All posts by Admin

Mambo humfanya mwanaume akupende sana na kukuchagua maishani

Kumekuwa na mahusiano mengi ambayo huanzishwa lakini hayafiki mbali kama lilivyo lengo kuu la mahusiano yao. Hali hii inafanya wanawake wengi wawe na wasiwasi katika mahusiano. Wamekua wakifikilia “Je, atanifanya niwewake wa maisha?” Lakini wanasahau kujiweka tayari kwaajili ya kuwa wanawake wa maisha.
Kuna vitu vidogo vidogo ambavyo vinaweza mfanya mwanaume akuweke moyoni na akufikilie kuwa wewe ni wake wa maishani. Hebu tumia muda wako kuvisoma hapa chini.

Mazoezi ya mwili ambayo husaidia katika Mapenzi BONYEZA HAPA>>>

Mambo humfanya mwanaume akupende sana na kukuchagua maishani

Tabasamu.

Kama unahitaji mwanaume avutiwe na wewe basi tambua kitu muhimu kufanya unapokuanae ni kutabasamu na kucheka. Usionyeshe uso usio na urafiki. Kuwa kama mtu anayependeza, mwenye urafiki, na mchangamfu. Ukijitahidi kuwa mtu mwenye furaha kuliko maugomvi. Onensha sura ya tabasamu kuliko makasiliko. Mapenzi yenu yanaweza kuwa na furaha pia na hakuna mwanaume asiependa mapenzi yenye furaha.

Whatsapp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa BONYEZA HAPA>>>

Kuwa mcheshi.

Wanaume kwa ujumla wanapenda wasichana wenye ucheshi ambao wanaweza kuwafanya wajisikie vizuri. Kuna muda mwambie hadithi za kufurahisha na usiogope kucheka. Kumbuka usizidi kupita kiasi hadi uonekane kama mchekeshaji. Ni vizuri kuwa na mwenzi ambaye anafurahisha, lakini ni watu wachache sana wanamawazo ya kuishi na mchekeshaji.

Toa kuliko kuchukua.

Ili kuongeza nafasi zako za kukupenda lazima utoe kuliko kuchukua. Mwanaume anaweza kutofautisha kwa urahisi kati ya msichana ambaye anataka kitu kutoka kwake na yule anayemjali.
Nadhani unajua kuna wasichana wengi ambao wanafuata pesa na wameweka mbele pesa kuliko mahusiano. Wanaume wengi wanao wafuata wanawake wa mtindo huu huwa hawana mpango nao wa maisha maana huona kama wananunua upendo hivi… Jitofautishe na wauzaji na aone unavutiwa naye kwa upendo wake na sio pesa yake au kitu kingine chochote. Yani hata akitanguliza gari mbele usishoboke nalo sana kuliko kumpenda yeye maana baadae anaweza anza kulisifu gari kwa kukukamata wewe na mbaya zaidi inaweza kuwa ni wanawake wengi walinaswa na gari hilo hivyo, haunajipya.

Mpenafasi ya kufanya kazi, Mshauri na kumtia Moyo.

Unaweza sikiliza hii

Katika maisha Mwanaume maranyingi huzungukwa na vitu vinavyomkatisha tamaa na kumuumiza lakini anatakiwa ajikaze tu kwasababu ni “Mwanaume”. Hii inaweza kuwa kazini, kwenye familia na maeneo mengine. Endapo mwanaume anaejielewa atapata mwanamke ambae anamsikiliza mambo yake magumu, anamshauri, anamtia moyo na kumsukuma kufanya maamuzi mazuri na maendeleo hata kwenye mambo madogo kwenye maisha, hawezi kumuacha mwanamke huyo aondoke maishani mwake. Kuna familia huwa zinainuka na kuwa na mafanikio kwasababu ya jambo hili, hasa zikiwa na mambo ya kidini ndani yake.

Kama muko kwenye mahusiano na mwanaume na anaonekana kuwa busy sana na kazi mpaka anafikia kuwa mbali na wewe, Usimfikilie tofauti moja kwa moja na kuanza vurugu. Mruhusu mwanaume afanye kazi kidogo ili kufanya maendeleo kisha vumilia pindi anapokua mbali na wewe ila usijisahau kumuonesha upendo sana.

Hili ni jambo ambalo linaweza kuongeza sana nafasi zako za kushinda upendo wake. Wanawake wegi wanakata tamaa na kumuacha mwanaume wanapoona yupo busy Sana na maisha… huzani kuwa hawana nafasi tena lakini jua kuwa wakati huo ndio wakati mzuri wa wewe kuongeza upendo wake kwako.

Jinsi ya kuwa romantic kwa mpenzi wako BONYEZA HAPA>>>


Muoneshe kuwa bado yupo moyoni wako, muoneshe kuwa unajua anachokifanya na ukipata muda muulize maswali au kumshauri, muoneshe kuwa bado unamjali hii itamfanya akuweke katika fikila zake za kimaisha. Usijekosa maisha mazuri anayokupambania kwa kukata tamaa.

Lakini unapo mruhusu afanye kazi mbali na wewe hakikisha unafanya vitu vya upendo ambavyo vitamfanya aanze waza kukuweka karibu yake au kuja karibu yako(kama atakua na uwezo huo). Ukipata nafasi pia mtembelee au fanya mautundu akutembele.

