Category Archives: Mahusiano

Sms za kulalamika kwa mpenzi wako (Mwanamke au Mwanaume)



Katika mahusiano ya mapenzi, si kila wakati mambo yanakwenda kama unavyotarajia. Kuna nyakati unaweza gundua kuwa mpenzi wako amebadilika, haonyeshi tena upendo na kujali kama zamani. Labda ameanza kuwa mbali, hajali hisia zako, au hata anaonyesha dalili za kuzingatia katika uhusiano wenu. Hali kama hizi zinaweza kuumiza moyo na kukufanya uhisi huzuni, mashaka, au hata hasira.

Pia, kuna wakati unaweza kugundua kuwa mpenzi wako amekusaliti kabisa. Hakuna kitu kinachouma kama kugundua kuwa mtu uliyempenda kwa dhati ana mtu mwingine au aheshimu uaminifu wenu. Usaliti unaweza kuleta maumivu makubwa na kukufanya ujihisi si wathamani.

Mtu unapopitia katika hali kama hizi, unaweza kuhitaji kumwandikia mpenzi wako ujumbe wa kulalamika, ili aelewe jinsi kitendo chake kilivyokuathiri na, pengine, abadilishe tabia yake , kiwezekana. Kutuma ujumbe wa kuelezea hisia zako kunaweza kuwa moja ya kutoa hisia zako na kufungua mzingo kifuani. Katika makala hii, tumekuandalia orodha ya sms za kulalamika ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ili kuelezea hisia zako kwa bila kupoteza muda.

Simulizi bora za kusoma katika The bestgalaxy BONYEZA HAPA>>>

Ujumbe wa kulalamika kwa mpenzi wako





Moyo wangu upo kwako ni vile tu Umeamua kuubuluza. Unayoyafanya yananiuza na Sina chakufanya kukukumbusha kuwa ulisema milele utanipenda. Ok, Fanya unachofanya ila milele usisahau ninakupenda!



Mimezikumbuka zile siku za furaha , zile siku tulikua tunatafutana kila mara na kuambiana hisia zetu. Na bado nakumbuka tuliambizana “unanipa furaha, sina mwingine, ni wewe tu”. Lakini sasaivi wewe sijui umepata mwingine kakubadilisha… eti ni umesahau???



Ulikuja kama mwanga kuyaangaza maisha yangu, ulileta matumaini na ndoto lakini ghafla unaniacha nikiwa nimevunjika moyo na kukata tamaa ya kupenda tena. Asante kwa yote lakini!



Natamani miaka ambayo nimekaa na wewe isingetokea katika Maisha yangu. Zile kumbukumbu nilizofurahia na wewe zinaniumiza kwasasa. Ninatamani kufuta kila kumbukumbu yako ila ndio hivyo uliniweza, nikakupenda kweli na sasa umenisaliti ninaumia.



Nitajuta milele vile nilikupenda bila kujua dhamira yako na kukuamini. Nilikupa kila kitu nilicho hisi kitakufurahisha; lakini katika malipo, umenitoa machozi kwa maumivu yasio isha.



Najitahidi kila mara kuwaza na kukufanyia mambo yatakayo kupa furaha lakini wewe umekua ukinilipa mambo yanayoniumiza. Najua hii inamaana; Pamoja na kukupenda, Bado haunipendi. Asante sana, naendelea kukupenda ila nimekuelewa!



Nilikupenda bila sharti lolote na bila kuuliza kurudishiwa ila ulichukulia upendo huo kuwa udhaifu wangu. Siwezi sema mengi ila umeniumiza vya kutosha sasa, niache niendelee na maisha yangu.



Nilikuamini kwa moyo wangu wote, lakini umeshindwa kuelewa hilo. Umenifanya nijifunze kuto kumuamini mtu hata nikimpenda sana. Ninakuchukia, lakini nashukuru kwa somo! Nashukuru kwa kunivunja moyo pia!

Huu ndio mwisho wa orodha yetu ila Kuna mambo mengi sana katika The bestgalaxy unaweza furahia. Kikubwa Endelea kuwa karibu nasi ili kujifunza mengi!

Mukijua mambo haya hamuwezi achana na mpenzi wako kirahisi

Unaponda sehemu flani ngeni kuishi, unaweza kutana na changamoto au mambo tofauti kwako. Mengine yanaweza kuwa ni yakushangaza na mengine yanaweza kuwa magumu ila baada ya kuishi kwa muda flani na kuyajua vizuri mambo ya hapo, unazoea na kuanza kuishi sehemu hiyo kama ni yakamaaida. Yani hata kama jirani wako umemkuta ni mkorofi, baada ya muda unaweza mchukulia kama alivyo na maisha ya ujirani yakaendelea.

Unapoingia katika mahusiano nako huwa kuna mambo flani hivi yanaweza kuibuka na kuleta changamoto ila wote wapenzi wawili mukiyajua mutaendelea na mapenzi ya muda mrefu bila kuachana. Yani mambo haya kama hata mmoja wenu akiyajua, ataweza kuokoa mapenzi yenu Kila yanapotaka kuvunjika na hata kuyatunza yewe imara. Lakini mukiyajua wote, inakua poa zaidi.

Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Mambo ambayo mukijua inakua sio rahisi wewe na mpenzi wako kuachana

Kutoelewana sio mwisho wa mahusiano

Wengi kwenye mapenzi ya sasa huwa wasipoelewana, wanaachana kirahisi sana. Yani wanaweza anzisha mwezi huu mahusiano alafu baada ya mwezi kuisha, wanaishia kwenye kutoelewana alafu wanaachana.


Ukweli ni kwamba kutoelewana kwenye mahusiano hakupingiki, na kama kila mahusiano yangekuua yanaishia pale wapenzi wasipoelewana katika mambo flani, basi kungekua hakuna watu wenye mahusiano ya kudumu.


Ili mahusiano yadumu, inabidi mufahamu kabisa kuwa kuna siku mnaweza kuwa hamuelewani kwasababu ya mambo mbalimbali. Ila nijukumu lenu wote kuyaweka mahusiano vizuri. Mukiwa na uwezo wa kutafutana bila aibu baada ya kutoelewana, mahusiano yenu yatadumu sana.

