Category Archives: Mahusiano

UTAMU WA JUMLA 03 (Simulizi ya Maandishi)


Ujumbe huo niiliona kama fulsa hivi kwasababu ulikua unaeleza kwamba kuna kampuni inaenda kuanzishwa na
kabla ya kuanzishwa Dar inatoa mafunzo kama miezi sita hivi na waliopata mafunzo ndio wataajriiwa. Kulikua kuna
namba zao pale kwenye ujumbe ili kupata maelezo zaidi.
Basi mimi nikachangamkia fulsa bila kulaza damu. Nikawaambia wazazi wangu ingawa walikua wabishi sana
kukubali lakini niliwaelewesha mpaka wakaelewa wakanipa pesa za kutosha kuishi Dar na za kulipia mafunzo
yatakayoendeshwa na kampuni maana ilikua sio bure. Nikafungua akaunti yangu ya binafsi ya benki kisha nikaweka
hizo hela. Baada ya hapo nikaenda Dar, Nikapanga chumba kimoja kwenye nyumba iliokua inavyumba vitatu
ambapo viwili vilikua pia vinawapangaji ambao walipanga kabla yangu. Siku ya kwaanza nilifika katika chumba
nilichopanga nikaweka mabeigi yangu humo nikalala. Siku ya pili nikanunua kitanda na vitu vingine vya muhimu
kwenya maisha ya kusoma ambayo naenda kuyaishi. Siku ya tatu ilikua ni jumatatu nikaanza kwenda kwenye
sehemu ya mafunzo ya hiyo kampuni. Nilikua naenda asubui narudi mchana mida ya saa 8 hivi.
Siku kama tano ivi zilipita bila kuwaona wapangaji wenzangu. Nilikua naona makufuli yamefungwa tu kila siku
lakini baada ya siku kadhaa nilipotoka kwenye mafunzo nilimkuta dada mmoja mweupe mzuri sana anafua nguo
karibu na mlango wa chumba kimoja kwenye hiyo nyumba niliopanga, kilicho tazamana na chumba chamgu. Alikua
amefunga khanga tu kifuani na amejiachia sana mpaka sehemu za juu ya usawa wa magoti zinaonekana. Nikajua
huwenda ni mke wa mpangaji wa chumba hicho maana chumba hicho kilikua kipo wazi muda huo. Nikamsalimia
“Habari Shemeji” akawa kama amesimama kufua hivi alafu akaniangalia vizuri usoni kwa macho yake mazuri alafu
akasema kwa sauti tamu sana “Maambo”. Mh basi me nikamjibu “Fresh tu” nikiwa nataka kufungua mlango kuingia
ndani akaniuliza “Ah wewe ndio umepanga chumba hicho?” nikamwambia “Ndio… wakati nahamia mwenye
nyumba aliniambia kunawapangaji wengine lakini nikawa nashangaa siwaoni”. Nilivyosema hivyo yule dada
akasema “Hahaha mimi nipo hapa nina mwezi sasa ila siku hizi chache nilikua nalala kwa rafiki yangu.
Nikamwambia “Anh na huyo mpangaji mwingine vipi?” akasema “Huyo kasafiri, nilimkuta anakaa hapa pekeake na
mimi nilikua mgeni kwake maaana mimi nina mwezi mmoja tu katika chumba hiki yeye nahisi ni mtu wa muda
kidogo hapa ila kwa sasa kasafiri”,. Nikamuuliza “Kwenye hicho chumba uko peke yako?” akatabasamu alafu
akajibu “Ndio, nipo pekeangu tu hapa hahaha”. Cheko na tabasamu lake tu vilikua kama vimeupasua moyo wangu
kwa furaha na kuamsha vihisia vya mapenzi juu yake.
Nilivyoona hivyo mimi nikasema “Anh sawa, we endelea kufua mimi niingie ndani” ili nikatishe maongezi kidogo
maana alishaanza kunichanganya kichwa na nilikua nimechoka muda huo. Yeye akasema “Sawa, mimi nipo…
ukinihitaji naitwa Salma” mimi hapo nikakumbuka sijamwambia hata jina langu, Nikamwambia jina langu alafu
nikafungua mlango kisha nikaingia ndani. Baada ya kuingia ndani nikatua daftari zangu pale ndani Huku kichwani
nikiwa nawaza “Huyu mwanamke anadawa nini? mbona mzuri alafu nilipokutana nae nimejiskia tofauti? yaani
nakutanane mara yakwanza na ananichanganya hivi… Au kisa sija mzoea? Mh itakua sijamzoea tu, Hana maajabu!
Alafu anaonekana kama mke wa mtu ila ananificha… hawezi ishi pekeake na uzuri huo”.
Sikua na ratiba ya kula muda huo maana huwa nikitoka kwenye mafunzo napitia kula kwanza kwa mama ntilie ndio
nakuja nyumbani. Tangu nifike hapo nilikua sipiki, nilikua nanunua chakula tu maana pesa nilikuanayo ya kutosha
na hata ingeisha nyumbani wangetuma tu. Vitu vikubwa nilivyokua nafanya nikiwa naishi hapo ni kunununua
chakula, kusoma mafunzo na kucheza magemu au kusikiliza muziki kwenye simu yangu.
Salma nae alikua ameongeza kitu katika maisha yangu ya pale maana ilikua kama nimepata rafiki wa kupiganae
stori mara moja moja nikiwa nyumbani. Mara nyigi nilikua nikikosa cha kufanya ndani natoka nje nikimkuta yeye
amekaa, anapika au anafanya kazi nyingine nje, tunapiga stori mpaka basi. Ila kiukweli Salma alikua ananivutia sana
maana alikua mzuri kupita maelezo. Alikua mweupe sana mwenye kifua kilicho simama vema na nzigo wa nyuma wa kutosha. Ukimuangalia usoni macho yeke ni makubwa alafu mazuri sana, tabasamu lake nlilikua linanimaliza na
akicheka ndio kabisa. Kuna muda nikiwa naongea na yeye akili yangu ilikua inahama najikuta namuangalia sehemu
kama kifuani au midooni mpaka najishtukia na yeyepia akiona hivyo alikua anaona viaibu kidogo.
Siku ya kwanza kuongea nae sana ilikua ni baada ya siku kama mbili hivi toka nikutane nae mara ya kwanza. Ilikua ni
mida ya jioni nimetoka kuangalia mpira, nimepitia kula chakula kwa mama ntilie ndipo nikaenda nyubani. Nilipofika
nyumbani nikamkuta amekaa mlangoni pake, mbele yake kuna jiko anapika chakula. Nilimsalimia akaitikia alafu
nikenda ndani nikachukua simu yangu ambayo kwa muda wote ambao sikuepo ilikua kwenye chaji. Baada ya
kuchukua simu nikaanza kucheza gemu nikiwa nipo ndani ya chumba changu lakini baada ya Dakika chache
wakakata umeme kukawa na giza mule ndani. Nikaamua kutoka nje nikakaa kwenye mlango tukawa tunaangaliana
na Salma akiwa amekaa mlangoni kwake na kwa muda huo alikua ameshikilia sahani mkononi anaanza kula.
Nikiwa nakaa pale mlangoni ili nianze kucheza gemu nikamsikia anasema “karibu tule” mimi nikajibu “Ah mimi
nimeshakula, asante”. Tukakaa kama dakika mbili hivi bila kuongea alafu nikasikia akijisemesha “Umeme nao
umetuachia giza bora warudishe mapema kabla simu yangu haijaisha chaji” mimi nikasema “Hahaha mimi simu
yangu inachaji yakutosha, wakate mpaka kesho tu” kusikia hivyo akacheka “Hahahahaha” alafu nikaongeza kusema
“Simu yangu hata nicheze gemu au kusikiliza muziki, kesho itafika ikiwa na chaji”. Nilipogusia muziki nikakuta
ananiambia “Enhe alafu kunanyimbo naomba unirushie kama unazo maana simu yangu mimi ni batani, siwezi pata
nyimbo mpaka niingiziwe”.

