All posts by Admin

Jinsi ya kutumia kipengele cha “WhatsApp screen share”


WhatsApp ni mtandao unaoleta pamoja watu kupitia groups, channels na kurahisisha sana mawasiliano. Ni moja ya mitandao mkubwa ulimwenguni milikiwa na Meta. Unatumiwa na watu kuwasiliana na watu wengine walio ndani na nje ya nchi.

Kwenye mtandao wa WhatsApp Kuna vipengele vingi sana mtu unaweza tumia katika kuungana au kuwasiliana na watu wengine. Katika vipengele hivyo, Kuna kipengele kinaitwa “WhatsApp screen share”.

WhatsApp screen share ni kipengele cha WhatsApp kinachowawezesha watumiaji wa WhatsApp kuoneshana Screen za simu zao. Kupitia kipengele cha hiki cha WhatsApp, unaweza kumuonesha mambo yalio katika kioo cha simu yako mtumiaji mwingine wa WhatsApp. Lakini hii inafanyika pindi mnapopigiana video call.

WhatsApp ilikuja na kipengele hiki cha WhatsApp screen share rasimi mwaka 2023 lakini huduma kama Google meet na Zoom zina uwezo kama huu pia. Katika makala hii, tutajikita katika huduma  ambayo inapatikana kwenye mtandao wa WhatsApp.

Jinsi ya kutumia kipengele cha “WhatsApp screen share”



Ukiwa unataka kumuonesha mambo yalio kwenye screen ya simu yako mtu mwingine kwa kutumia WhatsApp Screen share, fuata hatuna zifuatazo;

  • Mpigie au akupigie Video call
  • Mukianza video call, bonyeza Vidoti vitatu
  • Changua “Share screen” kwenye chaguzi zitakazotokea.
  • Baada ya hapo, utatakiwa kukubali kuwa Kila kinachofanyika kwenye screen ya simu yako, kionekane kwa yule mtu ulienae kwenye video call.
  • Ukikubari tu, WhatsApp wataanza kuionesha screen yako kwa yule mtu ulienae kwenye video call.

Kupitia kipengele hiki, unaweza kumuonesha mtu movie/video zililopo kwenye simu yako, kumfundisha Baadhi ya vitu kupitia simu yako na hata rekebisha matatizo kwa kufuata muongozo wake.

Jinsi ya kuona sms za WhatsApp kwenye simu nyingine BONYEZA HAPA>>>

Tabia ya Usiku (Simulizi ya Kusoma)

Siku moja nilikua nimefunga kiduka changu Usiku na kuanza safari ya kuelekea nyumbani. Ulikua ni usiku sana na nilikua natembea kidogo kidogo huku nikijiamini kwakua sio mara yangu ya kwanza.
Huko nyumbani nilikokua naelekea kilikua ni chumba changu nilichopanga hapo mjini. Palikua na umbali kidogo ambao ningeweza kuchukua usafiri kama ningekua nina haraka sana ya kufika lakini sikuchukua usafiri maana nilikua nina mpango wangu mwingine ambao nimepanga kufanya nikiwa njiani.

Mpango wangu ulikua ni kukutana na Madada wanaotembea usiku ili niende kulala nao. Tabia hii nilikua nimeanza miezi mwili iliopita. Ilikua ni tabia tamu sana kwangu maana niligundua kuna madada wazuri wanatembea barabarani ukiongea nao vizuri, wanakubari kulala nao.

Sasa siku hiyo nilikua natembea huku nikizingatia madada ninaopishana nao kama wanaingilika au vipi. Nakumbuka nilifika kwenye kibarabara kimoja kilichokua na giza nikaona Dada mmoja hivi mbele yangu anatembea kidogo. Alikua amevaa vinguo vifupi sana alafu nilipokua natembea nyuma yake, alipunguza mwendo kidogo.
Nilipo mwona amepunguza mwendo tu, nikajua huyo dada ndio moja ya Madada ninao watafuta maana nao hufanya hivyo. Basi sikupoteza muda, nilimsogelea tukaanza kutembea pamoja huku tukifanya maongezi. Alikua kashika Mkoba alafu anangozi nyeupe kiasi na mwili mkubwa kidogo kuliko mimi. Ila Mimi mwili wa hivyo ndio huwa nataka.
Nilimshawishi yule dada kwa pesa tukalale nae nyumbani kwangu na yeye alikubari. Nilimpeleka mpaka nyumbani, tukaingia ndani. Nilikua nimepanga chumba kimoja ila kizuri na kikubwa. Hivyo alipoingia hakukua na michakato mingi sana zaidi ya kulala nae kama tulivyokubaliana.
Mwili wake mkubwa mkubwa ulifanya nipagawe sana katika mchezo. Yani kwenye mchezo nilikua nikidondoka, yeye alikua anaenda juu na kurudi chini. Alifanya sekunde moja nahisi joto, sekunde nyingine nihisi baridi mpaka nikawa sielewi.
Nakumbuka tuliucheza ule mchezo mpaka nikachoka mimi. Yeye alikua haoneshi kachoka kabisa ila katika kunihudumia alikua yupo vizuri.

Baada ya mimi kuchoka, alidai anataka kwenda chooni mara moja. Mimi nilimueleza kuwa choo kipo nje na nikataka kumsindikiza maana huo ulikua ni usiku. Lakini yeye alikataa kusindikizwa.

Kabla ya kutoka njee kwenye chooni, alifungua Mkoba wake na kutoa chupa ilioonekana kama marashi kisha akawa kama anajipulizia hivi ingawa kwa asilimia kuwa ile kilichokua kwenye chupa kilikua inasambaa mule ndani.
Nikimuuliza “Unajipulizia nini?” Akaniambia “Natoa harufu kabla sjaenda chooni huko. Si unajua sisi wanawake tunatakiwa kuwa vizuri?” Mimi nakajibu “hahaha sawa” bila kuwaza mbali.

Baada ya kumaliza kujipulizia, akamuona anatoka njee kuelekea alilokua anasema anaenda. Baada ya dakika 2 za kumsubiri, nilikuta ghafla macho yanakua mazito sana. Kwa haraka haraka nikajua ni uchovu wa zoezi tulilolifanya na yule dada. Lakini baada ya dakika kuongezeka, nilichukuliwa na usingizi mzito sana bila kujitambua. Kiufupi sikuelewa chochote kilichoendelea.

