Category Archives: Uncategorized

Umuhimu wa kutumia Smartwatch katika Maisha ya sasa

Kuna vitu vingi vya kiteknolojia huwa vinatengenezwa na Makampuni lakini sio kila kitu huwa kina umuhimu katika Maisha ya kila siku au maisha ya kawaida. Katika upande wa vitu vya kiteknolojia vyenye umuhimu kwa sasa, Smartphone na Smartwatch ni kati ya vitu hivyo.


Watu wengi kwa sasa wanafahamu namna Smartphone zilivyona umuhimu katika Maisha ya sasa. Hivyo hatuta ongelea juu ya hilo hapa, ila tutazungumzia kuhusu Umuhimu wa kutumia Smartwatch katika Maisha ya sasa.

Smartwatch ni saa ambazo zinakupa mtumiaji uwezo wa kufanya mambo mengine ya kisasa mbali na yaliopo kwenye saa za kawaida.

Smartwatch huwa zinatofautiana uwezo na vipengele lakini kuna vipengele vya msingi ambayo smartwatch nyingi hazikosi kwakua ni muhimu kwa Watumiaji. Uwepo wa vipengele hivyo ni moja ya sababu za kufanya Smartwatch kuwa ni kifaa muhimu sana katika Maisha ya sasa.

Hapa chini tunaenda kuangalia umuhimu wa kutumia Smartwatch katika Maisha ya sasa. Tutakua tukifafanua kidogo na vipengele vya Smartwatch vinavyo husika pia.

Umuhimu wa kutumia Smartwatch katika Maisha ya sasa

Kupata mawasiliano kwenye matatizo

Smartwatch zinaweza kuunganishwa na simu ya smartphone alafu mtumiaji ukawa unapiga simu kwa kutumia kwenye Smartwatch (Saa). Mbali na kuunganishwa, Kuna Smartwatch ambazo zimeundwa kujitegemea katika mawasiliano na zinakuruhusu mtumiaji kuwasiliana na watu bila kuzihusianisha na simu yako.

Jambo hili kwenye Smartwatch linaweza kukupa urahisi wa kuwasiliana na watu unapokua kwenye mazingira hatarishi ambayo hauwezi tumia simu yako au wakati umeipoteza.

Kujua hali ya afya yako au kuitunza

Smartwatch pia ina vipengele vinavyo kuwezesha mtumiaji kujua hali ya afya yako na kuitunza pia. Kupitia kipengele cha “Heart rate monitor” Smartwatch zinaweza kukupa taalifa za mapigo ya moyo wako. Mbali na kipengele hicho Kuna kipengele unaweza angalia hali ya upumuaji wako na hata kutoa taalifa kwa watu pale unapodondoka kwa tatizo la kiafya.


Fall Detection ni kipengele kinaiwezesha saa kutoa taalifa kwa watu unapokua umedondoka kwa bahati mbaya. Kipengele hii inasaidia mtu kupata msaada wakati ambao hawezi hata kuomba msaada.

Kuelewa mizunguko yako

Kupitia kipengele cha Navigation katika Smartwatch, mtumiaji unaweza tambua mahali ulipo, unapo kwenda na ulipotoka. Kipengele hiki kinatumia GPS tracking kukupa taalifa za sehemu ulipo.
Endapo utakua unafanya mazoezi ya kutembea, kukimbia au kuendesha Toka sehemu kwenda nyingine, Navigation itakua msaada katika kufahamu mizunguko yako.

Kupata Burudani popote

Baadhi ya Smartwatch huwa na vitu ambavyo huburudisha. Mtumiaji unaweza furahia kucheza Games kwenye saa yako ukiwa popote bila kugusa simu yako. Mbali na games kuna hata Smartwatch zinazokupa uwezo wa kuperuzi mitandao ya kijamii na kusikiliza miziki.

Kupata msaidizi kwa haraka

Katika baadhi ya Smartwatch, kuna vipengele vya AI ambavyo zimelenga kumsaidia mtumiaji katika mambo mbalimbali. AI hizi zinaweza muwezesha mtumiaji kufanya mambo mbalimbali katika saa bila kugusa saa. Kwa kutumia sauti, mtu naweza washa mziki, kumtigia mtu na kufungua mambo mengine. Smartwatch zinaweza kuwa na Alexa AI na kuna Smartwatch nyingine zinakua Galaxy AI, Siri au AI nyingine.

Kama unahitaji kufurahia mambo yayo tulioyazungumza hapo juu lakini Bado hauna Smartwatch, basi kununua Smartwatch ni kunaweza kuwa ni uamuzi mzuri kwako.
Ni hayo tu katika The bestgalaxy, Endelea kuwa karibu na sisi.

WEUSI WEUPE (Simulizi ya Sauti)

Hapa The bestgalaxy tumekuletea simulizi iitwayo “WEUSI WEUPE”. Simulizi ya WEUSI WEUPE ni Simulizi inayoelezea kuhusu viumbe wa ajabu wanaweza kuishi katikati ya binadamu. Ni moja kati ya Fiction stories fupi na nzuri zilizo katika Lugha ya Kiswahili. Unaweza furahia kusikiliza simulizi hii, hapa chini.