Nikamuliza “Unataka nyimbo gani?” akanitajia na kwakua hizo nyimbo nilikua nazo
nikamwambia “lete simu nikurushie”.
Akachukua simu akanyanyuka na kuja kunipa huku akiwa ameshikilia sahani ya chakula mkononi. Mimi
nikachukua simu yake na kuanza kurusha nyimbo huku yeye akiwa hajarudi mlangoni kwake, alikua amesimama
pale karibu yangu akisubiri simu yake maana jambo la kurusha nyimbo si jambo la kuchukua muda mwingi.
Nilipokua nikirusha nyimbo nikakutana na kitatizo kidogo ambacho kilinifanya nichukue muda kidogo kuliko
kawaida. Yeye alivyoona nachelewa, akaamua kukaa na mimi pale mlangoni pangu akawa anaendelea kula huku
ananiangalia ninachokifanya kwenye simu na kuendelea kuongea na mimi. Mh alikua amejisogeza karibu yangu na
tulikua tumegusana kabisa kiasi kwamba nilikua najikuta nahisi vitu tofauti na kitu ninachokifanya muda huo. Mwili
wake mlaini ulileta joto la ajabu mwilini mwangu alipokua karibu yangu maaana alikua ni mwanamke mwenye kila
sifa ya kuamsha hisia kwa mwanaume. Ukiachana na hayo yote, alikua ananukia vizuri.


INAENDELEA…

Zingatia hii: Tafadhali fahamu kuwa hadithi hii ni mali ya mwandishi. Hairuhusiwi kunakili hadithi yote bila idhini. Unaweza kushiriki au kuchukua sehemu ndogo ya hadithi, lakini si kuichukua hadithi kamili. Asante kwa kuheshimu kazi ya mwandishi!

Sababu zinapelekea mtu kutodumu kwenye mahusiano

Kunazisha mahusiano ya mapenzi na mtu, kunaweza kuwa ndio safari ya kuishi mukiwa pamoja mpaka mwisho wenu. Lakini Safari hiyo, watu wengi hutengana na kuivuruga kabisa. Yani kwasasa sio kila mahusiano yanayoanza yanafika mbali, wengi huanzisha mahusiano ambayo hayadumu. Na asilimia kubwa ya mahusiano ambayo hayadumu ni mahusiano yanayohusha watu wenye umri wa 19-29. Watu wanaweza kuingia hata kwenye ndoa lakini Bado wasidumu.

Kwaiyo tatizo la kutodumu kwenye mahusiano ni jambo linalowagusa watu wengi sana. Hapa Duniani kuna wanawake na Wanaume wengi kwasasa wanajiuliza “Kwanini sidumu kwenye mahusiano” bila kupata majibu. Hivyo, ukiwa ni mmoja wa watu woanojiuliza kuhusu hili, basi tambua haukopekeako katika ulimwengu, kuna watu wengi sana.

Mahusiano yako yanaweza kuwa hayadumu kwasababu flani lakini ni gumu moja kwa moja kusema sababu hiyo. Ni ngumu maana kuna sababu nyingi zinazopeleake mtu kutodumu kwenye mahusiano. Hapa chini tumejaribu kuzungumzia sababu chache ili kusaidia mtu yoyote anaepitia tatizo hili kwasababu hizo. Kujua haya kunaweza kukusaidia katika Mahusiano utayopata au ulionayo.

Jinsi ya kupata Mpenzi mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Sababu zinapelekea mtu kutodumu kwenye Mahusiano

Woga wa kuumizwa

Kuna watu waliweka moyo katika Mahusiano ambayo yaliwaumiza sana. Na kama tunavyojua, Ukimpenda mtu sana au ukizama kwenye mahusiano nae sana, basi hata kuumizwa utaumizwa sana. Jambo hili likitokea kwa mtu, linaweza mfanya asidumu kwenye mahusiano mengine mapya tena kwasababu anakua anaogopa kuumizwa. Anaweza jitahidi kupenda lakini akikumbua maumivu au akiona dalili za kuumizwa, anajikuta anajiweka mbali na mahusiano.

Ikiwa unaona unashindwa kudumu kwenye mahusiano kwasababu hii, basi unatakiwa kujipa nafasi ya kupenda tena. Amini kuwa yaliopota yalikuumiza kwakua haukua na mtu sahihi tu kisha mpende anaekupenda. Tengeneza nae malengo bila woga maana woga utakufanya upoteze hata mtu sahihi kwako.

Matarajio makubwa

Asilimia kubwa ya watu (hasa vijana) huwa na matarajio makubwa juu ya wapenzi wao. Baada ya kuona wanachotajia hakipo, wanaona kama hawapendwi au hawana bahati ya kupata mahusiano wanayohitaji. Yani unaweza kuta mwanaume au mwanamke anatamani apate mpenzi mwenyewe maisha kama ya kwenye TV au mambo anayowaza yeye tu kichwani mwake. Akikutana na mtu anaehisi anafanana na huyo anaemuhitaji, basi anategemea kwenye mahusiano au kwenye maisha halisia atakua hivyo hivyo, jambo ambalo ni gumu kutokea.


Mambo mengi unayotarajia kuyapata kwa mpenzi wako au mahusiano yako, unaweza kuyakosa au ukayapa alafu baada ya muda yakapotea. Hivyo, ni vema ukapunguza mambo unayotarajia kwenye mahusiano au kwa mtu unaeingia nae kwenye mahusiano ili udumu nae. Usitege mpenzi wako atakua sahihi Kila wakati, atakua na hela kila wakati, atakua anakuzingatia sana wewe tu kila wakati au kufanya mambo mengine kama hayo.

Kutokutana na mtu sahihi

Wakati mwingine unaweza pitia kwenye hali ya Kila mahusiano kuvunjika na tatizo lisiwe kwako moja kwamoja. Tatizo linaweza kwa ni bado haujakutana na mtu sahihi atakae weza kuunda muhusiano na wewe yasiovunjiaka. Sio Kila mahusiano yanayovunjiaka yanavunjia kwa bahati mbaya, mengine huwa ya Bahati nzuri inayokupeleka kwa mtu atakae kupenda na kukuthamini.
Ili upate mtu sahihi, ni vema ukawa mtu sahihi pia. Kuwa mtu ulietayati kwa mahusiano yasiovunjiaka ili ukikutana na mwanaume au mwanamke atakaekupenda kwa dhati, ujione anabahati kukutana kukupata wewe.

Kukosa uvumilivu

Ukiwafuta wazee waliofanikiwa kuishi wakiwa pamoja kama mke na mume, na kuwaliza Siri ya kudumu wakiwa pamoja, watakuambia mengi ikiwemo “Uvumilivu”.
Ni ngumu kudumu kwenye mahusiano na binadamu mwenzio bila kuwa mvumilivu. Hii ni kwasababu kuna mambo mengi hutokea kwenye mahusiano ili kuharibu mahusiano na hakuna njia ya kuyashinda zaidi ya kuvumilia.

Tabia yako

Tabia yako inaweza kuwa chanzo cha mahusiano yako ya mapenzi kutodumu. Kuna tabia ambazo unaweza kuwa nazo na hauzizingatii lakini ndio hufanya mahusiano yako kuvunjika. Mambo kama Kiburi, dharau, uchafu, uvivu, kutoaminika, kuwa na wapenzi wengi au mambo mengine kama hayo.

Kama ni mpenzi wa simulizi, unaweza fuatilia simulizi ya UTAMU WA JUMLA ili kupata mwanga kwenye tabia zinavyoweza haribu mahusiano. Kwenye sehemu ndogo simulizi hiyo, kuna mtu alikua hadumu kwenye mahusiano kwasababu ya tabia yake.

Ni hayo tu katika ukurasa huu, Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy

Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako

Kuna wakati unaweza tulia na kuamua kumfurahisha mpenzi wako kupitia simu. Kuna mambo mengi sana unaweza mfanyia kupitia hiyo simu na akafurahi. Inaweza kuwa ni unampigia mnaongea mambo mazuri, unamtumia picha na hata ujumbe tu wa maandishi.

Na tena sio lazima muwe mnaishi mkiwa mbali mbali ndio mtumie simu kumfurahisha. Unaweza mfurahisha mpenzi wako kupitia simu hata kama mnaishi nyumba moja. Kumtumia ujumbe mzuri asio utarajia kwenye simu yake ni jambo unaloweza fanya kama utani ila linaweza kufanya afurahi sana hatakama mnaishi pamoja.

The bestgalaxy tumekua mstari wa mbele kuhakikisha hauumizi kichwa sana kwenye mambo ya mahusiano. Katika ukurasa huu, tumekuandalia orodha ya ujumbe mzuri kwa mpenzi wako. Kama unahitaji kumtumia mweza wako ujumbe unaoeleza hisia za upendo ulionao kwake, basi unaweza chukua itayokufaa hapa.

