Category Archives: Uncategorized

Jinsi ya kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG Mobile

PUBG Mobile ni Game linalokutupa katika eneo moja uwe kati ya wachezaji 100 wanao pambana kubaki hai katika eneo hilo. Gemu hili linachezwa na watu wengi sana hapa Duniani pamoja na kuzuiliwa kwenye baadhi ya nchi.


Mechi moja ya PUBG inaweza kuwa ngumu au nyepesi kwako maana unacheza na watu halisi unaoweza kutana nao alafu ukawazidi uwezo au wakakuzidi uwezo. Kiufupi ni ngumu sana kuwa mtu unaweza kumzidi kila unaekutana nae kwenye mechi ya gemu la PUBG. Kuna muda ukiwa kama mchezaji unaweza jikuta umefanya vibaya kwenye mechi na kutolewa kwenye mechi mapema.


Kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG ni jambo muhumu sana na hutoa points za uhakika. Hata usipokua na Eliminations nyingi, ukiishi kwa muda mrefu kwenye mechi utapewa points.
Kama umekua na changamoto ya kutoishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG, yafuatayo ni mambo yanayoweza kukufanya ukishi muda mrefu kwa urahisi kidogo.

Mambo ya kuzingatia kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG

Chukua Level three helmet

Unapotua na kukusanya vitu katika mechi ya PUBG, huwa ni ngumu kupata kitu unacho hitaji maana vitu huwa haviwi kwenye mpangilio unaoeleweka. Lakini kama utabahatika kupata “Level three helmet” usiiache. Level three helmet katika mechi ya PUBG hulinda zaidi kichwa chako pindi kinapo pigwa na maandui. Level three helmet inaweza kulinda kichwa chako hata ukipigwa na M24 ambayo watu huiogopa pindi inapo nguruma katika eneo.

Usitembee kwenye sehemu za wazi

Hata sehemu iwe inaonekana salama kiasi gani, hakikisha haupiti bila kuwaza utajificha wapi pindi utakapo sikia mtu kaanza kukushambulia. Ukiwa unapita sehemu ya uwazi katika gemu la PUBG ni rahisi mtu usiemuona kukuona wewe na kuanza kukushambulia. Hivyo ni vema ukawa na tabia ya kupita sehemu zisizo na uwazi ili usipoteze maisha mapema. Pendelea kupita sehemu zenye mawe makubwa, miti, majani marefu au nyumba ili kuishi mda mrefu katika mechi ya game la PUBG.

Usikimbilie Eliminations kuliko kulinda uhai wako

Kutafuta Eliminations kwenye game la PUBG mobile ni kitu kizuri tu. Ila kama utakua unacheza ukiwa na tamaa ya kupata Eliminations nyingi alafu unasahau swala la kujilinda mwenyewe, utakua haudumu sana kwenye mechi. Kabla ya kufuata mtu kushambulia, hakikisha upo kwenye upo kwenye usalama na unauhakika wa kumuweza. Kama unaona upo kwenye hali mbaya, kujificha au kukimbia inaweza kuwa uamuzi mzuri pia.

Kuwa makini unapofuata Airdrops

Airdrops zinaposhuka huwa watu wengi wanaangalia juu ili wajue zinapotua. Zikishatua tu, kuna watu wengi wanakua tayari wapo njiani kuzifuata. Sasa ukiwa mmoja kati ya watu wanaozikimbilia Airdrops hakikisha unakua makini maana watu wengi wanaenda sehemu unayoenda. Mukikutana, wanaweza kukuzidi au ukawazidili lakini sehemu za Airdrops bado huwa ni hatari maana watu wengi hushindwa.

Usitue sehemu zenye majina makubwa mara kwa mara.

Kuna sehemu Katika ramani za game la PUBG mobile huwa zinafahamika sana. Watu wengi huwa wanapenda kushuka katika sehemu hizi kiasi kwamba unaweza tua na kupoteza maisha ndani ya sekunde chache tu. Sasa ukitaka kuishi mda mrefu katika mechi ya gemu la PUBG, usiwe na tabia ya kutua katika maneno haya. Tua katika maneno ambayo watu wengi hawatui ili upate hata muda wa kujiweka sawa.

Mwisho; Game la PUBG mobile ni gemu linalohitaji ujipe muda wa kujifunza pia. Jipe muda wa kucheza Kila mara ili upate uzoefu wa kulicheza na huu uzoefu unaweza kukufanya uwe na wezo wa kuishi mda mrefu katika mechi. Asante sana na endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Mambo ya kuepuka katika mahusiano

Mahusiano ya mapenzi yanaweza kuwa na vitu vingi vya kuongelea na hapa Kwenye ukurasa huu tumechagua kuzungumza mambo ya kuepuka katika mahusiano. Katika mahusiano, Kuna mambo usipo ya epuka yanaweza hatarisha mapenzi au mahusiano yenu. Mambo haya haijalishi ni mwanaume au mwanamke, ni vema kuyaepuka.

Mahusiano ni kama mmea unaouotesha aldhini na kuhakikisha kuna uwepo wa mambo yanayo ruhusu mmea huo kuota au kuendelea kukua na sio kufa. Lakini pia Kuna vitu pia unahitaji kuepuka kwenye mahusiano ya mapenzi ili yasife kama mmea.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Mambo muhimu ya kuepuka katika mahusiano (wanawake na wanaume)

Kupoteza Imani


Uaminifu unatakiwa kuwa ni kati ya vitu muhimu sana katika kustawisha mahusiano. Pia uaminifu ni moja ya vitu ambayo sio rahisi kuvipata pindi mtu anapopoteza.
Kuaminiana kwenye mahusiano hufanya mahusiano ya mapenzi kuwa mazuri sana kwa wapenzi. Lakini endapo imani kati yao itatoweka, basi mahusiano yanaweza kuanza kuyumba hapo. Kama upo kwenye mahusiano na mpenzi wako ni vema kutunza na kuiheshimu imani ya mwenza wako kwako. Epuka kutumia imani yake kwako kumdanganya au kumuona mjinga siku imani ikitoweka, hata neno “Samahani” linaweza kuwa halina uzito.

