All posts by Admin

Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako

Kuna wakati unaweza tulia na kuamua kumfurahisha mpenzi wako kupitia simu. Kuna mambo mengi sana unaweza mfanyia kupitia hiyo simu na akafurahi. Inaweza kuwa ni unampigia mnaongea mambo mazuri, unamtumia picha na hata ujumbe tu wa maandishi.

Na tena sio lazima muwe mnaishi mkiwa mbali mbali ndio mtumie simu kumfurahisha. Unaweza mfurahisha mpenzi wako kupitia simu hata kama mnaishi nyumba moja. Kumtumia ujumbe mzuri asio utarajia kwenye simu yake ni jambo unaloweza fanya kama utani ila linaweza kufanya afurahi sana hatakama mnaishi pamoja.

The bestgalaxy tumekua mstari wa mbele kuhakikisha hauumizi kichwa sana kwenye mambo ya mahusiano. Katika ukurasa huu, tumekuandalia orodha ya ujumbe mzuri kwa mpenzi wako. Kama unahitaji kumtumia mweza wako ujumbe unaoeleza hisia za upendo ulionao kwake, basi unaweza chukua itayokufaa hapa.

Sms za kumwambia mpenzi wako kuwa unampenda BONYEZA HAPA>>>

Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako (Mwanaume au Mwanamke)

  • Unahisi kuna mwanaume anaependa mwanamke mzuri hivyo amkukose kisa mimi? Au wanawake wengine wanapenda unavyo kuwa na mimi? Hapana, hawapendi kuona tukipendana hao. Kuwa pamoja ni pigo letu kwao.
  • Penzi lako hunisukuma kutaka nikuulize “Nikupatie nini hapa Duniani ufurahi?” lakini nakumbuka siwezi kupa kila kitu. Ila ningekua na wezo, ningekupa tu kama nilivyokupa huu moyo wangu wa pekee uwe nao wewe mpenzi.
  • Sauti tamu ninayopenda kuisikia masikioni mwangu bila kuchoka ni Sauti yako. Mtu pekee ninaempenda bila kuchoka ni wewe. Kitu pekee ninachoweza pokea bila kuchoka ni penzi lako.
  • Waliopita walinifundisha kuwa mapenzi ni maumivu na nisiamini mtu. Wewe umenifundisha maana sahihi ya mapenzi na radha yake hadimu. Umenifanya niwasahau mazima, nimekupenda na nakukuona wewe tu.
  • Umenizamisha kwenye hisia za mapenzi mpaka najiona mimi na wewe tu kwenye Dunia. Na naogopa ila kwasababu nakuamini, naendelea. Nakupenda na naamini popote nikwa na wewe, sijapotea.
  • Nashindwa kuelezea jinsi nakupenda ila hebu fikiria; kila nyota angani ingekua inawakilisha jinsi ninavyokupenda. Unahisi ningekua nakupenda kiasi gani?
  • Niende nikaombe nini kwa jirani? Nikaombe Maji ili nikate kiu? Hapana, wewe tayari umeiweza kiu yangu. Siwezi hata kuiomba Asali kwao maana natosheka na vitamu unavyonipa malkia wangu.
  • Kuna muda huwa nakosa kabisa furaha na Sababu za kufurahia maisha yangu. Ila nikikumbuka nina wewe maishani, furaha humwagika kama maji ya mvua moyoni.
  • Usijiuze nakupendea nini mpenzi wangu. Utauchosha bongo wako Bure. Ninasababu nyingi sana za kukupenda wewe. Na hata ukiziondoa, bado nahisi Moyo wangu uliumbwa kukupenda wewe.
  • Kabla ya kukutana na wewe, nilitamani kukutana na mtu kama wewe nimpende maishani. Sasa nimekupata, nakupenda na kwenye maisha umekua kama Nuru gizani.
  • Najua kunamuda tunagombana au hatuelewani. Lakini tambua sijutii kukupata Ila najutia kuwa nawe mapema hapa Duniani. Moyo wangu unakupenda na umejaa mpaka akilini.

Katika orodha hii, Kuna ujumbe unaoweza kutuma kwa mwanamke na hata Mwanaume pia. Kwaiyo hii ni kwa watu wa jinsi a zote. Kikubwa hakikisha unatambua muda amambao utakua mzuri kwa mpenzi wako kupokea. Angalia na maana sahihi ya ujumbe ili mpenzi wako aelewe unacho maanisha unapomtumia.