#Muvumilie anaejali upendo na uvulilivu wako tu, Wanaume wengine hukimbia mazima.

Usimmiliki sana kuliko kumuonesha upendo.

Wanawake wengi hufanya makosa ya kumiliki sana mwanaume na wakati hata hawamuoneshi upendo. Unaweza kujaribu kumlinda sana asiende kwa wanawake wengine ili abaki kuwa na wewe pekee katika maisha yake lakini je anao wafuata wanamvuta kama jinsi unavyo fanya wewe?. Ni wazi kuwa wanamvuta kwa upendo na vitu vingine vizuri… hivyo na wewe kuwa mbunifu na kwenye kumuonesha upendo ambao utamvutia zaidi kisha mruhusu aamue kuchagua kinachomfaa. Ikiwa wewe ndiye wa kwake, hakika atakupenda.

”kwanini wanawake wazuri/warembo hawaolewi?” sababu zinaweza kuwa hizi BONYEZA HAPA>>>

Kuwa na maadili mema.

Maadili mazuri ni lazima katika kumshawishi mwanaume akupende zaidi na aweke moyo wote kwako maishani. Hakuna mtu anayetaka kujihusisha na mtu ambaye haeleweki,hasikii au hana nidhamu. Bila shaka kila mtu husita kumpa moyo mtu ambae hana maadili mazuri. Wanaume wanapenda wanawake ambao wana nidhamu. Hivyo basi muheshimu na pia uwevizuri nae ataona unafaa kuwa wake maishani. kuna mambo unawezasikia rafiki au mwanawake wa mitandaoni Eti “Ukinichiti nakuchiti” “Wanaume wote ni Mbwa” “Siwezi kuwa na mwanaume mwenye gari au pesa” “Siwezi olewa kwa sasa mimi ni mzuri” na mengine mengi kama hayo. Ukileta mambo hayo kwenye maisha yako unaweza angukia pua, ni vema kutula kuwa na maadili yatakayomkaribisha mtu kuwa na wewe maishani. Onesha heshima kwa Mwanaume hata wakikuita mshamba. Kuwa msafi, vaa vizuri na marafiki wastaarabu.

Jinsi ya kujua mtu mwingine anaona sms na unavyofanya WhatsApp kisiri

Whatsapp ni mtandao mkubwa ulimwenguni ambao watu huutumia sana katika mawasiliano. Unaweza kuwa ni mtandao wako pendwa katika mawasilioano ndio maana upo hapa… Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy, utajifunza vingi kuhusu mtandao huu.

Whatsapp ni mtandao mzuri kuutuumia katika kuwatumia watu Picha, Video, Audio au ujumbe wa maneno lakini unapofanya hivyo tambua kuwa kunajinsi ambavyo mtu mwingine anaweza kuona vitu vyote hivyo kwenye simu au kifaa chake bila wewe kutambua(kisiri). Kuna njia ambazo hata mtu asiebobea sana katika maswala ya Teknolojia anaweza tumia kuona sms au vitu unavyofanya kwenye Whatsapp. Lakini jambo hili lisikutishe maana hapa chini tunakwenda kukujuza jinsi ya kuangalia kama upo salama na jinsi ya kujilinda pia… Kwaiyo ondoa hofu na endelea kutumia Whatsapp yako kama kawaida.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kujua mtu mwingine anaona sms na vitu unavyofanya WhatsApp kisiri

Whatsapp kwa sasa inakuruhusu mtumiaji wake kuunganisha akaunti yako moja ya Whatsapp kwenye kifaa zaidi ya kimoja. Unaweza fannya akaunti yako moja ya WhatsApp iwe inatumika kwenye simu mbili mpaka 4 na namba ikawa hiyo hiyo moja. Mtu mingine anaweza kuitumia hii kunganisha akauti yako kwenye simu yake au kifaa chake na kuanza kukuchunguza unachofanya bila wewe kujua. Na mtu akitumia ataweza kusoma sms zako, kujibu, kuona na kuchua audio,video na vitu vingine unavyotuma na kutumiwa bila wewe kujua.

Ukitaka kujua kama akaunti yako ya Whatsapp imeunganishwa fanya yafuatayo:

  1. Fungua Whatsapp yako na uguse Vidoti Vitatu
  2. Ukifanya hivyo, Chagua “Linked divices”
  3. Baada ya kufanya hivyo utatupwa kwenye ukurasa ambao ukikuta kuna kifaa chochote kiorodheshwa basi jua whatsapp yako sio salama. Na kama hamna kifaa basi yawezekana upo salama. Unaweza angalia picha hapa chinikuelewa zaidi.

Endapo utakuta akaunti yako ya Whatsapp sio salama(hacked) unaweza gusa kifaa kilicho orodheshwa kwenye kwenye ukurasa huo alafu ukagusa vidoti vitatu itakavyoonekana juu kulia kisha utachagua “Remove device”.

Ili kuhakikisha kuwa WhatsApp yako iko salama kila mara, hakikisha unafanya kuangalia kama akaunti yako ya WhatsApp imeunganishwa mara kwa mara hasa baada ya kumruhusu mtu mwingine aishike simu yako bila uangalizi wako.

