Category Archives: Teknolojia

Jinsi ya kutuma pesa Kenya na Tanzania (Vodacom/Safaricom)

Kutuma pesa nje ya nchi ilikua ni jambo gumu sana katika miaka ya nyuma, lakini wakati huu jambo hili ni jambo jepesi kiasi kiasi kwamba unaweza fanya kiganjani pako ndani ya dakika mbili. Hii yote ni kwasababu ya Teknolojia ambayo lengo lake ni kurahisisha maisha ya Binadamu.

Hapa The bestgalaxy tunaenda kuangalia jinsi ya kutuma pesa Kenya na Tanzania kwakuhusisha Safaricom Kenya na Vodacom Tanzania. Kama upo nchi ya Tanzania, unaweza tumia mtandao wa Vodacom kumtumia pesa mtu kwa Mpesa akiwa kenya anatumia mtandao wa Safaricom. Pia ukiwa kenya unatumia Safaricom unaweza mtumia pesa mtu kwa Mpesa akiwa anatumia mtandao wa Vodacom Tanzania.

Jinsi ya kutengeneza Logo ya biashara au Binafsi BONYEZA HAPA>>>

Kutuma pesa Kenya na Tanzania (Vodacom/Safaricom)

Unataka kujua jinsi ya kutuma? Usijali, hapa chini kuna maelezo juu ya hatua unazoweza kufuata pale unapotaka kutuma pesa ukiwa Tanzania na kenya kwakutumia mtandao wa Vodacom au Safaricom.

Kutuma pesa toka Tanzania kwenda Safaricom Kenya kwa kutumia Mpesa(Vodacom)

  • Fungua App ya Mpesa na uguse sehemu ilioandikwa “Services” alafu utaletewa orodha ya huduma.
  • Chagua huduma ilioandikwa “International Transfers” kwenye orodha hiyo.
  • Baada ya kufanya hiyo utapelekwa kwenye ukurasa utakao takiwa kuchagua nchi unayotaka pesa iende. Utachagua Kenya kwakua ndiko unataka kutuma pesa.
  • Baada ya kuchagua nchi utaletewa ukurasa wa kuchagua mtandao. Wewe utachagua mtandao wa  Safaricom kwakua mtu unaemtumia anatumia Safaricom.
  • Baada ya kuchagua, utapelekwa kwenye ukurasa utakao takiwa kujaza namba ya simu ya mtu unaemtumia pesa kwa mfumo wa kimataifa (254xxxx) kisha andika kiasi unachotaka kutuma. Na ukishajaza utabonyeza kitufe kilichoandikwa “Endelea” ili kuendelea na hatua nyingine za uthibisho wa kutuma pesa yako.

Sending money from Kenya to Tanzania with Mpesa (Safaricom)

  •  Dial *334# to open Mpesa Global.
  • Select “Send Money Abroad”.
  • Select “Send to Mobile Number”
  • Select “Tanzania” as a county you want to send money.
  • Enter Recipient Mobile Number in International Format (255xxxxxx)
  • Enter Amount of Money you want to send.
  • Select  source of fund and purpose of Funds then confirm.

Mwisho ningependa kukukumbusha kuwa makini katika kutuma pesa yako ili kuepuka kutuma pesa kimakosa. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy na usiache kufuatilia The bestgalaxy.

Jinsi ya kuangalia video Youtube  bila kutumia bando sana(Okoa data)

Uangaliaji wa video online kupitia app  kama Youtube,Tiktok na Instagram unaweza kua ni moja ya vitu ambayo hupelekea bando la internet kutumika sana kwenye simu. Kiufupi kama mtu anapenda kuangalia video sana mtandaoni basi hata matamizi yake ya data yanaweza kuwa ni makubwa na kupelekea bondo kuisha haraka. Hii inweza kuwa kawaida au ikawa tatizo kwa baadhi ya watu.

Hapa The bestgalaxy tunaendea kuangalia mambo machache ambayo mtu anaweza fanya kuangalia video Youtube  bila kutumia bando sana. Kama unataka kujua mambo yaha hebu chukua muda wako kusomaa hapa chini.