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy

Jinsi ya kupata Tiketi za Ndege za bei rahisi

Unapokua na mpango wa safari mbele yako, unaweza kuwa na uwanja mkubwa wa kuchangua ni usafiri gani utaoutumia kwenye hiyo safari. Lakini hiyo safari ikiwa ni ndefu, usafiri wa anga ndio unaweza kuwa ni chaguo sahihi kwako. Katika usafiri wa anga, kupanda ndege kutaokoa sana muda wako ambao ungeupoteza kwenye vyombo vingine vya usafiri kama vile Gari au Meli. Kwa mfano; Ukiwa na safari inayokuchukua masaa mengi au siku nzima kwenye gari, katika ndege safari hiyo inaweza kukuchukua Dakika au masaa machache sana.

Kwaiyo, pamoja na kwamba kusafiri kwa ndege huonekana kama ni gharama sana, Bado ni chaguo zuri kwasababu huokoa muda. Ndani ya dakika au saa unaweza kuwa umefika katika sehemu unayohitaji kuwa. Na hii ndio Sababu kubwa ya watu kutumia njia ya anga katika safari zao ukiondoa Sababu zao nyingine binafsi.


Sasa hapa chini kwenye ukurasa huu, tunaenda kufungua ubongo wako juu ya jinsi gani wanaweza pata ticket za ndege za bei rahisi ili usafiri bila kutumia Pesa nyingi.

Tunazungumzia hilo kwasababu watu hupata ticket za ndege kwa bei tofauti tofauti. Kuna watu hulipia pesa nyingi kupata au kubook Ticket na pia Kuna watu hupata ticket hizo kwa bei rahisi. Na ikiwa wewe unahitaji kupata Ticket za ndege kwa bei rahisi, tumia njia hizi chini.

Unaweza kubook ndege kwa App ya M-Pesa BONYEZA HAPA>>>

Njia ya kupata Tiketi za ndege za bei rahisi

Tafuta Tiketi Mapema

Ukihitaji Tiketi za ndege za bei rahisi, njia moja ya kuzipata ni kuwahi kuzitafuta. Yani tafuta Tiketi za ndege angalau hata mwezi 1 kabla ya safari yako. Mara nyingi Tiketi za ndege huwa zinakua bei rahisi kama siku ya kusafiri ipo mbali. Alafu tena bei huwa inapanda kadri siku ya kusafiri inapokaribia.

Kwaiyo kuwahi kuzitafuta tiketi kunaweza kukusaidia wewe kulipia pesa kidogo. Hii itakusaidia kuokoa pesa zako hasa kwenye zile safari zisizo za dharura.

Linganishia Bei za Ticket

Kama unasafari ya kwenda mahali flani, fahamu kuwa una uwanja mpana wa kuchagua ndege utayoitumia iwe ya shirika gani na hata ticket utaipata sehemu gani. Mashirika ya ndege yanaweza tofautiana bei na hata sehemu unazoweza pata Tiketi zinaweza tofautiana bei pia.


Kwaiyo ni vema ukawa na tabia ya kuangalia Tiketi unayohitaji inapatikana katika sehemu ngapi na tofauti ya bei Iko vipi. Alafu baadae uchague ambayo ni bei rahisi kwako na ulipie.

Kwasasa mtandaoni kuna tuvuti nyingi za kulinganisha bei za Ticket za ndege kwa wanao book ticket mtandaoni. Mfano mzuri ni hii iitwayo Skyscanner

Tumia Ofa au Punguzo

Kuzingatia Ofa au Punguzo kunaweza kukufanya upate ticket za ndege kwa bei rahisi pia. Punguzo la bei au Ofa zinaweza tokea kwenye mashirika ya ndege au tuvuti za ticket kwaajili ya kuvutia wateja wao.

Ukizingatia mambo kama hayo, unaweza kujikuta unaokoa pesa yako kwenye baadhi ya safari zako za ndege. Nasema hivyo kwasababu Ofa na Punguzo, mara nyingi hufanya ulipie pesa kiasi kidogo kuliko ambayo unapaswa kulipia kikawaida.

