Category Archives: Uncategorized

Kwanini mwanaume anashindwa kusimamisha? Sababu hizi hapa

Kuna sababu nyingi zinazoweza pelekea kutokea kwa tatizo la mwanaume kushindwa kusimamisha yaani, kushindwa kuwa na uwezo wa kuamsha uume wake na kuwa imara na mgumu wakati wa tendo la ndoa . Kuna wanaume hukumbana na tatizo hili kwa muda mfupi au kuwa tatizo la kudumu. Hali hii anaweza kumbana nayo mwanaume wa umri wowote(Mzee au Kijana).

Fanya haya ili uchelewe kupiga bao BONYEZA HAPA>>>

Sababu za mwanaume kushindwa kusimamisha

Sababu zinazoweza sababisha mwanaume kushindwa kusimamisha zinaweza kuwa za kisaikolojia, afya ya mwili, mtindo wa maisha, magonjwa ya zinaa au umri. Hebu tuangaliae zaidi mambo au sababu hizi:

Saikolojia.

Mwanaume akiwa na mfadhaiko, wasiwasi, msongo wa mawazo, au hofu ya kutofanya vizuri wakati wa tendo, anaweza jikuta kashindwa kusimamisha. Yani kama mwanaume hajiamini au mawazo yapo mbali na tendo anaweza kumbana na tatizo hili.

Afya ya mwili.

Tatizo la kushindwa kusimamisha kwa wanaume wengine linaweza kusababishwa na masuala ya afya ya mwili. Mwanaume akiwa na mwili wenye ugonjwa wa kisukari, shinikizo la damu, matatizo ya moyo, unene uliopitiliza, au ugonjwa wa tezi dume, anaweza kumbana na tatatizo la kushindwa kusimamisha.

Mtindo wa maisha.

Mwanaume pia anaweza shindwa simamisha baada ya uwezo wake wa kusimamisha kuathiliwa na matumizi ya tumbaku, unywaji wa pombe kupindukia, na matumizi ya dawa za kulevya. Pia, kutofanya mazoezi ya kutosha na kula chakula au lishe duni kunaweza kusababisha mwanaume kupata matatizo ya nguvu za kiume.

Mazoezi ya mwili yatakayo kusaidia katika mapenzi BONYEZA HAPA>>>

Magonjwa ya zinaa.

Mwanaume kuwa na baadhi ya magonjwa ya zinaa kama vile kisonono na magonjwa mengine kunaweza muathiri uwezo wake na kupelekea matatizo ya nguvu za kiume.

Umri wake.

Kwa wanaume wengi, umri huathiri uwezo wa uwezo wa kusimamisha. Mwanaume mwenye umri mkubwa anaweza jikuta amepunguza uwezo wa kusimamisha kutokana na umri wake ingawa hali hii huwakuta pia wenye umri mdogo.

Ikiwa mwanaume anasumbuliwa na tatizo hili kwa muda mrefu au mara kwa mara ni vyema kumwona daktari au mtaalamu wa afya ili kupata ushauri na matibabu sahihi yanayoweza saidia kuweka hali sawa.

Asante kwa muda wako, endelea kufuatilia The bestgalaxy, endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Jinsi ya kupata simu janja/smartphone bila kuwa na pesa nyingi

Karibu The bestgalaxy na asante sana kwa kuwa hapa muda huu. Katika ukurasa huu tumekuandalia maelezo ya kukufungua ubongo juu ya jinsi ya kumiliki simu janja/smartphone bila kuwa na pesa nyingi. Maelezo haya yamelenga watu ambao hawatumii smartphone/simu janja mpaka sasa wakiamini hawawezi miliki simu hizi za kisasa kwasababu hawana pesa nyingi.

Ukweli ni kwamba usipokua unatumia simu janja kipindi hiki, unakuwa unapitwa na mambo mengi sana ambayo ungeyapata kiganjani kwako. Mfano mzuri ni kutumia app ya Whatsapp; kuna baadhi ya watu katika kazi zao wanashindwa kutuma au kutumiwa video,picha na vitu vingine kwasababu tu hawatumii app ya Whatsapp na sio kwamba hawapendi bali ni simu zao haziwezi.

Kuendelea kutumia hizo simu ndogo ni jambo zuri lakini kuanza kutumia simu janja kunaweza kuwa jambo zuri zaidi hasa ukijua matumizi mazuri na chanya kwako. Kama unataka kuanza kutumia simu janja lakini unauwezo mdogo sana kipesa unaweza fanya yafuatayo kupata simu janja kwa huo huo uwezo ulionao.