Mambo muhimu kufanya kwa mpenzi mwenye hasira au ukorofI BONYEZA HAPA>>>

Kukata Mawasiliano kati yenu

Mawasiliano pia husemwa kuwa ni moja kati ya vitu muhimu kwenye mahusiano ya mapenzi. Ni kweli mahusiano ni jambo muhumu na endapo mawasiliano yatafifia au kukatika katika mahusiano ya mapenzi, Unaweza kuwa ndio mwanzo wa mahusiano kuisha. Epuka kukata mahusiano kati ya wewe na mpenzi wako maana unaweza kuwa ndio mwisho wenu.

Kushusha heshima na kuiinua dharau.

Unaweza kuwa na mahusiano na mtu, mmezoeana sana kiasi kwamba unajua vitu vyake vingi sana vizuri na vibaya. Hata ujue sana, haushauriwi kushusha heshima na kuinua dharau. Kama kuna mambo ya kumsaidia, msaidie tu bila kumdharau. Kama kuna vitu vya kumvumilia, mvumilie bila kumuonesha dharau. Epuka kumtukana, kumsema vibaya kwa watu au kutomsikiluza. Ziheshimu hisia zake na kujali upendo wake kwako.

Maneno ambayo hautakiwi kusema kwa mwenza wako BONYEZA HAPA>>>

Kukosa Malengo

Mahusiano huwa na malengo pia. Mkishatulia kwenye mahusiano ni vema kuwa na malengo mnayojiwekea ili muishi kutimiza. Msipo kuwa na malengo kwenye mahusiano, mnaweza yumba kirahisi na kuachana kwasababu ya kukosa muelekeo. Malengo hufanya mahusiano ya mapenzi yawe na muelekeo. Malengo yanaweza kuwa ni mipango ya baadaye kama vile ndoa, familia, au malengo ya kifedha katika maisha yenu.

Kuingiliana kwenye mambo mengine

Wapenzi katika mahusiano huondoleana mipaka mingi sana. Lakini unapaswa kufahamu kuwa kuna baadhi ya vitu au mambo ukiwa kwenye mahusiano unashariwa kutoingilia. Kama kuna mambo yake au vitu anapenda na haviathiri mahusiano au maisha yenu, ni vema kuishia kuwa mshauri tu au kutomuingilia kabisa. Upuka kumuingilia kwenye mambo yake binafsi.

Mwisho; mambo yote tulio ya zungumzia hapa, yana umuhimu mkubwa katika mahusiano. Hatakama kutakua na changamoto katika kuyazingatia, ni vema ukapambana na kuanza kuyazingatia ukiwa kama mwanamke au mwanaume.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Siku hizi Mapenzi ni Pesa au bado Upendo wa kweli upo?

Uhusiano wa pesa na mahusiano ya mapenzi umekua ukifanya watu wa wawe na imani tofauti kuhusu mapenzi ya sasa. Kuna watu wanaamini kuwa kwasasa mapenzi bila pesa ni hayapo. Na pia Kuna watu wanaamini kuwa mapenzi bila pesa yapo.


Ukweli usio fichika ni kwamba pesa imekua na umuhimu mkubwa sana katika maisha ya binadamu katika kipindi hiki. Japo sio yote, lakini mambo mengi katika maisha ya binadamu huwa yahitaji pesa ukilinganisha na kipindi cha nyuma.

Mapenzi na Pesa

Pesa juu ya Upendo wa kweli


Katika mapenzi, mara nyingi pesa inaanza kuwa juu ya upendo wa kweli kutokana na uhitaji wa vitu au maisha yanayo hitaji pesa. Pesa haiwezi kuendesha au kuvuruga mahusiano ya mapenzi kama watu au wapenzi watakua hawahitaji kufuata maisha au vitu vinavyo hitaji pesa nje ya upendo au mahusiano yao.

Kwa watu ambao huingia kwenye mahusiano yenye upendo wa kweli lakini wanahitaji sana vitu au maisha ya juu yalio nje ya upendo wao au mahusiano walionayo, ni rahisi kutupa chini ndoa au mahusiano walionayo na kuanzisha mahusiano na mtu mwenye pesa au maisha wanayohitaji.


Kuna wanaume wapo tayari kuacha mahusiano yao na kufuata mwanamke mwenye pesa na pia kuna wanawake wapo tayari kuacha mahusiano na kufuata mwanaume mwenye pesa. Hii haipo kijinsia kwa sasa.

Watu hawa wanaweza kuwa hivi kutokana na mazingira waliokulia, hali ya Maisha walionayo, tamaa au mitazamo yao juu ya mapenzi na pesa. Ukizungukwa au ukikutana na watu kama hawa kwenye mahusiano, inaweza kuwa ngumu kuamini kuwa kuna upendo wa kweli tena.

Upendo wa kweli upo

Mapenzi ya kweli yapo na yataendelea kuwepo japo watu hutoa hoja nyingi za kwamba mapenzi ni pesa kwa sasa, hasa katika mitandao ya kijamii. Lakini tukienda kwenye uhalisia, kuna watu wengi tu walipendana na wanapendana bila kuzingatia maswala ya pesa. Kuna watu wengi pia ambao wanapesa nyingi lakini upendo haupo kati yao kiasi kwamba wanaanza kutafuta watu wengine hata wasio na pesa ili kufurahia upendo. Kuna watu mpaka ambao hukataliwa na watu wanaowataka pamoja na kutanguliza pesa zao mbele, yani mtu anachukiwa yeye na pesa zake. Mbali na hayo, Kuna watu wengine hupendwa bila kuwa na pesa.


