Category Archives: Uncategorized

App za kuangalia Movies/Filamu mtandaoni kwa simu

Katika ulimwengu wa sasa unaweza angalia movie kwenye simu yako ya kiganjani ukiwa popote ulimwenguni. Mara nyingi watu wakitaka kuangalia movie huwa wanatembelea website/tuvuti zinajihusisha na movie/filamu au hutumia app zinazojihusisha na filamu ili kupata huduma ya movies. Kuna baadhi ya tuvuti au app hukuwezesha kupata huduma ya movie bure na nyingine huwa zinakuhitaji ulipie. Huduma za kulipia huwa ni bora zaidi na zinausalama zaidi ukilinganisha na baadhi ya huduma za bure japo zote ni nzuri.

Hapa Tha bestgalaxy leo tunakupa orodha ya app chache kati ya app nyingi unazoweza tumia kuangalia movie kwenye simu yako mtandaoni(online).

App za kuangalia movies online(mtandaoni)

Netflix

Hii ni app ya kampuni ya kimalekni, Netflix ambayo inayotoa huduma ya kuangalia movies/filamu kupitia Internet. Unaweza ingiza kwenye simu yako ya mkononi na kuanza kufurahia filamu kiganjani pako. Unaweza kuangalia filamu nyingi nzuri na maalufu duniani kupitia app hii. Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba app hii ya netflix huwa haitoi huduma bure. Inaweza kukugharimu Tsh 7000 mpaka 23000(Makadilio).

ShowMax

ShowMax ni app inayotoa huduma ya kuangalia movies(filamu), michezo, vipindi vya TV na mambo mengine mengi, kiganjani pako. App hii inaweza kutumika kuangalia movie katika simu ya mkononi lakini sio bure pia. kufurahia huduma za app ya ShowMax utatakiwa kulipia kila mwezi. Kuna filamu nyingi unaweza angalia na pia kama ni mdau wa michezo, unaweza furahia michezo katika app hii. Kifurushi vyake vinaweza kugharimu Tsh 7800 mpaka 46000 kwa mwezi(Makadilio).

Youtube

Youtube ni app ambayo watu hutumia kuangalia video mbalimbali ambazo huwa zinapostiwa kwenye channel. Katika Youtube kuna channel ambazo hutuma filamu na unaweza angalia filamu hizo bure kabisa. Ukiachana na channel za filamu pia kuna kipengele cha Youtube kinachojihusisha na filamu tu(filamu za bure na kununua}. Kipengele hicho cha Youtube hakipatikani katika baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania kwa sasa ila unaweza soma maelezo ya kukuiona hapa chini.

Jinsi ya kuona kipengele cha movies cha YouTube Gusa hapa>>>>

Prime Video

App hii inaitwa “Amazon Prime Video” lakini kwa kifupi unaweza kuiita “Prime Video”. Ni moja ya app zinazoweza kukufanya ufurahie kuangalia movies na hata vipindi vya Tv pia kiganyani pako. Prime Video sio app ya bure lakini inakupa uwanja mpana unaofanana kiasi na netflix hivi katika filamu, unaweza angalia filamu nyingi maaalufu. Maelezo ya kiasi utakachotakiwa kulipa kwa mwezi yaliopo katika tuvuti yao yametaja kiasi kuwa ni USD 5.99 ambayo ni kama Tsh 14000 ivi…

~Viasi vya malipo vilivyo tajwa kwenye makala hii ni makadilio tu.

Maneno na maswali ya kurefusha maongezi na kumfurahisha mpenzi wako

Katika mahusiano wapenzi mnaweza ongea au kuwasiliana mpaka ikafika wakati mkakosa cha kuzungunzia, hasa kama hakuna mmoja kati yenu mwenye uwezo wa kuendesha mazungumzo. Ukiwa kwenye hali hii, unaweza ingizia maneno na vimaswali vilivyopo hapa chini kurefusha mazungumzo yenu, kumchekesha na hata kukusaidia kumjua vizuri mpenzi wako. Unaweza kuyatumia kama sms, au kuyaongea unapokua nae karibu au kwenye simu. Lakini unapotumia maneno na maswali haya hakikisha hamupo kwenye hali ambayo itamfanya mpenzi wako aone kero. Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Maneno na maswali ya kurefusha maongezi na mpenzi wako

