Category Archives: Uncategorized

Magame mazuri na rahisi kwa kila mtu unayoweza kucheza kwenye simu (Android)

Katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia, simu za mkononi zimekuwa sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku. Tunazitumia kwa mawasiliano, kuperuzi mitandao ya kijamii, na kwa burudani. Moja ya njia maarufu zaidi za kuburudika kwenye simu zetu ni kucheza magame mbalimbali. Magame kwa wengi ni njia ya kupumzika, kujifurahisha, na hata kujifunza mambo mapya maana kuna game zinazofunsha pia.

Ingawa kuna maelfu ya magame yanayopatikana kwenye internet, si magame yote yanakua yanaonekana mazuri kwa kila mtu. Kuna watu hawajajikita sana kwenye games na kama wakicheza game huwa wanapenda games zisizo na mambo mengi sana. Kwa bahati nzuri, kuna magame mazuri mengi rahisi ambayo yanaweza kuchezwa na watu wanamna hii, bila kujali umri au ujuzi wa teknolojia.

Magame ya mpira ya kucheza kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Katika makala hii, tutakuletea orodha ya magame mazuri na rahisi ambayo unaweza kucheza kwenye simu yako kama ni mtu wa namna hii. Kabla hatujaenda katika kuangalia games hizi, fahamu kuwa game zinaweza kusaidia kupunguza msongo wa mawazo na kuongeza furaha katika maisha yako ya kila siku.

Magame mazuri na rahisi kwa kila mtu unayoweza kucheza kwenye simu (Android)

Classic block falling

Hili game ni moja ya magame yenye muundo ambao baadhi watu husema ni “magame ya kupanga tofali”. Katika game hili unadondoshewa vitu kama tofali ambavyo huwa katika maumbo tofauti na utatakiwa kuyapanga vizuri. Unakua unapata score baada ya kufanikiwa kupanda vizuri tofari bila kuacha nafasi. Game kama hizi zipo nyingi na zinafahamika mno. Kucheza game la Classic block falling inaweza kuwa sio jambo gumu kulifanya kwa watu wengi.

Water color sort

Water color sort ni gemu lingine rahisi linaloweza kuchezwa na kila mtu. Kwenye game hili unapewa maji yenye rangi nyingi yaliowekwa kwenye chupa 2 au zaidi alafu utatakiwa kukusanya maji yenye rangi sawa na kuyaweka kwenye chupa zake. Water color sort linahitaji mchezaji atumie akili sana kabla ya kufanya maamuzi unapocheza. Kadri unavyoendelea kucheza na kushindwa ndivyo unaendelea kukutana na mafumbo yanayohitaji utumie akili zaidi. Ni game lisilo na mambo mengi kabisa na hufurahisha pia.

Bubble Shooter

Ukiwa umetulia na unahitaji game lisilo na mambo mengi kulicheza basi kumbuka kuna hili huitwa Bubble shooter. Hili game mchezaji unakua unatumia vimipira vyenye rangi kuvilenga vimipira vingine vinavyoning’inia juu. Ili kufanikiwa, unatakiwa kulenga vimipira vinavyo fanana rangi na ya mpira unaorengea. Yani kama umepewa mpira mwekundu wa kurengea basi utatakiwa kuulenga mpira wa rangi nyekundu pia.

Subway suffer

Subway suffer ni game maalufu sana ulimwenguni katika ulimwengu wa game ya simu za smartphone. Katika gemu hii, unacheza kama kijana anaekimbia ili kukwepa polisi anaemkimbiza baada ya kumkuta akichora maeneno ya treni. Unatakiwa kukimbia kwenye Barabara ya treni ili askari huyo asikukute. Katika kukimbia unakua unakutana na vitu mbalimbali unavyotakiwa kukwepa. Unakua unakimbia na kukwepa vitu kama ilivyo kwenye game kingine maalufu liitwalo Tempo run japo hayelekeani sana.

Racing in Car 2


Racing in Car 2 ni game la simu ambalo linakuweka kwenye ulimwengu wa kuendesha magari uwe kama Dereva. Game hili mchezaji anakua Dereva na anacheza kwa kuyumbisha simu ili kulielekeza gari upande wa kwenda pindi linapotembea barabarani. Katika barabara mchezaji anatakiwa kufanya vizuri kwa kupishana na magari mengine vizuri huku kuepuka ajali.

Huu ni mwisho wa orodha yetu lakini kuna game nyingine zaidi ya hizi tungeweza weka hapa. Lakini hatuwezi weka zote hivyo hizi zikikufaa, zijaribu na ufurahie.

Epuka kukopa pesa kama unatabia hizi ndani yako

Kuna uwezekanao wa kuwa na mambo mengi sana yanayoweza kusukuma mtu kukopa pesa za watu wengine au taasisi mbali mbali za kifedha. Na kukupa ni jambo zuri sana maana kuna muda mtu unaweza kukwama kifedha kwa kukumbana na jambo linalohitaji pesa ambayo hauna lakini ukalimudu kupitia mkopo.

Kuna watu hukopa pesa ili kurekebisha mambo yao yalioenda vibaya na kuna hata ambao hukopa ili kulifanikisha jambo lisilo na ulamazima sana. Kukopa kwasababu yoyote ile ni uamuzi mzuri lakini itakua uamuzi mzuri zaidi kama umefanikiwa kwenye jambo lako na kuulipa mkopo wako. Kama haujakamilisha jambo lako au umefanikisha lakini haujafanikiwa kulipa deni la mkopo wako, uamuzi wa kukopa unaweza kuwa mbaya kwako. Na endapo hali yakushindwa kulipa itakua inakuandama kila mara unapokopa ni vema ukaanza kujiweka mbali kidogo na mikopo.