Safari siku au misimu isio na mambo mengi

Kama ulikua haujui, basi leo fahamu kuwa Bei za tiketi huwa juu wakati wa likizo, mwisho wa wiki, na kipindi cha msimu wa sikukuu. Kwaiyo ukihitaji kupata Tiketi za ndege zinazosafiri katika wakati huo, utalipia kiasi cha pesa kinachoweza kuwa cha juu kuliko kawaida.

Kusafiri siku za katikati ya wiki na vipindi vingine mbali na msimu wa sikukuu, kutakufanya upate ticket za ndege kwa bei rahisi. Hii ni kwasababu muda huo Tiketi huwa katika bei ya kawaida.

Natumaini mambo au njia hizi zitakusaidia katika kupata Tiketi bila kutumia Pesa nyingi. Kikubwa unatakiwa kuwa makini sana unapokata Tiketi ili kuepuka usumbufu unapotaka kukamilisha safari ulioipanga.

Mambo ya kufanya kwa Mpenzi asieonesha kukupenda katika Mahusiano

Mahusiano mara nyingi huanza kwa msukumo wa hisia kali. Yani kila mmoja anajihisi kuwa na haja kubwa ya mwenzake. Kila jambo linaonekana kuwa jipya na lenye kuvutia, Wapenzi wote wanajitahidi kwa hali na mali kuhakikisha wanampendeza au kumfurahisha mwingine. Lakini, kadri muda unavyoenda, hali hii inaweza kubadilika, na baadhi ya watu huanza kuhisi kama hakuna mapenzi ya dhati kama awali.

Hii ni hali inawakumba watu wengi, hata walio kwenye ndoa za muda mrefu. Kuna wakati mtu anajikuta anaendelea kutoa upendo, lakini mwenzake haonyeshi kujali au kuonyesha hisia zozote za kurudisha upendo huo. Hali kama hii inaweza kumkatisha tamaa, kuleta Mawazo na kumfanya mtu ahisi vibaya, hasa pale anapokuwa amejitolea sana kwa ajili ya uhusiano hayo.

Katika Hali hii, kabla ya kuchukua hatua yoyote, ni muhimu kujua kwamba yapo mambo ambayo unaweza kufanya ili kuboresha hali hii na kufufua tena mapenzi kwenye uhusiano wenu. Katika makala hii, tutazungumzia mambo unayoweza kufanya ili kurekebisha hali hii ikiwa imekutokea ghafla kwenye mahusiano yako.

Ujumbe wa Mapenzi kwa umpendae BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kufanya kwa Mpenzi asieonesha kukupenda katika Mahusiano

Kuwa mpya au tofauti kwake



Kuna wakati mpenzi wako anaweza kuwa ameacha kukuzingatia kwasababu amekuzoea. Yani anaweza kuwa anaona vitu unavyofanya kwake au ukiwa nae ni vitu ambayo vinajitudia mpaka anakuona hauna cha kushangaza. Hapa nazungumzia vitu kama, jinsi unavyoongea nae, muda unaangeanae, zawadi zako, sehemu mnazoenda, ahadi unazoahidi na mambo mengine kama hayo.
Ikiwa tatizo ni ili, basi utatakiwa kuwa mtu mpya kidogo kwake. Yapindue mambo ambayo unamfanyia au mnafanya kwa pamoja. Na usiyapindue kwa ubaya, fanya baadhi ya mambo mzuri kwa kumjali lakini iwe ni tofauti na alivyozoea. Kufanya hivyo kwa mpenzi asieonesha kukupenda katika Mahusiano kunaweza mfanya aanze kukuzingatia kwa upendo.

Tafuta tatizo upande wako na wake



Kama kutokukuzingatia kwake kunaonekana kuwa ni jambo zaidi ya kukuzoea, basi jaribu kutafuta sababu ya hali hiyo. Kwanza kabisa jaribu kufikilia kama wewe ndie tatizo maana kuna mambo unaweza kuwa umemfanyia ndio maana hakuzingatii. Fanya kufikilia vitu alivyowahi kukuonya au ambayo unajua kabisa viko upande wako lakini yeye humchukiza. Ukipata tatizo upande wako, fanya kuliweka sawa.
Ukikuta upande wako hakuna sababu yoyote ya yeye kuwa hivyo, fanya kuhamia upande wake sasa. Jaribu kufikilia na kudadisi ni kitu gani kimembadilisha hivyo. Tafuta sababu ili ujue uitaweka vipi hali vizuri.