  1. Kuna watu walikua wanamsifia dada flani hivi kuwa anamacho mazuri, nilivyomwangalia yule dada nikajiuliza “Mh hivi wanamjua mpenzi wangu hawa? hahaha” Unamacho mazuri sana alafu nayapenda.
  2. Hivi hilo kovu ulifanya nini?, au ulikua cha utundu utotoni?
  3. Kama kuna zawadi ambayo ulipanga kumpa mtu atakae kupenda kwa dhati maishani mwako nipe tu maana nakupenda sana mpenzi, sitamani utoke maishani mwangu unanipa furaha mwenzio. Stamani niamke kwenye hii ndoto.
  4. Kwa mfano umeshida Milioni 80 sasa hivi, utanipa shingapi au utafanyia nini?
  5. Kukupenda ndio kitu ninachoweza kukifanya bila kuchoka duniani mpenzi wangu. Sijui niwe nakuita jina gani ili usije sahau kuwa nakupenda na usinitende…
  6. Ulivyo kuwa mdogo ulitaka ukiwa mkubwa uwe nani?
  7. Hebu fumba macho tuone… Hahaha Unamacho mazuri… ivi unajua kwamba una macho mazuri hivyo?
  8. Kwaiyo umelala peke yako? huogopi?
  9. Wiki ijayo nikumbushe nikwambie kitu… Ntakwambia kitu kizuri
  10. Kitu gani unapenda utimize kabla siku zako za kuishi duniani hazijaisha?
  11. Bebi, ivi nikikwambia utaje vitu vitano tu unavyo penda duniani utataja vitu gani?
  12. Unapenda mbwa au paka?
  13. Ivi katika maisha yako unaogopa nini?
  14. Ulifikiria nini mara ya kwanza nulipokwambia nakupenda?
  15. Niambie vitu vitatu tu ambavyo hauvipendi?
  16. Ivi umenipendea nini? au unapenda nini toka kwangu mpenzi?
  17. Ninavyokugusa huwa najiskia vizuri sana ivi wewe unahisi vipi?
  18. Unafanya nini sasa hivi?
  19. Upo na nani hapo kipenzi?
  20. Natamani nije hapo japo kukubusu tu lips zako nzuri hizo
  21. Ukichukia unapenda kufanya nini ili kutuliza hasira zako?
  22. Alafu usiku nilikuota
  23. Ivi umeishawahi poteza hela? ilikua kiasi gani?
  24. Niambie maneno matatu mazuri toka moyoni mwako
  25. Unapenda kuangalia filamu? unapenda filamu gani?
  26. Hahaha… nitakwambia kesho… au nipe zawadi nikwambie leo
  27. kwenye familia yenu wewe ni mtoto wa ngapi kuzaliwa?
  28. Ivi bebi Unapendelea zaidi kula chakula gani?
  29. Ugali kwa kiluga chenu munauitaje?
  30. Ukipewa nafasi ya kutembelea nchi tatu duniani ambazo hauja wahi tembelea, utachaguza zipi?

Whatsapp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa

Whatsapp ni mtandao unaotumiwa na watu wengi sana na umekua na msaada mkubwa kwa watu katika swala la mawasiliano. Katika kutumia mtandao huu unaweza kupambana na changamoto au vitatizo vidogo vidogo, hasa katika app za simu. Changamoto au matatizo huwa hayatokei mara kwa mara lakini hapa The bestgalaxy tumekuandalia orodha ya matatizo au changamoto unazoweza kutananazo katika kutumia whatsapp na maelezo ya jisi ya kutatua. Hii inaweza kuwa msaada pindi mtu unapokumbana na changamoto hizo. Pia usisahau kuungana nasi kwenye WhatsApp namba 0622586399.

Changamoto au Matatizo kwenye kutumia Whatsapp na jinsi ya kutatua

Whatsapp ban

Kama upo banned/umezuiwa kwenye WhatsApp unaweza kuona hivi

Mtandao wa whatsapp unasheria zake ambazo ukikiuka katika kutuumia mtandao huu, wanazuia akaunti yako. Kutumia app za whatsapp zisizo rasimi ni moja ya jambo linaloweza kufanya akaunti yako izuiliwe Whatsapp. Nikizungumzia “Whatsapp zisizo rasmi” namaanisha app kama vile OG Whatsapp, GB Whatsapp au FM whatsapp. Mtandao wa Whatsapp una app rasmi mbili tu. App ya kwanza inaitwa “Whatsapp messenger” na ya pili inaitwa “Whatsapp business”… App yoyote mbali na hizo ni app isio rasmi na inaweza kufanya akaunti yako izuiwe/ifungwe na mtandao wa Whatsapp.

Ukiachana na kutumia app zisizo rasmi, unaweza fungiwa au kuzuiwa akaunti baada ya kufanya mambo mengine yasio faa katika Whatsapp au watu kutoa taarifa kwa Whatsapp kuhusu akaunti yako kujihusisha na jambo flani lisilo ruhusiwa kwenye Whatsapp.

kuna namna mbali za kuzuiwa; unaweza zuiwa na whatsapp kwa muda mfupi au kwa muda mrefu. Ukizuiwa kwa muda mfupi, baada ya muda flani akaunti yako itaondolewa kizuizi na mara nyingi huwa app inaonesha kabisa muda ambao akaunti itaachiliwa. Lakini ikizuiwa kwa muda mrefu huwa inachukua muda mrefu sana kuachiliwa… ukikumbana na kizuizi hiki unashauriwa kufungua akauti nyingine ya whatsapp kwa namba nyingine au kama unahisi wamekuonea, wasiliana nao kupitia Support@whatsapp.com tuma ujumbe wa kuelezea tatizo lako ili wakusaidie.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>

Backup to Google drive

Backup katika whatsapp ni kipengele kinachokuwezesha kutunza sms za whatsapp na vitu vingine kwenye akaunti yako ya google drive ili iwe rahisi kupata au kurudisha sms na vitu hivyo pindi simu yako inapopotea au ukifuta app kwa bahati mbaya. Unaweza fungua whatsapp ukuta ghala tu wahatsapp imekuletea ujumbe unaoziba kioo kizima umeandikwa “Backup to Google drive” na kuna orodha ya chaguzi unazotakiwa kuzichagua pale. Kama hauelewi lolote kuhusu backup basi umaweza changua “Never” tu ili kuokeo muda na kuendelea kuitumia app yako ya Whatsapp.

