Category Archives: mengineyo

KAMA WEWE (Simulizi ya Sauti)

Simulizi ya “KAMA WEWE” ya kiswahili ni simulizi inayopatikana katika The bestgalaxy na unaweza sikiliza Bure kabisa. Simulizi hii ni fupi sana lakini imebeba ujumbe mzuri kuhusu maisha na mafanikio katika hayo Maisha.

Simulizi ya Sauti ya kama wewe

Hii ni moja ya simulizi nzuri sana kuisikiliza kama Burudani huku ukijifunza. Sote tuna jua kuwa mtu unapojifunza kupitia hadithi za watu wengine, tunapata mwanga juu ya mbinu walizotumia kukabiliana na changamoto.

WEUSI WEUPE (Simulizi ya Sauti)

Hapa The bestgalaxy tumekuletea simulizi iitwayo “WEUSI WEUPE”. Simulizi ya WEUSI WEUPE ni Simulizi inayoelezea kuhusu viumbe wa ajabu wanaweza kuishi katikati ya binadamu. Ni moja kati ya Fiction stories fupi na nzuri zilizo katika Lugha ya Kiswahili. Unaweza furahia kusikiliza simulizi hii, hapa chini.

Sehemu ya 1
Sehemu ya 2
Sehemu ya 3 (Mwisho)

Kusikiliza hadithi(simulizi) ni muhimu sana katika maisha yetu kwa sababu kunatusaidia kujifunza na kuelewa masomo ya maisha kutoka kwa wengine. Hadithi zinabeba maarifa, busara, na maadili ambayo yanaweza kutusaidia kufanya maamuzi bora na kushinda changamoto mbalimbali. Kwa kusikiliza hadithi, tunapata fursa ya kujifunza kupita maisha ya wengine, kujua mbinu walizotumia kukabiliana na matatizo, kuepuka makosa waliyoyafanya na hata kuburudika tena. Hii inatufanya tuwe na ufahamu mkubwa zaidi wa maisha na kutuwezesha kuboresha mienendo yetu.

Picha za maneno ya hekima na misemo ya maisha

Kama huwa unapenda kusoma au kufuatilia maneno ya busara au maisha, hapa tunajambo lako. Laini kabla hatuja enda moja kwa moja kwenye jambo au lengo letu, ni vema ukatambua kuwa unachokifanya ni kitu kizuri.

Inasemekana kwamba mtu anapopenda kufuatilia vitu flani kwa kuangalia au kusoma, maisha yake yanaweza anza kuendana na mambo anayofuatilia. Japo sio watu wote lakini inasemekana kuwa maisha ya mtu yanaweza badilika kwa kufuatilia mambo flani kwa kusikiliza, kusoma au kuangalia.

Hiyo ndio sababu unaweza ona watu mpaka sasa wanasoma vitabu alafu utawasikia wakisema “Kitabu hiki kimebadilisha maisha yangu”. Ukiachila mbali kusoma, kuna watu huwa wanasikiliza vitu au kuangalia alafu mwisho, maisha yao yanabadilika kutokana hilo jambo alilokua analifuatilia.

Kiufupi vitu unavyofuatilia kwa kusoma, kusikiliza au kuangalia vinaweza kukutuia moyo usikate tamaa, kukuburudiasha ukafurahi na hata kukuelimisha ukabadirika.

Hapa chini tumekuandalia picha chache ambazo zina ujumbe kuhusu maswalia ya maisha kiujumla. Unaweza pitia moja baada ya nyingine kuangalia itajkayokufaa. Kama utataka download pia itakua sio jambo baya kwetu The bestgalaxy, unaweza fanya tu.

Mambo 5 husaidia kukimbiza mafanikio katika miaka 25 mpaka 38 BONYEZA HAPA>>>

Picha za maneno ya hekima na misemo ya maisha

Kwa kumalizia, “picha zenye ujumbe kuhusu maisha” ni njia bora ya kuwasilisha ujumbe muhimu kuhusu maisha kwa ujumla. Picha hizi, zimebeba ujumbe wa kweli kuhusu maisha na ujumbe huu unaweza kuendanda na hali za maisha ya watu wengi.

Unaweza wasambazia marafiki na ndugu unaowapenda picha hizi kupitia WhatsApp, Facebook na mitandao mingine. Ukishindwa kuzidownload, zipige screenshot.

Jinsi ya kum-surprise au kumshangza mpenzi wako bila kutumia Pesa BONYEZA HAPA>>>

Mbinu za Kutimiza Malengo yako ya Mwaka

Wanasema mwaka mpya huja na mambo mapya. Unapoanza mwaka, watu wengi hujiwekea malengo wanayotaka kutimiza ndani ya mwaka huo. Jambo hili huwa linafanywa na watu wengi sana Duniani lakini kufikia malengo hayo mara nyingi inakua sio rahisi kama wanavyotarajia. Katika mambo mapya mwaka mpya unayokujanayo huwa unajumuisha na changamoto mpya zinazoweza kuweka ugumu kutimiza malengo.