Ni ngumu kuuteka moyo wa mwanamke au mwanaume mwenye pesa kwa kumpa pesa ila kuna watu huuteka moyo wa mwanamke au mwanaume mwenye pesa kwa mapenzi.

Mambo hayo yanaweza kuwa yanaashiria nini? Hii ni ishara ya kwamba Mapenzi sio pesa japo pesa inaweza athiri upendo wa baadhi ya watu wanaokimbiza zaidi vitu vinavyo hitaji pesa au maisha yanayo hitaji pesa.

Mpenzi kuomba pesa

Jambo la muhimu la kujua hapa ni kwamba maisha ya sasa ya binadamu yanahitaji pesa ili kufanya baadhi ya mambo. Mukiwa kwenye mahusiano, ukiachana na Magari, maisha ya juu na zawadi za gharama, mpenzi wako anaweza kuwa na shinda au mahitaji ya muhimu yanayohitaji pesa. Kuombwa pesa za vitu kama hivyo na mpenzi wako haina maana mbaya na kumpa ni kumsaidia tu, sio ujinga.


Akikuomba pesa kwanini usimpe kama ipo ndani ya uwezo wako? Unaweza kumsaidia vipi hiyo shida yake bila kutumia pesa? Kuna sehemu nyingine unayohisi anaweza chukua pesa?

Kama unajua kabisa wewe ndie mtu wa karibu na jambo lake lipo ndani ya uwezo wako, shughulikia shinda yake maana upendo ni pamoja na kusaidiana kwenye vitu hivyo ukiwa ni mwanaume au mwanamke.

Usipoonesha msaada kwa mpenzi wako mwanamke kwenye vitu vidogo vidogo vya muhimu vinavyo hitaji pesa, unaweza kumuweka kwenye hatari ya kushawishika na kuanza kukimbilia pesa nje ya penzi lenu. Ukiona anashida nyingi muanzishie hata biashara au michezo ya pesa ili asiwe anakuomba omba pesa moja kwa moja na wewe uwe unasehemu ya kumfukuzia.

Mwisho; Upendo wa kweli upo na kama mahusiano yenu yametawaliwa na upendo wa kweli ni jambo zuri. Uvumilivu ni jambo la msingi sana ili kudumisha penzi lenu pale mnapokua na hamna pesa. Tambua kuwa hakuna alie kamilika. Kuacha upendo na kuikimbiza pesa kunaweza kukufanya uangukie sehemu nzuri au sehemu mbaya. Unaweza fanikiwa kupata pesa na vitu vyote ulivyo hitaji lakini ukakosa upendo wa kweli maana upendo sio pesa wala mali. Ukiachilia mbali kukosa furaha au upendo wa kweli, unaweza angukia kwenye magonjwa au kupotezewa muda kisha kuachwa.

Pamoja na yote, hatuwezi zuia mitazamo. Mtazamo wako ni upi kuhusu Pesa na mapenzi?

Jinsi ya kuona sms za WhatsApp kwenye simu nyingine (Bila Kuigusa)

WhatsApp inatuwezesha watu kuwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki mtandaoni. App hii ina vipegele vingi na moja kati ya vipengele vyake kuna kipengele kinaitwa “Link a device”. Kipengele hiki kinamuwezesha mtumiaji wa Whatsapp kuunganisha akaunti ya WhatsApp kwenye vifaa viwili mpaka vinne. Baada ya kuunganisha WhatsApp kwenye vifaa hivyo sms na vitu vingine vingi vitakua vinaonekana kwenye simu zote hata zikiwa mbali. Na kila kifaa kitakua na uwezo wa kutumika kujibu na hata kufuta sms.

Kama ni mtu mwenye simu mbili na unahitaji kuona sms zako za Whatsapp kwenye simu nyingine bila kuigusa unaweza fanya hivyo kwa kutumia kipengele cha Whatsapp kiitwacho “Link a devices”. Hapa chini tunakupa mwanga juu ya jinsi unavyoweza kufanya kuungalisha na kuanza kuona sms za Whatsapp kwenye simu nyingine bila kuigusa. Hakikisha hautumii kipengele hiki kialifu.

Jinsi ya kuunganisha na kuona sms za WhatsApp kwenye simu nyingine bila kuigusa

Chukua simu zote mbili za smartphone na uziunganishe kwenye internet(ziwe na bando). Simu yenyewe unataka kuangalizia sms tutaiita simu ya pili, simu ambayo ina sms unazotaka uwe unaziona tutaiita simu ya kwanza. Baada ya kuziweka sawa simu hizo, fuata yafuatayo:

  • Chukua simu yenyewe unataka kuangalizia sms kwenye simu nyingine(simu ya pili) alafu ufungue web browser (Chrome) na kwenda katika website ya WhatsApp web ambayo ni https://web.whatsapp.com/
  • Baada ya kufanya hivyo, washa “Desktop site” kwenye hiyo web browser.
  • Baada ya kufanya hivyo, refresh ukurasa wa WhatsApp web alafu utaona kibox Cha QR code kimetokea kwenye ukurasa huo.
  • Baada ya kufanya hayo kwenye simu yako ya pili, sasa uchukue simu yenyewe itakua na sms unazotaka kuziona(simu ya kwanza) kisha fungua app ya WhatsApp.
  • Ukishafungua app ya WhatsApp, bonyeza vidoti vitatu vilivyo upande wa juu alafu chagua “Linked devices”.
  • Baada ya hapo utatupwa kwenye ukurasa wenye kitufe kilichoandikwa “Link a device”. Kibonyeze hicho kitufe alafu kamera ya simu hiyo itafunguka na utatakiwa kuitumia kamera hiyo kuscan QR code zinazooneshwa kwenye kile kibox kwenye simu nyingine. Ninaposema kuscan nnamaana elekeza hiyo kamera kwenye kibox kilichopo kwenye ukurasa wa WhatsApp web uliufungua kwenye ile simu nyingine.
  • Ukisha scan itaunganisha akaunti hiyo ya Whatsapp alafu utaandika jina lolote la kwenye sehemu ya device name itakayo jitokeza uijaze na kusave.
  • Baada ya hapo, utaanza kuona sms za Whatsapp kwenye simu zote mbili hata ukiwa mbali. Kiufupi utakua umefanikiwa kuziunganisha na utakua na uwezo wa kuangalia sms za Whatsapp za simu ya kwanza kwenye simu ya pili kupitia https://web.whatsapp.com/ ambayo ambayo inaitwa “WhatsApp web”.
  • Yani ukitaka kuangalia sms za WhatsApp za simu nyingine bila kuigusa, utaingia https://web.whatsapp.com/ kupitia Web browser yako na kuwasha “Desktop site” kwenye hiyo web browser ( Chrome) bila kuscan tena mara ya pili.
  • Ukifanya hivyo tu, moja kwa moja sms za simu ya kwanza utaziona kwenye simu ya pili kwa muonekano huu chini.

Hatua hizi zinaweza kuwa ngumu kama sio mtu unaejua sana vipengele vya simu. Lakini nadhani wengi wanaekewa vipengele vyote nilivyoelezea.


Mwisho; muunganiko huo utakatika endapo simu ya kwanza yenye sms itakua haijawa online kwa siku ya 14, ambazo ni sawa na wiki mbili.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Wanawake wanavutiwa na nini zaidi kwa wanaume

Mwanaume mara nyingi huwa ndio wanaonekana kuvutiwa na wanawake na sio wanawake wanavutiwa na wanaume. Lakini ukweli ni kwamba wanawake pia huvutiwa na wanaume japo hawana ujasili wa sema moja kwa moja kwa mwanaume kuwa kavutiwa nae.
Wanawake huwa wanavutiwa na wanaume na wengi wao wakitulia hukaa na kujadili wanaume wanao wapenda. Lakini wakikutana na hao wanaume wanao wapenda, ni ngumu kwa wao kuwa wazi kama jinsi wanaume wanavyo kuwa wazi wanapo kutana na wanawake wanao wapenda.


Hapa Kwenye ukurasa huu, The bestgalaxy tunaenda kukupa baadhi ya vitu au mambo wanawake wanavutiwa nayo zaidi kwa wanaume. Kuna vitu au mambo mengi wanawake wanaweza kuvutiwa nayo kwa mwanaume ila sisi hapa tumeeleza baadhi tu.

Mwanaume kuogopa wanawake wazuri kupita kiasi Fahamu kuhusu hii BONYEZA HAPA>>>

Wanawake wanavutiwa na nini zaidi kwa wanaume

Muonekano na harufu nzuri

Mwanaume mwenye muonekano mzuri huwa anawavutia wanawake. Lakini hapa swali ambalo linaluja ni “muonekano upi ni mzuri?”. Mwanaume msafi na anae vaa nguo zinazomkaa vizuri kuendana na mwili wake anaweza kuwavutia wanawake zaidi. Ndevu na nyele zilizo katika hali nzuri ya usafi huwafanya mwanaume awe na muonekano mzuri wa kuvutia wanawake.
Ukiachilia mbali mambo ya muonekano, harufu nzuri pia huwa inavutia wanawake. Tafiti nyingi zimekua zikionesha kuwa baadhi ya wanawake huwa wanavutiwa na harufu nzuri toka mwanaume.

Kuvutia kusomwa


Maisha ya binadamu ni kama simulizi inayoandikwa na watu wengine huwa wanasoma. Mambo mengi huwa tunasikia kuhusu watu kabla hatujakutananao na mambo haya huwa yanafanya tuwapende na tuwe na shauku ya kututana nao kabla hatuja kutana nao.
Sasa wanawake wanaweza kuvutiwa na mambo yako anayoyasikia alafu hata akikutana na wewe atatamani kuendelea kukujua na kukuosoma. Endapo ataendelea kugundua vitu vizuri kuhusu wewe, utamvutia kuendelea kukusoma na ndio basi utakua umemteka hivyo.

Kutokana na hili inashauriwa kutomwambia mwanamke mambo yote mazuri kuhusu wewe unapoingia nae kwenye mahusiano. Mambo mengi muache agundue mwenyewe au mwambie mbele ya safari.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika tendo BONYEZA HAPA>>>

Mwanaume anaejali na kuheshimu


Mwanamke anampenda mwanaume anaemjali. Kumjali ni jambo pana sana japo wengine huisi ni kumpa pesa na vitu vya thamani.
Mwanamke anampenda umjali kwa kumpa muda wako, kumsaidia kwenye baadhi ya mambo na kumuonesha tabia nyingine zinazoweza muaminisha kuwa yeye ni mwanamke unaemjali. Hatakama haupo nae kwenye mahusiano, kuna jinsi tu anaweza hisi unamjali na ukaugusa moyo wake akavutiwa na wewe japo ni ngumu kukuambia.

Ujasiri na msimamo

Wanaume wenye ujasiri na msimamo katika maisha yake anaweza vutia wanawake wengi sana. Unaweza onekana jasiri kwa mwanamke kwa kuchukua nafasi za uongozi, kuongea vizuri mbele ya watu, kuendesha maisha yako vizuri na kutatua changamoto mbalimbali. Msimamo katika mambo unayofanya inaweza mfanya avutiwe zaidi na wewe.

