Category Archives: Teknolojia

TikTok na Instagram zinakusaidia vipi kutafuta Ajira unayoitaka?

Katika dunia ya sasa, teknolojia imeleta mabadiliko makubwa katika njia tunazotumia kutafuta ajira. Mitandao ya kijamii imebadilika kutoka kuwa sehemu ya burudani tu hadi kuwa nyenzo muhimu kwa watu wanaotafuta kazi.

Watu wengi bado hawatambui kuwa nafasi za ajira hazipatikani tu kupitia barua pepe au matangazo ya kampuni. Kwa kutumia mitandao ya kijamii vizuri, unaweza pata nafasi ya kazi unayotafuta. Kinachohitajika ni kuelewa tu mbinu sahihi za kuitumia kwa faida yako.

Kabla hujaanza kutuma maombi ya kazi kila mahali bila mafanikio, ni vema kujua kuwa TikTok na Instagram imekupa nafasi za kurahisisha michakato ya kutafuta ajira. Na kama unataka kujua ni kwa namna gani, soma yafuatayo.

TikTok na Instagram zimekupa nafasi hizi katika kutafuta ajira

1. Kukutana na mamilioni ya waaajiri

TikTok na Instagram ni sehemu ambayo mtu anaetafuta ajira anaweza itumia kukutana na waajiri wengi sana. Hii ni mitandao ya kijamii ilio wakusanya watu na kampuni mbalimbali ambazo zinaweza kumuajiri mtu. Yani kwenye TikTok au Instagram, unaweza kutana kurasa za maduka makubwa ya nguo, makampuni ya simu na hata usafirishaji. Na unaweza tuma ujumbe au kuuliza mambo mbalimbali kirahisi kabisa.

Kwaiyo kama unatafuta ajira, fahamu kuwa mitandao hii (TikTok na Instagram) tayari imekuwekea karibu sehemu nyingi unazoweza kuomba ajira. Tena bila mipaka maana unaweza kuwa nje ya Dar lakini ukawa karibu na maduka au kampuni zilizo Dar.

2. Kuonesha ujuzi au uzoefu wako ili kuvutia waajiri

Nafasi ya pili unayopewa na TikTok na Instagram katika kutafuta ajira ni uwezo wa kuonesha ujuzi au uzoefu wako kwa waajiri wako. Hii ni nafasi nzuri sana unayoweza itumia na ukapata ajira.

Wote tunafahamu kuwa ajira zimekua ni chache kuliko wahitaji. Na ajira nyingi zinazo jitokeza katika kipindi hiki, muajiri huitaji mtu Bora, mwenye ujuzi wa hali ya juu au mzoefu kabisa.


Sasa ukiwa kama mtu unatafuta ajira, unaweza kuonesha ujuzi wako au uzoefu kwako kupitia video za TikTok au Instagram. Wengine hutumia video kuchekesha wengine, au kujipost wakicheza. Hili sio jambo baya lakini ni muhimu kufahamu kuwa video zinaweza kutumika kuonesha ujuzi flani pia. Video zako za ujuzi zinaweza kuangaliwa na mamilioni ya watu. Kati ya mamilioni ya watu huo, Kuna watu wengi wanaoweza kukuajiri.


Kwaiyo hii ni nafasi nzuri ya kuonesha ulichonacho kwa watu watakao kuajiri. Lakini katika kutengeneza video, unatakiwa kuwa mbunifu sana.

3. kujiajiri wakati ukiendelea kutafuta ajira

Nafasi ya tatu ambayo TikTok na Instagram imekupa mtu unaetaka ajira ni kujiajiri huku ukitafuta ajira unayoihitaji. Unaweza kujiajiri na ukawa unaingiza pesa kwa kutumia mitandao hii.

Sio lazima ikulipe moja kwa moja kwenye akaunti yako ya Bank, unaweza itumia kutangaza huduma yako inayokuingizia kipato kwa kipindi ambacho unasubiri ajira.

