Tag Archives: afya

App nzuri za simu katika kufanya mazoezi ya mwili

Kuna app nyingi ambazo tunaweza ziingiza kwnye simu zetu na zikawa msaada kwenye vitu au mambo tunayofanya kwenye maisha. Hapa kwenye ukurasa huu The bestgalaxy tumekusanya app chache zinazoweza saidi katika upande wa mazoezi ya mwili. Nadhani wengi tunajua umuhimu wa mazoezi ya mwili katika maisha ya mwanadamu, hasa katika kipindi hiki chenye mambo mengi yanayohatarisha afya ya mwili wa binadamu.

Binadamu wa sasa tumezungukwa na vyakula pamoja na tabia nyingi zisizo rafiki kwa Afya zetu, ukiwa kama mwanadamu wa kipindi hiki unashauriwa kufanya mazoezi ili kuuweka mwili sawa na kuepuka baadhi ya magonjwa. Kabla ya kwenda moja kwa moja kuangalia app hizi, nakukumbusha kuijenga na kuendelea kuilinda tabia ya kufanya mazoezi maana ni jambo la maana usiloweza kujutia maishani.

Home workouts app: credit

App nzuri za simu katika kufanya mazoezi ya mwili(Android na iOS)

Home workouts

Hii app ni maarufu sana katika upande wa app za mazoezi za simu. App ya Home workouts imejikita zaidi katika kusaidia watu wanaotaka kufanya mazoezi ya mwili wakiwa nyumbani. Inakupa mbinu za mazoezi ya kufanya ili kuweka misuli ya mwili vizuri, kupunguza uzito au kupunguza mwili. Inakuonesha jinsi unavyoweza fanya yote hayo ukiwa nyumbani bila kwenda GYM zilizo mbali na ulipo. Inaweza simama kama mwalimu au msimamizi wako wa mazoezi ya nyumbani ukiwa kama Mwanamke au Mwanaume unaempenda mazoezi.

Workout for Women

Hii app ni kwaajili ya mwanawake unaehitaji kufanya mazoezi. Kama wewe na mwanamke unaetaka kufanya mazoezi ya mwili lakini unakosa muda wa kutoka ulipo na kuelekea GYM, basi app hii inaweza kuwa masada zaidi kwako. App ya Workout for Women inasimama kama mwalimu wa nyumbani wa mazoezi ya kuweka mwili sawa. Inakupa mazoezi ya kupungiza tumbo, kuongea makalio na kufanya ujihisi mwepesi. Workout for Women inakupa mbinu za kufanya mazoezi hata ukiwa kitandani hivyo itakua ni juu yako tu kutenga dakika chache kujiweka sawa kila siku.

Strava

Strava ni app maalumu kwa watu wanaopenda kufanya mazoezi lakini mazoezi haya sio ya sehemu moja. Hii ni kwaajili ya mazoezi kama kukimbia au kuendesha baisikeli. Wengi hufanya mazoezi haya asubuhi au jioni ili kuwema miili yao sawa. App hii inasidia mtu kupima umbali anaokimbia kila siku na kujua anakimbia kutoka wapi kwenda wapi.

Inaweza kuunganishwa na saa za kidigitali zinazofahamika kama “Smartwatch” japo sio zote. Inasaidia kuangalia maendeleo katika mazoezi yako hirahisi kwenye simu. Unaweza angalia hata Hali ya mapigo yako ya moyo unapofanya mazoezi (Hii itakuitaji utumie Heart rate monitor au Smartwatch).

GYM DONE

App hii imejikita zaidi kwenye upande wa mazoezi ya GYM. Ni app inayoweza kukuongoza unapofanya mazoezi kwenye chumba Cha GYM kwakutumia vifaa mbalimbali. Kwenye app ya GYM Done unaoneshwa mbinu au namna ya kutumia vifaa vya GYM kuweka vizuri misuli ya sehemu tofauti za mwili. Mtumiaji unaweza pia kujiweka mipango yako ya mazoezi ili kukamilisha malengo yako.