Sehemu ya 1
Sehemu ya 2
Sehemu ya 3 (Mwisho)

Kusikiliza hadithi(simulizi) ni muhimu sana katika maisha yetu kwa sababu kunatusaidia kujifunza na kuelewa masomo ya maisha kutoka kwa wengine. Hadithi zinabeba maarifa, busara, na maadili ambayo yanaweza kutusaidia kufanya maamuzi bora na kushinda changamoto mbalimbali. Kwa kusikiliza hadithi, tunapata fursa ya kujifunza kupita maisha ya wengine, kujua mbinu walizotumia kukabiliana na matatizo, kuepuka makosa waliyoyafanya na hata kuburudika tena. Hii inatufanya tuwe na ufahamu mkubwa zaidi wa maisha na kutuwezesha kuboresha mienendo yetu.

Magame mazuri ya truck ya kucheza kwenye simu (Android)

Je, wewe ni mpenzi wa magari makubwa na unapenda kutumia simu yako ya Android kwa burudani ya games? Basi, hapa uko mahali sahihi. Katika dunia ya sasa, teknolojia imetupatia fursa ya kufurahia magame mengi ya truck moja kwa moja kwenye simu za smartphone. Muda huu, hapa The bestgalaxy wakati mzuri wa kuangalia game nzuri za truck zinazopatikana kwenye simu za Android.

Katika makala hii, tutaangalia game za truck ambazo yanakupa nafasi ya kuendesha magari haya makubwa katika mazingira tofauti na changamoto za kuvutia. Kuna game nyingi sana za mtindo huu lakini sio kila game la Truck ni zuri. Sisi hapa tutaangalia Magame machache mazuri tu. Ikiwa unatahitaji game zuri kutumia muda wako wa ziada kulicheza, unaweza changua kati ya yaliopo kwenye orodha yetu hapa bila kupoteza muda wako sana kutafuta.


Kabla ya kufika kwenye orodha yetu, ni muhimu kuelewa kwanini magame ya truck yamekuwa maarufu sana. Na pia haya magame sio tu yanakupa furaha, bali pia yanakusaidia kuboresha ustadi wako wa kuendesha na kushinda changamoto mbalimbali. Kwa hivyo, kaa mkao wa kula, tupo tayari kukuletea orodha ya magame bora zaidi ya truck kwa simu yako ya Android

Magame mazuri ya truck ya kucheza kwenye simu

Truck Simulator : Ultimate

Truck Simulator: Ultimate” ni game la simu ambalo linakupa fursa ya kusimamia biashara yako ya malori au truck. Katika game hili, wachezaji wanaweza kuendesha trucks tofauti ili kukamilisha misheni na katika mazingira tofauti tofauti. Muonekano wa mazingira na game kiujumla ni mzuri sana. Linaweza chezwa Online na offline pia.

Mbali na hayo, game la “Truck Simulator: Ultimate” lina kipengele cha multiplayer ambacho kinawaruhusu wachezaji kuungana na kushindana kutoka sehemu mbalimbali duniani. Jambo hii linafanya game kuwa na changamoto zaidi na kuongeza ushindani.

Truckers of Europe 3

Truckers of Europe 3” ni Offline game lililotengenezwa na Wanda Software, ambalo linakupa nafasi ya kuwa dereva wa lori katika bara la Ulaya(Europe). Mazingira yake ni mazuri na game pia limeundwa na picha nzuri sana ukilinganisha na baadhi ya magemu mengine.


Wachezaji wanaweza kuwa kwenye malori mbalimbali wakifanya kazi za usafirishaji na kupata pesa ambazo zinaweza kutumika kuboresha malori kwa ajili ya usafirishaji bora.
Wachezaji wanakutana na changamoto za kuendesha trucks barabarani kama vile hali mbaya ya hewa na barabara zenye vikwazo. Kiufupi, kama ni mpenzi wa game za malori au truck, hili game ni chaguo zuri pia.

Truck Simulator World

Truck Simulator: World” ni game la Truck la simu unalokuwezesha kuingia katika maisha ya udereva wa lori kwa kiwango cha kimataifa. Wachezaji wa game hili wanachukua kazi za usafirishaji, wanapata kupata mapesa au mapato na kutumia mapato hayo kuboresha malori yao.

Muonekano wa game upo vizuri pamoja na kuwa Offline game (haliitaji Data kucheza). Lakini unaweza cheza Online pia ili kufurahia kucheza game na marafiki au watu toka sehemu mbalimbali ulimwenguni.

European Truck Simulator

European Truck Simulator” ni game limetengenezwa na Ovidiu Pop na linakupa fursa ya kuendesha malori katika nchi mbalimbali za Europe. Wachezaji wanapata pesa kwa kukamilisha misheni za usafirishaji alafu wanazitumia pesa hizo kuboresha Trucks zao kama ilivyo kwenye game nyingine nyingi za Truck Simulator.


Ni moja ya magemu pendwa na tuck ambayo Mamilioni ya watu wanaotumia simu wanayapenda. Moja ya sababu game hili kuwa moja na magame pendwa ni uwezo wa kuchezwa bila Data. Sio lazima uwe na muunganiko wa internet ili kucheza game hili, unaweza cheza Offline na Online ukihitaji.

Mbali na games hizo, za truck, Kuna game nyingi sana unaweza jaribu na ukazipenda. Tumeziweka game hizi hapa ili kukurahisishia utafutaji wako tu. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine kuhusu games.