Hapa The bestgalaxy tunakupa tabia ambazo mara nyingi zikiwa ndani yako basi mikopo huwa karibu sana na pia huwa ni ngumu kuilipa. Sio kila mtu mwenye madeni au anaeangukia kwenye madeni anatabia hizi. Ni baadhi ya watu tu ndio huwa na tabia tunazoenda kuzielezea hapa. Niwesema hivyo maana wengine husukumwana na vitu vilivyo nje kabisa na uwezo wao  au sababu myingine mabali na tabisa hizi.

Mambo unayotakiwa kujua kuhusu simu za mkopo BONYEZA HAPA>>>

Epuka kukopa pesa kama unatabia hizi ndani yako

Kushindwa kuzirudisha pesa zako mwenyewe

Kama ni mtu mwenye malengo na huwa unajiwekea pesa kwaajili ya mambo mbalimbali basi kuna muda unaweza kuwa unajikopa mwenyewe. Yani unachukia pesa ulizojiwekea kwaajili ya jambo flani na kuzitumia kwenye jambo lingine tu huku ukiwaza kichwani “Nitazirudisha”. Ikiwa unatabia hiii na unakua na msimamo wa kuzirudisha tena hizo pesa basi unaweza usiteseke sana kulipa hata ukikopa kwa watu wengine. Lakini kama huwa haurudishi pesa hizo na ni tabia yako, kunaweza kuwa na ugumu pia unapokopa kwa wengine. Ni vema ukajaribu kujiimarisha ndani yako kabla ya kukopa kwa wengine. Hakikisha unapambana sana kurudishia pesa sehemu zako za dani ukichukua pesa.

Jinsi ya kupata Mkopo kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Kuhairisha mipango yako ulioianza

Kuna baadhi ya watu huwa na mipango ya biashara na Mambo mengine yanayoweza kuhitaji pesa ili kuingiza pesa. Kukopa kunaweza kuwa ni wazo la haraka kwa mtu mwenye mipango ya namna hii lakini hana mtaji au pesa inayohitajika.
Kukopa sio kitu kibaya kama umekusudia kuanza kupambana kutimiza mpango uliojiwekea. Lakini kama ni mtu unaempenda kuhairisha mipango ulioianza, kukopa kunaweza kuumiza.
Ukichukua Mkopo kwaajili ya mpango flani lakini ukahairisha na kwenda tofauti na mpango huo, kunakua na hatari kubwa ya kupoteza pesa hiyo. Pesa ikiisha bila kufanya kitu kilichosababisha ukope, unaweza jilaumu kuliko ungefanya na kushindwa.
Kama haujaweka vizuri mipango yako au haupo tayari kuipambania kwa asilimia 100, basi usikope pesa kwanza.

Kusahau shinda unapokamata pesa yoyote

Hali yako huwa inakua vipi muda ambao hauna pesa? Na hua inakua vipi ukipata pesa? Kama ukipata pesa yoyote mkononi mwako shida huwa unazisahau, unafanya matumizi na kuacha kabisa kutafuta pesa basi kukopa kunaweza kuwa kubaya kwako. Ukikopa pesa na kuishika mkononi pesa hiyo inabidi iwe kichwani kwako kuwa sio pesa yako na unahitajika kulipa. Hii inaweza kukusaidia kupata mpango wa kuilipa na kuwa makini unapozitumia pesa hizo za mkopo.
Ikiwa utaruhusu pesa hiyo ikusahaulishe shida na kuichukulia ni yako, basi unaweza kuwa ndio mwanzo wa kupuuza deni lako, kuridhika na kuanza ikiutumia pesa.
Usiache kuiona pesa ya Mkopo kuwa ni Mkopo hata ikiwa na mamilioni ya pesa.

Haupendi kudaiwa.

Kutopenda kudaiwa ni jambo zuri sana ila linakua zuri kama utakua na uwezo wa kujikumbusha mwenyewe kulipa pesa kabla haujadaiwa. Mbali na hapo ukiwa haupendi kudaiwa itabidi uanze kuepuka kukopa pesa maana kudaiwa ni lazima na ukichukia au kumfanyia vibaya anaekudai itakua ni kosa kwako tu kivyovyote maana umeshindwa kutimiza makubaliano. Wengine hufikia mpaka hatua ya kupambana kukata kulipa Kwasababu ya kudaiwa vibaya lakini hawajihukumu kwa kuchelewesha pesa muda mrefu kinyume na makubaliano.

Natumaini umesoma na kuelewa makala hii na inaweza kuwa msaada katika Maisha yako kwenye upande wa kukopa. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi.

Jinsi ya kumtuliza mpenzi wako mkikosana au kutoelewana

Kutokuelewana na kufanyiana makosa ni mambo ya kawaida na hutokea mara nyingi sana. Hakuna anaependa mambo hayo yatokee lakini mara nyingi hutokea bila kutarajia.


Kutokuelewana au kufanyiana makosa kunaweza fanya mahusiano ya mapenzi kutikisika na hata kuvunjika kabisa. Lakini hii inategemeana na jambo lililofanya wapenzi mufikie hatua mbaya na maamuzi au hatua muliochukua baada ya kukoseana au kutoelewana.


Katika mambo muhimu kujua katika Mahusiano ni jinsi ya kufanya mnapokoseana au kutoelewana na mpenzi wako. Ni muhimu Kwasababu kukosana na kutoelewana ni kama hakupingiki kwenye mahusiano, hutokea tu. Lakini ukiwa na ufahamu wa jinsi gani ufanye, itakusaidia kwenye kuweka sawa mahusiano kwenye hali hiyo.