App za mazoezi ya mwili zimekua zikitumika na mamilioni ya watu wanapofanya mazoezi na zimekua msaada mkubwa katika kujenga afya ya mwili. Ni app hizo tu katika orodha yetu lakini fahamu kuwa kuna app nyingi nzuri kwa mazoezi ya mwili. Endelea kuwa nasi kwa mambo mengine zaidi.

Jinsi ya kupunguza msongo wa mawazo kwa kutumia simu

Matatizo ya kifamilia, mahusiano, kazi au matatizo ya kiafya yanaweza kuwa sababu ya watu kuingia kwenye msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo ni jambo linalowatokea watu wengi katika maisha na hutofautina viwango. Watu wenye  msongo wa mawazo mara nyingi wanahisi uzito wa mawazo yasiyowezekana, wasiwasi, au hali ya kukosa amani ya akiil zao. Na hali hii ikizidi huwa inaleta athari kubwa tu. Ni vema kuchukua hatua ya kapambana na msongo wa mawazo pele unapoona unataka kukuzidi.

Kushugulisha mwili, Kufanya mazoezi ya mwili, Kubadilishana mawazo na watu au marafiki waliokuzunguka, Kufanya vitu vinavyokupa furaha na kuonana na wataalam/madaktari ni baadhi ya mambo au njia nzuri unazoweza kutumia kupambana na msongo wa mawazo.

Ukiachana na mambo hayo, hapa chini The Bestgalaxy tunakufungua juu ya jinsi simu yako inaweza kukusaidia kidogo katika kupambana na msongo wa mawazo. Tunaenda kuanagalia vitu vichache unavyoweza kuvifanya kwa wakati falani kwenye simu yako ili kupunguza au kupambana na msongo wa mawazo. Lakini kabla ya yote ningependa ufahamu kuwa baadhi ya vitu hivi sio vizuri sana na nitakwambia ni kwanini.

Jinsi ya kupunguza msongo wa mawazo kwa kutumia simu

Tafuta ufumbuzi wa tatizo lililopelekea msongo wa mawazo

Simu janja au smartmphone huwa zinakupa uwezo mkubwa kiganjani pako. Unaweza tumia simu hizi kujifunza jinsi ya kutatua mambo mbali mbali kwa kusoma au kuangalia video za mafunzo. Unaweza tumia mtandao kama Youtube au Google kuuliza na kujifunza jinsi ya kutatua tatizo linalopelekea wewe kuwa na msongo wa mawazo. Ufumbuzi au usaidizi utakao upata utakufanya upunguze msongo wa mawazo.

Ungana au zungumza na watu watakao kupa furaha

Simu huwa zinampa mtu uwezo wa kufanya mazungumzo na watu walio mbali nae. Mtu anaweza fanya mazungumzo na familia, marafiki na hata kuungana na watu asio wajua. Kufanya mazungumzo na watu wanaokupa furaha au kukushauri, husaidia kupunguza msongo wa mawazo.

Cheza magemu

Kwenye simu,unaweza cheza magemu ya aina nyingi. Kucheza magemu sio njia nzuri sana ya kupunguza msongo wa mawazo ila inategemeana na hali iliokukuta. Kabla ya kutumia njia hii ni vema ukatambua kuwa njia hii huwa inatumika kukimbia uhalisia au kukusahaulisha uhalisia tu ila haitibu tatizo lilikuletea msongo wa mawazo. Unaweza cheza  gemu na ukasahau kabisa uhalisia au hali ulionayo. Lakini baada ya kucheza unaweza kuwa unahisi furaha na nguvu ya kukabiliana tena na jambo linalokupa msongo wa mawazo au unaweza maliza kucheza gemu ukukuta tatizo liko palele na msongo wa mawazo ukakujia tena. Ni vema pia kuepuka kutumia muda mwingi kwenye kucheza gemu bila kutatua tatizo au kufanya mambomengine ya msingi maana hilo ni tatizo jingine pia.