Fanya haya kuangalia video Youtube  bila kutumia bando sana

Washa Data saving mode

Youtube imejali matumizi ya data ya watumiaji wa app ya Youtube kwa kuweka kipendele kinachopunguza matumiza ya Data. Kuna kipegele  ambaacho ukikiwasha katika app ya youtube, unakua unatumia bando lako la internet kidogo. Kipengelea hii kinaitwa Data saving mode na ukikiwasha huwa kinapunguza na kuzima baadhi ya vipengele vingine vya app ya  Youtube vinavyotumia Data. Ni jambo zuri kutumia njia hii kuoa data lakini video hua zinaonekana hazina ubora. Kuwasha Data saving mode nenda katika app alafu gusa Profile yako kisha bonyeza alama ya settings iliojuu kulia alafu chagua “Data saving”. Baada ya hapo, washa sehemu ya juu ilioandikwa “Data saving mode”.

Chagua video fupi

Youtube inavideo fupi na ndefu. Kati ya video fupi na video ndefu katika kutumia data tunaweza sema  uangaliaji wa video ndefu unaweza kufanya utumie data zaidi endapo video hizo zitakua na ubora wa picha sawa. Hivyo kama unahitaji kuangalia video Youtube  bila kutumia bando sana unaweza angalia video fupi badala ya kuangalia video  ndefu. Na hatakama utamaliza bado lako kwa uangalia video fupi utakua umeangalia video nyingi.

Zima Autoplay

“Autoplay” ni kipengele ambacho hufaya video ziwe zinaendelea kujiplay Moja baada ya nyingine mfulilizo pale zinapoisha. Kipengele hiki ni kizuri lakini ubaya wake ni kwamba ukijisahau unaweza kuta video nyingi sana zimejiplay na kumaliza bado lako la internet. Kama unahitaji kuzima kipengele hiki, nenda kwenye app yako ya Youtube kisha ingia kwenye Profile alafu gusa alama ya Settings na uchague “Autoplay”. Baada ya kufanya hivyo, zima Autoplay kwa kugusa kitue kilicho upende wa kulia.

Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy na usiache kutembelea mara kwa mara The Bestgalaxy ili kusoma vitu vingine.

Unaweza book ndege kwa app ya MPesa?

Moja ya app zinazotupa uwezo wa kufanya miamala ya kifedha katika viganja vyetu ni app ya Mpesa. App hii ni kwaajili ya watumiaji wa Vodacom. Moja ya faida za kutumia app ya Mpesa kwa mtumiaji wa Vodacom ni kwamba hata laini voda ikiwa haipo hewani au imepotea, unakua umebaki na uwezo wa kufanya miamala kwenye app hiyo kwa kutumia internet ambayo haihusiani na laini yako ya voda.  

Kuna baadhi ya watu wamekua wakiuliza juu ya kubook ndege za usafiri kwenye app ya Mpesa na hapa tunaenda kuangalia kuhusu hilo. Kama na wewe unahitaji kujua juu ya hili basi hapa unaweza pata mwanga.

Kubook ndege kwa app ya MPesa

Unaweza book ndege kwa app ya MPesa?

Ndio, inawezekana. Precision Air na Vodacom waliungana na kukuletea uwezo wa kubook ndege kwenye simu yako kupitia app ya Mpesa. Kwa sasa app ya Mpesa inavipengele vingi ikiwemo kipengele cha kubook ndege za usafiri. Precision Air wamekiri kuwa huduma ya kubook ndege kwa app ya Mpesa ni huduma rahisi na haraka kwa watumiaji. Na pia moja ya kitu kizuri kuhusu kubook ndege kupitia app ya Mpesa ni kwamba unapata punguzo la asilimia 20  ambayo inaokoa karibu robo ya pesa yako. Kwaiyo tunaweza sema pia hii ni njia ya kupata tiketi za ndege kwa bei rahisi.

Kipengele cha kubook ndege kwenye app ya MPesa

Ukifungua app ya Mpesa unaweza kiona kipengele cha kubook ndege maeneo ya chini kikiwa kimeandikwa “Book Flights”. Kama umeangalia chini na haujakiona, mbonyeza sehemu ilioandikwa “Services” alafu ukisha fanya hivyo utapelekwa kwenye orodha ya huduma na utaona kipengele kinachoitwa Book Flights kwenye orodha hiyo. Ukifungua kipengele hicho utakutana na ukurasa huu chini kwaajili ya kutafuta na kubook ndege itakayofanikisha safari yako.

Asante kwa muda wako, Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy na usisahau kutembelea kila mara kupata vitu vipya.