Whatsapp kumaliza bando

Whatsapp ni moja ya app zisizotumia bando la internet sana ila kama wewe ni mtu unaetumia Whatsapp kwenye upande wa video sana basi app hii inaweza kutumia bando zaidi. Nikisema upande wa video namaanisha kutuma au kupokea video nyingi kwenye vikundi au watu wa kawaida, kutumia video call sana, kuangalia status za watu wengi wilio weka video kwenye status zao. Kuacha au kupunguza mambo hayo kutafanya Whatsapp isile bando lako sana.

Whatsapp inajaza picha na video nisizozitaka kwenye simu

Whatsapp inaweza kuwa inajaza picha na video usizozijua au usizozipenda kwenye simu yako. Kama hili ni tatizo, unaweza tatua tatizo hili kwa kuzima kipengele cha whatsapp kinacho iruhusu app ya whatsapp kuingiza kwenye simu video au picha zinazotumwa kwenye magroup au unazotumiwa. hii itafaya kila video au picha unayotumiwa kutojiingiza kwenye simu yako mpaka utakapo gusa kuidownload.

jinsi ya kufanya hivyo; fungua app yako ya whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” kisha gusa “Storage and Data” alafu baada ya hapo ingia walipo andika “When using mobile data” na uondoe alama ya tiki kwenye vibox vyote au cha video na Photos tu. baada ya kufanya hivyo, bonyeza “Ok” na rudi nyuma kidogo kisha uingie kwenye “When connected on WiFi” alafu uondoe alama ya tiki katika vibox vyote au vibox vya “Photos” na “Videos” tu.

Mtu akikublock WhatsApp Fanya hivi kuchati nae BONYEZA HAPA>>>

Wananiunga kwenye magroup bila taharifa

kama umekua unajikuta umeingizwa kwenye magroup ya Whatsapp na watu usio wajua bila hata taharifa na haupendi hali hiyo basi kunakitu unaweza fanya hapa. Kwenye Whatsapp kunakipengele kinakuruhusu kuzuia mtu ambae hauna namba yake kukuingiza kwenye group. Unaweza kutumia kipengele hiki kuzuia watu ambao hauna namba zao wasikuingize kwenye group lolote bila kukutaharifu.

jinsi ya kufanya hivi; Fungua Whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” kisha gusa “Privacy”. Baada ya hapo, nenda eneo la chini kidogo uingie walipoandika “Groups” kisha chagua “My Contacts” alafu rudi nyumbani na uendelee kutumia app yako.

Nasumbuliwa na simu za watu nisio wajua

Whatsapp pia inakipengele cha kufanya watu watu ambano nambazao hazijawekwa kwenye simu yako wakikupigia usipate usumbufu. Mtu yoyote ambae anakupigia kwenye Whatsapp kwa namba ngeni, simu yako haita, itakua kimya tu bila kukusumbua. Kama ni mtu amabae huwa unapata simu nyingi kwenye Whatsapp toka kwa watu usio wajua na haupendi swala hiilo basi unaweza kutumia kipengele hicho kuondokana na jambo hilo.

Jinsi ya kufanya hivi; Fungua app yako ya Whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” alafu bofya “Privacy”. Baada ya hapo, nenda chini kidogo uingie katika “Call” alafu washa palipo andikwa “Silence unknown callers”.

Magemu ya simu ya kucheza Online (ufalme wa vita)

Ni sehemu nyingine tena tunaangalia Magemu mazuri unayoweza kucheza kwenye simu. Kwenye makala hii tutajikita kwenye magemu ya “battle royale” ambayo kwenye kuyacheza yanahusisha kutafuta ufalme wa vita. PUBG, COD au Free Fire ni moja magemu maalufu ya battle royale lakini ukachana magemu hayo, kuna magemu mengi sana ya muundo huu katika ulimwengu wa magemu… Na mengine yanaendelea kutoka karibu kila mwaka.

Hapa The bestgalaxy tumekuandalia orodha ya magemu machache ya Battle royale ambayo ni ya online(unatumia internet kuyacheza). Unaweza angalia orodha hii hapo chini na hata kujaribu gemu litakalo kuvutia. Ila tumejikita kwenye Andoid.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Magemu ya ufalme wa vita ya kucheza Online/mtandaoni kwa simu za android

Rules of Survival

Rules of Survival ni gemu aina ya battle royale ambalo lilitengenzwa na kampuni ya NetEase Games. Gemu hili ni moja ya magemu kama PUBG,COD au Fire. Lilitolewa kwa simu za Android pamoja na iOS. Linakutupa katika uwanja wa mapambano/vita wenye wachezaji wengine wa gemu hilo Online/mtandaoni.