Ukifanikiwa kupata tatizo linalomfanya mpenzi wako asikuoneshe kukupenda, jaribu kuliweka sawa ikiwezekana hata kwa kumshirikisha.

Kaeni muongelee hilo tatizo kwa pamoja



Njia rahisi ya kumaliza matatizo ni hii maana inafanya wote mufunguke yanayofanya musiwe sawa na kujadili mfanye nini ili hali iwe sawa. Fanya kukaa na mpenzi wako muongelee tatizo ambalo unaliona kwenye mahusiano yenu. Hakikisha unamtafuta mida mizuri ya kuongelea mambo haya ili aweze kufungua yaliomo moyoni kwake.

Usipokaanae muda sahihi, anaweza kukuficha yaliopo moyoni mwake. Kama ni mume au mke wako, unaweza ongea nae muda wa kulala au mkiwa metulia baada ya kucheza michezo yenu. Kama ni wapenzi tu, unaweza tafuta muda wenu mzuri wenye utulivu kama mida hiyo nilioiieleza. Usitumie simu kuongea, kutaneni ana kwa ana muongee ndio mtaweza elewana vizuri.


Mwisho; Ningependa kukukumbusha kuwa usisahau thamani yako. Kuna mambo mengi ya kuvunja moyo katika Mahusiano yanaweza kukuvunja moyo ila usisahau kuwa kuitambua thamani ni muhumu. Ikiwa unaona dalili za kuwa mpenzi wako hataki tena mahusiano na wewe, ni sawa kuheshimu maamuzi yake. Unaweza muacha alafu ukamtafuta mtu mwingine anaeijua thamani yako.

UTAMU WA JUMLA 02 (Simulizi ya Maandishi)