Kuchepuka kuna hasara kubwa kuliko faida

Asilimia kubwa ya watu wanaochepuka kwa wapenzi wao huishia kujilaumu sana. Na hujilaumu kwasababu kuchepuka kuna hasara kubwa nyingi kuliko faida. Kuchepuka kuna kufanya tuingie kwenye hatari ya magonjwa kama HIV. Alafu mbali na hayo, pia unaweza jiingiza kwenye utumwa wa Siri ambazo zinaweza kukutesa kwa miaka.


Mfano; Unakuta mtu anachepuka alafu kapewa au kumpa mimba mchepuko. Mtoto anazaliwa kwa siri huku mtu aliechepuka anashikiria Siri moyoni mpaka Raha ya maisha anaikosa.
Mukijua mapema haya kama wapenzi, nguvu ya kusalitiana inapungua kidogo.

Kuna muda mnapata hasira kwasababu mnapendana

Mwanamke au Mwanaume anaweza kufoka au kupandwa na hasira kwenye jambo dogo sana. Hizo hasira huwa zinakuja kwasababu ya upendo tu na sio jambo jingine.

Mukijua kuwa kunamuda munatiana hasira kwasababu mioyo yenu inaupendo, mtaweza kuwa kwenye mahusiano kwa muda mrefu sana. Maana asilimia kubwa ya wanaolijua hili, hujielewa kwanza wao alafu huelewa na wapenzi wao wanapokua na hasira.


Mfano; Kwenye ndoa hapa ndio unaweza kukuta mwanamke au mwanaume anakasirika sana na kumrushia maneno mpenzi wake anapochelewa kurudi. Kinachomfanya akasirike sana ni upendo tu na sio jambo jingine. Usipolielewa hili kwa mpenzi wako unaweza muona mbaya kwao.

Maongezi ya usiku ya kila mara ni muhimu

Mukiwa kama wapenzi mnaojenga mapenzi ya muda mrefu, kufanya mazungumzo au mawasiliano ya kila mara usiku ni muhumu sana. Yani kutenga nusu saa au saa moja la kuongea kila siku kutawafanya muwe karibu zaidi kifikra na kihisia.

Mtakua na uwezo wa kupanga mipango yenu pamoja, kujuana zaidi na kujenga imani.
Mbali na hayo, usingizi unaokuja baada ya kuongea na mpenzi wako huwa unakua mzuri sana. Hivyo ni njia moja ya kufanya mulale vizuri.

Kijana hizi ni athari za Wanawake wakubwa sana (Majimama/Mishangazi)




Wakati baadhi ya vijana Wakiume wanaongelea na hata kutafuta kabisa Majima au Mishangazi, hebu tunangalie athari zake. “Mishangazi” au “Majimama” ni majina ambayo kuna watu hutumia wakiwa na maana “Wanawake wakubwa wanaoingia kwenye mahusiano na vijana wadogo.” wanawake hawa wapo katika jamii zetu na kumekua na simulizi nyingi za vijana kujihusisha nao kimapenzi.

Mahusiano kati ya wanawake wakubwa na vijana yanaweza kuwa ni upendo toka moyoni kabisa. Yani wanaweza kuanza kwa mazoea ya kuwa karibu alafu mwisho, wakajikuta kwenye penzi zito. Ila kwakua wanasema, Mapenzi hayana umri, tunaweza sema ni jambo lisiloshangaza sana.

Lakini pia baadhi ya mahusiano ya namna hii huwa ni kama wanabadilishana pesa au maisha mzuri kwa mpenzi. Yani hapa Kijana wa kiume anawezakua anatoa mapenzi huku Mwanamke mkubwa akitoa pesa au maisha mzuri kwa Kijana. Kwaiyo Kuna namna Kijana wa kiume anaweza faidika hapa.

Pamoja na yote ambayo kijana wa kiume anaweza pata au kufaidika kwenye mahusiano ya namna hii, Bado sio Mahusiano salama. Kijana anaweza pata athari mbaya kubwa kwenye maisha yake anapokua na majimama au Mishangazi. Athari zinazo zungumziwa hapa ni zifuatazo:

Kijana hizi ni athari za Wanawake wakubwa sana (Majimama/Mishangazi)

Magonjwa



Kama tunavyo fahamu, magonjwa kama vile HIV huwa yanaweza ambukizwa kwa kushariki Ngono zembe. Ngono zembe ni kushiriki tendo la ndoa bila Kinga yoyote.

Kama upo kwenye mahusiano na mwanamke mkubwa, Tendo hili linaweza kuwa ni tendo la kawaida sana. Mnaweza zingatia kinga siku ya kwanza lakini ya pili mukazitupia mbali kwa kuamini haziwafurahishi kwenye tendo.

Sasa ikiwa mmeamua kutotumia Kinga Kuna hatari kubwa ya kuambukizana virusi ya ukimwi na magonjwa mengine.


Kuwachukulia poa wanawake wengine



Kijana wa kiume anapoingia kwenye mahusiano na mwanamke mkubwa anaweza jikuta anaanza kudharau mwanamke wa umri wake. Yani anaweza anza wachukulia poa sana mwanamke wa umri wake maana tayari anaoneshwa au kufanyiwa vitu vingi ambayo wanawake wengine hawafanyi.


Hali hii inaweza kumfanya huyo Kijana ajiamini sana anapokua na Mwanamke wengine. Lakini kujiamni huko ni matokeo ya kugundua kuwa mwanamke wengine hawajui mapenzi.

Kugeuka tegemezi


Kijana wa kiume akipata mwanamke mkubwa anaempa pesa kisa mapenzi, kuna hatari kubwa ya huyo Kijana kuwa tegemezi kwenye maisha yake. Anaweza fikia wakati hata akiachwa na jimama anaona maisha yake yameharibika.


Kwa kawaida mwanaume anatakiwa kubeba Majukumu, kujitegemea na kutegemewa. Huyo mwanaume akizoeshwa kutegemea mwanamke, inakua ni ngumu kwake kuchukua Majukumu, kujitegemea na kutegemewa tena. Huo kwake unakua ni mzigo mkubwa sana.

