Category Archives: Uncategorized

Jinsi ya kupata Views nyingi kwenye Status (WhatsApp)

WhatsApp Status views tunaweza sema ni idadi ya watu walioangalia au kuona status ya WhatsApp. Kipengele cha stutus katika WhatsApp kinakuruhusu mtumiaji wa WhatsApp kushiriki vitu na watu wengine kama vile picha, video au Audio.

Ili mtu kuona vitu ulivyoweka kwenye kipengele cha WhatsApp status ni lazima uwe umetunza namba yake kwenye simu yako na yeye pia we ameitunza namba yako. Ikiwa mmoja wenu atakua hajatunza namba ya simu, status hazitaonekana kwa yoyote kati yenu.

Lakini usipoona status ya mtu au asipoonekana kuwa ameangalia stutus, haina maana hajatunza namba yako. Anaweza kuwa mtu huyo hajaposti status ndio maana haujaiona status yake. Pia anaweza kuwa anatumia kipengele cha WhatsApp cha kuzuia usijue anapoangalia status zako. Kipengele hii wemewahi zungumzia katika ukurasa mwingine wa The bestgalaxy.

Kumekua na maswali mengi watu huuliza juu ya jinsi au namna ya kuongeza Stutus views. Jambo hili kwa sasa ni rahisi sana maana kila mtu anajua kuwa kadri jinsi unavyoongeza namba za watu kwenye simu yako ndivyo unaweza pata watu wa kuangalia status zako na pia utakua na uwezo wa kuangalia status zao. Kwaiyo kitu muhimu hapa ni kuungana na watu wengine wanaotumia WhatsApp.

Hapa chini, The Bestgalaxy tunaenda kukupata mambo machache yanayoweza kukusaidia katika safari yako ya kupata views nyingi katika WhatsApp status.

Mambo yanayokupa views nyingi kwenye status za WhatsApp

Kuungana na watu wengi kwenye WhatsApp

Ili kupata views nyingi, unatakiwa kuwa na watu wanaoangalia status. Sasa inamaana unatakiwa kwanza uungana na watu wako wa karibu kwenye WhatsApp. Yaani uchukue namba zao za simu na pia wachukue zako. Kama unamarafiki, ndugu, wateja au watu mnaojuana basi itakua vizuri ukichukua namba zao na kuwa nao pamoja kwenye WhatsApp. Jambo hili ni lakawaida kwa sasa, watu wengi wanapenda kuungana kwenye WhatsApp hivyo ni jambo rahisi.

Kupost mambo mazuri

Kwenye status za WhatsApp unaweza weka kitu chochote kisichovunja sheria za WhatsApp. Hivyo unaweza weka kitu chochote unachojiskia na watu wakakiangalia.

Lakini watu waoangalia status zako kunavitu ukiweka wanaweza wasivipende au visiwavutie kufungua status zako mara kwa mara. Kutokana na hili, kama unataka watu wengi wa view status zako ni vema ukawa unaposti vitu vizuri vitakavyo wafurahisha hata wao na sio kinacho kufurahisha wewe tu. Weka mbali majungu na matusi alafu jaribu kuposti mambo kama vichekesho, ushabiki wa mpira na vitu vingine vya kufurahisha.

Kuweka Video au Picha chache

Kuposti video nyingi au picha nyingi kwenye status za WhatsApp kunaweza punguza views. Unaweza fanya hivi mara chache isiwe na madhara lakini ukiweka kama ni tabia yako, kuna jinsi watu wanaweza anza kupuunza status zako Kwasababu ya kuokoa muda au bando.

Jaribu kuweka vitu vichache kwa siku kwenye WhatsApp status yako ili kuongeza status views. Watu wana status nyingi sana za kuview siku hizi. Hivyo jaribu kuweka stutus zitakazo wachukua dakika chache kuzimaliza.

Kujihusisha na WhatsApp stutus za watu wengine

Kama haupo kibiashara (upo kama mtu binafsi) jiwekee tabia ya kutoa maoni kwenye status nzuri za watu wengine. Jihusishe na status za WhatsApp za watu wengine alafu wakipenda, wanaweza anza kujihusisha na zako. Kama unawatu wengi inaweza kua ni ngumu, lakini ukiweza itakua ni jambo zuri pia.

Kwakufuata mambo haya unaweza kuwa ni mtu mwenyewe mafanikio katika kupata views nyingi kwenye status za WhatsApp. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy na usichoke kuitembelea.

SMS za kumchekesha mpenzi wako

Kumfurahisha mwanamke au mwanaume wako ni moja ya njia bora za kudumisha upendo na furaha katika mahusiano. Kutuma ujumbe mfupi wa kumchekesha ni njia rahisi na ya kupendeza ya kumfanya mpenzi wako afurahi. Ujumbe huu unaweza kumfanya atabasamu bila kutarajia, hata kama ana siku ngumu au anapitia changamoto fulani.

