All posts by Admin

Mambo ya kuepuka baada ya kuachana na Mpenzi wako

Muhusiano ya mapenzi yanaweza kuanza vizuri, yakakua, na watu wanaopendana wakawa na ndoto kubwa kwenye mahusiano hayo. Lakini katika safari ya kuelekea kutimiza ndoto zao katika upendo au maisha ya kua pamoja, kuna mambo mengi hutokea na kuyumbisha mahusiano ya mapenzi. Baadhi ya mahusiano huwa yanadumu na kuendelea kusonga mbele pamoja na mambo mengi yanayoyumbisha.


Lakini pia Kuna mahusiano huwa yanavunjika na kushindwa kuendelea kusonga mbele kabisa. Kuvunjika kwa mahusiano huwa kunazalisha watu wenye mitazamo tofauti juu ya mapenzi na tabia tofauti pia. Hapa ndio utasikia “mapenzi ya kweli hamna… siji kupenda tena” na mambo mengine kama hayo. Mitazamo hiyo mara nyingi huja baada ya maumivu yaliosababishwa na kuachana. Maumivu baada ya kuvunjika kwa mahusiano yanaweza kukusukuma ufanye vitu vingi sana.

Japo kuachana na mpenzi hufanya mtu awe na maumivu lakini kuna vitu au mambo ambayo ni vema kuyaepuka.

Mambo ya kuepuka baada ya kuachana na Mpenzi wako

Kufanya vitu ili kumuumiza

Baada ya kuachana, kunaweza kuwa na mawazo mengi sana ya kukusukuma kufanya vitu vitakavyo muumiza mtu ulieachananae. Msukumo huu unaweza kukufanya usiwe makini na kupelekea ufanye maamuzi mabaya ambayo utayaona kama yanamuumiza lakini kwa upande mwingine yana haribu maisha yako wewe. Mfano mzuri ni kujihusisha na wapenzi wengi baada ya kuachana na Mpenzi uliempeda; unaweza hisi unamuumiza ulieachana nae kwa kumuonesha kuwa watu wengi wanakuhitaji lakini kwa upande mwingine ni maamuzi hatari kwako na sio kwake. Unaweza pata magonjwa, unaweza poteza muda wako na vuruga vitu vingine ulivyopanga kufanya maishani.

Kujilaumu au kumlaumu

Baada ya kuachana na Mpenzi wako unaweza kuwa ni mtu wa kujilaumu sana au kumlaumu ulieachana nae. Lakini kujilaumu au kumlaumu hakuwezi fanya kitu zaidi ya kukuletea maumivu pindi unapofikilia. Ni vema kujisamehe wewe na yeye pia alafu ukakubali hali na kuendeleza maisha yako. Chukulia kama yaliopita yote yalipangwa kuwa hivyo kwenye maisha yako na mambo mengi mazuri yanakuja mbele ya maisha yako. Usijishushe thamani kwaajili ya mtu asiyeona thamani yako. Wewe bado ni wathamani na unapaswa kujipenda na kujithamini hata kama umeachana na mtu unaempenda.

Kufuatilia mambo yake

Kufuatilia mambo ya mtu ulieachana nae, kunaweza fanya ukawa unaumia zaidi. Ni vema kama umeachana na mtu, ukaacha kumfuatilia mambo yake maana utakua unaumia pindi atakapokua anafanya vitu vinavyo uumiza moyo wako. Epuka kumfuatilia kwa siri maana utakua unatumia kwa siri hivyo hivyo.

Uamuzi mzuri wa kufanya baada ya kuachana na Mpenzi wako na kuona hakuna uwezo wa kurudiana ni kukubaliana na hali halisi, kujipenda na kuendelea na maisha yako mpaka utakapo taka kuingia kwenye mahusiano tena. Asante kwa muda uliotumia kusoma makala hii na natumaini umejifunza kitu. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy kwa mambo mengine zaidi ya tuliozungumzia hapa.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Jinsi ya kupata Namba zilizofutika kwenye Simu

Kwenye simu huwa tunatuza namba na siku hizi Smartphone huturuhusu kutunza katika Email mbali na kuzitunza katika Laini na Simu yenyewe. Mara nyingi mtu unashariwa utunze namba za simu kwenye simu yako katika Email. Email ni sehemu nzuri ya kutunza namba zako maana huwa Inazitunza namba in cloud na kuzifanya iwe rahisi kuzipata hata utakapo ibiwa au kupoteza simu. Yani hata kama umeibiwa simu, ukiwa na taalifa za Email yako uliotunzia namba tu, unaweza ingiza email hiyo kwenye simu yako nyingine na ukapata namba za simu ulizotunza. Taalifa za Email tunazoziongelea ni Email yenyewe na Password yake tu.