Lakini Swala la watu kushindwa kutimiza malengo ya mwaka, lisiwe chanzo cha kushindwa kuipamga au kuendelea kuipambania mipango yako ya mwaka. Jambo hili linatakiwa kuwa ni chanzo cha kuweka umakini katika mipango ya mwaka na kuhakikisha unapambana sana kuiitimiza.

Ni muhimu kuwa na mbinu sahihi za kuhakikisha kwamba malengo yako ya mwaka hayabaki kuwa ndoto tu, bali yanakuwa uhalisia. Katika kurasa hii ya The bestgalaxy, tutajikita kwenye mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kusaidia kutimiza malengo yako ya mwaka. Mbinu hizi zimewekwa hapa ili kukupa mwanga utakaokisaidia katika safari yako ya kufikia mafanikio unayoitaka kuyapata ndani ya mwaka. Kila mbinu itakusaidia kuweka malengo yako kwenye mstari sahihi kama utaitumia kwenye safari yako.

Jinsi ya kuzilinda ndoto zako Maishani zisife BONYEZA HAPA>>>

Mbinu za kutimiza Malengo yako ya Mwaka

Kuandika mipango yako na hatua


Watu wachache sana wanauwezo wa kukamilisha mipango ya muda mrefu bila kuandika. Wengi wasio andika huwa na malengo yanayo badilika badilika mpaka mwaka unaisha hawajui jambo gani walilopanga mwanzo wa mwaka.
Kitendo cha kuandika malengo yako huwa kinasaidia kutosahau kirahisi ulichokusudia kukifanya katika mwaka. Na hata ukisahau unaweza kumbuka picha nzima ya lengo lako kwa kusoma ulipoandika.


Ukishaandika hakikisha unakua na tabia ya kuandika mambo yako kwenye kila hatua unayopiga. Jambo hili litakusaidia kutimiza malengo yako ya Mwaka na hata usipotimiza utakua na mambo ya muhimu sana ulioyaandika kwaajili ya maisha yako ya Mwaka mwingine.

Kiufupi usiache kutumia karamu na karatasi kwenye maisha yako maana kichwa unachotegemea kukutunzia vitu vyako kinaweza kumbana na mambo mengi maishani. Mambo ya mitandao, matatizo ya familia na changamoto nyingine zote zinasubiri kuingia kichwani mwako.

Kuweka malengo chini ya miezi mitatu

Unataka kukifika mwezi wa 12 ndio uanze kufikilia kama mwaka huu umezembea au vipi? Acha hiyo tabia. Anza kujiweka malengo madogo ya miezi mitatu yatakayokua yakuonesha kama umezembea kabla haijafika mwezi wa 12. Yani gawanya lengo lako la mwaka kwenye miezi mitatu mitatu alafu kila mwizi mitatu ikifika unatulia unajiuliza “Nipo ninapotakiwa kuwa au nimezembea? Nifanye nini?”. Kufanya hivi kutakufanya uongeze umakini kabla ya mwaka haujaisha. Kama malengo yako yanaruhusu, unaweza weka hata miezi miwili na ikawa msaada kwako.

Fanya mambo kwa kasi kabla ya muda

Ikiwa unamipango migumu uliopanga na unatamani kuzitimiza, njia nzuri ya kuzitimiza ni kuanza kuipambania kwa kasi mapema. Yani kama kunajambo unatakiwa kulifanya kila siku ndani ya siku Saba(7) ndio ulitimize, Anza siku ya kwanza kwa kufanya kazi ya siku tatu. Kama ni kuweka pesa kiasi flani kila siku, Anza kwa kuweka pesa nyingi zaidi ya hiyo ya siku moja.

Kiufupi ukipata nafasi ya kufanya vitu vya kesho au kesho kutwa katika siku ya Leo, basi fanya Leo maana kesho kunaweza kuwa na changamoto ambayo bado haujaijua.
Kufanya hivi kutafanya uweze kupambana na changamoto katika safari yako bila kuiathiri sana safari uliojiwekea. Na vile vile tabia hii inaweza kukujenga ukawa mtu makini sana kwenye mambo yako.

Ahadi ya kubeba kila changamoto bila kukata tamaa

Usije msingizia mtu tena kuhusu wewe kushindwa kutimiza malengo yako. Jitahidi kubeba kila kitu kigumu utakachokutana nacho bila kutaka tamaa.

Tambua kuwa hakuna mwaka ambao hautakuja na changamoto. Hata waliofanikiwa wamefanikiwa lakini bado wanapambana na changamoto. Adui mkubwa wa malengo ya mwaka ni muda. Uheshimu muda maana ukizembea alafu muda wa mwaka uliojiwekea ukiisha, utakua umepunguza mwaka moja kwenye maisha yako ya Duniani lakini haujafanikiwa kukifanya unachokitaka. Sasa upo tayari kupoteza mwaka mwingine wa Maisha yako kumlaumu mtu au watu?