Kuangalia na kusikiriza vitu vitakavyokupa furaha

Kupitia simu yako, unaweza kuangalia video zinakupa furaha au kusikiliza audio zinazokupa furaha. Kama unapenda vichekesho, filamu na video za burudani nyingine basi unaweza kuangalia video zote kwenye simu yako. Mbali na video unaweza pia kusikiliza nyimbo unazojipenda au simulizi. Lakini ni vema kufahamu kuwa kutumia muda mwigi kuangalia video huwa si uamuzi mzuri wa kupuguza msongo wa mawazo.

Kwanini mwanaume anashindwa kusimamisha? Sababu hizi hapa

Kuna sababu nyingi zinazoweza pelekea kutokea kwa tatizo la mwanaume kushindwa kusimamisha yaani, kushindwa kuwa na uwezo wa kuamsha uume wake na kuwa imara na mgumu wakati wa tendo la ndoa . Kuna wanaume hukumbana na tatizo hili kwa muda mfupi au kuwa tatizo la kudumu. Hali hii anaweza kumbana nayo mwanaume wa umri wowote(Mzee au Kijana).

Fanya haya ili uchelewe kupiga bao BONYEZA HAPA>>>

Sababu za mwanaume kushindwa kusimamisha

Sababu zinazoweza sababisha mwanaume kushindwa kusimamisha zinaweza kuwa za kisaikolojia, afya ya mwili, mtindo wa maisha, magonjwa ya zinaa au umri. Hebu tuangaliae zaidi mambo au sababu hizi:

Saikolojia.

Mwanaume akiwa na mfadhaiko, wasiwasi, msongo wa mawazo, au hofu ya kutofanya vizuri wakati wa tendo, anaweza jikuta kashindwa kusimamisha. Yani kama mwanaume hajiamini au mawazo yapo mbali na tendo anaweza kumbana na tatizo hili.

Afya ya mwili.

Tatizo la kushindwa kusimamisha kwa wanaume wengine linaweza kusababishwa na masuala ya afya ya mwili. Mwanaume akiwa na mwili wenye ugonjwa wa kisukari, shinikizo la damu, matatizo ya moyo, unene uliopitiliza, au ugonjwa wa tezi dume, anaweza kumbana na tatatizo la kushindwa kusimamisha.

Mtindo wa maisha.

Mwanaume pia anaweza shindwa simamisha baada ya uwezo wake wa kusimamisha kuathiliwa na matumizi ya tumbaku, unywaji wa pombe kupindukia, na matumizi ya dawa za kulevya. Pia, kutofanya mazoezi ya kutosha na kula chakula au lishe duni kunaweza kusababisha mwanaume kupata matatizo ya nguvu za kiume.

Mazoezi ya mwili yatakayo kusaidia katika mapenzi BONYEZA HAPA>>>

Magonjwa ya zinaa.

Mwanaume kuwa na baadhi ya magonjwa ya zinaa kama vile kisonono na magonjwa mengine kunaweza muathiri uwezo wake na kupelekea matatizo ya nguvu za kiume.

Umri wake.

Kwa wanaume wengi, umri huathiri uwezo wa uwezo wa kusimamisha. Mwanaume mwenye umri mkubwa anaweza jikuta amepunguza uwezo wa kusimamisha kutokana na umri wake ingawa hali hii huwakuta pia wenye umri mdogo.

Ikiwa mwanaume anasumbuliwa na tatizo hili kwa muda mrefu au mara kwa mara ni vyema kumwona daktari au mtaalamu wa afya ili kupata ushauri na matibabu sahihi yanayoweza saidia kuweka hali sawa.

Asante kwa muda wako, endelea kufuatilia The bestgalaxy, endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Uzazi wa mpango ni nini?

Karibu The bestgalaxy. Hapa unaenda kupata maaelezo yatakayo kufungua kidogo ubongo juu ya “Uzazi wa mpango. Uzazi wa mpango ni mpango au uamuzi wa mtu au watu katika kuzaa watoto .Lengo kuu la uzazi wa mpango ni kuruhusu wazazi kuchagua ni lini na idadi gani ya watoto wanataka kuwa nayo, kwa kuzingatia rasilimali walizo nazo zao, hali ya maisha, na malengo yao katika maisha. Kuna njia au hatua zinazochukuliwa na watu au jamii ili kudhibiti idadi ya watoto wanazozaa au kuepuka mimba zisizo tarajiwa.