App zinazo kupa pesa kwa kufanya kitu kidogo kwako (Unazitumia Kila siku)

Hapa chini The bestgalaxy nimekuandalia orodha ya app chache ambazo zinaweza kupa zawadi ya pesa kwa kufanya jambo flani dogo linaloweza kuwa jepesi kwako.  Lakini kabla ya yote ufahamu kuwa pesa hizi ni ndogo sana na haziwezi kukufanya upate utajiri. Pia fahamu kuwa hizi app ni app ambazo hutoa pesa kama zawadi lakini sio app rasim kwenye upande huo. Hizi ni app rasmi katika upande wa kurahisisha upatikanaji wa huduma au mahitaji kirahisi. Yawezekana unazitumia kila siku. Kuna wakati tutazungumzia kuhusu platform rasimi kwa kutengeneza pesa nyingi.

Tunaweka app kwenye simu zetu kwasababu mbalimbali na moja kati ya sababu ya kuweka baadhi ya app ni kupata huduma au amahitaji kirahisi kwa kutumia simu. Mfano, kuna app ambazo tunaweka kwenye simu ili tuweze kupata huduma za kifedha kihisi kwenye simu zetu na pia  kuna app hurahisisha manunuzi ya vitu kwa kutusogezea bidhaa tunazoweza nunua kwenye simu zetu.

App zinazo kupa pesa kwa kufanya kitu kidogo kwako (Android)

Farasi

Farasi ni moja ya app ambazo zinajihusisha na maswala ya usafili. Kwakutumia app hii unaweza pata usafiri wa kukutoa ulipo mpaka mahali unapotaka kwenda kirahisi. App hii inakutumika na watu wengi tu katika maswala ya usafiri. App hii hua inatoa zawadi kwa watumiaji wake pale wanapoitumia kupata usafiri. Kwasasa unapoanza kuitumia unapata Tsh 3000 mbali na zawadi nyingine utazopata unapotumia. Angalia app kwa KUBONEZA HAPA alafu kama utakua unajiunga usisahau kujaza namba 715233405 kwenye kibox cha referral code.

Branch app

App ya Branch ni app ya mikopo. Ni moja kati ya app nzuri sana katika upande wa app zinazokuwezesha kupata mikopo kwenye simu Tanzania. App hii inaweza kukupa zawadi ya pesa pele unaporudisha pesa kwa mara ya kwanza baada ya kuazima ila kupata zawadi hii ni lazimu uwe umealikwa. BONYEZA HAPA kupata maelezo zaidi ya app hii na zawadi zake

Tigo pesa app

App ya Tigo pesa ni app ambayo hurahisisha zaidi maswala ya kufanya miamala kwa watumiaji wa Tigo. App  hii huwa anatoa kiasi kido cha pesa kama zawadi pale unapomualika rafiki yako. Kama unarafiki ambae anatumia mtandapo wa Tigo lakini ana app, unaweza mualika huyo rafiki alafu akapatiwa zawadi ya pesa kwenye akaunti yako ya Tigo pesa. Kama hauna app ya Tigo pesa, INGIA HAPA kuipakua.

Mwisho ningependa kukukumbusa tu kuwa app hizi sio app rasimi kwa kutengeneza pesa, zinatoa pesa kama zawadi TU.

MIAKA IJAYO (Simulizi ya sauti)

Teknolojia imekua na msaada mkubwa sana katika maisha ya binadamu na imemuwezesha kufanya vitu vingi sana.

Wananadamu wamekua wakiiendeleza Teknolojia Kila siku kiasi kwamba inasemekana inaweza fikia wakati maisha ya binadamu yanaweza kuwa ya ajabu kuliko hivi sasa.

Sikiliza makala hii sehemu ya kwanza mpaka ya mwisho kupata picha ya maisha ya binadamu yanavyoweza kuwa kutokana na technology.

Miaka Ijayo: Sehemu Ya 1
Miaka Ijayo: Sehemu Ya 2
Ifahamu zaidi Simulizi ya MIAKA IJAYO

INAENDELEA…



Simulizi ya “MIAKA IJAYO” kutoka The Bestgalaxy ni simulizi ya sauti inayochunguza jinsi teknolojia inavyoendelea kubadilisha maisha ya binadamu na matarajio ya maisha ya baadaye. Unaposikiliza Simulizi hii, unapelekwa moja kwa moja katika ulimwengu wa baadae kwakua inatoa taswira ya dunia itakavyokua maendeleo ya kiteknolojia yatakapofika mbali. Inahimiza wasikilizaji kufikiria jinsi maisha yatakavyokuwa kutokana na maendeleo haya ya teknolojia.

