Category Archives: Uncategorized

Sms za kumwambia mpenzi wako kuwa unampenda

SMS inaweza kuwa njia nzuri ya kueleza hisia za upendo na mapenzi kwa mwanamke au mwanaume umpendae. Sms kama sms zinamchango mkubwa katika mahusiano ya sasa maana ndio mara nyingi huunganisha wapenzi wakiwa mbali.

Katika makala hii, tumekuangalia jumbe mbalimbali za SMS ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako kumwambia kuwa unampenda. Kuonyesha upendo kupitia maneno kunaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha uhusiano na kuongeza ukaribu kati yenu. Kunaweza mkumbusha jinsi gani unampenda na unahitaji.

Kwenye mahusiano ya mapenzi, maneno ni kitu kikubwa sana. Maneno yanaweza yumbisha mapenzi na hata kuyaweka sawa pia. Soto tunajua kwamba wakati mwingine mnaweza kuwa kwenye mahusiano lakini yakawa yanayumba. Kumwambia maneno mpenzi wako ya jinsi gani unampenda kunaweza mkumbusha mpenzi wako kushikamana na kuwa pamoja kwenye mahusiano. Na pia kuna muda mpenzi anaweza kuwa na kiu ya maneno mazuri toka kwako lakini akashindwa kusema maana na yeye haelewi.

SMS za kumsifia mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Sms za kumwambia mpenzi mwanamke/mwanaume unampenda

  • Yule mtu anaeweza ufurahisha au kuuvunja moyo wangu ni wewe. Kuwa nawe ni furaha ya moyo wangu, sitamani kuwa mbali na wewe.
  • Kama kukupenda ni ujinga basi nakubari kuwa hivyo. Penzi lako limeushika moyo wangu mpaka naogopa. Ukiona chozi langu la maumivu ya mapenzi limenidondoka jua ni wewe. Na ikitokea hivyo naomba usije sahau kuwa hata wakulifuta pia ni wewe. Nakupenda sana.
  • Nakupenda Toka moyoni, Ukaribu wako huichemsha damu. Kuwa na Wewe ni Ndoto yangu tamu, staki kukatishwa mpenzi maana hainiishi hamu.
  • Penzi lako limenipeleka kwenye ulimwengu wa mapenzi ambao sikuwahi jua upo. Unanipa Raha, nakua na furaha kama mtoto.
  • Zawadi kubwa ninayotamani kuendelea kupata toka kwako ni upendo wako. Moyo wangu umeisha lidhia kuwa na wewe maishani, na wewe ukibadilika tu, jua unaniumiza mwanzako.
  • Duniani karibu kila mtu ana anae mpenda kwa dhati toka moyoni na yupo akili kila mara. Katika Maisha yangu mtu huyo ni wewe!
  • Wanaweza kuwa wamekwambia au umesikia maneno mengi kuhusu mimi. Ila naomba upuuze na usikilize moyo wangu unasema nini sasaivi. Moyo wangu usema unakupenda wewe!
  • Nimekua nikipenda kuangalia vitu vizuri na vyakupendeza ili nifurahi. Tangu nilipokutia machoni sina haja ya kuangalia chochote kizuri mbali na wewe ili nifurahi. Macho na kila kitu toka kwako hunivutia.
  • Ninapomaliza kuongea na wewe kwenye simu hua nakata simu lakini natamani kuendelea kuisikia sauti yako tena. Sijawahi kuichoka sauti yako maana ni faraja ya moyo wangu. Nakupenda sana.
  • Sijawahi jihisi mpweke nikiwa karibu na wewe mpenzi. Naweza umia kwa kupoteza vingi maishani ila nitaumia zaidi nikikupoteza wewe kipenzi. Maana nanipa sababu ya kufurahia maisha.
  • Moyo wangu hupitia mambo mengi maishani. Lakini dawa yake kila mara huwa ni wewe. Unajua jua kuugusa bila kuushika. Unagusa sehemu wajinga hawawezi fika. Nitakupenda mpaka mwisho wa Maisha.
  • Siri ya furaha yangu ni kuwa na wewe. Najiona wa thamani kwasababu yako. Moyo wangu umenitoraka, upo kwako. Umeuvuta kwa Raha za penzi lako. Nakupenda sana Mpenzi.

SMS hizi ni nzuri kwako? Kama ni nzuri unaweza tumia Bure kwa unaempenda. Usisahau kuangalia sms nyingine za mapenzi ndani ya The bestgalaxy na useache kuifuatilia pia. Asante sana kwa muda wako ulioutoa kusoma makala hii.

Akili Bandia: Fahamu kuhusu AI kuchukua Ajira za watu

Teknolojia ya akili bandia (AI) imekuwa inaleta mabadiliko kwenye pande nyingi duniani, na suala la AI kuchukua ajira za watu limezua mjadala mkubwa miongoni mwa watu. Kuna watu wengi wanahofia kwamba AI itasababisha watu wengi kupoteza kazi. Swala hili limeongelewa na watu wengi sana lakini pamoja na yote, Teknolojia ya AI inaonekana haiwezi ondolewa Duniani kwa sasa.
Teknolojia hii inaendelea kuboreshwa kila siku na inaingizwa kwenye pande mbali mbali zinazohusu maisha ya binadamu. Na inasemekana kuwa Teknolojia ya AI haitaondoka, itaendelea kuwepo tu hapa Duniani.

AI ni nini na inaleta matokeo gani katika Ulimwengu BONYEZA HAPA>>>


Hapa The bestgalaxy, tunaenda kujalibu kuchimba kidogo juu ya swala hili ili kukujuza kiundani kuhusu AI na ajira za watu. Tumefanya hivi ili kutoa mwanga kwa watu wasiolielewa swala hili vizuri.