Jinsi ya kupata movie za kutafsiriwa kiswahili mtandaoni (2025)

Kuna watu wengi hupenda kutazama filamu  online. Filamu hizi za online hutoa burudani kwa watazamaji wa rika zote lakini nyingi ni lugha mbali na kiswahili. Si kila mtu anayeweza kuelewa lugha ya filamu hizo, hasa kama ni za Kiingereza, Kihindi au Kichina na ndiyo maana kutafsiri kwa Kiswahili imekuwa msaada mkubwa kwa watazamaji wengi wa Afrika Mashariki.

Kutokana na hitaji hilo kubwa, kumekuwa na sehemu za mtandaoni zinazotoa huduma ya kutafsiri filamu kwa Kiswahili. Sehemu hizi husaidia watu kufurahia movie kwa urahisi huku wakielewa kinachoendelea. Yani kutafsiri movie ni njia nzuri ya kuleta burudani inayowafikia watu wengi zaidi, bila vikwazo vya lugha.

Katika makala hii, tutakuletea orodha ya sehemu mbalimbali za kupata movie ambazo zimetafsiriwa kwa Kiswahili mtandaoni. Iwe unapenda movie za mapenzi, za vita, vichekesho au za kichawi, utajua wapi pa kutembelea ili upate burudani kwa Kiswahili ukiwa na ma DJ unaowapenda.

Sehemu za kupata movie za kutafsiriwa kiswahili mtandaoni

1. Katika YouTube



YouTube ni platform ya video ambayo pia ni sehemu nzuri kwa wapenzi wa filamu kuangalia movie. Katika YouTube unaweza kutana na movie nyingi za Kiingereza lakini baadhi ya movie zilizotafsiriwa kiswahili zipo pia.

Kuna baadhi ya movie nzuri sana unaweza zikuta YouTube zikiwa zimetafsiriwa kiswahili. Movie hizi nyingi huwa ni za zamani maana ndio YouTube wanaweza ziruhusu kidogo. Nyinge huwa na mpya kidogo ila zipo YouTube kutokana na kuchukuliwa kama Creative Commons Licensed movies.


Njia rahisi ya kupata movie hizi ni kuandika neno “Movie za kutafsiriwa kiswahili” katika sehemu ya kutafuta ya YouTube.

2. Group za WhatsApp na Telegram



Njia nyingine ya kupata movie za kutafsiriwa kiswahili mtandaoni ni kuingia katika Group za WhatsApp na Telegram zinazojihusisha na movie za kutafsiriwa. Kuna group hutangazwa na ma “DJ” au watafsiri wa movie kwenye movie zao au kwenye clip zao. Na wakitangaza huwa wanaweka wazi utaratibu wa kujiunga nao. Sasa ikiwa utahitaji movie, unatakiwa kufuata utaratibu wao na kujiunga kwenye hizo group.


Hakikisha unakua makini sana na huyo DJ anae toa namba maana kuna kutapeliwa pia. Ni vema ukaangalia kwanza kama DJ unaemsikiliza anajulikana na kuaminika. Kujilidhisha, fuata utaritibu alikupata huduma yake. Na hii Naweza kusema ni njia nzuri sana kuitumia katika mwaka 2025

3. App za movie za kutafsiriwa



Katika njia ambazo watu wengi walikua wanaotumia kupata movie za kutafsiriwa ni hii. Lakini kwasasa ni njia yenye changamoto sana kutokana na sawa la Copyright.

Ukihitaji app za movie za kutafsiriwa kwasasa unaweza ukapata lakini nyingi hukupa movie chache za zamani na nyingine huwa hazifanyi kazi kabisa. App nyingi za movie zinakufa kwa kutofuata utaratibu wa Copyright wa huku mtandaoni.


Kwakua ni moja ya njia ambayo inatumika, acha tuiweke hapa kama sehemu ya tatu ya kupata movie za kutafsiriwa kiswahili.

ZINGATIA: Makala hii imetolewa kwa lengo la kuelimisha (For education purpose).

App ya Gamehub imerahisisha kucheza game za Xbox katika simu

Wachezaji wa games kwenye simu wanazidi kupewa njia rahisi na za kisasa za kufurahia games wanazozipenda kwenye simu. App ya Gamehub ni moja ya suluhisho jipya ambalo limeleta mabadiliko makubwa kwa wapenzi wa games. Kupitia app hii, sasa inawezekana kucheza game za Xbox moja kwa moja kwenye simu yako ya mkononi bila haja ya kuwa na console ya Xbox.