Ukiona dalili hizi ujue akaunti yako ya Facebook si salama BONYEZA HAPA>>>


Katika ukurasa huu wa The bestgalaxy, hatuta zungumzia kuhusu utunzaji wa namba za simu zaidi ya hapa. Ila tunaenda kueleza jinsi ya kupata Namba za simu zilizofutika.

Jinsi ya kupata Namba za simu zilizofutika

Ikiwa umefuta namba yoyote kwenye simu yako na haipo tena kwenye Lain, Email na hata katika simu yenyewe, tambua bado unanafasi ya kuipata namba hiyo. Namba iliofutika kwenye simu inaweza kuwa katika akaunti yako ya Facebook iliopo kwenye app ya Facebook ya simu yako.

Ukiwa na app ya Facebook kwenye simu yako, huwa wanaomba ruhusa ya kuchukua namba za simu ulizotunza kwenye simu yako ili wazitumie kuiweka akaunti yako ya Facebook karibu na watu unaowajua. Hii ni moja ya sababu ambazo hupelekea kuwaona watu unaowajua kwenye Facebook.
Ukiruhusu ruhusu Facebook ichukue namba za simu kwenye simu yako, hata zikifutika kwenye simu, bado zitakuepo ndani ya akaunti yako ya Facebook. Kama uliiruhusu Facebook kuchukua namba za simu, unaweza fuata yafuatayo ili kupata Namba zilizofutika kwenye Simu yako.

  • Ingia katika Facebook na ubonyeze vimistari vitatu gusa “Settings”
  • Ingia kwenye settings alafu nenda kwenye “Accounts center”.
  • Ingia kwenye “Your Information and permissions” na ubonyeze kwenye “Upload contacts”
  • Chagua account yako ya Facebook utakayoiona Pele alafu utapelekwa kwenye ukurasa uliona orodha ya majina ya namba ambazo Facebook imeyatunza.
  • Baada ya hapo utakua ukigusa tu majina ili kuona namba. Kwenye orodha ya namba hizo unaweza kuziona namba ya simu iliofutika kwenye simu yako.

Kama haukuiruhusu Facebook kuchukua namba za simu kwenye simu yako, unaweza usiikute namba ambayo unaihitaji. Ni hayo tu tulio kuandalia hapa ila usiache kutembea The bestgalaxy.

sms za mapenzi kiingereza na kiswahili

Mapenzi ya siku hizi huwa yanahusisha sana sms kwasababu watu wengi kipindi hiki huwa wanawasilina kwa sms(ujumbe). Mara nyingi hapa The bestgalaxy tumekua tukizungumzia sms za mapenzi na hapa Kwenye ukurasa huu pia tunaenda kuangalia upende huu huu wa sms za mapenzi lakini tunajikita katika sms za mapenzi katika lugha mbili. Lugha hizi ni Lugha ya kiingereza na kiswahili. Yani tunaenda kuangalia sms za mapenzi kwa kiingereza na kiswahili.

Kuna sababu zinaweza kufanya ukawa unatumia lugha ya kiswahili lakini ukataka kumtumia mwenza wako sms ya mapenzi ya lugha ya kiingereza (English). Unaweza fanya hiyo ili kuonesha utofauti tu unapochati na mpenzi wako, unaweza kufanya hivyo pia kwasababu mpenzi wako ni mtu asie elewa kishwahili sana au anapenda kiingereza tu.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>

Kama upo vizuri katika lugha ya kiingereza, unaweza tuliza kichwa na kusuka sms itayo ugusa moyo wa mpenzi wako ikiwa katika kiingereza/English. Lakini kama haupo vizuri sana au unataka kutunza muda, unaweza tumia hizi chini kwa mwanamke au mwanaume.

Ujumbe/SMS za mapenzi 5 za Kiingereza na Kiswahili

Every time I’m with you I feel like my dream has come true. I cherish you always.
Kila wakati ninapokuwa na wewe nahisi ni kama ndoto yangu imetimia. Nakupenda daima.

I love you so much. In your arms, I have found my home. You complete my life in ways I never imagined. I don’t need to lose you in my life my love.
Nakupenda sana. Katika mikono yako, nimepata nyumba yangu. Wewe unanikamilisha maisha yangu katika njia ambazo sikuwahi kufikiria. Sihitaji kukupoteza kwenye maisha yangu mpenzi wangu.

Dalili za mahusiano yanataka kuvunjika na jinsi ya kuokoa BONYEZA HAPA>>>>

Your love is the melody that fills my heart with joy. Thank you for your love honey . I love you.
Mapenzi yako ni melody(wimbo) inayojaza moyo wangu na furaha. Asante kwa upendo wako honey. Nakupenda.

With you, every day is an adventure. Loving you is the greatest journey of my life. I enjoy having you in my life.
Nikiwa na wewe, kila siku ni safari. Kukupenda ni safari kubwa zaidi ya maisha yangu. Nafurahia kuwa na wewe maishani.