Jinsi ya kumiliki simu janja/smartphone bila kuwa na pesa nyingi.

Pata simu za mkopo na anza kulipa kidogo kidogo.

Moja kati ya vitu ambavyo watu hufanya sasaivi ni kuchukua simu za mikopo. Kuna makampuni huwa yanajihusisha na kutoa simu janja za mikopo. Unatakiwa kuwa na kiwango kidogo sana cha pesa ambacho utawapa alafu watakupa simu. Kiasi hicho cha pesa kinafahamika kama “kianzio” na kinaweza kuwa hata chini ya elufu 80 kwa baadhi ya simu(Ukubwa wa kianzio huwa kinategemeana na Thamani ya simu unayokopa). Baada ya kupewa hiyo simu utaanza kuitumia kama kawaida ila utatakiwa kuwa unalipia kiasi kidogo sana cha pesa kila siku mpaka utakapo maliza deni lako. Kiasi cha kulipa kila siku mara nyingi huwa kinakua ni chini ya Tsh 2000. Usipolipia simu hizi hua inajifunga na kukukumbusha kulipia ili uendelee kuitumia. Simu za mikopo ni nzuri sana kama hauna pesa nyingi za kununua simu ila unauhakika wa kupata pesa ndogo ya kulipia kila siku.

Nunua simu za ofa toka kwenye mitandao ya simu.

Mitandao ya simu kama vile Vodacom au Tigo huwa inakua na simu ambazo mtu unaweza zinunua kwa bei rahisi sana ukilinganisha na kuzinunua simu hizo kwenye maduka ya kawaida. Mara nyingi huwa mitandao hii inawaambia wateja wake kuwa watembelee katika maduka yao ili wajipatie simu za ofa. Ukienda katika maduka hayo utapata simu mpya za bei rahisi ambazo huwa zinakua mpaka chini ya 100000. Baada ya kununua simu hizo unaweza pewa bando la internet la kutumia mwaka mzima na pia huwa wanahitaji utumie mtandao wao kama mtando mkuu kwenye simu hizo. Hii ni njia nzuri ya kupata simu kwa bei rahisi hasa kama haupendi kuwa na deni.

Chukua simu zilizo tumika na mtu mwingine.

Muda huu kuna watu wanaziuza simu zao kwasababu mbali mbali na wamekosa wateja. Kuna watu wanauza simu laki 1 na waliinunua laki 3. Kuna watu wamezichoka simu zao wapotayari kuziuza hata chini ya laki. Unaweza pata simu nzuri tu toka kwa watu wanaoziuza simu zao ila utakiwa kuwa makini sana na simu hizi maana zinaweza kukupeleka pabaya. Ni vema ukikutana na mtu anaeuza simu ukamuuliza kwanini anauza, ametumia kwa muda gani inatatizo gani na kufuata taratibu zitakazo kuokoa pindi simu hiyo itakapokua imehuswa na tukio baya.

Ukitaka kupata simu inayouzwa mtaani kwako, tangaza kwa watu kuwa unahitaji simu ili hao watu wakisikia mtu anauzwa simu, wamlete muuzaji kwako. Kama hautaki kununua simu za mtaani kwako, unaweza tumia app kama Jiji au app ya Kupatana ila umakini unahitajika sana.

SMS nzuri kwa mpenzi aliembali(mapenzi ya mbali)

Ni kawaida sana kuona  wapenzi wanaopendana kukutana na sababu mbalimbali zinazopelekea wapenzi hao kuwa mbali. Sababu hizi zinaweza kuwa ni kazi, masomo na mambo mengine katika maisha. Wapenzi ambao wako mbali au  wanaoishi mbali ni vema wakazingatia sana mawasiliano na kuonyeshana upendo katika mawasiliano. 

Hapa The Bestgalaxy leo tunakupa orodha ya jumbe fupi za mapenzi ya mbali zinazoweza kutumika katika kuwasiliana. Kama mahusiano yapo kwenye hali hii basi unaweza tumia jumbe hizi:

Jinsi ya kuwa romantic kwa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

sms za mapenzi ya mbali

1. Umbali wowote kati yetu hauwezi kuuzima upendo wangu kwako Mpenzi. Kila siku nakuwaza na nazidi kukupenda tu huku natamani sana uwekaribu yangu.

