Category Archives: Uncategorized

Jinsi ya kutafuta nafasi za ajira/kazi kwa kutumia simu mtandaoni

Kama ni mmoja kati ya watu wanaotafuta nafasi za kazi basi hapa kunakitu kidogo unahitaji kuwanacho kichwani katika miaka hii ukiwa katika mchakato wa kutafuta ajira. Unachotakiwa kujua ni kwamba teknolojia kupitia internet/mtandao imerahisisha mchakato wa kutafuta ajira na kuufanya uweze kufanyika katika kiganja chako kwa kutumia simu yako(Smartphone).

Unaweza tumia simu yako kuangalia nafasi za ajira unayoihitaji zilizojitokeza katika sehemu mbalimbali za dunia (Ndani na nje ya nchi). Na kama utapply au kufuata maelezo ya kuipata iyo nafasi na kubahatika kuipata, utakua ni mmoja wa mamilioni ya watu waliopata na wanaoendelea kupata nafasi za kazi kwa msaada wa internet. Kama unataka kutafuta nafasi za ajira/kazi kwa kutumia simu mtandaoni lakini haufahamu ni jinsi gani unaeza fanya hivyo, basi hapa chini nakupa mwanga juu ya hili kwa njia 3. Lakini kabla ya yote ni vema ukajua kwamba kunabaadhi ya nafasi za kazi au ajira ziwekwa na matapeli mtandaoni na maranyingi humuitaji mtaka nafasi atoe pesa ili kupata nafasi ya ajira… kuwa makini ni ajira za mtindo huo ili usije tapeliwa.

Njia za kutafuta nafasi za ajira/kazi zilizojitokeza kwa kutumia simu mtandaoni

Tafuta nafasi za kazi kupitia Google search

Watu tu hutumia google search kutafuta vitu mbalimbali kirahisi mtandaoni na imekua msaada mkubwa kwa watu wengi, nafikili hata wewe unaweza kuwa mmoja wa watumiaji wake mzuri. Mtu unaweza tumia Google kupata vitu vinavyokufurahisha, vitu vitakavyo kuelimisha na vitu vingine muhimu ikiwemo nafasi za ajira zilizojitokeza sehemu mbalimbali (Ndani na nje ya Tzanzania). Na nirahisi sana… kiufupi utatakiwa kuandika maneno yanayomaanisha nafasi za kazi, aina ya kazi na mahali(kwa kingereza ili kupata matokeo mazuri). Yaani unawezakwenda Google na kuandika “””””Aina ya kazi unayoitaka + jobs in + sehemu“”””” kisha ukitafuta na kwenye matokeo utapata orodha ya nafasi za kazi kulingana ulichokiandika. Kwamfano ukiwa unataka kazi ya “Customer care service” hapa Tanzania, utaandika “Customer care service jobs in Tanzania” kwenye matokeo utapata orodha ya nafasi za kazi za customer care zilizojitokeza Tanzania. Baada ya google ikukupa nafasi za kazi itakua ni kazi kwako kusoma maelezo ya kazi hizo ili kuzielewa zaidi na kuapply ikiezekana. Lakini unapotumia njia hii inatakiwa kufahamu kuwa Google ni search engine tu, hivyo huwa haina nafasi za kazi, inakupeleaka sehemu ilipopostiwa kazi…

Jiunganishe na blog zinazohusiana na mambo ya nafasi za ajira

Kuna blog ambazo hujihusisha zaidi na kutoa tahalifa kwa watu juu ya nafasi za ajira zilizojitokeza. Maranyingi huwa zinapost tahalifa za nafasi za ajira au habari zinazohusiana na mambo hayo hayo. Mfano mzuri ni Ajiraleo.com au Ajirampya360.com. Sasa kwakua na wewe unahitaji nafasi za kazi basi unaweza anza kuwa karibu na blog za mtindo huu ili wakitoa tu tahalifa za nafasi za ajira zilizojitokeza, zikupate kwa wakati na kuanza mchakato wa kuzichangamkia. Unaweza kuwa nazo karibu kwa kuzifuata blog hizo au kurasa zao katika mitandao ya kijamii ili kupata vitu wanavyopost.

Tumia LinkedIn

Linkedin ni mtandao kama vile Facebook au twitter lakini mtandao huu unakusanya wataalamu wa mambo mbalimbali na umejikitia katika zaidi maswala ya biashara na ajira. jiunga kwenye mtandao Linkedin bure kabisa na kwenye profile yako utatakiwa kujaza taalifa sahihi kuhusu wewe na utaalamu wako. Mambo unayotakiwa kuyafanya ndani ya mtandao huu ni vema yakawa yanaendana na utaalamu wako na jambo zuri ni kwamba unaweza kupata ajira kupitia mtandao huu… kurahisisha zaidi mchakato wa kutafuta nafazi za kazi, kunakipengele cha mtandao huu kinauruhusu kutafuta nafasi za kazi zilizojitokeza kulingana na uhitaji wako na kuapply.