Katika makala hii, tutajadili jinsi ya kumtuliza mpenzi wako mnapokosana au kutoelewana. Kwa kuelewa na kufuata mbinu sahihi, unaweza kusaidia kurejesha amani na kuimarisha uhusiano wenu bila shida.

SMS za kumfanya mpenzi wako afurahi BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kufanya kumtuliza mpenzi wako mkikosana au kutoelewana

Muombe msamaha

Baada ya kukosana au kutokuelewana kulikosababishwa na wewe ni vema ukamuomba msamaha mpenzi wako. Neno “Samahani” linaweza muweka sawa mpenzi wako na kumrudishia katika hali ya kwaida. Neno hili ni moja ya maneno yenye nguvu za kurekebisha hisia za mtu na kumuweka sawa mnapokua mmekosana.
Ukimkosea mtu bila kumuomba msahama anaweza kuwa na mawazo mengi sana. Wengine usipo waomba msamaha huwa wanakupangia vitu vingi kichwani ili kukulipizia. Lakini ukiomba msamaha baada ya kukosea inaweza fanya mwenza wako asifike mbali sana kimawazo.

Muache peke yake kwa muda

Kuna baadhi ya watu wakikosewa au wakitokewa na kutokuelewana huwa wanahitaji kuwa peke yao kwa muda ndipo watarudi sawa. Usipo mpa muda wa kuwa peke yake hata msamaha wako hawezi kuuelewa.
Sio kila mtu yupo hivyo ila kama ukiwa kwenye mahusiano na watu wa namna hii basi uwe unaheshimu muda wake wa kuwa peke yake pale ambapo hamuelewani au mmekosana. Unaweza ukamuacha peke yake wa muda alafu ukaanza kujisogeza tena kidogo kidogo.
Hii inaweza kuwa sio njia ambayo mtu unaweza fikili kuitumia kwa haraka haraka ila ni njia muhumu ya kuweka sawa kiakili baadhi ya watu mnapokosana.

Mzawadie kitu anachokipenda

Baada ya kukosana au kutokuelewana unaweza muweka mpenzi wako kwenye hali ya furaha kwa kumpa zawadi. Tafuta zawadi nzuri unayohisi anaweza ifurahia alafu mpatie.
Wote tunajua hakuna asiependa au kufurahia kupewa zawadi za gharama Duniani, lakini zawadi sio lazima iwe ya gharama. Zawadi nzuri inaweza kuwa kitu chochote kizuri kinachoweza ugusa moyo wa mtu. Kwaiyo jaribu kufikilia kitu chochote kizuri kitakacho ugusa moyo wa mwanamke au mwanaume umpendae. Kama ukikipata cha bei ndogo au kubwa, fanya kumpatia ili kumtuliza au kumuweka sawa.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Mwambie maneno mazuri ya upendo

Kwenye mahusiano ya mapenzi maneno ya upendo huwa yananguvu sana. Neno moja au mawili mazuri ya upendo yanaweza upasua moyo kwa furaha. Hasira na makasiriko baada ya kutoelewana au kukosana, vinaweza tulizwa na maneno matamu ya upendo.
Ukikosana na mpenzi wako au kutoelewana nae, unaweza tumia maneno mazuri au matamu kumuweka sawa. Unaweza mkumbusha jinsi gani unampenda, umuhimu wake kwako, uzuri wake na mambo mengine ya kuvutia au kugusa moyo.

Ni hayo tu katika makala hii, natumai unaweza kuwa umeelewa jinsi gani unaweza mtuliza mtu wako mnapokua hamko sawa. Napenda kusisitiza kwamba watu tupo tofauti hivyo ni vema kufikilia kidogo kama njia unayataka kuitumia inamfaa mwanamke au mwanaume umpendae.

Kutafuta vitu hivi online kuna hatari kubwa ya kutapeliwa au kuibiwa

Katika ulimwengu wa kidijitali, ununuzi na utafutaji wa bidhaa au huduma mtandaoni umekuwa jambo la kawaida kwa watu. Lakini, pamoja na urahisi na faida zinazotokana na kutumia mtandao kwa shughuli hizi, kuna hatari nyingi wanazokumbana nazo watumiaji.

Moja ya hatari kubwa ni utapeli au wizi wa mtandaoni. Hii hua inatokea kutokana watu wasio waaminifu kutumia mbinu mbalimbali kuwalaghai wale wanaotafuta vitu au mambo flani mtandaoni. Utapeli wa mtandaoni umeongezeka kwa kasi sana katika miaka ya hivi karibuni na Hali hii ipo online dunia nzima.

Matapeli wanatumia teknolojia za kisasa na mbinu za ujanja ili kuwaibia watu taarifa zao za kibinafsi na fedha. Tatizo hili ni inasemekana kuwa ni gumu kumalizika maana Teknolojia inapokua, haiimarishi vifaa vya ulinzi tu, inaimarisha na mambo yao pia. Jambo la muhimu kupunguza jambo hili ni kila mtu kuwa makini na ufahamu wa mambo ya Teknolojia na usalama.

