Category Archives: Teknolojia

Jinsi ya kutengeneza Picha na Video za Ai Bure bila kikomo (Bing)

Kama wewe ni mfuatiliaji wa teknolojia ya AI (Artificial Intelligence), basi unajua kuwa sasa hivi kuna njia nyingi za kutengeneza picha na video kwa kutumia AI. Changamoto kubwa ni kwamba karibu kila platform ya AI maarufu huhitaji malipo kabla hujaweza kufurahia huduma zake.

Kwa mfano, sehemu ya kutengeneza video za AI mara nyingi ndiyo ghali zaidi. Kuna baadhi ya platform zikikugharimu hadi zaidi ya Tsh 200,000 kwa mwezi ili upate uhuru wa kutengeneza video kwa uhuru mkubwa.

Lakini sio kila mtu ana uwezo wa kulipia gharama hizi. Wapo wanaolipia kwa sababu wanatambua thamani yake; hasa wale wanaotumia video au picha za AI kutengeneza brand zao na hata kuingiza pesa kama content creators.

Habari njema ni kwamba sio lazima ulipie! Kuna njia halali na rahisi kabisa ambayo unaweza kutumia kutengeneza picha na video za AI bure na bila kikomo.

Jinsi ya kutengeneza Pesa Facebook BONYEZA HAPA>>>

Njia ya Kutengeneza Picha na Video za AI Bure

Njia hii ni kupitia huduma ya Bing. Hii ni injini ya utafutaji (search engine) inayomilikiwa na kampuni ya Microsoft. Watu huitumia kutafuta vitu mbalimbali kama ilivyo “Google” lakini inamilikiwa na kampuni tofauti.


Ukiachilia mbali kutafuta vitu mbalimbali, katika Bing kuna sehemu ya kutengeneza Video na Picha za Ai bure(Bing Image Creator na Bing Video Creator.). Hii sehemu ndio unaweza kuitembelea ukihitaji kutengeneza video au picha bila kulipia chochote.

  • Bing Image Creator: Hii ni sehemu inayokuwezesha kutengeneza picha za AI bure kabisa. Unachotakiwa kufanya ni kutembelea tovuti ya Bing(au Google) na kisha kutafuta Bing Image Creator. Hapo utaweza kuandika maelezo ya aina ya picha unayoitaka na AI itakutengenezea papo hapo.
  • Bing Video Creator: Kama unataka video, unaweza kutumia Bing Video Creator. Hii pia inapatikana mtandaoni bure kupitia Bing. Unachotakiwa kufanya ni kutafuta jina hilo kwenye Bing au Google, kisha utaelekezwa kwenye sehemu ya huduma hiyo.

MUHIMU KUJUA: Ili kutumia huduma hizi, utahitaji kuwa na akaunti ya Microsoft. Kama tayari unayo, unaweza kuingia moja kwa moja. Kama huna, unaweza kufungua akaunti mpya bure kabisa.

Kwa hiyo, kama umekuwa ukitaka kutengeneza picha na video za AI bure bila kikomo, usihangaike tena na gharama kubwa. Bing imekuletea suluhisho kwenye hili.

Facebook inalipa kiasi gani kwa kutazamwa mara 1000 (1k views)?



Facebook ni mtandao unaomilikiwa na kampuni ya meta. Katika Facebook kuna kipengele unachoweza kukiita “Facebook Ads” au “Meta Ads”. Kipengele hiki katika Facebook ni kwaajili ya makampuni au watu wanaohitaji kutangaza matangazo(Ads) kwenye mtandao wa Facebook. Kuna makampuni na watu wengi sana huwa wanailipa pesa hapo ili kuonesha matangazo kwenye mtandao wa Facebook.

Meta inatengeneza mabilioni ya pesa kwa mwaka kupitia watu wanaotangaza matangazo katika Facebook. Katika pesa hizo, huwa inachukua kiasi flani walizotengeneza na kuwalipa Content creator wa Facebook. Ili content creator kuanza kulipwa, anatakiwa kuingia katika program yao maalum kwanza(content monetization).


“Content creator” wa Facebook ni mtu ambaye huunda na kutoa maudhui (content) kwenye  Facebook ili kuwavutia, kuwaburudisha, kuwafundisha au kuhamasisha watazamaji. Na Maudhui au content zinazozungumziwa hapa ni Video, Picha na hata Makala za maandishi.

Ujuzi utakao kuwezesha kuingiza pesa mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Facebook inalipa kiasi gani kwa views 1000 za video?



Ukiwa kama content creator unaejihusisha na video katika Facebook, utalipwa pesa pale video zako zinapopata views (zinapoangaliwa na watu). Lakini fahamu kuwa Facebook haina kiwango maalum itakachokulipa kwa kupata views 1000 kwenye video zako. Facebook huwa inalipa kutokana na mfumo unaoitwa Cost Per Mille (CPM). Hii ina maana unalipwa kiasi kutokana na kiasi walicholipa watangazaji (watu walio lipa matangazo yanayooneshwa kwenye video zako). Yaani kama matangazo yanayooneshwa kwenye video zako hulipiwa pesa nyingi na watangazaji, basi unaweza kuingiza pesa nyingi pia ukiwa kama content creator.