Fahamu kuhusu AI kuchukua Ajira za watu


Ni kweli AI inachukua Ajira za watu?

Kuna vitu au Mashine zinazotumia AI zina uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na haraka kuliko au kama binadamu. Kadri siku zinavyo zidi kwenda, Teknolojia ya AI inakua Bora na kufanya vitu au Mashine hizo kuongezeka idadi na kuwa bora pia.
Kuna Makampuni huvutiwa na vitu au Mashine za Teknolojia ya AI na kuanza kuzitumia badala ya kuajili binadamu. Swala hili hufanywa ili waepuke gharama za kuwalipa watu na pia hufanya mambo yao yaende haraka kuliko ambavyo wangetumia binadamu. Kwa maelezo mengine hapa tunaweza sema AI inachukua Ajira za watu.

Inasemekana kuwa asilimia 60 ya kazi au Ajira zinaweza chukuliwa na AI. Na swala ya AI kuchukua Ajira ni jambo ambalo linaongelewa kwa uwazi kabisa hata na AI zenyewe.

Watu wanatakiwa kufanya nini?


Watu wanapaswa kuelewa kwanza AI itaendelea kuwepo na kuleta matokeo mengi kwenye maisha ya binadamu ikiwemo upande huu wa Ajira au kazi. Lakini kitu cha muhimu ni kuondoa hofu kisha kujifunza mambo ya AI ili kujua upande wako utaathiriwa vipi kwasasa au miaka ijayo.


Mtu unashauriwa pia kuiweka akili yako sawa na kuwa tayari kujifunza vitu vipya au ujuzi. Katika vitu unavyotakiwa kujifunza ni kuitumia AI maana AI inaweza tumika na mtu yoyote kufanya mambo ya maana yatakayokuingizia kipato pia au kuiboresha kazi hiyo hiyo unayoifanya. Kiufupi kitu kimoja cha AI kinaweza chukua ajira ya mtu alafu hapo hapo kitu kingine cha AI kinaweza kuwa kimerahisisha au kuzalisha kazi nyingine ambayo mtu huyo anaweza ifanya. Kuijuia hiyo kazi au fulsa itakuitaji kufungua akili yako kwenye ujuzi mpya. Na hii ndio sababu ya The bestgalaxy kusikiliza watu kufuatilia AI.

Jinsi ya kuwa mtu wa thamani kwa mpenzi wako

Karibu kila mtu anatamani kuwa mtu wa thamani kwa mpenzi wake. Katika makala hii, tutaorodhesha mambo muhimu yanayoweza msaidia mtu kuwa mpenzi bora na kuongeza thamani katika uhusiano. Unaweza fanya mambo ya kwenye makala hii ili kumfanya mpenzi wako anaekupenda akupende zaidi. Lakini pia Mahusiano ya mapenzi yakiwa hayapo sawa na unaona thamani yako kwa mpenzi wako imeshuka, unaweza jaribu mambo ya kwenye makala hii.

Ikiwa unataka kujua jinsi ya kuwa mtu wa thamani zaidi kwa mpenzi wako, endelea kusoma makala hii mpaka mwisho. Lakini tambua kuwa kupambana kuwa mtu wa thamani kwa mtu asiyekupenda kunaweza pelekea kuumizwa na kujishusha thamani yako pia. Kwaiyo ni vema kutotumia nguvu kubwa kutaka kuwa mtu wa thamani kwa mtu asiekupenda. Kuna muda mtu huvipa thamani vitu anavyo vipenda.

Sms za kumsifia mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Fanya haya kuwa mtu wa thamani kwa mpenzi wako

Kuwa upande wake na msaada kwenye matatizo au shida zake

Watu wa thamani sana katika Maisha ni watu wanaokua upande wako unapokua na shida. Watu wengi hukimbia linapokuja swala la shida na wanaobaki hua ni watu wa thamani sana katika Maisha. Sasa kama unataka kuwa mtu wa thamani kwa mpenzi wako, unaweza fanya hivyo kwakua na tabia ya kuwa upande wake na msaada kwenye matatizo au shida.
Unaweza kumsaidia ushauri au pesa kidogo kwenye matatizo au shida na akakuona wa thamani sana.

Kuwa muaminifu katika Mahusiano

Watu wengi hua wanatamani kuwa na wapenzi waaminifu kwenye mahusiano ili mioyo yao iwe na amani. Ukikutana na watu hawa ambao ni waaminifu na ukawa muaminifu kwao, unaweza kuwa mtu wa thamani sana. Uaminifu hutuliza moyo wa mpendwa wako na kufanya afurahie mapenzi kwa amani.

Weka nae malengo ya wazi

Watu wengi huona mtu wa thamani kwenye mahusiano ni yule mwenye malengo ya kuwa pamoja maishani. Ukiwa mtu unaeyaweka wazi malengo ya kuwa pamoja nae kwa mpenzi wako, utakua na thamani tofauti na watu wengine kwenye maisha yake. Ukifanya hivi kama mpenzi wako ana mapenzi ya dhati, anawezakuona unamalengo ya kuwa nae maishani na sio kumpotezea muda. Hii inaweza pelekea akuone wathamani sana kwenye maisha yake akiwa mwanamke au mwanaume.


Ni hayo tu katika ukurasa huu, The bestgalaxy tumekuandalia machache haya lakini Kuna mengi unaweza jifunza kupitia sisi. Kikubwa usiache kufuatilia The bestgalaxy.

