Category Archives: Uncategorized

Vichekesho vya kiswahili vunja mbavu




Karibu kwenye makala hii yenye vichekesho vya kusoma vinavyofurahisha! Katika ulimwengu wa hadithi za kuchekesha, tunakuletea mkusanyiko wa visa vya kufurahisha na kukuvunja mbavu. Kupitia makala hii, utaweza kufurahia na kucheka kwa kujitupa katika hadithi fupi zilizojaa kujifunza na kuchekesha pia.

Hadithi hizi za kuchekesha zimeandikwa na watu kwa ustadi na kubuniwa kwa kina ili kukuvutia wewe msomaji lakini hapa the bestgalaxy, zimekusanyawa tu. Hadithi inaweza kuja na mchanganyiko wa utani, kujikosoa, na vituko, kikubwa usiwe serious sana, lengo kubwa ni kucheka kufurahi hivyo jiachie.


Kucheka ni moja ya mambo muhimu katika maisha yetu ya kila siku. Kwanza kabisa, kucheka husaidia mtu kupunguza msongo wa mawazo na hali ya wasiwasi. Unapocheka, mwili wako huzalisha homoni za furaha kama vile endorphins, ambazo husaidia kupunguza mkazo na kuongeza hisia za nzuri.

Vichekesho vya kiswahili vunja mbavu

MUOKOTA MAKOPO:

Tamaa mbaya! Muokota makopo katika uokotaji wake wa makopo akaona chupa ambayo ndani kuna kikaratasi, alipoifungua chupa likatoka jitu la ajabu lisilo onekana na watu wengine. Lilikua likitetemeka na lilimwambia “kijana asante sana kwa kuniokoa omba vitu viwili sasa hivi”. Kijana kwa hofu akaomba pesa za kumiliki magari na majumba ya kifahari. Ghafla fuko liliojaa hela na pete ya dhahabu ya bahati vikadondoka mbele yake. Akaambiwa aseme ombi la pili, akasema “Nibadilishe niwe kivutio ili nipendwe sana nakina dada wazuri” Hapohapo jamaa akageuzwa akawa chipsi yai.!!

MTOTO MDOGO KATULIA NA BABA:

MTOTO: Hivi Baba ivi wewe umezaliwa wapi?
BABA: Nimezaliwa Mbeya
MTOTO: Mama nae kazaliwa Mbeya?
BABA: Hapana, amezaliwa Tanga
MTOTO: Na Mimi jee?
BABA: Dar
MTOTO: Mh Sasa tulikutanaje????
Baba akaangua kicheko

JAMAA BAADA YA KUCHELEWA KAZINI:

Boss: kwa nini umechelewa kazini

Juma: kuna mtu njiani alidondosha 5000 boss

Boss: anha kwahiyo ulikua unamsaidia kuitafuta

Juma: Hapana, bahati nzuri niliikanyaga nikawa nasuri aondoke.

MAWAZO YA VIKOBA:

(Mdada baada ya kufika kwa mpenzi wake akiwa na Mawazo mengi ya vikoba)

Mdada: Baby, naomba shilingi elufu kumi na tano nilipie taxi niliokua nayo.

(Mkaka kaingiza mkono mfukoni kutoa pesa lakini ghafla alipomuangalia mpenzi wake vizuri akashtuka!)

Mkaka: Unasema umekuja na Taxi? Mbona umejisahau umekuja na helmet ya Bodaboda?

Katika ukurasa huu, tuliokuandalia ni hayo tu lakini Kuna vichekesho vingi ndani ya The bestgalaxy ambayo unaweza furahia kuvisoma. Endelea kuwa karibu na sisi kwenye mambo mbalimbali tunayojihusisha nayo.

Stori za vichekesho vya kuvunja mbavu BONYEZA HAPA>>>

SMS za mafumbo ya Mapenzi kwa umpendae

Kama umezoea kumtumia sms za kawaida za mapenzi mwenza wako ni jambo zuri lakini tambua kuwa kuna sms za mafumbo za mapenzi ambazo ni nzuri pia kumtumia mtu unaempenda. Sms za mafumbo ya mapenzi ni sms ambazo nyingi ujumbe au maana ya sms huwa inajificha kidogo. Sms hizi  zanafanya mpenzi wako ahusishe ubongo wake kidogo kutambua maana sahihi ya kilicho maanishwa katika ujumbe wa mapenzi anao usoma.

Ni SMS nzuri sana kwa mpenzi na hapa The bestgalaxy tumekuandalia jumbe au SMS za mapenzi zilizochangamana na sms chache za mafumbo unayoweza kutumia kwa mapenzi wako. Kikubwa ukumbuke kuchagua sms inayoendana na hali yenu.