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kama makala kama hizi zinakua msaada kwako. Usisahau kuwa karibu nasi kwenye mambo mengine na kwenye mitandao ya kijamii pia.

Jinsi ya kutengeneza Logo ya biashara au binafsi BONYEZA HAPA>>>

Badilisha maisha yako kwa kubadilisha vitu hivi vidogo

Sote tunafahamu kuwa Maisha yanaweza kuwa na changamoto nyingi, lakini mara nyingi mabadiliko madogo yanaweza kuleta tofauti kubwa. Kila mmoja wetu anajitahidi kufikia sehemu anayohitaji au mafanikio. Lakini katika safari ya kufikia hayo, changamoto zinaweza kuwa zinaonekana nyingi na kubwa kiasi ambacho watu huona kabisa hawawezi kutimiza wanayo yahitaji. Watu hufikia kwenye hali hii baada ya kufikia hatua ya kuona wapo mbali sana na wanachokihitaji. Yani kunaweza kuwa na umbali mkubwa sana kati ya sehemu mtu anahitaji kuwa na sehemu alipo. Au umbali kati ya mtu anaehitaji kuwa na mtu aliopo.

Makala hii itakupa mwongozo juu ya mambo madogo muhimu ambayo, ukiyabadilisha, yanaweza kubadilisha Maisha yako. Mambo haya ni mambo madogo sana lakini yakibadilishwa yanaweza kukufanya uwe mtu unaetaka kuwa au kukufikisha sehemu unayoitaka kuwa.

Ukiyajua mambo haya, utapata mwanga na njia za kuboresha maisha yako kwa kubadilisha Maisha yako kuwa vile unahitaji.

Jinsi ya kulinda Ndoto zako Maishani zisife BONYEZA HAPA>>>

Badilisha maisha yako kwa kubadilisha vitu hivi vidogo

Mambo unayofuatilia

Mambo tunayofuatilia huwa yana athari kubwa kwenye maisha yako. Mambo haya yanaweza kuwa ni vitu tunavyosikiliza, tunavyoangalia na hata tunavyosoma.


Mfano; kunamtu alianza kufuatilia mpira kwa kuangalia kwenye Tv, kwenye simu alafu akaanza kwenda mpaka uwanjani kushapikia na sasa amepewa nafasi za juu katika timu ya mpira anayoishabikia. Sehemu aliopo ni zao la vitu anavyo fuatilia.


Sasa huo ni mfano tu lakini unaonesha jinsi gani kitendo cha kufuatilia vitu kwa kusoma, kusikia au kuangalia kunaweza ingilia maisha yako.
Kama wewe ni mtu unaependa mafanikio ya jambo flani basi usisahau kufuatilia vitu kuhusu jambo hilo kwenye maisha yako. Yani unaweza jifunza toka kwa watu unapotaka kuwa kama wao, soma au angalia video zinazohusu jambo unalohitaji na hata kusikiliza pia.

Mawazo unayowaza au mtazamo wako

Unawaza nini? Ni kibaya au kizuri? Kama ni kibaya, tafuta njia ya kuanza kuwaza vitu vizuri maana Mawazo yanaweza athiri maisha yako. Anza kwakuto jiwazia vibaya wewe, kisha usiwawazie vibaya watu wengine alafu usiwaze vibaya kuhusu vitu unavyohitaji.


Ukiwaza vibaya kuhusu kitu unachotaka kukifanya au kukipata hautaweza weka nguvu ya kutosha kukipata au kukifanya. Mfano ukitaka kuanza biashara huku unawaza “Biashara hii hailipi. Inaowalipa wote itakua wanatumia dawa, sio bure” basi kunajinsi unaweza kuwa hautumii akili yako sana kwenye kufanikiwa kwenye biashara mbali na kuwaza kupata dawa ya biashara.


Usiwe na mawazo ya kushindwa kwenye kichwa chako. Na ili usiwe na mawazo ya kushindwa mara kwa mara, unatakiwa uwe na mtazamo mzuri juu ya jambo lako alafu amini kuwa upo kujifunza.


Mfano; Ukiwa unataka kufanya biashara anza na “Biashara hii watu wengi haiwalipi lakini nataka kuwa kati ya wale inaowalipa. Ngoja nianze kujifunza kwa kuifanya huku nikiwaangalia waliofanikiwa wanafanya nini”. Kwa kuwaza hayo, unaweza kuwa mmoja wa waliofanikiwa maana utajifunza kitu sahihi wanachokifanya mbali na kuhisi tu kichwani mwako.

Ukiachana na upande huo, epuka mawazo yoyote mabaya maana huwa na athari kwenye maisha halisi. Yaelekeze Mawazo yako kwenye vitu vya msingi unavyovihitaji. Tenga muda wa kutulia na kuwaza kwa upana kuhusu maisha yako na vitu unavyo hitaji.