Michezo ya kuchati na Mpenzi wako kurefusha maongezi BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kujua kuhusu kutengeneza pesa mtandaoni

Watu wengi wasio na uelewa sana kuhusu mitandao wakisikia kutengeneza pesa mtandaoni huwa wanavutiwa sana na kutaka kujua kiundani. Wengine hawaishii kuvutiwa tu, hujaribu mambo mbalimbali yanayosemwa kuwa ni kutenge ngeneza pesa mtandoni au kumake money online.

Katika kujaribu, kunawatu huangukia kwa matapeli au kukutana vitu vingine vibaya wasivyo tarajia. Watu kukumbana na mambo hayo, bado hakumaanishi kutengeneza pesa online au mtandaoni, haiwezekani. Jambo hilo linawezekana kwa asilimia 100 ila kabla ya kujikita mtandaoni kwaajili ya kutengeneza pesa, fahamu mambo yafuatayo.

Jinsi ya kutengeneza Pesa kwa AI za kuunda Picha BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kujua kuhusu kutengeneza pesa mtandaoni

Sio rahisi kama inavyoonekana

Kutengeneza pesa mtanaoni sio rahisi kama ambayo mtu anaweza kukuelezea. Njia nyingi za kutengeneza pesa hukuhitaji ufanye kazi ambayo itakuletea hizo pesa unazohitaji. Kazi hizo zinaweza kuonekana rahisi kwasababu hazikutoi jasho lakini ni ngumu kichwani na zinaweza chukua muda wako pia bila kukupa matokeo uliotarajia. Uzoefu na elimu ya kitu unachokifanya inawezakukusaidia lakini bado sio rahisi kama wengi wanavyofikilia. Hakuna batani utayooneshwa mtandandaoni ambayo ukiibonyeza itatoa pesa “praaah!”, mara nyingi unahitajika ufanye kazi ndipo upate pesa.

Kuna matapeli

Ulimwengu wa mtandaoni haupo salama kwa asilimia 100 hivyo unatakiwa kuwa makini. Kuna matapeli wanaweza kutapeli pesa kwa kukudanganya kuhusu kutengeneza pesa. Mbali na pesa mtu unaweza potezewa muda na hata kuibiwa. Unapaswa kuwa makini sana ili usiingie kwenye mikono ya watu wabaya.

Uchaguzi wa njia unayoifurahia ni muhimu

Kunanjia zaidi ya moja za kutengeneza pesa mtandaoni unazoweza tumia lakini ni vema kuchagua kuanza na njia unayoifurahia. Njia nyingi huwa ni ngumu na huchukua muda kuleta matokeo lakini ukichangua njia unayoipenda unaweza usione ugumu kukimbiza ndoto yako.

Asente kwa kuchukua muda wako kusoma mambo hayo machache. Kama ni mmoja wa watu wanaokimbiza ndoto zao online, nakutakia heri na mafanikio. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Game zenye muonekano mzuri za Online battle Royale (simu)

Unatafuta magame mazuri ya kucheza? Hii ni moja ya makala usizotakiwa kukosa unapotaka magame ya kucheza kwenye simu. Kabla ya yote ningependa kukufahamisha hapa tunaenda kuangalia game nzuri zenye muonekano mzuri lakini game hizi ni game za Online battle loyale. Duniani kwasasa watu wengi hupenda kucheza game hizi kwa sasababu ni games zinazo jumuisha kushindana au kushirikiana na watu toka sehemu mbalimbali ulimwenguni.


Magame ya muundo huu husaidia watu kufahamiana au kupata marafiki. Kuna game za battle royal ukizicheza kwa muda wa saa moja unaweza kuwa umekutana na watu zaidi ya ishirini toka sehemu mbali za Dunia. Watu hao unaokutanana nao wanaweza kuwa marafiki zako japo haushauriwi sana kujenga urafiki na watu usio wajua tabia zao. Kuna watu huwa na tabia mbaya ambazo zinaweza kuwa ni wizi au utapeli mtandaoni, hivyo unatakiwa kuwa makini na watu unaokutana nao kwenye online games.

Game za mpira za kucheza kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Magame mazuri ya Battle Royale ya kucheza kwenye simu (Android na iOS)

Call of duty Warzone Mobile

Warzone Mobile ni moja games maarufu katika upande wa games za “Battle royale”. Game hili ni game la kivita ambalo ni FPS, yaani ni first person shooter ambalo lipo chini ya Activation kama games nyingine za Call of duty. Call of Duty: Warzone, ulioundwa kwa ajili ya vifaa vya simu na kutolewa mwaka 2024. Kabla ya hapo lilikua lipo lakini halikutolewa kwaajili ya simu.
Kwenye battle royal ya call of duty warzone Mobile mtu kwanza unafurahia graphics au muonekano mzuri. Mbali na Hilo Kuna mode zaidi ya moja unazoweza kuzifurahia.

Mambo ya kujua kuhusu game la Call of Duty warzone mobile BONYEZA HAPA>>>

PUBG mobile

PUBG mobile ni game lingine zuri katika upande wa battle royal. PUBG ni Third person shooter na vile vile ni First-Person Shooter. Ukitaka muonekano mzuri PUBG mobile ni chaguo sahihi lakini utatakiwa kujua kuwa Kuna “PUBG lite” ambayo hua ni game la PUBG lililopunguzwa ubora kwaajili ya simu zenye uwezo mdogo na kupunguza matumizi ya data. Ukitaka kufurahia ubora wa game la PUBG kwa asilimia 100, tumia PUBG mobile na sio PUBG lite.

Call of duty Mobile

Call of duty Mobile ni game lingine la Call of Duty lililoundwa kwaajili ya simu. Game hili lilikuepo kabla ya game la “Call of Duty warzone Mobile” halijatolewa kwaajili ya simu. Linawachezaji wengi na kitu kizuri ni kwamba linaweza chezwa kwenye simu zenye uwezo mdogo kidogo ukilinganisha ya Call of Duty warzone. Muonekano wake upo vizuri na katika modes lina mpaka mode ya zombies unayoweza furahia kucheza na marafiki.