Katika gemu la Rules of Survival, Ukiwa kama mchezaji wa gemu hili unaweza cheza ukiwa pekeako au kuwa katika timu. Unapoanza unaruka kutoka kwenye ndege na kushuka taratibu katika kwenye uwanja wa mapigano ukiwa huna silaha yoyote. Silaha utakua unazitafuta na kuzikuta kwenye uwanja huo huo wa mapigano huku ukiendelea kujitetea dhidi ya wachezaji wengine.

~Game hili kwa sasa limeondolewa ila kunatetesi kuwa linaweza kurudi.

Knives Out

Hili ni moja ya magemu mazuri ya online/mtandaoni ambayo huchezwa na watu zaidi ya moja. Gemu hili ni battle royale, hukusanya watu au wachezaji katika eneo moja kubwa na kutakiwa kupigana na kujitetea wakiwa kama timu au mtu mmoja mmoja. kufika haraka unapokwenda unaweza tumia gari.

Ni gemu bomba lililotolewa mwaka 2017 na waliolitoa gemu hili ni kampuni ya NetEase Games. Mpaka sasa gemu hili mamilioni ya wachezaji katika sehemu mbalimbali ulimwenguni na wechzaji hulicheza simu mpaka pc.

FARLIGHT84

Hili ni gemu ambalo linahusisha uongo wa kisayansi na ni moja ya magemu mzuri kaika ulimwengu wa magemu ya battle royale. Linakutupa katika mazingira ya ulimwengu wazi yaliyojaa sayari mbalimbali, vituo vya anga na viumbe vingine vya anga. Kiufupi gemu hili lina mazingira tofauti sana, vitu unavyokutananavyo katika gemu hili ni vya kisanyansi na mambo mengine ya uchunguzi wa anga.

Game la FARLIGHT84 limetolewa mwaka 2023 na mpaka sasa lina mamilioni ya wachezaji toka nchi au sehemu mbali hapa ulimwenguni. Kwa maana nyine tunaweza kusema gemu hili linapendwa na watu wengi.

Je, wajua haya kuhusu Kondomu na Ukimwi? soma hapa

Kondomu ni kifuko kinachotumiwa na wanaume tangu zamani kuzuia mimba na maambukizi ya maradhi ya zina. Siku hizi kuna kondomu ya kike pia.

Kondomu zinatengenezwa kwa ngozi ya mnyama, siku hizi hutengeneza kwa kutumia mpira.

Utengenezaji hufanyika katika mazingira ya baridi ili kuhifadhi uimara wa mpira.

Zinaunganishwa ngozi nyembamba mbili ili matundu ya ngozi ya kwanza yazibwe na ile ya pili na matundu ya ngozi ya pili yazibwe na ile ya kwanza.

Kisha kupimwa, kondomu huwekewa dawa ya kuzuia isiharibike: dawa hiyo ina madhara kwa afya.

Pamoja na kutumika kwa ajili ya kuzuia mimba kwa mafanikio makubwa (ingawa si 100%), mpira huo unatangazwa sana kama kinga imara dhidi ya virusi vya UKIMWI.

Lakini katika utafiti uliofanywa na shirika la Sexuality Information and Education Council la Marekani kwa majozi 122 ambapo mmojawao alikuwa mwathirika, wenzao 12 waliambukizwa (10%) ingawa walifanya ngono kwa kutumia kondomu kila mara na kwa usahihi.

Shirika la Human Life International lilifanya utafiti kwa aina mbalimbali za ngono. Kati ya waliotumia vizuri kondomu, mwaka wa kwanza waliambukizwa: 11% za waliofanya ngono ya kawaida, 30% za waliofanya ulawiti. Mwaka wa pili wakafikia 21% na 51%. Mwaka wa tatu wakawa 30% na 66%.

Kwa maneno mengine ni kwamba kondomu haizuii moja kwa moja, bali inaahirisha maambukizi: kama si leo, inaweza tokea kisababu kesho ukapata japo ni kwa uwezekano mdogo sana, hasa kama ukiwa muangalifu katika taratibu za utumiaji. Pamoja na yote hayo, huwezi kulinganisha hata kidogo kutumia kondomu na kutotumia kabisa. Bado kondomu ni kitu kinachozuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa asilimia kubwa sana ukilinganisha na kutoitumia. Ndio maana watu hushauriwa kutumia kondomu ili kuzuia maambukizi wanaposhirikiana kimwili bila kujua hali zao. Na endapo mtu akipata virusi vya ukimwi ni vema akajikubali, akeelewa kuwa sio mwisho wa maisha na pia kuwatu wengi katika Dunia au mazingira yake wanahali kama yake waishi kama kawaida.