Tofautisha kati ya kuwaza kuhusu mambo yako na kupata “Msongo wa Mawazo”. Baadhi ya watu hawajipi muda wa kuwaza mambo yako wakiamini kuwa huo ndio msongo wa Mawazo. Waza kuhusu maisha yako, vya kubadilisha vibadilishe na vya kukubaliana navyo, vikubali. Jifunze kutoka kwa muhusika mkuu kwenye simulizi ya SUKARI YA DADA alivyokua akitulia kufikilia maisha yake.

Mambo unayoongelea sana

Unapenda kuongea kuhusu nini? Unapenda kuongea na nani? Mambo hayo yanaweza kuwa na mchango mzuri kwenye maisha yako? Kama hakuna basi kunajinsi unatakiwa kubadilika.
Baada ya kuongea na mtu, akili yako inaweza kuwa imeongeza vitu na huyo mtu anaweza kuwa ameongeza kitu kwenye akili yake pia. Vitu hivyo vinaweza kuwa na athari kwenye maisha yenu wote.


Mfano; Mkikutana mmnao penda vilevi na kuongelea vilevi, mnaweza ondoka mmejuzana kuhusu vilevi msivyovijua alafu kichwani mkawa na mawazo ya kuvijaribu vilevi hivyo. Na mnaweza hata kujaribu kweli mkija kuviona.


Lakini watu wa biashara mkiongelea mambo ya mafanikio ya biashara, mnaweza kuwa mmeondoka na mbinu au taalifa muhimu kuhusu biashara. Na pia mnaweza tumia mambo hayo kwenye harakati za kibiashara.
Unapoongea na watu, pata muda wa kusikiliza, uliza maswali na utoe baadhi ya mambo unayoyajua pia.

Ni vema ukawa na maongezi ya vitu vitakavyo kujenga na ili kumpata mtu anaeongea mambo hayo inabidi uwe na tabia ya kuongea mambo hayo. Hii inaweza kukufungulia hata fulsa mbalimbali zinazoweza badilisha maisha yako.

Huu ndio mwisho wa makala hii. Kiufupi ni vitu huonekana vidogo kwenye maisha ya binadamu lakini ni vitu vyenye matokeo makubwa kwenye maisha yake. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Mambo 5 husaidia kukimbiza mafanikio katika miaka 25 mpaka 38

Katika safari ya maisha hapa Duniani, kuna vipindi ambavyo vinaweza kubadilisha mwelekeo wa mtu mwenye ndoto na malengo makubwa kwenye maisha yake. Kipindi cha umri wa miaka 25 hadi 38 ni moja wapo ya nyakati hizo muhimu sana katika Maisha ya mtu. Katika kipindi hiki, watu wengi wanakuwa na nguvu za ujana, mawazo mapya, na hamasa ya kutimiza malengo. Kipindi hiki mtu anaweza tengeneza maisha anayohitaji kuyaishi. Lakini hiki sio kipindi rahisi, ni kipindi kigumu kinachoweza kukufanya upoteze muelekeo wa Maisha kabisa na kupoteza mambo mengi uliopanga Maishani.

Kunaweza kuwa na mambo mengi sana magumu yanayoendelea kichwani kwa mtu katika kipindi cha miaka 25 mpaka 38 yanayohusu maisha yake. Mambo hayo yanaweza kuwa ni kutokana na taaluma zao, familia, au hata kufuatilia ndoto za muda mrefu ambazo zimekuwa zikisubiri utekelezaji.

Kutokana na ugumu wa kipindi hiki baadhi ya watu hukata tamaa katika kukimbiza mafanikio. Katika makala hii, tunaangalia mambo matano ya kuyaelewa ili kuendelea kukimbiza mafanikio au ndoto katika miaka 25 mpaka 38. Haya mambo matano yanaweza kuwa mwongozo wako wa kukusaidia kupitia changamoto na kufurahia matunda ya juhudi zako.

Fahamu kuhusu AI kuchukua Ajira za watu BONYEZA HAPA>>>

Mambo 5 husaidia kukimbiza mafanikio katika miaka 25 mpaka 38

Kuelewa kipindi ulichopo na game yako

Kipindi cha miaka 25 mpaka 38 ni kipindi ambacho mara nyingi huwa kigumu sana katika Maisha ya mwanadamu. Ni kipindi ambacho mtu anatakiwa kufanya mambo yatakayo tengeneza maisha yake huku akipitia changamoto mbalimbali. Kwaiyo ukiwa kwenye kipindi hiki na unapitia magumu na mawazo mengi juu ya maisha yako, fahamu ni kipindi sahihi mtu kufanya hivyo. Pamoja na yote unayopitia, ielewe game ya maisha yako iko vipi alafu usichoke kuicheza mpaka utakapofika unapotaka. Ninaposema “Ielewe game” namaanisha jielewe wewe ni nani, unakumbana na changamoto gani, utafanya nini ili uwe unapohitaji kisha fanya kinachotakiwa kufanywa kuwa unapotaka kuwa. Kila mtu anacheza game yake duniani na sio rahisi.