Sms za kumwambia mpenzi wako kuwa unampenda BONYEZA HAPA>>>

Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako (Mwanaume au Mwanamke)

  • Unahisi kuna mwanaume anaependa mwanamke mzuri hivyo amkukose kisa mimi? Au wanawake wengine wanapenda unavyo kuwa na mimi? Hapana, hawapendi kuona tukipendana hao. Kuwa pamoja ni pigo letu kwao.
  • Penzi lako hunisukuma kutaka nikuulize “Nikupatie nini hapa Duniani ufurahi?” lakini nakumbuka siwezi kupa kila kitu. Ila ningekua na wezo, ningekupa tu kama nilivyokupa huu moyo wangu wa pekee uwe nao wewe mpenzi.
  • Sauti tamu ninayopenda kuisikia masikioni mwangu bila kuchoka ni Sauti yako. Mtu pekee ninaempenda bila kuchoka ni wewe. Kitu pekee ninachoweza pokea bila kuchoka ni penzi lako.
  • Waliopita walinifundisha kuwa mapenzi ni maumivu na nisiamini mtu. Wewe umenifundisha maana sahihi ya mapenzi na radha yake hadimu. Umenifanya niwasahau mazima, nimekupenda na nakukuona wewe tu.
  • Umenizamisha kwenye hisia za mapenzi mpaka najiona mimi na wewe tu kwenye Dunia. Na naogopa ila kwasababu nakuamini, naendelea. Nakupenda na naamini popote nikwa na wewe, sijapotea.
  • Nashindwa kuelezea jinsi nakupenda ila hebu fikiria; kila nyota angani ingekua inawakilisha jinsi ninavyokupenda. Unahisi ningekua nakupenda kiasi gani?
  • Niende nikaombe nini kwa jirani? Nikaombe Maji ili nikate kiu? Hapana, wewe tayari umeiweza kiu yangu. Siwezi hata kuiomba Asali kwao maana natosheka na vitamu unavyonipa malkia wangu.
  • Kuna muda huwa nakosa kabisa furaha na Sababu za kufurahia maisha yangu. Ila nikikumbuka nina wewe maishani, furaha humwagika kama maji ya mvua moyoni.
  • Usijiuze nakupendea nini mpenzi wangu. Utauchosha bongo wako Bure. Ninasababu nyingi sana za kukupenda wewe. Na hata ukiziondoa, bado nahisi Moyo wangu uliumbwa kukupenda wewe.
  • Kabla ya kukutana na wewe, nilitamani kukutana na mtu kama wewe nimpende maishani. Sasa nimekupata, nakupenda na kwenye maisha umekua kama Nuru gizani.
  • Najua kunamuda tunagombana au hatuelewani. Lakini tambua sijutii kukupata Ila najutia kuwa nawe mapema hapa Duniani. Moyo wangu unakupenda na umejaa mpaka akilini.

Katika orodha hii, Kuna ujumbe unaoweza kutuma kwa mwanamke na hata Mwanaume pia. Kwaiyo hii ni kwa watu wa jinsi a zote. Kikubwa hakikisha unatambua muda amambao utakua mzuri kwa mpenzi wako kupokea. Angalia na maana sahihi ya ujumbe ili mpenzi wako aelewe unacho maanisha unapomtumia.

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy

Mambo ya kufanya kwa Mpenzi asieonesha kukupenda katika Mahusiano

Mahusiano mara nyingi huanza kwa msukumo wa hisia kali. Yani kila mmoja anajihisi kuwa na haja kubwa ya mwenzake. Kila jambo linaonekana kuwa jipya na lenye kuvutia, Wapenzi wote wanajitahidi kwa hali na mali kuhakikisha wanampendeza au kumfurahisha mwingine. Lakini, kadri muda unavyoenda, hali hii inaweza kubadilika, na baadhi ya watu huanza kuhisi kama hakuna mapenzi ya dhati kama awali.

Hii ni hali inawakumba watu wengi, hata walio kwenye ndoa za muda mrefu. Kuna wakati mtu anajikuta anaendelea kutoa upendo, lakini mwenzake haonyeshi kujali au kuonyesha hisia zozote za kurudisha upendo huo. Hali kama hii inaweza kumkatisha tamaa, kuleta Mawazo na kumfanya mtu ahisi vibaya, hasa pale anapokuwa amejitolea sana kwa ajili ya uhusiano hayo.

Katika Hali hii, kabla ya kuchukua hatua yoyote, ni muhimu kujua kwamba yapo mambo ambayo unaweza kufanya ili kuboresha hali hii na kufufua tena mapenzi kwenye uhusiano wenu. Katika makala hii, tutazungumzia mambo unayoweza kufanya ili kurekebisha hali hii ikiwa imekutokea ghafla kwenye mahusiano yako.

Ujumbe wa Mapenzi kwa umpendae BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kufanya kwa Mpenzi asieonesha kukupenda katika Mahusiano

Kuwa mpya au tofauti kwake



Kuna wakati mpenzi wako anaweza kuwa ameacha kukuzingatia kwasababu amekuzoea. Yani anaweza kuwa anaona vitu unavyofanya kwake au ukiwa nae ni vitu ambayo vinajitudia mpaka anakuona hauna cha kushangaza. Hapa nazungumzia vitu kama, jinsi unavyoongea nae, muda unaangeanae, zawadi zako, sehemu mnazoenda, ahadi unazoahidi na mambo mengine kama hayo.
Ikiwa tatizo ni ili, basi utatakiwa kuwa mtu mpya kidogo kwake. Yapindue mambo ambayo unamfanyia au mnafanya kwa pamoja. Na usiyapindue kwa ubaya, fanya baadhi ya mambo mzuri kwa kumjali lakini iwe ni tofauti na alivyozoea. Kufanya hivyo kwa mpenzi asieonesha kukupenda katika Mahusiano kunaweza mfanya aanze kukuzingatia kwa upendo.

Tafuta tatizo upande wako na wake



Kama kutokukuzingatia kwake kunaonekana kuwa ni jambo zaidi ya kukuzoea, basi jaribu kutafuta sababu ya hali hiyo. Kwanza kabisa jaribu kufikilia kama wewe ndie tatizo maana kuna mambo unaweza kuwa umemfanyia ndio maana hakuzingatii. Fanya kufikilia vitu alivyowahi kukuonya au ambayo unajua kabisa viko upande wako lakini yeye humchukiza. Ukipata tatizo upande wako, fanya kuliweka sawa.
Ukikuta upande wako hakuna sababu yoyote ya yeye kuwa hivyo, fanya kuhamia upande wake sasa. Jaribu kufikilia na kudadisi ni kitu gani kimembadilisha hivyo. Tafuta sababu ili ujue uitaweka vipi hali vizuri.

Ukifanikiwa kupata tatizo linalomfanya mpenzi wako asikuoneshe kukupenda, jaribu kuliweka sawa ikiwezekana hata kwa kumshirikisha.

Kaeni muongelee hilo tatizo kwa pamoja



Njia rahisi ya kumaliza matatizo ni hii maana inafanya wote mufunguke yanayofanya musiwe sawa na kujadili mfanye nini ili hali iwe sawa. Fanya kukaa na mpenzi wako muongelee tatizo ambalo unaliona kwenye mahusiano yenu. Hakikisha unamtafuta mida mizuri ya kuongelea mambo haya ili aweze kufungua yaliomo moyoni kwake.

Usipokaanae muda sahihi, anaweza kukuficha yaliopo moyoni mwake. Kama ni mume au mke wako, unaweza ongea nae muda wa kulala au mkiwa metulia baada ya kucheza michezo yenu. Kama ni wapenzi tu, unaweza tafuta muda wenu mzuri wenye utulivu kama mida hiyo nilioiieleza. Usitumie simu kuongea, kutaneni ana kwa ana muongee ndio mtaweza elewana vizuri.


Mwisho; Ningependa kukukumbusha kuwa usisahau thamani yako. Kuna mambo mengi ya kuvunja moyo katika Mahusiano yanaweza kukuvunja moyo ila usisahau kuwa kuitambua thamani ni muhumu. Ikiwa unaona dalili za kuwa mpenzi wako hataki tena mahusiano na wewe, ni sawa kuheshimu maamuzi yake. Unaweza muacha alafu ukamtafuta mtu mwingine anaeijua thamani yako.

