani kote. Kwa baadhi ya watu iPhone si kifaa cha mawasiliano, ni sehemu ya mtindo wa maisha.

Kila matoleo au kizazi kipya cha iPhone kinaleta ubunifu ambao si tu unarahisisha maisha, bali pia unafanya matumizi ya simu kuwa ya kuvutia zaidi. Kwa kutumia iPhone, unapata fursa ya kufurahia maelfu ya apps kwaajili ya mahitaji tofauti yanayoweza kuwa katika upande wa mawasiliano, burudani na hata uzalishaji/biashara.

Kwa upande wa kupiga picha nzuri; Kamera za hali ya juu za iPhone zinakupa uwezo wa kupiga picha nzuri sana na wengi hupenda iPhone kwaajili ya jambo hilo.

Mbali na Kamera mtumiaji hufurahia huduma za kipekee kama Siri, iCloud, na FaceTime ambazo hufanya utumiaji wa iPhone kuwa wa tofauti na simu nyingine.

Katika makala hii, tutaangazia website au tovuti chache ambazo ni kwaajili ya watumiaji wa iPhone. Hizi ni zile tuvuti ambazo zinaweza rahisisha zaidi baadhi ya mambo kwa mtumiaji wa iPhone.

YouTube channel za kuangalia Movies Bure BONYEZA HAPA>>>

Website/Tuvuti nzuri kwa watumiaji wa iPhone

Apple Support

Apple ni mahali ambapo mtumiaji wa iPhone anaweza kupata suluhu za matatizo mbalimbali ya kifaa cha iPhone. Kupitia Apple support, mtu unaweza badili password ya akaunti ya Apple, kuupdate kifaa chako ili kupata maboresho na mambo mengine.
Apple Support imeletwa na kampuni ya Apple ili kusaidia watumiaji wa bidhaa za Apple kama iPhone na hata bidhaa mbali na iPhone.

Tubi TV

Kwa wapenzi wa movie wanaonatumia iPhone, hii inaweza kuwafaa zaidi. Tubi TV ni tuvunti ambayo inawezesha watu kuangalia Movie bure katika Internet. Kupitia iPhone yako, unaweza itumia tuvuti ya Tubi TV kuangalia maelufu ya movie bila kulipia chochote(Bure).
Huduma hii ya movie inapatikana USA hivyo ukiwa nje ya sehemu husika, hautaweza ipata bila kutumia VPN.

Kwaiyo utatakiwa kupata VPN hata ya Bure kwenye iPhone yako alafu utaunganisha kwenye server za USA kisha ndio utaingia kwenye Tuvuti ya Tubi TV.com
Ukishaingia katika tuvuti, utatakiwa kuifungua tena tuvuti hiyo katika “Desktop view mode”(Washa kipengele cha “Request Desktop view”) ili isikulazimishe kudownload app ya Tubi TV. Usipofanya hivyo, hautafanikiwa kuangalia Movie hata moja.

MacRumors

Hii tuvuti ya MacRumors, inajihusisha na taalifa mbalimbali zinazohusu bidhaa za Apple. Kwakua iPhone ni bidhaa ya kampuni ya Apple, basi habari zake mpya huwa zinapatikana katika MacRumors. Mfano wa taalifa unazoweza kupata kupitia MacRumors ukiwa kama mtumiaji wa iPhone ni mabadiliko yaliofanywa katika iOS, Ujio wa iPhone mpya na mengineyo.
MacRumors sio sehemu pekee unayoweza kupata habari za simu za iPhone lakini ni moja ya sehemu bora za kupata habari muhumu kuhusu simu za iPhone na vifaa vingine vya kampuni ya Apple.

iPhone Photography School

Website ya iPhone Photography School inakuwezesha kunielewa zaidi Kamera ya iPhone. Kwenye tuvuti hii, unaweza pata masomo ya kuitumia kamera ya iPhone kwa ustadi mkubwa.