Kujisamehe makosa

Katika umri huu unaweza fanya makosa mengi sana na kichwa kinaweza kukuletea Mawazo mengi yanayohusisha neno “Ninge”. Fahamu kuwa unapaswa kujisamehe mambo yote unayohisi ulifanya makosa kwenye maisha yako ili uweze kusonga mbele. Achana na mambo yote ya nyuma Kisha igeukie sehemu unayoenda. Mtu ukiwa unakimbia alafu ukajigonga kidogo na jiwe kwenye mguu lakini ukaendelea kukimbia ukiangalia mbele unaweza fikia sehemu unayoenda. Ila ukiendelea kukimbia huku umegeukia jiwe lililokugonga, unaweza anguka kabisa.

Pesa sio kila kitu ila ni kitu muhimu kuwa nacho

Kama mafanikio kwako yanamaana inayojumuisha pesa elewa kwanza pesa sio kila kitu hapa Duniani lakini ukishaelewa usiache kutafuta pesa. Mambo mengi hapa Duniani yanahitaji pesa na ukiwa hauna pesa hauwezi yapata kirahisi. Pesa usiiweke mbele ila iweke kwenye vitu muhumu maana usipoiweka kwenye vitu muhumu unaweza ukakosa nguvu ya kuitafuta alafu utaanza kusukumwa kukitafuta pesa kwasababu ya shida ulizonazo. Penda kutengeneza pesa hata bila kusukumwa na shida. Jifunze mambo mbalimbali yanayohusiana na kuweka uchumi wako vizuri au kujiimarisha kwenye mambo ya pesa. Usiogope kuchukua Daftari na kuandika mambo yako na mahesabu ya pesa au mipango yako ya uchumi.

Muda haukusubiri na hakuna mzuri zaidi wa kukimbiza mafanikio

Fahamu kuwa kadri dakika zinavyozidi kwenda, watoto wanaenda kuwa vijana, vijana wanaenda kuwa watu wazima na wanaenda kuwa wazee. Kuna siku unaweza amka unaitwa “Babu” au “Bibi” na watoto wadogo. Hiyo sio tatizo ila kujua hili inaweza kuwa ni chanzo cha kupata nguvu ya kuchukua maamuzi ya kupambania mambo yako katika muda huu wa maika 25 mpaka 38. Ni muda mzuri sana wa kupambania maisha unayohitaji maana unakua na nguvu ya kutosha kuliko utakavyokua Mzee. Pamoja na Mambo mengi unayopitia usikate tamaa katika kipindi hiki, tafuta njia yakuwa unapopataka bila kuchoka.

Yaamini Mawazo yako

Watu wanamawazo mengi mazuri kuhusu maisha yao lakini hawayaamini kiasi ambacho wanashindwa kuyafanyia kazi. Kama una Mawazo mazuri juu ya jambo flani muhimu kuhusu maisha yako, sio lazima ukamueleweshe mtu mwingine aelewe ndio ujiamini. Unaweza fanya utafiti wako binafsi, unachukua hatua na ukuwaachia watu matokeo. Amini unachowaza maana wazo moja dogo sana linaweza badilisha maisha na kukuweka unapo hitaji. Lakini wazo hilo linaweza kuwa ujinga ghafla baada ya kulitoa kwa watu wasio sahihi.

Ni hayo tu katika The bestgalaxy na natumaini yanaweza kuwa msaada kwa watu wenye miaka iliotajwa. Hakikisha haukai mbali na sisi kwa mambo mengine zaidi.

Epuka kukopa pesa kama unatabia hizi ndani yako

Kuna uwezekanao wa kuwa na mambo mengi sana yanayoweza kusukuma mtu kukopa pesa za watu wengine au taasisi mbali mbali za kifedha. Na kukupa ni jambo zuri sana maana kuna muda mtu unaweza kukwama kifedha kwa kukumbana na jambo linalohitaji pesa ambayo hauna lakini ukalimudu kupitia mkopo.

Kuna watu hukopa pesa ili kurekebisha mambo yao yalioenda vibaya na kuna hata ambao hukopa ili kulifanikisha jambo lisilo na ulamazima sana. Kukopa kwasababu yoyote ile ni uamuzi mzuri lakini itakua uamuzi mzuri zaidi kama umefanikiwa kwenye jambo lako na kuulipa mkopo wako. Kama haujakamilisha jambo lako au umefanikisha lakini haujafanikiwa kulipa deni la mkopo wako, uamuzi wa kukopa unaweza kuwa mbaya kwako. Na endapo hali yakushindwa kulipa itakua inakuandama kila mara unapokopa ni vema ukaanza kujiweka mbali kidogo na mikopo.