Mtu akikublock WhatsApp Fanya hivi kuchati nae BONYEZA HAPA>>>

App za kuangalia Movies/Filamu mtandaoni kwa simu

Katika ulimwengu wa sasa unaweza angalia movie kwenye simu yako ya kiganjani ukiwa popote ulimwenguni. Mara nyingi watu wakitaka kuangalia movie huwa wanatembelea website/tuvuti zinajihusisha na movie/filamu au hutumia app zinazojihusisha na filamu ili kupata huduma ya movies. Kuna baadhi ya tuvuti au app hukuwezesha kupata huduma ya movie bure na nyingine huwa zinakuhitaji ulipie. Huduma za kulipia huwa ni bora zaidi na zinausalama zaidi ukilinganisha na baadhi ya huduma za bure japo zote ni nzuri.

Hapa Tha bestgalaxy leo tunakupa orodha ya app chache kati ya app nyingi unazoweza tumia kuangalia movie kwenye simu yako mtandaoni(online).

App za kuangalia movies online(mtandaoni)

Netflix

Hii ni app ya kampuni ya kimalekni, Netflix ambayo inayotoa huduma ya kuangalia movies/filamu kupitia Internet. Unaweza ingiza kwenye simu yako ya mkononi na kuanza kufurahia filamu kiganjani pako. Unaweza kuangalia filamu nyingi nzuri na maalufu duniani kupitia app hii. Lakini unachotakiwa kujua ni kwamba app hii ya netflix huwa haitoi huduma bure. Inaweza kukugharimu Tsh 7000 mpaka 23000(Makadilio).

ShowMax

ShowMax ni app inayotoa huduma ya kuangalia movies(filamu), michezo, vipindi vya TV na mambo mengine mengi, kiganjani pako. App hii inaweza kutumika kuangalia movie katika simu ya mkononi lakini sio bure pia. kufurahia huduma za app ya ShowMax utatakiwa kulipia kila mwezi. Kuna filamu nyingi unaweza angalia na pia kama ni mdau wa michezo, unaweza furahia michezo katika app hii. Kifurushi vyake vinaweza kugharimu Tsh 7800 mpaka 46000 kwa mwezi(Makadilio).

Youtube

Youtube ni app ambayo watu hutumia kuangalia video mbalimbali ambazo huwa zinapostiwa kwenye channel. Katika Youtube kuna channel ambazo hutuma filamu na unaweza angalia filamu hizo bure kabisa. Ukiachana na channel za filamu pia kuna kipengele cha Youtube kinachojihusisha na filamu tu(filamu za bure na kununua}. Kipengele hicho cha Youtube hakipatikani katika baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania kwa sasa ila unaweza soma maelezo ya kukuiona hapa chini.

Jinsi ya kuona kipengele cha movies cha YouTube Gusa hapa>>>>

Prime Video

App hii inaitwa “Amazon Prime Video” lakini kwa kifupi unaweza kuiita “Prime Video”. Ni moja ya app zinazoweza kukufanya ufurahie kuangalia movies na hata vipindi vya Tv pia kiganyani pako. Prime Video sio app ya bure lakini inakupa uwanja mpana unaofanana kiasi na netflix hivi katika filamu, unaweza angalia filamu nyingi maaalufu. Maelezo ya kiasi utakachotakiwa kulipa kwa mwezi yaliopo katika tuvuti yao yametaja kiasi kuwa ni USD 5.99 ambayo ni kama Tsh 14000 ivi…

~Viasi vya malipo vilivyo tajwa kwenye makala hii ni makadilio tu.

Maneno na maswali ya kurefusha maongezi na kumfurahisha mpenzi wako

Katika mahusiano wapenzi mnaweza ongea au kuwasiliana mpaka ikafika wakati mkakosa cha kuzungunzia, hasa kama hakuna mmoja kati yenu mwenye uwezo wa kuendesha mazungumzo. Ukiwa kwenye hali hii, unaweza ingizia maneno na vimaswali vilivyopo hapa chini kurefusha mazungumzo yenu, kumchekesha na hata kukusaidia kumjua vizuri mpenzi wako. Unaweza kuyatumia kama sms, au kuyaongea unapokua nae karibu au kwenye simu. Lakini unapotumia maneno na maswali haya hakikisha hamupo kwenye hali ambayo itamfanya mpenzi wako aone kero. Endelea kuwa karibu na The Bestgalaxy.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Maneno na maswali ya kurefusha maongezi na mpenzi wako