Sms za mafumbo ya mapenzi

  • Sioni ajabu Nzi kufia kwenye kidonda maana hata mimi najiona naweza kubari iwe hivyo nikipambania ninapopapenda. Milele nataka niwe kwako maana ni mahali nimependa.
  • Natamani ujue kuwa wewe ndie umenifanya niijue Radha halisi ya tunda la upendo. Sikuwahi fikilia kuwa siijui mpaka uliponipatia. Staki kukupoteza mpenzi, nimeridhika kuwa nawe, nataka kuendelea kufurahia.
  • Nilikua kila nikisikia simulizi juu ya watu waliopendana mpaka wakaamua kuanza kuishi pamoja, nawaza “wanapendana kiasi gani mpaka wanafikia mawazo hayo?”. Kwasasa nimewaelewa maana hali yangu kwako ni kama yao.
  • Nimezama kwenye penzi lako na staki mtu yoyote wa kuniopoa. Sipatishida, napata Raha. Hata nikitapatapa ni penzi tu limejaa. Sehemu nyingi nimepita ili kwako nije kukaa.
  • Siku Jua likichomoza jioni na kuzama asubuhi huenda labla ndio siku naweza kuwa nimebadilika kwako mpenzi wangu. Napo inaweza kuwa siko sawa. Lakini kama sio hivyo milele utakua wa muhimu kwangu kama pumzi. Nakupenda kipenzi.
  • Hata ungekua ni wewe; fikilia umekutana na mtu maishani anakupa furaha na anajua kujali pia. Mbali na mambo hayo, Bado moyo wako unampenda na hautaki uondoke maishani pia. Hivyo ndivyo jinsi ulivyo kwangu kwangu, Nakupenda my dear.
  • Penzi lako hunifanya ni hisi nipo juu sana. Ni Mbali linanifikisha tena ni zaidi ya usawa wa milima. Sijiwezi, nimeisha chizika sasa, napenda linako nipeleka na nampenda sana anaenipeleka.
  • Ukiziba vizuri masikio kwa mikono yako utagundua kelele zote pembeni hupotea na utulivu tu ndio hubakia. Hivyo ndio penzi letu linaweza kuwa endapo maneno ya watu tutayapuuzia. Nakupenda sana my love.
  • Umekuja kwangu kipindi ambacho nipo kwenye giza nene lakini umekuwa mwanga unaoangaza kila pande. Sasa sijui kitu gani unahisi kitafanya nisikupende? Tambua moyo wangu wote upo kwako na si kipande. Naomba usiniumize.
  • Nimekupatia moyo wangu kama zawadi yako kwa mapenzi matamu unayonipa. Naomba ushike taratibu mpenzi usije ukaniumiza.
  • Wewe ni lile ua ambalo limeota pekee kwaajili ya moyo wangu. Moyoni mwangu unahisi furaha nikikuwaza, nikikusikia na hata kukuona wewe. Pokea salamu Toka kwenye moyo wangu, unakupenda sana.

Unahitaji sms nyingine? Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy. Sms hizi ni moja ya sms nyingi ndani ya The bestgalaxy. Unaweza pitia kurasa nyingine za the bestgalaxy ili kupata mengine zaidi.

AI za kutengeneza picha kwa maneno (Akili bandia)

Inaweza kuwa sio mara ya kwanza kusikia neno “Akili bandia”. Akili bandia kwa kiingereza inaitwa AI na kirefu chake ni “Artificial intelligence”. Hii ni Teknolojia ambayo imeleta na inaendelea kuleta mabadiliko makubwa kwenye sehemu mbalimbali katika ulimwengu. Tumeisha zungumzia kuhusu hili kwenye makala za nyuma na hapa tunaenda kuangalia upande wa kutengeneza picha kwa kutengeneza AI.

AI ni nini na inamatokeo gani katika Ulimwengu? BONYEZA HAPA>>>


Kuna AI zenye uwezo wa kutengeneza/kuunda picha kulingana na maelezo yako tu ambayo huitwa “prompts”. Yani unaweza inambia AI ikutengenezee picha ya paka mweupe anaemkimbiza panya alafu AI ikaelewa ulichoeleza na kutengeneza picha inayoonesha tokio hilo. Maelezo yako ndio hufanya hizo AI zitoe picha au matokeo unayohitaji na AI nyingi hutaka uandike maelezo kwa kiingereza lakini kunanjia ya kulishinda hili ntakupa mwishoni. Kuna AI nyingine haziitaji utoemaelezo sana, unaweza zipa picha ya mfano alafu zikakutengenezea picha nyingine kama hiyo.


Kuna mambo mengi ya kuzungumzia kuhusu upande huu wa AI lakini tusipoteze muda, hebu tunangalie AI hizi za kutengeneza picha.

AI za kutengeneza picha kwa kuandika maneno (Akili bandia)

DALL-E 3

DALL-E 3 ni AI inayoweza badili maneno au maelezo inayopewa kuwa picha. Inauwezo mkubwa sana katika upande wa kutengeneza picha kwa maneno. Inaweza kutambua vizuri maelezo inayopewa na kutoa matokeo au picha zenye ubora wa hali ya juu ukilinganisha na baadhi ya huduma na model za Al nyingine.
DALL-E 3 imetengenezwa na kampuni ya OpenAI ambayo imetengeza Chatbot maalufu iitwayo ChatGPT. Ukihitaji kuitumia DALL-E 3 kwasasa utahitaji kujiunga na ChatGPT alafu ulipie “ChatGPT Plus” ambayo inaweza kukuchukua kama Tsh 49,000 kwa mwezi.