Sababu 5 za kukataliwa na Wanawake

Kukataliwa na wanawake ni jambo linaloweza kumkuta mwanaume yeyote, na mara nyingi linaweza leta huzuni na kuchanganyikiwa kabisa. Katika mambo mwanaume huogopa katika Maisha yake, kukataliwa na mwanamke ni moja wapo. Mwanaume anaweza mzawadia zawadi ya thamani mwanamke bila kumwambia anampenda kwasababu ya woga wa kukataliwa tu.


Kipindi cha nyuma baadhi ya wanaume wasio amini kuwa kuna maisha ya furaha baada ya kukataliwa na mwanamke, walikua wanajitupa hata kwenye maamuzi mabaya baada ya kukataliwa. Lakini kwa sasa watu wengi wameelimika na wanaamini kuna maisha yanaendelea baada ya kukataliwa na mwanamke.


Sababu za mwanaume kukataliwa ni nyingi na huwa tofauti. Na sio kila mwanamke husema Sababu ya kumkataa mtu, wengine huficha.
Katika Sababu hizo tofauti, kuna mambo au sababu huwa zinajirudia na wanaume wengi hukataliwa kwasababu hizo. Kama ni mtu ambae upo katika kipindi cha kutafuta mwenza wako, itakua vizuri kuzihafamu sababu hizi.


Kuzifahamu au kuzijua hizi sababu kunaweza kusaidia kuboresha mbinu zako za kumpata mwanamke unaempenda maishani. Katika makala hii ya The bestgalaxy, tunaenda zungumzia baadhi ya sababu zinaweza kusababisha mwanaume kukataliwa.

Sababu 5 za kukataliwa na Wanawake

Usafi au kutojipenda

Inasemekana kuna wanawake wengi wanavutiwa na mwanaume msafi anaejipenda. Kati yao, wanawake wengine huwa wanafikili mwanaume msafi ana anaejipenda anaweza kuwajali kama anavyojijali. Hapa ndio mara nyingi wanaume wanaoitwa “Mabishoo” huwa juu.


Usipo kuwa msafi na unaejipenda, unaweza kukumbana na changamoto za kukataliwa sana na wanawake. Mwanamke anaweza asikwambie moja kwa moja, lakini tatizo au sababu ya kukataa ikawa ni hiyo.

Kumuhitaji sana


Mwanamke anaweza sema anamtaka mwanaume anaempenda na kumjali lakini akawa na Wanaume wengi wanaomkata na wanapambana kumpata kwa kumfanyia vitu vingi vya kumjali ili awakubalie lakini anawakataa. Cha kushangaza, mwanaume ambae anaweza uteka moyo wa mwanamke wa namna hii anaweza kuwa ni mwanaume asieonesha kumuhitaji sana kama wengine.


Kiufupi baadhi ya wanawake hawataki mwanaume aoneshe uhitaji sana. Wanataka mwanaume anaewapa muda, anaewapa vimashaka mashaka kidogo lakini anaupendo wa kweli.
Kuonesha kumuhitaji sana mwanamke, kunaweza kufanya uonekane mjinga kwake na ukakataliwa.

Kutokujiamini

Wanawake wengi huvutiwa na mwanaume anaejiamni. Kujiamini kwenye maisha na mambo yako ukiwa kama mwanaume, kunaweza fanya wanawake wengi kuvutiwa na wewe alafu wakakukabari.
Usiwe ni mtu unaeonesha kutokujiami mbele ya wanawake. Kuna wanawake huchukizwa sana na mwanaume ambae hajiamni hata kwakuongea kinyonge tu kunaweza mchukiza.


Ukiwa ni mwanaume unaejiamni, mwanamke anaweza kukukubali na kuamini katika wewe. Kiufupi ukijiamni, wanawake watakuamni. Lakini katika kujiamni kwako hakikisha unaepuka kujisifu sana kwake.

Muelekeo wa maisha

Mwanaume anaweza mtongoza mwanamke bila kufikilia mbali kuhusu mahusiano na maisha. Lakini mwanamke anaweza mkubali mwanaume baada ya kufikilia mbali sana kuhusu maisha na mahusiano.


Mwanaume mwenye maisha mazuri au anaeweza kupambana kupata maisha mazuri anakua na nafasi kubwa ya kukubaliwa na wanawake. Unaweza mwanaume usiwe na pesa nyingi lakini upambanaji wako wa Maisha na muelekeo wako ukawa ni mzuri kiasi, utakubaliwa kirahisi.

Kukata Tamaa ya jibu zuri


Kuna wanaume hukata tamaa ya kuendelea kumfuata mwanamke ambae amekataa kuwa nae mara moja tu. Ukiwa ukiwa Mwanaume unaekata tamaa kwa kukataliwa mara moja, utakosa wanawake wengi sana wanaokupenda kwa dhati.


Baadhi ya wanawake hukataa unapowajia mara ya kwanza na kuwaambia hisia zako lakini moyoni mwao wanakupenda. Huwa wanakataa ili kukupima tu kama unaupendo wa kweli au unawajaribu. Yani wanawake wengine wanaweza kukubali baada ya kuwaelezea zaidi ya mara tatu.