SUKARI YA DADA šŸ”ž (Simulizi ya Sauti)

SUKARI YA DADA ni simulizi tamu iliotolewa na kijana wa miaka hii na mpaka sasa imefuatiliwa na maelfu ya watu na wameipenda. Sasa simulizi hii inapatikina kwa sauti na hii ni kumrahisishia mtu asietaka kupoteza muda kuisoma. Mbali na hivyo, kuna vitu vingi vya kufurahisha kwenye simulizi ya SUKARI YA DADA ya sauti kuliko ya maandishi japo ya maandishi pia ni nzuri sana kwa upande wake. Kama unahitaji simulizi hii unaweza anza kusikiliza sehemu za mwanzo Bure kabisa kwenye simu yako. Kitu cha kuzingatia ni kwamba hautakiwi kuwa na miaka chini ya 18 au kusikiliza sehemu zilizo na watu wa umri huo maana ndani ya simulizi kunavitu vilivyolenga watu wa umri wa miaka 18 na kuendelea.

Anza na simulizi hii kwa kusikiliza vipande vifuatavyo:

Sehemu ya 1:

Sehemu ya 2:

Sehemu ya 3:

Sehemu ya 4:

Sehemu ya 5:

Sehemu ya 6:

Kama utahitaji kupata simulizi nzima, ni Tsh 2000 tu(wahi OFA!)… Bofya kitufe kilichoandikwa “WhatsApp” hapa chini ili kuchati na sisi Whatsapp ili upewe nafasi ya kupata Simulizi full(vipande 17). Au piga simu 0715233405

Unaweza sikiliza maelezo haya

Isikilize simulizi ya SUKARI YA DADA katika mazingira ya utulivu

Kama utakua umeamua kuisikiliza ni vema ukazingatia mazingira ya utulivu ili ufurahie zaidi hii simulizi. mazingira tulivu yatakufanya umuelewe msimuliaji na kuielewa kirahisi simulizi hii nzuri. Ninaposema mazingira tulivu na maanisha mazingira yalio na makelele au vitu vingine vinvyoweza ondoa umakini unaouweka kwenye simulizi na kukufanya usisikie au kuelewa baadhi ya sehemu. Zingatia sana anachosema msimuliaji kuliko kuizingatia sauti yake.

Inaweza kusikilizwa na wanaume na wanawake

simulizi hii inaweza sikilizwa na jinsia zote. Nikisema jinsia zote basi nna maana inaweza sikilizwa na mwanaume na pia mwanaweke. Hivyo kama wewe na mwanaume, unaweza sikiliza simulizi hii… Ukiwa ni mwanaumke, unaweza pia sikiliza simulizi hii bila shida yeyote. cha kuzingatia hapo ni umri tu maana watu wasio na miaka 18 na kuendelea hawaruhusiwi kutega sikio za kwa msimuliaji.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Jinsi ya kujua kama simu inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine(anaona bila kuigusa)

Katika matumizi yako ya simu za Smartphone unatakiwa kuelewa kwamba vifaa hivi vinaweza kudukuliwa na mtu mwingine na kufanya mdukuzi au huyo mtu apate uwezo wa kuona vitu vilivyomo au vitu unavyofanya kwenye simu yako bila yeye kuigusa simu yako. Mbali na kuona vitu unavyofanya au ulivyohifadhi, Mtu aliedukua simu yako pia anaweza kuwa na uwezo wa kuitumia simu yako bila kuigusa… Mfano wa vitu anavyoweza kuvifanya ni kuitumia simu yako kutuma sms kwa mtu mwengine, kuitumia camera yako kuangalia unachokifanya, kuvujisha vitu vyako au kukuzuia kufanya baadhi ya vitu kwenye simu yako.

Lakini ukiwa kama mtumiaji wa smartphone wa miaka hii, hutakiwi kuwa na hofu sana juu ya hili kwani kunaviashilia vya kuangalia kwenye simu yako ili kujua upo salama au vipi. Hapa The beestgalaxy tutakupa mwanga juu ya jinsi ya kuangalia simu yako ya Android kama imedukuliwa na inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kuangalia kama simu yako inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine

katika matumizi ya simu watu huwa wanapenda kuingiza apps nyingine mbali mbali ukiachana na zile ambazo huwa wanazikuta tayari zipo kwenye simu. Kitu unachotakiwa kujua hapa ni kwamba kuna Program au apps ambazo unaweza kuingiza kwa bahati mbaya au ukaingiziwa kwenye simu yako na zikiwa kwenye simu yako zinakua zinatumika na mtu mwingine huona au kufanya vitu kwenye simu yako bila kuigusa.

Endapo katika simu yako kutaingizwa apps hizi kwa makusudi au bahati mbaya, simu yako itakua sio salama tena maana vitu. Lakini kitu kizuri ni kwamba kwenye sikuizi kwenye simu za Android kuna program inaitwa “Google play protect”. Program hii inamilikiwa na google na kazi yake kubwa kwenye simu ni kukulinda dhizi ya apps hatari unazoziingiza kwenye simu yako. Kama kuna app yoyote inayoweza kuwa hatari umeiingiza, Google play protect huwa inatoa taharifa na kukushari cha kuifanya. Unaweza kuitumia Google play protect kuangalia kama angalia kama simu yako ni salama au si salama. Unachotakiwa kufanya ni kufuata hatua hizi chini.