Usingizi huo ulikata mida asubuhi jua likiwa limechomoza kabisa. Niliangalia mazingira niliopo baada ya kuamka nikachanganyikiwa maana vitu vyangu vingi sikuviona. Nilikua nipo kitandani, mlango upo wazi, vitu vingi vya muhimu havipo alafu vilivyopo vimevurugwa hovyo hovyo. Jambo hilo lilifanya kumbukumbu zirudi na kuwaza kuwa huweda yule dada niliemchukua usiku alinipulizia Dawa ya usingizi na kafanya yote hayo.
Sikua na lakufanya kumpta ila ndio hivyo tabia yangu iliniponza nikapoteza baadhi ya vitu vyangu. Muda mwingine kuchukua mtu usiemjua na kumpeleka kwako ni sawa na kukaribisha matatizo.

Hii ilinitokea kipindi cha nyuma sana na sijui kama madada wa mtindo huu wapo mpaka sasa.

Simulizi Bora za kusoma katika The bestgalaxy BONYEZA HAPA>>>

Umecheza game la Delta Force Mobile kwenye simu yako?

Game la Delta Force Mobile ni game la first- person shooter lililotengenezwa na NOVA logic kwaajili ya simu za mkononi. Limekua likiangaliwa na watu wengi sana wanaotumia simu za mkononi kucheza game za online zinazohusisha kucheza pamoja na wengine. Hapa nazunguzia watu wanaocheza game la Warzone mobile, Blood strike na hata Arena breakout mobile au game nyingine kama hizo.

Kwenye kulicheza game la Delta force mobile, mtu unahitajika kutumia internet maana ni game la online. Lina Mode zaidi ya moja unawezoweza kucheza ukiwa na watu wengine kutoka pande mbalimbali Duniani. Mode zake zote ni nzuri ila inategemeana na umeipenda mode gani. Unaweza cheza mode ya Operations, Warfare au Black Hawk Down Kisha unachagua mode ambayo ni nzuri zaidi kwako. Watu wengi hupenda Warfare maana ni mode ya haraka inayofurahisha.

Katika muonekano, game la Delta Force Mobile Lina graphics nzuri sana zinazofanya uone picha nzuri zinazofanana na uhalisia unapolicheza. Na uzuri ni kwamba unaweza kupunguza ubora wa picha au kuongeza.

Chaguo la kuweka picha yenye ubora wa kawaida au ubora wa hali ya juu ni wako. Kama simu yako inaweza kuhimili game katika picha zenye ubora wa juu, basi unaweza kuongeza ili iwe na picha kali zaidi.


Hasara ya kucheza game zikiwa kwenye picha za ubora wa hali ya juu ni kupata moto kwa simu au kukumbana na lags. Kwaiyo ukitaka kuongeza ubora hakikisha simu yako inaowezo wa kuhimili pia.


Kulicheza game la Delta Force Mobile




Ili simu yako iweze kulicheza game la Delta Force Mobile inatakiwa iwe na vigezo vifuatavyo:
Kwa Android simu itatakiwa kuwa na angalau, Snapdragon 865, 8GB za RAM na Android 10 au zaidi. Kwa simu za iOS iphone itatakiwa kuwa na angalau A13 chip, 4GB za RAM na iOS 14+ (Ambayo ni iPhone 11)


Unapoliingiza game kwenye simu, unatakiwa pia kuwa na nafasi ya 12GB katika Storage. Hii iwe ni unatumia Android au iOS.

Kwasasa game la Delta Force Mobile limetoka rasimi na unaweza cheza kwa kutumia simu yako ya Android au iOS (iPhone). Limeachiliwa rasimi 22 Apr 2025 kwa watu wote ulimwenguni.

Kama unataka kujaribu kwasasa, pakua hapa chini.

Download Delta Force Mobile Android>>>

Download Delta Force Mobile iOS (iPhone)>>>

Sms za kulalamika kwa mpenzi wako (Mwanamke au Mwanaume)



Katika mahusiano ya mapenzi, si kila wakati mambo yanakwenda kama unavyotarajia. Kuna nyakati unaweza gundua kuwa mpenzi wako amebadilika, haonyeshi tena upendo na kujali kama zamani. Labda ameanza kuwa mbali, hajali hisia zako, au hata anaonyesha dalili za kuzingatia katika uhusiano wenu. Hali kama hizi zinaweza kuumiza moyo na kukufanya uhisi huzuni, mashaka, au hata hasira.

Pia, kuna wakati unaweza kugundua kuwa mpenzi wako amekusaliti kabisa. Hakuna kitu kinachouma kama kugundua kuwa mtu uliyempenda kwa dhati ana mtu mwingine au aheshimu uaminifu wenu. Usaliti unaweza kuleta maumivu makubwa na kukufanya ujihisi si wathamani.

Mtu unapopitia katika hali kama hizi, unaweza kuhitaji kumwandikia mpenzi wako ujumbe wa kulalamika, ili aelewe jinsi kitendo chake kilivyokuathiri na, pengine, abadilishe tabia yake , kiwezekana. Kutuma ujumbe wa kuelezea hisia zako kunaweza kuwa moja ya kutoa hisia zako na kufungua mzingo kifuani. Katika makala hii, tumekuandalia orodha ya sms za kulalamika ambazo unaweza kumtumia mpenzi wako ili kuelezea hisia zako kwa bila kupoteza muda.

Simulizi bora za kusoma katika The bestgalaxy BONYEZA HAPA>>>

Ujumbe wa kulalamika kwa mpenzi wako





Moyo wangu upo kwako ni vile tu Umeamua kuubuluza. Unayoyafanya yananiuza na Sina chakufanya kukukumbusha kuwa ulisema milele utanipenda. Ok, Fanya unachofanya ila milele usisahau ninakupenda!



Mimezikumbuka zile siku za furaha , zile siku tulikua tunatafutana kila mara na kuambiana hisia zetu. Na bado nakumbuka tuliambizana “unanipa furaha, sina mwingine, ni wewe tu”. Lakini sasaivi wewe sijui umepata mwingine kakubadilisha… eti ni umesahau???



Ulikuja kama mwanga kuyaangaza maisha yangu, ulileta matumaini na ndoto lakini ghafla unaniacha nikiwa nimevunjika moyo na kukata tamaa ya kupenda tena. Asante kwa yote lakini!