Honey, i need you to know that you are the reason I believe in love. Your presence lights up my world.
Honey, nataka ujue kuwa wewe ndiye sababu ya kuamini katika mapenzi. Uwepo wako unang’arisha ulimwengu wangu.

Mwisho; Ni hayo tu tuliokuandalia hapa. Lakini kabla ya kutuma sms za kiingereza unashauriwa kufikilia kama mwenza wako hupendelea kiingereza au laa. Maana kwa watu waliozoea kiswahili hata wakiwa wanajua kiingereza kunaweza kuwa na ugumu wa maneno ya kiingereza kuugusa moyo wake. Yani wanaweza wanajua kiingereza lakini wakasisimuka zaidi wakiambiwa “Nakupenda” kuliko “I love you”.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

WOWCube: Ni kifaa gani hiki na kinatumikaje?

Kama umewahi chezea “Rubik’s Cube” basi unaweza kuielewa zaidi WOWCube. “Rubik’s Cube” ni kifaa kilichoundwa na ErnÅ‘ Rubik mnamo mwaka 1974. Ni kifaa chenye puzzle au fumbo ambalo linajumuisha kurejesha sura sita za maraba katika usawa baada ya kuvurugwa. Kuna Cube nyingine zanaubo mbali na mraba. Rubik’s Cube imekuwa maarufu zaidi ulimwenguni na inachezwa na mamilioni ya watu ulimwenguni.

Sasa WOWCube(WOWCUBE® Entertainment System) ni kifaa ambacho ni kama “Rubik’s Cube” lakini kipo kidigitali zaidi. WOWCube ipo kisasa zaidi kiasi ambacho inaitwa kifaa cha kucheza games. Kina kuruhusu kucheza games nyingi na unakua unacheza kwa kukizungusha, kukitikisa na kugusa screen. Kifaa hiki kina screen ndogo 24 ambazo zinakufanya uone vitu au games unachocheza.
Unakua unakichaji kama unavyochaji vifaa vingine vya kuchaji vya kidigitali alafu unaweza kukiunganisha na simu ya smartphone kwakutumia Bluetooth. Haijali ni simu ya Android au iOS, zote zinaweza kufanya kazi na hiki kifaa.


Kuna app yake unatakiwa uiingize kwenye simu ya smartphone unayoiunganisha nacho. App hiyo inaitwa WOWCube connect na kazi yake kubwa ni kukupa uwezo wa kuendesha kifaa cha WOWCube. Kupitia app hiyo unaweza ingiza games pamoja na app mpya kwenye kifaa cha WOWCube na kurekebisha vitu kama mwanga ili kuwa vile wewe unapenda.

Mbali na hayo, WOWCube pia inauwezo wa kuonesha notifications za kwenye simu ukiunganisha, tarehe (kalenda kwa ujumla), unaweza soma comics na kujifunza mambo mengine. Ni kifaa kizuri kwa watoto na wakubwa pia. Pre order kwenye website ya WOWCube, imeandikwa unaweza pata kwa kama dora 549 za kimalekani hivi. Hiyo ni pre-order.

Moja ya stori kuhusu jina lake lilivyotokea; wanasema kabla hakijaitwa WOWCube, watu alipokua wakioneshwa walikua wanamshangao wa “Wow”. Basi baada ya mishangao hiyo kuwa mingi, wakaamua kukiita “WOWCube”.

Athari za mwanaume kutumia pesa kutafuta mpenzi

Kwa sasa watu husema “Mapenzi ni pesa” na moja ya mambo ambayo huongelea ni kwamba ukiwa na pesa ni rahisi kupata mpenzi. Kwa wanaume, wanasema pesa inaweza kukufungulia mwanaume nguvu kubwa ya kuweza kuwavutia wanawake.
Na wewe ni mmoja kati ya watu wanao amini hayo? Sawa, ila ukweli ni kwamba pesa inaweza kufanya uvutie wanawake. Kuna wimbo wa zamani sana wa kiingereza wa Cyndi Lauper uitwao “Money Changes Everything”, yaani “Pesa hubadilisha kila kitu”. Wimbo huu kuna sehemu ni kama mwanamke anamuacha mwanaume wake na kuzifuta ahadi zote kisha kujielezea kwenye pesa huku akimwambia “…Tuliapishana upendo wa milele. Nilisema, ndio, najua, lakini tulipofanya hivyo, kulikuwa na jambo moja ambalo hatukuwa tukiwaza nalo ni pesa. Pesa hubadilisha kila kitu…”.