Katika makala hii, tumekusanya orodha ya SMS za kuchekesha ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ili kuleta tabasamu la bila kutarajia usoni mwake. Ujumbe huu si tu utaimarisha uhusiano wenu, bali pia utaleta ladha na ucheshi ambayo watu wengi huipenda katika mahusiano. Kumfurahisha mpenzi wako kwa njia ya kumtumia sms za ucheshi, kunaweza weka hata ugumu kwa mpenzi wako kusahau.

Kabla ya kuingia moja kwa moja kwenye orodha, fahamu kuwa jambo hili linatakiwa kufanywa kwa kiasi tu. Usizidishe utani au vichekesho kwenye mahusiano ya mapenzi. Unatakiwa kujua wakati gani unafaa kufanya utani au vichekesho kwa mpenzi wako.

Soma Simulizi ya Sukari Ya Dada BONYEZA HAPA>>>

SMS za kumchekesha mpenzi wako (Mwanamke au Mwanaume)

  • Tangu uliponiambia “Nakupenda”, nahisi kama Dunia yote hii ni yangu mimi na wewe alafu Hawa wengine wapangaji wetu😂
  • Kitoto kidogo kilimwambia baba yake “Baba ivi wewe umezaliwa wapi?” Baba akajibu “Nimezaliwa Mbeya”. Mtoto akasema “Mama nae kazaliwa Mbeya?” Baba akajibu “Hapana, amezaliwa Tanga”. Mtoto akauliza “Na Mimi jee?” Baba akajibu “Dar”. Mtoto akasema “Mh Sasa tulikutanaje????” Baba cheko😂😂
  • Kabla sijakwambia “Nakupenda” nilikua nikijaribu mara nyingi sana kutaka kukuambia. Lakini kila nilipotaka kukuambia, nilikua nasahau maneno yote kama mtoto aliesahau alichotumwa dukani😂😂
  • Wewe kwangu ni kama WiFi tu. Ukinisogelea mtandao unapanda “Pap!”😂
  • Nikiamka asubuhi huwa nakuangalia wewe hapo kama umeamka salama na bado unanipenda. Yani kiufupi nakuangalia moyo wangu kama unadunda😂😂
  • Kuna mtoto wa mtu nampenda hapa mpaka nahisi nimelogwa. Au nikuulize wewe mwenyewe vizuri tu, ulienda kwa mganga gani kuniloga?😂😂
  • Watu watatu washamba walisafiri, walipofika kwa ndugu yao mjini wakapewa soda wakasemezana kuwa “Ni tamu sana”. Walipokua wakiondoka, mmoja alitia kizibo cha kisoda kwa siri kwenye mfuko. Baadae walipotoka nje akamnong’oneza mwenzie “Mwenzio nimechukua mbegu nikapande”😂😂.
  • Usiku nimeota nipo na wewe umenikiss alafu umeniambia chukua hii laki 5 kama zawadi. Nilivyoona unanipa hela nikashtuka 😂😂
  • Nilipokuona mara ya kwanza nilirudi nyumbani salama ila moyo ndio sikurudi nao. We mwizi uliniibia moyo mpaka nikakupa mazima😂
  • Jana nilipanga Leo nikupe 50,000 kama zawadi. Lakini mapenzi upofu mpenzi wangu, hapa pesa yenyewe hata siioni, nakuona wewe tu😂
  • Najua wivu ni mbaya kwenye mapenzi ila utanisame tu. Yani tangu niione, natamani kuifunga hiyo kitu nifaidi mimi tu😂
  • Mtu akituangalia tunakua kama watu wa heshima. Kumbe kuna muda mimi na wewe baby wangu tuna ruka ruka kama Spider-Man😂😂
  • Niliwaza kuanza kukupa Tsh 5000 Kila ukitabasamu maana unaupa Raha moyo wangu. Lakini nikaona nitafirisika maana unatabasamu kila mara na kunipa Raha hatari😂😂
  • Malaika wenzako wapo kupeperuka angani huko, wewe nimekukamata kimapenzi huku😂
  • Kwajinsi ninavyokupenda, ukiniacha nitajiribu kukuloga mpenzi wangu sikufichi😂
  • Nikifanikiwa kuwa Raisi wa nchi, utapenda nikupe Mkoa gani kama zawadi we mwanaume?😂😂
  • Kuna mlevi alikamatwa akikojoa eneo la Shule na Mwalimu mkuu akaulizwa “Hilo bango hapo limeandikwaje?” Mlevi akamjibu ‘Limeandikwa USIKOJOE HAPA’ Mwalimu akajibu “Kwahiyo umefanya nini hapo? Unataka nikupeleke polisi?” Mlevi kwa makini na upole akajibu “HAKI YA MUNGU NILIKUA NAJUA NDIO JINA LA SHULE!” 😂😂
  • Kwa jinsi ninavyo kupenda na ulivyo muhimu kwangu, Usije waza mimi kukuacha wewe. Kwani wewe unaweza kuacha kupumua?😂
  • Unanifanya nijione mwenyewe bahati kuwa na wewe mpaka natamani ni nimshukuru Ex wangu kwa kuachana na mimi😂
  • Umeshawahi kutembea bila viatu kwe barabara ya kokoto? Hiyo ndiyo hali ya moyo wangu bila wewe😂
  • Hebu fanya kuziba pua na mdomo kwa muda wa dakika 10 hivi. Hivyo ndio huwa nahisi nisipokuona au kuisikia sauti yako kwa muda My love😂
  • Kila ukijubu SMS moyo wangu kwa furaha unalia “Pah!” Umeniloga eti?😂😂
  • Hebu jibu sms haraka kabla sijakufuata. Yani nikikumiss kama hivi, Naweza hata kupaa nitue hapo😂