Mbali na njia hizo tatu, kuna njia au vitu vingine zaidi unaweza fanya kupata taalifa za nafasi za kazi zilizojitokeza lakini huenda tutazungumzia katika sehemu nyingine, hapa tumekupa mwanga kwa hayo machache. Na ni vema kuendelea kutafuta nafasi za kazi nje ya mtandaoni pia. Ishi kwa kutangaza utaalamu wako. Endelea kufuatilia The bestgalaxy.

Jinsi ya kumueleza hisia zako Mwanaume bila kusema unampenda

Kuna mtaalam mmoja wa mambo haya alisema hivi…

Mara nyingi kuwa na aibu ndio chanzo cha wanawake wengi kushindwa kuwaeleza hisia zao kwa wanaume wanao wahitaji na kibaya zaidi wanawake tunaweza kutunza siri zetu kwa muda mrefu hivyo, hutunza pia hizo hisia kama siri nyingine japo hutuumiza sana pale wanaume tunaowapenda  wanapoenda kwa wanawake wengine.

Wapo baadhi ya wanawake ambao hawana uoga katika kueleza hisia zao kwa wanaume na pia huwa huru pindi wanapokuwa karibu na wanaume. Lakini wanawake wengi ni sisi ambao tunashindwa hata kuongea pindi tunapo wakaribia wanaume tunaowapenda.

Sio kwamba tunakosa ustadi wa kimapenzi wa kimapenzi au hatujui kutamka maneno ya kueleza hisia zetu ila ni tunasikia raha na furaha inayotuzidi mpaka tunaogopa maana mapigo ya moyo hupiga kwa kasi na maneno yote hupotea na hurejea baada ya mwanaume uondoka.

Kuwa na aibu hakupaswi kukuzuia kumueleza mwanaume unayempenda hisia zako. Kuna mambo madogo madogo ambayo unaweza kuyafanya na ukafanikiwa kufikisha ujumbe wa hisia zako kwa mwanaume unayempenda lakini kitu cha msingi inatakiwa kujiamini tu.

Badala ya kumfuata na kumwambia mwanaume vile unajiskia juu yake unaweza tumia njia ya vitendo itakayo mfanya kukuzingatia na kuelewa kuwa unamuhitaji na utamfanya akuhitaji pia.

1.Wasiliana nae kwa macho.

Kuwasiliana kwa macho ni moja wapo ya njia rahisi na ya hila zaidi ya kumruhusu mwanaume ajue kuwa unavutiwa naye. Wakati mwingine wazo la kuwasiliana na mtu usiempenda linaonekana kuwa la kichefuchefu, lakini ikiwa unafikiria ni mzuri, muangalie. Kama ni muoga sana basi jaribu kuangaliana na picha yake kwenye simu yako. Usimtazame kama wewe ni polisi na yuko kwenye orodha ya watu wanaotafutwa. Mtazamo mfupi ndio unahitajika yaani muangalia mpaka ugonganenae macho na agundue ulikua unamungalia kisha acha kumuangalia na uiangalie sehemu nyingine (ila usingalie chini kamwe) huku ukiendelea na shughuli zako. Kitendo hiki ukiwa unakifanya kitamfanya ahisi kitu juu yako na anaweza kuanza mawazo ya upendo juu yako.

Katika Matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi (Unaweza juta!) GUSA HAPA>>>

2. Weka tabasamu.

Pindi unapomuangalia hakikisha anakukuta na tabasamu zuri la kupendeza. Sio anakukuta unamuangalia huku umeweka sura ya kawaida tu utamfanya asihisi chochote juu yako na akakuona ni mtu unaemfuatilia mambo yake hivyo hakikisha unaweka tabasamu zuri litalomuonesha kufurahishwa na yeye. Akikukuta katika hali hii moja kwa moja atagundua umevutiwa nae.

3. Muulize swali kuhusu jambo flani.

Hii ni njia nzuri sana kwaajili ya kuanzisha mahusiano kati yenu.

Kuuliza swali kuhusu jambo flani au kuomba usaidizi juu ya jambo flani. Unaweza muuliza mwaswali ambayo yatamfanta ajibu kwa urefu au atumie muda wake kukuelekeza.

Mfano: Eliy, nimependa wallpaper ya simu yako, naomba nielekeze jinsi ya kuweka wallpaper kama yako?

Naomba nielekeze jinsi ya kufanya kitu hiki?

Njia hii pia utakusaidia kuanzisha mazungumzo nae yaani pale unapokosa neno la kuongea au kuanza mazungumzo basi unaweza uuliza kuhusu kitu flani.

Mbinu 6 zitakazo kusaidia katika mapishi yako GUSA HAPA>>

4. Mtege kwa kujichezesha.

Kila mwanamke anavitu ambavyo anajua vinamshawishi zaidi mwanaume katika mwili wake. Vitu hivi vinaweza kuwa ni lips nzuri, macho na vinginevyo. Vitu hivi unaweza vitumia pale ambapo unakuambele ya macho yake au unapogundua anakuangalia. Kuvitumia vitu hivi kunaweza kumchanganya mwanaume kisawa sawa mpaka akashindwa kuongea na kumfanya avutiwe na wewe zaidi.