Screenshot ukionesha jinsi Facebook ilivyomlipa moja ya Content creator wa India kwa video 1 fupi (Reel).


Lakini pia kiasi unacholipwa Facebook creator kinaweza kuathiliwa na mambo mengine kama nchi ya mtazamaji, sekta unayojihusisha nayo na hata tabia za watu wako katika Ads wanazoangalia.

  • Nchi ya watazamaji wako (mfano Marekani na Ulaya CPM huwa kubwa kuliko Afrika).
  • Mada/sekta ya content zako (mfano video za biashara, fedha, teknolojia hulipa zaidi kuliko utani au burudani tu).
  • Tabia za watazamaji kwenye Ads(watazamaji wakiwa wanajihusisha na Ads kwa kuziangalia au kubonyeza).

Muhimu kujua: katika Facebook kuna aina mbili za video. Video ndefu na video fupi ambazo huitwa “Reels”. Malipo hati ya aina hizo za video huwa yanatofatulia kabisa. Ukijihusisha na Reel unaweza ulipwe pesa ndogo sana kwa views 1000 ila uzuri ni kwamba huwa zinaweza kufika views milioni 1 kirahisi kuliko video ndefu.

Reels zinaweza kulipa $0.20 – $1.00+ kwa views 1000 (kutegemeana na nchi au mengineyo). Alafu video ndefu zinaweza kuwa $1 – $10+ kwa views 1000, hasa kwenye niche za biashara, fedha au teknolojia.

Kubeti: Jinsi ya kupata mikeka ya uhakika kwa kutumia AI

AI(Artificial Intelligence) ni nini? Kwa Kiswahili huwa tunaita “Akili Bandia” na ni teknolojia inayoruhusu mashine au kompyuta kufanya maamuzi, kuchambua taarifa, na kutabiri matokeo kama vile binadamu. Hivi sasa Teknolojia ya Ai inawekwa katika sehemu mbalimbali ili kurahisisha mambo ambayo yalikua si rahisi kwa kila mtu kuyafanya. Imerahisisha mambo ya kuedit picha, kuunda video, kuandika na hata kwenye maswala ya kubeti pia.

AI hutumia data kubwa/taalifa nyingi, hesabu, na mifumo ya machine learning ili kutoa matokeo yenye usahihi wa kiwango cha juu.

Katika ulimwengu wa michezo na kubeti, AI hutumika kuchambua takwimu za mechi, historia ya timu, wachezaji, hali ya hewa, na hata mienendo ya dau (betting patterns) ili kutoa mapendekezo bora zaidi.

Orodha ya kampuni za kubeti ukiwa Tanzania BONYEZA HAPA>>>

Mikeka ya uhakika ni nini?

“Mikeka ya uhakika” ni neno linalotumika na wapenzi wa kubeti kumaanisha mikeka iliobashiri mechi zenye nafasi kubwa ya kushinda. Kwa kawaida, mikeka hii inatokana na uchambuzi wa kitaalamu wa michezo.

Hata hivyo, ni muhimu kuelewa kuwa hakuna dau lenye uhakika wa 100%, bali mikeka ya uhakika inamaanisha uwezekano mkubwa wa kushinda kulingana na uchambuzi ila lolote lisilotarajiwa linaweza kutokea.

Kupata mikeka ya uhakika kwa kutumia AI

Kama ilivyo katika sehemu nyingine, AI imeleta mapinduzi kwenye ulimwengu wa kubeti pia. Kwasasa kupitia platform za Ai za ubashiri, unaweza tumia kupata mkeka wa uwakika uliochambuliwa kitaalamu bila kupoteza muda sana. Huduma au platform hizi maalum hutoa uchambuzi wa haraka na sahihi uliofanywa na AI.

Kuna watu hivi sasa huwa wanatumia Ai katika kupata mikeka ya kubeti na hushinda baadhi ya mikeka yao. Hii imetusukuma sisi kukupa mwanga juu ya hili na pia tumekuandalia video inayofudisha jinsi ya kutumia AI kupata mikeka ya uhakika.

Haya ni Matokeo yaliobashiriwa na Ai kisha yakawa kweli kwa 100% baada ya mechi kuchezwa.

Ukihitaji video inayofundisha hayo kwa kina, unaweza kuipata kupitia WhatsApp. Utalipia Tsh 9000 TU kupata masomo haya lakini baada ya kujifunza utakua na uwezo wa kutengeneza mikeka yako kwa Ai na kushinda kirahisi.

Kiufupi Ai imekua msaada katika kupata mikeka uwakika kwa haraka ingawa haiwezi kukupa ushindi kwenye kila mkeka.


Yani inaweza kuongeza nafasi zako za kupata mikeka ya uhakika maana AI uondoa upendeleo na kutumia data kubwa au taalifa nyingi ambazo so rahisi kwa binadamu kuzifikilia kwa muda mfupi.