Katika huu mwisho wa orodha yetu, napenda kukukumbusha kuchagua wakati mzuri wa kumtania au kumchekesha mpenzi wako kwa SMS. Wakati mzuri ni ule muda ambao unahisi mpenzi wako anaweza soma SMS zako na kucheka. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine mazuri zaidi.

Michezo ya kuchati na Mpenzi wako kurefusha maongezi BONYEZA HAPA>>>

Warzone Mobile: Tatizo la kukwama katika “CONNECTING TO ONLINE SERVICES”

Call of Duty Warzone Mobile ni game maarufu la vita unaloweza cheza kwenye simu. Ni moja ya game za “shooting” zinazo ruhusu mchezaji kupambana au kushirikiana na watu wengine katika vita. Wachezaji wengi kutoka pande mbalimbali hapa ulimwenguni wanaweza kuungana kama Team ili kupambana pamoja katika vita ndani ya game hili.

Kitu kingine kizuri kuhusu game la Call of Duty Warzone Mobile ni kwamba linachezwa bure. Lakini kuna vipengele vya ziada ambavyo unaweza kununua kwa kuhushisha pesa halisi. Unaweza kununua mavazi maalum, vifaa vya kipekee na mambo mengine yanayokusaidia kuwa na nguvu zaidi katika mapambano.


Kiufupi, Warzone Mobile ni game zuri ingawa kunabaadhi ya Wachezaji wake hukumbana na changamoto au matatizo mbalimbali toka lilipotolewa. Moja ya matatizo ni kukwama katika “CONNECTING TO ONLINE SERVICES” unapolifungua game na kutaka kulicheza. Hapa chini, Kuna njia ambazo ukitumia, unaweza fanikiwa kujitoa katika kukwama huko.

Jinsi ya kucheza game za Xbox katika Simu BONYEZA HAPA>>>

Njia za kuondoka katika “CONNECTING TO ONLINE SERVICES” kwenye Warzone Mobile

Kuwa katika Internet yenye kasi

Kuna muda game la Warzone Mobile linaweza kwama unapolifungua Kwasababu haupo kwenye mtandao wa internet mzuri. Hili ni game la Online na huitaji internet yenye kasi ili uweze cheza bila matatizo. Internet yenye kasi ni jambo la msingi katika kufurahia kucheza Call of Duty Warzone Mobile maana game hu-stream Online baadhi ya vitu kuhusu game.


Kwaiyo kama utakumbana na tatizo la “CONNECTING TO ONLINE SERVICES” kwasababu hii, jaribu kuwa katika mtandao wa internet wowote wenye kasi zaidi ya unaotumia.

Tumia Data badala ya Wifi

Ikiwa umepata tatizo la kukwama katika Warzone Mobile alafu unatumia internet kutoka kwenye Wifi, fanya kutumia Data. Hamisha simu yako kutoka kwenye Wifi uliojiunganisha kisha washa Data la simu yako.

Kwa kufanya hivyo, unaweza kuona game haligandi katika sehemu ya “CONNECTING TO ONLINE SERVICES”. Baadhi ya watu hutumia njia hii kucheza game pale linapokwama. Lakini sio kila mtu akifanya hivi, tatizo huondoka. Kwa watu wengine, njia hii hugoma na huwa wanatumia njia iliopo hapa chini.

Vuka tatizo kwa VPN

Unapokuwa na tatizo la kukwama katika Warzone Mobile, unaweza kutumia VPN kuvuka sehemu uliokwama. Yani washa VPN kisha fungua game. Baada ya kufungua game, halita kwama tena ila ukivuka sehemu ambayo huwa inakwama, utatakiwa kuzima VPN ndipo uendelee kulicheza. Usipo Zima VPN unaweza ukashindwa kuingia katika mode yoyote kucheza.

Unaweza tumia VPN yoyote kufanya hivi na asilimia kubwa ya watu hutumia njia hii wanapokwama.