  1. Kuna watu walikua wanamsifia dada flani hivi kuwa anamacho mazuri, nilivyomwangalia yule dada nikajiuliza “Mh hivi wanamjua mpenzi wangu hawa? hahaha” Unamacho mazuri sana alafu nayapenda.
  2. Hivi hilo kovu ulifanya nini?, au ulikua cha utundu utotoni?
  3. Kama kuna zawadi ambayo ulipanga kumpa mtu atakae kupenda kwa dhati maishani mwako nipe tu maana nakupenda sana mpenzi, sitamani utoke maishani mwangu unanipa furaha mwenzio. Stamani niamke kwenye hii ndoto.
  4. Kwa mfano umeshida Milioni 80 sasa hivi, utanipa shingapi au utafanyia nini?
  5. Kukupenda ndio kitu ninachoweza kukifanya bila kuchoka duniani mpenzi wangu. Sijui niwe nakuita jina gani ili usije sahau kuwa nakupenda na usinitende…
  6. Ulivyo kuwa mdogo ulitaka ukiwa mkubwa uwe nani?
  7. Hebu fumba macho tuone… Hahaha Unamacho mazuri… ivi unajua kwamba una macho mazuri hivyo?
  8. Kwaiyo umelala peke yako? huogopi?
  9. Wiki ijayo nikumbushe nikwambie kitu… Ntakwambia kitu kizuri
  10. Kitu gani unapenda utimize kabla siku zako za kuishi duniani hazijaisha?
  11. Bebi, ivi nikikwambia utaje vitu vitano tu unavyo penda duniani utataja vitu gani?
  12. Unapenda mbwa au paka?
  13. Ivi katika maisha yako unaogopa nini?
  14. Ulifikiria nini mara ya kwanza nulipokwambia nakupenda?
  15. Niambie vitu vitatu tu ambavyo hauvipendi?
  16. Ivi umenipendea nini? au unapenda nini toka kwangu mpenzi?
  17. Ninavyokugusa huwa najiskia vizuri sana ivi wewe unahisi vipi?
  18. Unafanya nini sasa hivi?
  19. Upo na nani hapo kipenzi?
  20. Natamani nije hapo japo kukubusu tu lips zako nzuri hizo
  21. Ukichukia unapenda kufanya nini ili kutuliza hasira zako?
  22. Alafu usiku nilikuota
  23. Ivi umeishawahi poteza hela? ilikua kiasi gani?
  24. Niambie maneno matatu mazuri toka moyoni mwako
  25. Unapenda kuangalia filamu? unapenda filamu gani?
  26. Hahaha… nitakwambia kesho… au nipe zawadi nikwambie leo
  27. kwenye familia yenu wewe ni mtoto wa ngapi kuzaliwa?
  28. Ivi bebi Unapendelea zaidi kula chakula gani?
  29. Ugali kwa kiluga chenu munauitaje?
  30. Ukipewa nafasi ya kutembelea nchi tatu duniani ambazo hauja wahi tembelea, utachaguza zipi?

Whatsapp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa

Whatsapp ni mtandao unaotumiwa na watu wengi sana na umekua na msaada mkubwa kwa watu katika swala la mawasiliano. Katika kutumia mtandao huu unaweza kupambana na changamoto au vitatizo vidogo vidogo, hasa katika app za simu. Changamoto au matatizo huwa hayatokei mara kwa mara lakini hapa The bestgalaxy tumekuandalia orodha ya matatizo au changamoto unazoweza kutananazo katika kutumia whatsapp na maelezo ya jisi ya kutatua. Hii inaweza kuwa msaada pindi mtu unapokumbana na changamoto hizo. Pia usisahau kuungana nasi kwenye WhatsApp namba 0622586399.

Changamoto au Matatizo kwenye kutumia Whatsapp na jinsi ya kutatua

Whatsapp ban

Kama upo banned/umezuiwa kwenye WhatsApp unaweza kuona hivi

Mtandao wa whatsapp unasheria zake ambazo ukikiuka katika kutuumia mtandao huu, wanazuia akaunti yako. Kutumia app za whatsapp zisizo rasimi ni moja ya jambo linaloweza kufanya akaunti yako izuiliwe Whatsapp. Nikizungumzia “Whatsapp zisizo rasmi” namaanisha app kama vile OG Whatsapp, GB Whatsapp au FM whatsapp. Mtandao wa Whatsapp una app rasmi mbili tu. App ya kwanza inaitwa “Whatsapp messenger” na ya pili inaitwa “Whatsapp business”… App yoyote mbali na hizo ni app isio rasmi na inaweza kufanya akaunti yako izuiwe/ifungwe na mtandao wa Whatsapp.

Ukiachana na kutumia app zisizo rasmi, unaweza fungiwa au kuzuiwa akaunti baada ya kufanya mambo mengine yasio faa katika Whatsapp au watu kutoa taarifa kwa Whatsapp kuhusu akaunti yako kujihusisha na jambo flani lisilo ruhusiwa kwenye Whatsapp.

kuna namna mbali za kuzuiwa; unaweza zuiwa na whatsapp kwa muda mfupi au kwa muda mrefu. Ukizuiwa kwa muda mfupi, baada ya muda flani akaunti yako itaondolewa kizuizi na mara nyingi huwa app inaonesha kabisa muda ambao akaunti itaachiliwa. Lakini ikizuiwa kwa muda mrefu huwa inachukua muda mrefu sana kuachiliwa… ukikumbana na kizuizi hiki unashauriwa kufungua akauti nyingine ya whatsapp kwa namba nyingine au kama unahisi wamekuonea, wasiliana nao kupitia Support@whatsapp.com tuma ujumbe wa kuelezea tatizo lako ili wakusaidie.