  • Chukua simu yako na uingie katika app ya Play store
  • Baada ya hapo, gusa kiduara cha profile yako na uchague “Play protect
  • Bonyeza kitufe kilichoandikwa “Scan” na baada ya hapo Google play protect itaanza kuangalia kama kuna app zozote hatari kwenye simu yako alafu itakupa majibu.
  • Kama kutapatikana app yoyote hatari utaonyenshwa app hiyo alafu utashauriwa kuiondoa kwenye simu yako kwa kugusa kitufe cha “Uninstall“.

Google play protect ni njia nzuri na rahisi ya kuangalia kama simu iko salama ukiwa kama mtumiaji wa kawaida lakini huwa haikuhakikishii usalama kwa 100%.

Google play protect ikiwa “Active” kwenye simu yako huwa inatafuta na kulinda hii ya app hatari. Na endapo itakuta app harari imeingizwa au unataka kuiingiza kwenye simu yako, itakupa taharifa.

Mbali nna kutumia Google play protect kuangalia kama simu yako iko salama unaweza pia kujua kuwa simu kwa kuangangalia kama kwenye simu yako kuna vitu vifuatavyo.

Angalia orodha ya app zinazotumia sana internet na kama utakuta app ambayo haieleweki na hauitumi lakini ipo juu kwenye matumizi ya bando, inawezakua ni app hatari. Kama kamera ya simu yako ukiifungua inakuandikia ā€œCamera is being used by another applicationā€ au ā€œYou cannot use more than one application that uses cameraā€ au “Camera may be in use by another application” hiyo inaweza kuwa ni ishara ya kwamba simu yako sio salama. Mbali na hayo, kukuta vitu ambanyo haujavifanya lakini vimefanyika kunaweza kuwa kiashiria cha hatari pia.

Mazoezi ya kupunguza tumbo au kitambi (rahisi unafanya hata nyumbani)

Tumbo au kitambi imekua ni tatizo ambalo baadhi ya wanaume na wanawake hukumbananalo katika miili yao. Tukitungunzia kitambi katika mwili wa mwanadamu ni mafuta ambayo hujikusanya katika maeneo ya tumbo na kulifanya tumbo kuonekana limeongezeka ukubwa. Mara nyingi kitambi huibuka katika mwili wa mtu kutokana na mlo wa mtu mwenyewe au staili ya maisha yake kiujumla. Mazoezi ni njia salama na ya bure ya kuepukana au kuondokana na kitambi.

Kunawatu huwa wanashindwa kutumia njia hii na kufanikiwa kupunguza kitambi kutokana na kutarajia matokeo ndani ya siku moja au mbili. Ukiwa na mawazo hiyo kichwani hautaweza kufanikiwa kupunguza kitambi kwa njia ya mzaoezi maana matokeo huwa yanachukua muda. Yanaweza kuaanza kuonekana zaidi baada ya siku 30(mwezi).

Ukitaka kufanikiwa kirahisi, kichwa chako kiwe kinaelewa kwamba mazoezi unayoanza kufanya hayapunguzi tumbo tu, yanakufanya uweunacheza mchezo wa kitandani vizuri na kwakuchangamka, utachangamka pia katika shughuli zako nyingine tena utaepukana baadhi ya magonjwa. Ukifanya mazoezi vizuri kwa siku 7 tu unaweza anza kuona faida hizo nyingine hatakama tumbo halijapungua. Ni vema ukafanya mazoezi kuwa ni tabia yako tu ili faida zake uwe unazifurahia kila siku katika maisha yako.

Hapa chini tunashusha mazoezi matatu tu ambayo unaweza kuanza kuyafanya kila siku ili kupunguza kitambi au tumbo. Mazoezi haya ni kwaajili ya wanawake na wanaume pia. Yanaweza fanyawa hata nyumbani tu na kama hauna muda maalum wa mazoezi unaweza tafutiza dakika chache kila siku kabla haujaingia kuoga, ukayafanya. kwasiku za mwanzo unaweza pata maumivu kutokana na mwili kutozoea mazoezi lakini usikate tamaa, endelea kufanya tu maana maumivu huisha na hukuacha ukiwa imara zaidi.

Mazoezi matatu ya kupunguza Tumbo au kitambi (Mwanawake na Mwanaume)

Zoezi la kwanza

Tafuta sehemu nzuri na safi ambayo itakuruhusu kulala chali bila tatizo. Nenda katika sehemu hiyo kisha ulale chali. Nikisema “kulala chali” namaanisha kulala kwa kuangalia juu. Baada ya kulala chali hapo chini, kishike kichwa chako kwa mikono yako yote miwili alafu ukiwa hivyo hivyo, anza kujinyanyua kiwiliwili na kichwa juu alafu unarudi chini. Endelea kwenda juu na chini, juu chini bila kuibandua miguu yakochini. Angalia mfano katika picha hii;

Image:Giphy

Zoezi la pili

Katika zoezi hili, hatua ya kwanza ni kuchuchumaa chini. Baada ya kuchuchumaa nyoosha mikono yako mbele alafu shika chini katika sakafu. Baada kufanya hivyo, anza kuitegua na kuivuta miguu yako yote miwili kwa nyuma bila kiwili wili kugusa chini alafu irudishe tena miguu kama ilivyokua. Endelea kuifanya hivyo miguu kama inavyoonekana katika picha hii.