2. Kukaa mbali na wewe ni kazi ngumu sana mpenzi wangu. Kuna muda natamani nije huko uliko niwe na wewe ila nikikumbuka kuwa kuna siku tutaonana, napata amani kidogo, Nakupenda sana.

3. Hata kama tuko mbali kimwili, moyo wangu daima uko nawe huko uliko. Nakupenda sana.

4. Napenda tunanyowasiliana, unanifanya nijisikie karibu nawe japo tuko mbali. Kichwa changu na moyoni mwangu bado upo wewe mpaka tutakapokutana tena.

5. Kuna malaika wa upendo nimenitokea na kuniambia kuwa penzi letu linapendeza. Umbali hauwezi kututenganisha mpenzi wangu, tuendele kuwa pamoja milele.

6. Usiruhusu shetani atumie mwanya wa sisi kuwa mbal,i kuua penzi letu. Penzi letu ni kubwa kuliko umbali wetu. Siwezi kukuona au kukugusa huko uliko ila tambua moyo wangu wote upo kwako.

Jinsi ya kutunza mahusiano ya Mbali BONYEZA HAPA>>>

7. Sikuizi nakosa joto lako tamu unalonipa pindi nikigusa mwili wako. Lakini bado nakupenda kwa nguvu zote. Jina lako limeandikwa ndani ya moyo wangu na haliwezi futika milele. Unaeweza fanya niumie au niendelee kufurahi ni wewe.

8. Moyo angu hulipuka kwa furaha kila tunapowasiliana. Hii ni kwasababu nakupenda na siku zinavyozidi kwenda, nazidi kukupenda leo kulio jana. Sipati picha nitakavyokua tukikutana.

9. Moyo wangu uko nawe, hata kama mwili wangu uko mbali na wewe. Umbali hauwezi yumbisha penzi langu  kwako. Nikishindwa kuvuilia nipo tayari kukufuata na sio kukuacha kipenzi changu.

10. Jukumu la kulinda penzi letu ni langu mimi na wewe mpenzi. Tunapokua mbali au karibu ni vema tukakumbuka jukumu letu mpenzi. Tusije ruhusu walioharibu mapenzi yao waalibu na yetu. Nakupenda sana.

Jumbe au sms kama hizi zinaweza kusaidia kuimarisha uhusiano wenu wa mbali na kumfanya mpenzi wako ajisikie kuthaminiwa na kupendwa. Pia ni vema kukumbuka kuwa mawasiliano ya mara kwa mara na jitihada za kukutana zinaweza kuwa na mchango mkubwa kwenye uhusiano wa mbali.

Uzazi wa mpango ni nini?

Karibu The bestgalaxy. Hapa unaenda kupata maaelezo yatakayo kufungua kidogo ubongo juu ya “Uzazi wa mpango. Uzazi wa mpango ni mpango au uamuzi wa mtu au watu katika kuzaa watoto .Lengo kuu la uzazi wa mpango ni kuruhusu wazazi kuchagua ni lini na idadi gani ya watoto wanataka kuwa nayo, kwa kuzingatia rasilimali walizo nazo zao, hali ya maisha, na malengo yao katika maisha. Kuna njia au hatua zinazochukuliwa na watu au jamii ili kudhibiti idadi ya watoto wanazozaa au kuepuka mimba zisizo tarajiwa.

Kuna njia mbalimbali za uzazi wa mpango na hapa chini tunaenda kuangalia njia 6:

Njia za uzazi wa mpango

1. Dawa za Kuzuia Mimba(Njia ya kisasa): Hizi zinaweza kuwa dawa za kumeza au sindano ambazo zinaweza kuzuia ujauzito. Mwanamke anaweza kwenda kwenye kituo cha afya akachomwa sindano ya kuzuia mimba au akameza vidonge vya kuzuia mimba.

2. Kondomu(Njia ya kisasa): Kondomu ni mipira amayo huvaliwa katika tendo kuzuia mimba na kujikinga dhidi ya magonjwa ya zinaa. Mwanaume kuvaa kondomu katika tendo kunaweza fanya mwanamke asipate mimba. Lakini pia kuna kondomu za kike ambazo mwanamke anaweza vaa kumsaidia asipate mimba.

3. Vitanzi(Njia ya kisasa): Hivi ni vifaa vinavyowekwa ndani ya mfuko wa uzazi na huweza kuzuia mimba kwa muda mrefu.

4. Vipandikizi(Njia ya kisasa): Hivi ni vijiti vyenye ukumbwa kama njiti ya kiberiti ambavyo huwekwa katika mkono wa mwanamke kwa lengo la kuzuia mimba.