Hapa The bestgalaxy tunakupa tabia ambazo mara nyingi zikiwa ndani yako basi mikopo huwa karibu sana na pia huwa ni ngumu kuilipa. Sio kila mtu mwenye madeni au anaeangukia kwenye madeni anatabia hizi. Ni baadhi ya watu tu ndio huwa na tabia tunazoenda kuzielezea hapa. Niwesema hivyo maana wengine husukumwana na vitu vilivyo nje kabisa na uwezo wao  au sababu myingine mabali na tabisa hizi.

Mambo unayotakiwa kujua kuhusu simu za mkopo BONYEZA HAPA>>>

Epuka kukopa pesa kama unatabia hizi ndani yako

Kushindwa kuzirudisha pesa zako mwenyewe

Kama ni mtu mwenye malengo na huwa unajiwekea pesa kwaajili ya mambo mbalimbali basi kuna muda unaweza kuwa unajikopa mwenyewe. Yani unachukia pesa ulizojiwekea kwaajili ya jambo flani na kuzitumia kwenye jambo lingine tu huku ukiwaza kichwani “Nitazirudisha”. Ikiwa unatabia hiii na unakua na msimamo wa kuzirudisha tena hizo pesa basi unaweza usiteseke sana kulipa hata ukikopa kwa watu wengine. Lakini kama huwa haurudishi pesa hizo na ni tabia yako, kunaweza kuwa na ugumu pia unapokopa kwa wengine. Ni vema ukajaribu kujiimarisha ndani yako kabla ya kukopa kwa wengine. Hakikisha unapambana sana kurudishia pesa sehemu zako za dani ukichukua pesa.

Jinsi ya kupata Mkopo kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Kuhairisha mipango yako ulioianza

Kuna baadhi ya watu huwa na mipango ya biashara na Mambo mengine yanayoweza kuhitaji pesa ili kuingiza pesa. Kukopa kunaweza kuwa ni wazo la haraka kwa mtu mwenye mipango ya namna hii lakini hana mtaji au pesa inayohitajika.
Kukopa sio kitu kibaya kama umekusudia kuanza kupambana kutimiza mpango uliojiwekea. Lakini kama ni mtu unaempenda kuhairisha mipango ulioianza, kukopa kunaweza kuumiza.
Ukichukua Mkopo kwaajili ya mpango flani lakini ukahairisha na kwenda tofauti na mpango huo, kunakua na hatari kubwa ya kupoteza pesa hiyo. Pesa ikiisha bila kufanya kitu kilichosababisha ukope, unaweza jilaumu kuliko ungefanya na kushindwa.
Kama haujaweka vizuri mipango yako au haupo tayari kuipambania kwa asilimia 100, basi usikope pesa kwanza.

Kusahau shinda unapokamata pesa yoyote

Hali yako huwa inakua vipi muda ambao hauna pesa? Na hua inakua vipi ukipata pesa? Kama ukipata pesa yoyote mkononi mwako shida huwa unazisahau, unafanya matumizi na kuacha kabisa kutafuta pesa basi kukopa kunaweza kuwa kubaya kwako. Ukikopa pesa na kuishika mkononi pesa hiyo inabidi iwe kichwani kwako kuwa sio pesa yako na unahitajika kulipa. Hii inaweza kukusaidia kupata mpango wa kuilipa na kuwa makini unapozitumia pesa hizo za mkopo.
Ikiwa utaruhusu pesa hiyo ikusahaulishe shida na kuichukulia ni yako, basi unaweza kuwa ndio mwanzo wa kupuuza deni lako, kuridhika na kuanza ikiutumia pesa.
Usiache kuiona pesa ya Mkopo kuwa ni Mkopo hata ikiwa na mamilioni ya pesa.

Haupendi kudaiwa.

Kutopenda kudaiwa ni jambo zuri sana ila linakua zuri kama utakua na uwezo wa kujikumbusha mwenyewe kulipa pesa kabla haujadaiwa. Mbali na hapo ukiwa haupendi kudaiwa itabidi uanze kuepuka kukopa pesa maana kudaiwa ni lazima na ukichukia au kumfanyia vibaya anaekudai itakua ni kosa kwako tu kivyovyote maana umeshindwa kutimiza makubaliano. Wengine hufikia mpaka hatua ya kupambana kukata kulipa Kwasababu ya kudaiwa vibaya lakini hawajihukumu kwa kuchelewesha pesa muda mrefu kinyume na makubaliano.

Natumaini umesoma na kuelewa makala hii na inaweza kuwa msaada katika Maisha yako kwenye upande wa kukopa. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi.

Mguso Wa Dhahabu (Simulizi ya Sauti)

Karibu katika simulizi fupi ya sauti unayoweza sikiliza hapa The bestgalaxy. Simulizi hii inahusu Mfalme mpenda Dhahabu aliwahi hitaji kuwa mtu mwenye utajili kuliko watu wote Dunia.