Kama bado haujajua ni kwamba unaweza cheza game za Xbox kwenye simu  lakini hii itakuhitaji utumie huduma ya xcloud. Xcloud ni huduma inayokuwezesha mtu kucheza game za Xbox na nyingine nyingi katika mtandao (Online). Kupitia huduma hii, unaweza cheza game nyingi kubwa kwenye simu yako bila kuwa na simu yenye uwezo sana maana. Kikubwa utakachotakiwa kuwa nacho ni internet yenye kasi tu na tulisha zungumzia juaa ya hilo kwenye makala nyingine hivyo hatauta zungumzia sana hapa.

Game la Fortnite katika Xcloud

Hapa tunakujuza tu kuwa kuna app inaitwa Gamehub imerahisisha zaidi mchakato wa kucheza game za Xbox kupitia hiyo hiyo xcloud.

Kitu kizuri ilicho rahisisha ni kuondoa uhitaji kwa kutumia VPN ikiwa upo nje ya nchi zenye huduma (kama vile US). Yani kupitia app ya Gamehub utaweza kucheza game za Xbox kupitia xcloud popote bila kutumia VPN. Utafanikisha jambo kilo kupitia kipengele cha kuchagua unataka kucheza kama upo sehemu (location). Unaweza fanya yafuatayo kujaribu hiya.

Jinsi ya kucheza game za Xbox kwenye simu kwa app ya Gamehub

Unachohitaji ni kuwa na akaunti ya Xbox, simu yenye uwezo wa kuunganisha intaneti, na app ya Gamehub yenyewe.

  • Fungua app na ujisajiri
  • Baada ya kujisajili, nenda kwenye upande Xbox kwa kubonyeza alama ya Xbox
  • Ukiwa hapo, palasa sehemu ya pembeni katika upande wa kulia, kwenda kushoto kuelekea kulia.
  • Ukifanya hivyo utaletewa sehemu ambayo utachagua location (mahali). Wewe unaweza chagua USA au UK.
  • Baada ya hayo, Chagua game unalotaka kucheza alafu ujisajiri kwa akaunti yako ya Microsoft kama kawaida kwaajili ya kuanza kucheza.

Nakukumbusha tu kuwa kama haujalipia Xbox game pass ultimate, hautaweza kucheza game zaidi ya Fortnite.

Hii ni habari njema kwa watu ambao hawana nafasi au uwezo wa kununua vifaa vya Xbox lakini bado wanatamani kufurahia michezo hiyo.

The Bestgalaxy Yabadilisha Domain Yake

Katika juhudi za kuboresha huduma na kuhakikisha upatikanaji rahisi wa maudhui bora kwa wasomaji wake, The Bestgalaxy imefanya mabadiliko muhimu kwa kubadilisha domain yake. Kuanzia sasa, tovuti hii maarufu inaweza kupatikana kupitia http://www.thebestgalaxy.com.

Kwa Nini Mabadiliko Haya ni Muhimu?

Mabadiliko haya yanaleta faida kadhaa kwa wasomaji na watumiaji wa The Bestgalaxy:

  • Upatikanaji Rahisi: Domain mpya ni fupi, rahisi kukumbuka, na inaendana na utambulisho The Bestgalaxy.
  • Uboreshaji wa Uaminifu: Kutumia domain ya kiwango cha juu (.com) huongeza hadhi na uaminifu wa tovuti kwenye mtandao.
  • Uboreshaji wa Huduma: Maboresho haya yanahakikisha uzoefu mzuri wa watumiaji, ikiwa ni pamoja na kasi ya ufunguaji wa kurasa.

Jinsi ya Kupata Maudhui Yetu

Wasomaji wanaweza kuendelea kupata makala za kipekee, miongozo ya teknolojia, mbinu za kidigitali, na mengine mengi kwa kutembelea http://www.thebestgalaxy.com. Hakikisha umehifadhi domain hii mpya ili usikose maudhui bora tunayokuletea kila siku.

The Bestgalaxy

“The Bestgalaxy” ni sehemu unayoweza jifunza na kufurahia maswala mbali mbali kuhusu maujanja ya Teknolojia, Games, Mahusiano na Mengineyo!