Jinsi ya kutafuta simu iliyopotea au kuibiwa

Kupoteza simu ni jambo ambalo linaweza kumtokea mtu yeyote na linaweza kuwa na athari mbaya katika maisha yetu. Simu zetu zimejaa taarifa muhimu, picha za kumbukumbu, na mawasiliano ya shughuri zetu nyingine muhimu. Wakati simu inapopotea au kuibiwa, inaweza kuleta hasara kubwa, si tu kwa kwenye akili bali pia kwa taarifa binafsi na usalama wa mwenyewe simu.



Kuna mamilioni ya simu hupotea kila mwaka Duniani Kwasababu mbalimbali na wengi huwa hawazipati simu zao. Simu inapopotea, mtu anaweza kuingia kwenye hatari za kupoteza taarifa binafsi kama vile akaunti za benki, chats muhumu, na Akaunti za mitandao ya kijamii. Bila simu, tunaweza kupoteza mawasiliano na marafiki, familia, na hata kazi tunazofanya. Hali hii inafanya tukio la kupoteza simu kuwa na athari ya kufika mpaka kujaribu maisha ya mtu.



Katika ukurasa huu, tutaangalia njia mbalimbali ambazo zinaweza kukusaidia mtu kupata simu iliyoibiwa au kupotea. Njia hizi ni rahisi kufuata na zinaweza kusaidia kupunguza hasara na kurejesha mawasiliano yako haraka iwezekanavyo.

Game zenye muonekano mzuri za Online Battle Royale BONYEZA HAPA>>>

Njia za kutafuta simu iliyopotea au kuibiwa

Kuipigia au kutuma ujumbe kwenye namba iliopo kwenye simu

Njia ya kwanza unayoweza itumia kupata simu yako iliopotea na kuitumia ujumbe au kuipigia namba ya Laini (Sim card) iliopo kwenye simu. Kupiga simu kutafanya uongee na mtu alie na simu yako kama bado haijazimwa. Kama itakua haipatikani, tuma ujumbe au sms kwenye namba hiyo ili laini ikirudi hewani, upokee taalifa ya kuwa sms imefika (Delivered report) na kujua simu yako ipo imewashwa.

Hii ni njia nzuri na rahisi kuitumia kuitafuta hata simu ya batani ilioibiwa au kupotea.

Kutumia Find My Device kujua simu ilipo

Google Find My Device ni huduma ya Google ya Bure kabisa ambayo inawezesha watu kutambua simu zao zilipo kwa kuzionesha katika Ramani. Huduma hii inampa mtu nafasi ya kuifunga simu iliopotea au kufuta vitu vilivyomo ili visionwe na mtu mwingine.


Kutumia njia hii kupata simu iliopotea utatakiwa kudownload app iitwayo “Google Find My Device” kwenye simu nyingine. Baada ya hapo, utaifungua app hiyo na kujaza Email iliopo kwenye simu ulioibiwa kisha utaletewa taalifa za simu yako na sehemu iliopo.

Kama hiyo simu iliopotea itakua imeunganishwa kwenye internet alafu imewashwa Location, utafanikiwa kuiona ilipo na kuifuatilia. Lakini kama hivyo vitu vitakua vimezimwa, hautafanikiwa kuona simu yako ilipo.

Kwa watu wa iPhone, Find My Device ya Google haiwezi wasaidia maana ni maalumu kwa simu za Android. Ukiwa na iPhone utahitaji kutumia huduma kutoka Apple inaitwa “Find My” au “iCloud Find My Devices“.

Muonekano wa app ya Find My Device katika kuitafuta simu ya Infinix Hot 8 Lite iliopotea(Mfano).

Kutumia IMEI kupata Simu ilioibiwa

Utapatikanaji wa Simu iliopotea au kuibiwa ni ngumu kufanywa na mtu binafsi kwa njia hii. Jambo hili linahitaji uhusishe polisi na utatakiwa kuwa na Sababu ya kufanya hivyo maana police au vyombo vya usalama hawatakusaidia kama umeipoteza wewe mwenyewe kwa uzembe wako au umesahau ulipoweka. Ni vema kuwa na Sababu ya msingi na inayopelekeaa kuwahusisha polisi au vyombo vya usalama.

Mwisho ningependa kusisitiza swala la kuweka vitu vyako ikiwemo simu, katika hali ya usalama. Epuka kuweka simu yako mbali na mifuko yako au mikononi mwako unapokua mbali na nyumbani.

Picha za maneno ya hekima na misemo ya maisha

Kama huwa unapenda kusoma au kufuatilia maneno ya busara au maisha, hapa tunajambo lako. Laini kabla hatuja enda moja kwa moja kwenye jambo au lengo letu, ni vema ukatambua kuwa unachokifanya ni kitu kizuri.

Inasemekana kwamba mtu anapopenda kufuatilia vitu flani kwa kuangalia au kusoma, maisha yake yanaweza anza kuendana na mambo anayofuatilia. Japo sio watu wote lakini inasemekana kuwa maisha ya mtu yanaweza badilika kwa kufuatilia mambo flani kwa kusikiliza, kusoma au kuangalia.

Hiyo ndio sababu unaweza ona watu mpaka sasa wanasoma vitabu alafu utawasikia wakisema “Kitabu hiki kimebadilisha maisha yangu”. Ukiachila mbali kusoma, kuna watu huwa wanasikiliza vitu au kuangalia alafu mwisho, maisha yao yanabadilika kutokana hilo jambo alilokua analifuatilia.