Natamani miaka ambayo nimekaa na wewe isingetokea katika Maisha yangu. Zile kumbukumbu nilizofurahia na wewe zinaniumiza kwasasa. Ninatamani kufuta kila kumbukumbu yako ila ndio hivyo uliniweza, nikakupenda kweli na sasa umenisaliti ninaumia.



Nitajuta milele vile nilikupenda bila kujua dhamira yako na kukuamini. Nilikupa kila kitu nilicho hisi kitakufurahisha; lakini katika malipo, umenitoa machozi kwa maumivu yasio isha.



Najitahidi kila mara kuwaza na kukufanyia mambo yatakayo kupa furaha lakini wewe umekua ukinilipa mambo yanayoniumiza. Najua hii inamaana; Pamoja na kukupenda, Bado haunipendi. Asante sana, naendelea kukupenda ila nimekuelewa!



Nilikupenda bila sharti lolote na bila kuuliza kurudishiwa ila ulichukulia upendo huo kuwa udhaifu wangu. Siwezi sema mengi ila umeniumiza vya kutosha sasa, niache niendelee na maisha yangu.



Nilikuamini kwa moyo wangu wote, lakini umeshindwa kuelewa hilo. Umenifanya nijifunze kuto kumuamini mtu hata nikimpenda sana. Ninakuchukia, lakini nashukuru kwa somo! Nashukuru kwa kunivunja moyo pia!

Huu ndio mwisho wa orodha yetu ila Kuna mambo mengi sana katika The bestgalaxy unaweza furahia. Kikubwa Endelea kuwa karibu nasi ili kujifunza mengi!

Jinsi ya kutengeneza pesa katika Facebook (Content Monetization)


Facebook ni mtandao mkubwa wa kijamii unaomilikiwa na kampuni ya Meta na unaunganisha watu wengi Duniani. Watumiaji wa mtandao wa Facebook wanaweza furahia kuwasiliana na wepandwa wao, kuangalia picha, video na kusoma mambo mbalimbali.


Katika kufurahia mambo hayo, Facebook nimekua ni moja ya mitandao muhimu kwa watu wanaojiajiri. Ina vipengele vingi sana vinavyoweza msaidia mtu aliejiajiri, kukuza hudama yake. Mfano mzuri ni kile kipangele kutangaza biashara; mtu anaweza kutumia upande huo kutangaza biashara au huduma yake.


Mbali na upande huo, Facebook wana program iitwayo “Facebook Content monetization” ambayo inawawezesha watu kutengeneza pesa kwa content zao. Yani hapa unaweza lipwa kwa vitu unavyoandika na kupost, video na picha unazopost. Na unaweza fanya hivyo kupitia akaunti unayoitumia kila siku au Facebook page kama unayo. Ila kama unatumia akaunti ya kawaida utatakiwa kuweka kwenye “Professional mode” kwanza.

Jinsi ya kutengeneza video za katuni kwa simu ili kutengeneza pesa BONYEZA HAPA>>>

kuanza kulipwa katika Facebook Content monetization



Ili uanze kulipwa katika Facebook utatakiwa kuanza kujiunga na hiyo Facebook monetization. Na kabla haujajiunga, utatakiwa kutimiza vigezo vyao lakini vigezo vyao huwa vimetofautiana na hubadilika kutokana na kwamba mfumo wao kwa sasa upo kwenye maboresho.


Ukihitaji kuwavutia kwa kipindi hiki ili uingizwe kwenye program yao, ni vema ukawa na kuanzia followers 5000 na video zilizoangaliwa zikawa na jumla ya dakika 60000.

Pia ni vema ukatengeza video zako mwenyewe maana kuchukua video za watu bila maboresho yoyote ni kosa litakalokupunguzia nafasi ya kutengeneza Pesa.

Jinsi ya Kuangalia kama upo tayari kulipwa na Facebook

Ukitaka kuangalia kama tayari umekidhi vigezo vya kuingia kwenye Facebook Monetization program, nenda kwenye Dashboard ya akaunti yako alafu ingia kwenye kipengele cha “Monetization”. Ikiwa utakutana na neno “eligible” au kipengele cha “Content monetization ” kimefunguka, basi fahamu kuwa akaunti yako inaweza ingizwa kwenye Facebook monetization program.


Baada ya kuwa vizuri sehemu hiyo, unaweza pokea ujumbe kwenye email yako kuwa wamekuarika kwenye program ya Content monetization program bila hata kufanya Chochote au ukakuta to vipengele vya kutengeneza pesa vimejifungua kwenye Dashboard. Unaweza pata hata notification kwenye Facebook ikikwambia umekua “eligible” hivyo set taalifa muhimu ili ulipewe.



Zingatia: kwasasa Facebook Content monetization program ipo kwenye marekebisho hivyo kuna namna utaratibu wake haupo sawa. Hasa kwa nchi za huku Afrika mashiriki. Lakini kupata content monetization na kutengeneza pesa inawezekana!

Kama unahitaji mafunzo kamili ya yatakayo kuelezeza jinsi ya kuanza na kufanikiwa kutengeneza pesa katika Facebook, unaweza kuchati na sisi kwa kugusa HAPA au kitufe hapa chini.

Utapewa mafuzo yote muhimu kwa Tsh 25,000 TU. Mafuzo haya yatakuongoza jinsi ya kutengeneza pesa katika Facebook na mbinu za kufanikiwa.

Ni Mafunzo mazuri kwa hata walio na followers 0 maana yanaweka wazi namna ya kukua katika Facebook pia.

Mambo ya kuepuka  ili kutengeneza Pesa katika Facebook BONYEZA HAPA>>>

Mukijua mambo haya hamuwezi achana na mpenzi wako kirahisi

Unaponda sehemu flani ngeni kuishi, unaweza kutana na changamoto au mambo tofauti kwako. Mengine yanaweza kuwa ni yakushangaza na mengine yanaweza kuwa magumu ila baada ya kuishi kwa muda flani na kuyajua vizuri mambo ya hapo, unazoea na kuanza kuishi sehemu hiyo kama ni yakamaaida. Yani hata kama jirani wako umemkuta ni mkorofi, baada ya muda unaweza mchukulia kama alivyo na maisha ya ujirani yakaendelea.

Unapoingia katika mahusiano nako huwa kuna mambo flani hivi yanaweza kuibuka na kuleta changamoto ila wote wapenzi wawili mukiyajua mutaendelea na mapenzi ya muda mrefu bila kuachana. Yani mambo haya kama hata mmoja wenu akiyajua, ataweza kuokoa mapenzi yenu Kila yanapotaka kuvunjika na hata kuyatunza yewe imara. Lakini mukiyajua wote, inakua poa zaidi.

Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>

Mambo ambayo mukijua inakua sio rahisi wewe na mpenzi wako kuachana

Kutoelewana sio mwisho wa mahusiano

Wengi kwenye mapenzi ya sasa huwa wasipoelewana, wanaachana kirahisi sana. Yani wanaweza anzisha mwezi huu mahusiano alafu baada ya mwezi kuisha, wanaishia kwenye kutoelewana alafu wanaachana.


Ukweli ni kwamba kutoelewana kwenye mahusiano hakupingiki, na kama kila mahusiano yangekuua yanaishia pale wapenzi wasipoelewana katika mambo flani, basi kungekua hakuna watu wenye mahusiano ya kudumu.


Ili mahusiano yadumu, inabidi mufahamu kabisa kuwa kuna siku mnaweza kuwa hamuelewani kwasababu ya mambo mbalimbali. Ila nijukumu lenu wote kuyaweka mahusiano vizuri. Mukiwa na uwezo wa kutafutana bila aibu baada ya kutoelewana, mahusiano yenu yatadumu sana.

Kuchepuka kuna hasara kubwa kuliko faida

Asilimia kubwa ya watu wanaochepuka kwa wapenzi wao huishia kujilaumu sana. Na hujilaumu kwasababu kuchepuka kuna hasara kubwa nyingi kuliko faida. Kuchepuka kuna kufanya tuingie kwenye hatari ya magonjwa kama HIV. Alafu mbali na hayo, pia unaweza jiingiza kwenye utumwa wa Siri ambazo zinaweza kukutesa kwa miaka.


Mfano; Unakuta mtu anachepuka alafu kapewa au kumpa mimba mchepuko. Mtoto anazaliwa kwa siri huku mtu aliechepuka anashikiria Siri moyoni mpaka Raha ya maisha anaikosa.
Mukijua mapema haya kama wapenzi, nguvu ya kusalitiana inapungua kidogo.

Kuna muda mnapata hasira kwasababu mnapendana

Mwanamke au Mwanaume anaweza kufoka au kupandwa na hasira kwenye jambo dogo sana. Hizo hasira huwa zinakuja kwasababu ya upendo tu na sio jambo jingine.

Mukijua kuwa kunamuda munatiana hasira kwasababu mioyo yenu inaupendo, mtaweza kuwa kwenye mahusiano kwa muda mrefu sana. Maana asilimia kubwa ya wanaolijua hili, hujielewa kwanza wao alafu huelewa na wapenzi wao wanapokua na hasira.


Mfano; Kwenye ndoa hapa ndio unaweza kukuta mwanamke au mwanaume anakasirika sana na kumrushia maneno mpenzi wake anapochelewa kurudi. Kinachomfanya akasirike sana ni upendo tu na sio jambo jingine. Usipolielewa hili kwa mpenzi wako unaweza muona mbaya kwao.

Maongezi ya usiku ya kila mara ni muhimu

Mukiwa kama wapenzi mnaojenga mapenzi ya muda mrefu, kufanya mazungumzo au mawasiliano ya kila mara usiku ni muhumu sana. Yani kutenga nusu saa au saa moja la kuongea kila siku kutawafanya muwe karibu zaidi kifikra na kihisia.

Mtakua na uwezo wa kupanga mipango yenu pamoja, kujuana zaidi na kujenga imani.
Mbali na hayo, usingizi unaokuja baada ya kuongea na mpenzi wako huwa unakua mzuri sana. Hivyo ni njia moja ya kufanya mulale vizuri.

Kijana hizi ni athari za Wanawake wakubwa sana (Majimama/Mishangazi)




Wakati baadhi ya vijana Wakiume wanaongelea na hata kutafuta kabisa Majima au Mishangazi, hebu tunangalie athari zake. “Mishangazi” au “Majimama” ni majina ambayo kuna watu hutumia wakiwa na maana “Wanawake wakubwa wanaoingia kwenye mahusiano na vijana wadogo.” wanawake hawa wapo katika jamii zetu na kumekua na simulizi nyingi za vijana kujihusisha nao kimapenzi.

Mahusiano kati ya wanawake wakubwa na vijana yanaweza kuwa ni upendo toka moyoni kabisa. Yani wanaweza kuanza kwa mazoea ya kuwa karibu alafu mwisho, wakajikuta kwenye penzi zito. Ila kwakua wanasema, Mapenzi hayana umri, tunaweza sema ni jambo lisiloshangaza sana.

Lakini pia baadhi ya mahusiano ya namna hii huwa ni kama wanabadilishana pesa au maisha mzuri kwa mpenzi. Yani hapa Kijana wa kiume anawezakua anatoa mapenzi huku Mwanamke mkubwa akitoa pesa au maisha mzuri kwa Kijana. Kwaiyo Kuna namna Kijana wa kiume anaweza faidika hapa.

Pamoja na yote ambayo kijana wa kiume anaweza pata au kufaidika kwenye mahusiano ya namna hii, Bado sio Mahusiano salama. Kijana anaweza pata athari mbaya kubwa kwenye maisha yake anapokua na majimama au Mishangazi. Athari zinazo zungumziwa hapa ni zifuatazo:

Kijana hizi ni athari za Wanawake wakubwa sana (Majimama/Mishangazi)

Magonjwa



Kama tunavyo fahamu, magonjwa kama vile HIV huwa yanaweza ambukizwa kwa kushariki Ngono zembe. Ngono zembe ni kushiriki tendo la ndoa bila Kinga yoyote.

Kama upo kwenye mahusiano na mwanamke mkubwa, Tendo hili linaweza kuwa ni tendo la kawaida sana. Mnaweza zingatia kinga siku ya kwanza lakini ya pili mukazitupia mbali kwa kuamini haziwafurahishi kwenye tendo.

Sasa ikiwa mmeamua kutotumia Kinga Kuna hatari kubwa ya kuambukizana virusi ya ukimwi na magonjwa mengine.


Kuwachukulia poa wanawake wengine



Kijana wa kiume anapoingia kwenye mahusiano na mwanamke mkubwa anaweza jikuta anaanza kudharau mwanamke wa umri wake. Yani anaweza anza wachukulia poa sana mwanamke wa umri wake maana tayari anaoneshwa au kufanyiwa vitu vingi ambayo wanawake wengine hawafanyi.