Onyo: Hauruhusiwi kubeti ukiwa chini ya Miaka 18

Jinsi ya kuuza Beats za Muziki Mtandaoni (Online)

Watu wengi(Music Producers) wana kipaji cha kutengeneza beats za muziki lakini changamoto kubwa inabaki kuwa jinsi ya kuziuza na kupata kipato. Kwa sasa, teknolojia imerahisisha sana upande huu, unaweza kuuza beats zako kwa wasanii bila hata kuwa na studio kubwa. Tena unaweza kuwafikia watu Toka nchi mbalimbali wakawa Wateja wako.

Hapa chini kuna njia tatu bora za kuuza beats zako mtandaoni. Unaweza zitumia ikiwa wewe ni producer unahitaji kutengeneza Pesa mtandaoni kupitia Beats zako.

Njia 3 za kuuza beats zako mtandaoni:

  1. Tumia Platform Maalum kwa Uuzaji wa Beats

Kuna tovuti nyingi ambazo zimetengenezwa mahsusi kwa wauzaji wa beats. Hizi platform zinakuwezesha ku-uproad kazi zako na kuziuza moja kwa moja kwa wasanii kutoka sehemu mbalimbali duniani. Baadhi ya mifano ni:

BeatStars

Airbit

Traktrain

Unachohitaji ni kufungua akaunti(inaweza kuhitaji kulipia ili kuanza kuitumia), kuweka bei zako, na ku-uproad beats zako. Hii ni njia rahisi na salama kwa sababu wateja wengine watatoka ndani ya hiyo hiyo platform ana watalipia kupitia mfumo wanaoujua, na wewe unapokea malipo yako.

Huu ni ukurasa wa tuvuti/website ya Beatstars ukionesha Beats zinazouzwa.
  1. Kuwa na Website Yako ya Kuuza Beats

Kama unataka kuwa na brand yako binafsi, basi kuwa na website ni muhimu. Kupitia website yako, Wateja wataona beats zako zote kwa mpangilio mzuri. Unaweza kuweka mfumo wa malipo (Card, Crypto, Skrill, M-Pesa, n.k).

Inakusaidia kujenga jina lako kama producer professional.

Website yako inaweza pia kuwa sehemu ya kuonyesha huduma nyingine unazotoa kama mixing & mastering, au hata tutorials za muziki.

  1. Uza Kupitia Mitandao ya Kijamii

Mitandao ya kijamii ni soko kubwa la bure. Tumia Instagram, TikTok na Facebook kuonyesha vipande vya beats zako. Unaweza ku-uproad video fupi za beats alafu wasanii watakao lipenda beat, wanakua wanakutafuta inbox kwaajili ya maelewano ya kibiasha.

Unaweza pia kutumia captions nzuri na kutoa challenge mbalimbali kwa wasanii juu ya Beats zako ili kupata Wateja zaidi.

Mitandao ya kijamii hukusaidia kufikia watu wengi bila gharama kubwa, ila unahitaji kuwa consistent na ubunifu kwenye content unayoshare.

Kuuza beats mtandaoni siyo kazi ngumu kama ukipanga vizuri mfumo wako. Unaweza kuanza na platform za kuuza beats, kisha kujenga website yako, na hatimaye kutumia nguvu ya mitandao ya kijamii kupata wateja zaidi. Yani mfumo wako ukiwa vizuri, unaweza tumia njia zote tatu kama ulimwengu wa kuuza beats zako.

Kutengeneza au kurekodi nyimbo kwa simu BONYEZA HAPA>>>

Orodha ya Kampuni 5 za kubeti  ukiwa Tanzania

Sekta ya kubeti nchini Tanzania imekua kwa kasi kubwa katika miaka ya karibuni. Kuanzia vijana wa mijini hadi mashabiki wa mpira/michezo vijijini hutumia simu zao kuweka dau kwenye makampuni ya kubeti ili kucheza. Na uzuri ni kwamba, kampuni zipo nyingi kiasi kwamba wachezaji huwa na uwanja mpana wa kuchagua.
Lakini swali kubwa hapa huwa ni moja; Kampuni ipi bora na salama kutumia kwenye kubet?

Kwa kuwa zipo kampuni nyingi zinazojitokeza kila siku, tumekuchambulia chache TU kwenye kampuni nyingi zenye leseni kutoka Gaming Board of Tanzania (GBT), na zimethibitishwa kuwa na huduma bora. Tumekuorodheshea kampuni hizi hapa ili kuokoa muda wako ikiwa unaanza kubeti au unatafuta kampuni nyingine salama.

Makampuni mazuri ya kubeti Tanzania



1. Betway Tanzania

Betway ni miongoni mwa makampuni makubwa duniani, na hapa Tanzania imejikita vizuri sana katika upande wa kutoa huduma za kubeti. Inajulikana kwa huduma bora, promosheni/zawadi za mara kwa mara na odds nzuri pia.


Nini cha kuvutia? Unapojiunga unapata zawadi za ukaribusho, Malipo ni kupitia mitandao ya simu, lugha ya Kiswahili, na huduma kwa wateja masaa 24. Ukiachana na hiyo, unaweza kubeti hata ukiwa na pesa ndogo ( Tsh 100).