Kuingia kwenye migogoro



Baadhi ya wanawake wanaoitwa “Majimama” au “Mishangazi” ni wake za watu au Mama za watu. Kutokana na hili, pamoja na yote wanayofanya, Bado ni wanawake ambao wana ndungu na jamaa kwenye maisha yao.

Kijana anaweza ingia kwenye migogoro ya kifamilia bila kujua. Ukiwa kama kijana, unaweza kuwa chanzo cha mke na mume kukosana, unaweza chukiwa na watoto wake au ndungu. Mongogoro mingi inaweza kuibuka hapa.

Simulizi Bora za kusoma au kufuatilia katika The bestgalaxy

Katika moja ya mambo watu hufurahia kwenye simu zao ni kufuatilia simulizi mbalimbali kwa kusoma au kusikiliza. Hili ni jambo zuri ambalo mtu anaweza kulifanya kwenye simu mbali na kuwasiliana na watu. Sio kila muda mtu anaposhika simu anawasiliana na watu, Kuna muda anawezakua anafuatilia simulizi anazozipenda toka The bestgalaxy au sehemu nyingine.

The bestgalaxy ni sehemu unayoweza kujifunza mambo mbalimbali kuhusu mahusiano, Teknolojia na mengineyo. Katika the Bestgalaxy mtu unaweza pata simulizi pia. Na simulizi nyingi za The Bestgalaxy zimejikita kwenye mahusiano kwasababu ya kuburudisha na kuelimisha kwenye upande huo.


Katika makala hii tumeorodhesha simulizi chache nzuri za kusoma unazoweza pata kutoka The bestgalaxy. Kama unapenda kusoma simulizi za mahusiano/Mapenzi, basi zingatia orodha hii.

Hizi ni Simulizi Bora za kusoma au kufuatilia (Mapenzi na Maisha)

SUKARI YA DADA

Sukari ya dada ni simulizi inayomuhusu Kijana ambae alienda Dar es salaam kwaajili ya kufanya kazi za ndani baada kutofanya vizuri kidato cha nne. Kwenda huko ilikua ni njia pekee alioiona itamsaidia maishani kwa wakati huo lakini katika kuelekea anapohitaji, anakutana na changamoto nyingi sana kutokana na ujana.
Unaposoma simulizi hii, unapelekwa moja kwa moja katika kuyaona maisha ya kijana huyo. Lakini katika kuisoma simulizi ya SUKARI YA DADA, unatakiwa kuwa ni mtu uliefikisha umri wa maika 18 au zaidi.
Ukimaliza kuisoma simulizi ya SUKARI YA DADA mpaka mwisho, unaweza soma pia simulizi nyingine 2 ambazo ni UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA kwasababu zinauhusiano. Tutafafanua zaidi kuhusu simulizi hizi huku tukiwa tunaendelea na orodha.

UNANIITA?

Simulizi hii ni fupi na inamhusu kijana mdogo ambaye kazi yake ni kuendesha bodaboda mjini. Siku moja, anakutana na mteja mpya aitwaye Zena, mwanamke mrembo anayekabiliwa na changamoto katika uhusiano wake wa ndoa. Kupitia safari zao pamoja, Zena anafunguka kuhusu matatizo anayopitia na jinsi anavyojisikia kupuuzwa na mume wake. Kijana huyu anajaribu kumpa ushauri wa kumsaidia kuboresha mawasiliano na mumewe.
Hii ni moja ya simulizi nzuri sana lakini ni fupi.

UTAMU WA JUMLA

Unaposoma simulizi hii, unafuatilia maisha kijana aliyekulia Tabora na baadaye kuhamia Dar es Salaam kwa ajili ya masomo ya biashara chuoni. Akiwa chuoni, anakuwa na urafiki na Jimmy. Unaangalia maisha yake na changamoto anazopitia akiwa kama kijana amambe amesoma chuo na akiwa na ndoto au matarajio ya kufanikiwa maishani.
Hii simulizi inahusiano na simulizi 2 ambazo ni SUKARI YA DADA na MZIGO WA WAKUBWA. Kama umeisoma simulizi nzima ya SUKARI YA DADA na unataka simulizi nyingine, basi soma simulizi hii. Lakini unapoisoma, umri wako uwe umefia miaka 18.

SIRI NA SHEMEJI

SIRI NA SHEMEJI ni simulizi fupi inayomfuata Anisa, mwanamke mwenye heshima na upendo kwa mume wake, Kevin. Wakati ndoa yao ni changa, Anisa anabeba siri nzito kuhusu uhusiano wake wa zamani. Jambo hilo linamletea Anisa wasiwasi na hatimaye kusababisha mgogoro mkubwa katika ndoa yake na Kevin. Simulizi hii inagusia mada za uaminifu, siri, na msamaha katika mahusiano ya ndoa.
Ni simulizi isio ndefu lakini ni nzuri na inaweza kukupa burudani bila kupoteza muda wako sana.

MZIGO WA WAKUBWA

Katika simulizi hii, unaingia katika Maisha ya kijana anaekua na kuanza kuyazingatia maisha huku akishikilia Mahusiano ya mapenzi. Kijana huyu katika simulizi, anafanya baadhi ya maamuzi ya kukimbia mizingo akihisi ni yawakubwa.
Kama umeisoma simulizi ya SUKARI YA DADA na UTAMU WA JUMLA, basi simulizi ya MZIGO WA WAKUBWA ni simulizi unayotakiwa kumalizia kuisoma. Simulizi hizo tatu zinauhusiano na msomaji anashauriwa kuzisoma zote Loki kupata mocha moja nzuri na yaajabu sana.

Unachotakiwa kujua kuhusu simulizi ya SUKARI YA DADA, UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA

Simulizi ya SUKARI YA DADA, UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA ni simulizi unazoweza zisima pamoja ili kupata picha nzuri. Zimesimuliwa na watu tofauti ila zinakupa picha moja nzuri sana inayohusu mahusiano(Mapenzi)na maisha kwa ujumla. Na katika upande wa majina, kila jina Lina maana katika simulizi. Mfano; jina la MZIGO WA WAKUBWA katika simulizi lina maana “Majukumu”.