5. Upasuaji wa Kuzuia Mimba(Njia ya kisasa): Kwa wanaume, upasuaji wa kufunga mirija ya uzazi (vasectomy) unaweza kutumika kuzuia mimba. Kwa wanawake, upasuaji wa kufunga mirija ya fallopian (tubal ligation) ni njia nyingine.

6. Kufuatilia mzunguko wa hedhi au kutumia kalenda(Njia ya asili): Pia unaweza zuia mimba zisizotarajiwa kwa kufuatilia mzuguko wa hedhi kisha kuepuka kufanya tendo katika siku za hatari.

Uzazi wa mpango unaweza kusaidia kudhibiti idadi ya watoto na kuboresha afya na ustawi wa wazazi na familia kwa kutoa fursa ya kuchagua lini na jinsi ya kupata watoto. Lakini unapawa kutambua kuwa njia nyingi za uzazi wampango za kisasa zimekuwa zilieta madhara kwa watumiaji. Ni vema kufika katika kitua cha afya na kupewa muongozo zaidi juu ya njia za kisasa za uzazi wa mpango. Njia ya Kufuatilia mzunguko wa hedhi au kutumia kalenda ni njia ya asili isio na madhara kwa mtumiaji ila ina hitaji umakini sana.

Mambo matano yanayoweza kusaidia kufanikiwa maishani

Kufikia mafanikio katika maisha yako kunaweza kuwa lengo linalohitaji juhudi na muda. Hapa kuna mambo matano unayoweza kufanya ili kuboresha nafasi zako za kufanikiwa:

  1. Jiwekee Malengo Maalum. kama unataka kufanikiwa nivema ukaanza kujiwekea malengo. Fahamu unataka kufanya nini na nini maaana ya mafanikio kwako. Jiulize lengo lako ni lipi, Unataka kufikia wapi na kwanini.
  2. Kuwa tayari kujifunza vitu au ujuzi mpya. Usijifunge kwenye kujifunza unapotaka kufanikiwa maana unapokua katika safari ya mafanikio unaweza kutana na vitu vingi sana na karibu vyote huwa vimelenga kukufundisha na kukukomaza kufikia pale unapopahitaji. Pia wewe mwenyewe unatakiwa kuwa ni mtu ambae unatafuta kujifunza vitu usivyovijua. Fanya utafiti na jifunze kutoka kwa wataalamu katika eneo unalotaka kufanikiwa. Jiunge na kozi, semina, au programu za kujifunza ili kuboresha ujuzi wako na kujiendeleza.
  3. Usiache Kujituma au kujisukuma kwa Bidii. Kuwa tayari kufanya kazi kwa bidii na kujitolea kufikia malengo yako. Kufanikiwa mara nyingi kunahitaji juhudi za ziada na uvumilivu. Kisukume kuendelea kufanya kazi kwa bidii hata wakati wa changamoto.
  4. Jenga mahusiano na watu waliofanikiwa au wanaoweza kukusaidia. Jiweke karibu na watu wenye uzoefu na wanaoweza kukusaidia kufikia malengo yako. Watu hawa wanaweza kutoa fursa za kujifunza, kushirikiana, na kujenga uhusiano ambao utarahisisha wewe kufikia malengo yako.
  5. Usiogope kuwa mbunifu au tofauti. Usiogope kufikiria nje ya box na kutafuta njia za ubunifu za kutatua matatizo ili kufikia malengo yako. Usiogope kuwa tofauti katika mambo yako maana sio kila kilicho tofauti hakipo sahihi.

Kumbuka kwamba mafanikio yanaweza kutofautiana kwa kila mtu na yanaweza kuwa na maana tofauti. Ni muhimu kuwa na uvumilivu na kujifunza kutokana na changamoto zinazojitokeza kwenye safari yako ya kufikia mafanikio.

UTAMU WA JUMLA 🔞 (Simulizi ya sauti)

Simulizi ya UTAMU WA JUMLA ni simulizi yenye uhusiano kidogo na simulizi ya SUKARI YA DADA. Unaweza sikiliza simulizi hii ukiwa ndani ya The Bestgalaxy Bure kabisa na pia unaweza ipakua na kufurahia kwenye simu au kifaa chako. Sikiliza simulizi hii katika mazingira tulivu yatakayo ruhusu kuielewa kirahisi.