Wengi huwa tunatumia kamera za simu zetu bila kuzingatia vipengele vya upigaji mzuri wa picha. Katika iPhone, watu wanaweza piga picha nzuri sana lakini wengi kati yao hawajui kwa upana kamera ya iPhone. Kiufupi watu hutumia Kamera ya iPhone kwa mazoea lakini inamambo mengi sana na yanahitaji mtu utenge muda wa kuelewa kila kipengele na kukitumia.

Ni hayo tu katika orodha hii. Unadhani ni tuvuti gani nyingine nzuri kwa watumiaji wa iPhone? Tuandikie kwenye sehemu ya maoni ili kusaidia wengine.

App za kuangalia Movies/Filamu mtandaoni kwa simu

Katika ulimwengu wa sasa unaweza angalia movie kwenye simu yako ya kiganjani ukiwa popote ulimwenguni. Mara nyingi watu wakitaka kuangalia movie huwa wanatembelea website/tuvuti zinajihusisha na movie/filamu au hutumia app zinazojihusisha na filamu ili kupata huduma ya movies. Kuna baadhi ya tuvuti au app hukuwezesha kupata huduma ya movie bure na nyingine huwa zinakuhitaji ulipie. Huduma za kulipia huwa ni bora zaidi na zinausalama zaidi ukilinganisha na baadhi ya huduma za bure japo zote ni nzuri.

Hapa Tha bestgalaxy leo tunakupa orodha ya app chache kati ya app nyingi unazoweza tumia kuangalia movie kwenye simu yako mtandaoni(online).

App za kuangalia movies online(mtandaoni)

Netflix

Hii ni app ya kampuni ya kimalekni, Netflix ambayo inayotoa huduma ya kuangalia movies/filamu kupitia Internet. Unaweza ingiza kwenye simu yako ya mkononi na kuanza kufurahia filamu kiganjani pako. Unaweza kuangalia filamu nyingi nzuri na maalufu duniani kupitia app hii. Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba app hii ya netflix huwa haitoi huduma bure. Inaweza kukugharimu Tsh 7000 mpaka 23000(Makadilio).

ShowMax

ShowMax ni app inayotoa huduma ya kuangalia movies(filamu), michezo, vipindi vya TV na mambo mengine mengi, kiganjani pako. App hii inaweza kutumika kuangalia movie katika simu ya mkononi lakini sio bure pia. kufurahia huduma za app ya ShowMax utatakiwa kulipia kila mwezi. Kuna filamu nyingi unaweza angalia na pia kama ni mdau wa michezo, unaweza furahia michezo katika app hii. Kifurushi vyake vinaweza kugharimu Tsh 7800 mpaka 46000 kwa mwezi(Makadilio).

Youtube

Youtube ni app ambayo watu hutumia kuangalia video mbalimbali ambazo huwa zinapostiwa kwenye channel. Katika Youtube kuna channel ambazo hutuma filamu na unaweza angalia filamu hizo bure kabisa. Ukiachana na channel za filamu pia kuna kipengele cha Youtube kinachojihusisha na filamu tu(filamu za bure na kununua}. Kipengele hicho cha Youtube hakipatikani katika baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania kwa sasa ila unaweza soma maelezo ya kukuiona hapa chini.

Jinsi ya kuona kipengele cha movies cha YouTube Gusa hapa>>>>

Prime Video

App hii inaitwa “Amazon Prime Video” lakini kwa kifupi unaweza kuiita “Prime Video”. Ni moja ya app zinazoweza kukufanya ufurahie kuangalia movies na hata vipindi vya Tv pia kiganyani pako. Prime Video sio app ya bure lakini inakupa uwanja mpana unaofanana kiasi na netflix hivi katika filamu, unaweza angalia filamu nyingi maaalufu. Maelezo ya kiasi utakachotakiwa kulipa kwa mwezi yaliopo katika tuvuti yao yametaja kiasi kuwa ni USD 5.99 ambayo ni kama Tsh 14000 ivi…

~Viasi vya malipo vilivyo tajwa kwenye makala hii ni makadilio tu.