Mwisho; Warzone Mobile ni game nzuri sana na huchukua nafasi kubwa katika simu pia. Swala hili linaweza kuleta ugumu wa kufanya maamuzi ya kulifuta katika simu na kuliingiza tena. Lakini kama mbinu zote zitashindikana, unaweza fanya maamuzi ya kufuta na kuliiingiza upya katika simu yako ili kutatua tatizo. Njia hii sio nzuri sana lakini inaweza kuweka mambo sawa pia.

Jinsi ya kutengeneza Pesa mtandaoni ukiwa Mwanamuziki (Muimbaji)

Kutengeneza pesa ukiwa kama Mwanamuziki ni ndoto ya watu wengi. Ndoto hii inaweza kuwa inaonekana ni ngumu kuitimiza lakini kwa kiasi flani mitandao au internet, imewawezesha wanamuziki wengi kutimiza ndoto zao. Kuna njia nyingi sana zinaweza muingizia pesa Mwanamuziki katika Internet kwasasa.


Mbali na kuingiza pesa, internet au mtandao, umekua na mchango mkubwa sana katika muziki. Zamani mtu akiwa anataka kusambaza muziki wake alilazimika kutumia nguvu na gharama kubwa kuusambaza muziki ukiwa kwenye vifaa kama CD au Tape. Lakini hivi sasa, Mwanamuziki anaweza sambaza Muziki wake mtandaoni ukawafikia watu wengi kwa muda mfupi bila kutumia nguvu kubwa.

Nafikiri hata wewe umeisha wahisikia nyimbo nyingi za wasani wa hivi sasa hufikia mamilioni ya wasikilizaji ndani ya masaa 24 tu. Jambo la nyimbo kuwafikia mamilioni ya watu katika masaa 24 lilikua ni jambo ngumu sana hapo zamani.


Kiufupi ni kwamba, nyakati hizi zimefungua njia nyingi za wasani wa muziki kuonesha kazi zao kwa watu na kutengeneza pesa. Hapa The bestgalaxy tunaenda kukupa njia za kutengeneza pesa mtandaoni ukiwa kama Mwanamuziki Muimbaji. Hii inaweza kuwa na msaada sana kama utakua ni mwimbaji uliedhamilia kutengeneza pesa online (mtandaoni).

Njia za kutengeneza pesa mtandaoni ukiwa Mwanamuziki (Muimbaji)

Kulipwa na platform za kusikilizia muziki



Kuweka nyimbo zako ulizoimba katika platform za kusikilizia muziki kama YouTube, Spotify na Boomplay, kunaweza kuingizia pesa pindi utakapo pata wasikilizaji wengi. Hii ni njia ya kisasa ya kuuza muziki katika kipindi hiki na wasanii wengi wakubwa wanaitumia kupata mamilioni ya pesa inazowawezesha kuishi maisha ya ndoto zao.
Mara nyingi, pesa unayopata katika platform hizi huathiliwa na mambo kama idadi ya wasikilizaji na nchi wanayotoka. Lakini unapoanza ni vema ukaweka mbali kidogo maswala ya pesa alafu ukatumia platform hizi kujenga Brand tu.

Kutangaza biashara za watu katika kurasa



Ukiwa mwimbaji mzuri unaefuatiliwa na watu mpaka katika kurasa za mitandao ya kijamii, unaweza tumia kurasa hizo kutengeneza pesa. Watu au wafanya biashara wanaweza kuwa wanakulipa ili kutangaza biashara zao katika kurasa zako. Ukiwafanikiwa kuwa na ushawishi mkubwa, unaweza wavutia watu wengi wakafanya deals zitakazokufanya uione thamani ya kufanya Muziki wako.

Kuimba ukiwa LIVE kwenye platform zenye zawadi



Kuna Platform zinazomruhusu mtu kuwa LIVE kupitia kamera ya simu au vifaa vingine alafu watu wanakua wanamuangalia anachofanya na kumpa zawadi wakipenda(Mfano: TikTok). Ukiwa kama Muimbaji, unaweza kutumia “LIVE” kama sehemu ya kufanyia performance za nyimbo zako. Watu wengi wapo kwenye mitandao kama TikTok wanaingia LIVE na kuimba nyimbo zao zinazogusa mioyo ya watu mpaka wanatoa zawadi.
Zawadi hizi zinaweza kuwa ni pesa nyingi sana kama watu wanaokuangalia watakua wanakuunga mkono kwa unachofanya.

Kutumia muziki kuonesha huduma zako nyingine mtandaoni



Kuna huduma yoyote unayoitoa na inaweza kupa pesa mbali na Muziki? Kama unayo, Muziki wako ukifanikiwa kufanya vizuri mtandaoni basi tumia shughuri zako za kimuziki kutangaza huduma hiyo mtandaoni. Ukichanganya vitu hivyo vizuri, unaweza nufaika na Muziki wako kuliko kitu chochote kwenye muziki. Watu wengi waliofanya hivi na kufanikiwa, huielewa nguvu yao na kueshimu sana muziki.