Katika kuisikiliza ukiwa kama msikilizaji hakikisha unazingatia umri maana simulizi hii haitakiwi kusikilizwa na mtu mwenye umri chani ya miaka 18.

kama umebonyeza na inachelewa kuanza basi huenda ni tatizo la mtandao wako. Jaribu mara kadhaa kwa kusubiri.

Sehemu ya 1
Sehemu ya 2
Sehemu ya 3
Sehemu ya 4
Sehemu ya 5
Sehemu ya 6
Sehemu ya 7
Sehemu ya 8
Sehemu ya 9
Sehemu ya 10
Sehemu ya 11 (mwisho)

Kupata taharifa ya simulizi mpya na mambo mwengine, hakikisha unatembelea The bestaglaxy kila mara na pia unaweza jiunga kwenye group letu la Whatsapp Bure.

Maneno ya kumwambia Mpenzi wako usiku

Mukiwa katika mahusiano ya mapenzi mnaweza kuwa mnatumia muda mwingi kuongea au kuwasiliana kipindi cha usiku. Hii inaweza kuwa ni mmepigiana simu, mnatumiana sms(kuchati) au mupo sehemu moja mnaongea. Hapa chini kuna kuna orodha ya maneno ya kumwambia Mpenzi wako usiku pindi unapoishiwa maneno ya kuongea. Maneno haya yanaweza saidia kuanzisha mada nyingine usiku huo na kumfanya mpenzi wako afurahi au ajisikie vizuri kuwa na wewe usiku huo. Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy.

Jinsi ya kujua mtu mwingine anaona sms na unavyofanya WhatsApp kisiri SOMA HAPA>>>

Maneno ya kumwambia Mpenzi wako usiku (Mwanaume au Mwanamke)

Bebi ivi umeliona giza la usiku wa leo huko nje? Maisha yangu yanaweza kuwa zaidi ya hivyo bila wewe… sitamani utoke maishani mwanagu, nakupenda sana.

Yani natamani tungelala wote leo, natamani kuona macho yako mazuri ukiyafumba,natamani kusikia sauti za chini za ndoto zako za ucku huku nikiwa nimekukumbatia dear.

Ukiniambia nitaje vitu ninavyopenda toka kwako naweza anza kuvitaja usiku huu mapaka asubui na nisimalize.

Huku niliko ni baridi sana natamani nipate kumbato lako muda huu.

Ukihesabu nyota zote angani alafu idadi ya hizo nyota uizidishe mara milioni 100 ndio idadi ya sababu za moyo wangu kukupenda wewe.

Leo ukitaka kulala niambie mimi ntaendelea kuwa macho kukulinda mpenzi wangu.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika Mapenzi SOMA HAPA>>

Hapa sina usingzi, natamani nije nikukiss ndipo nilale.

Unaupa furaha moyo wangu usiku huu mpaka nashindwa kuelezea huraha hii.

Anaesoma ujumbe huu ni mtu ninaempenda sana na moyo wangu hudunda kwa furaha “Pah!” kila nikiona simu au sms toka kwake.

Sisi ni binadamu, Kuna muda huwa tunapatia na kuna muda tunakosea… Moja ya vitu vikubwa ambavyo nimepatia hapa duniani ni kukupenda wewe mpenzi.

Mtu anaesoma ujumbe huu ni mtu pekee ninaempenda katika maisha yangu. kunamuda nawaza nimwambie neno gani zaidi ya “Nakupenda” ili ajue nampenda sanaaa ila nakosa jibu, unaweza nisaidia kumwambia?

Nikiamka nikakuta hii ni ndoto nitafanya chochote ili nilale tena maana ninafuraha sana kuwa na wewe muda huu. Nahisi nipo ulimwengu mwingine.

Jinsi ya kuwa romantic kwa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Penzi lako kama pumzi, nalitaka kila muda… Ni zaidi ya Utamu wa asali au tunda.

Katika ulimwengu wa mapenzi ni bahati sana kupata mpenzi anaejua mapenzi siku hizi… Mimi bahati hii niliipata pale lipokupata wewe mpenzi wangu.

Najivunia kuwa na wewe usiku huu.

Namna 3 za kutumia mitandao ya kijamii vizuri (Kaa kijanja!)