Wimbo wa Cyndi Lauper uitwao “Money Changes Everything”


Lakini sio wanawake wote hua hivyo, kuna wengine wamekulia katika hali za juu za kimaisha kiasi ambacho pesa haiwashtui sana na wengine wanawaogopa au wameisha fanyiwa vitu wasivyo penda na wanaume wenye pesa mpaka wakatenganisha mapenzi na pesa kwenye vichwa vyao.

Ukiwa mwanaume mwenye pesa na uwezo au mwanaume ambae hujifanya unapesa ili kuwakamata wanawake, hiyo inaweza kuwa ni njia rahisi kwako ya kuwavutia wanawake. Lakini njia hii ya kutumia pesa au kujifanya mwenye uwezo, inathari zake mnapokua kwenye mahusiano(au ndioa kabisa).

Athari 3 za mwanaume kutumia pesa kutafuta mpenzi

Kupotea kwa hisia za upendo.

Ukitumia pesa kumvutia mwanamke ambae anavutiwa na pesa au hali yako ya juu ya kimaisha unaweza jikuta unapoteza hisia za upendo mnapoendelea kuwa Katika mahusiano. Hii inaweza kutokea endapo mwanaume utatulia na kuona mwanamke amejisahau na kuweka mbele kukutoa pesa kuliko kuonesha upendo. Yani unaweza kufikia wakati ukaona kama hauna mwenza ila una mtu mnafanya nae biashara hivi na sio mahusiano. Hali hii inaweza fanya usijihisi kupendwa wala kupenda kabisa.

Kufilisika au kupoteza uwezo wako.

Mwanaume kutumia pesa kumvutia mwanamke ambae amevutiwa na pesa inaweza sababisha ukafirisika au kupoteza muelekeo wa kimaisha pindi mukiingia kwenye mahusiano. Hii inaweza tokea kama mwanamke atakua si mshauri mzuri au atakua mtu anae bomoa uwezo wako ili kujijenga yeye bila kujali chochote kuhusu wewe. Mbaya zaidi unaweza potea kimaisha alafu ukaachwa bila mwanamke huyo kujali hali yako.

Kunyanyaswa na kudanganywa.

Unaweza itumia pesa kuingia kwenye mahusiano na mtu asiekupenda kwa dhati na baada ya muda akachoka tu kukuigizia upendo pamoja na uwepo wa pesa. Hapa unaweza nyanyaswa kihisia au ukawa unadanganywa wazi wazi. Unaweza bambeleza sana mambo yawe mazuri lakini unakua haueleweki.

Mwisho; Sio Kila mwanamke unaempata kwa kuvutiwa na pesa au uwezo wako anaweza fanya mambo hayo. Ni baadhi tu ambao wako hivyo. Wanawake wengine unaweza kuwapata kwa kuvutiwa na pesa zako lakini wakakupenda na kuwa na mchango mkubwa katika maisha yako mukiwa kwenye mahusiano. Kikubwa ni kuwa makini ili kuepuka athari tulizo zungumzia. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Jinsi ya kutumia bando kidogo unapokua Instagram

Mtandao wa instagram ni moja ya mitandao huwa inatajwa sana katika upande wa mitandao yenye kutumia sana data au bando la internet kwenye simu. Katika uzoefu wako wa kutumia mtandao huu kutoka Meta, unahisi unatumia sana bando la internet? Mh sijui kwa upande wako unawazo gani lakini ukweli ni kwamba mitandao ukiwemo instagarm ambayo hujihusisha na video huwa inatumia sana bando.

Instagram ina video ambazo hua zinajiplay bila hata uamuzi wa mtumiaji na video hizi hua zinachukua bando zinapojiplay. Mbali na video, picha zenye ubora pia zipo katika Instagram na picha zenye ubora hua zinachukua bando kuliko zisizo na ubora. Lakini hatuwezi sema mambo hayo kwenye instagram ni mabaya maana ndio kati ya mambo hufanya mtu ufurahie kutumia mtandao huu. Kama jambo la bando linakuumiza sana unawezafanya yafuatayo kutumia bando kidogo unapokua Instagram.

WhatsApp yako inatatizo? Jifunze jinsi ya kutatua hapa>>>>

Jinsi ya kutumia bando kidogo unapokua Instagram

Njia rahisi na rasmi ya kupunguza matumizi ya data au bando lako la internet ni kutumia App ya Instagram Lite. App ya Instagam Lite ni app ambayo imeundwa tofauti na jinsi ilivyo App ya Instagram ya kawaida. App hii ni ndogo kuliko app ya kawaida na imepunguzwa baadhi ya mambo au vipengele ambavyo hutumia bando lako ikiwemo ubora wa picha na video . Hivyo, unapoitumia app ya  Instagram Lite unakua unatumia bando kidogo kuliko ambavyo ungetumia app ya Instagram ya kawaida. Haitumi bando lako sana app hii na inaweza fanya vizuri hata kama mtandao wa internet kwenye simu yako haupo vizuri.