Hali hii inaweza kumfanya huyo Kijana ajiamini sana anapokua na Mwanamke wengine. Lakini kujiamni huko ni matokeo ya kugundua kuwa mwanamke wengine hawajui mapenzi.

Kugeuka tegemezi


Kijana wa kiume akipata mwanamke mkubwa anaempa pesa kisa mapenzi, kuna hatari kubwa ya huyo Kijana kuwa tegemezi kwenye maisha yake. Anaweza fikia wakati hata akiachwa na jimama anaona maisha yake yameharibika.


Kwa kawaida mwanaume anatakiwa kubeba Majukumu, kujitegemea na kutegemewa. Huyo mwanaume akizoeshwa kutegemea mwanamke, inakua ni ngumu kwake kuchukua Majukumu, kujitegemea na kutegemewa tena. Huo kwake unakua ni mzigo mkubwa sana.

Kuingia kwenye migogoro



Baadhi ya wanawake wanaoitwa “Majimama” au “Mishangazi” ni wake za watu au Mama za watu. Kutokana na hili, pamoja na yote wanayofanya, Bado ni wanawake ambao wana ndungu na jamaa kwenye maisha yao.

Kijana anaweza ingia kwenye migogoro ya kifamilia bila kujua. Ukiwa kama kijana, unaweza kuwa chanzo cha mke na mume kukosana, unaweza chukiwa na watoto wake au ndungu. Mongogoro mingi inaweza kuibuka hapa.

Jinsi ya kutengeneza App ya simu

Kikawaida, kutengeneza app ni mchakato unaohusisha kuandika “Code” ambazo ni maelezo katika lugha ya computer. Hivyo ukitaka kutengeneza app kwa utaalam zaidi, unapaswa kujua namna ya kuandika Code katika lugha mbalimbali za computer.

Kwa mtu unaetaka kuwa mtaalam wa kutengeneza app za simu, unaweza jifunza lugha za computer kama vile JavaScript, Kotlin, Java, Python, Java na nyinginezo. Ukiwa mtaalam wa lugha za computer na ukawa na uwezo wa kutengeneza app, alafu utaitwa “App developer”.


App developer anaweza kuingiza pesa kwa kuajiliwa sehemu mbalimbali anazoweza kufanya kazi kama “Developer”. Mfano; Kampuni ya Meta ambayo inaumiliki Instagram, Facebook na WhatsApp, huwa zina watu ambao hufaamika kama “Developer” ambao huusika na maboresho ya app hizo. Ni wachache Duniani ila huingiza pesa nyingi sana.

Mbali na kuajiliwa, App developer anaweza ingiza pesa kwa project zake mwenyewe. Yani anaweza pambana kutengeneza kitu anachokiwaza alafu kikamuingizia pesa kwa kukiuza au kukiingiza katika mifumo itakayomuingizia pesa. Mfano mzuri ni Kutengeneza game linalo muingizia pesa au kuwatengenezea watu app za kurahisisha mambo yao ya kibiashara.

Jinsi ya kutengeneza Pesa kwa kucheza games mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Jinsi ya kutengeneza app za simu kwenye simu za bila  kujua Code

Pamoja na hayo yote, sio lazima mtu uwe mtaalam ndio utengeneze app za simu. Mtandaoni kuna tuvuti/website nyingi ambazo zimerahisisha mchakato wa kutengeneza app za simu.

Website nyingine zinarahisisha mchakato wa kutengeneza app kiasi ambacho mtu yoyote anaweza kutulia na zitumia kutengeneza app za Simu. Unaweza usijue kabisa maswala ya lugha za computer lakini ukafanikisha kutengeneza app kupitia website hizo.

Ukizitafuta website za mtindo huu katika mtandao, utazikuta nyingi sana lakini asilimia kubwa zinahitaji ulipie pesa. Mfano mzuri ni tuvunti ya Andromo, AppMySite na Appypie. Ni kati ya website rahisi kuzitumia katika kutengeneza app za simu (Android na iOS)lakini ili kupata uhuru kwenye app yako, utatakiwa kulipia.

kutengeneza app za simu kwenye simu BURE


Lakini swala la kulipia, lisikukwamishe maana Kuna tuvuti nyingine zinakupa uhuru mkubwa kabisa bure. Mfano wa tuvuti hizo ni hii hiitwayo “Appcreator24” au tuvuti iitwayo “Appsgeyser“. Website hizi unaweza kuzitumia kutengeneza app za simu kwa urahisi sana na bila kulipia.

Hapa the bestgalaxy tunakupa mwanga wa jinsi ya kutengeneza app ya simu kupitia tuvuti ya Appcreator24. Hapa chini tumekupa hatua muhimu zakuchukua ili kutengeneza app kwenye tuvuti hiyo ila utatakiwa kuwekeza muda wako kujifunza kiundani.

  1. Ingia kwenye website ya Appcreator24 ujisajili
  2. Bonyeza “Create app” kuanza kutengeneza app
  3. Jaza taalifa za app unayotaka na uchague mtindo wake
  4. Maliza kwa Download app yako ikiwa kama Apk au AAB file

Baada ya hapo utachangua wewe kwa kuipeleka. Unaweza kuiweka kwenye simu yako au kuipeleka sehemu kama Playstore ili watu waipakue kisha upate pesa kwa kuonesha matangazo. Na kama unataka kuiboresha au kuiweka vizuri, basi utaingia kwenye hiyo website ya Appcreator24 ili kurekebisha.

Pamoja na yote hayo, fahamu kuwa website nyingi za kulipia ndio hutumia kutengeneza app nzuri zaidi. Na pia, kujua code kunaweza kufanya uwe bora zaidi katika kuzitumia tuvuti zote za kuunda app. Watu engine hutumia AI kuandika Code katika kuunda app na hufanikiwa kutengeneza app nzuri sana. Lakini sio lazima kufanya hivyo, unaweza tengeneza app bila kujihusisha na code!

Simulizi Bora za kusoma au kufuatilia katika The bestgalaxy

Katika moja ya mambo watu hufurahia kwenye simu zao ni kufuatilia simulizi mbalimbali kwa kusoma au kusikiliza. Hili ni jambo zuri ambalo mtu anaweza kulifanya kwenye simu mbali na kuwasiliana na watu. Sio kila muda mtu anaposhika simu anawasiliana na watu, Kuna muda anawezakua anafuatilia simulizi anazozipenda toka The bestgalaxy au sehemu nyingine.