Kiufupi vitu unavyofuatilia kwa kusoma, kusikiliza au kuangalia vinaweza kukutuia moyo usikate tamaa, kukuburudiasha ukafurahi na hata kukuelimisha ukabadirika.

Hapa chini tumekuandalia picha chache ambazo zina ujumbe kuhusu maswalia ya maisha kiujumla. Unaweza pitia moja baada ya nyingine kuangalia itajkayokufaa. Kama utataka download pia itakua sio jambo baya kwetu The bestgalaxy, unaweza fanya tu.

Mambo 5 husaidia kukimbiza mafanikio katika miaka 25 mpaka 38 BONYEZA HAPA>>>

Picha za maneno ya hekima na misemo ya maisha

Kwa kumalizia, “picha zenye ujumbe kuhusu maisha” ni njia bora ya kuwasilisha ujumbe muhimu kuhusu maisha kwa ujumla. Picha hizi, zimebeba ujumbe wa kweli kuhusu maisha na ujumbe huu unaweza kuendanda na hali za maisha ya watu wengi.

Unaweza wasambazia marafiki na ndugu unaowapenda picha hizi kupitia WhatsApp, Facebook na mitandao mingine. Ukishindwa kuzidownload, zipige screenshot.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Michezo ya kuchati na Mpenzi wako (Hufurahisha na kurefusha Maongezi)

Kuchati na mpenzi kwenye simu ni njia nzuri ya kuimarisha uhusiano na kujenga hisia za ukaribu kati yenu. Katika ukurasa huu, The bestgalaxy inaenda kukupa michezo michache ambayo mnaweza kucheza pamoja katika kuchati na Mpenzi. Michezo hii itasaidia kurefusha maongezi, kuburudisha na kuongeza furaha katika uhusiano wenu.

Kuna muda wapenzi mnaweza kosa kabisa mambo ya kuchati na hii hutokea mara nyingi. Lakini kama mmoja kati yenu atakua anauelewa juu ya michezo ya kuchati, mnaweza ianzisha na kufanya maongezi yaendele katika kuchati kwenu. Michezo hii ya kuchati ni mbinu nzuri ya kufanya maongezi yaendele katika kuchati kwa wapenzi. Kwa kiingereza michezo hii inaitwa “Texting Games” na ipo mingi sana japo hapa tutaangalia michezo michache tu.

Michezo hii michache ni rahisi na inahitaji muda mchache kumuelewesha mpenzi wako kama haijui unapotaka mcheze. Haina haja ya kuwa na vifaa maalum au kuwa pamoja kimwili ili kueleweshana. Endelea kusoma ili kuijuia na kuielewa michezo hii ya kuchati.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Michezo ya kuchati na Mpenzi wako wa kiume au wakike

Kwasababu nakupenda

Mchezo huu unachezwa na wapenzi ambao mnapendana alafu mmetulia mnachati kwa sms. Wapenzi mnatakiwa kuwa mnatumiana sms zenye ujumbe unaojumuisha maneno “Kwasababu nakupenda”.

Kwamfano; unaweza mwambia mpenzi wako “Nimekupa moyo wangu wote kwasababu nakupenda”. Huu ni mfano tu lakini mnatakiwa kutumiana sms za muundo huo zinazogusa mioyo yenu na kuelezea hisia zenu. Mchezo wa “Kwasababu nakupenda” unaweza kuwafurahisha na vilevile mtakua mnajenga mahusiano yenu kwa kuambiana mambo mazuri mnayoweza kufanya,mlio yafanya na mnayotaka kufanya Kwasababu ya upendo.

Maliza au taja wimbo

Mchezo mwingine ni huu unaitwa “Maliza au Taja wimbo”. Wapenzi katika mchezo huu mnakua manatajiana mistari ya nyimbo za mapenzi alafu kila anaetajiwa atatakiwa kumalizia mstari au kutaja jina la nyimbo aliotajiwa.

Kutuma mistari mitamu ya kisisimua, kutamfurahisha zaidi mpenzi unaechati nae kwenye mchezo huu.
Kwenye mchezo huu mnatakiwa kuwa ni watu mnaosikiliza na kufuatilia nyimbo za mapenzi. Kama ni watu wa namna hiyo, basi mnaweza furahia zaidi mchezo.

Jinsi ya kulinda Ndoto zako Maishani zisife BONYEZA HAPA>>

Kisia nilipo

Mchezo huu unachezwa na wapenzi na wanaucheza kwa kukisia mazingira ambayo wapo. Yani unaweza anza kwa kukisia sehemu alipo, anachokifanya na hata vitu vilivyo mzunguka. Yeye atakua anakwambia kama umekosea au umepatia.

Mtakua mnapokezana pale mmoja wenu anapopatia kukisia. Mchezo huu wa kukisia unakua mzuri zaidi kama watu wote ni wakweli alafu mnapendana kiasi cha kuweza kuumiza kichwa kufikilia na sio kutaja tu mnachojiskia. Kila mchezaji anatakiwa kufikilia jibu kulingana na anavyomjua mwenza wake.