Simulizi hii ilichapishwa kwa mara ya kwanza katika 2024 na inapatikana kwa mfululizo (series). Unaweza kuisikiliza bure katika tuvuti hii ya The Bestgalaxy.

Jinsi ya kupata simu janja/smartphone bila kuwa na pesa nyingi

Karibu The bestgalaxy na asante sana kwa kuwa hapa muda huu. Katika ukurasa huu tumekuandalia maelezo ya kukufungua ubongo juu ya jinsi ya kumiliki simu janja/smartphone bila kuwa na pesa nyingi. Maelezo haya yamelenga watu ambao hawatumii smartphone/simu janja mpaka sasa wakiamini hawawezi miliki simu hizi za kisasa kwasababu hawana pesa nyingi.

Ukweli ni kwamba usipokua unatumia simu janja kipindi hiki, unakuwa unapitwa na mambo mengi sana ambayo ungeyapata kiganjani kwako. Mfano mzuri ni kutumia app ya Whatsapp; kuna baadhi ya watu katika kazi zao wanashindwa kutuma au kutumiwa video,picha na vitu vingine kwasababu tu hawatumii app ya Whatsapp na sio kwamba hawapendi bali ni simu zao haziwezi.

Kuendelea kutumia hizo simu ndogo ni jambo zuri lakini kuanza kutumia simu janja kunaweza kuwa jambo zuri zaidi hasa ukijua matumizi mazuri na chanya kwako. Kama unataka kuanza kutumia simu janja lakini unauwezo mdogo sana kipesa unaweza fanya yafuatayo kupata simu janja kwa huo huo uwezo ulionao.

Jinsi ya kumiliki simu janja/smartphone bila kuwa na pesa nyingi.

Pata simu za mkopo na anza kulipa kidogo kidogo.

Moja kati ya vitu ambavyo watu hufanya sasaivi ni kuchukua simu za mikopo. Kuna makampuni huwa yanajihusisha na kutoa simu janja za mikopo. Unatakiwa kuwa na kiwango kidogo sana cha pesa ambacho utawapa alafu watakupa simu. Kiasi hicho cha pesa kinafahamika kama “kianzio” na kinaweza kuwa hata chini ya elufu 80 kwa baadhi ya simu(Ukubwa wa kianzio huwa kinategemeana na Thamani ya simu unayokopa). Baada ya kupewa hiyo simu utaanza kuitumia kama kawaida ila utatakiwa kuwa unalipia kiasi kidogo sana cha pesa kila siku mpaka utakapo maliza deni lako. Kiasi cha kulipa kila siku mara nyingi huwa kinakua ni chini ya Tsh 2000. Usipolipia simu hizi hua inajifunga na kukukumbusha kulipia ili uendelee kuitumia. Simu za mikopo ni nzuri sana kama hauna pesa nyingi za kununua simu ila unauhakika wa kupata pesa ndogo ya kulipia kila siku.

Nunua simu za ofa toka kwenye mitandao ya simu.

Mitandao ya simu kama vile Vodacom au Tigo huwa inakua na simu ambazo mtu unaweza zinunua kwa bei rahisi sana ukilinganisha na kuzinunua simu hizo kwenye maduka ya kawaida. Mara nyingi huwa mitandao hii inawaambia wateja wake kuwa watembelee katika maduka yao ili wajipatie simu za ofa. Ukienda katika maduka hayo utapata simu mpya za bei rahisi ambazo huwa zinakua mpaka chini ya 100000. Baada ya kununua simu hizo unaweza pewa bando la internet la kutumia mwaka mzima na pia huwa wanahitaji utumie mtandao wao kama mtando mkuu kwenye simu hizo. Hii ni njia nzuri ya kupata simu kwa bei rahisi hasa kama haupendi kuwa na deni.

Chukua simu zilizo tumika na mtu mwingine.