Kama hautataka kutumia app ya Instagram lite basi ni unaweza punguza matumizi ya data kwa kuwasha kipengele cha Data saver ambacho hupatika kwenye app ya Instagram ya kawaida. Kuwasha kipengele hiki, gusa vimistari vitatu vilivyo juu upande wa profile yako ya Instagram. Baada ya hapo ingia kwenye “Data usage and media quality” na uwase sehemu ya Data saver utakayoiona hapo.

Mbali na njia hiyo, unaweza punguza pia idadi ya video unazoangalia au ukapunguza muda unaotumia katika mtandao huu ili kupunguza matumizi ya bando lako.

Katika matumizi yako ya simu usifanye vitu hivi GUSA HAPA>>>

Sms za kubembeleza mpenzi wako

Kubembeleza mpenzi wako sio kuwa mjinga. Ni moja katika ya mambo muhimu kufanya unapokua kwenye mahusiano ya mapenzi na mtu anaekupenda. Na kubembeleza hua kuna nyakati zake na sio kila wakati. Unaweza hitajika kumbembeleza mpenzi wako baada ya tukio lililomuumiza hisia zake, baada ya kuchukizwa, kuonesha hali ya kukataa jambo unalohitaji au unapohitaji kumtuliza moyo wake na kumuweka sawa katika penzi lenu.
Kuna baadhi ya watu husema “mimi sjui kubembeleza kwenye mapenzi” au “mimi siwezi kubembeleza kwenye mapenzi” lakini unapaswa kufahamu kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kubembeleza hawaujui.

Jinsi ya kufanya mpenzi wako akuwaze kila mara BONYEZA HAPA>>>


Kubembeleza mpenzi wako huonyesha upendo na kujali kwako kwake. Yani kunajinsi anahisi unamjali. Kubembeleza mpenzi wako pia kunaweza kuimarisha uhusiano wenu kwa kufanya muwe na maelewano ya amani. Kubembeleza mpenzi wako kunaweza kusaidia kukuza uhusiano wa kimwili na kihisia kati ya wewe na mpenzi wako. Kubembeleza mpenzi wako kunaweza kusaidia kujenga imani kati yenu pia.
Huo ni muhimu wa kubembeleza katika mahusiano ya mapenzi ila kabla hatujaendelea, ukizidi sana kubembeleza inaweza kuwa sio jambo zuri tena. Lakini katika ukurasa huu tunaenda kuangalia sms za kubembeleza mpenzi.
Kutokana na utandawazi, watu hutumia sms kuwasiliana na wapenzi wao. Sasa ukiwa mmoja wa watu hawa, kuna sms ambazo mtu unaweza mtumia mpenzi kubembeleza kwenye mambo mbali mbali kwenye mahusiano yenu. Sms hizo unaweza tulia na kuziandika mwenyewe au unaweza angalia sms zitakazo kufaa hapa chini na kuzitumia.

Maneno ambayo hautakiwi kusema kwa mwenza wako BONYEZA HAPA>>>

Sms za kubembeleza mpenzi wako

  • Wewe ndiye wangu mahabuba unaejua kunipa huba. Mwanamke ambae moyo umeushika. Nitabaki na wewe milele, sitochoka kukupenda malaika.
  • Kuna muda nakaa nawaza jinsi gani naweza fanya ili nioneshe moyo wangu unakupenda kiasi gani ili tu uondoe mashaka juu ya upendo wangu kwako kipenzi. Natamani hata kukupeleka kwa wangu wazazi. Nakupenda sana mpenzi.
  • Usije choka kunipenda honey. Na mimi siwezi choka kukupenda pia. Siwezi hata kuelezea jinsi nafurahi kuwa na wewe dear. Ninapokwambia “nakupenda” moyo wangu ndio unanituma kukuambia.
  • Amini kuwa mimi nakupenda wewe japo wanaonitamani ni wengi. Moyoni mwangu kuna chumba chako wewe, sina vyumba vya wengi na humo upo wewe tu mpenzi.
  • Tumekua hatuelewani sana katika siku hizi. Yawezekana ni shetani amekuja kutuchezea. Hebu tumshinde kwa kuanza siku ya leo vizuri kipenzi. Pamoja na yote tunayopitia, tambua sitamani kukupoteza. Moyo wangu bado unakupenda.
  • Nisikupende wewe ili nimpende nani kwenye hii Dunia? Kuwa na wewe ni ndoto niliokua nasubiri kutimiza hapa chini ya jua. Hakuna anaeweza kuniamsha kwenye ndoto hii zaidi yako. Na sitamani itokee maana nakupenda sana.
  • Ivi katika maisha yako umewahi ona penzi lililodumu kwa kusikiliza sana maneno ya watu? Mimi sijawahi, ila nimeona watu wanaodumu kwa kusikilizana tu. Hebu tupuuze ya watu twende mbele mpenzi wangu, nakupenda wewe tu.
  • Nyakati za usiku wewe hua mwezi na wakati wa mchana wewe unakua jua langu. Kiufupi umekua msaada kila wakati ili nisipote kwenye giza. Nakupenda sana mpenzi.
  • Wewe ni wapeke maishani na ninakupenda, sifikirii kukusaliti na wala sifikirii kukutenda. Nakuomba tuendelee kupendana kila siku siku habbity wangu.
  • Unataka kuondoka kwenda wapi? Unataka kunicha na nani mwenzio? Unataka kuniumiza kweli? Atatibu nani majeraha unayota kuniachia? Hebu tumia dakika chache kufikilia tulipotokea. Kumbuka kuwa nakupenda sana mpenzi wangu.