Wakati ukiendelea kuyafikilia hayo yote tulioyaweka hapa juu, ni vema ukajua kuwa kila njia iliopo hapa, inakuhitaji upambane kidogo maana sio rahisi japo inawezekana. Ila ukifanikiwa unaweza kuwa unaetengeneza mamilioni ya pesa kwa mwezi huku ukiishi maisha ya ndoto zako.

Mambo hautakiwi kukurupuka kumshauri rafiki kuhusu Mahusiano

Kuna nyakati ambazo marafiki wanaweza kuhitaji msaada wako wanapopitia changamoto katika mahusiano yao ya kimapenzi. Lakini ni muhimu kukumbuka kwamba si kila mara unapaswa kutoa ushauri. Wakati mwingine, jambo bora zaidi unaloweza kufanya ni kumsikiliza tu rafiki yako bila kutoa maoni au mapendekezo yasiyoombwa. Na hata ukihitajitajika kutoa ushauri, unatakiwa kufikilia sana kabla ya kutoa.



Mahusiano ya mapenzi ni jambo binafsi na yana mambo mengi ambayo kila mtu anaweza kuwa na njia yake ya kushughulikia matatizo au kuchukua maamuzi. Unaweza kuwa na nia njema ya kutoa ushauri kwa mtu kuhusu mahusiano yake lakini baadae ukaonekana unania mbaya au ukagundua umewapeleka sehemu mbaya.



Kama umeletewa jambo na rafiki yako kuhusu mahusiano yake, hakikisha unalichimba kwa kina jambo hilo kabla hauja litolea ushauri. Baadhi ya mambo ambayo ambayo ukiletewa hautakiwi kukurupuka kuyatolea ushauri ni yafuatayo:

Dalili za Ex wako kukupenda BONYEZA HAPA>>>

Mambo hautakiwi kukurupuka kumshauri rafiki kuhusu mahusiano

Kuachana na mpenzi wake



Mahusiano ya mapenzi yanaweza pelekea rafiki yako kutaka ushauri ambao unahusiana na kuachana na ampendae. Kabla hauja mshauri lolote juu ya kuachana kwao, fahamu kuwa kugombana au kuyumba kwa mahusiano kunaweza kuwa sio mwisho wa mahusiano.

Watu wengi hugombana na kutoelewana kwenye mahusiano lakini baadae hutulia na kuwa sawa.
Sasa ushauri wako kwa wapenzi waliogombana ni vema ukawa ni ushauri wa kujenga mahusiano au kuwasaidia kurejesha amani kati yao. Ikishindikana kabisa au kukiwa na sababu ya msingi sana ndio unaweza washauri kuachana kama wanavyohitaji kufanya.

Hatua juu ya ujauzito wasio utarajia



Swala la kuzuia mimba zisizotarajiwa ni jambo la muhimu sana kushaurina na kuliongelea hata na marafiki. Lakini Swala la hatua za kuchukua juu ya ujauzito uliotokea bila kutarajiwa ni swala linanowahusu zaidi wapenzi na sio marafiki.


Kuna watu wengi hupata ujauzito katika hali ya kutotarajia, huzaa watoto na watoto hao huwa baraka ambayo hawakutarajia katika Maisha yao. Kwaiyo unapoletewa swala na rafiki kuhusu ujauzito ambao hawakutarajia ni vema ukawa upande chanya zaidi. Na kama utakua na ushauri hasi, basi kuwe na Sababu ya msingi sana.

Kutafuta ubaya wa mpenzi wake



Unaweza taka kumshauri rafiki yako kuhusu kuutafuta ubaya wa mpenzi wake lakini fahamu kuwa jambo hili sio la kurupuka. Anaweza kua hata anakuhusisha kabisa kumchunguza mpenzi wake lakini hautakiwi kuwa mstari wa mbele kwenye jambo hilo.


Kama rafiki anamchunguza sana mpenzi wake kwa kuutafuta ubaya au uzuri wake, hata akikwambia “yule mpenzi wangu nipo nae tu ila simpendi”, jua ni anampenda. Ni ngumu kumchunguza mtu usiempenda hapa Duniani.

Rafiki akiwa anasema hampendi sana mpenzi wake alafu anataka kufuatilia mambo ya huyo mpenzi (kama vile, sms au michepuko alionayo) jua tu ni anampenda ila naficha maumivu.



Kuwa na tahadhari unapotaka kushirikiana nae au kueleza mambo mabaya kuhusu mwenza wa rafiki yako. Ukikulupuka unaweza kuzua chuki au mgogoro zaidi.

Mwisho, ni muhimu kujua kwamba kila mtu ana njia yake ya kutatua changamoto za kimapenzi. Kuomba au kutoa ushauri ni jambo zuri pia lakini kwenye baadhi ya mambo, ushauri unatakiwa kutolewa bila kukurupuka.