Mambo ya kuzingatia unaponunua bidhaa mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Kutafuta vitu hivi mtandaoni kunaleta hatari kubwa ya kutapeliwa au kuibiwa

Kupata App au software za bure

Kama kuna app au software yoyote inayouzwa au kulipiwa ni vema ukafuata utaratibu rasimi wa kuipata na sio Bure. Njia nyingi za kupata app au software hizo za Bure sio salama. Unaweza pata sehemu ambayo inatoa Bure lakini ukiingiza software au app hiyo kwenye kifaa chako inaiba taalifa zako na kuweka hatarini mambo yako pamoja na watu unaowasiliana nao. Sio rahisi kufahamu hili kama hauna ufahamu juu ya usalama kwenye upande wa Teknolojia ila unaweza epuka hatari hii kwa kutoingiza za app za Bure ovyo.

Mikopo ya haraka bila utambulisho

Kuna watu huwa wanatafuta mikopo ya hataka lakini hawataki kutoa taalifa zao nyingi kuogopa kutafutwa wakishimdwa kulipa. Sasa jaribu kufikilia ungekua wewe ndio unaekopesha ungeweza kumpa mtu pesa nyingi bila kumjua vizuri? Au bila kutafuta atakaposhindwa kulipa?

Ni wazi kuwa inaweza kuna ni jambo gumu kidogo hata kwako. Sasa endapo ukitafuta mtandaoni Mkopo mkubwa ambao unasema kuwa utapewa bila mtoa Mkopo kukujua vizuri basi fahamu kuwa unaweza kuwa hatarini. Unaweza kuwa hatarini kwasababu mtoa Mkopo wa mtindo huo kwa asilimia 60 anaweza kuwa ni Tapeli. Mtoa Mkopo wa kweli anataka akujue vizuri ili iwe rahisi kukupata na hii ndio maana hata app za mikopo huwa zinachukua taalifa nyingi kwenye simu unapozitumia. App za mikopo zinaweza chukua mpaka namba za watu ulizonazo kwenye simu.

Kutengeneza pesa nyingi mtandaoni kwa haraka au rahisi

Kama ni mtu unaefuatalia mambo ya kutengeneza Pesa na kujiweka sawa kiuchumi basi unaweza vutiwa na “kutengeneza pesa mtandaoni “. Jambo hili linaweza kuwa ni rahisi sana kuliongea lakini linaweza kuwa sio rahisi kwenye matendo.

Kuna Platform zinaweza kukuambia kuhusu kutengeneza nyingi rahisi lakini safari ikawa ngumu ila kukawa na ukweli ndani yake. Pia kuna Platform nyingine nyingi zinaweza sema hivyo kukuvutia ili zikutapeli. Hivyo ni vema kuwa makini unapokua kwenye upande huu.

Kuona sms za mtu mwingine bila kugusa simu

Watu wengi hutamani kujua juu ya hili na kuna maelezo mengi kuhusu jambo hili katika internet. Maelezo mengi yaliopo mtandaoni juu ya kuchunguza mtu mwingine sio ya kweli na yanaweza kukuweka kwenye hatari ya kutapeliwa au kuibiwa. Kuna maelezo yanaweza kukufanya uibiwe pesa, uharibu simu yako na hata kuvujisha vitu(sms,picha au video) vyako vya kwenye simu au simu ya mlengwa.

Unasisitizwa kuwa makini unapofanya au kutafuta mambo mtandaoni ili kuwa salama. Lakini pia ukipata matatizo kwa bahati mbaya unatakiwa kutokata tamaa. Usiruhusu mambo hayo yakuzuie kufaidika na mtandao.

App nzuri za simu katika kufanya mazoezi ya mwili

Kuna app nyingi ambazo tunaweza ziingiza kwnye simu zetu na zikawa msaada kwenye vitu au mambo tunayofanya kwenye maisha. Hapa kwenye ukurasa huu The bestgalaxy tumekusanya app chache zinazoweza saidi katika upande wa mazoezi ya mwili. Nadhani wengi tunajua umuhimu wa mazoezi ya mwili katika maisha ya mwanadamu, hasa katika kipindi hiki chenye mambo mengi yanayohatarisha afya ya mwili wa binadamu.

Binadamu wa sasa tumezungukwa na vyakula pamoja na tabia nyingi zisizo rafiki kwa Afya zetu, ukiwa kama mwanadamu wa kipindi hiki unashauriwa kufanya mazoezi ili kuuweka mwili sawa na kuepuka baadhi ya magonjwa. Kabla ya kwenda moja kwa moja kuangalia app hizi, nakukumbusha kuijenga na kuendelea kuilinda tabia ya kufanya mazoezi maana ni jambo la maana usiloweza kujutia maishani.

Home workouts app: credit

App nzuri za simu katika kufanya mazoezi ya mwili(Android na iOS)

Home workouts

Hii app ni maarufu sana katika upande wa app za mazoezi za simu. App ya Home workouts imejikita zaidi katika kusaidia watu wanaotaka kufanya mazoezi ya mwili wakiwa nyumbani. Inakupa mbinu za mazoezi ya kufanya ili kuweka misuli ya mwili vizuri, kupunguza uzito au kupunguza mwili. Inakuonesha jinsi unavyoweza fanya yote hayo ukiwa nyumbani bila kwenda GYM zilizo mbali na ulipo. Inaweza simama kama mwalimu au msimamizi wako wa mazoezi ya nyumbani ukiwa kama Mwanamke au Mwanaume unaempenda mazoezi.

Workout for Women

Hii app ni kwaajili ya mwanawake unaehitaji kufanya mazoezi. Kama wewe na mwanamke unaetaka kufanya mazoezi ya mwili lakini unakosa muda wa kutoka ulipo na kuelekea GYM, basi app hii inaweza kuwa masada zaidi kwako. App ya Workout for Women inasimama kama mwalimu wa nyumbani wa mazoezi ya kuweka mwili sawa. Inakupa mazoezi ya kupungiza tumbo, kuongea makalio na kufanya ujihisi mwepesi. Workout for Women inakupa mbinu za kufanya mazoezi hata ukiwa kitandani hivyo itakua ni juu yako tu kutenga dakika chache kujiweka sawa kila siku.