Mwisho; Sms hizi zinaweza tumika na wanawake au wanaume. Kikubwa unapotumia, hakikisha inaendana na hali yenu ya mahusiano au mazungumzo.

Jinsi ya kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG Mobile

PUBG Mobile ni Game linalokutupa katika eneo moja uwe kati ya wachezaji 100 wanao pambana kubaki hai katika eneo hilo. Gemu hili linachezwa na watu wengi sana hapa Duniani pamoja na kuzuiliwa kwenye baadhi ya nchi.


Mechi moja ya PUBG inaweza kuwa ngumu au nyepesi kwako maana unacheza na watu halisi unaoweza kutana nao alafu ukawazidi uwezo au wakakuzidi uwezo. Kiufupi ni ngumu sana kuwa mtu unaweza kumzidi kila unaekutana nae kwenye mechi ya gemu la PUBG. Kuna muda ukiwa kama mchezaji unaweza jikuta umefanya vibaya kwenye mechi na kutolewa kwenye mechi mapema.


Kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG ni jambo muhumu sana na hutoa points za uhakika. Hata usipokua na Eliminations nyingi, ukiishi kwa muda mrefu kwenye mechi utapewa points.
Kama umekua na changamoto ya kutoishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG, yafuatayo ni mambo yanayoweza kukufanya ukishi muda mrefu kwa urahisi kidogo.

Mambo ya kuzingatia kuishi muda mrefu katika mechi ya game la PUBG

Chukua Level three helmet

Unapotua na kukusanya vitu katika mechi ya PUBG, huwa ni ngumu kupata kitu unacho hitaji maana vitu huwa haviwi kwenye mpangilio unaoeleweka. Lakini kama utabahatika kupata “Level three helmet” usiiache. Level three helmet katika mechi ya PUBG hulinda zaidi kichwa chako pindi kinapo pigwa na maandui. Level three helmet inaweza kulinda kichwa chako hata ukipigwa na M24 ambayo watu huiogopa pindi inapo nguruma katika eneo.

Usitembee kwenye sehemu za wazi

Hata sehemu iwe inaonekana salama kiasi gani, hakikisha haupiti bila kuwaza utajificha wapi pindi utakapo sikia mtu kaanza kukushambulia. Ukiwa unapita sehemu ya uwazi katika gemu la PUBG ni rahisi mtu usiemuona kukuona wewe na kuanza kukushambulia. Hivyo ni vema ukawa na tabia ya kupita sehemu zisizo na uwazi ili usipoteze maisha mapema. Pendelea kupita sehemu zenye mawe makubwa, miti, majani marefu au nyumba ili kuishi mda mrefu katika mechi ya game la PUBG.

Usikimbilie Eliminations kuliko kulinda uhai wako

Kutafuta Eliminations kwenye game la PUBG mobile ni kitu kizuri tu. Ila kama utakua unacheza ukiwa na tamaa ya kupata Eliminations nyingi alafu unasahau swala la kujilinda mwenyewe, utakua haudumu sana kwenye mechi. Kabla ya kufuata mtu kushambulia, hakikisha upo kwenye upo kwenye usalama na unauhakika wa kumuweza. Kama unaona upo kwenye hali mbaya, kujificha au kukimbia inaweza kuwa uamuzi mzuri pia.

Kuwa makini unapofuata Airdrops

Airdrops zinaposhuka huwa watu wengi wanaangalia juu ili wajue zinapotua. Zikishatua tu, kuna watu wengi wanakua tayari wapo njiani kuzifuata. Sasa ukiwa mmoja kati ya watu wanaozikimbilia Airdrops hakikisha unakua makini maana watu wengi wanaenda sehemu unayoenda. Mukikutana, wanaweza kukuzidi au ukawazidili lakini sehemu za Airdrops bado huwa ni hatari maana watu wengi hushindwa.

Usitue sehemu zenye majina makubwa mara kwa mara.