Jinsi ya kuongeza ubora wa picha zako za zamani kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Capilot image generator

Capilot ni AI inayomilikiwa na Microsoft na AI hii inajihusisha na kufanya mambo mengi ikiwemo kutengeneza/kuunda picha. Kuna kipingele cha Capilot kinakuruhusu mtumiji wake kutengeneza picha kwa kuandika maelezo ya picha anayohitaji. Kipengele hiki kimewezeshwa na DALL-3 ambayo tumeizungumzia hapo juu hivyo unaweza tumia hii badala ya DALL-3 moja kwa moja.
Microsoft waimeiweka Capilot image generator kama kipengele cha Bing search. Ukihitaji kuitumia Capilot image generator kirahisi na Bure unaweza ingia Bing kwenye kipengele cha Bing image generator ukaitumia kutengeneza picha bure. Unaweza tumia hata kiswahili katika kuelezea picha unayohitaji ila inaweza isilete matokeo mazuri.

Muonekano wa capilot image generator katika bing unapotengeneza picha.

Midjourney

Midjourney ni moja ya AI maarufu sana katika Ulimwengu wa content creation. AI hii haijihusishi na kutengeneza picha kwa maneno tu, inajihusisha mambo mengine yanayohusu kutengeneza content kama vile video. Kipindi cha nyuma kulikua na uwezekano wa kutumia midjourney Bure lakini kwasasa hakuna nafasi hiyo.
Ukitaka kuitumia kwa sasa utatakiwa kuingia kwenye tuvuti yao kujisajili na kuchagua kifurushi/plans kati ya vifurushi vyao visivyojumuisha “Bure”.

Adobe Firefly

Adobe imejikita katika AI pia na kwasasa unaweza tumia huduma zake nyingi zikiwa zimewezeshwa na AI. Kiufupi haijabaki nyumba katika Teknolojia ya akili bandia na katika picha inakuwezesha kutengeneza picha kwa maneno kupitia “Adobe Firefly”. Adobe Firefly ni moja ya AI nzuri katika kubadirisha maneno kuwa picha. Unaweza ielezea jinsi unavyo hitaji picha iwe na ikakuletea matokeo mazuri ya picha. Inaruhusu pia kuijaribu bila malipo kwenye tuvuti yao ila idadi picha utazo tengeneza bure zinakikomo kwa mwezi na alama ya “Adobe Firefly” itakuepo kwenye hizo picha. Ukihitaji kupata uhuru zaidi basi itabidi uhusishe malipo kwenye kupata huduma yao.

Fotor

Hii Fotor pia ni AI ambayo inaweza elewa maelezo unayoipa na ikakutengenezea picha kutokana na maelezo unayoipa. Ipo vizuri sana inatoa nafasi ya kuijaribu bila malipo ingawa kuna kikomo pia. Unapewa nafasi hiyo baada ya kufungua akaunti mpya kupitia app au tuvuti yao. Inasifika zaidi kwa kutengeneza picha za michoro au kuchora japo unaweza tumia kutengeneza picha za mitindo mingine pia.

Ni hizo tu tulizokuandalia hapa ila fahamu kuwa kuna nyingine nyingi nzuri. Tumeorodhesha hizi kwenye ukurasa huu kwakua ni katika ya AI hizo nzuri.

Kama kiingereza ni kinakushinda katika kuelezea picha unayohitaji, tumia translator kubadirisha maelezo yako ya kiswahili kwenda kiingereza alafu paste maelezo hayo ya kiingereza kwenye AI. Usiache kuendelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi.

Jinsi ya kutengeneza Pesa kwa AI za kuunda Picha BONYEZA HAPA>>>

Vitu vya kushangaza ambavyo hutokea ukimpenda mpenzi wako sana

Mahusiano ya mapenzi ni jambo la asili ambalo binadamu tunajihusisha nalo katika maisha yetu. Naweza sema mahusiano ya mapenzi ni jambo linaloweza fanya binadamu afurahie maisha yake. Ingawa kwa wengine wanaweza pitia maumivu kwenye maisha kwasababu ya mpenzi, lakini bado mahusiano ya mapenzi ni jambo la kumfurahisha katika maisha yake.

Ila hii haimaanishi kuwa ukiwa kwenye mahusiano yenye maumivu, haupo kwenye mahusiano sahihi kwenye maisha yako. Maumivu yanawezakua ni mapito tu katika mahusiano yako. Na mahusiano ya mapenzi ni zaidi ya kuishi mukiwa na raha au furaha ndio maana watu wanaopendana wanaapishwa kuendelea kuwa pamoja kwenye shida na Raha. Hapo hapo tena mahusiano yanaweza sababisha upate furaha na faraja kwenye shida.

Hapa the bestgalaxy leo tunaenda kuangalia mambo ya kushangaza ambayo watu husema yanawatokea wanapo mpenda sana mtu kwenye mahusiano. Bila kupoteza muda, hebu tuangalie mambo haya.

Vitu vya kushangaza ambavyo hutokea ukimpenda mpenzi wako sana

Unasukumwa kukutananae au kuongeanae bila sababu

Inasemekana ukimpenda mtu sana unaweza jikuta mara nyingi unatamani kuongea nae lakini hauna cha kuongea. Yani unaweza piga simu ili tu muongee na mpenzi wako au ukakutananae lakini jambo kuu la kufanya hivyo usilijue. Unakua ni msukumo tu usioelezaka unaotoka moyoni kutaka ufanaye hivyo bila sababu ya msingi ila upendo tu.