“The Bestgalaxy” ni jukwaa maarufu linalotoa simulizi za sauti pia. Simulizi hizi zimeandaliwa kwa umahiri mkubwa. Kupitia The bestgalaxy wasikilizaji wanapata fursa ya kuingia katika dunia za kufikirika na kushuhudia matukio ya kusisimua, ya kichekesho, na hata ya kuhuzunisha. Mbali na kusikiliza, msikilizaji anaweza soma simulizi na kufurahia muda wake. Tunaweza sema The bestgalaxy inafanya iwe rahisi kwa mtu yeyote mwenye simu au vifaa vingine kufurahia burudani bora bila matatizo.

Jinsi ya kulinda Ndoto zako Maishani zisife

Katika maisha, kila mtu ana ndoto ambazo anatarajia kutimiza akiwa hai. Ndoto hizi zinaweza kuwa kuhusu elimu, familia, au mambo mengine . Mara nyingi, safari ya kuelekea kutimiza ndoto inaweza kuwa na changamoto nyingi zinazohitaji uvumilivu na mapambano ili kuzitimiza. Wengi hukata tamaa na kushindwa timiza ndoto zao wakiwa bado waopo hai. Ni muhimu kufahamu mambo ya kufanya ili kulinda ndoto zako na kuhakikisha unafanikiwa kutimiza pamoja na changamoto nyingi utakazopitia njiani.

Kuna muda mtu unapokimbiza ndoto zako unakua na nguvu ya kuendelea kuzifuata. Lakini katika safari hiyo, Kuna muda mtu unaweza fikia hauna nguvu tena ya kuendelea kuikimbiza ndoto kutokana na mambo unayokutana nayo safarini. Inaweza fikia wakati mtu unaamu kupuuza ndoto yako kwa kuamini kuwa “haiwezi kuwa kweli” na kujiona mjinga kwa hatua zote ulizopiga ili kufikia.

Kama unandoto na unahitaji kutimiza, Hapa The bestgalaxy tunaenda kukupa mambo machache muhimu yatakayo ilinda ndoto yako isife kama ndoto za watu wengine.

Mambo matano yanayoweza kukusaidia kufanikiwa Maishani BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kulinda ndoto zako Maishani zisife

Vutiwa na mafanikio ya wengine bila kuchukia


Unapokimbiza ndoto yako unaweza kuwa unaona watu wengi wakitimiza ndoto zao wakati wewe bado. Kushuhudia wengine wakipata unachokosa inaweza kuwa ni jambo gumu kwa moyo. Unaweza jihisi vibaya na hata kuanza kuwachukia waliofanikiwa kwenye jambo ambalo wewe linakuumiza na haufanikiwi.
Ili kuzilinda ndoto zako ni vema ukavutiwa na kufurahia mafanikio ya wengine. Ukifanya hivyo itakua rahisi hata kujifunza mambo ambayo waliofanikiwa wameyafanya ili kufanikiwa. Lakini ukiwachukia utakua huoni la kujifunza na ukionawanaendelea kufanikiwa, utaumia na kupoteza muelekeo wako.

Unayoyapitia yanakuandaa kwa yajayo

Kila magumu unayopitia kwenye kuikimbiza ndoto yako, yanakuandaa kwaajili ya kutimiza ndoto unayoikimbilia. Hivyo haina haja ya kukata tamaa unapopitia magumu. Ukidondoka au kuumizwa, nyanyuka futa machozi, jiulize jambo hilo limekufunza nini kisha songa mbele. Kuna watu wanasema “hauwezi kuiona thamani ya kitu muhimu maishani ulichopata kama haujapata shida kukitafuta”. Vitu vingi vya thamani vinakua na ugumu kuvipata na huo ugumu ndio thamani yake.

Chagua mtazamo mzuri juu ya kifo

Upande wa kifo ni upande ambao watu wachache huuongelea linapokuja swala la kutimiza ndoto maishani. Watu wengi wanapokua wanaona Matukio kuhusu kifo katika mazingira yaliowazunguka, ndoto zao huyeyuka. Huwa wanakosa nguvu ya kuendelea kukimbilia ndoto zao huku moyoni wakijisemea “Duniani Tunapitia”. Hatugusii upande wa kidini ila Kama unandoto na upo hai jambo hilo lisiwe kisingizio cha kutotimiza ndoto yako. Amini vyovyote ila usitupe ndoto zako ukiwa hai maana ndoto zako zinaweza kuwa ni zaidi ya uhai wako. Mungu anaweza kuwa anataka hata kizazi chako kukibadilisha ila ni baada ya wewe kutimiza ndoto. Ndoto ya mtu inaweza kuwa ni kubwa kuliko hata Dunia ndio maana kuna ndoto watu walizikimiza wakajikuta wamebadilisha Dunia.

Kuwa na Sababu kubwa kuliko wewe ya kutimiza ndoto zako

Ili ndoto yako iwe imara na isije kufa kizembe, unganisha ndoto hiyo na mambo makubwa kuliko wewe. Unapofikilia Sababu za kuikimbiza ndoto yako, weka sababu kubwa ya kutimiza ndoto yako na sio vitu vidogo kama gari au nyumba. Fikilia kuhusu maisha ya watoto wako, familia yako na vitu vingine vikubwa na vya muhimu kama hivyo.