Fortnite

Fortnite Mobile ni toleo la game maarufu la ” Fortnite battle royale” lililoundwa na Epic Games kwajili ya watu wanaotumia simu kucheza games. Game hili lilipititia matatizo ambayo huenda yangefanya game hili liwe limesahulika kwasasa lakini kutokana na ubora na kuwa game zuri mpaka Leo hawazisahau. Tatizo ambalo game la Fortnite battle royal mobile lilipitia ni kuondolewa kwenye platform kubwa ya Playstore. Jambo hili lilileta ugumu kwenye upatikanaji wa game hili kwenye simu.

Jinsi ya kucheza game la Fortnite kwenye simu bila kudownload BONYEZA HAPA>>>

Free Fire


Free Fire ni game la simu la aina ya “battle royale” lililotengenezwa na Garena. Katika game hili, wachezaji wanarushwa kwenye kisiwa ambapo wanapaswa kupambana na wachezaji wengine hadi awepo mshindi atakae simama hai. Hii ni kama battle royal za game nyingine ila lina mazuri yake tofauti. Free Fire ni game maalufu ulimwenguni na hukubali kuchezwa kwenye simu zenye uwezo mdogo kidogo ukilinganisha na baadhi ya game nyingine kubwa za battle royal.

Huo ndio mwisho wa orodha yetu katika ukurasa huu. Kama imekua msaada kwako, unaweza wajuza na rafiki zako juu game hizi. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Jinsi ya kujua mpenzi ulienae anakupotezea muda

Katika safari ya mapenzi, ni muhimu kujua kama mpenzi ulienae anakufaa kwa muda mrefu au anakupotezea muda. Wengi tunajua mahusiano ya mapenzi yanaweza anza popote na yanapoelekea inabidi yawe ni mahusiano ya kuwa pamoja katika Maisha. Hata dini huwa zinasimamia juu ya hili ndio maana watu wanaopendana kidini wanatakiwa waingie katika ndoa na kuishi pamoja.


Katika kutafuta mpenzi ambae utakua nae kwenye maisha, unaweza kutana na watu wengi, ukaingia nao kwenye mahusiano na musifanikiwe kuwa pamoja maishani. Endapo utatumia muda mrefu kuwa na mtu au mpenzi ambae hawazi kuwa nawewe maishani unaweza jilaumu baadae kwa kupotezewa muda. Jambo hili ni baya kwa mwanamke na hata mwanaume.

Bahati mbaya ni kwamba inaweza kuwa ngumu kujua moja kwa moja mtu ambae hatafika na wewe mbali. Lakini uzuri ni kuna ishara unawezeza kuziona zinaweza kuwa ni ishara za mpenzi ulienae kukupotezea muda. Ishara hizi The Bestgalaxy tumeziweka hapa chini.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kujua mpenzi ulienae anakupotezea muda

Kufanya mahusiano yenu siri.

Ukiwa kwenye mahusiano ya dhati mara nyingi huwa manashindwa kujizuia kuyaonesha kwa watu wengine. Lakini kama utakua kwenye mahusiano na mtu anekupotezea muda atakua makini sana kufanya mahusiano yenu yasijulikane na wengine. Anaweza hata kukuambia usimwambie mtu kuhusu mahusiano yenu ili mue kwenye mahusiano ya Siri. Sasa swali hapa ni “kitu gani kina mfanya awe makini na usiri?”. Mara nyingi inakua ni kwasababu anampenzi mwingine anaemuheshimu kuliko wewe. Kama ni mwanaume anaweza kukupa pesa na kila kitu cha gharama ili mladi mahusiano yawe Siri. Hii inaweza kuwa ni ishara kuwa hana mpango na wewe na anakupotezea muda.

Mnatafutana kwa haja za mwili au pesa.

Sawa mnaweza kuwa kwenye mahusiano ya mapenzi na mnaambiana “nakupenda” kila mara lakini kitu gani kikubwa huwakutanisha na kufanya mkumbukane? Kama ni shida za pesa au shida za mwili basi hizo ni dalili mbaya. Mapenzi kuwa pamoja maishani ni zaidi ya pesa na tamaa za mwili. Kama hakuna kitu kinachowaweka pamoja mkakumbukana mbali pesa au shida za mwili basi mnaweza kosa hata uwezo wa kuwa pamoja maishani. Ukiona dalili hii kwa mpenzi wako, kuwa makini maana si nzuri.

Mambo ya kuepuka katika Mahusiano BONYEZA HAPA>>>

Huficha mambo yake na hataki kujua sana kuhusu wewe.

Kwenye mahusiano mtu anaekupotezea muda huwa hataki ujue vitu vingi kuhusu yeye. Anaweza kukuficha kuhusu ndugu zake, sehemu anayotoka na hata jina lake kamili. Mbali na hayo hata ikija kwa upande wake utaona hajishughulishi kujua kuhusu wewe sana. Anaweza asitake kujua kitu zaidi ya jina lako na namba ya simu. Hataki kukuingiza sana kwenye maisha yake na pia hataki ingia sana kwenye maisha yako kwasababu anajijua kuwa kwako si wakudumu.

Hajali kuhusu wewe kwenye vitu muhumu.

Unaweza umwa au kuwa na jambo la muhimu lakini asijishughulishe kwa chochote. Kiufupi unaweza kuwa nae kwenye mahusiano lakini haoni kama mambo yako yanamuhusu sana. Anaweza kuwa Hana wivu kabisa na wewe.
Hii ni dalili ya kuwa yupo kukupotezea muda na anajiona kabisa hayupo karibu na wewe hivyo kuwa makini.