Muda huu kuna watu wanaziuza simu zao kwasababu mbali mbali na wamekosa wateja. Kuna watu wanauza simu laki 1 na waliinunua laki 3. Kuna watu wamezichoka simu zao wapotayari kuziuza hata chini ya laki. Unaweza pata simu nzuri tu toka kwa watu wanaoziuza simu zao ila utakiwa kuwa makini sana na simu hizi maana zinaweza kukupeleka pabaya. Ni vema ukikutana na mtu anaeuza simu ukamuuliza kwanini anauza, ametumia kwa muda gani inatatizo gani na kufuata taratibu zitakazo kuokoa pindi simu hiyo itakapokua imehuswa na tukio baya.

Ukitaka kupata simu inayouzwa mtaani kwako, tangaza kwa watu kuwa unahitaji simu ili hao watu wakisikia mtu anauzwa simu, wamlete muuzaji kwako. Kama hautaki kununua simu za mtaani kwako, unaweza tumia app kama Jiji au app ya Kupatana ila umakini unahitajika sana.

Namna 3 za kutumia mitandao ya kijamii vizuri (Kaa kijanja!)

Hapa The bestgalaxy, tunakufungua kidogo juu ya namna gani unaweza tumia mitandao ya kijamii vizuri. Mitandao ya kijamii imekua na mchango mkubwa katika mambo mbalimbali kwa binadamu wa sasa. Moja ya vitu vikubwa Teknolojia kupia mitandao ya kijamii imefanya ni kutuweka binaadamu pamoja na kutufanya tuwe na uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii kufanya au kupata vitu mbalimbali kirahisi. Zifuatazo na namna tatu za kutumia mitando ya kijamii vizuri.

Namna 3 za kutumia mitandao ya kijamii vizuri

Kupata burudani

Kama unapenda burudani basi Mitandao ya kijamii ndio sehemu ambayo inaweza ukukupa vitu vingi unavyoweza hitaji kuburudika. mitandao ya kijamii imekusanya vitu vingi sana ambavyo huburudisha na kufanya mtu apunguze msomgo wa mawazo. Ikiwa unataka kutumia mitandao ya kijamii kujiburudisha fanya kuingia kwenye vikundi vya burudani au kuzifuata kurasa zinanzo jihusisha na burudani ili kupata burudani toka kwenye kurasa hizo kirahisi. Pia usiache kutoa maoni na kuonesha umependezwa na vitu vinavyokuburudisha ili mitandao hiyo ya kijamii iwe inakuonesha mambo yatakayokuburudisha zaidi.

kujifunza vitu vipya

Kwenye mitandao ya kijamii unaweza jifunza vitu vipya pia. Kuna vikundi na kurasa ambazo hufundisha mambo mbali mbali kama vile, Ujasiliamali, Afya na Teknolojia. Endapo utakua ni mfutatiliaji mzuri wa vikundi na kurasa za namna hii, unaweza kuwa unajifunza vitu vipya vinavyo weza kuwa na msaada kwenye hata maisha yako. Katika matumizi yako ya mitandao ya kijamii, kwa na muda wa kufuatilia mambo yatakayokujenga na kukufungua ufahamu wa mambo mbalimbali ya msingi katika maisha yako.

kufanya biashara au kuingiza pesa

Ukiachana na kupata burudani na kujifunza vitu vipya, mitandao ya kijamii pia inaweza kutumika kufanya biashara au kuingiza pesa kiujumla. Hii ni mada pana sana maana kunanjia njingi za kufanya hayo na huwa zinatofautiana kutokana na mitandao kuwa tofauti pia. lakini kifupi sana ni kwamba unaweza tumia mitandao ya kijamii kuonesha biashara yako ili kuwafikia watu wengi wanaoweza hitaji huduma yako. Ukiachana na biashara, mitandao ya kijamii mingine huwa inatoa nafasi kwa content creators kuingiza pesa.

Angalizo: kufanya biashara au kuingiza pesa kwenye mitandao kuweza kuwa sio rahisi kama baadhi ya watu wanavyofikilia. Mara nyingi huwa kunahitaji uwekeze Akili, Pesa au Muda ili kufika unapo hitaji. Ukiingia kichwa kichwa unaweza poteza pesa na muda.

Jinsi ya kujua mtu mwingine anaona sms na unavyofanya WhatsApp kisiri

Whatsapp ni mtandao mkubwa ulimwenguni ambao watu huutumia sana katika mawasiliano. Unaweza kuwa ni mtandao wako pendwa katika mawasilioano ndio maana upo hapa… Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy, utajifunza vingi kuhusu mtandao huu.