Kuna njia mbalimbali za uzazi wa mpango na hapa chini tunaenda kuangalia njia 6:

Njia za uzazi wa mpango

1. Dawa za Kuzuia Mimba(Njia ya kisasa): Hizi zinaweza kuwa dawa za kumeza au sindano ambazo zinaweza kuzuia ujauzito. Mwanamke anaweza kwenda kwenye kituo cha afya akachomwa sindano ya kuzuia mimba au akameza vidonge vya kuzuia mimba.

2. Kondomu(Njia ya kisasa): Kondomu ni mipira amayo huvaliwa katika tendo kuzuia mimba na kujikinga dhidi ya magonjwa ya zinaa. Mwanaume kuvaa kondomu katika tendo kunaweza fanya mwanamke asipate mimba. Lakini pia kuna kondomu za kike ambazo mwanamke anaweza vaa kumsaidia asipate mimba.

3. Vitanzi(Njia ya kisasa): Hivi ni vifaa vinavyowekwa ndani ya mfuko wa uzazi na huweza kuzuia mimba kwa muda mrefu.

4. Vipandikizi(Njia ya kisasa): Hivi ni vijiti vyenye ukumbwa kama njiti ya kiberiti ambavyo huwekwa katika mkono wa mwanamke kwa lengo la kuzuia mimba.

5. Upasuaji wa Kuzuia Mimba(Njia ya kisasa): Kwa wanaume, upasuaji wa kufunga mirija ya uzazi (vasectomy) unaweza kutumika kuzuia mimba. Kwa wanawake, upasuaji wa kufunga mirija ya fallopian (tubal ligation) ni njia nyingine.

6. Kufuatilia mzunguko wa hedhi au kutumia kalenda(Njia ya asili): Pia unaweza zuia mimba zisizotarajiwa kwa kufuatilia mzuguko wa hedhi kisha kuepuka kufanya tendo katika siku za hatari.

Uzazi wa mpango unaweza kusaidia kudhibiti idadi ya watoto na kuboresha afya na ustawi wa wazazi na familia kwa kutoa fursa ya kuchagua lini na jinsi ya kupata watoto. Lakini unapawa kutambua kuwa njia nyingi za uzazi wampango za kisasa zimekuwa zilieta madhara kwa watumiaji. Ni vema kufika katika kitua cha afya na kupewa muongozo zaidi juu ya njia za kisasa za uzazi wa mpango. Njia ya Kufuatilia mzunguko wa hedhi au kutumia kalenda ni njia ya asili isio na madhara kwa mtumiaji ila ina hitaji umakini sana.

Je, wajua haya kuhusu Kondomu na Ukimwi? soma hapa

Kondomu ni kifuko kinachotumiwa na wanaume tangu zamani kuzuia mimba na maambukizi ya maradhi ya zina. Siku hizi kuna kondomu ya kike pia.

Kondomu zinatengenezwa kwa ngozi ya mnyama, siku hizi hutengeneza kwa kutumia mpira.

Utengenezaji hufanyika katika mazingira ya baridi ili kuhifadhi uimara wa mpira.

Zinaunganishwa ngozi nyembamba mbili ili matundu ya ngozi ya kwanza yazibwe na ile ya pili na matundu ya ngozi ya pili yazibwe na ile ya kwanza.

Kisha kupimwa, kondomu huwekewa dawa ya kuzuia isiharibike: dawa hiyo ina madhara kwa afya.

Pamoja na kutumika kwa ajili ya kuzuia mimba kwa mafanikio makubwa (ingawa si 100%), mpira huo unatangazwa sana kama kinga imara dhidi ya virusi vya UKIMWI.

Lakini katika utafiti uliofanywa na shirika la Sexuality Information and Education Council la Marekani kwa majozi 122 ambapo mmojawao alikuwa mwathirika, wenzao 12 waliambukizwa (10%) ingawa walifanya ngono kwa kutumia kondomu kila mara na kwa usahihi.