 Mfano, unaweza zichezesha lips zako pindi anapokuangalia na kukuelekeza kitu fulani ulicho omba akuelekeze.

Kwakufanya vitendo Kama hivi kutachochea hisia zake kwako.

5. Toa maoni juu ya kile unachokiona kwake na pia usisahau kumsifia na kusifu anavyovipenda.

Kila mtu anapenda kusifiwa na  sikuzote watu huwapenda watu wanaowasifu pia unachotakiwa kujua ni kwamba  wanaume wengi huongeza juhudi katika jambo fulani pale wanaposifiwa yaani kama ni mchezaji mpira alafu ukawa unamwabia kuhusu uchezaji wake mzuri wa mpira basi utamfanya ajiskie vizuri mpaka ataanza kukualika mazoezini ili tu umuone anachokifanya na umsifie tena. Hivyo basi kumsifu inaweza kuwa njia nzuri ya kufanya avutiwe na wewe.

6. Usichukue vitu kibinafsi.

Ikiwa umemfanyia yote hayo na bado haoneshi matokeo mazuri juu yako, Usihisi kuwa wewe ni mbaya au hunamvuto. Huenda haoneshi dalili nzuri juu yako kwasababu hataki kukuchezea hivyo unapaswa kuheshimu pia mawazo yake na kuendelea na maisha yako huku ukimtafauta anaekupenda kwa dhati. 

Njia 3 za kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu yako

Kama ni shabiki mzuri wa mpira wa miguu unaweza kua ni mmoja wa watu wanopenda kufuatilia matokeo ya mechi mbalimbali katika ulimwengu wa kabumbu. Teknolojia imeisharahisisha mambo mengi sana katika soka. Kupitia simu yako ya mkononi unaweza kuangalia mechi live na ukafurahia, kiganjani pako!.. Mbali na nakushuhudia mechi live kiganjani pako, unaweza pia kuangalia matokeo ya mechi zilizochezwa au zinazoendelea kuchezwa hapo hapo kiganjani pako. Hii inasadia sana maana unaweza kua hauna muda wa kutulia na kuangalia mechi lakini lakini ukawa unajua mechi katika upende wa scoles ziko vipi.

Kuna njia zaidi ya moja zinaweza kutumika kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu na watu huzitumia kila siku yaani kuangalia matokeo ya mechi za leo, jana na siku zaidi hiyo. Hapa The bestgalaxy tunaweka wazi njia 3 unazoweza kuzitumia kuangalia matokeo ya mpira kwenye simu yako ya mkononi.

Njia 3 za kuangalia matokeo ya mechi za mpira kwenye simu

1. App na site/tuvuti maalum kwaajili ya kuangalia matokeo

Unapotaka kujua matokeo ya mechi mbalimbali kwenye simu yako, tambua kuna app za simu ambazo ni maalum kaajili ya matokeo ya mechi za mpira wa miguu na michezo mingine. Unaweza ingiza moja ya app za muundo huu kwenye simu yako na ukawa unatumia kuangalia matokeo ya mechi unazozihitaji kwenye simu. Uzuri wa app hizi ni kwamba nyingi huwa zinakua zinatoa huduma ya kukupatia matokeo bure kabisa japo kila utakapotaka kuzitumia utatakiwa kutumia internet. Mfano wa app hizi ni app iitwayo “LiveScore” na pia hii nyingine inaitwa “GOAL Live Scores”. Mbali na app izo kuna App ningine nyingi sana unaweza tumia kuangalia Scores. kwenyewe app hizi unaweza pia kufurahia vipengele vingine kama vile habari za michezo na ratiba za michezo.

Ukiachana na uwepo wa app, pia kuna websites/tuvuti unaweza tumia kuangalia matokeo ya mechi. App nyingi zinazojihusisha a matokeo ya mechi huwa ni za websites. mfano mzuri ni hii appp ya LiveScore; kuna website inatwa “LifeScore” na hiyo website ndio inaapp iitwayo “LiveScore”. kwahiyo hapo unakua uamuzi wako kuangalia matokeo mechi zako kupitia website au app.

2. Angalia matokeo ya mpira kupitia Google search

watu wengi hutumia google search kupata taharifa mbalimbali kwa haraka. Kunavitu ukivitafuta google unawezeza kuvipata kwa shida lakini sio matokeo ya mechi(hasa kama mechi inatambulika). Google inaweza kukupa matokeo moja kwa moja ya mechi ilioisha unayoihitaji bila mizungusho mingi. Na kitu kizuri ni kwamba kupitia Google unaweza pata taalifa nyingine kuhusu mechi kirahisi sana na bila kupoteza muda wala kutumia bando sana kama baadhi ya njia nyingine. Unaweza tumia njia hii kuangalia matokeo ya mechi za simba na yanga bila utata.