Unaweza waza mpenzi wako na akatokea mazingira uliopo

Kuna watu husema kwamba walikua kwenye mazingira falani wakiwaza kuhusu mpenzi wanaempenda alafu akatokea katika mazingira hayo. Linaweza kuwa ni jambo ambalo halimtokei kila mtu au mara kwa mara lakini baadhi ya watu wana sema wamewahi patwa na jambo hili kwa wapenzi wao wanaowapenda mara moja au zaidi. Wanasema unaweza kuwa katika mazingira kama sokoni ukamuwaza mpenzi wako alafu ghafla ukamuona anapita maeneo hayo.

Unaweza muita mtu jina lake

Kumuita mtu kwa jina la mpenzi wako unaempenda, nalo ni jambo la kushangaza. Kuna watu wengi wanakumbana na hili jambo wanapokua wamempenda sana mtu. Unaweza ukawa ni mwanaume au mwanamke mwenye mpenzi mwenye jina lililo kukaa kichwani sana mpaka unajisahau mara chache unawaita watu jina la lake kimakosa.

Ukiona dalili hizi ujue akaunti yako ya Facebook si salama BONYEZA HAPA>>>

Ukisikia jina lake moyo unadunda

Unaweza mpenda sana mtu kiasi ambacho moyo unakua ni kama umeshikana na jina la huyo unaempenda. Yani ukisikia tu jina la mpenzi wako kitu cha kwanza kukushtua kwenye mwili wako ni moyo. Moyo unaweza dunda pigo moja kuwa nguvu “Pah” baada ya jina hilo kuingia masikioni mwako. Wengine hata wakisoma tu jina la mpenzi huwa moyo hautulii.

Ni hayo tu katika ukurasa huu wa The bestgalaxy, Ni jambo gani kati ya haya limewahi kukutokea katika safari yako ya mahusiano? Watu wengi huona mambo haya wanapopenda mtu, hivyo kama umeyaona, hauko peke yako.

Sehemu za kuuza bidhaa zako zilizotumika Mtandaoni (Vitu used)

Unaweza kuwa hata sio mtu unaefanya bishara kama sehemu kuu ya kupata pesa lakini ukawa na vitu vyako unavyotamani kuuza. Vitu hivi vinaweza kuwa ni Simu yako ya zamani, PC, Tv, Redio na hata magari. Watu wengi wana vitu kama hivyo na wanatamani kuviuza lakini kwakua sio watu waliojikita kwenye bishara basi wanashindwa kupata sehemu ya kuviuza hivyo vitu na hata muda wa kufanya hivyo wanaweza kosa.


Teknolojia kupitia mtandao (internet), unamuwezesha kila mtu mwenye bidhaa anayotaka kuiuza akutane na watu wanaweza kununua bidhaa mtandaoni. Kupitia simu yako yenye uwezo wa internet au kifaa kingine cha internet, utaweza ukauza vitu vyako used kwa watu wengine. Njia ya kuuza vitu used kupitia mtandao, inaweza kuokoa muda wako muuzaji kwa kufanya kitu au bidhaa used unayouza ionekane kwa watu wengi wanaweza kuinunua huku ukiwa unaendelea na shudhuli zako nyingine.

Kwenye ukurasa huu, The bestgalaxy tumekuandalia orodha ya app chache zinazokuwezesha kuuza vitu used mtandaoni kupitia simu yako. Katika orodha hii, hatujaangalia upande wa Dunia, ila tumengalia katika upande wetu huu tu hivyo usishangae kutoziona platform kama eBay na Amazon.

Mambo ya kuzingatia unaponunua bidhaa mtandaoni (Online) BONYEZA HAPA>>>

App za kuuza bidhaa zako zilizotumika Mtandaoni (Vitu used)

Facebook

Kuna mtu anaweza jiuliza “Facebook inakujaje kwenye orodha ya app za kuuzia vitu used?” hebu tuanze na hili. Facebook inaingizwa kwenye orodha ya app za kuuzia vitu used kwasababu inakipengele kiitwacho “marketplace”. Kipengele cha Facebook marketplace kinakuruhusu mtumiaji wa Facebook kuuza na kununua bidhaa, ikiwemo used. Ukiwa na akaunti ya Facebook, utaweza kuweka picha na maelezo ya kitu unachouza pale alafu wanunuzi wakakutafuta kwaajili ya kununua. Zamani walikua wanaruhusu kuweka hadi namba ya simu lakini kwasasa hawaruhusu kwasababu za kiusalama.

Kupatana

Kupatana ni app rasmi kwaajili ya kuuza na kununua bidhaa mtandaoni. Mtu unaweza itumia kuuza vitu na pia unaweza itumia kununua vitu kutoka kwa wengine. Inatumika na watu wengi hivyo inaweza kuwa rahisi kumpata mnunuzi wa bidhaa yako used au kupata mtu anaeuza bidhaa unayohitaji. Inaruhusu kuweka picha na maelezo ya bidhaa yako ili anahitaji aelewe vizuri unachouza kabla hajakutafuta.

Jiji

Hii JiJi ni app nyingine kubwa ya kuuza na kununua bidhaa ambayo unaweza itumia kuuza vitu vyako used. Haina watumiaji wachache, wengi tu huuza na kununua vitu used kupitia app hii hivyo utakua sio mtu wa kwanza kuuza vitu used ndani yake. Ukiweka picha, maelezo ya bidhaa yako na mawasiliano yako vizuri, unaweza pata mnunuzi ndani ya app hii bila kupoteza muda sana maana watumiaji wapo wengi. Ni nzuri zaidi kwenye bidhaa za kielekroniki na magari alafu pia imepewa nyota 4.5 kati ya nyota 5 katika playstore.