Kuchepuka Kuna faida ila hizi ni hasara zake BONYEZA HAPA>>>

Fahamu kuhusu vifurushi vya internet vya bei rahisi (SME)



Matumizi ya internet katika ulimwengu wa sasa yamekua ni makubwa sana. Hadi kufikia mwaka 2024 mwezi Julai, Asilimia 67.1 ya watu Duniani walikua wanatumia internet. Asilimia hiyo ya watumia internet ni sawa na kusema watu billioni 5.45 wanatumia internet hapa Duniani. Hii yote ni Sababu internet imekua ikirahisisha mambo mengi katika maisha ya binadamu na kuwa muhimu kwenye mambo mengine mengi anayofanya kwenye Duniani ya sasa.



Katika kutumia internet, watu wanao ongoza kutumia internet ni wamiliki wa simu za mkononi. Simu za mikononi zimekua ni kati ya vifaa ambavyo watu huvutumia zaidi katika matumizi ya internet kuzidi PC. Asilimia kuwa ya watu hawa hutumia internet kupata habari na kujiunga na ndugu au marafiki kupita mitandao ya kijamii.



Katika mitandao ya kijamii ukiwa sehemu yoyote, yawezekana ukawa kutana na watu wakiongelea vifurushi vya internet vya bei rahisi. Baadhi ya wanao zungumiza vifurushi, huongelea vifurushi vya SME. Hapa tunaenda kuvizungumzia vifurushi hivi ili kuwapa mwanga watu wasio vijua.

Vifurushi vya SME

Kabla ya kufahamu moja kwa moja vifurushi hivi, unapaswa kufahamu maana ya SME. SME ni kifupi cha maneno ya Lugha ya kiingereza ambayo ni “Small and Medium-sized Enterprises” yenye maana “Biashara Ndogo na za Kati”. Kwamaana hiyo, “Vifurushi vya SME” ni vifurushi kwaajili ya Biashara Ndogo na za Kati.

Faida ya vifurushi vya SME

Mitandao ya simu kama Vodacom, Tigo, Halotel na Airtel imekaua ikitoa vifurushi vya internet, dakika na SMS kwaajili ya Biashara Ndogo na za Kati(SME). Vifurushi hivyo hupatika kwa bei rahisi ukilinganisha na vifurushi vya kawaida.

Vifurushi hivi vimekua ni msaada mkubwa kwa wafanya bishara kwa kupunguza gharama wanazotakiwa kutumia kupata SMS, Dakika na internet katika shughuri zao za kibiashara.

Katika upande wa internet, vifurushi vya biashara vinaweza kumsaidia mtu kupata vifurushi vikubwa vya internet kwa bei ndogo. Hii ni moja ya sababu watu wengi huviongelea katika mitandao ya kijamii.

Upatikanaji

Ukihitaji kupata vifurushi vya biashara kwenye mtandao wa Simu unaoutumia (Vodacom, Airtel, Halotel au Tigo, unaweza anza kwa kuwasiliana na kampuni inayokupa huduma. Tuma maelezo kwenye kurasa zao za kijamii au wapigie na uwaulize kuhusu utaratibu wa kupata huduma ya vifurushi vya biashara.

Kama itawezekana, unaweza tembelea katika maduka yao maalumu ili kufuata utaratibu wa kupata vifurushi hivi.

Mara nyingi huwa wanahitaji uthibitisho wa taalifa zako na vitu kama TIN number. Uhitaji wa vitu hivyo, huwa unatofautiana kidogo.

Baadhi ya watu ambao hawana muda wa kufuatilia mpaka kuvipata vifurushi hivi, huwatumia watu wa mitandaoni ili kujiunga na huduma hii. Kutumia watu kupata vifurushi vya SME ni wazo zuri japo ni hatari sana kutokana na uwepo wa matapeli mtandaoni.

Ukihitaji mtu wa uhakika kukuunga katika Vifurushi vya SME ili kupata internet, dakika na SMS kwa bei rahisi, unaweza tumia ujumbe kwenye WhatsApp tukakusaidi kupata huduma hii kwenye baadhi ya mitandao.

KAMA WEWE (Simulizi ya Sauti)

Simulizi ya “KAMA WEWE” ya kiswahili ni simulizi inayopatikana katika The bestgalaxy na unaweza sikiliza Bure kabisa. Simulizi hii ni fupi sana lakini imebeba ujumbe mzuri kuhusu maisha na mafanikio katika hayo Maisha.

Simulizi ya Sauti ya kama wewe

Hii ni moja ya simulizi nzuri sana kuisikiliza kama Burudani huku ukijifunza. Sote tuna jua kuwa mtu unapojifunza kupitia hadithi za watu wengine, tunapata mwanga juu ya mbinu walizotumia kukabiliana na changamoto.