Tunashukuru kwa sapoti yako na tunatarajia kukuona ukiendelea kufurahia maudhui yetu kwenye tovuti yetu mpya!

Karibu The Bestgalaxy – Sasa kwenye http://www.thebestgalaxy.com!

Una download vipi video za Facebook kwenye simu yako?

Facebook ni moja ya mitandao maarufu sana kwa kutazama na kushare video mbalimbali. Mara nyingi, unaweza kuona video nzuri unayotaka kuihifadhi kwenye simu yako ili uitazame baadaye bila intaneti. Lakini tatizo ni kwamba Facebook haina chaguo la moja kwa moja la kudownload video hizo ziingie kwenye kifaa chako. Kwa bahati nzuri, kuna njia rahisi unazoweza kutumia kupakua video kutoka Facebook bila shida.

Katika ukurasa huu, tutakuelekeza hatua kwa hatua jinsi ya kudownload video za Facebook moja kwa moja kwenye simu yako. Haijalishi unatumia simu ya Android au iPhone, kuna mbinu rahisi ambazo zinafanya kazi kwa wote. Utajifunza jinsi ya kutumia website/tovuti maalum au programu zinazoweza kukusaidia kupakua video hizo kwa urahisi.

Ikiwa umewahi kuona video inayokuvutia kwenye Facebook na ukashindwa kuipakua, basi makala hii ni kwa ajili yako. Fuata mwongozo huu kwa makini ili uweze kuhifadhi video zako unazopenda na kuzitazama wakati wowote bila kuwa na wasiwasi wa data au intaneti.

Jinsi ya kudownload video za Facebook katika simu yako

Kiufupi njia rahisi ya kudownload video za Facebook ni kutumia App au tuvuti maalum kwaajili ya kudownload video hizo. Kuna app na tuvuti nyingi hukuwezesha mtu kupakua video za Facebook. Huwa zanahitaji uzipatie link ya video ambayo unataka alafu baada ya hapo, zinakuwezesha kuchukua video na kuiweka kwenye simu yako.

Mfano wa app za mitindo hii ni app iitwayo Video downloader iliotolewa na Inshot inc. Na kama utahitaji website unaweza tumia tuvuti Fdown.net ikakuwezesha bila tatizo.

Hatua za kudownload ya Facebook kwenye simu

  • Copy link ya video ulioiona katika Facebook
  • Paste link ya video katika tuvuti au app  maalum (katika app ya Video downloader au tuvuti ya Fdown.net)
  • Iruhusu app au tufuti kufanya mchakato wake kisha bonyeza kitufe cha kudownload video kitakacho letwa baada ya mchakato.

Kwa kufanya hayo utakua umefanikiwa kupakua video ya Facebook kwenye simu yako. Ila kabla ya kuondoka katika ukurasa huu ni vema kufahamu kuwa upakuaji wa video za watu bira ruhusa ya wamiliki ni kosa ingawa unaweza kufanya ikiwa video ipo katika kundi la video zisizo na madhara.

Jinsi ya kutumia kipengele cha “WhatsApp screen share”


WhatsApp ni mtandao unaoleta pamoja watu kupitia groups, channels na kurahisisha sana mawasiliano. Ni moja ya mitandao mkubwa ulimwenguni milikiwa na Meta. Unatumiwa na watu kuwasiliana na watu wengine walio ndani na nje ya nchi.

Kwenye mtandao wa WhatsApp Kuna vipengele vingi sana mtu unaweza tumia katika kuungana au kuwasiliana na watu wengine. Katika vipengele hivyo, Kuna kipengele kinaitwa “WhatsApp screen share”.

WhatsApp screen share ni kipengele cha WhatsApp kinachowawezesha watumiaji wa WhatsApp kuoneshana Screen za simu zao. Kupitia kipengele cha hiki cha WhatsApp, unaweza kumuonesha mambo yalio katika kioo cha simu yako mtumiaji mwingine wa WhatsApp. Lakini hii inafanyika pindi mnapopigiana video call.

WhatsApp ilikuja na kipengele hiki cha WhatsApp screen share rasimi mwaka 2023 lakini huduma kama Google meet na Zoom zina uwezo kama huu pia. Katika makala hii, tutajikita katika huduma  ambayo inapatikana kwenye mtandao wa WhatsApp.