Ukiona dalili hizi Jua Account yako ya Facebook  imedukuliwa na si salama GUSA HAPA>>>>

Backup to Google drive

Backup katika whatsapp ni kipengele kinachokuwezesha kutunza sms za whatsapp na vitu vingine kwenye akaunti yako ya google drive ili iwe rahisi kupata au kurudisha sms na vitu hivyo pindi simu yako inapopotea au ukifuta app kwa bahati mbaya. Unaweza fungua whatsapp ukuta ghala tu wahatsapp imekuletea ujumbe unaoziba kioo kizima umeandikwa “Backup to Google drive” na kuna orodha ya chaguzi unazotakiwa kuzichagua pale. Kama hauelewi lolote kuhusu backup basi umaweza changua “Never” tu ili kuokeo muda na kuendelea kuitumia app yako ya Whatsapp.

Whatsapp kumaliza bando

Whatsapp ni moja ya app zisizotumia bando la internet sana ila kama wewe ni mtu unaetumia Whatsapp kwenye upande wa video sana basi app hii inaweza kutumia bando zaidi. Nikisema upande wa video namaanisha kutuma au kupokea video nyingi kwenye vikundi au watu wa kawaida, kutumia video call sana, kuangalia status za watu wengi wilio weka video kwenye status zao. Kuacha au kupunguza mambo hayo kutafanya Whatsapp isile bando lako sana.

Whatsapp inajaza picha na video nisizozitaka kwenye simu

Whatsapp inaweza kuwa inajaza picha na video usizozijua au usizozipenda kwenye simu yako. Kama hili ni tatizo, unaweza tatua tatizo hili kwa kuzima kipengele cha whatsapp kinacho iruhusu app ya whatsapp kuingiza kwenye simu video au picha zinazotumwa kwenye magroup au unazotumiwa. hii itafaya kila video au picha unayotumiwa kutojiingiza kwenye simu yako mpaka utakapo gusa kuidownload.

jinsi ya kufanya hivyo; fungua app yako ya whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” kisha gusa “Storage and Data” alafu baada ya hapo ingia walipo andika “When using mobile data” na uondoe alama ya tiki kwenye vibox vyote au cha video na Photos tu. baada ya kufanya hivyo, bonyeza “Ok” na rudi nyuma kidogo kisha uingie kwenye “When connected on WiFi” alafu uondoe alama ya tiki katika vibox vyote au vibox vya “Photos” na “Videos” tu.

Mtu akikublock WhatsApp Fanya hivi kuchati nae BONYEZA HAPA>>>

Wananiunga kwenye magroup bila taharifa

kama umekua unajikuta umeingizwa kwenye magroup ya Whatsapp na watu usio wajua bila hata taharifa na haupendi hali hiyo basi kunakitu unaweza fanya hapa. Kwenye Whatsapp kunakipengele kinakuruhusu kuzuia mtu ambae hauna namba yake kukuingiza kwenye group. Unaweza kutumia kipengele hiki kuzuia watu ambao hauna namba zao wasikuingize kwenye group lolote bila kukutaharifu.

jinsi ya kufanya hivi; Fungua Whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” kisha gusa “Privacy”. Baada ya hapo, nenda eneo la chini kidogo uingie walipoandika “Groups” kisha chagua “My Contacts” alafu rudi nyumbani na uendelee kutumia app yako.

Nasumbuliwa na simu za watu nisio wajua

Whatsapp pia inakipengele cha kufanya watu watu ambano nambazao hazijawekwa kwenye simu yako wakikupigia usipate usumbufu. Mtu yoyote ambae anakupigia kwenye Whatsapp kwa namba ngeni, simu yako haita, itakua kimya tu bila kukusumbua. Kama ni mtu amabae huwa unapata simu nyingi kwenye Whatsapp toka kwa watu usio wajua na haupendi swala hiilo basi unaweza kutumia kipengele hicho kuondokana na jambo hilo.

Jinsi ya kufanya hivi; Fungua app yako ya Whatsapp, gusa vidoti vitatu, chagua “Settings” alafu bofya “Privacy”. Baada ya hapo, nenda chini kidogo uingie katika “Call” alafu washa palipo andikwa “Silence unknown callers”.

Magemu ya simu ya kucheza Online (ufalme wa vita)

Ni sehemu nyingine tena tunaangalia Magemu mazuri unayoweza kucheza kwenye simu. Kwenye makala hii tutajikita kwenye magemu ya “battle royale” ambayo kwenye kuyacheza yanahusisha kutafuta ufalme wa vita. PUBG, COD au Free Fire ni moja magemu maalufu ya battle royale lakini ukachana magemu hayo, kuna magemu mengi sana ya muundo huu katika ulimwengu wa magemu… Na mengine yanaendelea kutoka karibu kila mwaka.

Hapa The bestgalaxy tumekuandalia orodha ya magemu machache ya Battle royale ambayo ni ya online(unatumia internet kuyacheza). Unaweza angalia orodha hii hapo chini na hata kujaribu gemu litakalo kuvutia. Ila tumejikita kwenye Andoid.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Magemu ya ufalme wa vita ya kucheza Online/mtandaoni kwa simu za android

Rules of Survival

Rules of Survival ni gemu aina ya battle royale ambalo lilitengenzwa na kampuni ya NetEase Games. Gemu hili ni moja ya magemu kama PUBG,COD au Fire. Lilitolewa kwa simu za Android pamoja na iOS. Linakutupa katika uwanja wa mapambano/vita wenye wachezaji wengine wa gemu hilo Online/mtandaoni.