The bestgalaxy ni sehemu unayoweza kujifunza mambo mbalimbali kuhusu mahusiano, Teknolojia na mengineyo. Katika the Bestgalaxy mtu unaweza pata simulizi pia. Na simulizi nyingi za The Bestgalaxy zimejikita kwenye mahusiano kwasababu ya kuburudisha na kuelimisha kwenye upande huo.


Katika makala hii tumeorodhesha simulizi chache nzuri za kusoma unazoweza pata kutoka The bestgalaxy. Kama unapenda kusoma simulizi za mahusiano/Mapenzi, basi zingatia orodha hii.

Hizi ni Simulizi Bora za kusoma au kufuatilia (Mapenzi na Maisha)

SUKARI YA DADA

Sukari ya dada ni simulizi inayomuhusu Kijana ambae alienda Dar es salaam kwaajili ya kufanya kazi za ndani baada kutofanya vizuri kidato cha nne. Kwenda huko ilikua ni njia pekee alioiona itamsaidia maishani kwa wakati huo lakini katika kuelekea anapohitaji, anakutana na changamoto nyingi sana kutokana na ujana.
Unaposoma simulizi hii, unapelekwa moja kwa moja katika kuyaona maisha ya kijana huyo. Lakini katika kuisoma simulizi ya SUKARI YA DADA, unatakiwa kuwa ni mtu uliefikisha umri wa maika 18 au zaidi.
Ukimaliza kuisoma simulizi ya SUKARI YA DADA mpaka mwisho, unaweza soma pia simulizi nyingine 2 ambazo ni UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA kwasababu zinauhusiano. Tutafafanua zaidi kuhusu simulizi hizi huku tukiwa tunaendelea na orodha.

UNANIITA?

Simulizi hii ni fupi na inamhusu kijana mdogo ambaye kazi yake ni kuendesha bodaboda mjini. Siku moja, anakutana na mteja mpya aitwaye Zena, mwanamke mrembo anayekabiliwa na changamoto katika uhusiano wake wa ndoa. Kupitia safari zao pamoja, Zena anafunguka kuhusu matatizo anayopitia na jinsi anavyojisikia kupuuzwa na mume wake. Kijana huyu anajaribu kumpa ushauri wa kumsaidia kuboresha mawasiliano na mumewe.
Hii ni moja ya simulizi nzuri sana lakini ni fupi.

UTAMU WA JUMLA

Unaposoma simulizi hii, unafuatilia maisha kijana aliyekulia Tabora na baadaye kuhamia Dar es Salaam kwa ajili ya masomo ya biashara chuoni. Akiwa chuoni, anakuwa na urafiki na Jimmy. Unaangalia maisha yake na changamoto anazopitia akiwa kama kijana amambe amesoma chuo na akiwa na ndoto au matarajio ya kufanikiwa maishani.
Hii simulizi inahusiano na simulizi 2 ambazo ni SUKARI YA DADA na MZIGO WA WAKUBWA. Kama umeisoma simulizi nzima ya SUKARI YA DADA na unataka simulizi nyingine, basi soma simulizi hii. Lakini unapoisoma, umri wako uwe umefia miaka 18.

SIRI NA SHEMEJI

SIRI NA SHEMEJI ni simulizi fupi inayomfuata Anisa, mwanamke mwenye heshima na upendo kwa mume wake, Kevin. Wakati ndoa yao ni changa, Anisa anabeba siri nzito kuhusu uhusiano wake wa zamani. Jambo hilo linamletea Anisa wasiwasi na hatimaye kusababisha mgogoro mkubwa katika ndoa yake na Kevin. Simulizi hii inagusia mada za uaminifu, siri, na msamaha katika mahusiano ya ndoa.
Ni simulizi isio ndefu lakini ni nzuri na inaweza kukupa burudani bila kupoteza muda wako sana.

MZIGO WA WAKUBWA

Katika simulizi hii, unaingia katika Maisha ya kijana anaekua na kuanza kuyazingatia maisha huku akishikilia Mahusiano ya mapenzi. Kijana huyu katika simulizi, anafanya baadhi ya maamuzi ya kukimbia mizingo akihisi ni yawakubwa.
Kama umeisoma simulizi ya SUKARI YA DADA na UTAMU WA JUMLA, basi simulizi ya MZIGO WA WAKUBWA ni simulizi unayotakiwa kumalizia kuisoma. Simulizi hizo tatu zinauhusiano na msomaji anashauriwa kuzisoma zote Loki kupata mocha moja nzuri na yaajabu sana.

Unachotakiwa kujua kuhusu simulizi ya SUKARI YA DADA, UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA

Simulizi ya SUKARI YA DADA, UTAMU WA JUMLA na MZIGO WA WAKUBWA ni simulizi unazoweza zisima pamoja ili kupata picha nzuri. Zimesimuliwa na watu tofauti ila zinakupa picha moja nzuri sana inayohusu mahusiano(Mapenzi)na maisha kwa ujumla. Na katika upande wa majina, kila jina Lina maana katika simulizi. Mfano; jina la MZIGO WA WAKUBWA katika simulizi lina maana “Majukumu”.

MZIGO WA WAKUBWA 01  (Simulizi ya Kusoma)




Tulikua tupo mimi na rafiki yangu Samsoni kwenye chumba chetu tunacholala ambacho watu huita Geto. Ilikua mida ya kama saa moja au mbili usiku hivi alafu muda huo rafiki yangu alikua ananihadithia mechi ya mpira ambayo imetoka kumalizika saa 2 zilizo pita na sikwenda kuiangalia kwenye vibanda vya mpira siku hiyo kutokana na mawazo. Mawazo yalifanya kichwa changu kiwe vibaya sana muda huo kiasi kwamba nilikua naonekana kumsikiliza Samsoni lakini kiukweli nilikua hata simuelewi japo nilikua nacheka kila akicheka na kuitikia “Ebwana ee” ili asigundue kua akili yangu haipo kabisa kwenye anayonisimilia.