3. Angalia scores kwenye app au tuvuti za kubeti

Ukiachana na njia hizo mbili ambazo unaweza tumia kuangalia scores, njia ya tatu ni kucheki scores kupitia app au tuvuti za kubeti. Kama wewe ni mtu unaebeti kupitia simu, hainaaja ya kujitesa kuangalia matokeo ya mechi zinanoendelea kuchezwa. Unaweza kuangalia kirahisi kupitia kipengele cha “LIVE” katika website au app ambayo unaitumia kubeti. Kipengele hiki huwa kinakupa taalifa za mechi zinazochezwa muda huo na Moja ya taalifa utakazo zipata ni pamoja na magoli. Kipengele hiki ni kwaajili ya kubeti lakini unaweza kukitumia kuangalia scores za mechi unazozijitaji.

”kwanini wanawake wazuri/warembo hawaolewi?” sababu zinaweza kuwa hizi

Mara nyingi wanawake warembo na wenye mvuto wa kumvutia kila mwanaume huishia kuzisikia ndoa kwa wenzao tu kutokana na sababu mbalimbali.

Wengi huwa na tabia ambazo huudhi na huwaogopesha wanaume wanaowahitaji bila wao wenyewe kujijua.

Ivi unaweza kuchagua kuwa na kitu chenye muonekano mzuri maishani mwako kitakachokupa shida na maumivu milele?

Ikiwa watu hushindwa kuvumilia kuishi na vidonda vinavyowapatia nyumba, magari na pesa, unafikiri urembo/uzuri unaweza kuwa na nini cha ajabu kwenye maisha?

Wanaume huwa sio wajinga na katika asilimia kubwa ya wanawake wanaoolewa huwa ni wanawake wa kawaida sana ukiwaangalia kwa macho jinsi walivyo, mpaka unakuta wengine wanajiuliza “mbona kamchagua mwanamke wa kawaida sana pamoja na malizote zile?”

Ukiwa mrembo/mzuri utapendwa na wanaume wengi ila watakupenda kwa lengo la kupata Penzi tu, baada ya hapo utakuwa wa kuchezewa na baadhi ya sababu zinazopelekea wanaume kufanya hivyo ni zifuatazo;

Tabia

Wanawake kama hao huwa na tabia mbaya na nikiongelea tabia mbaya basi najumuisha uvaaji, ukaaji, viwanja vya starehe, lugha zisizo nzuri na marafiki pia. Vitu hivyo humtenganisha mwanamke mzuri na wanaume wa oaji. Labla akutane na mtu wa tabia yake lakini asilimia kubwa ya wanaume wenye tabia hizo huwa wanatafuta wanawake waliotulia huku wakiendelea wanawake warembo wasio tulia. Wanaume wengi huwa hawapendezwi na tabia za aina hiyo hata mwanamke awemrembo kiasi gani.

Kuwa na maringo sana

Unakuta mwanamke ameweka kucha ndefu, nzuri,za kuvutia na anamaringo kiasi kwamba mwanaume mwenye mpango wa kuoa akimuona anajiuliza 

“Sasa kwa hizi kucha atanifuliaje nguo?… Anamaringo sana sijui itakuaje tukipishana?… Anaanzaje kuosha vyombo?… Ivi atakubali kutulia na kulea mtoto?.. Inaonekana hata kupika hajui”

Mwisho mwanaume anaona hafai wala haoneshi tabia zozote za mwanamke ambae anatakiwa kukaa katika nyumba.

Katika Matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi (Unaweza juta!) GUSA HAPA>>>

Ghali kuwatunza

Wanawake warembo huwa ghali kuwatunza kwa sababu wamejiwekea dhana kuwa wanafaa kupelekwa katika hoteli kubwa kubwa na maeneo yaliyo na bidhaa ghali. Huwa hawalegezi msimamo hasa kuhusu mahitaji yao na wanakotaka kwenda kununua bidhaa.

Mwanaume akipiga hesabu za haraka haraka kuhusu ghalama ambazo anatumia kipindi cha ambacho yupo na mwanamke mrembo anaependa kulidhishwa kwa kufanyiwa mambo makubwa huwa anagundua kumuoa ni sawa na kubeba mzigo mzito sana kichwani.

Ni wabinafsi

Wanawake wa aina hiyo huishi wakifikiria dunia ni yao na kwamba wanafaa kuabudiwa na kila mwanamume. Wanaume wengi hupenda kuwa katika mahusiano nao na hii ndio sababu kubwa ya wanawake hawa kujiona wa hali ya juu sana.

Wasichojua ni kuwa wanaume huwatumia tu na kuwaacha kutokana na tabia zao ili kutafuta mwanamke mzuri wa kuoa. Kibaya zaidi ni kwamba, wanawake hawa huendelea kutiwa moyo na uzuri wao huku wakisahau kuwa umri walionao hauwasubiri.