Katika gemu la Rules of Survival, Ukiwa kama mchezaji wa gemu hili unaweza cheza ukiwa pekeako au kuwa katika timu. Unapoanza unaruka kutoka kwenye ndege na kushuka taratibu katika kwenye uwanja wa mapigano ukiwa huna silaha yoyote. Silaha utakua unazitafuta na kuzikuta kwenye uwanja huo huo wa mapigano huku ukiendelea kujitetea dhidi ya wachezaji wengine.

~Game hili kwa sasa limeondolewa ila kunatetesi kuwa linaweza kurudi.

Knives Out

Hili ni moja ya magemu mazuri ya online/mtandaoni ambayo huchezwa na watu zaidi ya moja. Gemu hili ni battle royale, hukusanya watu au wachezaji katika eneo moja kubwa na kutakiwa kupigana na kujitetea wakiwa kama timu au mtu mmoja mmoja. kufika haraka unapokwenda unaweza tumia gari.

Ni gemu bomba lililotolewa mwaka 2017 na waliolitoa gemu hili ni kampuni ya NetEase Games. Mpaka sasa gemu hili mamilioni ya wachezaji katika sehemu mbalimbali ulimwenguni na wechzaji hulicheza simu mpaka pc.

FARLIGHT84

Hili ni gemu ambalo linahusisha uongo wa kisayansi na ni moja ya magemu mzuri kaika ulimwengu wa magemu ya battle royale. Linakutupa katika mazingira ya ulimwengu wazi yaliyojaa sayari mbalimbali, vituo vya anga na viumbe vingine vya anga. Kiufupi gemu hili lina mazingira tofauti sana, vitu unavyokutananavyo katika gemu hili ni vya kisanyansi na mambo mengine ya uchunguzi wa anga.

Game la FARLIGHT84 limetolewa mwaka 2023 na mpaka sasa lina mamilioni ya wachezaji toka nchi au sehemu mbali hapa ulimwenguni. Kwa maana nyine tunaweza kusema gemu hili linapendwa na watu wengi.

Je, wajua haya kuhusu Kondomu na Ukimwi? soma hapa

Kondomu ni kifuko kinachotumiwa na wanaume tangu zamani kuzuia mimba na maambukizi ya maradhi ya zina. Siku hizi kuna kondomu ya kike pia.

Kondomu zinatengenezwa kwa ngozi ya mnyama, siku hizi hutengeneza kwa kutumia mpira.

Utengenezaji hufanyika katika mazingira ya baridi ili kuhifadhi uimara wa mpira.

Zinaunganishwa ngozi nyembamba mbili ili matundu ya ngozi ya kwanza yazibwe na ile ya pili na matundu ya ngozi ya pili yazibwe na ile ya kwanza.

Kisha kupimwa, kondomu huwekewa dawa ya kuzuia isiharibike: dawa hiyo ina madhara kwa afya.

Pamoja na kutumika kwa ajili ya kuzuia mimba kwa mafanikio makubwa (ingawa si 100%), mpira huo unatangazwa sana kama kinga imara dhidi ya virusi vya UKIMWI.

Lakini katika utafiti uliofanywa na shirika la Sexuality Information and Education Council la Marekani kwa majozi 122 ambapo mmojawao alikuwa mwathirika, wenzao 12 waliambukizwa (10%) ingawa walifanya ngono kwa kutumia kondomu kila mara na kwa usahihi.

Shirika la Human Life International lilifanya utafiti kwa aina mbalimbali za ngono. Kati ya waliotumia vizuri kondomu, mwaka wa kwanza waliambukizwa: 11% za waliofanya ngono ya kawaida, 30% za waliofanya ulawiti. Mwaka wa pili wakafikia 21% na 51%. Mwaka wa tatu wakawa 30% na 66%.

Kwa maneno mengine ni kwamba kondomu haizuii moja kwa moja, bali inaahirisha maambukizi: kama si leo, inaweza tokea kisababu kesho ukapata japo ni kwa uwezekano mdogo sana, hasa kama ukiwa muangalifu katika taratibu za utumiaji. Pamoja na yote hayo, huwezi kulinganisha hata kidogo kutumia kondomu na kutotumia kabisa. Bado kondomu ni kitu kinachozuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa asilimia kubwa sana ukilinganisha na kutoitumia. Ndio maana watu hushauriwa kutumia kondomu ili kuzuia maambukizi wanaposhirikiana kimwili bila kujua hali zao. Na endapo mtu akipata virusi vya ukimwi ni vema akajikubali, akeelewa kuwa sio mwisho wa maisha na pia kuwatu wengi katika Dunia au mazingira yake wanahali kama yake waishi kama kawaida.

SUKARI YA DADA 🔞 (Simulizi ya Sauti)

SUKARI YA DADA ni simulizi tamu iliotolewa na kijana wa miaka hii na mpaka sasa imefuatiliwa na maelfu ya watu na wameipenda. Sasa simulizi hii inapatikina kwa sauti na hii ni kumrahisishia mtu asietaka kupoteza muda kuisoma. Mbali na hivyo, kuna vitu vingi vya kufurahisha kwenye simulizi ya SUKARI YA DADA ya sauti kuliko ya maandishi japo ya maandishi pia ni nzuri sana kwa upande wake. Kama unahitaji simulizi hii unaweza anza kusikiliza sehemu za mwanzo Bure kabisa kwenye simu yako. Kitu cha kuzingatia ni kwamba hautakiwi kuwa na miaka chini ya 18 au kusikiliza sehemu zilizo na watu wa umri huo maana ndani ya simulizi kunavitu vilivyolenga watu wa umri wa miaka 18 na kuendelea.