Katikati ya hadithi zake za mpira tukasikia simu imeanza kuita katika kisehemu tunachozichaji simu kilichokua pembeni kidogo ya dirisha la chumba hicho. Simu yangu na ya Rafiki yangu Samsoni, zote zilikua zipo chaji alafu simu yangu niliichomeka chaji ikiwa imezimwa. Hivyo simu iliokua ikiita muda huo ilikua ni ya rafiki yangu na tuliigeukia wote ilipokua inaita maana ilitushtua kwa kupiga kelele katikati ya maongezi. Baada ya hapo Samsoni  alinyanyuka huku akijisemesha “Sijui nani huyu… itakua watu wa mpira hawa” alafu akaenda kuichukua ile simu mimi nikiwa namuangalia tu. Alipoishika simu na kusoma jina, nilimsikia akasema “Ah wewe Mpenzi wako huyu ananipiga huku. Sijui umekifanya nini tena kitoto cha watu”

Mimi nikashtuka kidogo alafu nikamuuliza “Ni Sabrina?” Samsoni alijibu “Ndio” alafu akasema tena “Ngoja nipokee nimsikilize” huku akiipokea simu na kuiweka sikioni. Mimi muda huo nilitaka nimwambie asipoke ila alikua ameishapokea kabla hata sijanyanyua mdomo kumwambia. Baada ya Samsoni kupokea simu, nilimsikia akisema “Halo Dada… niambie” alafu nikasikia kisauti kidogo cha Sabrina akasema “mambo vipi?” Samsoni akaitikia “kama kawa, vipi huko?”  Sabrina akasema “safi. Mbona rafiki yako hapatikani kwenye simu? Upo nae hapo?”. Mimi kusikia hivyo nikashtuka, nikamwambia kwa ishara rafiki yangu Samsoni asiseme yupo na mimi.

Samsoni alinielewa akamjibu “Sipo nae. mimi niko mbali kidogo muda huu”. Sabrina alipoambiwa hivyo, akasema “Sawa, ukionana nae mwambie namtafuta” Samsoni akajibu “sawa” kisha simu ikakatwa. Baada ya hapo rafiki yangu alirudisha simu kwenye chaji huku akisema “Haya si umesikia? Eti anakutafuta. Sauti yake tu inaonekana mmezinguana nyie. Huu ugomvi siingilii” mimi nikacheka kwanza kidogo alafu nikasema “nitamcheki baadae”.

Baada ya hapo Samsoni aliniaga kuwa anatoka kidogo hivyo mimi nilibaki mule ndani nikiwa nimetulia tu ila kichwani kwangu mawazo ni mengi sana. Wakati akiondoka alisema pia “Alafu nilipokua anaangalia mpira, Tino alinipigia akaniambia amekutafuta hakupati hivyo umpigie” mimi nikaitikia “Ah sawa”.

Nilipokua pekeangu mule ndani, Mawazo yalinituma ninyanyue godolo tunalolatila maana Samsoni alikua anatabia ya kuweka pesa huko. Nilipofanya hivyo, nilizikuata pesa zake nyingi kiasi na nikazichukua maana niliona kama zinaweza nisaidia katika hali niliokuanayo kwenye wakati huo. Nilikua ni kama na muibia Rafiki yangu kabisa ili tu niweze kukimbia tatizo linalonipa Mawazo.


Mawazo niliokuanayo siku hiyo yalikua yamesababishwa na matokeo ya mimi kuanza kuzifungua kurasa za mapenzi katika maisha yangu. Nakumbuka miaka michache iliopita kambla ya siku hiyo nilikua nasoma sekondari kidato cha tatu na nilikua nasoma shule za kutokea nyumbani. 

Tangu nilipoanza sekondari nilikua sijawahi jihusisha au kuwaza kuwa na mpenzi shuleni japo nilikua natamani. Hii ilikua ni kutokana na mambo mengi ikiwemo sheria za shule zilizokua zikikumbushwa kila siku na walimu. Na pia nilikua nawaogopa wazazi wangu kuniona nimejiingiza kwenye maswala ya mapenzi. Mbali na hayo, nilikua naogopa sana jinsia tofauti. Kuwasogelea na kuongea nao kulikua ni mthihani mkubwa sana kwangu kipindi hicho, hasa akiwa ananivutia.

Kwenye mambo ya kufanya vizuri shuleni kwa bahati mbaya nilikua siko sana huko. Uwezo wangu katika madaftari na mithihani ulikua wa kawaida sana. Nakumbuka darasani nilikua nakaa viti vya nyuma sana. Huko nyuma nilikua nakaa na rafiki zangu wawili ambao mmoja wapo ndio huyo  anaitwa Samsoni, alafu kuna mwingine alikua anaitwa Tino. Kwaiyo tulikua kama tuna kikundi cha watu watatu nyuma ya Darasa. Darasa letu lilikua lina viti vinavyo ruhusu kukaa wawili na kiti nilichokua na kaa mimi, tulikua tunakaa mimi na Samsoni ila mwalimu akitoka tu, Tino alikua anakuja kwenye kiti kile, tunajibana watatu, tunapiga stori. Tino alikua anakaa kiti cha pembeni yetu ambacho kilikua karibu sana na sisi.

Tino alikua ni mwenzetu ila mambo yake yalikua mengi mno. Alikua ni msumbufu sana kiasi kwamba kila mtu alikua anamjua kwa usumbufu wake hapo shuleni. Watu walianza kumjua baada ya kuletwa na mzazi wake shuleni na kupigwa kutokana na kutolala kwao pamoja na kutokuja shule kwa siku 5 mfululizo katika kidato cha kwanza.

Tulikua tuna shirikiana sana Tino lakini usumbufu wangu haukufikia usumbufu wa Tino. Samsoni nae  alikua kama mimi tu, hakumfikia usumbufu Tino hata kidogo. Ila katika mambo ya kwenye vitabu, wote tulikua hatufanyi vizuri sana japo hatui wamwisho Darasani. 

Kuna siku asubuhi tulikua watatu Darasani kule nyuma ya Darasa tunapiga stori kwa kujiachia lakini ghafla akaingia mwalimu. Alivyoingia tu, tukafunga midomo alafu kila mtu kati yetu alikaa vizuri anapokaaga kisha watu wote darasani tukasimama kumsalimia Mwalimu. Baada ya kumsalimia, akaturuhusu tukae alafu nikakuta tu anasema “Nyie watatu uko nyuma hebu simameni”. Mh alivyosema hivyo nikawa nawaza “Anaongelea mimi na rafiki zangu au? Mbona anaangalia huku nyuma?” wakati najiuliza nikakuta mwalimu anasema tena “Nyie muliokua mnapiga kelele mpaka darasa zima mnasikika nyie huko nyuma simameni kabla sijawafuata.” Basi mimi nikaona huenda anatuongelea sisi, nikasimama na bada ya mimi kusimama, nikakuta na Rafiki zangu wawili wanasimama.