Image:Giphy

Zoezi la tatu

Kwenye zoezi hili utatakiwa kuanza kwa kulala chali kama katika zoezi la kwanza. Lakini baada ya kulala chali utatakiwa kuwa unanyanyua miguu yako yote miwili, wa kushoto na wakulia na kulileta juu kwa pamoja alafu unairudisha Tena chini. Endelea kufanya hivyo kwa kurudia kwenda juu na chini. Unaweza angalia picha ili kuelewa zaidi.

Image:Giphy

Magemu mazuri ya mabasi kucheza kwa simu za Android

Magemu ya mabasi yamekua ni kati ya magemu pendwa sana kipindi hiki. Magemu haya yapo mengi sana na watu huyacheza kupitia simu, pc na baadhi ya vifaa vingine kama hivyo vinavyo tuwezesha kucheza magemu. Katika makala hii tunazungumzia magemu mazuri ya mabasi lakini tutajikita katika upande wa simu za Android hivyo kama wewe ni mtumiaji wa simu yoyote ya Android, unapenda na kutaka magemu mazuri ya mabasi, hii ni kwaajili yako.

Kutokana na wingi wa magemu ya mabasi kwa simu za Android, inaweza kuwa ngumu kwa mtu kujaribu kila gemu ili kujua lipi ni zuri na lipi ni baya kwake ingawa unaweza fanya hivyo pia. Hapa sisi tunakupa orodha ya magemu macheche ya mabasi ambayo ni mazuri unayoweza kuyacheza katika simu yako na yanachezwa na watu wengi duniani. nafikili hii inaweza kukusaidia katika utafutaji wa gemu zuri kwako.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Magemu ya mabasi za kucheza kwenye simu za Android(5)

1. Bus simulator 2023

Katika magemu ya Android mazuri ya nayohusiana na uendeshaji wa mabasi, kunage hili linaitwa “Bus simulator 2023”.Bus simulator 2023 ni gemu la mabasi lililotoewa na Ovidiu Pop kwa simu za Android pamoja na iOS. Lilinakutupa katika ulimwengu ambao unakua ni deleva wa mabasi na kuna modes nyingi unaweza kuwa unafurahia humu ndani. Unaweza kucheza na marafiki aua watu wengine online na pia kwenye upande wa muonekano uko poa. Asilimia kubwa ya watu waliolicheza gemu hili,wamelipenda kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo muonekano.

2. Bus simulator indonesia

Kama ni mfuatiliaji mzuri wa The bestgalaxy unawezakuwa umegundua kuwa gemu la Bus Simulator Indonesia tumeliongelea zaidi ya hapa. Hii ni kwasababu nigemu zuri sana na usioweza kuyaacha unapozungumzia magemu ya simu ya kuendesha mabasi. kwasasa gemu la Bus simulator indonesia imeishaingizwa kwenye simu na watu zaidi ya milioni 100 kutoka sehemu mbalimbali za dunuia. Mazingira na mabasi ya katika gemu hili ya yanaendana na mabasi na maingira halisi ya huko Indonesia. Muonekano wa gemu hili ni mzuri na pia uzuri mwingine wa gemu hili ni hutohitaji kutumia data/internet katika kulicheza ingawa ukihitaji kucheza na watu au marafiki, utahitaji kuwa na muunganiko wa internet(data).

3. Coach Bus Simulator

Hili ni gemu la mabasi ambalo mpaka sasa watu zaidi ya milioni 10 wamelipakua katika vifaa vyao vya Android OS. Ndani ya gemu hili mchezaji unaendesha mbasi ya abilia ya masafa kuwatoa sehem moja kwanda nyingine. Na ukiwa kama dereva wa mbasi unakumbana na changamoto mbalimbali katika kazi yako unapokua barabaradi. Linamuonekano mzuri. Ovidiu Pop ndio waliotoa gemu hili na linapatikana bure kabisa kwa watu wote wanaohitaji kulicheza katika Android. Unaweza kulipakua kupitia Playstore na ukaanza kufurahia kulicheza kila siku bila kutumia data(Ni gemu la Offline).

4. Bus simulator ultimate

Katika mwaka 2019 “Zuuks Games” walitoa gemu la Bus Simulator Ultimate na toka hapo mpaka sasa kuna mamilioni ya watu wamepakua gemu hili na wanaendelea kulicheza. Zuuks Games walisema gemu lao la bus simhlator limekua ni miongoni mwa magemu ya mabasi yaliopakuliwa na watu wengi… limeshafikisha zaidi ya watu milioni 200. idadi hiyo ya watu inajumuisha watu kutoka US,UK,Canada na sehemu nyingine yingine nyingi za dunia, ikiwemo Tanzania. Unaweza kulidowmload au kulipakua gemu hili bure ila kulicheza utahitaji kutumia data(internet).