Anza na simulizi hii kwa kusikiliza vipande vifuatavyo:

Sehemu ya 1:

Sehemu ya 2:

Sehemu ya 3:

Sehemu ya 4:

Sehemu ya 5:

Sehemu ya 6:

Kama utahitaji kupata simulizi nzima, ni Tsh 2000 tu(wahi OFA!)… Bofya kitufe kilichoandikwa “WhatsApp” hapa chini ili kuchati na sisi Whatsapp ili upewe nafasi ya kupata Simulizi full(vipande 17). Au piga simu 0715233405

Unaweza sikiliza maelezo haya

Isikilize simulizi ya SUKARI YA DADA katika mazingira ya utulivu

Kama utakua umeamua kuisikiliza ni vema ukazingatia mazingira ya utulivu ili ufurahie zaidi hii simulizi. mazingira tulivu yatakufanya umuelewe msimuliaji na kuielewa kirahisi simulizi hii nzuri. Ninaposema mazingira tulivu na maanisha mazingira yalio na makelele au vitu vingine vinvyoweza ondoa umakini unaouweka kwenye simulizi na kukufanya usisikie au kuelewa baadhi ya sehemu. Zingatia sana anachosema msimuliaji kuliko kuizingatia sauti yake.

Inaweza kusikilizwa na wanaume na wanawake

simulizi hii inaweza sikilizwa na jinsia zote. Nikisema jinsia zote basi nna maana inaweza sikilizwa na mwanaume na pia mwanaweke. Hivyo kama wewe na mwanaume, unaweza sikiliza simulizi hii… Ukiwa ni mwanaumke, unaweza pia sikiliza simulizi hii bila shida yeyote. cha kuzingatia hapo ni umri tu maana watu wasio na miaka 18 na kuendelea hawaruhusiwi kutega sikio za kwa msimuliaji.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Jinsi ya kujua kama simu inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine(anaona bila kuigusa)

Katika matumizi yako ya simu za Smartphone unatakiwa kuelewa kwamba vifaa hivi vinaweza kudukuliwa na mtu mwingine na kufanya mdukuzi au huyo mtu apate uwezo wa kuona vitu vilivyomo au vitu unavyofanya kwenye simu yako bila yeye kuigusa simu yako. Mbali na kuona vitu unavyofanya au ulivyohifadhi, Mtu aliedukua simu yako pia anaweza kuwa na uwezo wa kuitumia simu yako bila kuigusa… Mfano wa vitu anavyoweza kuvifanya ni kuitumia simu yako kutuma sms kwa mtu mwengine, kuitumia camera yako kuangalia unachokifanya, kuvujisha vitu vyako au kukuzuia kufanya baadhi ya vitu kwenye simu yako.

Lakini ukiwa kama mtumiaji wa smartphone wa miaka hii, hutakiwi kuwa na hofu sana juu ya hili kwani kunaviashilia vya kuangalia kwenye simu yako ili kujua upo salama au vipi. Hapa The beestgalaxy tutakupa mwanga juu ya jinsi ya kuangalia simu yako ya Android kama imedukuliwa na inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kuangalia kama simu yako inafuatiliwa/inachunguzwa na mwingine

katika matumizi ya simu watu huwa wanapenda kuingiza apps nyingine mbali mbali ukiachana na zile ambazo huwa wanazikuta tayari zipo kwenye simu. Kitu unachotakiwa kujua hapa ni kwamba kuna Program au apps ambazo unaweza kuingiza kwa bahati mbaya au ukaingiziwa kwenye simu yako na zikiwa kwenye simu yako zinakua zinatumika na mtu mwingine huona au kufanya vitu kwenye simu yako bila kuigusa.

Endapo katika simu yako kutaingizwa apps hizi kwa makusudi au bahati mbaya, simu yako itakua sio salama tena maana vitu. Lakini kitu kizuri ni kwamba kwenye sikuizi kwenye simu za Android kuna program inaitwa “Google play protect”. Program hii inamilikiwa na google na kazi yake kubwa kwenye simu ni kukulinda dhizi ya apps hatari unazoziingiza kwenye simu yako. Kama kuna app yoyote inayoweza kuwa hatari umeiingiza, Google play protect huwa inatoa taharifa na kukushari cha kuifanya. Unaweza kuitumia Google play protect kuangalia kama angalia kama simu yako ni salama au si salama. Unachotakiwa kufanya ni kufuata hatua hizi chini.

  • Chukua simu yako na uingie katika app ya Play store
  • Baada ya hapo, gusa kiduara cha profile yako na uchague “Play protect
  • Bonyeza kitufe kilichoandikwa “Scan” na baada ya hapo Google play protect itaanza kuangalia kama kuna app zozote hatari kwenye simu yako alafu itakupa majibu.
  • Kama kutapatikana app yoyote hatari utaonyenshwa app hiyo alafu utashauriwa kuiondoa kwenye simu yako kwa kugusa kitufe cha “Uninstall“.