Fahamu hakuna binadamu anaona ndoto yako kama uionavyo

Hakuna binadamu anaeona vitu unavyoona au kufikilia. Hivyo hivyo hakuna mtu anaeona ndoto unayoikimbiza kama jinsi unavyoona wewe. Hivyo ukimuona mtu anakucheka, anakukatisha tamaa au kukudharau, usikate tamaa maana hakuna analojua kuhusu wewe na ndoto yako. Ndoto yako inakuhusu wewe hivyo unaiona wewe pekeako alafu watu wengine wanaona matokeo tu. Usihangaike na watu wanaokudharau, kuogopesha au kukukatisha tamaa, wewe endelea kufanywa kinachotakiwa kufanywa ili uwe unapotakiwa kuwa kwenye maisha yako.

Natumaini makala hii itakua msaada katika Maisha yako na huu ndio mwisho lakini The bestgalaxy inavitu vingi kwaajili yako. Endelea kuwa karibu nayo kwa mengine zaidi.

Vichekesho vya kiswahili vunja mbavu




Karibu kwenye makala hii yenye vichekesho vya kusoma vinavyofurahisha! Katika ulimwengu wa hadithi za kuchekesha, tunakuletea mkusanyiko wa visa vya kufurahisha na kukuvunja mbavu. Kupitia makala hii, utaweza kufurahia na kucheka kwa kujitupa katika hadithi fupi zilizojaa kujifunza na kuchekesha pia.

Hadithi hizi za kuchekesha zimeandikwa na watu kwa ustadi na kubuniwa kwa kina ili kukuvutia wewe msomaji lakini hapa the bestgalaxy, zimekusanyawa tu. Hadithi inaweza kuja na mchanganyiko wa utani, kujikosoa, na vituko, kikubwa usiwe serious sana, lengo kubwa ni kucheka kufurahi hivyo jiachie.


Kucheka ni moja ya mambo muhimu katika maisha yetu ya kila siku. Kwanza kabisa, kucheka husaidia mtu kupunguza msongo wa mawazo na hali ya wasiwasi. Unapocheka, mwili wako huzalisha homoni za furaha kama vile endorphins, ambazo husaidia kupunguza mkazo na kuongeza hisia za nzuri.

Vichekesho vya kiswahili vunja mbavu

MUOKOTA MAKOPO:

Tamaa mbaya! Muokota makopo katika uokotaji wake wa makopo akaona chupa ambayo ndani kuna kikaratasi, alipoifungua chupa likatoka jitu la ajabu lisilo onekana na watu wengine. Lilikua likitetemeka na lilimwambia “kijana asante sana kwa kuniokoa omba vitu viwili sasa hivi”. Kijana kwa hofu akaomba pesa za kumiliki magari na majumba ya kifahari. Ghafla fuko liliojaa hela na pete ya dhahabu ya bahati vikadondoka mbele yake. Akaambiwa aseme ombi la pili, akasema “Nibadilishe niwe kivutio ili nipendwe sana nakina dada wazuri” Hapohapo jamaa akageuzwa akawa chipsi yai.!!

MTOTO MDOGO KATULIA NA BABA:

MTOTO: Hivi Baba ivi wewe umezaliwa wapi?
BABA: Nimezaliwa Mbeya
MTOTO: Mama nae kazaliwa Mbeya?
BABA: Hapana, amezaliwa Tanga
MTOTO: Na Mimi jee?
BABA: Dar
MTOTO: Mh Sasa tulikutanaje????
Baba akaangua kicheko

JAMAA BAADA YA KUCHELEWA KAZINI:

Boss: kwa nini umechelewa kazini

Juma: kuna mtu njiani alidondosha 5000 boss

Boss: anha kwahiyo ulikua unamsaidia kuitafuta

Juma: Hapana, bahati nzuri niliikanyaga nikawa nasuri aondoke.

MAWAZO YA VIKOBA:

(Mdada baada ya kufika kwa mpenzi wake akiwa na Mawazo mengi ya vikoba)

Mdada: Baby, naomba shilingi elufu kumi na tano nilipie taxi niliokua nayo.

(Mkaka kaingiza mkono mfukoni kutoa pesa lakini ghafla alipomuangalia mpenzi wake vizuri akashtuka!)

Mkaka: Unasema umekuja na Taxi? Mbona umejisahau umekuja na helmet ya Bodaboda?

Katika ukurasa huu, tuliokuandalia ni hayo tu lakini Kuna vichekesho vingi ndani ya The bestgalaxy ambayo unaweza furahia kuvisoma. Endelea kuwa karibu na sisi kwenye mambo mbalimbali tunayojihusisha nayo.

Stori za vichekesho vya kuvunja mbavu BONYEZA HAPA>>>