Hapa The bestgalaxy, tunakufungua kidogo juu ya namna gani unaweza tumia mitandao ya kijamii vizuri. Mitandao ya kijamii imekua na mchango mkubwa katika mambo mbalimbali kwa binadamu wa sasa. Moja ya vitu vikubwa Teknolojia kupia mitandao ya kijamii imefanya ni kutuweka binaadamu pamoja na kutufanya tuwe na uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii kufanya au kupata vitu mbalimbali kirahisi. Zifuatazo na namna tatu za kutumia mitando ya kijamii vizuri.

Namna 3 za kutumia mitandao ya kijamii vizuri

Kupata burudani

Kama unapenda burudani basi Mitandao ya kijamii ndio sehemu ambayo inaweza ukukupa vitu vingi unavyoweza hitaji kuburudika. mitandao ya kijamii imekusanya vitu vingi sana ambavyo huburudisha na kufanya mtu apunguze msomgo wa mawazo. Ikiwa unataka kutumia mitandao ya kijamii kujiburudisha fanya kuingia kwenye vikundi vya burudani au kuzifuata kurasa zinanzo jihusisha na burudani ili kupata burudani toka kwenye kurasa hizo kirahisi. Pia usiache kutoa maoni na kuonesha umependezwa na vitu vinavyokuburudisha ili mitandao hiyo ya kijamii iwe inakuonesha mambo yatakayokuburudisha zaidi.

kujifunza vitu vipya

Kwenye mitandao ya kijamii unaweza jifunza vitu vipya pia. Kuna vikundi na kurasa ambazo hufundisha mambo mbali mbali kama vile, Ujasiliamali, Afya na Teknolojia. Endapo utakua ni mfutatiliaji mzuri wa vikundi na kurasa za namna hii, unaweza kuwa unajifunza vitu vipya vinavyo weza kuwa na msaada kwenye hata maisha yako. Katika matumizi yako ya mitandao ya kijamii, kwa na muda wa kufuatilia mambo yatakayokujenga na kukufungua ufahamu wa mambo mbalimbali ya msingi katika maisha yako.

kufanya biashara au kuingiza pesa

Ukiachana na kupata burudani na kujifunza vitu vipya, mitandao ya kijamii pia inaweza kutumika kufanya biashara au kuingiza pesa kiujumla. Hii ni mada pana sana maana kunanjia njingi za kufanya hayo na huwa zinatofautiana kutokana na mitandao kuwa tofauti pia. lakini kifupi sana ni kwamba unaweza tumia mitandao ya kijamii kuonesha biashara yako ili kuwafikia watu wengi wanaoweza hitaji huduma yako. Ukiachana na biashara, mitandao ya kijamii mingine huwa inatoa nafasi kwa content creators kuingiza pesa.

Angalizo: kufanya biashara au kuingiza pesa kwenye mitandao kuweza kuwa sio rahisi kama baadhi ya watu wanavyofikilia. Mara nyingi huwa kunahitaji uwekeze Akili, Pesa au Muda ili kufika unapo hitaji. Ukiingia kichwa kichwa unaweza poteza pesa na muda.

Mambo humfanya mwanaume akupende sana na kukuchagua maishani

Kumekuwa na mahusiano mengi ambayo huanzishwa lakini hayafiki mbali kama lilivyo lengo kuu la mahusiano yao. Hali hii inafanya wanawake wengi wawe na wasiwasi katika mahusiano. Wamekua wakifikilia “Je, atanifanya niwewake wa maisha?” Lakini wanasahau kujiweka tayari kwaajili ya kuwa wanawake wa maisha.
Kuna vitu vidogo vidogo ambavyo vinaweza mfanya mwanaume akuweke moyoni na akufikilie kuwa wewe ni wake wa maishani. Hebu tumia muda wako kuvisoma hapa chini.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika Mapenzi BONYEZA HAPA>>>

Mambo humfanya mwanaume akupende sana na kukuchagua maishani

Tabasamu.

Kama unahitaji mwanaume avutiwe na wewe basi tambua kitu muhimu kufanya unapokuanae ni kutabasamu na kucheka. Usionyeshe uso usio na urafiki. Kuwa kama mtu anayependeza, mwenye urafiki, na mchangamfu. Ukijitahidi kuwa mtu mwenye furaha kuliko maugomvi. Onensha sura ya tabasamu kuliko makasiliko. Mapenzi yenu yanaweza kuwa na furaha pia na hakuna mwanaume asiependa mapenzi yenye furaha.

Whatsapp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa BONYEZA HAPA>>>

Kuwa mcheshi.