Vitu vya kushangaza ambavyo hutokea ukimpenda mpenzi wako sana BONYEZA HAPA>>>

Ucheshi na uwezo wa kujieleza

Wanawake mara nyingi huvutiwa na wanaume wenye hisia za ucheshi na uwezo wa kujieleza. Mwanaume ambae anaweza ongea na mwanamke vizuri na kumfurahisha au kumchangamsha kwa ucheshi wake, anaweza mvutia mwanamke kirahisi.


Ukiachilia mbali ucheshi, uwezo wa kujieleza unaweza fanya mwanamke akupende pia. Kunawezakuwa kujieleza hisia zako, kujitetea pindi unapokosea na mambo mengine kama hayo.

Mwisho; Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy ila kabla haujaondoka katika ukurasa huu, ni vema kutambua kwamba kila mwanamke anaweza kuwa na mambo binafsi anayovutiwa nayo kwa mwanaume.

Apple vision pro: Fahamu kuhusu Miwani hii ya Apple

Miwani ya VR(VR headsets) ni vifaa vya kisasa ambayo huvaliwa na watu na hufanya watu kuanza kuona mazingira ya kisasa au yalioundwa tofauti na mazingira ya ulimwengu halisi. Ukivaa Miwani hii unaweza kuona upo kwenye ulimwengu mwingine kabisa na ulimwengu ulio uzoea alafu utakua na uwezo wa kufanya vitu katika ulimwengu huo.


Makampuni mengi hujihusisha na utengenezaji wa Miwani hii ya VR ikiwemo kampuni ya Apple inayotoa simu za iPhone. Katika February 2, 2024 huko US, kampuni ya Apple ilitoa Miwani ya VR itwayo Apple vision pro. Miwani hii ilikua ikisubiriwa sana na watu wanaofuatilia mambo ya VR maana ilikua ikiongelewa sifa na mambo ambayo itakua nayo kabla Apple hawajaitoa.

Mambo kuhusu Apple vision pro

Apple vision pro imebeba vingi vizuri

Kwasasa Miwani hii imeisha toka na unaweza ipata kama bidhaa nyingine za Apple tunazozifahamu kutoka kampuni Apple. Baada ya Miwani ya Apple vision pro kutoka kumekua na mambo mengine yameongelewa kuhusu badhaa hii ya Apple. Machache kati ya mambo hayo ni yafuatayo.

Apple vision pro Ina vitu vingi vizuri tunavyoweza viongelea. Kwanza kabisa Miwani hii ina “eye and hand tracking”. Kupitia hii unaweza ivaa na kugusa au kuchagua vitu unavyooneshwa na Miwani hiyo bila kutumia kifaa kingine. Unaweza kuchagua au kugusa vitu kwakutumia macho tu au mikono yako bila kuwa na kifaa kingine chochote mkononi.

Kwenye kioo, Apple vision pro Iko na micro-OLED displays zenye pixels milioni 23, ambazo zitafanya ufurahie ubora wa picha za 4k kwenye Kila jicho.
Kwa usaidizi wa kamera, Apple Vision Pro inaweza kuunda Avatar ambae ataonekana unapowapigia kupiga video call watu wengine kupitia Miwani hiyo.

Kiufupi, Apple vision pro ni bidhaa nzuri sana toka kampuni ya Apple na imetikisa ulimwengu wa bidhaa za VR katika mwanzo wa mwaka 2024. Angalia video hii hapa chini.

Video ya Apple vision pro

Bei


Moja katika ya vitu watu wameongelea sana baada ya Apple vision pro kutoka ni bei yake. Ukihitaji kununua bidhaa hii kutoka kampuni ya Apple kwasasa itakuhitaji uwe na $3,499. Hiyo ndio bei yake katika Dola za kimalekani, ukiigeuza kibongo bongo(Tsh) inaweza kuwa kama milioni 8 na laki 9 hivi.

Kuna baadhi ya watu ikiwemo CEO wa kampuni ya Meta, Mark Zuckerberg wamezungumza kuwa ni ghalama sana kuliko Miwani ya Meta Quest 3 inayofanya baadhi ya vitu kama Apple vision pro japo haina ubora sana kwenye baadhi ya vitu pia. Miwani ya Meta Quest 3 inapatikana kwa Dola 499.99 za kimalekani.

Lakini Kuna waataalamu wameeleza kuwa Apple vision pro imeundwa nah baadhi ya vitu vyenye gharama kuliko Meta Quest 3, hivyo inaweza kuwa ni sawa kuwa na gharama kubwa.

Credit: Apple

Haipo vizuri kwenye games

Baadhi ya watu wanonunua miwani ya VR huwa wanapenda kutumia zaidi upande wa games. Kucheza VR Games kwenye Miwani ya VR kunaweza huwa kunafurahisha sana. Sasa Apple vision pro bado haiko sawa katika upande huu.

Hand tracking yake haiko vizuri sana ukilinganisha na Meta Quest 3 na haina game nyingi za VR unazoweza furahia kuzicheza. Pia hand tracking haiko vizuri sana kiasi cha kukufanya ufurahie zaidi kucheza game za VR. Ila Meta Quest 3 ndio imetajwa kuwa vizuri katika upande huu wa games kuliko Apple vision pro.

Inaendelea kuboreshwa

Apple vision pro ni bidhaa nzuri Toka apple lakini ni toleo la kwanza, yani “first-generation product”. Mara nyingi bidhaa toleo la kwanza huwa zinakuja na matatizo na madogo madogo madogo ambayo kampuni huwa inaangalia namna ya kutatua na kuboreshwa bidhaa yao hiyo au zijazo. Apple vision pro nayo ipo kuboreshwa na kampuni ya Apple ili iweze kuwa bora zaidi.

Ni hayo TU katika ukurasa huu, usiache kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi.