MZIGO WA WAKUBWA 01  (Simulizi ya Kusoma)




Tulikua tupo mimi na rafiki yangu Samsoni kwenye chumba chetu tunacholala ambacho watu huita Geto. Ilikua mida ya kama saa moja au mbili usiku hivi alafu muda huo rafiki yangu alikua ananihadithia mechi ya mpira ambayo imetoka kumalizika saa 2 zilizo pita na sikwenda kuiangalia kwenye vibanda vya mpira siku hiyo kutokana na mawazo. Mawazo yalifanya kichwa changu kiwe vibaya sana muda huo kiasi kwamba nilikua naonekana kumsikiliza Samsoni lakini kiukweli nilikua hata simuelewi japo nilikua nacheka kila akicheka na kuitikia “Ebwana ee” ili asigundue kua akili yangu haipo kabisa kwenye anayonisimilia.

Katikati ya hadithi zake za mpira tukasikia simu imeanza kuita katika kisehemu tunachozichaji simu kilichokua pembeni kidogo ya dirisha la chumba hicho. Simu yangu na ya Rafiki yangu Samsoni, zote zilikua zipo chaji alafu simu yangu niliichomeka chaji ikiwa imezimwa. Hivyo simu iliokua ikiita muda huo ilikua ni ya rafiki yangu na tuliigeukia wote ilipokua inaita maana ilitushtua kwa kupiga kelele katikati ya maongezi. Baada ya hapo Samsoni  alinyanyuka huku akijisemesha “Sijui nani huyu… itakua watu wa mpira hawa” alafu akaenda kuichukua ile simu mimi nikiwa namuangalia tu. Alipoishika simu na kusoma jina, nilimsikia akasema “Ah wewe Mpenzi wako huyu ananipiga huku. Sijui umekifanya nini tena kitoto cha watu”

Mimi nikashtuka kidogo alafu nikamuuliza “Ni Sabrina?” Samsoni alijibu “Ndio” alafu akasema tena “Ngoja nipokee nimsikilize” huku akiipokea simu na kuiweka sikioni. Mimi muda huo nilitaka nimwambie asipoke ila alikua ameishapokea kabla hata sijanyanyua mdomo kumwambia. Baada ya Samsoni kupokea simu, nilimsikia akisema “Halo Dada… niambie” alafu nikasikia kisauti kidogo cha Sabrina akasema “mambo vipi?” Samsoni akaitikia “kama kawa, vipi huko?”  Sabrina akasema “safi. Mbona rafiki yako hapatikani kwenye simu? Upo nae hapo?”. Mimi kusikia hivyo nikashtuka, nikamwambia kwa ishara rafiki yangu Samsoni asiseme yupo na mimi.

Samsoni alinielewa akamjibu “Sipo nae. mimi niko mbali kidogo muda huu”. Sabrina alipoambiwa hivyo, akasema “Sawa, ukionana nae mwambie namtafuta” Samsoni akajibu “sawa” kisha simu ikakatwa. Baada ya hapo rafiki yangu alirudisha simu kwenye chaji huku akisema “Haya si umesikia? Eti anakutafuta. Sauti yake tu inaonekana mmezinguana nyie. Huu ugomvi siingilii” mimi nikacheka kwanza kidogo alafu nikasema “nitamcheki baadae”.

Baada ya hapo Samsoni aliniaga kuwa anatoka kidogo hivyo mimi nilibaki mule ndani nikiwa nimetulia tu ila kichwani kwangu mawazo ni mengi sana. Wakati akiondoka alisema pia “Alafu nilipokua anaangalia mpira, Tino alinipigia akaniambia amekutafuta hakupati hivyo umpigie” mimi nikaitikia “Ah sawa”.

Nilipokua pekeangu mule ndani, Mawazo yalinituma ninyanyue godolo tunalolatila maana Samsoni alikua anatabia ya kuweka pesa huko. Nilipofanya hivyo, nilizikuata pesa zake nyingi kiasi na nikazichukua maana niliona kama zinaweza nisaidia katika hali niliokuanayo kwenye wakati huo. Nilikua ni kama na muibia Rafiki yangu kabisa ili tu niweze kukimbia tatizo linalonipa Mawazo.


Mawazo niliokuanayo siku hiyo yalikua yamesababishwa na matokeo ya mimi kuanza kuzifungua kurasa za mapenzi katika maisha yangu. Nakumbuka miaka michache iliopita kambla ya siku hiyo nilikua nasoma sekondari kidato cha tatu na nilikua nasoma shule za kutokea nyumbani. 

Tangu nilipoanza sekondari nilikua sijawahi jihusisha au kuwaza kuwa na mpenzi shuleni japo nilikua natamani. Hii ilikua ni kutokana na mambo mengi ikiwemo sheria za shule zilizokua zikikumbushwa kila siku na walimu. Na pia nilikua nawaogopa wazazi wangu kuniona nimejiingiza kwenye maswala ya mapenzi. Mbali na hayo, nilikua naogopa sana jinsia tofauti. Kuwasogelea na kuongea nao kulikua ni mthihani mkubwa sana kwangu kipindi hicho, hasa akiwa ananivutia.

Kwenye mambo ya kufanya vizuri shuleni kwa bahati mbaya nilikua siko sana huko. Uwezo wangu katika madaftari na mithihani ulikua wa kawaida sana. Nakumbuka darasani nilikua nakaa viti vya nyuma sana. Huko nyuma nilikua nakaa na rafiki zangu wawili ambao mmoja wapo ndio huyo  anaitwa Samsoni, alafu kuna mwingine alikua anaitwa Tino. Kwaiyo tulikua kama tuna kikundi cha watu watatu nyuma ya Darasa. Darasa letu lilikua lina viti vinavyo ruhusu kukaa wawili na kiti nilichokua na kaa mimi, tulikua tunakaa mimi na Samsoni ila mwalimu akitoka tu, Tino alikua anakuja kwenye kiti kile, tunajibana watatu, tunapiga stori. Tino alikua anakaa kiti cha pembeni yetu ambacho kilikua karibu sana na sisi.

Tino alikua ni mwenzetu ila mambo yake yalikua mengi mno. Alikua ni msumbufu sana kiasi kwamba kila mtu alikua anamjua kwa usumbufu wake hapo shuleni. Watu walianza kumjua baada ya kuletwa na mzazi wake shuleni na kupigwa kutokana na kutolala kwao pamoja na kutokuja shule kwa siku 5 mfululizo katika kidato cha kwanza.