Tisitano

Tisitano pia ni app kwaajili ya kuuza na kununua bidhaa. Inawakutanisha wauzaji wa vitu au bidhaa na wanunuzi wa vitu au bidhaa hizo. Inaweza tumika kuuza vitu vyako used kupitia simu yako ya mkononi bila kupoteza muda wako sana. Unaweza iweka bidhaa yako ndani ya app hii na ikaonwa na watu wengi kama app ya Kupatana au JiJi. Kuna maelfu ya watu huitumia app kwenye maswala ya kuuza na kununua vitu mtandaoni.

Mwisho, tunapenda kukukumbusha umakini unapouza na kununua bidhaa mtandaoni kupitia app hizi. Fahamu kuwa unaweza kutana na matapeli au watu wenye nia mbaya pia. Lakini hii isikuzuie kufurahia njia hii ya kuuza vitu used mtandaoni maana watu kama hawa wapo pia kwenye maisha yetu ya kila siku. Endelea kufuatilia The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi.

SMS za kumfanya mpenzi wako afurahi

Hapa kwenye ukurasa huu tunaenda tena kuangalia za sms za mapenzi unazoweza tumia kwa mpenzi wako. SMS tunazozingatia hapa ni kama ilivyoelezwa kwenye kichwa cha makala hii, yani tunaenda kuangalia sms zile zinazoweza mfurahisha mpenzi. Sio kila sms tutazoangalia hapa zinaweza mfurahisha mapenzi wako lakini kupitia orodha ya sms za mapenzi tulizoweka hapa chini unaweza pata sms nzuri inayoweza kumfurahisha mpenzi wako.

Usimtumie sms bila kufikilia kama ataipenda kwa jinsi unavyo mjua mweza wako. Kiufupi unatakiwa kuchagua sms kulingana na hali ya mahusiano yenu au hali ya mpenzi wako wakati unamtumia.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika tendo BONYEZA HAPA>>>

Sms za kufanya mpenzi wako afurahi

  • Asubuhi njema mpenzi wa moyo wangu! Kila siku ninapoanza na wewe, moyo wangu hujaa furaha na upendo siku nzima. Nakutakia siku yenye neema na mafanikio.
  • Leo ni siku ya kipekee kwa sababu nakupenda zaidi ya jana. Na usiwaze kuhusu kesho maana uko moyoni mwangu milele na kesho ntakupenda zaidi ya leo.
  • Ninapopitia picha zetu za pamoja, nakumbuka jinsi kila wakati tunavyopendana na kusaidiana. Kiukweli wewe ni nguzo yangu, na nakushukuru kwa kunifanya niwe na wewe maishani, Nakupenda sana.
  • Nakupenda sana Mpenzi wangu. Unanifanya nihisi nipo kwenye bahari ya mapenzi ambayo kuzama kwenye maji ni Raha na kuibuka raha. Unajua kunisafisha nakuwa mweupe, stamani kwenda kwengine nikachafuke.
  • Ningependa kushare nawe furaha yangu, maumivu yangu, na kila wakati wa maisha yangu. Kila ujumbe toka kwako hunijaza nguvu na matumaini. Nakupenda sana.
  • Hakuna neno la kutosha kueleza jinsi unavyonifanya nijisikie. Kila wakati ninaiona picha yako mbele yangu, moyo wangu unagonga kwa furaha kiwaza kuhusu wewe. Nakupenda sana mpenzi wangu, usije niacha mwenyewe.
  • Nashukuru kwa uwepo wako katika ulimwengu yangu. Umejaza moyo wangu furaha, upendo, na kufanya nitambue maana mapenzi ni nini. Kwangu maana ya mapenzi ni wewe. Nimeridhika kuwa nawe, Nakupenda.
  • Unaponikumbatia, nahisi niko salama na nina amani. Hakuna mahali pengine napendelea kuwa zaidi ya mikononi mwako. Nakupenda na nipo tayari kula kiapo.
  • Nimefurahi sana kuwa nawe katika kila hatua ninayoipiga maishani mwangu. Najua kwamba si kila changamoto tutayokutananayo maishani ni rahisi lakini siwezi yumba nikiwa na wewe kipenzi wangu.
  • Nakupenda sana na napenda vile umejua kunipa ninachotaka na naridhika nikikipata. Nitataka nini tena wakati penzi lako tamu nimenikamata? penzi lako ni hadimu, mbali na wewe siwezi pata.

Ni hayo tu, tuliokuandalia hapa Kwenye ukurasa huu. Usiache kufuatilia The bestgalaxy ili kujifunza mambo mengine yanayoweza kuwa muhimu kwako.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Jinsi ya kuongeza ubora wa picha zako za zamani kwenye simu

Unaweza piga picha yenye ubora kwenye simu yenye kamera nzuri lakini baada ya muda au kipindi flani ukawa na picha hiyo uliopiga ikiwa inaonekana haina ubora. Picha hiyo ya zamani unawezaona haina ubora baada ya kupitia kwenye mitandao ya kijamii na michakato mingine inayopunguza ubora wa picha. Mbali na hayo, baada ya kupata simu yenye kamera inayotoa picha zenye ubora zaidi, unaweza anza kuona picha ya zamani haina ubora.