Mambo Wanawake hujutia kutoyajua Mapema

Katika maisha, kila mtu hupitia changamoto na maamuzi ambayo yanaweza kuleta furaha au kuleta majuto baadaye. Mwanamke, kama binadamu yeyote yule, anakutana na hali mbalimbali ambazo zinaweza kuathiri maisha yake kwa namna tofauti hapa Duniani. Kuna mambo mengi ambayo mwanamke anaweza kuyapitia lakini baadaye akaona kuwa yalikuwa na athari zisizo nzuri katika maisha yake.

The bestgalaxy hapa, tutajadili mambo machache ambayo wanawake wengi hupitia na kujutia kutoyajua baadae. Lengo si kumuhukumu mtu yeyote bali ni kutoa mwangaza na uelewa juu ya mambo ambayo yanaweza kuathiri maisha ya mwanamke. Mambo haya yanaweza kuwa yale ambayo yamepitia katika maisha yako, unayapitia au unayoiona kwa wengine .

Ukitambua mambo haya mapema, inaweza kusaidia mwanawake kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kufanya maamuzi bora na kuepuka majuto yanayoweza kuepukika. Tunatumaini kwamba, kupitia makala hii, utaweza kujifunza kitu.

Maneno Matamu kwa mpenzi wako wa kiume BONYEZA HAPA>>>

Mambo wanawake hujutia kutoyajua Mapema

Uzuri hauna mchango mkubwa sana kwenye ndoa

Mwanamke akiwa mzuri anaweza kuwa anajiamini sana na uzuri wake. Kuwa mzuri ni jambo zuri na hufanya wanaume wengi wazimike. Lakini katika ndoa, uzuri ni jambo lisilo na nguvu sana ikiwa mwanamke utashindwa kuwa na heshima pamoja na kutimiza wajibu wako.


Ndoa ni zaidi ya kuwa mzuri, ndoa ni maisha na haya maisha yana mambo mengi zaidi kuangaliana mwili. Kuna muda itakubidi utumie akili, kuna muda utatakiwa kuwa mjinga mwenye heshima pamoja na uzuri ulionao.

Upendo wa kweli sio pesa

Wakati baadhi ya wanawake wanaamini mwanaume anaewapa pesa sana ndie anae wapenda kwa dhati, Kuna wanaume wanaweza toa pesa sana kwa wanawake wasio wapenda. Baadhi ya wanaume hawa humwaga pesa kwa mwanamke kama malipo ya kumpeteza muda tu japo hawasemi kwa uwazi.
Kukimbiza pesa kwenye mapenzi hufanya wanawake kuingia kwenye majuto. Kuna watu hupata magonjwa na hata kuingia kwenye mahusiano yasio faa kisa pesa lakini hujutia mwishoni.

Kuwa katika familia ni Bora kuliko katikati ya marafiki

Mwanamke kuwa na marafiki ni jambo zuri lakini kila jambo huwa na wakati wake. Mwanamke akifikia wakati ambao maisha yake yanamvuta kujenga familia, ni vema akakubari kujiondoa katikati ya marafiki.


Mwanamke anaweza kuwa ameolewa(kapata mume), amepata mtoto na muda mwingi anahitajika kuwa katika familia sio kuzungukwa na marafiki. Kuacha kutumia muda mwingi mukifurahi na marafiki sehemu mbalimbali ni jambo gumu lakini sio muhimu kuliko kuijali ndoa, watoto au familia kiujumla.
Hii haimaanishi usiwe na marafiki, unaweza kuwa nao ila itakua vizuri kama utakua na wale wanao heshimu hali yako ya ndoa au familia. Yani wale wanoweza kukupa ushauri chanya kuhusu mtoto, ndoa na hata kuwa upande wako pale unapopitia magumu.

Mambo mengi ya mitandao si mazuri katika uhalisia

Utakutana video nyingi sana kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mahusiano au maisha. Lakini tambua asilimia kubwa ya mambo yaliyo kwenye hizo video, yanaweza kuwa hatari kuyafuata kwenye maisha au mahusiano ya uhalisia. Ni vema ukiwa kama Mwanamke wa kipindi hiki ukawa na uwezo wa kufikilia na kuchuja kila unachokiona kwenye mitandao hatakama kimetoka kwa watu maalufu.

Kutumia na akili yako na mafuzo uliyoyachukua kwa wazazi wako ni muhimu zaidi kuliko kupelekwa na upepo wa mitandao maana kwa asilimia kubwa upepo huo huwa ni Burudani tu. Ukifuata upepo wa mitandao unaweza kukuweka kwenye mtindo wa Maisha na mitazamo mibaya utakayoijutia baadae.

Ni hayo tu katika The bestgalaxy na itakua vizuri kama utatufuta katika mitandao ya kijamii ili kuwa mwana familia.