Kuna sehemu Katika ramani za game la PUBG mobile huwa zinafahamika sana. Watu wengi huwa wanapenda kushuka katika sehemu hizi kiasi kwamba unaweza tua na kupoteza maisha ndani ya sekunde chache tu. Sasa ukitaka kuishi mda mrefu katika mechi ya gemu la PUBG, usiwe na tabia ya kutua katika maneno haya. Tua katika maneno ambayo watu wengi hawatui ili upate hata muda wa kujiweka sawa.

Mwisho; Game la PUBG mobile ni gemu linalohitaji ujipe muda wa kujifunza pia. Jipe muda wa kucheza Kila mara ili upate uzoefu wa kulicheza na huu uzoefu unaweza kukufanya uwe na wezo wa kuishi mda mrefu katika mechi. Asante sana na endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.

Mambo ya kuepuka katika mahusiano

Mahusiano ya mapenzi yanaweza kuwa na vitu vingi vya kuongelea na hapa Kwenye ukurasa huu tumechagua kuzungumza mambo ya kuepuka katika mahusiano. Katika mahusiano, Kuna mambo usipo ya epuka yanaweza hatarisha mapenzi au mahusiano yenu. Mambo haya haijalishi ni mwanaume au mwanamke, ni vema kuyaepuka.

Mahusiano ni kama mmea unaouotesha aldhini na kuhakikisha kuna uwepo wa mambo yanayo ruhusu mmea huo kuota au kuendelea kukua na sio kufa. Lakini pia Kuna vitu pia unahitaji kuepuka kwenye mahusiano ya mapenzi ili yasife kama mmea.

Maneno ya kumwambia mpenzi wako usiku  BONYEZA HAPA>>>

Mambo muhimu ya kuepuka katika mahusiano (wanawake na wanaume)

Kupoteza Imani


Uaminifu unatakiwa kuwa ni kati ya vitu muhimu sana katika kustawisha mahusiano. Pia uaminifu ni moja ya vitu ambayo sio rahisi kuvipata pindi mtu anapopoteza.
Kuaminiana kwenye mahusiano hufanya mahusiano ya mapenzi kuwa mazuri sana kwa wapenzi. Lakini endapo imani kati yao itatoweka, basi mahusiano yanaweza kuanza kuyumba hapo. Kama upo kwenye mahusiano na mpenzi wako ni vema kutunza na kuiheshimu imani ya mwenza wako kwako. Epuka kutumia imani yake kwako kumdanganya au kumuona mjinga siku imani ikitoweka, hata neno “Samahani” linaweza kuwa halina uzito.

Mambo muhimu kufanya kwa mpenzi mwenye hasira au ukorofI BONYEZA HAPA>>>

Kukata Mawasiliano kati yenu

Mawasiliano pia husemwa kuwa ni moja kati ya vitu muhimu kwenye mahusiano ya mapenzi. Ni kweli mahusiano ni jambo muhumu na endapo mawasiliano yatafifia au kukatika katika mahusiano ya mapenzi, Unaweza kuwa ndio mwanzo wa mahusiano kuisha. Epuka kukata mahusiano kati ya wewe na mpenzi wako maana unaweza kuwa ndio mwisho wenu.

Kushusha heshima na kuiinua dharau.

Unaweza kuwa na mahusiano na mtu, mmezoeana sana kiasi kwamba unajua vitu vyake vingi sana vizuri na vibaya. Hata ujue sana, haushauriwi kushusha heshima na kuinua dharau. Kama kuna mambo ya kumsaidia, msaidie tu bila kumdharau. Kama kuna vitu vya kumvumilia, mvumilie bila kumuonesha dharau. Epuka kumtukana, kumsema vibaya kwa watu au kutomsikiluza. Ziheshimu hisia zake na kujali upendo wake kwako.

Maneno ambayo hautakiwi kusema kwa mwenza wako BONYEZA HAPA>>>

Kukosa Malengo

Mahusiano huwa na malengo pia. Mkishatulia kwenye mahusiano ni vema kuwa na malengo mnayojiwekea ili muishi kutimiza. Msipo kuwa na malengo kwenye mahusiano, mnaweza yumba kirahisi na kuachana kwasababu ya kukosa muelekeo. Malengo hufanya mahusiano ya mapenzi yawe na muelekeo. Malengo yanaweza kuwa ni mipango ya baadaye kama vile ndoa, familia, au malengo ya kifedha katika maisha yenu.

Kuingiliana kwenye mambo mengine

Wapenzi katika mahusiano huondoleana mipaka mingi sana. Lakini unapaswa kufahamu kuwa kuna baadhi ya vitu au mambo ukiwa kwenye mahusiano unashariwa kutoingilia. Kama kuna mambo yake au vitu anapenda na haviathiri mahusiano au maisha yenu, ni vema kuishia kuwa mshauri tu au kutomuingilia kabisa. Upuka kumuingilia kwenye mambo yake binafsi.