Jinsi ya kutumia kipengele cha “WhatsApp screen share”



Ukiwa unataka kumuonesha mambo yalio kwenye screen ya simu yako mtu mwingine kwa kutumia WhatsApp Screen share, fuata hatuna zifuatazo;

  • Mpigie au akupigie Video call
  • Mukianza video call, bonyeza Vidoti vitatu
  • Changua “Share screen” kwenye chaguzi zitakazotokea.
  • Baada ya hapo, utatakiwa kukubali kuwa Kila kinachofanyika kwenye screen ya simu yako, kionekane kwa yule mtu ulienae kwenye video call.
  • Ukikubari tu, WhatsApp wataanza kuionesha screen yako kwa yule mtu ulienae kwenye video call.

Kupitia kipengele hiki, unaweza kumuonesha mtu movie/video zililopo kwenye simu yako, kumfundisha Baadhi ya vitu kupitia simu yako na hata rekebisha matatizo kwa kufuata muongozo wake.

Jinsi ya kuona sms za WhatsApp kwenye simu nyingine BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kutengeneza pesa na Facebook Content Monetization Program


Facebook ni mtandao mkubwa wa kijamii unaomilikiwa na kampuni ya Meta na unaunganisha watu wengi Duniani. Watumiaji wa mtandao wa Facebook wanaweza furahia kuwasiliana na wepandwa wao, kuangalia picha, video na kusoma mambo mbalimbali.


Katika kufurahia mambo hayo, Facebook nimekua ni moja ya mitandao muhimu kwa watu wanaojiajiri. Ina vipengele vingi sana vinavyoweza msaidia mtu aliejiajiri, kukuza hudama yake. Mfano mzuri ni kile kipangele kutangaza biashara; mtu anaweza kutumia upande huo kutangaza biashara au huduma yake.


Mbali na upande huo, Facebook wana program iitwayo “Facebook Content monetization” ambayo inawawezesha watu kutengeneza pesa kwa content zao. Yani hapa unaweza lipwa kwa vitu unavyoandika na kupost, video na picha unazopost. Na unaweza fanya hivyo kupitia akaunti unayoitumia kila siku au Facebook page kama unayo. Ila kama unatumia akaunti ya kawaida utatakiwa kuweka kwenye “Professional mode” kwanza.

Jinsi ya kutengeneza video za katuni kwa simu ili kutengeneza pesa BONYEZA HAPA>>>

kuanza kulipwa katika Facebook Content monetization



Ili uanze kulipwa katika Facebook utatakiwa kuanza kujiunga na hiyo Facebook monetization. Na kabla haujajiunga, utatakiwa kutimiza vigezo vyao lakini vigezo vyao huwa vimetofautiana na hubadilika kutokana na kwamba mfumo wao kwa sasa upo kwenye maboresho.


Ukihitaji kuwavutia kwa kipindi hiki ili uingizwe kwenye program yao, ni vema ukawa na kuanzia followers 5000 na video zilizoangaliwa zikawa na jumla ya dakika 60000.

Pia ni vema ukatengeza video zako mwenyewe maana kuchukua video za watu bila maboresho yoyote ni kosa litakalokupunguzia nafasi ya kutengeneza Pesa.

Mambo ya kuepuka ili kutengeneza Pesa katika Facebook BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya Kuangalia kama upo tayari kulipwa na Facebook

Ukitaka kuangalia kama tayari umekidhi vigezo vya kuingia kwenye Facebook Monetization program, nenda kwenye Dashboard ya akaunti yako alafu ingia kwenye kipengele cha “Monetization”. Ikiwa utakutana na neno “eligible” au kipengele cha “Content monetization ” kimefunguka, basi fahamu kuwa akaunti yako inaweza ingizwa kwenye Facebook monetization program.


Baada ya kuwa vizuri sehemu hiyo, unaweza pokea ujumbe kwenye email yako kuwa wamekuarika kwenye program ya Content monetization program bila hata kufanya Chochote au ukakuta to vipengele vya kutengeneza pesa vimejifungua kwenye Dashboard. Unaweza pata hata notification kwenye Facebook ikikwambia umekua “eligible” hivyo set taalifa muhimu ili ulipewe.