UTAMU WA JUMLA 02 (Simulizi ya Maandishi)


Wakati nakusanya nguo ghafla mlango ukagongwa “Ngo ngo ngo” na sauti ya Jimmy akisema “Oi wewe”.
Niligundua ni Jimmy nikasema “Oya… Umerudi sasa haha” akawa anasukuma malango huku anasema “Ahaha
nimekuja na shemeji yako huyu” huku akimruhusu mtu aingie. Mimi nikatupa macho kuangalia mtu anaeingia ni
nani, nikakuta ni Zuwena amevaa nguo nyeusi fupi alafu inaangaza kiasi ambacho baadhi ya sehemu zake za mwili
zinaonekana na Jimmy alikua anamshika kiuno alipokua akiingia ndani. Nilipomuona Moyo wangu ulidunda kwa
mshtuko “Nduh” na nikahisi kama kuishuwiwa nguvu hivi…
Nikaona bora nijikaze tu ila nisiwe na maneno mengi hapo maana nawezajikuta nimesema kitu kibaya. Nakumbuka
nilimsalimia Zuu kama ndio mara ya kwanza nakutana nae hapo. Na yeye alikua ananisalimia kama sijawahi ongea
nae kwa ukaribu. Baada ya kuwasalimia nikatoka nje na nguo nilizokusanya ili kuzifua na kuwaacha mule ndani.
Nilivyotoka tu, Jimmy aliufunga mlango ili mtu yoyote asiingie mule ndani na mimi sikua na hofu juu ya hilo
maana vitu vyote ambavyo vilikua vinahitajika ili nifue vilikua vinapatikana nje.
Nilichukua ndoo nikachota maji, nikavuta kiti pembeni ya chumba nilichukua nakaa alafu nikaanza kufua. Kichwa
changu muda huo kilikua hakipo sawa kabisa maana nilikua naona rafiki yangu Jimmy anaenda kula tunda la mtu
ninaempenda na kwakua sikumwambia basi nikaona acha niendelee kuumia moyoni tu kimya kimya huku nikifua
japo bado kichwani nilikua najiuliza “Amempataje huyu kiiumbe? Mbona sijawahi waona wakiwa karibu? Dah yani
Zuu nae inaonekana hanikubali kabisa maana aliponiona hata hakushtuka.ila namtamani sana huyu mwanamke”.
Wakati naendelea kufua ghafla nikaanza kusikia visauti toka ndani kupitia kidilisha kilichokua karibu na nilipokua
nafua. Mara ya kwanza nilikua nimevipuuza visauti hivyo nikawa nahisi ni Jimmy na Zuu wanaongea kawaida
kimahaba lakini baadae nikaanza kusikia sauti inaongezeka na inakua kama Zuu anabishana na Jimmy mule ndani.
Hali hiyo ilinifanya niache kufua nisogee zaidi kwenye dilisha nijue wanabishana nini humo ndani badala ya kuanza
mambo yao. Nilipotega sikio nikasikia Zuu akiwa na sauti kama amechukia hivi akisema “Usiniguse kwanza, Mimi
nataka uniambie ukweli kwanza… umesema hapa ni kwa nani?” Jimmy akawa anajibu “Kama nilivyokwambia
Zuwena, kwa rafiki yangu hapa… Kwanini unakua mgumu kunielewa” Zuu akajibu “We endelea kunidanganya tu, si
umeniona mimi mtoto mdogo? hiyo michezo naijua, usiniguse”. Nilimsikia Jimmy akisema “Tatizo huniamini…
Kama nilivyokwambia, mimi nakaa kule ila funguo kuna mtu ameondoka nayo ndio maana nimekuja kwa rafiki
yangu huku. Hata kodi ya hapa huwa nalipa mimi, huyo jamaa alietoka hapo nje huwa ni kama namsaidia tu maana
hayupo vizuri kipesa. Alafu nilishakwambia habari ya huyo jamaa hapo… Sasa kinachokufanya ubadilike sijui ni kitu
gani”. Nikakuta Zuu anamuuliza Jimmy “Yani umeniona mimi mjinga sana bora hata ungekua mkweli tu… Mimi
naona humu ndani kuna nguo zako ninazo zijua na hata viatu alafu bado unasema hapa sio pako. Sawa, kwasasa
naomba uniache niondoke maana nimekuchoka”. Mimi hadi hapo nikaanza kupata picha kidogo ya kinachoendelea
humondani. Kwa maongezi yale nilio yasikia nikajua tu huenda Jimmy hadi amemfikisha hapo huyo mwanamke ni
baada ya kumdanganya sana na muda huo uongo wake uligundulika na jambo hilo lilpelekea mpaka huyo
mwanamke kutaka kutoka humo ndani.
Basi nikatoka pale dilishani nikarudi nilipokua nafua ili kama wanatoka wasijenikuta pale na kugundua nilikua
nawasikiliza. Baada ya dakika kama tano hivi nikasikia mlango unafunguliwa, wakatoka kama wapo vizuri tu japo
Zuu alikua na sura inayoonesha amekasirika na Jimmy alikua ni kama anaaibu kiasi kutokana na kilicho mtokea.
Nakumbuka waliniaga pale alafu wakawa wanaondoka na kuniacha nikwa nafua. Kiukweli siku walivyokua
wanaondoka waliniacha nikiwa na furaha sana moyoni kwangu kutokana na kutofanikiwa kufanya mambo yao
humo ndani. Nilikua napenda sana Jimmy afanikiwe kwenye mipango yake kwasababu ni rafiki yangu lakini kwenye
Suala la kumkamata Zuu, sikulipenda maana mimi pia nilikua nampenda sana Zuu japo sikumwambia.
Nilipokua nikiendelea kufua na kufurahia tukio lililotokea, gafla nikaanza kufikilia tena yale maneno nilioyasikia
dilishani na kuanza kuwaza “Inamana Jimmy amemwambia Zuu mambo mengi kuhusu mimi alafu mimi sijui… Dah
na najua hawezi kuongea ukweli au jambo la kunisifu, lazima alikua ananiponda ili aonekane ni mtu wa juu”. Na kweli baada ya tukio hilo chuoni kulikua na watu wengi wajua juu ya Jimmy na Zuu. Zuu alimchafua sana jimmy
hapo chuoni kwa kuwaambia watu vitu alivyokua anaambiwa na Jimmy. Kulikua na maneno mengi ya Jimmy
kujigamba kwa Zuu ambayo yalienea kwa watu pale chuoni ila moja ya vitu nilivyosikia mwenyewe Jimmy
alimwambia Zuu ni kwamba ananilipia kodi tu lakini hakai na mimi. Jambo hili liliniumiza sana maana nilihisi
huenda ndio chanzo cha Zuwena kunipuuza nilipokua namtafuta. Lakini kwakua Jimmy alikua ni rafiki yangu,
nilipuuzia na tukaendelea kuwa pamoja hapo chuo.
Pamoja na yote yaliotokea, sikuwahi mtafuta tena Zuu. Nilikua nimetulia na mpenzi wangu sara na alikua anasema
ananipenda kweli. Niliweka moyo wangu wote hapo huku nikiwa na soma sana lakini nilivyozama sana katika penzi
lake, nikakuta Sara anaanza kunibadilikia tena. Ghafla tu alianza tabia ya kutonitafuta mpaka nimtafute na hata
nikimtafuta anaweza sema atanitafuta lakini hafanyi hivyo. Hali hii iliniumiza sana maana nilikua najua kwamba ni
dalili ya kuwa Sara amepata mwanaume mwingine. Nilichanganyikiwa sana kipindi hicho mpaka masomo nilikua
naona hayaeleweki. Hakuniambia kwamba tuachane ila tabia yake ilionesha kuwa tayari ameishaniacha ila ni mmi
tu ndio sijui. Nilifuatilia nikakuta kumbe kapata Mwanaume mfanyakazi na anamiliki mpaka gari. Niliwahi shuhudia
kwa macho yangu Sara akiingia kwenye gari baada ya kutoka chuoni. Niliumia sana na nikaamua kukubaliana na
uhalisia kuwa nimeachwa ila moyoni nikajisemea “Siku nikipata ajira na kuwa na hela nitawakamata sana
wanawake… yani nitawala sana. Ntanunua gari na ntakuwa na wanawake kila kona… Siwezi mpa moyo wangu
mwanamke auchezee kama hivi, ntakuwa nao wengi ili niwachezee wao… Pesa nyingine nitakua natumia na
marafiki tu maana ni bora marafiki kuliko kuwa na mpenzi”.