Mwisho; mambo yote tulio ya zungumzia hapa, yana umuhimu mkubwa katika mahusiano. Hatakama kutakua na changamoto katika kuyazingatia, ni vema ukapambana na kuanza kuyazingatia ukiwa kama mwanamke au mwanaume.

Kuwa mjanja! Tufuate kwenye akaunti zetu mpya za kijamii ; Instagram na Facebook

Matumizi ya simu ya zamani unaponunua mpya (usiiuze au kuidharau)

Mara nyingi watu, hutumia simu walizonunua alafu hununua nyingine mpya baada ya muda flani. Sababu za kununua hutofautiana maana kila mtu huwa na jambo lake liliomsukuma kutoa pesa yake na kunua simu mpya. Kuna watu hununua simu mpya baada ya kuona simu ya zamani imeharibika kabisa, wengine hununua baada ya kupoteza simu, pia kuna wengine huwa wananuanua simu mpya kutokana na kuichoka simu ya zamani au kutamani kubadilisha simu tu.

Kama unatabia ya kununua simu mpaya ili kubadilisha simu au kwenda na wakati ni jambo zuri. Simu mpya huwa zinakuja na maboresho pamoja vitu vingine vizuri kwa huo wakati zinaotolewa. Hivyo kwenda na wakati katika upande wa simu ni jambo zuri. Lakini unaponunua simu, mpya simu ya zamani huwa unafanya nini?
Kama haujui matumizi ya simu yako ya zamani unapo nunua simu mpya, soma hapa chini ili kufahamu jinsi wanavyoweza itumia.

Matumizi ya simu ya zamani unapo nunua mpya

Badili kuwa kifaa cha games

Simu yako ya zamani kama ipo vizuri na inaweza kuwekwa games za kucheza, basi ibadili kuwa kifaa cha games. Kuna games nzuri sana ambazo unaweza zijaza kwenye simu hiyo alafu ukitulia ukawa unazicheza. Sio lazima iwe wewe tu unacheza, hata ukiwapa watoto inaweza kuwa vizuri pia.

Ifanye WiFi ya nyumbani

Simu za smartphone huwa zina WiFi ambayo unaweza unganisha vifaa vingine vinavyotumia internet alafu vikatumia internet kupitia simu hiyo. Sasa endapo itakua na simu ya zamani na laini ya simu usioitumia, unaweza weka bando la kutosha kwenye hiyo laini alafu ukiingiza kwenye simu kisha ukawa unaitumia iyo simu kama WiFi ya nyumbani kwako. Kama unatumia internet kwenye PC au simu yako, hii inaweza kuwa nzuri kwako maana utakua unaiunganisha kifaa chako kwenye simu hiyo ya zamani ili kupata internet.

Iweke kuwa simu ya nyumbani

Unasimu ambayo ukiwa mbali na nyumbani ukiipiga mtu yoyote aliopo nyumbani anaweza ipokea? Mh sawa. Ni vema kuwa na simu ya nyumbani ili ukipata dharura au wakipata dharaura watu alioko nyumbani muwasiliane. Kama hauna simu ya zamani, unaweza ibadili kuwa simu ya nyumbani kwa kuiwekea laini na kuwaambia wanaoshinda nyumbani waitumie kama simu ya nyumbani tu.

Badili kuwa kifaa Cha Muziki na video

Kama unapenda kusikiliza nyimbo na kuangalia filamu, basi simu yako ya zamani inaweza kukufurahisha kwenye hilo. Unaweza ijaza nyimbo zote ambazo huwa ukitulia unazisikiliza sana bila kuchoka au ukajaza filamu unazozipenda sana. Baada ya kufanya hivyo ukipata muda utakua unachukua iyo simu na kusikiliza nyimbo au filamu zako bila Kuigusa simu yako mpya na kumaliza betri.

Tunzia file usizotaka kutembea nazo au zipotee

Simu yako ya zamani pia inaweza tumika kama kifaa cha kuhifadhia vitu vyako. Unaweza ingiza mafaili ambayo hautaki yapotee au hautaki yawe kwenye simu yako mpya. Ukishaingiza, unaweza ficha hiyo simu sehemu ambayo unahisi ni salama. Kama ni mtu unaekumbuka password, basi unaweza weka na password kwenye simu hiyo.

Unaponunua simu mpya, usisahau kuwa thamani ya simu ya zamani bado ipo. Kikubwa ujue jinsi gani utaitumia simu ya zamani baada ya kupata simu hiyo maana usipojua hautaiona thamani yake.

Mbali na yote, kuiuza au kuigawa ni jambo zuri pia maana unakua ni kama unawasaidia watu wengine kupata simu na kuwaonesha upendo.