Whatsapp ni mtandao mzuri kuutuumia katika kuwatumia watu Picha, Video, Audio au ujumbe wa maneno lakini unapofanya hivyo tambua kuwa kunajinsi ambavyo mtu mwingine anaweza kuona vitu vyote hivyo kwenye simu au kifaa chake bila wewe kutambua(kisiri). Kuna njia ambazo hata mtu asiebobea sana katika maswala ya Teknolojia anaweza tumia kuona sms au vitu unavyofanya kwenye Whatsapp. Lakini jambo hili lisikutishe maana hapa chini tunakwenda kukujuza jinsi ya kuangalia kama upo salama na jinsi ya kujilinda pia… Kwaiyo ondoa hofu na endelea kutumia Whatsapp yako kama kawaida.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kujua mtu mwingine anaona sms na vitu unavyofanya WhatsApp kisiri

Whatsapp kwa sasa inakuruhusu mtumiaji wake kuunganisha akaunti yako moja ya Whatsapp kwenye kifaa zaidi ya kimoja. Unaweza fannya akaunti yako moja ya WhatsApp iwe inatumika kwenye simu mbili mpaka 4 na namba ikawa hiyo hiyo moja. Mtu mingine anaweza kuitumia hii kunganisha akauti yako kwenye simu yake au kifaa chake na kuanza kukuchunguza unachofanya bila wewe kujua. Na mtu akitumia ataweza kusoma sms zako, kujibu, kuona na kuchua audio,video na vitu vingine unavyotuma na kutumiwa bila wewe kujua.

Ukitaka kujua kama akaunti yako ya Whatsapp imeunganishwa fanya yafuatayo:

  1. Fungua Whatsapp yako na uguse Vidoti Vitatu
  2. Ukifanya hivyo, Chagua “Linked divices”
  3. Baada ya kufanya hivyo utatupwa kwenye ukurasa ambao ukikuta kuna kifaa chochote kiorodheshwa basi jua whatsapp yako sio salama. Na kama hamna kifaa basi yawezekana upo salama. Unaweza angalia picha hapa chinikuelewa zaidi.

Endapo utakuta akaunti yako ya Whatsapp sio salama(hacked) unaweza gusa kifaa kilicho orodheshwa kwenye kwenye ukurasa huo alafu ukagusa vidoti vitatu itakavyoonekana juu kulia kisha utachagua “Remove device”.

Ili kuhakikisha kuwa WhatsApp yako iko salama kila mara, hakikisha unafanya kuangalia kama akaunti yako ya WhatsApp imeunganishwa mara kwa mara hasa baada ya kumruhusu mtu mwingine aishike simu yako bila uangalizi wako.

Mtu akikublock WhatsApp Fanya hivi kuchati nae BONYEZA HAPA>>>

App za kuangalia Movies/Filamu mtandaoni kwa simu

Katika ulimwengu wa sasa unaweza angalia movie kwenye simu yako ya kiganjani ukiwa popote ulimwenguni. Mara nyingi watu wakitaka kuangalia movie huwa wanatembelea website/tuvuti zinajihusisha na movie/filamu au hutumia app zinazojihusisha na filamu ili kupata huduma ya movies. Kuna baadhi ya tuvuti au app hukuwezesha kupata huduma ya movie bure na nyingine huwa zinakuhitaji ulipie. Huduma za kulipia huwa ni bora zaidi na zinausalama zaidi ukilinganisha na baadhi ya huduma za bure japo zote ni nzuri.

Hapa Tha bestgalaxy leo tunakupa orodha ya app chache kati ya app nyingi unazoweza tumia kuangalia movie kwenye simu yako mtandaoni(online).

App za kuangalia movies online(mtandaoni)

Netflix

Hii ni app ya kampuni ya kimalekni, Netflix ambayo inayotoa huduma ya kuangalia movies/filamu kupitia Internet. Unaweza ingiza kwenye simu yako ya mkononi na kuanza kufurahia filamu kiganjani pako. Unaweza kuangalia filamu nyingi nzuri na maalufu duniani kupitia app hii. Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba app hii ya netflix huwa haitoi huduma bure. Inaweza kukugharimu Tsh 7000 mpaka 23000(Makadilio).