2. SportyBet Tanzania



Ikiwa unapenda betting kwa upande wa simu zaidi, SportyBet inaweza kuwa ni chaguo sahihi. App yake ni nyepesi, haina ulaji mwingi wa data na inakuja na “dark mode” kwaajili ya kulinda afya ya macho. Uzuri wake mwingine ni odds nzuri, rahisi kutumia na mambo mengi mengi ambayo mchezaji unaweza kufurahia.


3. PremierBet Tanzania



Hii pia ni moja ya kampuni kongwe nchini. PremierBet haijaishia tu mtandaoni bali pia ina maduka ya betting katika miji mingi. Inakubali njia nyingi za malipo kama Selcom na mitandao ya simu.
Uzuri wa Premier bet ni kwamba wana  uzoefu mkubwa kwenye sekta hii na pia kuna uwepo wa maduka ya huduma zao hapa Tanzania.



4. LeonBet Tanzania



Ingawa bado ni jina jipya sokoni, LeonBet inaonyesha dalili za ukuaji mkubwa. Inajulikana kwa odds nzuri na ofa za mara kwa mara. Haijawa na jina kubwa sana Duniani kama Betway ,Premierbet lakini inafanya vizuri sana huduma zake huku ukiendelea kutumiwa na wengi katika kubashiri. Odds zao ni nzuri, kutoa promosheni au zawadi ni mara kwa mara.



5. BetPawa Tanzania


BetPawa imevutia wapenzi wengi wa kubeti kutokana na dau lake dogo kabisa. Unaweza kubeti kwa shilingi chache tu. Pia inalipa haraka na mara nyingi huendesha promosheni maarufu kama vile “Pawa6” ambayo ni kama zawadi kwa watumiaji wake. Kwenye Betpawa unabet kwa dau dogo, malipo ni ya haraka.

MWISHO; Kila kampuni kati ya hizi ina uzuri wake na mapungufu yake pia. Kujaribu kunaweza kuukupata ufahamu zaidi juu ya kampuni gani ya kubeti ni Bora kwako.


Pia kumbuka; Kubeti ni burudani, kwaiyo usiweke chanzo kama cha kipato cha kudumu. Tumia akili na weka dau unaloweza kupoteza bila kuathirika kivyovyote.

Jinsi ya kupata Code za mikeka ya leo (Prediction Today)

Mchakato wa kuchambua timu na kusuka mikeka ya kubeti huwa unachukua muda sana kwa baadhi ya watu. Kuna watu huumiza akili zaidi ya saa 1 kufikilia mkeka uwake uwe vipi kabla hajaweka dau.

Kama wewe ni mmoja kati ya wanaotumia muda mwingi katika kusuka mikeka ya kubeti, fahamu kuwa unaweza okoa muda wako wa kusuka mikeka kwa kuchukua mikeka iliosukwa na  watu wengine. Kuchukua mikeka iliosukwa na watu wengine na kuibetia, ni njia rahisi ya kubeti inayoweza kukufanya uwe unashinda baadhi ya mikeka bila kupoteza sana muda wako. Kitu kikubwa hapa ni kuhakikisha mkeka uliouchukua, Umetoka kwa mtu ambae anafikilia vizuri kabla ya kuutengeneza.

Kufanya hivi hakuna maana utakua ukishinda kila siku, lakini baadhi ya siku unaweza kushinda mpaka ukampongeza aliekupa mkeka.


Siku hizi katika makampuni ya kubeti, wamerahisisha maswala ya kuchukua mikeka iliosukwa na watu wengine. Kuna kipengele cha “Code za mikeka” ambacho kinakuwezesha kuchukua mikeka kwa wengine kwa kujaza code tu. Yani ukitaka mkeka wa mtu, unachukua Code ya mkeka huo na kuujaza katika akaunti yako kwaajili ya kubeti. Hizo code huitwa “Booking Code” pia. Na yote haya ni kuokoa muda wako tu.

Kuwa makini na utapeli huu katika kubeti BONYEZA HAPA>>>

Sehemu za kupata Code za mikeka bure (Booking Codes)

1. Katika tuvuti ya kampuni unalobetia




Baadhi ya makampuni makubwa ya kubeti huwa yanakipengele maalum kwa code za mikeka. Kwenye kipengele hicho unakutana na Codes za mikeka mbalimbali iliotengenezwa na watu wengine alafu unaweza kutumia kubeti mkeka kwa upande wako.

Mbali kuchukua Code, unaweza sambaza na code za mikeka yako ikiwa utahitaji. Betway ni kati ya makampuni ya kubeti yenye kipengele cha “Booking Code” kwenye tuvuti zao. Katika tuvuti ya Betway kipengele hiki kinajulikana kama “Booking Codes”.

2. Tuvuti maalum kwa code za mikeka



Kuna tuvuti maalum ambazo huwa zinajihusisha na code za mikeka. Katika tuvuti hizi unapata code za mikeka unayoweza kubeti katika makampuni mbalimbali. Humu unakutana na orodha kubwa sana ya code za mikeka na Odds zake pia. Naweza kusema katika tuvuti hizi unaweza kupata mkeka wa kila Odds unazohitaji.