Strava

Strava ni app maalumu kwa watu wanaopenda kufanya mazoezi lakini mazoezi haya sio ya sehemu moja. Hii ni kwaajili ya mazoezi kama kukimbia au kuendesha baisikeli. Wengi hufanya mazoezi haya asubuhi au jioni ili kuwema miili yao sawa. App hii inasidia mtu kupima umbali anaokimbia kila siku na kujua anakimbia kutoka wapi kwenda wapi.

Inaweza kuunganishwa na saa za kidigitali zinazofahamika kama “Smartwatch” japo sio zote. Inasaidia kuangalia maendeleo katika mazoezi yako hirahisi kwenye simu. Unaweza angalia hata Hali ya mapigo yako ya moyo unapofanya mazoezi (Hii itakuitaji utumie Heart rate monitor au Smartwatch).

GYM DONE

App hii imejikita zaidi kwenye upande wa mazoezi ya GYM. Ni app inayoweza kukuongoza unapofanya mazoezi kwenye chumba Cha GYM kwakutumia vifaa mbalimbali. Kwenye app ya GYM Done unaoneshwa mbinu au namna ya kutumia vifaa vya GYM kuweka vizuri misuli ya sehemu tofauti za mwili. Mtumiaji unaweza pia kujiweka mipango yako ya mazoezi ili kukamilisha malengo yako.

App za mazoezi ya mwili zimekua zikitumika na mamilioni ya watu wanapofanya mazoezi na zimekua msaada mkubwa katika kujenga afya ya mwili. Ni app hizo tu katika orodha yetu lakini fahamu kuwa kuna app nyingi nzuri kwa mazoezi ya mwili. Endelea kuwa nasi kwa mambo mengine zaidi.

Kuna utofauti wa simu za bei ya kawaida na bei kubwa?

Simu za smartphone Kuna watu huziweka kwenye makundi mawili. Kuna simu huangaliwa kama za bei kubwa(Bei ghali) na pia kuna simu huangaliwa kama ni za bei ndogo(kawaida/rahisi).


Wakati mwingi, watumiaji wanapotaka kufanya uamuzi wa kununua simu mpya, wanajiuliza kama wanapaswa kuchagua kifaa cha bei rahisi au kuwekeza katika kifaa cha bei ya juu. Hatakama hawana uwezo wa kumikili simu za bei ya juu hununua simu za bei rahisi na kuendelea kuzitolea macho simu za bei ya juu.


Simu za bei ya juu zinaweza kuwa chaguo zuri sana kwa mtu. Lakini itakua vizuri zaidi kama utajua tofauti zinazoitofautisha simu ya bei ya juu na bei rahisi.

Mambo unayotakiwa kujua kuhusu simu za mkopo BONYEZA HAPA>>>

Simu za bei ya chini na Simu za gharama

Makampuni kupanga bei ya simu

Simu za smartphone huwa zinaundwa na vitu vingi sana. Mpaka simu ya smartphone imetangazwa na kampuni kuwa imetolewa na watu wanaweza nunua, huwa inakua imeundwa na vitu vingi tena kutoka kwenye Makampuni mbili mbali. Vitu kama vioo, battery, processor au camera, vinaweza kuwa vimeundwa toka kwenye Makampuni mengine.


Kampuni ya simu inaweza kuwa imetumia gharama nyingi sana kupata vitu hivyo kwenye Makampuni mengine na utengenezaji wa teknolojia ya hali ya juu. kwaiyo inapoiuza simu hua inaangalia gharama hizo na gharama nyingine za utengenezaji ili kupanga bei itakayorudisha gharama za utengenezaji na kuleta faida pia.

Utofauti kati ya simu za bei ya juu na bei ya chini

Kampuni kama itatumia Teknolojia ya hali ya juu na vitu bora katika utengenezaji wa simu inaweza kuwa imetumia gharama kubwa pia. Jambo hili linaweza fanya simu iwe Bora alafu iuweze kwa bei kubwa. Hivyo simu za bei kubwa mara nyingi zinakua Bora na zimeundwa vizuri kuliko simu za bei ya chini japo sio zote.

Simu za gharama zinaweza kuwa na uwezo wa kufanya vitu vikubwa kwa haraka, Camera zenye ubora na vipengele vingine bora au vizuri kwa mtumiaji.

Lakini Kampuni huwa zinajua kuwa sio kila mtu anaweza fikia gharama za hiyo simu bora yenye gharama kubwa.

Huwa mara nyingi kampuni zinapotoa simu moja mpya, zinatoa matoleo mawili, matatu au zaidi. Matoleo haya hutofautiana bei na hata ubora au vitu utakavyofurahia ndani yake. Kunakua na matoleo ya juu ambayo huwa na bei ya juu na huongezwa majina kama vile “Pro” “Utra” au “Max” alafu pia kunakua na matoleo ya bei chini yanayoweza kuitwa “Mini”. Mfano kwenye kampuni ya Samsung kuna simu inaitwa “Samsung Galaxy S24”, lakini inatoleo la juu kabisa linaitwa “Samsung Galaxy S24 Utra”

Mbali na matoleo tofauti ya simu moja, Kuna kampuni hutoa aina ya simu ziliozo rasimi kabisa kwa lengo la kuuza bei ya chini.