Basi siku zilisonga hapo chuo mpaka tukamaliza na kurudi nyumbani Tabora. Nakumbuka mimi na Jimmy tulirudi
nyumbani na tulikua tunaishi kwa wazazi wetu. Kwetu na kwakina Jimmy ni karibu sana. Kwao ni nyumba ya tatu
kutoka kwetu. Tulivyokua wadogo hatukua pamoja, familia yake ilihamia hapo kipindi nipo sekondari na yeye
alikua sekondari na tulipokutana tukawa marafiki mpaka tulipoenda chuo pamoja na kurudi pamoja. Tulivyorudi
tulikua mabishoo sana na tunapendeza juu mpaka chini kila muda na masimu yetu makubwa ya kupalasa.
Baada ya miezi kadhaa ishu ya chuo tukawa tumeimaliza kabisa tukawa tunamawazo ya kupata Ajira kichwani
mwetu kutokana na vyeti tulivyopata. Lakini tulianza kuona kama neno “ajira” linaongelewa kwenye ma TV alafu
hatuzioni mtaani na hata wakiziongelea kwenye TV mara nyingi wanasema “changamoto ya upungufu wa ajira”.
Jambo hili lilinifanya nijiulize “Inamaana pamoja nakuwa na vyeti Ajira naweza kupata au nisipate? Duh!”. Siku moja
nikakuta tu ghafla jamaa yangu Jimmy kasafili. Na hakuniambia kwamba anasafiri mpaka nilipomcheki kwenye simu
“Wewe uko wapi mwanangu, mbona haujaonekana leo” ndio akaniambia amerudi Dar. Mimi nikamuliza “Mbona
hukuniambia rafiki yangu?” akasema “Hahaha ilikua ni ghafla mzee, Nitakucheki tutaongea vizuri”. Mh Mimi
nikajua atanicheki kweli lakini haikua hivyo, siku zilizidi kusongea tu hanicheki na hata nikimcheki ananiambia
“ntakucheki”. Baadae nikakata tamaa kabisa ya kumtafuta maana nilikua najua nimuongo hivyo ukimsikiliza
unapoteza muda nikakata mawasiliano nae. Kiukweli baada ya Jimmy kuniacha kule Tabora nilianza kuwa na
mtizamo tofauti kidogo juu ya Marafiki, nilikua kama nimegundua kuwa marafiki hawajashikana na maisha yangu,
wanaweza ondoka muda wowote.
Nikaendelea kukaa pale nyumbani bila mafanikio ya kupata ajira na wazazi nilikua naona hawaniwazi tena kwenye
mambo ya pesa, wao walikua wapo tayari walipie mamilioni sehemu nisome au nipate kazi kuliko kunipa mimi pesa
ya hivi hivi tu. Kadri siku zilivyo zidi kusonga nilianza kuchakaa kimuonekano kutokana na kukosa hela. Wakati
nakuja kutoka chuo nilikua napendeza kiasi kwamba nikikutana na mtu ananiuliza “Hiyo sendo uliovaa mguuni
shingapi?” nikimwambia bei anasifia “Dah nzuri sana hiyo sendo!” lakini mambo yalibadilika kiasi kwamba
nakutana na mtu ananiangalia juu mpaka chini alafu anauliza “Hiyo gundi ni supagruu?” namuuliza “Wapi? hapa
kwenye sendo?” Anajibu ” ndio, hapo mguuni” namwambia “Ndio ni yenyewe” ananijibu “Gundi nzuri sana
hiyo!”. Kiukweli nilichakaa sana na hali hiyo ilinifanya niwe na kiu ya kufanya chochote nipate ajira na ilikua kama
bahati hivi nilikutana na tangazo ambalo liliingia kwenye simu yangu kama ujumbe. Ujumbe huo niiliona kama fulsa
hivi kwasababu ulikua unaeleza kwamba kuna kampuni inaenda kuanzishwa na kabla ya kuanzishwa Dar inatoa
mafunzo kama miezi sita hivi na waliopata mafunzo ndio wataajiriwa. Kulikua kuna namba zao pale kwenye ujumbe
ili kupata maelezo zaidi…

INAENDELEA….

Hii ni simulizi ya UTAMU WA JUMLA ilio katika maandishi. Ina uhusiano kidogo na Simulizi ya SUKARI YA DADA na MZIGO WA WAKUBWA. Inapatikana katika Sauti pia. Inavipande 11.

KUMBUKA: Hairuhusiwi kusomwa na mtu mwenye umri chini ya miaka 18.

Ukihitaji simulizi zote 3, Njoo WhatsApp

Kabla ya kumuacha Mpenzi kwa kukusaliti fikiria Mambo haya kwanza

Kila mtu anatamani kuwa na mpenzi mwaminifu na anayejali, kwani uaminifu ndio msingi wa mahusiano yenye furaha na utulivu. Si mwanaume wala mwanamke, wote wanapenda huwa na mahusiano na mtu asiewasaliti. Hisia za upendo na kuaminiana, hujenga mahusiano imara ambayo hutoa faraja na usalama wa moyo kwa wapenzi wote wawili. Hakuna anayependa kuwa na mashaka au wasiwasi kuhusu tabia za mwenzi wake, hasa linapokuja suala la kuwa na mpenzi mwingine. Hii ndio maana mwanzo wa mahusiano wapenzi husisitiza sana kutosalitiana kwa kuambiana maneno kama “Nitakupenda milele… Sina mwingine zaidi yako… Siwezi kukusaliti”.

Lakini wakati mwingine, hali ya kusalitiwa hujitokeza, na hii inaweza kuwa ngumu sana kwa aliesalitiwa kukubaliana nayo. Watu wengi hujawa na maumivu makubwa wanapogundua kwamba wamechezewa au kudanganywa na mtu alieshika furaha ya moyo wao. Hupata hisia zinazovunja moyo na kuumiza, na mara nyingi hisia hizi humfanya mtu kujiuliza kama anapaswa kuendelea na uhusiano huo au kuachana nao kabisa.

Uamuzi wa kumwacha mpenzi kwa sababu ya usaliti ni jambo zito maana ni kuharibu kabisa uhusiano uliokuwepo bila kujali mmetoka wapi. Ni muhimu kufikiria kwa makini kabla ya kuchukua hatua yoyote ili kuhakikisha kuwa unafanya uamuzi sahihi maana sio kila kusalitiwa kunatakiwa kuwa mwisho wa Mahusiano. Katika makala hii, tutaangazia mambo ya kujiuliza au kufikiria kabla ya kuchukua uamuzi wa mwisho.

Jinsi ya kujua kama mpenzi ulienae anakupotezea Muda tu BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kufikiria kabla ya kumuacha mpenzi kwa kukusaliti

Ni kweli?

Kuna mambo au matukio yanaweza kukufanya uamini kuwa mpenzi wako anakusaliti au amekusaliti lakini ikawa sio kweli. Ni ngumu kuamini kuwa mpenzi wako hajakusaliti wakati umeyaona mazingira ya kukusaliti. Watu wengine huwa Wanaamini kuwa wamesalitiwa hata kwa kuambiwa tu au kusikia maneno ya watu. Unachotakiwa kujua ni kwamba kuna wakati inaweza kuwa sio kweli.


Ni vema kabla ya kufanya uamuzi wa kumuacha kipenzi cha Roho yako, ukathibitisha ni kweli amekusaliti au hajakusaliti. Usije muacha mpenzi wako sahihi kwa vitu vya kuhisi au kusikia. Ukiona mambo yanakuchanganya, unaweza kukaa nae mukaongea kuhusu unachohisi au ulioyasikia kisha ukaangalia anayachukuliaje hayo mambo na yeye.

Chazo ni wewe, yeye au mtu mwingine?

Wengi likitokea jambo la kusalitiwa huwa tunaona mbaya ni aliesaliti lakini kuna wakati mtu mbaya unaweza kuwa ni wewe uliesalitiwa au akawa mtu mwingine tu mbali na nyie.
Ukiwa na uwezo au moyo mkubwa, unaweza jiuliza nini chanzo cha usaliti uliofanyiwa. Kuna watu wengi tu huwa wanasalitiana kwenye mahusiano lakini baadae wanagundua nini chanzo, wanarekebisha walipokosea alafu wanaendelea na mahusiano. Unaweza gundua kuwa wewe ndio umesababisha yeye kufanya hivyo au Kuna mtu mwingine ameamua kuwavuruga.