Convertbetcodes ni moja ya tuvuti ambazo hujikita kwenye code za mikeka unayoweza kuitumia. Tuvuti hii inatumika ku-convert code za kampuni moja kwenda nyingine lakini pia ina orodha ya code nyingi sana za mikeka iliosukwa na watu wengine. Unaweza kupata hata code za mikeka ya Leo.

3. Katika mitandao ya kijamii


Unatumia mitandao ya kijamii kama Facebook, X na Instagram? Basi fahamu kuwa kuna namna unaweza kupata code za mikeka humohumo. Baadhi ya watu siku hizi hutumia muda wako kuunda mikeka na kutoa au kusambaza Code kwa wengine kupitia mitandao ya kijamii.

Kuchukua Code wanazosambaza na kuzitumia, kunaweza kuwa njia nzuri ya kukwepa kupoteza muda wa kuunda mikeka. Mfano wa watu wanaotoa code za mikeka yao mitandaoni ni Samkicheko.

Ni hayo tu katika Makala hii lakini nakukumbusha; Kabla haujafanya uamuzi wowote katika kubeti, fahamu kuwa kubeti kunahitaji ustaharabu pia. Zingatia hii kata kwenye kutafuta code za mikeka ya leo. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy!

Disclaimer: This article is for education only and is not financial advice. Always do your own research before making any decisions.

Unataka kujua Cryptocurrency ni nini? Jifuze hapa



Kiufupi Cryptocurrency ni sarafu au pesa ya kidigitali ambayo mtu anaweza kutuma au kuipokea mtandaoni lakini huwa ipo huru kwa kutokua chini ya Benk kuu au serikali. Ni watu tu huamini na kuanza kuitumia au kuacha kutumia. Na hauwezi kuigusa kama pesa za kawaida maana ipo mtandaoni tu.

Sarafu hii ya kidijitali (digital currency) inatumia mbinu za usalama za kisasa (cryptography) ili kuhakikisha miamala (transactions) ni salama na kudhibiti uundwaji wa sarafu mpya(bandia. Unaweza kuzituma pesa hizi kwa mtu kama malipo au ukazipokea na kuzitunza kama ilivyo kwenye pesa za kawaida.

Cryptocurrency(pesa za mtandaoni) huwa zipo nyingi na zina majina tofauti. Mfano wa cryptocurrency maalufu duniani ni:

  1. Bitcoin (BTC)
  2. Ethereum (ETH)
  3. Binance Coin (BNB)
  4. Tether (USDT)

Unatunza vipi Cryptocurrency?



Cryptocurrency huwa zinatunzwa katika mfuko maalum wa pesa za kidigitali. Mfuko huu huitwa  “digital crypto wallet” na hufanya kazi kama sehemu unayoweza kutunza pesa zako kidigitali au kufanya miamala. Mtu alieweka cryptocurrency kwenye digital crypto wallet ni sawa mtu alieweka pesa za kawaida katika Bank au akaunti nyingine za pesa kama Mpesa.

Kuna platform nyingi mtandaoni huwa zinakuwezesha mtu kufungua akaunti na kumiliki mfuko wako wa kuwekea Cryptocurrency Bure kabisa. Mfano wa platform hizo ni Binance.

Mtu alieweka cryptocurrency kwenye digital crypto wallet kama Binance ni sawa mtu alieweka pesa za kawaida katika Bank au akaunti nyingine za pesa kama Mpesa.

Jinsi ya kutengeneza Pesa mtandaoni kwa kuandika BONYEZA HAPA>>>

Unawezaje kupata Cryptocurrency?





Kama na wewe unahitaji kuwa na pesa za crypto, utahitajika kuwa na mfuko kwanza wa kutunzia(crypto wallet). Baada ya hapo unaweza tumia njia hizi mbili za kupata Cryptocurrency kwenye mfuko wako:



Njia ya kwanza ya kupata Cryptocurrency ni kuzinunua kwa pesa zako za kawaida. Yani unatumia pesa yako ya kawaida kuinunua pesa ya mtandaoni (cryptocurrency) alafu unaitunza kwenye mfuko wako wa crypto. Hii tunaweza kuiita “kubadilishana na pesa za kawaida”, yaani exchange. Mfano; Ukitaka kupata USDT moja (1), utatakiwa kuwa na kama Tsh 2600 (makadilio). Ukitaka BITCOIN moja (1), unaweza kuipata kwa Tsh milioni 200 na zaidi.

Thamani za huwa zinatofautiana alafu pia huwa zinapanda na kushuka. Mbali ya hilo, fahamu tu kuwa Kuna zenye thamani ndogo  na kuna zenye thamani kubwa pia.

Njia ya pili ni kutoa huduma au kufanya huduma itakayokupa au kukulipa kwa cryptocurrency. Kuna huduma unaweza kutoa mtandaoni alafu ukapewa cryptocurrency kama malipo bila kutumia pesa yako ya kawaida. Mfano wa huduma hizi ambayo ni rahisi kabisa ni huduma ya Opera news hub ambayo tumeizungumzia sana kwenye Makala za The Bestgalaxy.