Zingatia: kwasasa Facebook content monetization program ipo kwenye marekebisho hivyo kuna namna utaratibu wake haupo sawa. Hasa kwa nchi za huku Afrika mashiriki. Unaweza kuchati na sisi kwa kugusa HAPA.

Jinsi ya kutengeneza Pesa katika channel za WhatsApp BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kutengeneza App ya simu

Kikawaida, kutengeneza app ni mchakato unaohusisha kuandika “Code” ambazo ni maelezo katika lugha ya computer. Hivyo ukitaka kutengeneza app kwa utaalam zaidi, unapaswa kujua namna ya kuandika Code katika lugha mbalimbali za computer.

Kwa mtu unaetaka kuwa mtaalam wa kutengeneza app za simu, unaweza jifunza lugha za computer kama vile JavaScript, Kotlin, Java, Python, Java na nyinginezo. Ukiwa mtaalam wa lugha za computer na ukawa na uwezo wa kutengeneza app, alafu utaitwa “App developer”.


App developer anaweza kuingiza pesa kwa kuajiliwa sehemu mbalimbali anazoweza kufanya kazi kama “Developer”. Mfano; Kampuni ya Meta ambayo inaumiliki Instagram, Facebook na WhatsApp, huwa zina watu ambao hufaamika kama “Developer” ambao huusika na maboresho ya app hizo. Ni wachache Duniani ila huingiza pesa nyingi sana.

Mbali na kuajiliwa, App developer anaweza ingiza pesa kwa project zake mwenyewe. Yani anaweza pambana kutengeneza kitu anachokiwaza alafu kikamuingizia pesa kwa kukiuza au kukiingiza katika mifumo itakayomuingizia pesa. Mfano mzuri ni Kutengeneza game linalo muingizia pesa au kuwatengenezea watu app za kurahisisha mambo yao ya kibiashara.

Jinsi ya kutengeneza Pesa kwa kucheza games mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kutengeneza app za simu kwenye simu za bila  kujua Code

Pamoja na hayo yote, sio lazima mtu uwe mtaalam ndio utengeneze app za simu. Mtandaoni kuna tuvuti/website nyingi ambazo zimerahisisha mchakato wa kutengeneza app za simu.

Website nyingine zinarahisisha mchakato wa kutengeneza app kiasi ambacho mtu yoyote anaweza kutulia na zitumia kutengeneza app za Simu. Unaweza usijue kabisa maswala ya lugha za computer lakini ukafanikisha kutengeneza app kupitia website hizo.

Ukizitafuta website za mtindo huu katika mtandao, utazikuta nyingi sana lakini asilimia kubwa zinahitaji ulipie pesa. Mfano mzuri ni tuvunti ya Andromo, AppMySite na Appypie. Ni kati ya website rahisi kuzitumia katika kutengeneza app za simu (Android na iOS)lakini ili kupata uhuru kwenye app yako, utatakiwa kulipia.

kutengeneza app za simu kwenye simu BURE


Lakini swala la kulipia, lisikukwamishe maana Kuna tuvuti nyingine zinakupa uhuru mkubwa kabisa bure. Mfano wa tuvuti hizo ni hii hiitwayo “Appcreator24” au tuvuti iitwayo “Appsgeyser“. Website hizi unaweza kuzitumia kutengeneza app za simu kwa urahisi sana na bila kulipia.

Hapa the bestgalaxy tunakupa mwanga wa jinsi ya kutengeneza app ya simu kupitia tuvuti ya Appcreator24. Hapa chini tumekupa hatua muhimu zakuchukua ili kutengeneza app kwenye tuvuti hiyo ila utatakiwa kuwekeza muda wako kujifunza kiundani.

  1. Ingia kwenye website ya Appcreator24 ujisajili
  2. Bonyeza “Create app” kuanza kutengeneza app
  3. Jaza taalifa za app unayotaka na uchague mtindo wake
  4. Maliza kwa Download app yako ikiwa kama Apk au AAB file

Baada ya hapo utachangua wewe kwa kuipeleka. Unaweza kuiweka kwenye simu yako au kuipeleka sehemu kama Playstore ili watu waipakue kisha upate pesa kwa kuonesha matangazo. Na kama unataka kuiboresha au kuiweka vizuri, basi utaingia kwenye hiyo website ya Appcreator24 ili kurekebisha.