Tulikua tuna shirikiana sana Tino lakini usumbufu wangu haukufikia usumbufu wa Tino. Samsoni nae  alikua kama mimi tu, hakumfikia usumbufu Tino hata kidogo. Ila katika mambo ya kwenye vitabu, wote tulikua hatufanyi vizuri sana japo hatui wamwisho Darasani. 

Kuna siku asubuhi tulikua watatu Darasani kule nyuma ya Darasa tunapiga stori kwa kujiachia lakini ghafla akaingia mwalimu. Alivyoingia tu, tukafunga midomo alafu kila mtu kati yetu alikaa vizuri anapokaaga kisha watu wote darasani tukasimama kumsalimia Mwalimu. Baada ya kumsalimia, akaturuhusu tukae alafu nikakuta tu anasema “Nyie watatu uko nyuma hebu simameni”. Mh alivyosema hivyo nikawa nawaza “Anaongelea mimi na rafiki zangu au? Mbona anaangalia huku nyuma?” wakati najiuliza nikakuta mwalimu anasema tena “Nyie muliokua mnapiga kelele mpaka darasa zima mnasikika nyie huko nyuma simameni kabla sijawafuata.” Basi mimi nikaona huenda anatuongelea sisi, nikasimama na bada ya mimi kusimama, nikakuta na Rafiki zangu wawili wanasimama.


Baada ya hapo mwalimu akaanza kufoka “Hivi nyie mna matatizo gani? Inamana hapa shuleni mmekuja kupiga makelele au?” baada ya kusema hayo akaninyoshea mkono na kusema “Wewe hapo wewe inaonekana msumbufu maana hata Nywele haujanyoa. Hizo nywele ni siku ya ngapi nakwambia sitaki kuziona? Hebu sogea hapa mbele” mimi nikiwa mnyonge sana nilisogea taratibu pale mbele ya Darasa. Mwalimu aliniuliza “Unataka ni kupige ndio uanze unijibu?” mimi nikiwa naogopa sana nikamjibu “Hapana, samahani mwalimu nilitaka kunyoa jana ila umeme walikata”. Baada ya kumjibu mwalimu alifikilia alafu akasema “Kesho nisione hizo nywele, sawa!?” nikamjibu “Sawa” alafu nikakuta ananiambia “Na kule nyuma unakokaa, uhame. Kabebe madaftari yako kule nyuma uyalete hapa mbele kwenye hiki kiti ambacho hakina mtu”.

Baada ya mwalimu kusema hivyo nilishtuka maana nilikua sijazoea kukaa viti vya mbele ya Darasa, nikamwambia “Mwalimu hapo wanakaa watu wawili, itakua wameitwa nje”. Mwalimu akasema “Hatakama wakija hao wanao kaa hapa, waambie mimi ndio nimekuweka hapa. Kwanzia leo utakua unakaa hapa mbele. Nawakija hao, waambie wachukue kiti kingine wakae sehemu nyingine ila sio hapa”. Dah nilikua mnyonge sana siku hiyo, nikachukua vitu vyangu nyuma ya Darasa na kuhamia mbele ya darasa huku mwalimu akiniangalia.


Baada ya kukaa mbele mwalimu alianza kufundisha somo lake maana ndio ulikua muda wake huo. Mimi pele mbele nilikua sina amani kabisa maana sijazoea kukaa hapo alafu mbali na hilo, Daftari la mwalimu huyo nilikua sina. Lakini mwalimu alipoanza kufundisha nilichukua kidaftari flani cha ajabu, nikakiweka pale mbele ili kuzuga.

Nakumbuka baada ya kama dakika 10 hivi Mwalimu alipoanza kufundisha, alikuja mwalimu Mkuu akiwa ameambatana na wanafunzi kama watano hivi na mwanafunzi wa kike alikua mmoja. Darasa zima tulijikuta tunavutiwa kumuangalia yule mwanafuzi wa kike. Mwalimu mkuu alianza mazungumzo na Mwalimu aliekua Darasani na mazungumzo yao yalikua ni kwamba hao wanafunzi watano ni wageni na kwanzia siku hiyo watakua wanasoma humo Darasani. Walimu walipomaliza kuzungumza, wale wanafunzi wakaingia ndani ya Darasa alafu yule Mwalimu aliekua Darasani akawaambia watafute nafasi za kukaa mule Darasani. Kabla hata hawajapiga hatua sana, nikakuta mwalimu ghafla anamwambia yule mwanafuzi mgeni wa kike “Wewe usiende huko. Kaa hapa na huyu”. Mimi moyo ulishtuka sana maana alikua anamuelekeza yule Mwanafunzi wa kike akae na mimi kwenye kiti kimoja. Kiukweli mimi nilikua naogopa kukaa na jinsia tofauti hasa wakiwa wazuri ndio napoteza uhuru kabisa yani. Na Mwalimu alikua anamzingatia yule mwanafuzi wa kike kwa kiasi flani, kama ni ndugu yake hivi.

Nakumbuka yule mwanafunzi alikaa na mimi pele huku akiwa na viaibu aibu vya ugeni alafu na mimi wakati huo nina viaibu vya kumuogopa.  Tukiwa tumekaa  pale mwalimu aliwauliza jina wageni wote waliokuja na nilisikia yule Mwanafunzi wa kike akijitambulisha kuwa anaitwa Zuwena.  Basi baada ya hapo mwalimu aliendelea kufundisha na mimi nikawa kama namsikiliza  hivi ingawa akili yangu ilikua inahama. Yani nikua nikitupa jicho langu mara moja moja kwa yule Mwanafuzi wa kike kumuangalia jinsi alivyo. Japo nilikua naogopa, ila alikua anavutia sana kumuangali alafu alikua msafi sana. Kuna muda nilimtupia macho tukagongananae alafu akaona viaibu. Mimi nilipogongananae macho nilishtuka na nikaingiwa na woga zaidi ila woga ulipungua nipowaza “ Inamaana na yeye ananiogopa huyu. Dah ila mzuri mpaka raha. Ingawa naogopa ila hapa nijitahidi niwe hata rafiki yake tu. Sina hata rafiki wakike ujue”. Nakumbuka niliwaza mambo mengi sana kuhusu huyo mgeni bila kujua kuwa ndio namuingiza moyoni hivyo mtoto wa watu.