ShowMax

ShowMax ni app inayotoa huduma ya kuangalia movies(filamu), michezo, vipindi vya TV na mambo mengine mengi, kiganjani pako. App hii inaweza kutumika kuangalia movie katika simu ya mkononi lakini sio bure pia. kufurahia huduma za app ya ShowMax utatakiwa kulipia kila mwezi. Kuna filamu nyingi unaweza angalia na pia kama ni mdau wa michezo, unaweza furahia michezo katika app hii. Kifurushi vyake vinaweza kugharimu Tsh 7800 mpaka 46000 kwa mwezi(Makadilio).

Youtube

Youtube ni app ambayo watu hutumia kuangalia video mbalimbali ambazo huwa zinapostiwa kwenye channel. Katika Youtube kuna channel ambazo hutuma filamu na unaweza angalia filamu hizo bure kabisa. Ukiachana na channel za filamu pia kuna kipengele cha Youtube kinachojihusisha na filamu tu(filamu za bure na kununua}. Kipengele hicho cha Youtube hakipatikani katika baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania kwa sasa ila unaweza soma maelezo ya kukuiona hapa chini.

Jinsi ya kuona kipengele cha movies cha YouTube Gusa hapa>>>>

Prime Video

App hii inaitwa “Amazon Prime Video” lakini kwa kifupi unaweza kuiita “Prime Video”. Ni moja ya app zinazoweza kukufanya ufurahie kuangalia movies na hata vipindi vya Tv pia kiganyani pako. Prime Video sio app ya bure lakini inakupa uwanja mpana unaofanana kiasi na netflix hivi katika filamu, unaweza angalia filamu nyingi maaalufu. Maelezo ya kiasi utakachotakiwa kulipa kwa mwezi yaliopo katika tuvuti yao yametaja kiasi kuwa ni USD 5.99 ambayo ni kama Tsh 14000 ivi…

~Viasi vya malipo vilivyo tajwa kwenye makala hii ni makadilio tu.

Whatsapp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa

Whatsapp ni mtandao unaotumiwa na watu wengi sana na umekua na msaada mkubwa kwa watu katika swala la mawasiliano. Katika kutumia mtandao huu unaweza kupambana na changamoto au vitatizo vidogo vidogo, hasa katika app za simu. Changamoto au matatizo huwa hayatokei mara kwa mara lakini hapa The bestgalaxy tumekuandalia orodha ya matatizo au changamoto unazoweza kutananazo katika kutumia whatsapp na maelezo ya jisi ya kutatua. Hii inaweza kuwa msaada pindi mtu unapokumbana na changamoto hizo. Pia usisahau kuungana nasi kwenye WhatsApp namba 0622586399.

Changamoto au Matatizo kwenye kutumia Whatsapp na jinsi ya kutatua

Whatsapp ban

Kama upo banned/umezuiwa kwenye WhatsApp unaweza kuona hivi

Mtandao wa whatsapp unasheria zake ambazo ukikiuka katika kutuumia mtandao huu, wanazuia akaunti yako. Kutumia app za whatsapp zisizo rasimi ni moja ya jambo linaloweza kufanya akaunti yako izuiliwe Whatsapp. Nikizungumzia “Whatsapp zisizo rasmi” namaanisha app kama vile OG Whatsapp, GB Whatsapp au FM whatsapp. Mtandao wa Whatsapp una app rasmi mbili tu. App ya kwanza inaitwa “Whatsapp messenger” na ya pili inaitwa “Whatsapp business”… App yoyote mbali na hizo ni app isio rasmi na inaweza kufanya akaunti yako izuiwe/ifungwe na mtandao wa Whatsapp.

Ukiachana na kutumia app zisizo rasmi, unaweza fungiwa au kuzuiwa akaunti baada ya kufanya mambo mengine yasio faa katika Whatsapp au watu kutoa taarifa kwa Whatsapp kuhusu akaunti yako kujihusisha na jambo flani lisilo ruhusiwa kwenye Whatsapp.

kuna namna mbali za kuzuiwa; unaweza zuiwa na whatsapp kwa muda mfupi au kwa muda mrefu. Ukizuiwa kwa muda mfupi, baada ya muda flani akaunti yako itaondolewa kizuizi na mara nyingi huwa app inaonesha kabisa muda ambao akaunti itaachiliwa. Lakini ikizuiwa kwa muda mrefu huwa inachukua muda mrefu sana kuachiliwa… ukikumbana na kizuizi hiki unashauriwa kufungua akauti nyingine ya whatsapp kwa namba nyingine au kama unahisi wamekuonea, wasiliana nao kupitia Support@whatsapp.com tuma ujumbe wa kuelezea tatizo lako ili wakusaidie.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>