Jambo hili limejitokeza kwenye simulizi fupi iitwayo “SIRI NA SHEMEJI” na inaweza kuwa vizuri sana kama utafuatilia simulizi hii.

Bado anakupenda na anajutia kukusaliti?

Kuna watu wanasema “Usimwamini au kuendelea na mwanamke au mwanaume aliekusaliti”. Lakini kiukweli kwenye jamii zetu mambo ya kusalitiwa hutokea kwasababu mbalimbali na watu husameheana na kuendelea kujenga mahusiano yao kama hakuna kilichotokea.
Kabla ya kumuacha au kumsaheme mpenzi aliekusaliti ni vema ukajiuliza “Bado anakupenda?” na pia usisahau kujiuliza kuwa “Anajutia kukusaliti?”. Kama unaona kabisa mtu bado anakupenda sana na hataki kukupeteza kwenye maisha yake, kumsamehe unaweza kuwa uamuzi mzuri. Ila inabindi ujilidhishe kabisa ili usijejutia uamuzi wa kumsaheme.

Pia Jambo limejitokeza kwenye simu fupi iitwayo “SIRI NA SHEMEJI” na inaweza kuwa vizuri sana kama utafuatilia simu hii ili kuelewa zaidi.

Unaweza kusahau na kumpenda bila kujali?

Baada ya mpenzi wako kukusaliti, angalia moyo wako kama unaweza sahau yote na kuendelea kumpenda. Kama unaona kabisa hauwezi kumsamehe au kusahau alichofanya, ni vema ukamuacha tu maana ulionayo moyoni yanaweza pelekea kufanya jambo baya kwake kama kisasi.

Kwaiyo ni vema ukajipima kwanza kama unaweza sahau yote na kuendelea kupendana nae kama hakufanya kitu kibaya kwako. Yani kama umemsaheme, usije waza mabaya yake tena.

Hautakua wakwanza kufanya hivo, watu wengi hufanya kwa wapenzi wao, waume zao au mwake zao. Lakini ukiona hauwezi, jiweke mbali nae maana kuna siku moyo unaweza kukusukuma kumfanyia mabaya.

Ni hayo tu katika ukurasa huu wa The bestgalaxy, lakini kama ni mtu anaependa kuelewa zaidi, unaweza soma Simulizi ya “SIRI NA SHEMEJI” ili kuburudika huku ukiongeza uelewa kuhusu swala hili.

Mambo ya kufanya Mpenzi akiwa hakupigii simu au kukutafuta

Simu imekuwa sehemu muhimu sana katika mahusiano ya siku hizi. Kupitia simu, wapenzi wanaweza kuwasiliana kwa urahisi, kubadilishana mawazo, na kueleza hisia zao bila kujali umbali uliopo kati yao. Kutopokea simu au kutokutafutwa na mpenzi wako kwa muda mrefu kunaweza kuleta wasiwasi, hasa katika mahusiano yenye mawasiliano ya mara kwa mara.

Kwa kuwa mazungumzo kupitia simu ni njia rahisi ya kutunza uhusiano, ni jambo la kawaida kwa mpenzi kujisikia vibaya au kutokuwa na amani mpenzi wake anapokaa muda mrefu bila kupiga simu. Kutozungumza kwa muda mrefu kunaweza fanya mtu kujihisi kutothaminiwa kwenye mahusiano yake ya mapenzi au kuhisi jambo jingine baya limeingia kwenye mahusiano.

“Kutokupigiwa simu na mpenzi” hali inayoweza kuwa na sababu nyingi na pia inaweza ikatokea kwa namna nyingi. Lakini badala ya kuwa na wasiwasi au kuchukia, kuna mambo kadhaa unaweza kufanya ili kuiweka sawa.
Ikiwa mpenzi wako hakupigii simu kwa namna yoyote na haujui nini Cha kufanya, hapa chini kuna jinsi tumeeleza mambo unayoweza kufanya.

Mambo ya kufanya mpenzi akiwa kakupigii simu au kukutafuta

Tengeneza tabia ya kumpigia sana wewe alafu ghafla uiache kwa muda

Unaweza kufanya Jambo hili kama mpenzi wako mpya anatabia ya kutokukupigia simu lakini ukimpigia, mnaongea vizuri tu na mahusiano yenu yametulia.
Utachotakiwa kufanya hapa ni kuzidisha kumjali na kumpigia simu za mara kwa mara alafu unaamua kutulia bila kumpigia ghafla. Jambo hili linaweza mfanya akupigie kujua ni nini tatizo maana sio kawaida yako.
Akikupigia kwa mara ya kwanza, inaweza kuwa ndio tabia yake ya kukupigia imeanzia hapo.

Maswali ya kumuuliza Mpenzi wako Mpya BONYEZA HAPA>>>

Kuwa na mambo mazuri ya kuongelea kwenye simu

Kuna watu muda huu, hawakupigii kwasababu hakuna jambo la kuongelea. Inaweza kuwa hivyo pia kwenye mahusiano. Mpenzi wako anaweza kuwa hakupigii simu mara kwa mara kwasababu mnakosa vitu vizuri vya kuongelea.
Kuna watu wengi tu huwa wanashindwa kuongea vizuri na wapenzi wao kwenye simu. Na baadhi ya wanaoongea, huwa hawaongei mambo mazuri ya kuvutia kiasi kwamba mpenzi awe anatamani kupiga simu na kuongea tena.

Kama unapitia jambo la kutopigiwa simu kwa namna hii, basi fanya kutengeneza uwezo wa kuongea na mpenzi wako kwenye simu mpaka awe anatamani kukupigia ili muongee.

Onana nae mzungumzie mahusiano yenu vizuri

Ikiwa hakupigii simu na hataki kuongea na wewe kwa namna yoyote ile kama mtu aliepandwa na hasira, basi hakikisha unamtafuta muonane ana kwa ana. Unaweza kumfuata mahari alipo na ukaongea nae kuhusu mahusiano yenu vizuri ili kujua nini tatizo. Kama utakua mbali nae, unaweza watumia ndungu au marafiki kumuuliza kuhusu tatizo linalomfanya asitake kuwasiliana na wewe.

La kumaliza ni kwamba, Kuna muda mtu anaweza kuwa hakupigii simu wala kupokea simu yako kwasababu ana matatizo yaliomkuta au yupo mazingira yasiomrusu. Hivyo uwe unafikilia upande huu pia kwa mwanamke au Mwanaume wako. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Ujumbe wa Mapenzi kwa umpendae (Meseji)

Natumaini unafahamu kuwa kutuliza akili na kutuma ujumbe wa mapenzi kwa umpendaye inaweza kuonekana kama jambo la kitoto lakini ni muhimu sana kwenye mahusiano. Ujumbe wa maneno ya upendo unaweza kuwa na uzito mkubwa kuliko tunavyodhani. Na hii ndio maana mara nyingi The bestgalaxy tunakuandalia makala zinazohusu mambo yanayohusu ujumbe wa mapenzi.

Wanawake na wanaume, wote hufurahia sana wanapopokea ujumbe wa mapenzi, haijalishi wana umri gani. Hata watu wenye umri mkubwa wanapoona maneno machache ya upendo kutoka kwa watu au wapendwa wao, hufurahi na kuhisi kuthaminiwa.

Mtu unaweza mtumia umpendae Ujumbe wa aina hii hatakama tayari mupo kwenye ndoa. Kikubwa ujumbe huo uwe mzuri na umpate mke au mume wako kwenye wakati mzuri atakao furahia.

SMS za kumchekesha mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Katika ulimwengu wa sasa, ujumbe mfupi ndio mzuri kuliko Ujumbe mrefu sana. Ujumbe wa maneno machache ya upendo unatosha kufikisha hisia zako na kumfurahisha bila kuhitaji maneno mengi. Ni njia bora ya kuonyesha kuwa unamjali mtu bila kutumia muda mwingi. Lakini hii haina maana kuwa ujumbe mrefu hauna umuhimu, bado unaumuhimu mkubwa sana. Kama unapenda kumtumia mpenzi wako ujumbe au sms ndefu za upendo, basi isiwe kila muda au mara kwa mara.