Nikawaida watu kuwa na picha zao wanazoziona hazina ubora na kama ni mmoja watu hawa, hapa The bestgalaxy tunakupa mwanga kuhusu kuziongeza ubora. Unapokua na picha zisizo na ubora, kumbuka kuna huduma zinazokuwezesha kuongeza ubora wa picha. Huduma hizi ni software ambazo nyingi huiongezea picha ubora bila kukuhitaji ufanye vitu vingi. Zimewezeshwa na AI hivyo ni rahisi kutumia kiasi ambacho mtu yoyote anaweza tumia kuongeza ubora wa picha zake.

AI ni nini na inaleta matokeo gani katika Ulimwengu? BONYEZA HAPA>>>>

Jinsi ya kuongeza ubora wa picha zako za zamani kwenye simu za Android

Kwenye simu za Andoid kupata huduma ya kuongeza ubora wa picha, unaweza tumia app iitwayo UpFoto. App hii inatumia internet ila inaweza pandisha ubora wa picha yako bure na rahisi sana kuitumia. Ukihitaji kujaribu kwenye picha zako zilizopoteza ubora, fuata maelezo yafuatayo;

 

  • Nenda katika Playstore na uipakue app iitwayo UpFoto kwenye simu yako.
  • Fungua, chagua Lugha ya “English” alafu bonyeza “Start” kwenye ukurasa utaopelekwa.
  • Baada ya hapo bonyeza kitufe cha “Try now” kwenye sehemu ilioandikwa “Enhance” kisha uchague picha unayotaka kuiboresha.
  • Baada ya kuchagua, Bonyeza kitufe kilicho andikwa “Enhance” ili kuanzisha mchakato wa kuboresha hiyo picha.  
  • App ikimaliza mchakato, utaletewa picha ilioboreshwa alafu utatakiwa kubonyeza kitufe kilichoandikwa “Save” ili kuiweka picha hiyo kwenye simu yako.

Kwa kufanya hayo utakua umefanikiwa. Lakini unapaswa kujua kwamba app ya UpFoto inamatangazo ambayo utakua unakutana nayo katika kufuata hatua hizo. Mbali na matangazo, app hii itakuomba access chache kwenye simu yako na utakua unabonyeza “Allow” kuiruhusu.

Kama ubora utakua haujakulidhisha unaweza chukua picha iliotoka kwenye app hiyo, alafu ukairudisha kwenye app kuiongeza ubora kwa mara ya pili.

Dalili za kuwa mpenzi wako anakupendea pesa tu




Hapa tunaenda kuangalia viashiria au dalili za kuwa mpenzi wako anakupendea pesa. Kuna jinsi pesa inaumuhimu kwenye mahusiano ya mapenzi ya sasa na hii sio kwenye mahusiano, ni maisha kiujumla. Hata watu wa jinsia tofauti mukiamua kuwa pamoja tu kwa kushirikiana bila kuwa wapenzi bado kuna jinsi maisha yatahitaji pesa kutokana na mahitaji mulionayo kama binadamu wa dunia hii ya sasa. Hivyo pesa sio kitu kibaya au kitu cha ajambu kwenye mahusianio ya mapenzi. Lakini kitu hatari kwenye mahusiano ni kuwa kwenye mahusiano na mtu asiekupenda wewe ila anaigiza kukupenda ili apate au kufurahia pesa zako tu. Hii ni hatari maana baada ya muda au baada ya pesa kuyumba, mtu aliependa kweli anaweza anza kuumizwa.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika tendo BONYEZA HAPA>>>

Dalili za kuwa mpenzi wako anakupendea pesa tu

Kila nyuma ya jambo la upendo ni pesa




Mtu asiekupenda wewe lakini anapenda pesa zako anaweza kuwa anatumia upendo wa kuigiza kupata pesa. Unaweza tanguliza kitu kinachoonesha anakupenda lakini hapo hapo unagundua lengo la yote ni kupata pesa toka kwako. Anaweza kuwa mgomvi na hakupigii simu wala kukutafuta lakini siku akitulia na akikutafuta ni siku ambayo anashida au anahitaji pesa toka kwako.

Vitu vya kushangaza ambavyo hutokea ukimpenda mpenzi wako sana BONYEZA HAPA>>>

Usipo husisha pesa hakuzingatii kwa chochote




Pia mtu asiekupenda anaweza kuwa na tabia ya kukupuuza unaposema hauna pesa . Yani mahusiano yako na yeye yanaweza fikia wakati unaona kabisa unapotoa pesa, anakuonesha upendo lakini usipotoa anakasirika na kukupuuza kabisa kiasi ambacho upendo wake kwako unakua haupo. Kiufupi pesa ndio inakua kitu pekee kinachofanya akuzingatie na kukwambia anakupenda. Usipompatia anatafuta kila sababu ya kukasirika, kutokukutafuta na kukufanya ujione umemkosea sana.

Hatoi au kutumia pesa zake kwenye matatizo yako



Yani hata iwe unaumwa au umepata tazizo linalomuhitaji yeye aje kwa nauli au anunue kitu kawaajili yako bado atakuhusisha kwenye pesa atazotumia. Kiufupi anataka ulipie kila kitu anachokifanya kwaajili yako. Unaweza pata shida inayohitaji aje kwako au aende sehemu lakini akiambiwa anaweza kujibu “Sina nauli, nitumie”. Hawezi tumia pesa yake kwenye jambo lako hata iweje, atakuomba pesa tu.