Kuna watu husema “Simu za kichina ni bei rahisi alafu hazidumu” lakini ukweli ni kwamba china hutafuta njia za kupunguza gharama za utengenezaji wa vitu ili kuuza vitu kwa bei ndogo ambayo ni rafiki kwa mtumiaji. Lakini pia China huwa ina simu au bidhaa zenye ubora wa hali ya juu ambazo hudumu ila hupatikana kwa bei kubwa pia.

Unapaswa kuchagua simu gani?

Hakuna ulazima wa kuwa na simu yenye gharama kubwa wakati hauna uwezo au matumizi makubwa. Na pia hakuna ulazima wa kuwa na simu ya bei ndogo wakati unauwezo wa kuwa na simu ya bei kubwa yenye uwezo unaouhitaji. Kiufupi kuchagua simu ipi ya kununua ni uamuzi wako. Lakini kabla haujachagua simu simu, tambua unataka nini kwenye simu. Kama umepata simu inayokupa unachokitaka, haijalishi ni bei ya chini au juu, hiyo ni simu bora kwako. Ni vema ukaangalia zaidi kama inaendana na matumizi yako na sio kuwalidhisha watu.

Mguso Wa Dhahabu (Simulizi ya Sauti)

Karibu katika simulizi fupi ya sauti unayoweza sikiliza hapa The bestgalaxy. Simulizi hii inahusu Mfalme mpenda Dhahabu aliwahi hitaji kuwa mtu mwenye utajili kuliko watu wote Dunia.

“The Bestgalaxy” ni jukwaa maarufu linalotoa simulizi za sauti pia. Simulizi hizi zimeandaliwa kwa umahiri mkubwa. Kupitia The bestgalaxy wasikilizaji wanapata fursa ya kuingia katika dunia za kufikirika na kushuhudia matukio ya kusisimua, ya kichekesho, na hata ya kuhuzunisha. Mbali na kusikiliza, msikilizaji anaweza soma simulizi na kufurahia muda wake. Tunaweza sema The bestgalaxy inafanya iwe rahisi kwa mtu yeyote mwenye simu au vifaa vingine kufurahia burudani bora bila matatizo.

Mwanaume usimfanyie mwanamke mambo haya katika Mahusiano (Fikilia kwanza)

Ni muhimu kuzingatia na kuheshimu hisia na mahitaji ya mwenzi wako. Hili lina umuhimu mkubwa zaidi kwa wanawake, ambao mara nyingi wanahitaji uangalifu maalum ili kuhisi kuthaminiwa na kuungwa mkono ndani ya mahusiano na hata maisha kiujumla. Hapa The bestgalaxy ukurasa huu unaenda kukujuza mambo ambayo si vema ukayafanya kwa mwanamke unapokua nae kwenye mahusiano. Makala hii inaweza onekana imelenga mwanaume lakini kila mtu anaweza isoma. Mbali na hayo kuna makala nyingine tutakuja lenga wanawake pia na itaweza somwa na yoyote.

Katika Mahusiano mnaweza kutana na watu wenye tabia tofauti, mkaelewana na kuwa pamoja. Kuwa pamoja kama wapenzi kunaweza kuwa na mambo mengi sana mnafanya au kufanyiana. Mambo mengine yanaweza onekana mazuri na mengine yakaonekana wazi kuwa mabaya. Mengine yanaweza kuonekana mazuri au ya kawaida lakini ni mabaya baada ya muda.

Jinsi ya kumfurahisha mwanamke katika Mahusiano BONYEZA HAPA>>>

Mambo mwanaume kumfanyia mwanamke si vizuri

Usitoe siri au mambo mabaya ya mwanamke wako kwa wengine

Unaweza ukawa na mpenzi mwanamke mwenye mambo ambayo si vema kuyaonglelea kwa watu. Yanaweza kuwa ni mambo yanayofanya mtu amshushe thamani na kumchulikia vibaya.

Ikiwa unatabia ya kuongea mambo hayo kwa watu na bado upo nae kwenye mahusiano hata wewe unaemuongelea unakua unajichafua pia. Itakua ni vizuri kama utakua unatabia ya kutomuongelea vizuri mwanamke wako maana thamani yake ikiwa kubwa kwa watu na wewe unaonekana wathamani pia. Ni bora usimuongelee kabisa kuliko toa Siri au kumuongelea vibaya mtu ulienae kwenye mahusiano.

Usimshawishi kufanya mambo hatari kupinga ujauzito

Kama unampenzi na hamjafikia hatua ya kukubaliana kuzaa, basi hakikisha ukiwa kama mwanaume unakua mungalifu pia kwenye kuzuia ujauzito. Usiwe ni mtu ambae unaenda mara kwa kama hauoni au kuelewa mwanamke anatumia njia zipi alafu anakua makini kusisitiza mwanamke atumie njia hatari kuzuia matokeo ya uzembe.

Njia hatari zikizidi zinaweza msababishia mwanamke matatizo ya kizazi. Sasa unaweza muelewa kirahisi pindi atakapo patwa na matatizo hayo na kushindwa kupata ujauzito?


Ukiona mwanamke wako haelewi au anatumia sana njia za hatari bila kukushirikisha, hakikisha unamsaidia na kumuelimisha. Sio Kila mwanamke anaufahamu mzuri juu ya mambo ya uzazi. Fanya hivyo ili muuzuie ujauzito kwa njia salama na awe vizuri mpaka mtakapo amua kupata mtoto.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Usimpuuze bila kumsifia au kumpa maneno mazuri baada ya tendo

Baada tu ya tendo hasa la mara ya kwanza kwa mwanamke anaweza kuwa na mawazo mengi ya kutaka kujua kama yupo vizuri kwako au laa. Ukiendelea na mambo yako na kuondoa ukaribu baada ya tendo Hilo unaweza kumfanya mwanamke ahisi vibaya juu yake mwenyewe.