Google play protect ni njia nzuri na rahisi ya kuangalia kama simu iko salama ukiwa kama mtumiaji wa kawaida lakini huwa haikuhakikishii usalama kwa 100%.

Google play protect ikiwa “Active” kwenye simu yako huwa inatafuta na kulinda hii ya app hatari. Na endapo itakuta app harari imeingizwa au unataka kuiingiza kwenye simu yako, itakupa taharifa.

Mbali nna kutumia Google play protect kuangalia kama simu yako iko salama unaweza pia kujua kuwa simu kwa kuangangalia kama kwenye simu yako kuna vitu vifuatavyo.

Angalia orodha ya app zinazotumia sana internet na kama utakuta app ambayo haieleweki na hauitumi lakini ipo juu kwenye matumizi ya bando, inawezakua ni app hatari. Kama kamera ya simu yako ukiifungua inakuandikia “Camera is being used by another application” au “You cannot use more than one application that uses camera” au “Camera may be in use by another application” hiyo inaweza kuwa ni ishara ya kwamba simu yako sio salama. Mbali na hayo, kukuta vitu ambanyo haujavifanya lakini vimefanyika kunaweza kuwa kiashiria cha hatari pia.

Mazoezi ya kupunguza tumbo au kitambi (rahisi unafanya hata nyumbani)

Tumbo au kitambi imekua ni tatizo ambalo baadhi ya wanaume na wanawake hukumbananalo katika miili yao. Tukitungunzia kitambi katika mwili wa mwanadamu ni mafuta ambayo hujikusanya katika maeneo ya tumbo na kulifanya tumbo kuonekana limeongezeka ukubwa. Mara nyingi kitambi huibuka katika mwili wa mtu kutokana na mlo wa mtu mwenyewe au staili ya maisha yake kiujumla. Mazoezi ni njia salama na ya bure ya kuepukana au kuondokana na kitambi.

Kunawatu huwa wanashindwa kutumia njia hii na kufanikiwa kupunguza kitambi kutokana na kutarajia matokeo ndani ya siku moja au mbili. Ukiwa na mawazo hiyo kichwani hautaweza kufanikiwa kupunguza kitambi kwa njia ya mzaoezi maana matokeo huwa yanachukua muda. Yanaweza kuaanza kuonekana zaidi baada ya siku 30(mwezi).

Ukitaka kufanikiwa kirahisi, kichwa chako kiwe kinaelewa kwamba mazoezi unayoanza kufanya hayapunguzi tumbo tu, yanakufanya uweunacheza mchezo wa kitandani vizuri na kwakuchangamka, utachangamka pia katika shughuli zako nyingine tena utaepukana baadhi ya magonjwa. Ukifanya mazoezi vizuri kwa siku 7 tu unaweza anza kuona faida hizo nyingine hatakama tumbo halijapungua. Ni vema ukafanya mazoezi kuwa ni tabia yako tu ili faida zake uwe unazifurahia kila siku katika maisha yako.

Hapa chini tunashusha mazoezi matatu tu ambayo unaweza kuanza kuyafanya kila siku ili kupunguza kitambi au tumbo. Mazoezi haya ni kwaajili ya wanawake na wanaume pia. Yanaweza fanyawa hata nyumbani tu na kama hauna muda maalum wa mazoezi unaweza tafutiza dakika chache kila siku kabla haujaingia kuoga, ukayafanya. kwasiku za mwanzo unaweza pata maumivu kutokana na mwili kutozoea mazoezi lakini usikate tamaa, endelea kufanya tu maana maumivu huisha na hukuacha ukiwa imara zaidi.

Mazoezi matatu ya kupunguza Tumbo au kitambi (Mwanawake na Mwanaume)

Zoezi la kwanza

Tafuta sehemu nzuri na safi ambayo itakuruhusu kulala chali bila tatizo. Nenda katika sehemu hiyo kisha ulale chali. Nikisema “kulala chali” namaanisha kulala kwa kuangalia juu. Baada ya kulala chali hapo chini, kishike kichwa chako kwa mikono yako yote miwili alafu ukiwa hivyo hivyo, anza kujinyanyua kiwiliwili na kichwa juu alafu unarudi chini. Endelea kwenda juu na chini, juu chini bila kuibandua miguu yakochini. Angalia mfano katika picha hii;

Image:Giphy

Zoezi la pili

Katika zoezi hili, hatua ya kwanza ni kuchuchumaa chini. Baada ya kuchuchumaa nyoosha mikono yako mbele alafu shika chini katika sakafu. Baada kufanya hivyo, anza kuitegua na kuivuta miguu yako yote miwili kwa nyuma bila kiwili wili kugusa chini alafu irudishe tena miguu kama ilivyokua. Endelea kuifanya hivyo miguu kama inavyoonekana katika picha hii.

Image:Giphy

Zoezi la tatu

Kwenye zoezi hili utatakiwa kuanza kwa kulala chali kama katika zoezi la kwanza. Lakini baada ya kulala chali utatakiwa kuwa unanyanyua miguu yako yote miwili, wa kushoto na wakulia na kulileta juu kwa pamoja alafu unairudisha Tena chini. Endelea kufanya hivyo kwa kurudia kwenda juu na chini. Unaweza angalia picha ili kuelewa zaidi.

Image:Giphy