Wanaume kwa ujumla wanapenda wasichana wenye ucheshi ambao wanaweza kuwafanya wajisikie vizuri. Kuna muda mwambie hadithi za kufurahisha na usiogope kucheka. Kumbuka usizidi kupita kiasi hadi uonekane kama mchekeshaji. Ni vizuri kuwa na mwenzi ambaye anafurahisha, lakini ni watu wachache sana wanamawazo ya kuishi na mchekeshaji.

Toa kuliko kuchukua.

Ili kuongeza nafasi zako za kukupenda lazima utoe kuliko kuchukua. Mwanaume anaweza kutofautisha kwa urahisi kati ya msichana ambaye anataka kitu kutoka kwake na yule anayemjali.
Nadhani unajua kuna wasichana wengi ambao wanafuata pesa na wameweka mbele pesa kuliko mahusiano. Wanaume wengi wanao wafuata wanawake wa mtindo huu huwa hawana mpango nao wa maisha maana huona kama wananunua upendo hivi… Jitofautishe na wauzaji na aone unavutiwa naye kwa upendo wake na sio pesa yake au kitu kingine chochote. Yani hata akitanguliza gari mbele usishoboke nalo sana kuliko kumpenda yeye maana baadae anaweza anza kulisifu gari kwa kukukamata wewe na mbaya zaidi inaweza kuwa ni wanawake wengi walinaswa na gari hilo hivyo, haunajipya.

Mpenafasi ya kufanya kazi, Mshauri na kumtia Moyo.

Unaweza sikiliza hii

Katika maisha Mwanaume maranyingi huzungukwa na vitu vinavyomkatisha tamaa na kumuumiza lakini anatakiwa ajikaze tu kwasababu ni “Mwanaume”. Hii inaweza kuwa kazini, kwenye familia na maeneo mengine. Endapo mwanaume anaejielewa atapata mwanamke ambae anamsikiliza mambo yake magumu, anamshauri, anamtia moyo na kumsukuma kufanya maamuzi mazuri na maendeleo hata kwenye mambo madogo kwenye maisha, hawezi kumuacha mwanamke huyo aondoke maishani mwake. Kuna familia huwa zinainuka na kuwa na mafanikio kwasababu ya jambo hili, hasa zikiwa na mambo ya kidini ndani yake.

Kama muko kwenye mahusiano na mwanaume na anaonekana kuwa busy sana na kazi mpaka anafikia kuwa mbali na wewe, Usimfikilie tofauti moja kwa moja na kuanza vurugu. Mruhusu mwanaume afanye kazi kidogo ili kufanya maendeleo kisha vumilia pindi anapokua mbali na wewe ila usijisahau kumuonesha upendo sana.

Hili ni jambo ambalo linaweza kuongeza sana nafasi zako za kushinda upendo wake. Wanawake wegi wanakata tamaa na kumuacha mwanaume wanapoona yupo busy Sana na maisha… huzani kuwa hawana nafasi tena lakini jua kuwa wakati huo ndio wakati mzuri wa wewe kuongeza upendo wake kwako.

Jinsi ya kuwa romantic kwa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>


Muoneshe kuwa bado yupo moyoni wako, muoneshe kuwa unajua anachokifanya na ukipata muda muulize maswali au kumshauri, muoneshe kuwa bado unamjali hii itamfanya akuweke katika fikila zake za kimaisha. Usijekosa maisha mazuri anayokupambania kwa kukata tamaa.

Lakini unapo mruhusu afanye kazi mbali na wewe hakikisha unafanya vitu vya upendo ambavyo vitamfanya aanze waza kukuweka karibu yake au kuja karibu yako(kama atakua na uwezo huo). Ukipata nafasi pia mtembelee au fanya mautundu akutembele.

#Muvumilie anaejali upendo na uvulilivu wako tu, Wanaume wengine hukimbia mazima.

Usimmiliki sana kuliko kumuonesha upendo.

Wanawake wengi hufanya makosa ya kumiliki sana mwanaume na wakati hata hawamuoneshi upendo. Unaweza kujaribu kumlinda sana asiende kwa wanawake wengine ili abaki kuwa na wewe pekee katika maisha yake lakini je anao wafuata wanamvuta kama jinsi unavyo fanya wewe?. Ni wazi kuwa wanamvuta kwa upendo na vitu vingine vizuri… hivyo na wewe kuwa mbunifu na kwenye kumuonesha upendo ambao utamvutia zaidi kisha mruhusu aamue kuchagua kinachomfaa. Ikiwa wewe ndiye wa kwake, hakika atakupenda.