Kama ni mpenzi wako, hakikisha haumuachi kwenye Mawazo hayo kila mara. Jitahidi kukumbuka kumtafuta na kumpa maneno mzuri juu ya alicho kufanya na wewe. Hii pia inaweza kumfanya ajiamini au kuwa huru anapokutana na wewe tena kwenye tendo.

Epuka mahusiano ya muda marefu kama haunampango wa kumuoa

Kati ya mwanamke na mwanaume, mahusiano yakianza mara nyingi anaewaza mbali kuhusu mahusiano ni mwanamke. Anaweza waza kuhusu familia na hata watoto kipindi mahusiano hayajafikia hata kuishi pamoja. Hili sio jambo baya maana ni moja ya ndoto zao.


Unapokua na mwanamke kwenye mahusiano ya muda mrefu anaweza kuwa anawekeza sana akili yake kwako na kufanya amini utakua nae milele. Sasa kama hauna mpango wa kumuoa au kuwa nae maishani basi ni wazi mahusiano ya muda marefu ni maandalizi ya kumuumiza tu. Ikiwa hautaki kumuumiza mwanamke usie na mpango nae, mahusiano ya muda mrefu ni yakuyaepuka sana ili usimuuze. Usipofanya hivyo unaweza uumiza na kumpotezea muda wa kumtafuta atakae mpenda milele au kumuoa.


Mambo tuliozungumzia hapo juu yanaweza kuwa marahisi kusahau au kupuuza lakini ni mambo muhimu. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy na useache kuwa nasi.

Jinsi ya kutuma picha, video au sauti kwenye app ya sms za kawaida (Android RCS)

Kama unatumia simu ya smartphone ya Android, unapaswa kufahamu kuwa unaweza tumia app ya sms za kawaida zaidi ya ilivyozoeleka. Unaweza tuma jumbe za maandishi, sauti na hata kutuma video au kupokea vitu hivyo kwa watu wengine. Kama ilivyo kwenye app ya WhatsApp au Telegram ndivyo app yako ya sms za kawaida inaweza tumika. Hapa The bestgalaxy unaenda kujuzwa kuhusu jinsi ya kufanya hivyo ila kabla ya yote hebu tuelewe maana ya “RCS messaging” kwanza.


“RCS messaging” (Rich Communication Services) ni njia mpya ya kutuma na kupokea jumbe kati ya simu za smartphone. Njia hii hua inatumia data(internet) badala ya SMS za kawaida kwenye Lain yako. Kupitia huduma au njia ya RCS messaging, watu wanaweza tumiana vitu vingi ikiwemo video, picha na Audio. Kwa watu wa iPhone jambo kama hili walikuanalo kwenye app ya iMessages japo kuna utofauti.

Jinsi ya kutuma picha, video, sauti au kwenye app ya sms za kawaida (Android)

Unaweza kutuma picha, video au sauti kwenye app ya sms za kawaida kupitia RCS messaging. Kufanya hivi ukiwa na simu ya android utahitajika kutumia app ya sms ya Google). App hii inaitwa “Google messages”, inapatikana playstore. App hii kwenye baadhi ya simu inakuepo tu bila kuiiingiza(kuiinstall). Lakini kwenye simu nyingine inakua haipo hivyo, tutatakiwa kuingiza mwenyewe kutoka Playstore.
Kama unataka kuingiza app ya Google messages au kuanza kutumia RCS messaging kwa ujumla, unaweza fuata hatua zifuatazo;

  • Ingia Playstore utafute app inayoitwa “Google messages” kisha iingize kwenye simu. Kama tayari unayo fanya ku-Upate tu.
  • Baada ya hapo ifungue na kukubali Sheria za RCS messaging kwakubonyeza “Agree”. Kama itakuomba nafasi ya kuwa “Default SMS app” utatakiwa kukubali pia.
  • Baada ya yote kuwa sawa app ya Google messages, app hiyo inaweza kukuomba namba ya simu kwaajili kuanza kutumia RCS messaging. Jaza namba ya simu na baada ya hapo ukiwa na namba ya mtu ambae pia ameset RCS kwenye simu yeke, mtafurahia kutumiana video, picha na video kupitia app hiyo.
  • Kama haujaletewa sehemu ya kujaza namba, gusa profile au icon inayopatikana juu upande wa kulia kwenye app ya Google messages. Baada ya hapo ingia kwenye kipengele cha Settings cha app ya Google messages kisha changua RCS Chats na uiwashe RCS. Katika kuiwasha utaulizwa namba ya simu. Baada kuweka sawa namba ya simu utakua tayari umeanza kuitumia RCS messaging kwenye simu yako.


Faida za kutumia RCS messaging ni kupata uwezo wa kutuma na kupokea picha na video zenye ubora wa juu, Kuona mtu anapo andika ujumbe “Typing”. Mbali na hayo, mtumiaji utaona SMS ulizotuma kama zimefika au kusomwa(Delivery receipts). Unaweza kuunda magroup pia.

Kama utakua unahitaji mwanga zaidi katika hili, unaweza wasiliana na The bestgalaxy ukasaidiwa.