Hajali kuhusu muelekeo wako au mahusiano yenu


Unaweza fanya maamuzi mabaya kuhusu pesa mbele yake na asikwambie kitu kuhusu maamuzi hayo. Hana wivu na wewe kwenye mahusiano unapoonekana na watu wengine, kikubwa kwake ni kumpa pesa tu. Mipango ya mbele ya pamoja kuhusu mahusiano huwa haileti na hata ukiileta haonekani kuona inamaana sana kwake. Anaweza kuwa na matumizi ya pesa mengi sana yasio husisha kujenga familia au maisha ya pamoja.



Pamoja na kuyaona mambo hayo yote kwa mwanaume au mwanaumke unaehisi anakupendea pesa inaweza kuwa haimaanishi kwa asilimia 100 yupo hivyo. Hivyo ni viashiria tu ambavyo ukiviona, itabidi uchanganye na mawazo yako kuchanganua kuwa mwanamke au mwanaume ulienae anakupendea pesa au upendo wake ni wakweli.

Game nzuri za PSP za kucheza kwenye Simu na PC

Kampuni ya Sony ni kampuni kubwa sana katika upande wa games kutokana na sababu nyingi ikiwemo kuleta vifaa vya games vyenye mafanikio makubwa ulimwenguni. Katika Miaka ya nyuma Sony ilitengeneza kifaa kidogo cha mkononi kiitwacho PSP (PlayStation Portable) kama moja ya vifaa vya games ambacho kinamuwezesha mtu kucheza games popote kama vile inavyotumika simu siku hizi. Hii PSP ilitolewa rasmi na Sony mwaka 2005 na ilikua ni bidhaa iliopokelewa vizuri sana na watu.

Kulikua kuna magemu/gemes kama 1900 hivi na zaidi ambayo mtu ukinunua PSP, unaweza kuyacheza. Lakini Baada ya muda Sony walitangaza kusitisha projekti yao ya PSP. Baada ya Sony kufanya hivyo Games za PSP na vifaa vya PSP vikaacha kuzalishwa mpaka leo. Lakini kutokana na ubora wa vifaa vya PSP na game zake kwa kipindi kile, watu mpaka sasa hawajaisahau PSP. Kuna watu mpaka sasa wana vifaa vya PSP, wengine wanaiga kutengeneza vifaa vya PSP na wengine wametafuta njia ya kuyacheza magemu ya PSP kwenye PC na Simu.

Ukitaka kucheza magame ya PSP kwenye simu au PC, utahitajika kutumia app au software ziitwazo Emulators. Moja ya Emulators za magame ya psp zinazotumika sana inaitwa “PPSPPP PSP Emulator“. Hii inafanya mpaka baadhi ya watu kuyafahamu magame ya PSP kama “Magame ya PPSPP”.

Magame ya mpira ya kucheza kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Game nzuri za psp za kucheza kwenye simu au PC

GTA Liberty City Stories

GTA Liberty City Stories psp

Liberty City Stories ni sehemu ya mfululizo maarufu wa magame ya Grand Theft Auto ambayo yapo chini ya Rockstar. Game hili katika upande wa PSP, ni kati ya game zuri sana kucheza katika PC na Simu pia. Unapo cheza game hili unacheza kama jamaa mmoja muhuni au muhalifu aitwae Toni Cipriani, ambaye anarudi mjini baada ya kukaa mbali kwa muda. Unaingia katika ulimwengu wa uhalifu wa Liberty City na kupambana kuwa juu katika mji huo.

God of War chain of Olympus

God of War chain of Olympus PSP

Game hili pia ni mfululizo wa magame ya God of War ambayo ni maarufu pia kwenye ulimwengu wa games. Humu unacheza kama Kratos ukipigana na miungu pamoja kutatua changamoto mbali kwa mtiririko wa simulizi ya God of War. Liliundwa SCE Santa Monica Studio na kuchapishwa na Sony Computer Entertainment kwaajili ya vifaa vya PSP. Ni game la PSP zuri kulicheza mpaka sasa.

Assassin’s Creed bloodlines

Assassin’s Creed bloodlines

Assassin’s Creed: Bloodlines katika psp ni game ambalo ambao lilitoka mwaka 2009. Magemu ya Assassin’s Creed yapo mengi katika ulimwengu wa games na hili ni moja kati ya hayo. Katika Assassin’s Creed bloodlines hili unacheza kama mtu aitwae Altair Ibn-La’Ahad. Huyo ni muhusika mkuu katika game na yupo katika miji ya Kilatini wakati wa karne ya 12(Zamani). Game la Assassin’s Creed bloodlines bado linaweza kuwa chaguo zuri mpaka sasa unahitaji kucheza game za psp maana sina stori nzuri na muonekano mzuri pia.

NFS most wanted

Need For Speed Most wanted

Ukiwa unapenda magame ya magari na unataka kufurahia game hizi upande wa PSP, game NFS most wanted linaweza kuwa zuri kwako. Game hili linaitwa “Need For Speed Most” wanted lakini unaweza liita “NFS most wanted” kwa ufupi. Need For Speed ni moja majina makubwa kwenye video games na hili game tunaloliongelea hapa, lina jina hili Kwasababu ni sehemu ya game za Need For Speed. Lilichapishwa na Electronic Arts Katika PSP na unaweza furahia mpaka sasa maana bado lipo vizuri.