Hawataki kuwa wazazi

Wanawake hao hupenda kusalia wakiwa wanapendeza, hivyo huwa wanaogopa kuzaa wasipate mikunjo, wasinenepe au kuwa na matiti kulegea. Kwa kawaida, hakuna mwanamume anayependa kuoa mwanamke ambaye hawezi kumzalia, hasa kwa sababu ya utamaduni wa Kiafrika. 

wavivu kutatua changamoto za mahusiano

Kuna wanawake ni warembo na wazuri sana kiasi ambacho wanaume huwafananisha au huwasifu kuwa ni kama malaika. Kutokana na kusifiwa sana hujiona wazuri sana na hupenda kuwa kama yai kwenye mahusiano. Ukweli ni kwamba hata uwe mzuri vipi, kuna changamoto utakutananazo kwenye mahusiano. Nikizungumzia changamoto inaweza kuwa umekuta mweza wako kabadilika ghafla au kunajambo limetokea katiyenu na linafanya musielewane. Wanawake wazuri wanapokutana changamoto hizi huwa hawajisumbui kutatua changamoto…. Wanaona bora kubadilisha mwanaume kuliko kutafuta njia inayoweza rekebisha mahusiano yao hatakama wao ndio chanzo cha kuyumbisha mahusiano. Hali hii inawafanya wawewanabadilisha tu wanaume na hawafikii hatua ya ndoa… Na hata wakiingia kwenye ndoa huwa sio wavumilivu maana ndoa inachangamoto nyingi zaidi.

Sasa kama una sifa za aina hiyo, huenda ni wakati wako kubadilika ikiwa unataka kupata mume. 

Mbinu 6 zitakazo kusaidia katika mapishi yako

Moja ya jambo muhimu sana kwa mtu anaependa kupika vyakula vizuri ni ubunifu. Kwaiyo kama unaependa kuwa mtu unaepika chakula kizuri basi zingatia zaidi katika ubunifu wa mapishi na kujua jinsi ya kukianda chakula katika mitindo mbalimbali. Na mara nyingi hii katika kukipika chakula ndio huwatofautisha wapishi na kuamua nyupi ni bora zaidi na kama ni mama wa nyumbani basi tambua kuwa mapashi ya kibunifu na mitindo mbalimbali yanaweza ifanya familia ikifurahie chakula na kujenga afya pia. Tukiachana na maswala ya hayo, hapa tumekuandalia mbinu au mambo unayoweza kuyafanya ili kurekebisha mapishi yako yanapokua vibaya au kurahisisha upishi wako.

Mbinu 6 zitakazo kusaidia katika mapishi

1. Mchuzi ukizidi Maji na kuwa mwepesi, kwangua kiazi mviringo kwenye kikunio cha nyanya weka katika mchuzi wako ili kuufanya uwemzito.

2. Chumvi ikizidi kwenye chakula weka kiazi mviringo kilichomenywa katika chakula ili kupunguza chumvi.

3. Laza maharage yanayochelewa kuiva kwenye chupa ya chai yenye maji ya moto kisha asubuhi chemsha kwa dakika 30 tu yatakuwa tayari yameiva (yataiva haraka)

4. Ukimaliza kuosha vyombo kwa kutumia Still Ware,itunze still ware kwa kuiweka kwenye Maji ili isiharibike na ifae kwa matumizi ya kesho.

5. Ukiunguza wali kata kitunguu maji nusu kisha weka kwenye wali na ufunike kwa dakika tano. Kitunguu maji kinasaidia kutoa harufu ya moshi

6. Mchuzi wa maini ukitaka uwe rost nzito au mchuzi wowote na hauna nyanya za kutosha… Weka kijiko kimoja cha chakula cha unga wa ngano ukoroge na maji kidogo alafu weka kwenye mchuzi kisha acha uchemke dakika 5

Katika Matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi (Unaweza juta!) GUSA HAPA>>>

Jinsi ya kuweka kitu WhatsApp status bila mtu au watu flani kukiona

Kama huwa unaambiwa umuweke status kitu lakini unashindwa kwasababu mbalimbali na kupelekea kutoelewana kati yenu au unakitu unahitaji kuiweka status bila watu au mtu flani kujua basi leo nakufundisha jinsi ya kufanya hivyo.

WhatsApp status ni kipengele cha WhatsApp ambacho mtu hutumia kupost vitu mbalimbali ambayo huonwa na watu wengine walio na namba yake kwenye simu kama alivyo nazo zao yeye kwenye simu yake. Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba katika kipengele hiki unauhuru wa kuchagua mtu au watu gani waone status yako na watu gani wasione… Hii inamaanisha unaweza chagua watu au mtu pekee unahitaji aone status yako kisha ukapost kitu kwenye status yako na akakina yeyetu.