Jinsi ya kupata namba zilizofutika kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kulinda Ndoto zako Maishani zisife

Katika maisha, kila mtu ana ndoto ambazo anatarajia kutimiza akiwa hai. Ndoto hizi zinaweza kuwa kuhusu elimu, familia, au mambo mengine . Mara nyingi, safari ya kuelekea kutimiza ndoto inaweza kuwa na changamoto nyingi zinazohitaji uvumilivu na mapambano ili kuzitimiza. Wengi hukata tamaa na kushindwa timiza ndoto zao wakiwa bado waopo hai. Ni muhimu kufahamu mambo ya kufanya ili kulinda ndoto zako na kuhakikisha unafanikiwa kutimiza pamoja na changamoto nyingi utakazopitia njiani.

Kuna muda mtu unapokimbiza ndoto zako unakua na nguvu ya kuendelea kuzifuata. Lakini katika safari hiyo, Kuna muda mtu unaweza fikia hauna nguvu tena ya kuendelea kuikimbiza ndoto kutokana na mambo unayokutana nayo safarini. Inaweza fikia wakati mtu unaamu kupuuza ndoto yako kwa kuamini kuwa “haiwezi kuwa kweli” na kujiona mjinga kwa hatua zote ulizopiga ili kufikia.

Kama unandoto na unahitaji kutimiza, Hapa The bestgalaxy tunaenda kukupa mambo machache muhimu yatakayo ilinda ndoto yako isife kama ndoto za watu wengine.

Mambo matano yanayoweza kukusaidia kufanikiwa Maishani BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kulinda ndoto zako Maishani zisife

Vutiwa na mafanikio ya wengine bila kuchukia


Unapokimbiza ndoto yako unaweza kuwa unaona watu wengi wakitimiza ndoto zao wakati wewe bado. Kushuhudia wengine wakipata unachokosa inaweza kuwa ni jambo gumu kwa moyo. Unaweza jihisi vibaya na hata kuanza kuwachukia waliofanikiwa kwenye jambo ambalo wewe linakuumiza na haufanikiwi.
Ili kuzilinda ndoto zako ni vema ukavutiwa na kufurahia mafanikio ya wengine. Ukifanya hivyo itakua rahisi hata kujifunza mambo ambayo waliofanikiwa wameyafanya ili kufanikiwa. Lakini ukiwachukia utakua huoni la kujifunza na ukionawanaendelea kufanikiwa, utaumia na kupoteza muelekeo wako.

Unayoyapitia yanakuandaa kwa yajayo

Kila magumu unayopitia kwenye kuikimbiza ndoto yako, yanakuandaa kwaajili ya kutimiza ndoto unayoikimbilia. Hivyo haina haja ya kukata tamaa unapopitia magumu. Ukidondoka au kuumizwa, nyanyuka futa machozi, jiulize jambo hilo limekufunza nini kisha songa mbele. Kuna watu wanasema “hauwezi kuiona thamani ya kitu muhimu maishani ulichopata kama haujapata shida kukitafuta”. Vitu vingi vya thamani vinakua na ugumu kuvipata na huo ugumu ndio thamani yake.

Chagua mtazamo mzuri juu ya kifo

Upande wa kifo ni upande ambao watu wachache huuongelea linapokuja swala la kutimiza ndoto maishani. Watu wengi wanapokua wanaona Matukio kuhusu kifo katika mazingira yaliowazunguka, ndoto zao huyeyuka. Huwa wanakosa nguvu ya kuendelea kukimbilia ndoto zao huku moyoni wakijisemea “Duniani Tunapitia”. Hatugusii upande wa kidini ila Kama unandoto na upo hai jambo hilo lisiwe kisingizio cha kutotimiza ndoto yako. Amini vyovyote ila usitupe ndoto zako ukiwa hai maana ndoto zako zinaweza kuwa ni zaidi ya uhai wako. Mungu anaweza kuwa anataka hata kizazi chako kukibadilisha ila ni baada ya wewe kutimiza ndoto. Ndoto ya mtu inaweza kuwa ni kubwa kuliko hata Dunia ndio maana kuna ndoto watu walizikimiza wakajikuta wamebadilisha Dunia.

Kuwa na Sababu kubwa kuliko wewe ya kutimiza ndoto zako

Ili ndoto yako iwe imara na isije kufa kizembe, unganisha ndoto hiyo na mambo makubwa kuliko wewe. Unapofikilia Sababu za kuikimbiza ndoto yako, weka sababu kubwa ya kutimiza ndoto yako na sio vitu vidogo kama gari au nyumba. Fikilia kuhusu maisha ya watoto wako, familia yako na vitu vingine vikubwa na vya muhimu kama hivyo.

Fahamu hakuna binadamu anaona ndoto yako kama uionavyo

Hakuna binadamu anaeona vitu unavyoona au kufikilia. Hivyo hivyo hakuna mtu anaeona ndoto unayoikimbiza kama jinsi unavyoona wewe. Hivyo ukimuona mtu anakucheka, anakukatisha tamaa au kukudharau, usikate tamaa maana hakuna analojua kuhusu wewe na ndoto yako. Ndoto yako inakuhusu wewe hivyo unaiona wewe pekeako alafu watu wengine wanaona matokeo tu. Usihangaike na watu wanaokudharau, kuogopesha au kukukatisha tamaa, wewe endelea kufanywa kinachotakiwa kufanywa ili uwe unapotakiwa kuwa kwenye maisha yako.

Natumaini makala hii itakua msaada katika Maisha yako na huu ndio mwisho lakini The bestgalaxy inavitu vingi kwaajili yako. Endelea kuwa karibu nayo kwa mengine zaidi.