Baada ya hapo mwalimu akaanza kufoka “Hivi nyie mna matatizo gani? Inamana hapa shuleni mmekuja kupiga makelele au?” baada ya kusema hayo akaninyoshea mkono na kusema “Wewe hapo wewe inaonekana msumbufu maana hata Nywele haujanyoa. Hizo nywele ni siku ya ngapi nakwambia sitaki kuziona? Hebu sogea hapa mbele” mimi nikiwa mnyonge sana nilisogea taratibu pale mbele ya Darasa. Mwalimu aliniuliza “Unataka ni kupige ndio uanze unijibu?” mimi nikiwa naogopa sana nikamjibu “Hapana, samahani mwalimu nilitaka kunyoa jana ila umeme walikata”. Baada ya kumjibu mwalimu alifikilia alafu akasema “Kesho nisione hizo nywele, sawa!?” nikamjibu “Sawa” alafu nikakuta ananiambia “Na kule nyuma unakokaa, uhame. Kabebe madaftari yako kule nyuma uyalete hapa mbele kwenye hiki kiti ambacho hakina mtu”.

Baada ya mwalimu kusema hivyo nilishtuka maana nilikua sijazoea kukaa viti vya mbele ya Darasa, nikamwambia “Mwalimu hapo wanakaa watu wawili, itakua wameitwa nje”. Mwalimu akasema “Hatakama wakija hao wanao kaa hapa, waambie mimi ndio nimekuweka hapa. Kwanzia leo utakua unakaa hapa mbele. Nawakija hao, waambie wachukue kiti kingine wakae sehemu nyingine ila sio hapa”. Dah nilikua mnyonge sana siku hiyo, nikachukua vitu vyangu nyuma ya Darasa na kuhamia mbele ya darasa huku mwalimu akiniangalia.


Baada ya kukaa mbele mwalimu alianza kufundisha somo lake maana ndio ulikua muda wake huo. Mimi pele mbele nilikua sina amani kabisa maana sijazoea kukaa hapo alafu mbali na hilo, Daftari la mwalimu huyo nilikua sina. Lakini mwalimu alipoanza kufundisha nilichukua kidaftari flani cha ajabu, nikakiweka pale mbele ili kuzuga.

Nakumbuka baada ya kama dakika 10 hivi Mwalimu alipoanza kufundisha, alikuja mwalimu Mkuu akiwa ameambatana na wanafunzi kama watano hivi na mwanafunzi wa kike alikua mmoja. Darasa zima tulijikuta tunavutiwa kumuangalia yule mwanafuzi wa kike. Mwalimu mkuu alianza mazungumzo na Mwalimu aliekua Darasani na mazungumzo yao yalikua ni kwamba hao wanafunzi watano ni wageni na kwanzia siku hiyo watakua wanasoma humo Darasani. Walimu walipomaliza kuzungumza, wale wanafunzi wakaingia ndani ya Darasa alafu yule Mwalimu aliekua Darasani akawaambia watafute nafasi za kukaa mule Darasani. Kabla hata hawajapiga hatua sana, nikakuta mwalimu ghafla anamwambia yule mwanafuzi mgeni wa kike “Wewe usiende huko. Kaa hapa na huyu”. Mimi moyo ulishtuka sana maana alikua anamuelekeza yule Mwanafunzi wa kike akae na mimi kwenye kiti kimoja. Kiukweli mimi nilikua naogopa kukaa na jinsia tofauti hasa wakiwa wazuri ndio napoteza uhuru kabisa yani. Na Mwalimu alikua anamzingatia yule mwanafuzi wa kike kwa kiasi flani, kama ni ndugu yake hivi.

Nakumbuka yule mwanafunzi alikaa na mimi pele huku akiwa na viaibu aibu vya ugeni alafu na mimi wakati huo nina viaibu vya kumuogopa.  Tukiwa tumekaa  pale mwalimu aliwauliza jina wageni wote waliokuja na nilisikia yule Mwanafunzi wa kike akijitambulisha kuwa anaitwa Zuwena.  Basi baada ya hapo mwalimu aliendelea kufundisha na mimi nikawa kama namsikiliza  hivi ingawa akili yangu ilikua inahama. Yani nikua nikitupa jicho langu mara moja moja kwa yule Mwanafuzi wa kike kumuangalia jinsi alivyo. Japo nilikua naogopa, ila alikua anavutia sana kumuangali alafu alikua msafi sana. Kuna muda nilimtupia macho tukagongananae alafu akaona viaibu. Mimi nilipogongananae macho nilishtuka na nikaingiwa na woga zaidi ila woga ulipungua nipowaza “ Inamaana na yeye ananiogopa huyu. Dah ila mzuri mpaka raha. Ingawa naogopa ila hapa nijitahidi niwe hata rafiki yake tu. Sina hata rafiki wakike ujue”. Nakumbuka niliwaza mambo mengi sana kuhusu huyo mgeni bila kujua kuwa ndio namuingiza moyoni hivyo mtoto wa watu.

Baadae, mwisho wa kipindi cha mwalimu aliekua akifundisha ulifika na mwalimu alituachia maswali ya kufanya nyumbani tuyaandike alafu akasema anaondoka. Lakini kabla hajaondoka akasema “Nyie muliofika leo hakikisheni munaazima madaftari Kwa wenyeji ili muandike vitu vyote vya nyuma. Wewe Zuwena utachukua Daftari kwa huyo uliekaanae hapo, sawa!?”. Nikiwa pembeni ya Zuwena nikamsikia Zuwena akiitikia “Sawa” huku nikiwa nimeshtuka mno maana Daftari wanalo liongelea sina. Kichwani nikaanza kuwaza “Hapa mbona kama naenda kuumbuka kwa mgeni sasa. Huyu mwalimu na huyu mgeni wanajua Daftari ni hili lililopo Mezani lakini ukweli ni kwamba sina Daftari. Nikijieleza kwa huyu mgeni kuwa sina daftari, nitaonekana mjinga sana kwake na naweza shindwa kuwa rafiki yake. Dah tena anaonekana anaakili sana huyu, ntaumbuka leo.”



INAENDELEA…