Shirika la Human Life International lilifanya utafiti kwa aina mbalimbali za ngono. Kati ya waliotumia vizuri kondomu, mwaka wa kwanza waliambukizwa: 11% za waliofanya ngono ya kawaida, 30% za waliofanya ulawiti. Mwaka wa pili wakafikia 21% na 51%. Mwaka wa tatu wakawa 30% na 66%.

Kwa maneno mengine ni kwamba kondomu haizuii moja kwa moja, bali inaahirisha maambukizi: kama si leo, inaweza tokea kisababu kesho ukapata japo ni kwa uwezekano mdogo sana, hasa kama ukiwa muangalifu katika taratibu za utumiaji. Pamoja na yote hayo, huwezi kulinganisha hata kidogo kutumia kondomu na kutotumia kabisa. Bado kondomu ni kitu kinachozuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa asilimia kubwa sana ukilinganisha na kutoitumia. Ndio maana watu hushauriwa kutumia kondomu ili kuzuia maambukizi wanaposhirikiana kimwili bila kujua hali zao. Na endapo mtu akipata virusi vya ukimwi ni vema akajikubali, akeelewa kuwa sio mwisho wa maisha na pia kuwatu wengi katika Dunia au mazingira yake wanahali kama yake waishi kama kawaida.

Mazoezi ya kupunguza tumbo au kitambi (rahisi unafanya hata nyumbani)

Tumbo au kitambi imekua ni tatizo ambalo baadhi ya wanaume na wanawake hukumbananalo katika miili yao. Tukitungunzia kitambi katika mwili wa mwanadamu ni mafuta ambayo hujikusanya katika maeneo ya tumbo na kulifanya tumbo kuonekana limeongezeka ukubwa. Mara nyingi kitambi huibuka katika mwili wa mtu kutokana na mlo wa mtu mwenyewe au staili ya maisha yake kiujumla. Mazoezi ni njia salama na ya bure ya kuepukana au kuondokana na kitambi.

Kunawatu huwa wanashindwa kutumia njia hii na kufanikiwa kupunguza kitambi kutokana na kutarajia matokeo ndani ya siku moja au mbili. Ukiwa na mawazo hiyo kichwani hautaweza kufanikiwa kupunguza kitambi kwa njia ya mzaoezi maana matokeo huwa yanachukua muda. Yanaweza kuaanza kuonekana zaidi baada ya siku 30(mwezi).

Ukitaka kufanikiwa kirahisi, kichwa chako kiwe kinaelewa kwamba mazoezi unayoanza kufanya hayapunguzi tumbo tu, yanakufanya uweunacheza mchezo wa kitandani vizuri na kwakuchangamka, utachangamka pia katika shughuli zako nyingine tena utaepukana baadhi ya magonjwa. Ukifanya mazoezi vizuri kwa siku 7 tu unaweza anza kuona faida hizo nyingine hatakama tumbo halijapungua. Ni vema ukafanya mazoezi kuwa ni tabia yako tu ili faida zake uwe unazifurahia kila siku katika maisha yako.

Hapa chini tunashusha mazoezi matatu tu ambayo unaweza kuanza kuyafanya kila siku ili kupunguza kitambi au tumbo. Mazoezi haya ni kwaajili ya wanawake na wanaume pia. Yanaweza fanyawa hata nyumbani tu na kama hauna muda maalum wa mazoezi unaweza tafutiza dakika chache kila siku kabla haujaingia kuoga, ukayafanya. kwasiku za mwanzo unaweza pata maumivu kutokana na mwili kutozoea mazoezi lakini usikate tamaa, endelea kufanya tu maana maumivu huisha na hukuacha ukiwa imara zaidi.