Baadae, mwisho wa kipindi cha mwalimu aliekua akifundisha ulifika na mwalimu alituachia maswali ya kufanya nyumbani tuyaandike alafu akasema anaondoka. Lakini kabla hajaondoka akasema “Nyie muliofika leo hakikisheni munaazima madaftari Kwa wenyeji ili muandike vitu vyote vya nyuma. Wewe Zuwena utachukua Daftari kwa huyo uliekaanae hapo, sawa!?”. Nikiwa pembeni ya Zuwena nikamsikia Zuwena akiitikia “Sawa” huku nikiwa nimeshtuka mno maana Daftari wanalo liongelea sina. Kichwani nikaanza kuwaza “Hapa mbona kama naenda kuumbuka kwa mgeni sasa. Huyu mwalimu na huyu mgeni wanajua Daftari ni hili lililopo Mezani lakini ukweli ni kwamba sina Daftari. Nikijieleza kwa huyu mgeni kuwa sina daftari, nitaonekana mjinga sana kwake na naweza shindwa kuwa rafiki yake. Dah tena anaonekana anaakili sana huyu, ntaumbuka leo.”



INAENDELEA…

Ujumbe mzuri kwa Mke au Mume aliye mbali na wewe

Katika maisha ya ndoa, kuna nyakati ambazo wanandoa wanalazimika kuwa mbali kwa sababu mbalimbali kama vile kazi, masomo, au majukumu mengine ya maisha. Ingawa umbali unaweza kuwa changamoto, ni muhimu kuendelea kudumisha mawasiliano na kuonyesha upendo na kujaliana hata mkiwa mbali. Kwa bahati nzuri, ujumbe wa maandishi ni njia rahisi na ya haraka ya kufikisha hisia kwa mke au Mume, huku ukimpa moyo na kumhakikishia kuwa yupo akilini kila wakati.

The Bestgalaxy, katika makala hii tumekusudia kutoa mifano ya ujumbe mzuri kwa mke au mume aliye mbali. Ujumbe huu unaweza kumtia moyo, kumfariji, au hata kumpongeza kwa kukuweka moyoni, bila kujali umbali uliowatenganisha. Maandishi haya madogo lakini yenye maana kubwa yanaweza kuimarisha uhusiano wenu na kumfanya mwenzako ajisikie kupendwa na kuthaminiwa hata akiwa maili nyingi kutoka kwako.

Mambo ya kuzingatia katika kuwasiliana na mpenzi aliye mbali BONYEZA HAPA>>>

Ujumbe mzuri kwa Mke au Mume aliye mbali na wewe

  • Tupo mbali ila unavyonionesha upendo ni kama nipo karibu na wewe. Nakupenda na sitoacha kukupenda maana nililiandika Jina lako kwenye moyo wangu kwa wino usiofutika milele.


  • Kwenye familia yangu wewe ni malkia, mama watoto wangu na ndio familia yangu kiufupi. Kila nikikumbuka unavyonipenda, kunipa furaha, kunisaidia na kusimama nami, najiona nimekupata kama bahati. Ni maisha tu yananiweka mbali nawe ila nakupenda na natamani nirudi.

  • Nipo mbali kwasasa ila tambua Moyo na Mawazo yangu vipo kwako. Kila siku yangu ya huku haiwezi kuwa sawa bila kajua hali yako. Nakupenda sana na nakuahaidi kutunza penzi letu mpaka tutakapo onana.


  • Wanasema “Umbali si kitu kwenye mapenzi ya kweli”. Umenifanya niamini hivyo kwasababu haujapunguza penzi lako kwangu. Umekua na mimi kwa simu kila moyo unapohitaji, tumekua wanandoa ambayo ni marafiki kwenye kila hali. Nakupenda sana na asante kwa kuwa nami.
  • Huwa nakuona kwenye ndoto zangu. Na hata nikifumbwa macho kwenye maisha siku hizi sioni giza, nakuona wewe mwanga wangu. Asante kwa kuwa rafiki na mshauri na mzuri kwangu. Usijesahau kuwa nipo mbali ila nakupenda sana.

  • Ni wanawake wengi huitaji mahusiano ila wachache hukubali kuwa Mama. Asante kwa kukubari kuwa mama watoto wangu. Pia ni wanawake wechache huvumilia mume anapokua mbali lakini wewe unafanya hivyo. Asante kwa kuniheshimisha na sichoke kuniheshimisha. Nakupenda sana mke wangu.


  • Mungu akulinde huko uliko mume wangu. Unapambana sana juu ya maisha yetu. Naweza kuwa sipo vizuri katika kukushukuru kwa kila jambo ila tambua nakupenda na kukuombea kwenye kila unalofanya. Nakupenda sana mme wangu.

  • Nakukumbuka kila mara Mme wangu. Siku ya kuonana na wewe naiona kama ipo mbali sana ila kamwe siwezi punguza upendo wako. Naomba kwa mungu nafasi zetu ziwe pamoja milele, na akusaide kwenye kila jambo lako kipenzi.

Unapomtumia ujumbe mzuri mke au mume wako aliye mbali unamkumbusha kuwa unampenda, unamjali na haujamsahau. Kwaiyo jambo hili ni muhimu sana katika Mahusiano.

Zingatia haya ili usichokwe na Mpenzi wako

Kuchokwa na mpenzi wako ni mojawapo ya changamoto kubwa ambazo watu wengi hukutana nazo katika mahusiano ya kimapenzi. Wakati mwingine, bila hata kugundua nini sababu ya kuchokwa, mtu anajikuta tu amechokwa. Hili si jambo la kushangaza, kwani mahusiano yanahitaji juhudi, uelewa, na ubunifu ili yaendelee kuwa yenye afya nzuri kwa pande zote mbili(Upande wa Mwanamke na Mwanaume).