Ni hayo tu katika ukurasa huu. Natumaini yanaweza kuwa msaada kwa mwanamke au mwanaume yoyote ambae yupo kwenye safari ya kutafuta mtu wa Maisha. Endelea kuwa karibu na ulimwengu wa The bestgalaxy.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Robot 5 zilizoundwa kama Binadamu (Humanoid)


Katika dunia ya sasa maendeleo ya Teknolojia makubwa yamewezesha wataalamu kuunda robot zinazofanana na binadamu. Robot zilizoundwa kwa mfano wa Binadamu zinaitwa humanoid. Safari ya kutengeneza robot za muundo huu zilianzishwa muda kidogo na wataalamu mbalimbali na mpaka kufikia sasa Kuna uwepo wa robot zenye uwezo mkubwa ukilinganisha na kipindi cha nyuma. Kufuatia uwepo wa Teknolojia ya AI (Akili bandia) robot nyingi zilizo undwa kwa mfano wa Binadamu zimekua na uwezo mkubwa katika kuingiliana na binadamu halisi. Teknolojia ya AI ni kama inafanya kuzipa akili robot za humanoid na kuziwezesha kufanya baadhi ya mambo kama binadamu.

AI ni nini na inamatokeo gani katika Ulimwengu? BONYEZA HAPA>>>


Kadri Teknolojia ya AI inavyoendelea kukua ndio robot za Humanoid zinaendelea kuwa na uwezo mkubwa katika kufanya mambo kama binadamu. Inasemekana Teknolojia ya AI ikifika katika hatua za juu, humanoid robot zinaweza kuwa na uwezo mkubwa kuliko binadamu kwenye kufanya mambo mengi. Na pia tunaweza fikia wakati robot za mfano wa Binadamu zikaweza jichanganya na binadamu kufanya shughuli mbalimbali katika Maisha ya kila siku.
Inasemekana wakati huo roboti hizi za humanoid zitakua nyingi na zitakua zikitoa msaada na huduma katika sekta tofauti. Zinaweza kuwa kwenye huduma za afya, elimu, viwanda na hata burudani.


Roboti za humanoid nyingine tayari zimeanza kuwa sehemu ya maisha ya binadamu kwasasa. Kuna robot za muundo huu ambazo tayari zinafanya kazi au kutoa huduma.
Katika makala hii hatuta chimba sana kuhusu robot za humanoid sana. Kwasasa hebu tuangalie robot chache za humanoid zilizo tengenezwa vizuri Duniani.

Robot 5 zilizoundwa kama Binadamu (Humanoid)

Ameca

Ameca ni roboti lililoundwa kama binadamu wa kiume linalojulikana kwa uwezo wake wa kuingiliana na binadamu. Imetengenezwa na kampuni ya Engineered Arts ya Uingereza.
Ameca imewezeshwa na teknolojia ya hali ya juu ya AI kuweza kuelewa na kujibu mambo katika maongezi inayoyafanya na binadamu. Anauwezo wa kuona na kutambua vitu anavyo viona kupitia camera zilizoundwa kama macho. Katika lugha, Ameca huelewa na kuzungumza lugha zaidi ya moja.

Sophia

Sophia ni roboti mwingine ambae amekuwa na umaarufu sana duniani. Aliwahi kuzua gumzo baada ya kutamka kuwa atawaharibu wanadamu. Sophia alipokua katika mahojiano CNBC alijibu “Okay, I will destroy humans,” alipokua aliulizwa kuhusu kuharibu wanadamu.
Sophia robot yupo vizuri sana katika maongezi na hii ni Kwasababu umewezeshwa na Teknolojia ya juu ya AI. Anapoongea sauti inayotoka ni ya kike na hata sura pia Kwasababu ameundwa kuwa roboti wa kike. Aliundwa na kampuni ya Hanson Robotics.

Atlas

Atlas ni humanoid robot alieletwa na kampuni ya Boston Dynamics kwaajili ya kufanya kazi zinazohitaji nguvu na usahihi. Huwezi muweka katika kundi la Sophia robot au Ameca huyu maana yeye umeundwa kwaajili ya mambo yanayo jumuisha kukimbia, kuruka na kubeba vitu.
Ni robot mwenyewe Teknolojia ya juu inayomuwezesha kufanya vitendo mbali mbali kama binadamu mkakamavu. Anaweza hata kuruka sarakasi ya kujirusha na kujigeuza hewani bila kugusa chini na akatua salama.

Optimus

Optimus ni robot alietengenzwa kwaajili ya kusaidia katika shughuli mbalimbali kama vile kazi za nyumbani, viwandani na maeneno mengine kama hayo. Robot hili hufahamika pia kama Telsa bot, ni moja ya robot maalufu katika Ulimwengu wa Teknolojia. Limetengenezwa na kampuni ya Telsa ambayo ipo chini ya Elon musk ambae ni mmiliki wa mtandao wa X.
Optimus anaweza kuwa sehemu muhimu ya nguvu kazi katika Maisha ya baadaye, kwa kuwasaidia binadamu kupunguza mzigo wa kazi za kila siku.

Jia Jia


Huyu ni roboti wa kike wa kibinadamu aliyeundwa na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha huko China. Alizinduliwa rasmi mwaka 2016 na anajulikana kwa sura yake ya kuvutia na uwezo wa kuingiliana na binadamu katika maongezi. Imeundwa ili kuonekana kama binadamu, na yupo vizuri katika kusikiliza na kujibu maswali anayouliza na binadamu.