5. Public Transport Simulator C

Gemu jingine zuri la mabasi kwa upande wa Android ni hili linaitwa Public Transport Simulator C. 2019 ndio mwaka SkisoSoft walilitoa na tokalitolewe mpaka sasa limechezwa na zaidi ya watu milioni 50. Kutokaa na uzuri wake asilimia kubwa ya watu wanaolidownload na kulicheza wanalipenda na hii imeionesha kupita reviews ambazo zimekua zikitolewa na wachezaji wa game hili katika Playstore. Pamoja na kwamba gemu hili limetolewa mwaka 2019 lakini bado linaendelea kuboreshwa na hupata updates kila baada ya muda flani… Lakini jambo hili halifanywi kwenye gemu hili tu, hufanywa kwenye mgemu mengine. Kiufupi ni kwamba magemu yanaboreshwa Kila siku na Unaweza ona Gemu ni baya Leo lakini baada ya mwaka likawa limeboreshwa na kuwa zuri.

Mbali na magemu haya unafikili ni gemu gani lingine zuri kwa upande wako? Huu ni mwisho wa orodha yetu,, usiache kuwa kalibu nasi…

SMS nzuri za kumtumia mpenzi wako asubuhi

Asubuhi ni mwanzo wa siku na kuianza siku vizuri kunaweza kuwa ni pamoja na kupokea sms ya maneno ya upendo toka kwa watu tunaowapenda. Kumpa maneno mazuri ya upendo mpenzi wako wa moyoni anaekupenda kunaweza kufanya aifurahie siku nzima na pengine kufanya aendele kukuamini kwamba unamjali, upo yupo kichwani mwako na unamuwaza huko uliko. Hivyo kama unataka kufanya jambo hili, tambua kuwa hizo ni kati ya faida zake katika mahusiano. Na kama unahitaji sms za maneno mazuri za asubuhi zitakazo mgusa roho mpenzi wako, unaweza ukoa muda kwa kuangalia sms fupi ziliopo hapa chini zitakazo endana na hali ya penzi lenu.

Mambo ya kuepuka katika mahusiano BONYEZA HAPA>>>

SMS za asubuhi njema kwa umpendae

Asubuhi njema… Natamani siku ya leo tungeamka kitanda kimoja na wewe. Tena sikufichi, huku niliko nakosa vitu vingi sana kwasababu niko mbali na wewe mpenzi wangu… Ila nikikumbuka kuwa unanipenda na pia nakupenda, moyo wangu unatulia kidogo na kusubilia siku tutakayoonana ingawa naona kama nachelewa kukutana na wewe malaika wangu, nakupenda sana.

Upendo ni zawadi ya pekee sana mungu aliyoiweka ndani ya mioyo yetu bure na mimi nimeitumia vema sasa zawadi hii kwa kukupenda wewe. Nakupenda sana na sijawahi jutia kukupenda mpenzi wangu. Asubuhi njema wangu.

Sms za kumfanya mpenzi wako afurahi BONYEZA HAPA>>>

Kuna mtu mmoja mzuri, anaakili sana, mkarimu na nampenda saaaana, yupo anaisoma sms hii niliomtumia pekeyake asubuhi hii. Ameuteka moyo wangu na sihitaji kuunasua maana anaupa raha kwa penzi lake, Asubuhi njema kwake.

Natumai ulikuwa na usingizi mzuri sana. Tafadhali amka sasa kwa sababu asubuhi yangu haiwezikamilika kujua hali yako wewe. Habari ya asubuhi mpenzi!

kila siku huwa nawaza kukusu wewe na mapenzi yetu kiujumla… nimegungua najifunza vitu vingi sana toka kwako, pia upendo wako unaboresha maisha yangu na kunifanya niishi kwa furaha sana. Asante kwa kuwa mimi, nimekuweka moyoni, nakupenda na nazidi kukupenda kila siku mpenzi wangu, Asubui njema kwako.

Natumai umelala kama malkia. Sasa tafadhali amka kama nyota na utawale ulimwengu wangu kwa siku ya leo tena. Habari za asubuhi!

Katika penzi letu kunamuda tunagombana alafu tunapatana. Hii isije kukufanya uamini kuwa sikupendi. Kama jinsi jua linavyo chomoza asubuhi hii na kuleta mwanga palipo na giza ndivyo uwepowako unaleta furaha kwenye maisha yangu. Nakupenda sana na najivunia kuwa na wewe…. Nakutakia asubuhi njema wangu.

Tunapitia vitu vingi katika penzi letu lakini sijawahi jutia kukupenda wala kuwa na wewe kwenye penzi. Mimi huwa naamini mimi ni Mfalme na wewe ni Malkia katika safari ya maisha na penzi letu, naamini unanipenda na nakupenda sana. Nakutakia asubuhi njema na siku yenye furaha.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>

Leo nimeamka nikiwa na mawazo yako tu akilini mwangu. Huwezi amini nilivyo kumiss hapa. Siezi kufurahia asubuhi hii nzuri bila wewe mpenzi wangu. Amka!

Najisikia kubarikiwa sana kila asubuhi ya maisha yangu ninapojua hali yako ni salama. Umeamka poa?