Watu wengi wanatumia cryptocurrency kulipia vitu au kufanya biashara mtandaoni kwa sasa lakini Teknolojia yake ipo kwenye hatua ya ukuaji na maboresho. Huwa inaaminika kuwa cryptocurrency inaweza kuwa ndio pesa zitakazokua zinatumiaka katika miaka ijayo badala ya kutumia pesa za kawaida.

Mambo gani muhimu ya kujua kuhusu cryptocurrency?





Pamoja na yote, Kuna changamoto ambazo kila mtu anapaswa kujua kabla ya kuingia kwenye ulimwengu wa crypto. Kati ya Changamoto kubwa ni zifuatazo:

Usalama wa crypto ni mdogo kuliko pesa za kawaida. Usipokua na kuelewa mzuri, unaweza kutapeliwa kirahisi kutokana na wingi wa matapeli katika upande huu.


Cryptocurrency zinaweza kushuka thamani muda wowote. Yani unaweza kutuza cryptocurrency zako Leo zenye thamani ya milioni 1, alafu kesho ukaamka na kukuta zimeshuka thamani kutokana na jambo flani, zomekua ni laki 5. Kwaiyo kwenye ulimwengu huu unatakiwa kuwa mtu unaweza ku-manage risk.


Cryptocurrency huwa haiwezi kulipia vitu vingi sana kwenye maisha ya kawaida. Kuna huduma nyingi ambazo Bado hazijaitambua cryptocurrency katika malipo kwasababu mbalimbali.

Disclaimer: This article is for education only and is not financial advice. Always do your own research before making any decisions.

Kuna faida ya kuchelewa kununua toleo jipya la simu?



Karibu kila mwaka, makampuni ya simu huwa yanatoa matoleo mapya ya simu. Makampuni haya ya simu huyatoi tu matoleo ya simu, bali huwa yanashindana kutoa simu zenye maboresho na Teknolojia mpya ilio Bora kwa watumiami.
Watu wengi huwa wanaumiza kichwa sana namna gani wanaweza kupata matoleo haya mapya.

Vijana ambao huwa wanamtindo wa kuhitaji kujaribu vitu vipya, huwa wanahitaji matoleo mapya. Kujaribu vitu vipya ni jambo zuri sana ila ni nzuri zaidi kama liko ndani ya uwezo wako.
Ikiwa hauna uwezo wa kipesa wa kununua kila toleo jipya la simu, basi usiumize sana kichwa juu ya matoleo haya ya simu. Sababu za kutoumiza kichwa sana ni zifuatazo;

Mambo unatakiwa kujua kuhusu simu za mkopo BONYEZA HAPA>>>

Sababu za kutonunua kila toleo jipya la simu




Uzalishaji wa simu upo kibiashara




Fahamu kuwa makampuni ya simu yapo kibiashara na simu ndio moja ya bidhaa wanazouza. Kama zilivyo biashara nyingine, wanahitaji bidhaa ziuzike na wapate faida walioikusudia kisha wauze tena. Kutoa toleo jipya la simu ni sawa na kuingiza mzigo mpya sokoni ili watu wanunue. Hii ndio moja ya sababu simu hutoka kila mara na kuuzwa kama zilivyo bidhaa nyingine.

Kwaiyo endapo utakua hauna uwezo wa kununua toleo jipya la simu, usijisikie kuachwa nyuma. Nasema hivyo kwasababu wao wametoa toleo jipya kwasababu ya faida yao ya kibiashara na sio yako moja kwa moja. Yani kama bidhaa hauwezi ilimiliki, isikunyime usingizi.

Matoleo mapya hushuka bei baada ya muda



Kama umekua karibu na maswala ya kununua simu, utagundua kwasasa simu nyingi huwa zinapungua Bei kwa kasi sana baada ya mwaka moja au mwili toka zitolewe. Yani simu nyingi sana zilizouzwa bei ghali mwaka Jana na mwaka juzi unaweza zikuta kwa bei rahisi mwaka huu. Kuna watu walinunua simu kwa laki 9 kipindi hicho lakini kwa sasa simu walioinunua inapatikana kwa laki 3 tu. Na kadri siku zinapozidi kwenda ndio simu hushuka bei zaidi kutokana na matoleo mapya kuwa mengi na sababu nyingine.

Kwaiyo hapa Naweza kusema kutokimbilia matoleo mapya kunaweza kukufanya uiokoe pesa yako. Unaweza kuwa unasubiri simu mpya zishuke bei ndio ununue kwa bei rahisi.

Baadhi ya matoleo mapya ya simu huja na matatizo



Kwenye historia za simu, kuna matoleo mapya mengi sana yaliokuja na matatizo. Yani simu inaweza kutolewa kipindi hiki lakini baada ya muda mchache, watuamaji wakaanza kukumbana na matatizo ya kiufundi. Mfano wa matatizo yaliowahikutokea sana kwenye historia za matoleo ya simu ni kupata moto sana, vioo kutokwa na mistari, kuzima ghafla na mambo mengine mengi.


Kwaiyo kuchelewa kununua matoleo mapya ya simu kunaweza kukusaidia kuepuka matatizo kama haya. Yani utaona watu wanalalamika juu ya matatizo haya kabla haujatoa pesa yako kuinunua.