Backup to Google drive

Backup katika whatsapp ni kipengele kinachokuwezesha kutunza sms za whatsapp na vitu vingine kwenye akaunti yako ya google drive ili iwe rahisi kupata au kurudisha sms na vitu hivyo pindi simu yako inapopotea au ukifuta app kwa bahati mbaya. Unaweza fungua whatsapp ukuta ghala tu wahatsapp imekuletea ujumbe unaoziba kioo kizima umeandikwa “Backup to Google drive” na kuna orodha ya chaguzi unazotakiwa kuzichagua pale. Kama hauelewi lolote kuhusu backup basi umaweza changua “Never” tu ili kuokeo muda na kuendelea kuitumia app yako ya Whatsapp.

Whatsapp kumaliza bando

Whatsapp ni moja ya app zisizotumia bando la internet sana ila kama wewe ni mtu unaetumia Whatsapp kwenye upande wa video sana basi app hii inaweza kutumia bando zaidi. Nikisema upande wa video namaanisha kutuma au kupokea video nyingi kwenye vikundi au watu wa kawaida, kutumia video call sana, kuangalia status za watu wengi wilio weka video kwenye status zao. Kuacha au kupunguza mambo hayo kutafanya Whatsapp isile bando lako sana.

Whatsapp inajaza picha na video nisizozitaka kwenye simu

Whatsapp inaweza kuwa inajaza picha na video usizozijua au usizozipenda kwenye simu yako. Kama hili ni tatizo, unaweza tatua tatizo hili kwa kuzima kipengele cha whatsapp kinacho iruhusu app ya whatsapp kuingiza kwenye simu video au picha zinazotumwa kwenye magroup au unazotumiwa. hii itafaya kila video au picha unayotumiwa kutojiingiza kwenye simu yako mpaka utakapo gusa kuidownload.

jinsi ya kufanya hivyo; fungua app yako ya whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” kisha gusa “Storage and Data” alafu baada ya hapo ingia walipo andika “When using mobile data” na uondoe alama ya tiki kwenye vibox vyote au cha video na Photos tu. baada ya kufanya hivyo, bonyeza “Ok” na rudi nyuma kidogo kisha uingie kwenye “When connected on WiFi” alafu uondoe alama ya tiki katika vibox vyote au vibox vya “Photos” na “Videos” tu.

Mtu akikublock WhatsApp Fanya hivi kuchati nae BONYEZA HAPA>>>

Wananiunga kwenye magroup bila taharifa

kama umekua unajikuta umeingizwa kwenye magroup ya Whatsapp na watu usio wajua bila hata taharifa na haupendi hali hiyo basi kunakitu unaweza fanya hapa. Kwenye Whatsapp kunakipengele kinakuruhusu kuzuia mtu ambae hauna namba yake kukuingiza kwenye group. Unaweza kutumia kipengele hiki kuzuia watu ambao hauna namba zao wasikuingize kwenye group lolote bila kukutaharifu.

jinsi ya kufanya hivi; Fungua Whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” kisha gusa “Privacy”. Baada ya hapo, nenda eneo la chini kidogo uingie walipoandika “Groups” kisha chagua “My Contacts” alafu rudi nyumbani na uendelee kutumia app yako.

Nasumbuliwa na simu za watu nisio wajua

Whatsapp pia inakipengele cha kufanya watu watu ambano nambazao hazijawekwa kwenye simu yako wakikupigia usipate usumbufu. Mtu yoyote ambae anakupigia kwenye Whatsapp kwa namba ngeni, simu yako haita, itakua kimya tu bila kukusumbua. Kama ni mtu amabae huwa unapata simu nyingi kwenye Whatsapp toka kwa watu usio wajua na haupendi swala hiilo basi unaweza kutumia kipengele hicho kuondokana na jambo hilo.

Jinsi ya kufanya hivi; Fungua app yako ya Whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” alafu bofya “Privacy”. Baada ya hapo, nenda chini kidogo uingie katika “Call” alafu washa palipo andikwa “Silence unknown callers”.