Unaweza fanya hivyo kwa kufunya yafuatayo;

  1. Fungua app ya WhatsApp kisha gusa vidoti vitatu vilivyo juu kulia.
  2. Utakuta orodha ya maneno machache, Chagua “Settings” Kwakuigusa.
  3. Katika settings utakuta orodha pia, Chagua “Account” Kwakuigusa na itakuletea orodha tena chagua “privacy”
  4. Ukisha chagua privacy, utakuta orodha tena,Chagua neno “Status” Kwakuigusa
    Hapo utaletewa orodha hii:

My Contact
My Contact except..
Only share with…


orodha hii inakidoti ambacho wewe unachagua kiwe katika nenolipi kati ya hayo.Na kidoti hicho utakikua kwenye “My Contact” wewe inabidi upeleke kwenye “Only shere with..”
ukikipeleka hapo itakuletea namba za watu wako kwenye simu,inabidi umchague yule unaetaka aione hiyo status alafu gusa “Ok” kisha “Done”
ukisha maliza nenda kaposti hiyo status, nenda kapost kitu anachotaka kwenye status yako na atakiona yeye tu!

Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Fanya haya baada ya kondomu kupasuka katika tendo

Mpira wa kondomu hutumika katika tendo la kujamiiana ili kuzuia mimba na vile vile hutumika kwa lengo la kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi na magonjwa mengine ya zinaa. 

Katika utumiaji wa mipira ya kondomu kupasuka kwa kondomu hutokea mara nyingi Sana bila kutarajiwa. Mara nyingi kitendo hiki husababisha mimba zisizotarajiwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa. Hapa kuna hatua nne unazoshauriwa kuzifuata iwapo kondomu imepasuka:

1. Kuwa mtulivu na tafuta kondomu hiyo iliopasuka.



Mara nyengine kwa mwanamke vipande vya mpira huo wa kondomu vinaweza kuingia ndani ya mwili.

Ingiza vidole vyako ndani ya mwili, vishike na kuvitoa nje.

Mipira ama vipande vya kondomu vinavyosalia ndani ya mwili wa binadamu vinaweza kusababisha hasara hivyobasi ni muhimu kuangalia na kuhakikisha kuwa umetoa kondomu yote.

2. Tumia dawa za kuzuia kushika mimba iwapo hamjakubaliana kupata mtoto(Kwa mwanamke)



Dawa hizi zinapaswa kutumiwa katika kipindi cha saa 72 tu. Zinauzwa madukani yaani zinapatikana katika maduka ya dawa.

Iwapo huna mpango mbadala unaweza kutumia dawa za kupanga uzazi.



3. Kupimwa magonjwa ya zinaa hususan HIV iwapo hujui hali ya mwenzako




Nenda katika kituo cha dharura karibu nawe na umwambie daktari yaliofanyika.

Pia unaweza kuchukua dawa aina ya Post Exposure Prophylaxis (PEP) katika kipindi cha saa 72.

PEP ni mchanganyiko wa dawa za kukabiliana dhidi ya virusi vya ukimwi ambazo zinakuzuiwa kutoambukizwa HIV iwapo mwenzako ni mwathiriwa.

Kumbuka kwamba kila ugonjwa wa zinaa una muda wake wakati unapoambukizwa na wakati utakapoonyesha unapopimwa.

Unashauriwa kufanyiwa vipimo zaidi vya vya magonjwa ya zinaa baada ya mwezi na baada ya miezi sita ili kujua hali yako.



4. Jiulize kuhusu kilichosababisha na usirudie kosa.





Wapenzi wengi huruka hatua hii bila kujua kuwa hayo ni makosa makubwa, kwa sababu utakapoelewa ni kwa nini mpira huo ulipasuka ndipo unaweza kujiweka vizuri katika mchezo mwingine. Hivyobasi jiulize kuhusu hilo.

Vunja mbavu sms za vichekesho (soma hapa)

BANGE SIO CHAI..

Siku moja Nyani alikuwa kakaa kijiweni anavuta bangi,Mjusi(lizard) akaja akampa “Hi” akajiunga na kumuomba puff.

Nyani akamuonya kuwa ile bangi ilikuwa ni kali sana,ni kipisi cha kutoka Milimani huko. Mjusi akapokea wakaanza kuvuta bangi kwa raha zao…baada ya muda mjusi akawa hoi kwa stimu akamuambia nyani “Duh nasikia koo langu limekauka acha niende mtoni nikanywe maji!”

Mjusi kufika mtoni kwa kuwa alikuwa na stimu nyingi akatumbukia mtoni. Bahati nzuri Mamba alikuwa pembeni, akawahi kumuokoa mjusi na kumtoa nje ya maji.

Baada ya kumuokoa, Mamba akamuuliza mjusi “Ina kuwaje bro mbona umetumbukia mtoni kipuuzi vile?” Mjusi akajibu “Nilikuwa na nyani tunavuta bangi nikasikia kiu ya ajabu nikajikuta kwenye maji bila kujua!” Mamba akasema “Aaah wacha niende huko kwa nyani nikamuone.”

Mamba kufika akamkuta nyani ndo anamalizia kipisi chake,kazidiwa hata macho ni tabu kufungua. Mamba akamuita “Oya” Nyani akafungua macho,kumuona Mamba akashtuka Et”Duh! Mshikaji kwani umekunywa maji yote mtoni! Mbona umerudi mkubwa hivyo!!”