Roboti hizi zinaweza fanya mambo mengi kama binadamu lakini kiukweli robot hizi bado hazipo sawa kwa 100%. Kuna makosa na mambo mengi ambayo unaweza uoneshwe kwenye video au mitandao ya kijamii lakini fahamu kuwa kuna makosa yanafanywa na robot hizi. Zinaweza fanya makosa katika kujibu maswali au kufanya matendo.

Jinsi ya kum-surprise/kumshangaza mpenzi wako bila kutumia Pesa


Katika maisha ya mahusiano na mtu kunakua na vitu vingi ambavyo mnaweza fanyiana ili kufurahishana mkiwa kama wapenzi. Maisha ya upendo yanakua na mambo mengi ya kufurahisha kiasi ambacho ukikaa na kuyafikilia, tabasamu linaweza kukujia tu. Matukio muliofanyiana kwa msukumo wa upendo mukiwa kama wapenzi ndio mara nyingi hubakia akilini na kufurahisha moyo kila mkiyakumbuka au kufikilia. Lakini pia Matukio haya huwa yanaumiza pindi mtakapoachana au mkishindwa kutimiza ahadi zenu za kuwa pamoja mlizojiwekea.



Kumfanyia surprise mpenzi wako ni jambo zuri la kumfurahisha mapenzi wako na pia hutengeneza kumbukumbu nzuri katika safari ya mahusiano. Watu wengi wanapotaka kuwafanyia surprise wapendwa wao huwaza mambo yanayohusisha pesa tu na kusahau kuwa surprise sio lazima iwe hivyo.


Kum-surprise mpenzi wako ni kufanya jambo au kitu cha upendo cha kumshangaza na kumuacha na furaha. Unaweza fanya jambo linalo husisha pesa kum-surprise lakini kuna mambo yasio husisha pesa unaweza yafanya pia na akafurahi. Hapa chini The bestgalaxy tumejaribu kukufungua kidogo kwa kukupa matokio au mambo ambayo unaweza fanya kumshangaza mpenzi bila kutumia Pesa.

Zawadi za kumpa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kum-surprise/kumshangaza mpenzi wako yasio husisha Pesa

Kumpiga simu usiku sana kumwambia umemkumbuka



Ikiwa mkombali na sio kawaida wewe na yeye kuongea kwa simu usiku, njia hii inaweza kuwa nzuri na itamshangaza zaidi. Subiri usiku ufike kisha jaribu kumpiga simu itakayo muamsha usingizini. Inaweza kwa sio rahisi kumuamsha kwa simu lakini kama ukifanikiwa akapokea basi atakua ameshangazwa na simu yako. Akili itakua inatamani kujua nini kimekufanya upige simu usiku na bila kusita unaweza kumwambia sababu ni kumkumbuka, yaani umemiss. Unaweza isindikiza sababu hiyo na maneno matamu kuonesha moyo wako ulikua unatamani sana kusikia sauti yake usiku huo mpaka ukashindwa vumilia kukuche.

Kumsaidia au kufanya kazi ambazo kikawaida hufanya yeye



Kama kuna kazi au mambo ambayo kikawaida mpenzi wako huwa anafanya yeye unaweza afanya wewe ili kumshangaza. Kama ni mwanaume unaweza mkupikia mwanamke wako au ukamsaidia kupika huku ukipiganae stori kama rafiki tu. Mbali na kupika unaweza msaidia kufanya usafi wa nyumbani ambayo kikawaida hufanya yeye. Jambo hili linaweza mshangaza sana mpaka akakuuliza. Unaweza mjibu kuwa “nimeamua kukusaidia tu mpenzi wangu, nakupenda sana” au maneno mengine kama hayo.

Kumuandikia barua ya karatasi ya kawaida kwa mkono wako



Kutokana na Teknolojia watu tunatumia sana simu katika kuwatumia maneno mazuri tunao wapenda. Lakini ukihitaji kumshangaza mpenzi wako kwa sasa, mfikishie ujumbe huo kwa karatasi ya kawaida. Hakikisha unaiandika kwa mkono wako mwenyewe na unaiandika kwenye karatasi ya kawaida tu na sio karatasi maalumu. Hatakama unapesa za kununua zile kadi za upendo zenye maneno ya mapenzi, fahamu kuwa njia ya kuandika mwenyewe ni yakushangaza zaidi. Kunajinsi mpenzi wako anaweza hisi unampenda mno na yupo kichwani mwako sana. Mbali na hayo utakua umeweka kumbukumbu isio sahaulika kirahisi akili mwake.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Kumuimbia wimbo mzuri wa mapenzi



Ninapoongelea kuimba simaanishi uwe msanii alafu umtolee nyimbo ambayo atakua anasikiza kwenye Redio. Na maanisha kuimba mbele yake nyimbo yoyote ya msanii iliobeba ujumbe wa mapenzi kuhusu nyinyi. Sio lazima uwe na sauti nzuri, kikubwa ni umshangaze tu. Unaweza jitoa ufahamu kidogo ukamwambia akuangalie na kukusikiliza mpaka mwisho bila kukukatisha. Jambo hili ninaweza mshangaza sana kama sio kawaida yako na litatengeneza kumbukumbu nzuri kati yenu wapenzi.



Mambo tuliozungumzia hapo juu ni machache kati ya mengi unayoweza kufanya kumshangaza mtu wako bila pesa. Mambo madogo madogo kama haya kwenye mapenzi huwa yanaunda historia nzuri isioweza futwa kirahisi. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy, tunaenda kujifunza mambo mengine zaidi.

Mambo unayotakiwa kujua kuhusu Simu za Mkopo

Siku hizi hauhitaji kujiumiza sana kupata simu Janja au smartphone maana kuna mpaka simu za Mkopo. Simu hizi zinasaidia sana watu katika kuingia kwenye ulimwengu wa kisasa na kufurahia matunda ya Teknolojia.