Image credit: Apple

Zingatia haya katika kulala na mme au mpenzi wako usiku

Kulala na mme au mpenzi wa kiume katika chumba inaweza kuwa sio sawa na kulala peke yako. Kunaweza kuwa sio sawa kwasababu ya uwepo mtu anaekupenda katika chumba. Mtu huyo anaekupenda anaweza kukupenda jinsi ulivyo na mambo yako katika kulala lakini kuna mambo au vitu ukivizingatia unaweza ukamfurahisha zaidi anapolala na wewe chumba kimoja.

Unahitaji kumfurahisha mwenza wako wakati wa kulala usiku? Sawa, hapa The bestgalaxy tunaenda kukufungua juu ya mambo ya kuzingatia katika kulala na mme au mpenzi wako usiku. Tumia muda wako kusoma mambo haya hapa chini na kama kunakitu ulikua hukizingatii basi unaweza anza kukizingatia ili kumfurahisha mume au mpenzi munapolala wote usiku.

Mambo humfanya mwanaume akupende sana na kukuchagua maishani BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kuzingatia katika kulala na mme au mpenzi wako usiku

Usafi

Hili tumeweka jambo la kwanza Kwasababu ni jambo muhumu sana. Usafi ukizingatiwa unaweza mfurahisha sana mme au mpenzi wa kiume katika kulala usiku. Tunapo zungumzia usafi, tunamaanisha Mwili unatakiwa kuwa msafi na pia chumba kinatakiwa kuwa kisafi. Hakikisha unaonga na sehemu zote za Mwili wako safi ikiwemo mdomo wako. Chumba chenu kifanye kiwe safi na kiwe kwenye mpangilio mzuri. Ondoa vitu vyenye harufu mbaya kisha ikiwezekana ongeza vitu vyenye harufu nzuri ya kumvutia. Kama chumba sio chako, yaani umemtembelea tu basi kuwa msafi wa Mwili wako inatosha.

Pozi la kulala

Huwa unalala mtindo gani ukiwa peke yako chumbani? Unahisi mtindo huo unaweza ruhusu mwema wako kulala vizuri mnapo lala wote? Kama haumruhusu kulala kwa uhuru kwenye kitanda, basi ni vema ukibadilisha mtindo huo ili kumfurahisha mume au mpenzi wako unapokua na usingizi. Unapojali usingizi wako, kumbuka kujali na usingizi wake pia kwa kulala vizuri usiku.

Mambo muhimu kufanya kwa mpenzi mwenye hasira au ukorofI BONYEZA HAPA>>>

Nguo nyepesi

Ukiwa mwanamke, sio kila nguo inafaa kuvaa unapo lala na mtu wako usiku. Kuna nguo ambazo unatakiwa kuvaa na ukizivaa wakati wa kulala usiku, utamfurahisha mme au mpenzi wako wa kiume. Unashariwa kuvaa nguo nyepesi sana na ikiwezekana ziwe zinateleza kiasi, laini au fupi. Usivae nguo inaoufunga Mwili wako kama mzingo, jiachie bila kuona aibu.

Sauti na utulivu katika maongezi

Kama mtakua na maongezi kabla ya kulala basi sauti yako katika maongezi inatakiwa kuwa ya mahaba. Jitahidi uwe mtulivu na uongeaji wako usiwe wa dharau au kufokea. Maongezi ya usiku yanatakiwa kuwa ya kupendeza na wewe kama mwanamke ndio unaweza fanya yapendeze zaidi kwa kutoa sauti itakayo gusa moyo wa mwanaume wako huku mukiwa mnatafuta usingizi.

Ni hayo tu Katika ukurasa huu. Nafikili itakua ni vizuri ukiendelea kuwa karibu na The bestgalaxy ili kujifunza mambo mengine ukiachana mambo hayo.

Mambo ya kuzingatia katika kununua bidhaa Mtandaoni (Online)

Kufanya manunuzi mtandaoni ni jambo watu hufanya sana katika miaka hii. Watu hununua vitu kwenye kwenye platfom maalumu za kuuza badhaa mtandaoni au kwenye mitandao ya kijamii.
Kununua vitu mtandaoni au online ni jambo zuri na huweza kufanyika kupitia vifaa kama simu au PC. Faida moja ya kununua vitu mtandaoni ni kuokoa pesa yako maana kuna bidhaa ambazo hupatikana kwa bei ya chini huku mtandaoni.

Ukiachilia mbali faida, kunachanga moto unaweza kutana nazo katika kufanya manunuzi mitandaoni. Hapa hatutazungumzia moja kwa moja changamoto hizi ila tunakupa mambo ya kuzingatia katika kununua bidhaa Mtandaoni. Mambo haya yanaweza kusaidia katika baadhi ya changamoto.

Mambo 5 ya kuzingatia katika kununua bidhaa Mtandaoni

Maelezo kuhusu badhaa

Bidhaa zinazouzwa mitandaoni huwa mara nyingi zinawekwa maelezo ambayo ukiwa kama mnunuzi unatakiwa kuyasoma ili kuielewa bidhaa. Unatakiwa usiishie kuangalia picha na bei tu, hakikisha unasoma na maelezo yaliowekwa kwenye hiyo bidhaa pia. Alafu usisahau kulisoma jina la hiyo bidhaa mara mbili mbili.
Ukiwa na tabia ya kununua vitu mtandaoni bila kusoma maelezo unaweza nunua kitu tofauti na ulichokusudia. Yani badala ya kununua simu, unaweza jikuta umelipia kupata kava la simu.