Ni kawaida kwa watu kupuuza umuhimu wa mambo madogo yanayochangia uimara wa mahusiano alafu mahusiano yanayumba. Muda mwengine, mambo hayo tukiyafanya kwa kuzidi, yanafanya watu wachokwe kwenye mahusiano.
Kwa bahati nzuri, kuna mambo muhimu ya kuzingatia ili kufanya usichokwe kirahisi kwenye mahusiano. Baadhi ya mambo hayo ni yafuatayo;

Ujumbe wa mapenzi kwa umpendae BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kuzingatia ili usichokwe na mpenzi wako

Kuwa chanzo cha furaha na Amani kwake

Hapa Duniani tukiwa binadamu huwa tunapenda sana kuwa kwenye nyakati za Amani na furaha. Mara nyingi huwa tunapenda na kuwakumbuka sana watu wanaotupa Amani na furaha maishani. Na ni ngumu sana kumchoka mtu anaekupa furaha na Amani maishani, hivyo kuwa mtu huyo kwake. Kuwa mtu ambae anajua kabisa akiwa na wewe anapata amani na furaha.
Hakikisha kunamuda ukiwa nae unaweka lawama, kesi na matatizo pembeni alafu mnafanya mazungumzo ya furaha na Amani.

Mfanye akukose kwa muda flani (Akumiss)


Ni sawa kwa na mpenzi wako pamoja kwa muda mrefu lakini isiwe ni kila mara. Kuna muda inabidi ujiweke mbali nae kidogo ili akukumbuke na kujua umuhimu wako. Wataalam huwa wanasema kitu ambacho huonekana au kupatikana kirahisi hupunguza thamani. Na kwenye mahusiano hii inawezatokea pia.

Kuna muda jiweke busy na mambo yako, usipatikane kirahisi mpaka akutafute. Hii isiwe ni ugomvi, fanya kama kumkumbusha umuhimu wako kidogo kwa kuwa mbali nae alafu jirudi tena kwake kama kawaida. Kwa lugha nyingine tunaweza sema mfanye “Akumiss” kidogo kwa muda alafu kuwa nae karibu tena. Ukiwa unafanya hivi inaweza kuwa ngumu kwa mpenzi wako kukuchoka.

Kuwa na tabia ya kumfanyia asivyotarajia

Kama upo kwenye mahusiano alafu mambo yote unayomfanyia mpenzi wako ni yanayojirudia au yamezoeleka, basi kuna siku unaweza chokwa.
Ni vema ukawa na tabia ya kufanya baadhi ya vitu bila yeye kutarajia.

Usitabilike kwenye baadhi ya mambo katika Tendo au katika Maisha ya kuishi nae kawaida.

Kutengeneza nae mambo yajayo(future)

Mahusiano ya mapenzi bila future, yanawezekana ila huwa yanafika sehemu mnachokana. Yani kama ni Tendo tu ndio huwakutanisha pamoja na mpenzi wako, basi tambua tu kuna siku unaweza chokwa au wewe mwenyewe ukamchoka mwenzako.


Mahusiano ya mapenzi ni pamoja na kuwa pamoja au kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kimaisha. Na ili usichokwe, ni vema ukawa na tabia ya kupanga mambo mtayofanya pamoja mbali na tendo. Mfano, naweza panga na mpenzi wako kwenda kwenye sharehe pamoja, kuishi nyumba moja, kununua kitu flani pamoja na hata kukutana tu mupige stori.

Ukizingatia hayo yote, unaweza fanya iwe kungumu kwa mpenzi wako mwanamke au mwanaume kukuchoka. Anaweza kuwa anatamani kila siku uzidi kwa nae kwenye maisha yake.

Utataka Tena Au (Simulizi ya Maandishi)

Nilihamia Dar es Salaam kutafuta maisha, nikitegemea msaada wa kaka yangu ambaye hakuwa ameoa. Nilipokaa kwake, sikutilia sana mkazo kujenga maisha yangu. Badala yake, niliweka nguvu kwenye starehe za usiku, yani nikifanya kumbi za burudani kuwa sehemu yangu ya nisioweza kukoswa.

Huko kwenye kumbi, nilikutana na Merry. Mwanamke wa kuvutia, mwenye mwili wa mzuri sana. Uhusiano wetu ulianza kama biashara. Yani nilimpa pesa, naye alinipa penzi. Lakini kadri tulivyozidi kuzoeana, pesa zikawa si muhimu tena. Tulianza kufurahia penzi letu bila malipo, lakini tulikua tunakutana tu katika kumbi za starehe. Hakukuwa na mipango ya zaidi ya starehe.

Baada ya muda, niliona kuwa maisha yangu hayakuwa na mwelekeo ninao uelewa. Nilirudi kijijini kujaribu kujijenga upya. Nilijihusisha na kilimo na nikapata pesa za kutosha. Nikiwa kijijini, nilisikia kwamba kaka yangu ameoa na sasa anaishi na mkewe. Habari hizo zilinipa furaha na msukumo wa kurudi mjini ili kuanza maisha yangu binafsi.

Nilipofika mjini, nilipanga nyumba yangu na kuanza kujitegemea. Kabla ya kumtembelea kaka, niliendelea na starehe zangu maana ndio kitu nilichukua nakupenda sana hapo mjini. Nakumbuka nilipofika tu, Nikawasiliana na Merry ili tukutane kwe starehe tufanye mambo yetu. Lakini Merry aliniambia kuwa ameacha mambo ya zamani na hafiki tena kwenye kumbi za starehe kwakua ameolewa. Nilisikitika, lakini nikajitahidi sana mkushawi ili nipate tu penzi lake mara moja au turudi kwenye penzi letu kabisa. Baada ya mazungumzo marefu, alikubali na akasema atanifuata nyumbani kwangu tu na sio kwenye kumbi za starare tena.
Nilimuelekeza sehemu ambayo anatakiwa aje alafu alipokuaja, nikachukua hapo na kumpeleka ndani kwangu. Alikua ameva nguo nyeusi alafu fupi kiasi cha kuonesha sehemu za juu kidogo ya miguu. Muonekano wake ulikua unavutia sana na mapigo yangu ya moyo yalikua yanaongezeka kwa tamaa tulipoingia ndani. Ni kawaida yake kunichemsha Damu kiivyo maana ni mwanamke mwenye umbo zuri la kuvutia Kila mwanaume.