Kuna mambo mwengi mtu anaweza ya kosa akiwa hana simu hizi za kisasa. Na pia Kuna vitu vingi mno mtu anaweza nufaika navyo kupitia simu hizi. Ukiwa kama mtu unaeishi ulimwengu wa hivi sasa, smartphone ni kitu muhimu usichotakiwa kukikosa japo faida au umuhimu hutokana na matumizi yako.

Kuna watu wengi kwa sasa wanatumia simu za smartphone za Mkopo na zimekua msaada mkubwa kwao huku wakiendelea kulipa Mkopo kidogo kidogo. Pia kuna watu wameisha maliza malipo ya Mkopo na wanaendelea kufurahia simu wakiwa na umiliki wa simu hizi kwa 100%.

Unaweza ukawa ni mtu unaetumia au unahitaji simu hizi za Mkopo. Hapa The bestgalaxy, tunajaribu kukupa mwanga kidogo kuhusu simu za Mkopo kwa kuangalia mambo machache kuhusu simu hizi. Unaweza kupitia mambo haya kwa makini hapa chini.

Katika matumizi yako ya simu usifanye mambo haya BONYEZA HAPA>>>

Mambo unayotakiwa kujua kuhusu simu za Mkopo

Ni njia rahisi ya kupata simu mpya unayohitaji ukiwa na pesa ndogo

Kupitia huduma za Mikopo ya simu unaweza kupata simu mpya unayohitaji ukiwa hauna pesa ya kutosha kuinunua. Unaweza usiwe na shilingi laki 500,000 kamili mkononi lakini ukapata simu mpya yenye thamani ya pesa hiyo kwa Mkopo baada ya kutoa posa kidogo tu kama kianzio. Hivyo ni njia nzuri kama unatamani kupata simu mzuri mpya bila kuwa na pesa ya bei yake kamili.

Kikubwa unatakiwa kuwa na pesa ya kianzio tu ambayo mara nyingi hutegemeana na bei ya simu unayokopa na hata sehemu unayopata huduma ya Mkopo huo. Kama unakopa simu ya bei kubwa kianzio nacho huwa kinakua kikubwa.

Sio chaguo zuri kama hauna pesa ya uhakika ya kila siku

Kama unaona kabisa hautakua na pesa ya uhakika ya kulipia kila siku, simu hizi zinaweza kuwa sio chaguo zuri kwako. Simu hizi zinahitaji mtu alipie au awe amelipia malipo ya siku ili atumie. Kama mtu hatalipia, simu hua inajifunga na kumnyima mtumiaji nafasi ya kutumia mpaka atapo lipia.

Sasa ukiona hali yako ya pesa inaweza kufanya ukose pesa ya kulipia mpaka unafungiwa kwa muda mrefu, hili sio chaguo zuri sana. Ni vema ile pesa unayopanga kuweka kwenye kianzio ukachagua kununua simu used ya bei ndogo ambayo hautatakiwa kutoa pesa nyingine kuitumia. Kama hauna pesa za kulipia simu hizi unaweza kuona kero zinapojifunga wakati ni haki yao kukufungia.

Unaweza pata simu za mkopo kwenye Makampuni ya mawasiliano ya simu

Ukihitaji kupata huduma za simu za Mkopo, unaweza zipata toka kwenye maduka maalumu kwa mikopo hiyo yaliopo sehemu mbalimbali hapa Tanzania. Lakini pia hii mitandao ya mawasiliano ya simu kama Tigo na Vodacom, imejiingiza kwenye utoaji wa huduma za mikopo ya simu.

Unaweza kukopa simu kwenye mtandao wa simu unaotumia kama Vodacom au Tigo alafu ukawa unalipwa kidogo kidogo huku ukiendelea kuitumia. Unaweza wasiliana na mtandao wako wa simu kupata maelezo juu ya jambo hili. Uzuri wa kukopa katika mitandao ya simu ni kwamba unapewa OFA za vifurushi kwenye Laini ya simu. Lakini pia sehemu nyingine za kukopa simu zipo vizuri pia.

Taalifa za malipo hutunzwa

Unapotumia simu ya Mkopo ni vema ukajua taalifa zako na malipo yako mara nyingi huwa zinatunzwa ili kukusaidia pale unapokwama au usumbufu unapojitokeza. Taalifa hizi zinaweza kuwa ni namba uliotumia kulipia na hata kiasi.

Ni jambo zuri sana kama ni muaminifu lakini kama sio muaminifu kuna uwezekano wa kutafutwa kupitia taalifa hizo japo wengi hawafikii hatua hiyo. Na hata ukiibiwa taalifa za malipo anayotoa mtu anaelipia na kuitumia baada ya kuibiwa zinaweza tumika kujua simu ipo kwa nani.

Ni hayo machache katika ukurasa huu, Endelea kuwa nasi na usisahau kwa simu za mikopo ni msaada mkubwa kwa watu katika kipindi hiki. Hazina usumbufu wa kukunjana mashati na kuaibisha wakati wa kukudai.

SMS za kumsifia mpenzi wako (Mwanamke au Mwanaume)

Karibu the bestgalaxy na hapa katika makala tunaenda kuangalia SMS za kumsifia mpenzi wako. Hakuna raha kama kusifiwa na mtu unaempenda. Mtu ukisifiwa na unaempenda toka moyoni unaweza hisi Duniani upo juu na wathamani sana. Kiufupi maneno mazuri ya kusifu yakitoka kwa wapenzi au watu tunao wapenda huwa yanaupasua moyo kwa furaha na kufanya tuhisi kuwa tunathamani. Hivyo ukitaka kuugusa moyo wa mpenzi wako kwa kiasi hicho si vibaya ukatumia sms nzuri za mapenzi za kumsifia mpenzi wako. Hii inaweza kufanya awe na furaha, aione thamani yake na kujua umetambua thamani yake pia.