SIPATI PICHA INGEKUAJE…

Jamaa yangu mmoja alikuja kunitembelea kule Mburahati Madoto. Sasa wakati namsindikiza tukafika kituo cha madoto mwisho

kusubiri daladala. Mara jamaa yangu akanyewa na kunguru kichwani. Jamaa akaangalia juu alivyogundua amenyewa akamuona

kungulu usawa wake, jamaa akaangua kicheko sana yaani. Mi nilikuwa naona yote yanayotokea nikamuuliza “sasa unacheka nini

ndugu yangu wakati umenyewa?” Jamaa akajibu “We acha tu, afadhali bata hawapai angani kama kunguru”

AMRI KUMI KWA WAPENDAO OFA

  1. Muheshimu anayekununulia
  2. Muamkie mtoa ofa kabla hujakaa kitini
  3. Uwe ndie mchekeshaji wa kikao, lakini usimkatishe mazungumzo anaetoa ofa
    . Mtoa ofa akikutuma popote usikatae
  4. Mtoa ofa akiupenda muziki fulani, we anza kucheza kwa bidii kabisa
  5. Usinywe kwa pupa, kunywa mafunda madogomadogo
  6. Mtoa ofa akitoa kichekesho cheka sana hata kama hakichekeshi

Jinsi ya kuongeza speed ya internet kwenye simu

Unasumbuliwa na speed ndogo ya internet? Usiwe na wasi tena! Hapa The Bestgalaxy tunakufungua juu ya nini unachoweza kukifanya kufurahia internet nyenye kasi kwenye simu yako ya smartphone.


Moja ya vitu ambavyo huudhi katika katika matumizi ya internet ni speed/ kasi ndogo. Speed ndogo ya internet sio tu huudhi bali pia hupoteza muda wa mtu anaetumia internet kwasababu kitu ambacho alitaka kukifanya kwa dakika 1 kwenye internet kinaweza mchukua mpaka dakika 5 ikiwa speed ya internet itakua ni ndogo. Watu wengi wanao thamini muda huchukizwa na swala hili.


Lakini tukirudi kufikilia kahusu historia ya internet utagundua internet imebadilika Sana na huwezi fanananisha na kipindi cha nyuma. Hata internet ya sasa isumbue vipi kwenye speed lakini huwezi ilinganisha na zamani maana huko nyuma internet ilikua haina kasi kabisa kama ya sasa. Kudownload nyimbo Moja tu yenye Mb 5 ilikua inaweza kukuchukua mpaka saa 1. Kama ni mtumiaji wa muda mrefu wa internet unaweza kuwa unajua kuhusu hili.

Yafuatayo ni mambo ambavyo Unaweza fanya kuongeza speed ya internet kwenye simu yako (hayahusishi matumizi ya WiFi)

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Namna ya kuongeza speed ya internet kwenye simu

1. Hakikisha unatumia laini ya 4G au 5G na Simu 4G au 5G

Kwasasa ukitaka kufurahia kasi nzuri ya internet basi inatakiwa iwe ni kuanzia kasi ya 4G. Ukitaka kufurahia kasi hii ya internet kwenye simu yako ya smartphone inatakiwa iwe na laini ya 4G na pia simu yako iwe ni ya 4G au 5G. Mbali na havyo pia ni vema “preferred network type” yako ikaiseti kwenye “Auto“. Kuiset preferred network type kwenye simu yako nenda kwenye “settings” ingia kwenye na uende katika “Network & internet” alafu ingia kwenye “SIM cards” kisha ingia kwenye “Mobile network“. Baada ya hapo gusa “Preferred network type” na uchague “Auto“.

2. Hamia kwenye mtandao wa simu wenye huduma ya internet yenye kasi.

Kuna muda mtu anaweza kuwa unakumbana na changamoto ya kasi ndogo ya internet katika matumizi ya internet kutokana na mtandao wa simu unaokupa huduma ya internet kutokua vizuri katika maeneo uliopo. Jaribu kufanya utafiti kwa watu uwalio kuzunguka ili kujua mtandao wanotumia kupata internet na speed yake ya internet iko vipi. Unaweza tu kuwaambia watu “Mimi ninatumia mtandao flani kupata huduma ya internet lakini naona Kama haupo vizuri Sana katika speed kwenye maeneo haya… Ivi ni mtandao gani nyinyi mnautumia na upo vizuri?”

Fanya haya kabla simu yako haijaibiwa ili kuipata ikiibiwa GUSA HAPA>>>


Kama kutakua na mtandao wanao sema upo vizuri basi jaribu na uangalie kama utakua vizuri kwako pia. Unaweza pia wasiana na watu wanao husika na mtandao wako wa simu na kuwataalifu kuhusu Jambo unalopitia kwenye eneo lako ili warekebishe. Tena bahati nzuri ni kwamba sikuizi makampuni ya mitandao ya simu ina kurasa zake katika mitandao ya kijamii na Unaweza watumia ujumbe kule na wakakujibu.