Nishawishi tulale

Katika michezo, mchezo mzuri sana wa mapenzi katika kuchati ni huu. Mchezo wa “Nishawishi tulale” ni mchezo unachezwa wakati wa usiku unapochati na mpenzi.
Unachezwa kwa kuahidiana kuwa hamtalala na mtachati pamoja mpaka asubuhi. Kama mmoja anataka kulala kabla ya asubuhi, tatatakiwa kumshawishi mweza wake walale kwa kufanya au kumwambia jambo lolote litakalomshawishi mwenza wake.
Mtu anaetaka kulala aweza ahidi zawadi, akatoa maneno mtamu au jambo lolote litakalo mfanya mpenzi asietaka kulala, alale. Wachezaji wote mnatakiwa kujali sheria za mchezo na kutimiza ahadi zenu.

Mpelelezi

Machezo wa “Mpelelezi” ni mchezo wa kuchati ambao unahusu kuulizana maswali. Wapenzi mnakua mnapeana maswali kwa kupokezana na kila swali linatakiwa kujibiwa.

Idadi ya maswali inaweza kuwa 5 kwa kila mtu na hata 20 mkipenda. Kikubwa hapa ni kuulizana maswali mazuri yatakayo wafurahisha wote wawili.
Mchezo huu wa kuchati unaweza fanya watu mnaopendana mjuane zaidi ya mnavyojuana kwenye mambo mbalimbali. Ukipata nafasi ya kucheza mchezo huu, kuuliza maswali ya kusisimua na kujenga mahusiano yenu ni muhimu sana.

Michezo yote hii tulioiweka hapa ni rahisi sana kumfurahisha mpenzi wako wa mwanamke au mwanaume. Na huwa inafaida kubwa kwenye kujenga umahusiano ya wapenzi wanapenda kuchati. Unaweza ucheza na mume wako, mke wako bila tatizo lolote. Unaweza pia mtumia mwenza wako makala hii ili kuokoa muda wa kumulelezae ingawa ni vizuri kumuelekeza mwenyewe.

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy!

Jinsi ya kubadilisha Namba ya WhatsApp bila kupoteza Chats na vingine

Kubadilisha namba ya WhatsApp inaweza kuonekana kama kazi ngumu na yenye kuleta wasiwasi wa kupoteza mazungumzo yako muhimu, picha, video, groups na vitu vingine. Lakini, ukifuata hatua sahihi, unaweza kufanya mabadiliko ya namba kwa urahisi bila kupoteza chochote. Ni muhimu kwa kila mtumiaji wa WhatsApp kujua njia sahihi ya kubadili namba ili kuepuka kupoteza vitu muhumu.

Wapo watu ambao hubadilisha namba bila kutumia njia sahihi na huishia kupoteza vitu muhumu. Kwa kuliona hilo The bestgalaxy, tumeamua kuwasaidia watu hawa na watu wengine wasio jua njia sahihi.

Katika makala hii, tunakupa hatua za jinsi ya kubadilisha namba yako ya WhatsApp bila kupoteza data yako(Android). Kama hajui kuhusu hili na unataka kubadilisha namba, hapa utapata mwongozo wa kufanikisha unachohitaji. Lengo ni kuhakikisha unafanya mabadiliko haya kwa usalama, huku ukiendelea kufurahia matumizi yako ya WhatsApp.

Jinsi ya kuchati alieku-block WhatsApp BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kubadilisha Namba ya WhatsApp bila kupoteza Vitu (Android)

Kwanza unatakiwa kujua kuwa Akaunti yako ya WhatsApp na namba yako ya simu ni vitu viwili tofauti. Unapotumia WhatsApp inamaana una Akaunti ya WhatsApp iliofungukiwa kwa namba ya simu. Na namba ya simu inaweza badilishwa bila kubadilisha akaunti yako ya WhatsApp. Hii itakufanya usipoteze vitu vyako(Chats, Groups, na vingine). Kufanya hivi, fuata hatua zifuatazo;

  • Ingia kwenye WhatsApp na ubonyeze Vidoti vitatu vilivyopembeni juu.
  • Chagua “Settings” kwenye orodha ya chaguzi utazoziona.
  • Chagua “Account” kwenye chaguzi zitazokuja tena Kisha bonyeza “Change number”.
  • Bonyeza kitufe kilichoandikwa “Next” Kisha andika namba mpya na namba ya zamani kwenye ukurasa utaoletewa.
  • Baada ya kuandika namba kwa usahihi utatakiwa kubonyeza “Next” ili kuendelea na uthibitisho namba hizo. Utatakiwa kuthibitisha namba hizo kwa kupokea code watakazozituma. Ukiweza kuthibitisha, WhatsApp wataweza kubadilisha Namba yako na kama utashindwa kuthibitisha, hautaweza kubadili namba.

Uzuri wa kubadilisha Namba kwa njia hii ni kwamba, Rafiki zako na watu wengine ulioungana nao kwenye WhatsApp watajulishwa. Wataambiwa kuwa umebahatisha namba alafu watapewa na namba yako mpya ya WhatsApp.
Epuka kufanya mabadiliko kama haya kama hutumii WhatsApp rasimi.

Mbinu za Kutimiza Malengo yako ya Mwaka

Wanasema mwaka mpya huja na mambo mapya. Unapoanza mwaka, watu wengi hujiwekea malengo wanayotaka kutimiza ndani ya mwaka huo. Jambo hili huwa linafanywa na watu wengi sana Duniani lakini kufikia malengo hayo mara nyingi inakua sio rahisi kama wanavyotarajia. Katika mambo mapya mwaka mpya unayokujanayo huwa unajumuisha na changamoto mpya zinazoweza kuweka ugumu kutimiza malengo.