Ujumbe wa mapenzi kwa umpendae

  • Nikikwambia “Nikinywa maji nakuona kwenye glasi” najua utanicheka na hautaniamini. Lakini hiyo sentensi huwa inaana “Nakuwaza kila wakati”. Na ni kweli na kuwaza kila wakati kwasababu nakupenda sana kipenzi.
  • Umenipa Raha ya ajabu. Umeniacha sina usemi kama bubu. Ladha sio Sukari, sio Asali na ni zaidi ya “Tamu”.
  • Yani muda huu nimetulia hapa, watu wanaweza sema nawaza hela. Kumbe nakuwaza wewe kipenzi cha Roho yangu. Vipi Hali yako we malaika?

  • Jinsi ninavyokupenda ni kama nilikuweka ndani ya moyo wangu alafu funguo za moyo nimepoteza. Siwezi ingiza tena mtu na huwezi toka bila maumivu mpenzi, UMENIWEZA!

  • Moyoni ni nakupenda, akilini naamini kuwa tunapendana. Mambo ni mengi sana ya kufanya tusiwe sawa. Ila unapo lala au kuamka, usisahau kuwa nakupenda sana.

  • Ukisema “Nakupenda” nahisi furaha sana moyoni. Ukiwa karibu, huwa staki uende mbali. Wewe ni kile chakula naweza shiba na nikaendelea kukitamani.


  • Wanasema “Mtu hauwezi kuiona raha ya Dunia bila kuwa na furaha”. Mimi nasema siwezi kuiona raha ya Dunia bila wewe. Kwasababu wewe ndie furaha yangu, nakupenda kuliko unavyo fikilia.

  • Nakushukuru kwa kila tabasamu, kila kumbatio, na kila neno zuri uliloniambia. Nakuona kama ni zawadi ambayo kila siku inanikumbusha thamani yangu. Nakupenda sana na naomba usije choka kunipenda.

  • Nahisi umenizamisha kwenye usingizi mzito sana. Najiona kama naota ndoto tamu na ndoto hii, ni kuwa na wewe kipenzi. Ikiwa kweli hii ni ndoto, basi iwe hivi milele maana nikiamshwa nitaumia.

  • Nikikwambia “Siwezi kuishi bila wewe” unaweza nicheka kwa kuhisi ni uongo. Lakini mimi nakwambia hivyo nikiwa na maana “Siwezi kuishi maisha ninayotaka bila wewe”. Mimi nataka niishi maisha ya kupendana na wewe milele. Sasa nitawezaje kuyaishi bila wewe?
  • Nikikukumbuka sana, moyo wangu hunipa masharti ya kutimiza ili nipate FURAHA. Sharti la kwanza ni kuwa karibu yako na ikishindikana, basi nikupigie simu nisikie sauti yako. Uwe unapokea simu sasa mpenzi, utaniua mwenzako.

  • Binadamu tumeumbiwa makosa mpenzi, huenda kunakitu nakosea maana mimi si malaika. Lakini kumbuka nina Moyo, mpenzi. Na huo moyo unamapenzi ya dhati na wewe.


  • Upendo wako ni amani katika Dunia iliojaa vurugu na kelele nyingi juu ya MAPENZI. Wakati watu wangine wanatafuta wapenzi wanaojua mapenzi, mimi nasherekea kukupata kipenzi changu.
  • Nakupenda sana mpenzi. Yani hata kama wewe ungekua ni Mti alafu mimi ni ndege nilietua kwenye Mti kwa bahati mbaya katika matembezi. Bado ninge hamia kwenye mti huo mazima maana unakila ninachotaka.

Ni jumbe hizo tu katika ukurasa huu ila kuna makala nyingi unaweza soma katika The bestgalaxy ili kupata sms au Jumbe nyingi zaidi za mapenzi. Endelea kuwa karibu na sisi na pia usisahau kufuatilia mambo mengine ikiwemo simulizi.

DAWA CHUNGU (Simulizi Fupi ya Kusoma)

Nina mke mzuri sana, na nampenda. Nina uhakika na yeye pia ananipenda. Tumebarikiwa na mtoto mdogo mmoja. Nafanya kazi, lakini kuna kipindi mambo yangu ya kikazi yalienda vibaya. Kipato kikawa kidogo sana. Mke wangu alianza kudai mahitaji ya nyumbani na mtoto kila wakati. Kila alivyodai, ndivyo nilivyoanza kumwona kama kero, maana hachoki kusema. Hali hii ilinipeleka kwenye uhusiano wa pembeni na binti mmoja mzuri, mdogo alafu mjanja mjanja, anayekaa mtaa wa tatu kutoka kwangu.

Nilikutana naye katika sehemu za starehe. Nilienda pale kupoteza mawazo kwa kunywa pombe kama wanavyoseoma. Tulipokutana huko, furaha yangu ilianza kufufuka hivi. Kila nilipopata pesa kidogo, badala ya kupeleka nyumbani, nilikua naenda kwenye sehemu za starehe, nampigia simu huyo binti aje tuwe wote. Yeye alinipa furaha zaidi kuliko mke wangu kwa kipindi hicho, maana tulilewa pamoja, tulikuatunacheka, na kufanya mambo mengi ambayo sikufanya na mke wangu. Mke wangu tukitulia alikua nawaza kunidai na kuniambie matatizo. Hali hii huwa inatesa sana.

Pamoja na yote hayo, bado nilimpenda sana mke wangu. Niliweka siri hiyo, sikutaka ajue chochote maana najua na yeye ananipenda sana ila maisha ndio yanatufanya tuwe kwenye hali hiyo. Mioyo yetu inapendana sana ila mifumo ya maisha ndio tatizo.

Siku moja kazini, mpango mmoja niliokuwa nao ulienda vizuri, nikapata pesa nyingi kiasi kwa mpigo. Nilikuwa na furaha kubwa, nikaingiziwa pesa kwenye simu. Badala ya kufikiria familia yangu au mke wangu, akili yangu ilikimbilia kwenye starehe maana ilikua ni kama nimezoea hivi. Mwanzo nilianza kwa lengo la kupoteza mawazo lakini mwisho ikawa tabia yangu bila kushtuka.

Sika hiyo nilipanga kujipongeza kwa kukutana na yule binti tufanye starehe. Nilifika kwenye sehemu ya starehe, nikapata chupa moja ya pombe na kuanza kunywa. Wakati nakunywa nikatuma ujumbe kwa yule binti “Njoo sasa, nina furaha sana kuliko siku zote, nataka uje tufurahi pamoja.” Siku jieleza sana maana niliongea nae kabla.

Kabla huyo binti hajajibu, nikakuta mke wangu anapiga simu. Siku taka kupokea, niliiacha ikiita huku nikiendelea kunywa pombe kidogo kidogo. Baada ya muda simu iliacha kuita, nikakuta ujumbe toka kwa mke wangu unaingipia. Sikutaka hata kufungua hivyo sikujua alichoniandikia. Baada ya dakika moja yule pinti alinijibu ujumbe niliomtumia.
Alinijibu kuwa alikuwa na matatizo yaliyohitaji kiasi fulani cha pesa. Alisema akiipata hiyo pesa popote, atakuja. Kwakua mimi nilikua na pesa, nikamwambia asiwe na wasiwasi, nitamtumia hiyo pesa ndani ya dakika tano.
Baada ya kumwambia hayo, nilianza mchakato wa kumtumia pesa yule binti. Nikachukua simu na kuandika kiasi cha pesa anachohitaji kisha nikatuma.
Baada ya kutuma tu, nikamuandikia yule binti ujumbe uliosemeka “Tayari nimeisha tuma. Itumie hiyo pesa kwenye hayo mambo yako yote alafu tufurahi wote maana ninafura na furaha yangu nataka nifurahi nikiwa na wewe mpenzi wangu” kisha nikautuma.

Lakini baada ya dakika nilishangaa kuona ujumbe wa shukrani kutoka kwa mke wangu. “Asante sana mume wangu. Sijui nikupe nini wewe mwanaume. Mungu akulinde na kukubariki sana pacha wangu. Najiona nina bahati kuwa na wewe”

Nilishangaa sana. Nilipochunguza, nikakumbuka kuwa sikuusoma ujumbe wa kwanza wa mke wangu. Nipousoma nikaona ulikuwa ni wamalalamiko mengi kuhusu mahitaji ya nyumbani na mtoto wetu.