Pamoja na yote hayo, fahamu kuwa website nyingi za kulipia ndio hutumia kutengeneza app nzuri zaidi. Na pia, kujua code kunaweza kufanya uwe bora zaidi katika kuzitumia tuvuti zote za kuunda app. Watu engine hutumia AI kuandika Code katika kuunda app na hufanikiwa kutengeneza app nzuri sana. Lakini sio lazima kufanya hivyo, unaweza tengeneza app bila kujihusisha na code!

Jinsi ya kutafuta Jina la movie kupitia kipande cha video

Kwasasa ukizunguka katika mitandao ya kijamii, unaweza pata video fupi ambazo ni vipande vya movie. Video hizi fupi zinaweza kuonesha sehemu nzuri ya movie flani lakini kupata jina la movie hiyo inaweza kuwa changamoto. Mfano; Kuna siku nimewahi kutana na video katika Mtandao Facebook. Hiyo video ilikua inaonesha sehemu ya kusisimua ya movie. Sehemu hiyo ya movie ilinifanya nitamani kutafuta na kuangalia movie hiyo mwanzo mpaka mwisho. Lakini nilishindwa kufanya hivyo kutokana na kutojua jina la movie yenye kipande hicho.
Sawa hili huwa linapitiwa na watu wengi sana katika kipindi hiki. Watu huona vipande vya movie kwenye TikTok, Facebook na WhatsApp lakini wanashindwa kujua majina ya movie zenye vipande hivyo. Baadhi ya watu huwa wanabahatika kupata Jina la movie kwenye sehemu ya maoni (Comment) japo sio mara zote utapata watu waliotaja jina kwenye sehemu hiyo. Lakini hayo yasikutie shaka maana kuna njia Bora ya kutafuta Jina la movie kupitia kipande kifupi cha video ulichokiona sehemu yoyote. Ukihitaji kujua juu ya hili? soma yafuatayo hapoa chini.

Jinsi ya kutafuta Jina la Movie kwa kipande cha kifupi cha Video

  1. Piga Screenshot sehemu nzuri ya video.

Kitu Cha kwanza unatakiwa kufanya ni kuplay kipande cha video fupi ulionayo alafu upige screenshot sehemu nzuri. Ninapozungumzia sehemu nzuri, ninamaana sehemu ambayo inawaonesha waingizaji na mazingira yao vizuri.
Unaweza piga Screenshot mbili au zaidi ili upate screenshot moja itakayokua vizuri kuliko zote.

  1. Ingiza Screenshot katika Google Lens.

Baada ya kupata screenshot moja nzuri sana, utatakiwa uiingiza Katika Google Lens. Hii Google Lens inakuwezesha kutafuta taalifa za vitu kupitia picha. Mfano; ukiipatia Google Lens Screenshot (picha), itakupa taalifa mbalimbali kuhusu hiyo screenshot. Na kama utaipatia Screenshot ulioipiga katika kipande cha movie, unapata taalifa zinazojumuisha Jina la movie.

App ya Google Lens inapatikana Playstore kwa watu wanaotumia simu za Android(Ina alama ya kamera. Lakini kwa iPhone unaweza tumia Google chrome. Inapatikana kama kipengele kidogo katika Google. Kama unatumia Google kupitia Chrome, utakiona kipengele cha Google Lens kikiwakilishwa na alama ya kamera.
Kutumia Google Lens ni rahisi tu; unaifungua, unachagua picha au screenshot iliopo kwenye simu yako alafu unaiacha ikupe taalifa Toka Google kuhusu hiyo screenshot.

  1. Kupata jina, angalia kwa umakini matokeo ya Google.

Google itakupa matokeo mengi kuhusu hiyo screenshot lakini kwakua unataka jina la movie, utatakiwa kuwa makini kuchambua. Umakini unahitajika maana kama screenshot yako haikua vizuri, unaweza pata taalifa tofauti na unazotafuta.
Lakini kama utajiridhisha kuwa majibu ni sahihi, utakua umefanikiwa kupata jina la movie kama ulivyohitaji.