Lakini Swala la watu kushindwa kutimiza malengo ya mwaka, lisiwe chanzo cha kushindwa kuipamga au kuendelea kuipambania mipango yako ya mwaka. Jambo hili linatakiwa kuwa ni chanzo cha kuweka umakini katika mipango ya mwaka na kuhakikisha unapambana sana kuiitimiza.

Ni muhimu kuwa na mbinu sahihi za kuhakikisha kwamba malengo yako ya mwaka hayabaki kuwa ndoto tu, bali yanakuwa uhalisia. Katika kurasa hii ya The bestgalaxy, tutajikita kwenye mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kusaidia kutimiza malengo yako ya mwaka. Mbinu hizi zimewekwa hapa ili kukupa mwanga utakaokisaidia katika safari yako ya kufikia mafanikio unayoitaka kuyapata ndani ya mwaka. Kila mbinu itakusaidia kuweka malengo yako kwenye mstari sahihi kama utaitumia kwenye safari yako.

Jinsi ya kuzilinda ndoto zako Maishani zisife BONYEZA HAPA>>>

Mbinu za kutimiza Malengo yako ya Mwaka

Kuandika mipango yako na hatua


Watu wachache sana wanauwezo wa kukamilisha mipango ya muda mrefu bila kuandika. Wengi wasio andika huwa na malengo yanayo badilika badilika mpaka mwaka unaisha hawajui jambo gani walilopanga mwanzo wa mwaka.
Kitendo cha kuandika malengo yako huwa kinasaidia kutosahau kirahisi ulichokusudia kukifanya katika mwaka. Na hata ukisahau unaweza kumbuka picha nzima ya lengo lako kwa kusoma ulipoandika.


Ukishaandika hakikisha unakua na tabia ya kuandika mambo yako kwenye kila hatua unayopiga. Jambo hili litakusaidia kutimiza malengo yako ya Mwaka na hata usipotimiza utakua na mambo ya muhimu sana ulioyaandika kwaajili ya maisha yako ya Mwaka mwingine.

Kiufupi usiache kutumia karamu na karatasi kwenye maisha yako maana kichwa unachotegemea kukutunzia vitu vyako kinaweza kumbana na mambo mengi maishani. Mambo ya mitandao, matatizo ya familia na changamoto nyingine zote zinasubiri kuingia kichwani mwako.

Kuweka malengo chini ya miezi mitatu

Unataka kukifika mwezi wa 12 ndio uanze kufikilia kama mwaka huu umezembea au vipi? Acha hiyo tabia. Anza kujiweka malengo madogo ya miezi mitatu yatakayokua yakuonesha kama umezembea kabla haijafika mwezi wa 12. Yani gawanya lengo lako la mwaka kwenye miezi mitatu mitatu alafu kila mwizi mitatu ikifika unatulia unajiuliza “Nipo ninapotakiwa kuwa au nimezembea? Nifanye nini?”. Kufanya hivi kutakufanya uongeze umakini kabla ya mwaka haujaisha. Kama malengo yako yanaruhusu, unaweza weka hata miezi miwili na ikawa msaada kwako.

Fanya mambo kwa kasi kabla ya muda

Ikiwa unamipango migumu uliopanga na unatamani kuzitimiza, njia nzuri ya kuzitimiza ni kuanza kuipambania kwa kasi mapema. Yani kama kunajambo unatakiwa kulifanya kila siku ndani ya siku Saba(7) ndio ulitimize, Anza siku ya kwanza kwa kufanya kazi ya siku tatu. Kama ni kuweka pesa kiasi flani kila siku, Anza kwa kuweka pesa nyingi zaidi ya hiyo ya siku moja.

Kiufupi ukipata nafasi ya kufanya vitu vya kesho au kesho kutwa katika siku ya Leo, basi fanya Leo maana kesho kunaweza kuwa na changamoto ambayo bado haujaijua.
Kufanya hivi kutafanya uweze kupambana na changamoto katika safari yako bila kuiathiri sana safari uliojiwekea. Na vile vile tabia hii inaweza kukujenga ukawa mtu makini sana kwenye mambo yako.

Ahadi ya kubeba kila changamoto bila kukata tamaa

Usije msingizia mtu tena kuhusu wewe kushindwa kutimiza malengo yako. Jitahidi kubeba kila kitu kigumu utakachokutana nacho bila kutaka tamaa.

Tambua kuwa hakuna mwaka ambao hautakuja na changamoto. Hata waliofanikiwa wamefanikiwa lakini bado wanapambana na changamoto. Adui mkubwa wa malengo ya mwaka ni muda. Uheshimu muda maana ukizembea alafu muda wa mwaka uliojiwekea ukiisha, utakua umepunguza mwaka moja kwenye maisha yako ya Duniani lakini haujafanikiwa kukifanya unachokitaka. Sasa upo tayari kupoteza mwaka mwingine wa Maisha yako kumlaumu mtu au watu?

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kama makala kama hizi zinakua msaada kwako. Usisahau kuwa karibu nasi kwenye mambo mengine na kwenye mitandao ya kijamii pia.