Nakumbuka tulikaa dakika chache tukiongea mule ndani mwangu kisha tukaanza kufanya kilichotukutanisha. Sauti za Merry za kuimba “Aahh mmh aissh aishii” ndizo zilitawala humo ndani huku tukiwa tunacheza hiyo nyimbo kwa kunesanesa.
Alilala na mimi usiku mzima ili kunifurahisha. Raha za kucheza mziki zilizidi mpaka alipokua anaondoka asubuhi, nilimshawishi aje tena akipata muda na akakubari.

Uhusiano wetu wa kimapenzi uliendelea kwa siku kadhaa tukiwa tunafurahia sana. Lakini moja, niliona ni vyema kumtembelea kaka yangu baada ya kukaa bila kuonana toka niingie hapo mjini. Nilipofika kwake, nilipigwa na mshangao wa ghafla kwasababu nilimkuta Merry akiwa ndiye mke wa kaka yangu!

Macho yetu yalikutana kwa sekunde chache tukaona aibu, lakini tuliweka sura za kutojali kama hatujawahi kuonana. Aibu ilitawala mioyo yetu, lakini hakuna aliyeweza kusema neno. Kila mmoja wetu alijua kwamba siri hiyo haikustahili kufichuliwa. Tangu siku hiyo, ni kama tulikubaliana kuwa kimya na kuacha kila kitu kilichotokea nyuma yetu.
Kuna muda nilikua nawaza “Huyu mke wa kaka huenda sio mtu mzuri… Alikua anawezaje kulala na mimi usiku wakati kaolewa?” Lakini nilikua nikifikilia tena kwa Mimi ndio niliepambana sana kumshawishi aje kunipa penzi wakati ananiambia ameolewa, naamua kuendelea kuwa kimya tu.
Mwisho nilianza maisha mapya, nikijifunza kuwa baadhi ya siri ni lazima zibaki kuwa siri, hasa zinapogusa heshima na furaha ya wengine.

MWISHO

SMS za kumiss Mpenzi wako (Mwanamke au Mwanaume)

Katika maisha ya mahusiano ya kimapenzi, kuna nyakati ambapo hisia za kumkumbuka mpenzi wako zinakuwa nyingi sana. Hali hii hutokea pale mnapokuwa mbali au hata wakati mnakuwa karibu lakini shughuli za kila siku zinawazuia kuwa pamoja. Kumkosa mtu unayempenda kwa muda ni huleta hali ngumu sana hata mnapokua na mapenzi ya dhati. Lakini ni jambo zuri ni kwamba, kuieleza hali hiyo kwa mpenzi wako hufanya ajue umuhimu wake kwako na hata kukupenda zaidi. Yani unaweza kumtumia hata ujumbe wa sms mzuri wa kumueleza jinsi gani umemiss na akafurahi na kujua unamuhitaji.

Mfano; Ujumbe mdogo wa “Nimekukumbuka mpenzi wangu, natamani niwe karibu na wewe” unaweza kubeba uzito wa hisia zako zote na kuonyesha jinsi gani unamuhitaji mpenzi wako. Wakati mwingine, huenda mpenzi wako anajihisi mpweke au hana uhakika wa hisia zako ila akiwa anapata ujumbe wako wa kummiss, anaweza kuwa ni faraja anayoihitaji. Ni jambo dogo kulifanya lakini lenye nguvu ya kuimarisha uhusiano na kuonyesha kwamba unamjali.

Mambo yasiofaa kuwambia marafiki kuhusu Mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Katika makala hii, tumekusanya orodha ya SMS bora ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako kumjulisha jinsi unavyomkumbuka. Unaweza zitumia bura kuleta furaha kwenye mahusiano wako.

SMS za kumiss mpenzi wako

  • Nipo hapa nimetulia ila kila nikifikilia jinsi nafurahia nikiwa karibu yako, natamani nikufuate ulipo. Nakumiss sana mpenzi, natamani niwepo ulipo.
  • We ni ile tamu waliosema “haionjwi” kwasababu mtu akionja hunogewa. Tangu nilipo onja ukaribu wako, nautamani kila mara. Nakumiss sana.
  • Upo mbali mpenzi wangu, lakini moyo haujawahi punguza upendo wako. Bado nahitaji wewe uwe wangu, na Bado nahitaji niendelee kuwa wako.
  • Unauzuri wa kushangaza kama nyota angani. Nikiangalia nyota na vitu vingine vyenye uzuri wa kushangaza, huwa nakukumbuka sana wewe.
  • Kuna muda unaweza waza eti nitakuacha na maumivu niende mbali. Huko mbali nafika vipi bila wewe? Moyo unakuhitaji kila dakika. Hata sasa nimekumiss nakuwaza wewe…
  • Nakupenda sana. Tafadhali njoo unijaze furaha ya uwepo wako Kipenzi. Moyo wangu umemiss zile hisia za kuwa karibu yako.
  • Huku Moyo uliokupenda unanisumbua kuhusu wewe. Umekukumbuka sana mpenzi wangu, natamani uje useme nao kwa ukaribu. Umechoka, uhitaji kukuona wewe Tabibu.
  • Njoo niyaone yale macho yako mazuri Mpenzi. Njoo unilishe kile chakula mimi hupenda. Nimekumiss mpaka onaona giza, siioni furaha bila ya wewe ninaekupenda.
  • Kile na hitaji nikiwa na huzuni, ni wewe. Na hata kile nile nahitaji nikiwa na furaha, ni wewe. Kiufupi, maisha yangu nayaona ni mzuri nikiwa na wewe. Nimekumiss mpenzi wangu.
  • Nakupenda na ninakutaka karibu nami zaidi ya kitu chochote ulimwenguni. Nakuhitaji zaidi ya chupa ya maji jangwani. Uko wapi mpenzi?

Sms hizi za kumiss ni nzuri kwa walio kwenye ndoa (Mume au mke) na hata kwa wasio kwenye ndoa (Wapenzi). Kikubwa unatakiwa kuchagua sms au ujumbe unapenda na hali yenu. Na pia ni muhimu kujua ni wakati gani wa kumtumia sms huyo umpendae.