”kwanini wanawake wazuri/warembo hawaolewi?” sababu zinaweza kuwa hizi BONYEZA HAPA>>>

Kuwa na maadili mema.

Maadili mazuri ni lazima katika kumshawishi mwanaume akupende zaidi na aweke moyo wote kwako maishani. Hakuna mtu anayetaka kujihusisha na mtu ambaye haeleweki,hasikii au hana nidhamu. Bila shaka kila mtu husita kumpa moyo mtu ambae hana maadili mazuri. Wanaume wanapenda wanawake ambao wana nidhamu. Hivyo basi muheshimu na pia uwevizuri nae ataona unafaa kuwa wake maishani. kuna mambo unawezasikia rafiki au mwanawake wa mitandaoni Eti “Ukinichiti nakuchiti” “Wanaume wote ni Mbwa” “Siwezi kuwa na mwanaume mwenye gari au pesa” “Siwezi olewa kwa sasa mimi ni mzuri” na mengine mengi kama hayo. Ukileta mambo hayo kwenye maisha yako unaweza angukia pua, ni vema kutula kuwa na maadili yatakayomkaribisha mtu kuwa na wewe maishani. Onesha heshima kwa Mwanaume hata wakikuita mshamba. Kuwa msafi, vaa vizuri na marafiki wastaarabu.

Jinsi ya kujua mtu mwingine anaona sms na unavyofanya WhatsApp kisiri

Whatsapp ni mtandao mkubwa ulimwenguni ambao watu huutumia sana katika mawasiliano. Unaweza kuwa ni mtandao wako pendwa katika mawasilioano ndio maana upo hapa… Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy, utajifunza vingi kuhusu mtandao huu.

Whatsapp ni mtandao mzuri kuutuumia katika kuwatumia watu Picha, Video, Audio au ujumbe wa maneno lakini unapofanya hivyo tambua kuwa kunajinsi ambavyo mtu mwingine anaweza kuona vitu vyote hivyo kwenye simu au kifaa chake bila wewe kutambua(kisiri). Kuna njia ambazo hata mtu asiebobea sana katika maswala ya Teknolojia anaweza tumia kuona sms au vitu unavyofanya kwenye Whatsapp. Lakini jambo hili lisikutishe maana hapa chini tunakwenda kukujuza jinsi ya kuangalia kama upo salama na jinsi ya kujilinda pia… Kwaiyo ondoa hofu na endelea kutumia Whatsapp yako kama kawaida.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kujua mtu mwingine anaona sms na vitu unavyofanya WhatsApp kisiri

Whatsapp kwa sasa inakuruhusu mtumiaji wake kuunganisha akaunti yako moja ya Whatsapp kwenye kifaa zaidi ya kimoja. Unaweza fannya akaunti yako moja ya WhatsApp iwe inatumika kwenye simu mbili mpaka 4 na namba ikawa hiyo hiyo moja. Mtu mingine anaweza kuitumia hii kunganisha akauti yako kwenye simu yake au kifaa chake na kuanza kukuchunguza unachofanya bila wewe kujua. Na mtu akitumia ataweza kusoma sms zako, kujibu, kuona na kuchua audio,video na vitu vingine unavyotuma na kutumiwa bila wewe kujua.

Ukitaka kujua kama akaunti yako ya Whatsapp imeunganishwa fanya yafuatayo:

  1. Fungua Whatsapp yako na uguse Vidoti Vitatu
  2. Ukifanya hivyo, Chagua “Linked divices”
  3. Baada ya kufanya hivyo utatupwa kwenye ukurasa ambao ukikuta kuna kifaa chochote kiorodheshwa basi jua whatsapp yako sio salama. Na kama hamna kifaa basi yawezekana upo salama. Unaweza angalia picha hapa chinikuelewa zaidi.

Endapo utakuta akaunti yako ya Whatsapp sio salama(hacked) unaweza gusa kifaa kilicho orodheshwa kwenye kwenye ukurasa huo alafu ukagusa vidoti vitatu itakavyoonekana juu kulia kisha utachagua “Remove device”.

Ili kuhakikisha kuwa WhatsApp yako iko salama kila mara, hakikisha unafanya kuangalia kama akaunti yako ya WhatsApp imeunganishwa mara kwa mara hasa baada ya kumruhusu mtu mwingine aishike simu yako bila uangalizi wako.

Mtu akikublock WhatsApp Fanya hivi kuchati nae BONYEZA HAPA>>>