Hapo akili yangu ilianza kukaa vizuri: kumbe pesa niliyotuma, nilimtumia mke wangu kimakosa badala ya yule binti! Mbaya zaidi, nilikuwa nimeandika kiasi kikubwa cha pesa kuliko nilivyokusudia. Sijui zilikua ni pombe au nini ila kukosea kuandika kiasi cha pesa kulifanya pesa nilioituma kuwa kubwa sana kuliko iliobaki kwenye simu yangu. Na kumbe hata ule ujumbe nilipotaka kumtaalifu yule binti,nimemtumia mke wangu pia.

Nilichanganyikiwa. Pombe kichwani ilikata ghafla. Nikabaki nimekaa pale, huku simu ya mke wangu ikiendelea kuingia na ujumbe wa shukrani ukija mmoja baada ya mwingine.
Hakukuwa na maneno mengi ya kumwambia. Nilijua ningesema jambo lolote, basi ningeharibu ndoa yangu. Ingenibidi nieleze hiyo pesa nyingi hivyo nilikua natuma wapi alafu pia ujumbe niliokosea kumtumia kwanini una neno “mpenzi”.
Nilijaribu kuwasiliana na watu wa mtandao kidogo ili warudishe ila nikaacha. Nikaona kama hiyo pesa imeokolewa na mungu maana kiasi kile cha pesa kingeenda kwa yule binti mjanja wa mjini, sidhani kama ningefaidika chochote. Bora mke wangu kaipata maana ni kama nimepunguza matatizo ya nyumbani kidogo.

Baade nilirudi nyumbani nikamkuta mke wangu anafuraha sana. Yani alikua ananiangalia hanimalizi maana hakutegemea jambo lile. Alikuwa amenipikia chakula kizuri, na kila kitu kilionekana kama sherehe humo ndani. Alinipongeza na kunishukuru kwa msaada wa kifedha ambao kimoyomoyo sikupanga kumpa. Akili yangu ilikuwa kwenye pesa yangu kuwa nimetuma kimakosa.

Sikuweza kurudisha pesa hiyo mikononi mwangu wala kuliongelea sana. Ila kufidia kidogo pesa yangu nilimkopa mke wangu kiasi kidogo baada ya wiki na akakubali bila kusita maana ananiamini. Hiyo pesa niliyokopa, sina mpango wa kuirudisha japo yeye anadhani nitarudisha.

Pamoja na yote siwezi jilaumu sana kuhusu tukio hilo maana lilimfanya mke wangu aanze kuelewa kidogo nikimwambia niko vibaya kwenye pesa. Alikua anaamini kuwa nikipata pesa huwa namkumbuka. Na kweli kwanzia tukio hilo limenitokea, huwa namkumbuka sana mke wangu. Ukimfanyia jambo lolote zuri la bila kutarajia huwa anachanganyikiwa kwa furaha.

Mwisho

Unataka kupata Mpenzi au Rafiki wa kizungu Mtandaoni?

Mtandao umekuwa daraja linalounganisha watu kutoka pembe zote za dunia na kuzalisha uhusiano wa kirafiki au kimapenzi. Kupata mpenzi au rafiki kutoka nchi au bara tofauti, kunaweza kuwa ni jambo zuri sana linalowezeshwa na Teknolojia kwa sasa. Unaweza pata mtu Toka marekani, uingereza na sehemu nyingine ulimwengu kwa kutumia simu yako tu.

Pamoja na uzuri wa jambo hilo, kama ilivyo kwa mambo mengine, kuna pande mbili za kuzijua. Kuingia kwenye uhusiano wa mtandaoni kunaweza kuwa na faida nyingi kama vile kujenga urafiki wa kawaida, kujifunza lugha mpya, na hata kupata fursa za kusafiri au kazi. Lakini pia kuna changamoto na hatari zake. Uaminifu wa mtu unaekutana nae mtandaoni unaweza kuwa mgumu kujua upo vipi, na kuna visa vya watu wengi kudanganywa au kuibiwa pesa kwa kupitia uhusiano wa namna hii mtandaoni. Ni muhimu kuwa makini na kuchukua tahadhari kabla ya kuweka hisia zako kwenye mahusiano haya ya mitandaoni.

Kwa hiyo, kama unafikiria au kutamani kupata mpenzi au rafiki wa kizungu mtandaoni, unapaswa kuziangalia faida bila kusahau hasara zake pia. Mtandao unatoa fursa nzuri za kukutana na watu wapya, lakini vilevile, unahitaji kuwa makini ili kuepuka matatizo.

Katika makala hii, tutajadili njia rahisi ambazo watu hutumia kujenga uhusiano na wazungu wa kiume au wakike mtandaoni kwasasa.

Jinsi ya kupata Mpenzi mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Njia za kupata Mpenzi au Rafiki wa kizungu Mtandaoni

Tuvuti za Uchumba na Urafiki

Hii ndio njia kuu na maalumu kwa mahusiano ya namna hii. Kuna tuvuti ambazo zinawakutanisha watu wanaohitaji mahusiano na watu wengine. Tuvuti hizi tunakusanya watu toka pande mbalimbali za Dunia.

Unaweza zitumia tuvuti hizi kuanzisha mahusiano ya Urafiki au mapenzi hata kama akiwa mbali na nchi uliopo. Unaweza pata mzungu kupitia tuvuti hizi na akawa Rafiki yako au Mpenzi wako kabisa. Mfano wa tuvuti hizi ni Tinder. Tinder Ina app akabisa ambayo unaweza iingiza kwenye simu yako ili kuitumia kirahisi.

Magemu ya kucheza watu wengi mtandaoni

Kwasasa Kuna game nyingi zinakusanya watu toka nchi mbalimbali na wanacheza kwa pamoja mtandaoni(Hasa game za battle Royale). Sasa hizi game zinaweza kuwa chazo cha kukutana na watu toka nchi nyingine na kuanzisha uhusiano nao. Katika game ili upate Marafiki kirahisi inabindi uwe ni mtu unaejua kucheza game vizuri na unakua msaada kwao. Yani inabidi unacheza nao tofauti mpaka wasipo kuwa na wewe, wanakukumbuka.


Ukiwa hivyo kwenye game za mtandaoni, unaweza jizolea marafiki ikiwemo wazungu maana inaweza kifika kipindi wanakutafuta kwenye simu ucheze nao. Na hapa kuzijua lugha na kuwa mchangamfu kidogo ni kitu muhimu.

Magame mazuri ya battle Royale ya kucheza kwenye simu BONYEZA HAPA>>>

Magroup ya kulipia ya elimu au mambo muhimu

Ukiachana na magroup ambayo mtu unaweza jiunga kwa kubonyeza link katika mitandao, fahamu kuwa kuna magroup ya kulipia ambayo yanakusanya watu toka pande mbalimbali za Dunia. Magroup haya mara nyingi yanakua chini ya watu maalufu mitandaoni na huwa ni kwaajili ya elimu au mambo mengine muhimu. Mfano kwenye YouTube; kuna watu huwa wanaanzisha group hizi kwaajili ya kuwafundisha watu wao kwa ukaribu zaidi. Ukijiunga kwenye group hizi, utaona watu huwa watulivu sana humo ndani maana wamelipia kuwa humo. Mbali na kuwa watulivu, huwa wanakua wanajidili na kushilikiana kwenye mambo yaliowaleta humo.

Sasa katika kujadiliana na kushirikiana, unaweza jikuta umekua na marafiki wa nchi nyingine au kizungu ambao mnaongeo kuhusu maswala flani tu. Mahusiano ya mapenzi yanaweza kuanza hivyo pia lakini inaweza kuwa baada ya kuzoeana sana maana. Hii ni kama vile mtu unaenda shule kwaajili ya Kusoma lakini unajikita kwenye mahusiano na mwanafuzi mwenzako.

Unapohitaji kupata Mpenzi au Rafiki wa kizungu Mtandaoni, njia hizo ni njia mbazo tunaweza ziita rahisi kuzitumia. Na pia fahamu kuwa kupata mwanamke au Mwanaume wa kizungu inawezekana ila unatakiwa kuwa makini sana. Epuka kuwasumbua sana watu wa nchi nyingine maana huwezi jua wanauchukuliaje usumbufu wako. Jambo linaweza kuwa sawa kwako lakini lisichukuliwe sawa kwao.