3. Boost speed ya internet kwa kuwasha “Flight mode” na kuizima.

Kama speed yako ya internet inasubua subua wakati unaitumia unaweza kuwa unaiboost kwa kuwasha “Flight mode” na kuizima. Flight mode huwakilishwa na kialama Cha “ndege ya usafiri” na hupatikana katika kisehemu Cha simu unachokifuata pindi unapo washa Data kwaajili ya kuanzia kutumia internet.

4. Tumia app zinaweza ongeza Speed ya internet.

Kuna baadhi ya app za VPN zinaweza ongeza speed ya internet. Hii inaweza onekana zaidi unapo download vitu au ku-stream vitu online ukiwa unatumia VPN. Lakini app za VPN zipo maalum kwaajili ya kuufanya muunganiko wako wa internet uwe salama na si kuongeza speed. Na pia sio kila unapotumia VPN utapata internet yenye kasi, VPN zinaweza pia kupunguza kasi kabisaa.

Mbali na app za VPN pia Kuna app zinazohusisha zaidi DNS zinaweza kuongeza kikasi Cha internet unapotumia. Mfano mzuri ni app iitwayo WARP… Unaweza ijaribu kwuingiza kwenye simu yako ya Android kwa lugusa hapa au iPhone kwa kugusa hapa

SMS za mchana mwema kwa mpenzi wako

Ukiwa kwenye mahusiano Unaweza kufanyia vitu vingi kwema kwa mweza wako ili kuonesha unamjali. Kutumia ujumbe wa mapenzi mpenzi wako ni Moja ya Jambo linaloonesha kujali pia… Mukiwa ni wapenzi mulio mbali hii inaweza kuwa ni kitu muhimu kinachojenga mahusiano kuliko hata kutuma tuma pesa.

Zifuatazo ni SMS au meseji za kumtakia mchana mwema mpenzi wako. Kama unahitaji Unaweza chagua zinazoendana na mahusiano yako kwa sasa kisha ukazitumia kwa umpendae. Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy kwa mambo mengine mazuri zaidi.

SMS za mchana mwema kwa mpenzi wako

Upendo wangu kwako huongezeka kila wakati ninapokutazama. Hautafifia wala kuisha kwa sababu hauna mwisho. Kila mara kumbuka kuwa Nakupenda sana na kwa muda huu nakutakia mchana mwema kipenzi changu.



Mpenzi, muda huu nakukumbusha tu kuwa wewe ndio chaguo langu. Yaani naomba ujue kuwa wewe ni Mfalme wa kasri langu na kwamba moyo uliokaa kifuani mwangu utalidunda jina lako. Ninakupenda zaidi ya ninavyoweza kusema nakupenda. Mchana mwema mpenzi wangu.






Nakutakia mume/mke mtamu zaidi ulimwenguni siku njema. Hakuna mtu katika ulimwengu mzima anaweza kuwa mpenzi wa maisha yangu kwa sababu nafasi hiyo tayari imechukuliwa na wewe, mume/mke wangu mpendwa. Nakupenda Saana na napenda kukupenda.



Asante kwa kupenda kila kitu changu, pamoja na kutokamilika kwangu. Mungu alinipa zawadi isiyo na kifani maishani mwangu pale alipokuumba wewe mpenzi wangu. Nakupenda sana kuliko ujuavyo.




Tambua kuwa wewe ni mtu pekee katika ulimwengu wote ambaye hufanya maisha yangu kuwa kamili kabisa na maridadi. Mpendwa, asante kwa kuleta joto na mwangaza katika maisha yangu. Sijawahi jutia kukupenda.





Nina nafasi moyoni mwangu ambayo hakuna mtu anayeweza kuchukua kwa sababu hakuna mtu mwingine anayeweza kunifanya nifurahi kama unavyonifanya. Nakutakia mchana mwema.




Wewe ni damu ambayo hupitia mishipa yangu. Wewe ndiye kipande muhimu ambacho hufanya roho yangu ikamilike. Siwezi kamwe kuishi katika ulimwengu huu bila wewe, mpenzi wangu wa thamani. Kuwa na siku mchana mwema huko uliko!


SMS za kumtakia mpenzi wako usiku mwema GUSA HAPA>>>




Kuangalia machoni pako kunanipeleka kwenye ulimwengu wenye zaidi ya maelfu ya furaha. Penzi lako hufanya nijihisi Niko paradiso. Umeniweza sasa, naomba kokote uendako usisahau kuwa nakupenda mpenzi wangu. Mchana mwema kwako.

Kila nikiona simu au SMS toka kwako moyo wangu hudunda kwa furaha… Kiufupi nakupenda na natamani kuelezea upendo wangu zaidi ya kukuambia “nakupenda” ili tu utambue na usije kuniumiza. Tambua hilo kipenzi changu… Nakutakia mchana mwema.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>