Angalia maoni toka kwa walionunua

Kabla ya kununua bidhaa Mtandaoni inashauriwa kuangalia maoni kabla ya kufanya maamuzi ya kununua. Mara nyingi watu huwa wanatoa maoni juu ya bidhaa walizonunua mtandaoni na kama bidhaa mbaya au nzuri huwa wanaweka wazi ili wengine wajue. Unaweza ingia YouTube, Facebook au ndani ya platfom unayotumia kununua bidhaa alafu ukaangalia maoni toka kwa walionunua katika kipengele cha “Reviews”.
Hii itakusaidia kujua kitu unachotaka kununua ni vizuri au kibaya. Ila unatakiwa kuwa makini na maoni ya uongo pia. Na fahamu kuwa baadhi ya vitu huwa vinakua vibaya kwa wengine ila ni vizuri kwako.

Utaratibu wa kurudisha bidhaa

Mambo mengi yanaweza tokea baada ya kulipia na kuletewa bidhaa ulioiona mtandaoni. Unaweza letewa bidhaa ikawa haina tatizo, ukaendelea kutumia au ikawa na tatizo, ukataka kurudisha.
Bidhaa ikiwa vizuri ni jambo zuri lakini ukiwa na matatizo alafu ukataka kuirudisha unapaswa kujua kuwa sio kila huduma huwa zinakuruhusu kurudisha bidhaa. Sasa ukiwa kama mnunuzi ambae unaona unaweza chukua bidhaa yenye matatizo kwa bahati mbaya, ni vema ukaangalia utaratibu wa kurudisha bidhaa zenye matatizo kabla hauja nunua hiyo bidhaa Mtandaoni.

Linganisha bei

Badhaa za mtandaoni huwa zinatofautiana bei. Unaweza kuta sehemu flani bidhaa inauzwa kwa bei kubwa kuliko sehemu nyinge lakini ni bidhaa moja. Kutokana na hili, inashauriwa kuwa mtu ambae ukiwa unataka bidhaa mtandaoni, uangalie hiyo badhaa katika sehemu tofauti tofauti na kulinganisha bei. Kwa kufanya hivyo, utapata sehemu ambazo bidhaa unayoihitaji inaizwa kwa bei rahisi.

Usalama wa pesa zako

Unapofanya manunuzi mitandaoni, usisahau kuzilinda pesa zako. Hakikisha unanunua bidhaa mtandaoni katika sehemu inayoaminika ili usiibiwe pesa zako. Hakikisha unajaza taalifa za malipo vizuri ili usije kosea kulipia. Hakikisha haudanganyiki katika kutoa taalifa za akaunti yako ya pesa.

Kama unatumia credit card katika kulipia, epuka kujaza taalifa za Credit card ukiwa umeunganisha kifaa chako na public WiFi bila VPN.

Mambo hayo machache yanaweza kusaidia katika kuepuka baadhi ya changamoto ambazo watu hukutana nazo. Hii inaweza kuwa kwenye platfom za kununua bidhaa kama; Alibaba, kikuu, Jiji na nyinginezo au mitandao ya jamii kama; Facebook na Instagram.

Namna ya kuchati na mpenzi wako

Siku hizi kuchati tunaweza sema ndio moja ya vitu watu hufanya sana kwenye simu. Katika muhusiano, mawasiliano ni muhimu sana kati ya wapenzi wanaopenda. Watu wengi wakiwa Katika mahusiano kuchati ndio huwa mawasiliano yao. Kuna watu kwenye mahusiano hutumia app kama WhatsApp,Telegram au huduma za sms za kawaida, kuchati na wapendwa wao. Yote ni sawa na kuchati ni jambo zuri maana huwaweka wapenzi karibu hatakama wako mbali. Kwa namna nyingine tunaweza sema kuchati huimarisha mahusiano ya mapenzi.

Hapa The bestgalaxy tunaenda kukufungua juu ya namna ya kuchati na mpenzi wako akiwa ni wakiume au wakike. Lakini unapaswa kufahamu kuwa hakuna namna moja ya kuchati na mpenzi, upo huru kuchati na mpenzi wako vile mnavyoona inafaa na inawapa furaha. Ila kama utaona inapendeza au unahitaji msaada, unaweza pia soma yafuatayo ili kujua jinsi au namna nzuri ya kuchati na mpenzi wako.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku BONYEZA HAPA>>>

Namna ya kuchati na mpenzi wako (Mwanamke/Mwanaume)

Weka utaratibu wa kumjulia hali


Salamu au kujuliana hali ni muhimu katika mahusiano na ukiwa unachati na mpenzi wako ni vema ukiwa umeweka utaratibu wa kumsalimia na kumjulia hali. Hii itamfanya mpenzi wako kujua unamjali na umemuweka akilini mpaka unakumbuka kutaka kujua yupo kwenye hali gani.
Unaweza kuwa na tabia ya kumjulia hali mida ya Asubuhi, mchana au muda wowote baada ya kuwa kimya kwa muda. Sio lazima iwe ni kila mara na sio lazima umjulie hali mara chache pia, kikubwa usimsumbue tu.

Maswali au maoini yanaweza kurefusha maongezi

Fahamu mbinu za kurefusha maongezi maana maongezi kuna muda yanaweza kuwa magumu kuyaendeleza. Mnapochati alafu mukafika hatua ambayo maongezi ni magumu kuyaendeleza, Kumbuka kuwa maswali au maoini yanaweza kurefusha maongezi yenu. Muulize maswali kuhusu yeye, vitu anavyopenda na kuhusu mambo mengine. Hii itamfanya awe anajieleza na kufanya maongezi yenu kurefuka. Pia na wewe usiwe mvivu kutoa maoni kwenye majibu yake ili kwenda nae sawa.