Kupitia ujumbe mfupi wa SMS, unaweza kumwambia mpenzi wako jinsi unavyomheshimu, kumjali, kumkumbuka na kwanini upo hivyo kwake. Unaweza fungua moyo wako kwake na kumwagia sifa zake zote nzuri.
Makala hii imekukusanyia ujumbe au sms ambazo unaweza kutumia kumsifia mpenzi wako mwanaume au mwanamke ili ajisikie vizuri na kujua jinsi unavyomthamini. Kama utahitaji unaweza ziangalia hapa sms chini

Zawadi za kumpa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

SMS za kumsifia mpenzi wako (mwanaume au mwanamke)

  • Ninafuraha kwakua nina Bahati sana. Bahati ya kwanza ni kufikia siku ya Leo na bahati ya pili ni kuwa na wewe mpaka leo. Nitakupenda Milele mpenzi wangu, wewe ni mtu muhimu kwangu.
  • Ivi ni nani alikufundisha Mapenzi? Yani hata kukuchiti siwezi, naona ushenzi. Nanenepa kwa Mahaba yako na chini ya shuka nakula mpaka mfupa, sitemi.
  • Najua huwenda kunasiku unahisi umewahi niudhi na kuna pia siku unahisi unanifurahisha. Lakini ukweli ni kwamba nazifurahia siku zote nilizokua na ntazokua na wewe. Nakupenda sana furaha yangu.
  • Hapo zamani nilikua naomba mungu nikutane na mwanaume jasiri, anaenipenda, anae nijali na kunithamini. Nashukuru mungu kwa kunileta karibu nawe. Mwanaume upo moyoni, unazunguka kwenye damu mpaka akilini. Nakupenda honey.
  • Wanasema “mapenzi ni matamu” ni kweli, umenipa nikaamini. Wanasema “Raha ya mapenzi umpate anae kupenda na kuyajua” hata siwezi pinga maana Raha naiona tangu ulivyoungana na mimi. Nakupenda na sihitaji kutoka penzini.
  • Mapenzi unayonipa yamenifanya nione maajabu. Siku hizi nikifumba macho sioni giza, nakuona wewe. Moyo unajawa na furaha, najikuta natabasamu kila nikikuwaza wewe. Yani naishi maisha ya furaha kwasababu nimekuchagua wewe.
  • Kila siku nikikutazama nakuona mpya katika uzuri wako. Na unanivutia kiasi ambacho tukiwa karibu natamani kugusisha moyo wangu na wako. Nimeisha kuwa teja wa penzi lako.
  • Nilikua natamani kupata na kumpenda mtu mwenyewe sifa nyingi nzuri. Nashukuru mungu kunikutanisha na wewe. Nimekupata sasa, nakupenda na napenda jinsi ulivyo.
  • Nilipokua mdogo nilikua napenda sana kuangalia mwezi na nyota angani. Zilikua zinanivutia sana kila nikizitizama. Siku hizi napenda kuangalia macho yako. Ni mazuri zaidi sana.
  • Lips tu ni tamu zaidi ya pipi, na vingine vitamu havielezeki, nitavitoa wapi kama si kwako? Huniishi hamu na wala wewe si bigG, hivyo sahau swala la mimi kuondoa moyo wangu kwako.
  • Huwa napenda vile unavyo vaa, unajipatia wewe malaika. Ni msafi unaependeza. Unakua kama nyota inayong’aa angani ambayo mungu ameichukua amenipa.
  • Ndoto yangu ya kuwa na mtu ninaempenda maishani, ilianza kutimia nilipokutana na wewe kipenzi changu. Kwasasa nipo pamoja na wewe, najiona naishi kwenye ndoto yangu, Nakupenda sana.
  • Macho yangu yakikutana na yako, moyo wangu hulipuka kwa furaha. Wewe ni mzuri kama malaika ulieshushwa kwangu, namuomba mungu, usiote mbawa.
  • Hakuna njia ya kuachana na mimi isio niumiza. Siwezi kukupoteza alafu nikwa na furaha au bila kuumia. Nimekuweka moyoni mpenzi, wewe ni muhimu kwangu . Nahisi nakupenda.
  • Mambo mazuri yote nilianza kuyaona maishani nilipokupata wewe. Umekua ni mwanamke mzuri unaevutia mambo mazuri kama ulivyo wewe.
  • Maua hufanya bustani ipendeze na kuvutia. Upendo wako wewe, hufanya nijione wa thamani kwenye hii Duniani. Nakupenda sana.
  • Uwezo wako wa kunitambua na kuelewa ninachohitaji bila kusemwa, hufanya mahusiano yetu kuwa ya kipekee sana. Unanipenda sana, najua. Na Mimi nakupenda kuliko unanyojua. Nitaishi nikiwa nawe moyoni mpaka mwisho wa Dunia.
  • Unajua kupenda malaika wangu. Penzi lako hufanya nione bahati kuwa na wewe. Sauti yako, hunibembeleza. Najihisi kuishi mbingu ya saba na upendo wako ndio umenileta.

Sms hizi zimewekwa hapa kwaajili ya watu wa Jinsi zote. Kama ni mwanaume unataka kumtumia mwanamke/mke unaempenda, unaweza pata sms inayofaa. Na hata ukiwa mwanamke pia unaweza pata sms kwaajili ya Mwanaume/mme. Wakati ukifurahia hayo, endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.