Matoleo mapya hayawi tofauti sana na yaliopo



Siku hizi kampuni kama Apple na Samsung huwa zinatoa matoleo kila mwaka lakini haina maana kuna ulazima wa kuchukua kila toleo jipya. Baadhi ya watu kwasasa huwa wananunua hata matoleo ya zamani ya simu za kampuni hizo kwasababu ya kuepuka bei. Mbali na bei, siku hizi kunakua na utofauti mdogo sana wa toleo jipya na toleo la zamani.


Tofauti wanazoweka kwasasa ni Teknolojia ambayo sio ya lazima sana kwa mtumiaji wa kawaida. Mfano; unawezakukuta simu toleo jipya ni bei ghali alafu inasifika kwa kamera inayozoom umbali mrefu sana… Mtumiaji wa kawaida hii itakusaidia nini? Haina umuhimu sana.

Kwa kuangalia hayo yote tuliozungumzia hapo juu, utagundua kunafaida ya kutokimbilia matoleo mapya ya simu. Matoleo mapya ni mazuri lakini kama hauna uwezo wa kununua kila toleo bila Mawazo, basi kuyaacha yapite kwa muda ni chaguo zuri pia.

Jinsi ya kutengeneza Pesa katika channel ya WhatsApp kwa kutumia Opera news hub

Mtandao wa WhatsApp unaweza kufanya uungane na kuwasiliana watu mbalimbali. Lakini katika mtandao huu unaweza pia ukaingiza pesa na kuwa moja ya watu wanaotumia mtandao vizuri.


Watu wengi huwa wanatamani kujua ni jinsi gani mtu anaweza kuingiza pesa mtandaoni. WhatsApp ni moja ya mitandao ambayo mtu anaweza kujifunza kuutumia kutengeneza Pesa na akawa amefanikiwa kuitwa mtu anaetengeneza pesa mtandaoni. Kwaiyo ikiwa wewe ni mmoja wanaotaka kujua namna ya kutengeneza Pesa mtandaoni, mtandao huu unaweza kuwa upande mzuri.

Jinsi ya kutengeneza Pesa kwa kucheza games mtandaoni BONYEZA HAPA>>>



Kwenye Makala hii, unaenda kujifunza namna ya kutengeneza Pesa kwenye Channel ya WhatsApp(WhatsApp channel) na tutatumia Opera news hub kufanya hivyo. Tuanze kwa kufahamu vitu hivi viwili kwanza;

  • Channel ya WhatsApp(WhatsApp channel): Hiki ni kipengele cha WhatsApp ambacho kina kuwezesha mtumiaji wa WhatsApp kuwa na Followers/wafuasi. Unaweza kuwatumia wafuasi Picha, Makala na kushiri nao mambo mbalimbali kama ilivyo kwenye kurasa za Instagram au Facebook. Kila mtumiaji wa WhatsApp anaweza kumiliki channel yake bila shida yoyote.
  • Opera news hub: Hii ni platform ambayo huwa inalipa watu kwa kuandika Makala mbalimbali. Mtu huwa analipwa pesa kutokana makala zake zilizosomwa na watu. Wingi wa wasomaji, unaweza kuwa ndio wingi wa mapato pia. Kusoma zaidi kuhusu hii BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kutengeneza pesa katika WhatsApp channels kwa kutumia Opera news hub




Iwapo mtu utafanikiwa kumili channel ya WhatsApp yenye wafuatiliaji wengi, Kuna namna unaweza kuitumia kuingia pesa kupitia Opera news hub. Utakua unaitumia channel ya WhatsApp kupata wasomaji wa Makala zako za Opera news hub ili ulipwe na Opera news hub. Utakachotakiwa kufanya ili kufanikisha hayo yote ni kufuata hatua zifuatazo tu;

  • Fungua akaunti ya Opera news hub kisha utaanza kuandika Makala nzuri kwaajili ya followers wako wa Channel ya WhatsApp. Mfano; Unaweza kuandika Makala za Michezo kama channel yako ni kuhusu Michezo.
  • Baada ya hapo, utakua ukizituma link za Makala katika Channel yako ya WhatsApp.
  • Endapo Makala zako zitapata wasomaji wengi wanaozisoma kutoka kwenye channel yako ya WhatsApp, utaingiza pesa kwenye akaunti yako ya Opera news hub.



Kwa kufuata hayo yote, utakua umefanikiwa kuingiza pesa kwenye WhatsApp channel yako kwa msaada wa Opera news hub. Pesa ambazo unaweza kuzitengeneza, zinategemeana na watu ambao ni wasomaji wa Makala zako. Kama utakua na watu wengi wanaozisoma, pesa pia itakua ni nyingi.