Jinsi ya kutengeneza Logo ya biashara au binafsi BONYEZA HAPA>>>

Unajuaje kama Ex wako anakupenda? Dalili ni hizi

Mahusiano ya mapenzi yanaweza kuwafanya watu waamini kuwa watakua pamoja milele lakini sio kila mahusiano hufikia huko. Baadhi ya watu hushindwa kufikia malengo ya mahusiano yao baada ya kukumbana na mambo ambayo hutikisa au kuvunja mahusiano. Lakini pia sio kwamba Mahusiano yanayodumu huwa hayapitii mambo kama hayo, hupitia mambo magumu. Kuna watu huvunja mahusiano kabisa na kuitana “ex” lakini baada ya muda hurudiana tena na kuendelea kuwa pamoja. Kiufupi kurudiana na mpenzi wa zamani ni jambo la kawaida ambalo watu hufanya.

Kama bado mpenzi wako wa zamani unampenda, kujaribu kumuelewa mpenzi wako wa zamani inaweza kuwa ni changamoto. Wakati mwingine, mpenzi wako wa zamani anaweza kutoa dalili za kukupenda lakini kichwani kwako ukawa unawasiwasi na hauzielewi. Hapa katika The bestgalaxy, tutazungumzia kuhusu dalili za mpenzi wa zamani(ex wako) kukupenda. Kujua dalili hizi husaidia kumuelewa au kujua kama bado mpenzi wako anakupenda na kuna nafasi ya kurudisha upendo wenu ikiwa na wewe Bado unampenda.

Kujua dalili hizi kunaweza kukupa uwezo wa kujua hisia zake na kusaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu kurudisha uhusiano wenu. Wakati ukifanya hayo, ni vema kufahamu kuwa maamuzi ya kurudisha na mpenzi wa zamani yanaweza kuwa maamuzi mabaya pia kama hautafanya utafiti vizuri juu ya lengo lake kwako.

Mambo ya kuepuka baada ya kuachana na mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Dalili za mpenzi wa zamani kukupenda

Kuweka ugumu katika mawasiliano

Kuna watu mkiachana huwa wanakata njia za mawasiliano haraka na kukuwekea ugumu wa kuwapata lakini moyoni wanaokua bado wanakupenda. Mtu hufanya hivyo kwa msukumo wa hasira tu au ili aone unamtafuta na ajiridhishe kuwa anamuhitaji. Anaweza kublock kwenye simu na kukuwekea ugumu wa kukutananae lakini siku akiona umepambana na kukutananae mkaogea, atajisikia vizuri kuliko kawaida.

Mara nyingi hii hutokea endapo wewe ndio chanzo cha mahusiano kuvunjika. Adhabu anayokupa ni kuwa mbali na wewe kwa kukata ukaribu ili angalau uone umuhimu wake na kutambua makosa yako. Kupambana kumtafuta kunaweza fanikisha kurudisha uhusiano wenu.

Kukutafuta au kufungua njia za mazungumzo

Mpenzi wa zamani anaweza kuwa anakutafuta kwa njia mbalimbali na kufungua njia za mazungumzo kati yenu. Hii inaweza kuwa dalili ya mpenzi wa zamani kutamani murudiane. Anaweza kuwa anafanya hivi baada ya kukumbuka ukaribu wako na Mapenzi yenu kwa ujumla.


Kukupigia simu, kukutumia sms, kukuondolea block kwenye simu au kutafuta vinjia vingine vya kufanya maongezi na wewe ni ishara za kutaka murudiane. Wengine huwa wanashindwa kuficha kabisa hisia zao na kutaka mzungumzie mambo ya mahusiano yenu. Hapa ndio utasikia akisema mambo kama “Ulienae kwa sasa anafaidi… Umenifanya mapenzi niyaogope… Msalimie mpenzi wako” ili tu muongelee mahusiano yenu.

Wivu unapokua karibu na watu wengine

Njia rahisi ya kujua ex wako anakupenda au hakupendi ni wivu. Ni ngumu sana kwa mpenzi wa zamani kukuficha wivu wake anapo kuona na watu wengine. Kama hakupendi, anaweza asiwe na wivu ila kama anakupenda, moyo wake hauwezi muacha salama pindi unapooneka upo karibu na watu wengine. Anaweza kukosa amani au kufanya jambo lingine linaloonesha anawivu na wewe. Kama ni mtu wa “WhatsApp Status” basi wivu juu ya jambo aliloliona kwako atauweka kwenye Status yake kwa maneno ya kukuumiza au kuonesha ameumizwa.

Yupo makini sana na wewe au mambo yako

Ex anaekupenda anaweza igiza kukupuuza lakini hawezi kukupuuza kirahisi. Unapoongea nae anaweza igiza kukupuuza lakini huwa anazingatia kila neno. Mkiwa sehemu moja anaweza igiza kutokukuzingatia lakini macho na akili yake inakua kwako. Kuna muda unaweza gongana nae macho akiwa anakuangalia alafu akazuga kufanya mambo mengine. Yote ni kwasababu anakupenda na upo kwenye akili yake.

Ni hayo tu katika makala hii ya The bestgalaxy, kama utapenda unaweza Endelea kusoma makala nyingine. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi huku ukijiunga nasi kwenye mitandao ya kijamii.