Jinsi ya kudownload nyimbo Mpya kwenye simu (Audio na Video)

Muziki ni sehemu muhimu ya maisha yetu ya kila siku kwa sasa. Unatupa faraja, unatuburudisha na hata kutusaidia kuunganisha hisia zetu kwa undani zaidi. Watu wengi wanapenda kusikiliza nyimbo wakati wa safari, wakiwa nyumbani, au hata wakati wanapofanya kazi, kwa sababu muziki unaweza kukufanya ujisikie vizuri.


Unajua kuwa sasa ni rahisi sana kupata nyimbo mpya kuliko zamani? Kutokana na maendeleo ya teknolojia, simu zetu za mkononi zimekuwa kama vituo vya burudani. Ukiwa na simu ya intaneti, unaweza kupata nyimbo na video za wasanii unaowapenda kwa urahisi na kuzisikiliza muda mchache tu baada ya kutoka. Zamani jambo hili lilikua ni gumu sana. Watu walikua wanapata ugumu kwenye kupata nyimbo za wasani wanaowapenda.


Hapa The bestgalaxy, inakupa maelezo ya Jinsi mtu unaweza pata au kudownload nyimbo Mpya kwenye simu. Hili ni jambo rahisi sana kwa watu wengine lakini baadhi ya watu hawalielewi. Kama utakua ni mmoja wao, fahamu njia rahisi za kufanya jambo hili vizuri hapa chini.

Njia za kudownload nyimbo Mpya kwenye simu

Kupakua nyimbo katika Audiomack app

Audiomack ni moja ya Platform za music ambazo ni maarufu sana katika ulimwengu wa music. Platform hii inawezesha watumia simu za mkononi kusikiliza na hata kudownload nyimbo Mpya kutoka kwa wasanii. Wasanii wengi wa Afrika mashariki kwa sasa huweka nyimbo zao mpya katika Audiomack na hii inafanya Audiomack kuwa moja ya sehemu nzuri ya kupata nyimbo mpya. Katika ya nchi ambazo hushika nafasi ya juu katika kutumia Audiomack ni Nigeria, Ghana na United States.
Uzuri wa Audiomack ni kwamba nyimbo nyingi unaweza sikiliza na kudownload bure. Utakachohitaji kuwa nacho ni App ya Audiomack kwenye simu yako tu kufurahia.

Kudownload nyimbo katika Boomplay app

Boomplay ni platform ya music iliotengenezwa na Transsnet Music Limited. Huduma ya Boomplay ililetwa kwa mara ya kwanza na TECNO Mobile katika nchi ya Nigeria na imekua na mpaka sasa imepata mafanikio ya kuwa kwenye nchi nyingine nyingi mbali Nigeria.
Katika Boomplay, mtumiaji unaweza kupata nyimbo nyingi mpya kwa wakati maana kunawasanii wengi hupandisha nyimbo zao kwa wakati katika Boomplay. Unaweza kusikiliza na kudownload nyimbo nyingi za Afrika mashariki bure. Kufurahia hayo, utahitajika kuwa na apo ya Boomplay kwenye simu.

Kupata nyimbo Kupitia BekaBoy

Hii ni moja ya website/tuvuti maalufu sana katika ulimwengu wa music upande wa Afrika mashariki. Katika tuvuti hii ya BekaBoy, unaweza pata nyimbo Mpya kutoka kwa wasanii mbalimbali na unadownlod Bure(Audio na video). Ni sehemu nzuri sana ya kupata au kudownload nyimbo za zamani pia maana imekua ikisukuma music wa Afrika mashariki kwa muda mrefu. Kiufupi BekaBoy ni website yenye mchango mkubwa sana katika muziki wa Afrika mashariki.


Unaweza Pata huduma ya BekaBoy kwenye tuvuti ya BekaBoy moja kwa moja na hata kupitia app pia (kama utahitaji). Kutumia app ya BekaBoy ni jambo zuri lakini unaweza usipate nyimbo za zamani kirahisi. Kama unataka nyimbo za zamani itakuhitaji utumie website.

Kuchukua nyimbo katika DJmwanga

Hii pia ni website ambayo inafahamika sana katika ulimwengu wa music upande wa Afrika mashariki. Katika tuvuti ya DJmwanga unaweza pata nyimbo Mpya na ukazipakua bila matatizo(Audio na video). Nyimbo nyingi za zamani zipo pia kwakua ni tuvuti kubwa inayosukuma mziki kwa muda mrefu. Kama unatumia simu, unaweza pakua app ya DJmwanga kwenye simu ili kupata nyimbo mpya kwa wakati lakini hautafanikiwa kupata za zamani kama ilivyo app ya BekaBoy.

Mbali na njia hizo juu, kuna namna nyingi sana unaweza kudownload nyimbo Mpya kwenye simu. Kuna watu wengine hutumia Spotify, YouTube music, Vidmate na platform nyingine nyingi zinazojihusisha na Muziki kwa sasa ambazo unaweza zitumia pia.