Jinsi ya Kuangalia movie Bure mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Mambo mazuri unayoweza kufanya kwa App ya Mtandao wako wa Mawasiliano



Kutokana na ukuaji wa Teknolojia, mitandao ya mawasiliano imekua na app za pesa ambazo tunazitumia kwenye simu za smartphone. App ninazozingumia hapa ni app ya Mpesa, My Halo, Mixx by yas, My Airtel na nyingine kama hizo.
Watu wengi wenye smartphone hutumia app hizi na zimekua zikirahisisha sana mchakato wa kutuma pesa kwa ndugu na marafiki zao. Uzuri wa app hizi katika kutuma pesa ni huwa zinarahisisha mchakato mzima wa kutuma pesa. Zinapunguza na changamoto ambazo hujitokeza mara nyingi mtu anapotuma pesa.


Mfano wa changamoto hizo ni kukosea na namba ya mtumiajia na kupata lile tatizo la “Invalid MMI code.” Unapochelewa kufanya uchaguzi katika Menu za kawaida.

Ukiwa unatumia app, kunakuwa na uwezekano mdogo wa kukosea namba ya mtu maana unaweza ichukua moja kwa moja kwenye majina uliotunza.



Sasa mbali na mambo ya kutuma pesa kwa ndugu na marafiki, app hizi Kuna mambo zimeyarahisisha sana. Kama unatumia moja ya app hizi, basi angalia orodha ya mambo mazuri unayoweza fanya kwa urahisi kupitia app hizi za pesa.

Jinsi ya kutafuta simu iliopotea au kuibiwa BONYEZA HAPA>>>

Mambo mazuri unayoweza fanya kwa app ya mtandao wako wa Mawasiliano

Kutafuta wakala waliokaribu na wewe


Kama unatumia app za pesa za Makampuni ya mawasiliano, kwasasa unaweza tafuta Mawaka waliokaribu na wewe kwenye eneo ulilopo. Yani hatakama umefika kwenye eneo geni kwako, unaweza fungua app na kuangalia mawakala waliopo kwenye eneo lako na unaweza hata kuwapigia. Kipengele hiki ni kizuri zaidi kwa watu wanaosafiri kwenda sehemu mbalimbali wasizozijua vizuri.

Kubook ndege



Ukitaka kupata ticket za ndege kwa haraka na urahisi, unaweza tumia app hizi pia. Tumewahi zungumzia jinsi ya kubook ndege kwa app ya Mpesa, hivyo jambo hili linaweza kuwa sio jambo geni. Ila kama haujasoma makala iliozungumzia hayo, basi fahamu kuwa unaweza kubook na kupata Tiketi za ndege kupitia app ya Mpesa na app nyingine zenye kipengele cha kulipia ticket za ndege kwasasa.

Kulipia kwenye tuvuti za mtandaoni



Katika tuvuti nyingi ulimwengu huwa zinaweka mfumo wa kulipia kwa kutumia Visa au Mastercard. Mfano; ukihitaji kulipia bidhaa katika tuvuti ya Amazon au AliExpress kwasasa, utahitajika kuwa na Visa au Mastercard. Jambo la kupata Visa au Mastercard limerahisishwa sana kwenye app za pesa za mitandao ya mawasiliano tunayotumia. Unaweza zitengeneza kwa urahisi kupitia App ya Mpesa, Mixx by yas na app nyingine ndani ya dakika 5 tu. Jifunza za zaidi swala hili hapa.

Kusimamia, kuwekeza pesa au Kukopa pesa


Ukitaka kusimamia vizuri pesa zako unazotunza kwenye simu, ni vema ukawa unatumia app maana zimeweka urahisi. Unaangalia Salio la akaunti yako kirahisi na hata kufanya miamla ukiwa nje nchi. Kiufupi usimamizi wa pesa yako unakua ni rahisi zaidi.


Mbali na usimamizi, app hizi kwasasa zinakupa uwezo wa kuwekeza pesa kwa urahisi ili kuizalisha. Ukiachana na kuwekeza, unaweza hata kukopa pia.


Ni hayo tu tuliokuandalia katika makala hii, Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mengine zaidi.