Mazoezi matatu ya kupunguza Tumbo au kitambi (Mwanawake na Mwanaume)

Zoezi la kwanza

Tafuta sehemu nzuri na safi ambayo itakuruhusu kulala chali bila tatizo. Nenda katika sehemu hiyo kisha ulale chali. Nikisema “kulala chali” namaanisha kulala kwa kuangalia juu. Baada ya kulala chali hapo chini, kishike kichwa chako kwa mikono yako yote miwili alafu ukiwa hivyo hivyo, anza kujinyanyua kiwiliwili na kichwa juu alafu unarudi chini. Endelea kwenda juu na chini, juu chini bila kuibandua miguu yakochini. Angalia mfano katika picha hii;

Image:Giphy

Zoezi la pili

Katika zoezi hili, hatua ya kwanza ni kuchuchumaa chini. Baada ya kuchuchumaa nyoosha mikono yako mbele alafu shika chini katika sakafu. Baada kufanya hivyo, anza kuitegua na kuivuta miguu yako yote miwili kwa nyuma bila kiwili wili kugusa chini alafu irudishe tena miguu kama ilivyokua. Endelea kuifanya hivyo miguu kama inavyoonekana katika picha hii.

Image:Giphy

Zoezi la tatu

Kwenye zoezi hili utatakiwa kuanza kwa kulala chali kama katika zoezi la kwanza. Lakini baada ya kulala chali utatakiwa kuwa unanyanyua miguu yako yote miwili, wa kushoto na wakulia na kulileta juu kwa pamoja alafu unairudisha Tena chini. Endelea kufanya hivyo kwa kurudia kwenda juu na chini. Unaweza angalia picha ili kuelewa zaidi.

Image:Giphy

Fanya haya baada ya kondomu kupasuka katika tendo

Mpira wa kondomu hutumika katika tendo la kujamiiana ili kuzuia mimba na vile vile hutumika kwa lengo la kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi na magonjwa mengine ya zinaa. 

Katika utumiaji wa mipira ya kondomu kupasuka kwa kondomu hutokea mara nyingi Sana bila kutarajiwa. Mara nyingi kitendo hiki husababisha mimba zisizotarajiwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa. Hapa kuna hatua nne unazoshauriwa kuzifuata iwapo kondomu imepasuka:

1. Kuwa mtulivu na tafuta kondomu hiyo iliopasuka.



Mara nyengine kwa mwanamke vipande vya mpira huo wa kondomu vinaweza kuingia ndani ya mwili.

Ingiza vidole vyako ndani ya mwili, vishike na kuvitoa nje.

Mipira ama vipande vya kondomu vinavyosalia ndani ya mwili wa binadamu vinaweza kusababisha hasara hivyobasi ni muhimu kuangalia na kuhakikisha kuwa umetoa kondomu yote.

2. Tumia dawa za kuzuia kushika mimba iwapo hamjakubaliana kupata mtoto(Kwa mwanamke)



Dawa hizi zinapaswa kutumiwa katika kipindi cha saa 72 tu. Zinauzwa madukani yaani zinapatikana katika maduka ya dawa.

Iwapo huna mpango mbadala unaweza kutumia dawa za kupanga uzazi.



3. Kupimwa magonjwa ya zinaa hususan HIV iwapo hujui hali ya mwenzako




Nenda katika kituo cha dharura karibu nawe na umwambie daktari yaliofanyika.

Pia unaweza kuchukua dawa aina ya Post Exposure Prophylaxis (PEP) katika kipindi cha saa 72.

PEP ni mchanganyiko wa dawa za kukabiliana dhidi ya virusi vya ukimwi ambazo zinakuzuiwa kutoambukizwa HIV iwapo mwenzako ni mwathiriwa.

Kumbuka kwamba kila ugonjwa wa zinaa una muda wake wakati unapoambukizwa na wakati utakapoonyesha unapopimwa.

Unashauriwa kufanyiwa vipimo zaidi vya vya magonjwa ya zinaa baada ya mwezi na baada ya miezi sita ili kujua hali yako.



4. Jiulize kuhusu kilichosababisha na usirudie kosa.





Wapenzi wengi huruka hatua hii bila kujua kuwa hayo ni makosa makubwa, kwa sababu utakapoelewa ni kwa nini mpira huo ulipasuka ndipo unaweza kujiweka vizuri katika mchezo mwingine. Hivyobasi jiulize kuhusu hilo.