Opera News Hub: Jinsi ya kufungua akaunti, kutengeneza pesa na kupokea

Opera News Hub ni platform ambayo inawezesha watu kuingiza pesa kwa kutengeneza contents (mahudhui). Kama ni muandishi, hii inaweza kuwa moja ya platform nzuri kuitumia unapokua unahitaji kutengeneza Pesa kwa kuandika ukiwa Tanzania. Kuna kipindi platform hii hilikua haipatikani kwa waandishi wa Tanzania huku baadhi ya nchi jirani wakiwa na uwezo wakuitumia. Lakini kwasasa Mwandishi, ukiwa Tanzania unaweza kufungua akaunti, kutengeneza pesa na kuzipokea bila tatizo.

Jinsi ya kufungua akaunti ya Opera news hub



Ukihitaji kufungua account ya Opera news hub, Anza kwa kutembelea tuvuti ya Opera news hub ambayo ni https://hub.opera.com/ kwenye web browser yako. Baada ya kuingia kwenye tuvuti, utatakiwa kuanza kutengeneza akaunti yako kwa Gmail au Facebook akaunti. Kutumia Gmail ni chaguo zuri zaidi maana unaweza pata matatizo kwenye akaunti yako ya Facebook kirahisi zaidi kuliko Gmail(Gmail ni salama zaidi katika kufungua akaunti).


Kwenye mchakato wa kutengeneza akaunti utatakiwa kujaza taalifa zako kama kama vile majina Kamili, nchi unayotoka na namba za kitambulisho chako na jina unalotaka kuitumia kwenye Opera news hub. Mbali na taalifa hizo kuna namba za wallet utatakiwa kizijaza. Namba hizi za wallet utazipata kwa kupakua app ya Minipay na kufungua akaunti ya Minipay kwa kutumia namba yako ya simu.

Minipay ni app ambayo inatumika kama mfuko wa kupokea hela za mtandaoni. App hii inapatikana kwenye Playstore and hata Appstore ukihitaji kuipakua. Katika ku verify namba yako kwenye Minipa, verification code zitatumwa kwenye WhatsApp hivyo hakikisha namba tunayoitumia, unatumia kwenye WhatsApp pia.

Ukishajaza namba ya wallet na vitu vingine, utafanikiwa kutengeneza akaunti yako Bure kabisa. Utakua na uwezo wa kuingia kwenye akaunti yako ya Opera news hub kwa kutumia simu yako au PC. Uzuri ni kwamba kama unahitaji app ya Opera news hub pia ipo!  Unaweza ichukua Toka Playstore au Appstore.

Jinsi ya kutengeneza pesa katika Opera news hub



Katika Opera news hub, waandishi wanaweza andika Makala zao na kuzichapisha ili zisomwe na watu wengine. Endapo Makala za muandishi zitakua zikisomwa watu, pesa itakua inaingia katika akaunti ya muandishi kwakua amefanya kazi nzuri inayochaguliwa au kupendwa na watu. Hapa nazungumiza zile Makala ambazo zinapata click nyingi (Mibofyo), likes, na hata comments (maoni).


Ili kufanya vizuri zaidi kwenye Opera news hub kama muandishi, ni vema ukawa unatoa Makala za habari na vitu vinavyo trend. Hii itakusaidia kupata wasomaji wengi na kuingiza pesa zaidi. Uwe na uwezo wa kutengeneza hata Makala 5 au 10 kabisa kwa siku ili kutengeneza Pesa nzuri katika mwezi. Pesa zote utakazotengeneza kwenye Makala yako, utakua unaziona kwenye akaunti yako.

Pesa zilizotengenezwa na mmoja wa waandishi wa Opera news hub (Sio kila mtu anaweza tengeneza kiasi hiki)



Jinsi ya kupokea pesa katika Opera news hub


Pesa ulizotengeneza kwenye Opera news hub utakua ukizipokea kila mwezi. Pesa hizo zitakua zinaingia kwenye akaunti yako ya Minipay.

Minipay ni app ambayo inatumika kama mfuko wa kupokelea hela mtandaoni. Uzuri ni kwamba tumeisha iongelea hapo juu, hivyo hatutazungumzia sana hapa.
Kwaiyo pesa zitaingia kwenye akaunti yako ya Minipay na utakua na uwezo wa kuzitoa hata kwenye simu yako tu kupitia Mpesa, Mixx by Yas, Airtel Money na hata Bank ikiwezekana.

Kwa kufanya hayo yote, utakua umefanikiwa kuingiza pesa kwa kuandika mtandaoni kupitia Opera news hub. Mwisho, ningependa kusisitiza kuwa Makala za mambo ya habari na mambo “trend” huwa zina nafasi kubwa ya kufanya vizuri. Ikiwa utakua na Makala mbali na hizo itakuhitaji uweke jitihada zaidi kwenye kuchapisha Makala mpya kila mara.

Muhimu: Maelezo haya yanajitosheleza kabisa kukusaidia wewe kuanza kuingiza pesa endapo utayafuata na kuanza kazi.

Lakini kama utahitaji msaada wa moja kwa moja wa kufunguliwa akaunti na kuunganisha kila kitu bila kupoteza muda, unaweza kutuma ujumbe  WhatsApp +255 622 586 399 tukusaidie kila kitu ili kazi yako inayobaki ni kuandika Makala na kuhesabu mapato yako.

Jinsi ya kutengeneza Pesa Facebook Bonyeza Hapa>>>