Spider man 3

Spider man 3 PSP

Hili game la Spider man 3 la PSP la Spider-Man 3 ni sehemu ya mfululizo wa magame ya Spider-Man. Kuna magemu mengi ya spider man na hili ni moja ya magemu hayo lilichapichwa kwaajili ya PSP ambalo linafurahisha mpaka sasa. Humu ndani ukiwa kama spider man utapambana na maadui kama Sandman, Venom, na New Goblin.

Hapo juu tumeweka games chache TU lakini games za psp zipo nyingi sana nzuri mbali na hizo. Lakini unapaswa kujua games za psp zilisimama kutolewa hivyo hakuna games mpya za psp ambazo ni rasmi. Ila u aweza kutana na game za zamani za psp zilizo boreshwa lakini sio rasmi. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo kuhusu games na mengine.

Jinsi ya kuachana na mtu asiyekupenda

Mapenzi au mahusiano yana mambo mengi sana ya kufurahisha na kuumiza pia. Kupenda usipo pendwa ni moja ya jambo la maumivu sana katika mapenzi. Jambo hili kama haujawahi pitia, basi unaweza kuwa umewahi ona kwenye filamu au kwa mtu mwingine wa karibu yako. Ni jambo linaloumiza sana na huwa linamuumiza aliependa tu, asiependa huwa haumii maana moyo yake unakua hauhisi au kujali chochote.

Ikiwa upo kwenye hali ya kumpenda mtu asiekupenda inaweza fikia wakati akakuelewa na kuanza kukupenda pia. Hivyo usiwe mwepesi sana wa kukata tamaa.
Ila ukiona hakuna dalili nzuri za kukugeukia na kukupenda, kuachana nae ni uamuzi mzuri pia maana maumivu ya mapenzi yakizidi sio mazuri. Ni rahisi sana kumfanya mtu anaekupenda, akuchukie kuliko kumfanya mtu asiyekupenda, akupende. Kuna watu hupata magonjwa na hata kupoteza maisha kutokana na maumivu wanayopata katika kulazimisha kupendwa wasipopedwa. Kama utapenda, unaweza fuata hatua zifuatazo katika kuachana na mtu asiyekupenda kabisa.

Mambo ya kuepuka baada ya kuachana na Mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Hatua za kuachana na mtu asiyekupenda

Kuwa muwazi kwake

Moyo wako unaweza kuwa unakusukuma kusema Mambo mengi sana kuhusu pendo wako kwake. Unapotaka kuachana nae, ni vema ukaufungua moyo wako kwake kwa kusema Mambo yote unayotamani ajue. Tua Kila kitu kilichokua moyoni mwako ili moyo wako na akili yako iwe huru pindi utakapokua umemgeuzia mgongo. Unaweza fanya hivi kwenye simu lakini itakua vizuri zaidi kama mtaonana kabisa na kufanya mazungumzo. Kama ni mwanaume au mwanamke, kuwa huru kumwambia vitu ambavyo badae havita uvuta moyo na kukusumbua kuwa huku mwambia. Mwambie jinsi gani unapenda, unatamani aweje kwako na ikiwezekana mwambie na anakupa shida kiasi gani.

Kumbuka thamani yako

Kumpenda mtu kunaweza kusahaulisha thamani yako. Ukiwa unalazimisha sana kupendwa usipopendwa, kunajinsi unaweza jihisi hauna thamani. Lakini ukweli ni kwamba, thamani hua inakua pale pale. kila mtu ana thamani hapa Duniani haijalishi unapendwa au haupendwi. Kikubwa ukumbuke au utambue thamani yako tu alafu baada ya hapo unaweza anza kujiamini kwenye mambo yako na maamuzi yako.

Zingatia vitu vingine na kujiweka mbali nae

Kumzingatia mwanamke au mwanaume alietambua upendo wako kunaweza kukuyumbisha hata kimaisha au kiuchumi bila kukuletea faida yoyote mwishoni. Ni vema ukaanza kuzingatia vitu vingine vinavyoweza rahisiha maisha yako au kukuletea faida mwishoni. Wekeza muda wako kwenye kujifunza vitu vipya, kufanya mazoezi au kazi. Wakati ukifanya hayo hakikisha unajiweka mbali na mtu asiyekupenda.

Jipe muda wa kusahau

Tambua kuwa maumivu ya kumuacha mtu unaempenda hayawezi kuisha katika siku moja au mbili. Yanaweza kuchukua muda mrefu kidogo na ili uweze kufikia hatua ya kuto kuumia. Unapaswa kukubaliana na kila kitu alafu ujipe muda wa kusahau. Pamoja na maumivu unavyoweza pitia unapaswa pia kujikumbusha kuwa “Maumivu yote yataisha,utakua vizuri na utapenda mtu mwingine”. Kunasiku unaweza fanikiwa kumtoa moyoni au kupunguza maumivu aliokupatia.

Wakati unajipa muda wa kusahau usisahau kufuahi, fanya vitu salama vinavyokupa furaha huku ukipanga mipango mipya ya siku zijazo.