SMS za kumbembeleza mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Usiwe serious sana mtaishiwa mada

Ukiwa unachati na mpenzi wako, unaweza kuwa na mada nyingi ambazo unaweza ongeanae ili mada hizi ukiwa serious, utaziona hazina maana au zinakera. Kiufupi ikiwa kila unapochati na mpenzi wako unakua serious sana, mambo ya kuongelea yanakua machache sana kiasi ambacho unaweza ukashindwa pata mada kabisa.
Kwaiyo ni vema ukawa haupo serious sana ila mada ziwe zinatiririka kwenye maongezi yenu. Sehemu ya kucheka chekeni, sehemu ya kutaniana tanianeni, sehemu ya kubembelezana bembelezaneni, sehemu za kuongelea ujinga jifanyeni wajinga na kwenye sehemu ya mambo ya msingi ndio kueni serious.

Acha kuchati kabla hamjachoka kuchati

Kama unamtindo wa kuchati sana na mpenzi wako, hakikisha unakua na ujanja huu ili usimkere mwenza wako. Hakikisha ukichatinae sana unaacha kuchati kabla hamjafika hatua ambayo kila mtu amechoka kuchati. Tumia muda wako kuchati na mpenzi wako ila ukiona tu anaelekea kuchoka, acha kuchati nae. Unaweza katisha maongezi kwa kusema “nitakutafuta baadae kidogo mpenzi wangu” au ukatafuta kisingizio kingine. Kama atakua anataka kuendelea kuchati, kunajinsi anaweza endeleleza mwenyewe maongezi.

Usitume sms nyingi sana anapokua kimya

Ni kawaida kuwa na hali ya kushindwa kujizuia kutuma sms pale mwenza wako anapokua kimya. Ila Hali hii inabidi isikusukume kuwa kero kwa mwenza wako. Ni vema ukiwa kwenye hali hii ukahakikisha hautumi sms nyingi zisizo na maana kwa mpenzi wako. Tuma sms chache zenye kueleweka alafu kama atakua anasoma, atakuelewa na kukujibu.

Mambo ya kuepuka katika mahusiano BONYEZA HAPA>>>

Mwisho; usisahau kutumia maneno mazuri kwenye kuchati kwenu. Kama muko kwenye mahusiano ni vema mkawa mnachati kama wapenzi na sio marafiki. Kuna muda unatakiwa kuziweka mbali hizo “wewe” “Oya” na kuanza kuzitumia “mpenzi” “mke” “mme” na maneno mengine kama hayo.
Ni hayo tu tulio kuandalia katika ukurasa huu The bestgalaxy, usisahau kuwa karibu na sisi ili kufahamu mambo mengine mengi.

Jinsi ya kucheza game za Xbox kwenye simu

Kama ni mpenzi wa magemu ya Xbox na una magemu yako pendwa ya xbox ambayo hua unayacheza kwenye vifaa vya xbox basi leo napenda kukufahamisha kuwa kuna uwezekano wa kuyacheza magemu hayo kwenye simu yako. Na hapa The Bestgalaxy tunaenda kukueleza njia ya kucheza game za xbox kwenye simu.

Haijalishi ni Simu ya Android au iOS(iPhone), njia inayoenda kuelezwa hapa inaweza tumika kwenye  simu hiyo vizuri tu ila inajumuisha malipo ya huduma.

Jinsi ya kucheza game za Xbox kwenye simu

Unaweza cheza magemu ya Xbox kwenye simu yako kwakutumia huduma ya Xbox cloud gaming. Huduma hii ni huduma ya Xbox inayowezesha watu kucheza magemu ya xbox na yasio ya Xbox kwenye simu kwa kutumia internet. Unaweza kucheza magemu hayo kwenye huduma hiyo bila kudownload. Kupitia huduma hii tunaweza sema sio lazima kununua kifaa cha xbox ndio ucheza magemu ya Xbox maana unaweza yacheza kwenye sumu yako kwakutumia internet kupitia huduma hiyo ya xbox cloud gaming..

Kujiunga na huduma ya Xbox cloud gaming ni bure kabisa ila baada ya kujiunga utakua na uwezo wa kucheza bure game la Fortine tu. Ili kucheza magemu mengine itabidi ulipie moja vifurushi vyao ambayo kwa mfumo wao huitwa “Xbox Game pass”. Kivurushi hivi huanza kwa bei ya ofa ya dola 1 tu kwa siku 14 alafu baada ya siku hizo kuisha utaendelea na malipo yao ya kawaida ya vifurushi.

Fuata hatua zifuatazo kucheza game za Xbox kwenye simu kwa huduma ya xbox cloud gaming.

  • Fungua VPN kisha uunganishe server ya USA kama haupo usa kwa sasa.
  • Ingia Google kwa web browser.
  • Tafuta “Xbox game pass” kisha ingia kwenye matokeo ya juu toka xbox.com
  • Baada ya kufanya hivyo, utatua kwenye ukarasa unaokukaribisha kujiunga kwa kuchukua moja ya vifurushi vyao kwa bei ya ofa. Bonyeza kitufe kilichoandikwa “JOIN FOR $1” kuanza taratibu za kujiunga.
  • Kabla ya kuendelea utapelekwa kwenye ukurasa wa kuingia na akaunti ya Microsoft au kutengeneza mpaya(kama hauna utatengeneza mpya na kama unayo utaiweka)
  • Chagua kifurushi chako cha “Ultimate” alafu bonyeza “Next” kuendelea mpaka kwenye ukurasa wa malipo kwaajili ya kulipia.
  • Ukisha lipia tu, utakua na uwezo wa kucheza magemu ya Xbox kwenye simu ndani ya hiyo huduma yao bila kudownload. Utakua unatumia mtandao tu.

Unapocheza magemu kwa njia ya cloud, ni vema ukawa na mtandao uliotulia sana maana hicho ndio kitu kikubwa kwenye kucheza magemu kwa njia hii. Endapo mtandao utakua haujatulia, game pia litakua linasumbua unapolicheza. Asante kwa muda wako, endelea kuwa na The bestgalaxy kwa mambo mengine mazuri.