Wakati nakusanya nguo ghafla mlango ukagongwa “Ngo ngo ngo” na sauti ya Jimmy akisema “Oi wewe”.
Niligundua ni Jimmy nikasema “Oya… Umerudi sasa haha” akawa anasukuma malango huku anasema “Ahaha
nimekuja na shemeji yako huyu” huku akimruhusu mtu aingie. Mimi nikatupa macho kuangalia mtu anaeingia ni
nani, nikakuta ni Zuwena amevaa nguo nyeusi fupi alafu inaangaza kiasi ambacho baadhi ya sehemu zake za mwili
zinaonekana na Jimmy alikua anamshika kiuno alipokua akiingia ndani. Nilipomuona Moyo wangu ulidunda kwa
mshtuko “Nduh” na nikahisi kama kuishuwiwa nguvu hivi…
Nikaona bora nijikaze tu ila nisiwe na maneno mengi hapo maana nawezajikuta nimesema kitu kibaya. Nakumbuka
nilimsalimia Zuu kama ndio mara ya kwanza nakutana nae hapo. Na yeye alikua ananisalimia kama sijawahi ongea
nae kwa ukaribu. Baada ya kuwasalimia nikatoka nje na nguo nilizokusanya ili kuzifua na kuwaacha mule ndani.
Nilivyotoka tu, Jimmy aliufunga mlango ili mtu yoyote asiingie mule ndani na mimi sikua na hofu juu ya hilo
maana vitu vyote ambavyo vilikua vinahitajika ili nifue vilikua vinapatikana nje.
Nilichukua ndoo nikachota maji, nikavuta kiti pembeni ya chumba nilichukua nakaa alafu nikaanza kufua. Kichwa
changu muda huo kilikua hakipo sawa kabisa maana nilikua naona rafiki yangu Jimmy anaenda kula tunda la mtu
ninaempenda na kwakua sikumwambia basi nikaona acha niendelee kuumia moyoni tu kimya kimya huku nikifua
japo bado kichwani nilikua najiuliza “Amempataje huyu kiiumbe? Mbona sijawahi waona wakiwa karibu? Dah yani
Zuu nae inaonekana hanikubali kabisa maana aliponiona hata hakushtuka.ila namtamani sana huyu mwanamke”.
Wakati naendelea kufua ghafla nikaanza kusikia visauti toka ndani kupitia kidilisha kilichokua karibu na nilipokua
nafua. Mara ya kwanza nilikua nimevipuuza visauti hivyo nikawa nahisi ni Jimmy na Zuu wanaongea kawaida
kimahaba lakini baadae nikaanza kusikia sauti inaongezeka na inakua kama Zuu anabishana na Jimmy mule ndani.
Hali hiyo ilinifanya niache kufua nisogee zaidi kwenye dilisha nijue wanabishana nini humo ndani badala ya kuanza
mambo yao. Nilipotega sikio nikasikia Zuu akiwa na sauti kama amechukia hivi akisema “Usiniguse kwanza, Mimi
nataka uniambie ukweli kwanza… umesema hapa ni kwa nani?” Jimmy akawa anajibu “Kama nilivyokwambia
Zuwena, kwa rafiki yangu hapa… Kwanini unakua mgumu kunielewa” Zuu akajibu “We endelea kunidanganya tu, si
umeniona mimi mtoto mdogo? hiyo michezo naijua, usiniguse”. Nilimsikia Jimmy akisema “Tatizo huniamini…
Kama nilivyokwambia, mimi nakaa kule ila funguo kuna mtu ameondoka nayo ndio maana nimekuja kwa rafiki
yangu huku. Hata kodi ya hapa huwa nalipa mimi, huyo jamaa alietoka hapo nje huwa ni kama namsaidia tu maana
hayupo vizuri kipesa. Alafu nilishakwambia habari ya huyo jamaa hapo… Sasa kinachokufanya ubadilike sijui ni kitu
gani”. Nikakuta Zuu anamuuliza Jimmy “Yani umeniona mimi mjinga sana bora hata ungekua mkweli tu… Mimi
naona humu ndani kuna nguo zako ninazo zijua na hata viatu alafu bado unasema hapa sio pako. Sawa, kwasasa
naomba uniache niondoke maana nimekuchoka”. Mimi hadi hapo nikaanza kupata picha kidogo ya kinachoendelea
humondani. Kwa maongezi yale nilio yasikia nikajua tu huenda Jimmy hadi amemfikisha hapo huyo mwanamke ni
baada ya kumdanganya sana na muda huo uongo wake uligundulika na jambo hilo lilpelekea mpaka huyo
mwanamke kutaka kutoka humo ndani.
Basi nikatoka pale dilishani nikarudi nilipokua nafua ili kama wanatoka wasijenikuta pale na kugundua nilikua
nawasikiliza. Baada ya dakika kama tano hivi nikasikia mlango unafunguliwa, wakatoka kama wapo vizuri tu japo
Zuu alikua na sura inayoonesha amekasirika na Jimmy alikua ni kama anaaibu kiasi kutokana na kilicho mtokea.
Nakumbuka waliniaga pale alafu wakawa wanaondoka na kuniacha nikwa nafua. Kiukweli siku walivyokua
wanaondoka waliniacha nikiwa na furaha sana moyoni kwangu kutokana na kutofanikiwa kufanya mambo yao
humo ndani. Nilikua napenda sana Jimmy afanikiwe kwenye mipango yake kwasababu ni rafiki yangu lakini kwenye
Suala la kumkamata Zuu, sikulipenda maana mimi pia nilikua nampenda sana Zuu japo sikumwambia.
Nilipokua nikiendelea kufua na kufurahia tukio lililotokea, gafla nikaanza kufikilia tena yale maneno nilioyasikia
dilishani na kuanza kuwaza “Inamana Jimmy amemwambia Zuu mambo mengi kuhusu mimi alafu mimi sijui… Dah
na najua hawezi kuongea ukweli au jambo la kunisifu, lazima alikua ananiponda ili aonekane ni mtu wa juu”. Na kweli baada ya tukio hilo chuoni kulikua na watu wengi wajua juu ya Jimmy na Zuu. Zuu alimchafua sana jimmy
hapo chuoni kwa kuwaambia watu vitu alivyokua anaambiwa na Jimmy. Kulikua na maneno mengi ya Jimmy
kujigamba kwa Zuu ambayo yalienea kwa watu pale chuoni ila moja ya vitu nilivyosikia mwenyewe Jimmy
alimwambia Zuu ni kwamba ananilipia kodi tu lakini hakai na mimi. Jambo hili liliniumiza sana maana nilihisi
huenda ndio chanzo cha Zuwena kunipuuza nilipokua namtafuta. Lakini kwakua Jimmy alikua ni rafiki yangu,
nilipuuzia na tukaendelea kuwa pamoja hapo chuo.
Pamoja na yote yaliotokea, sikuwahi mtafuta tena Zuu. Nilikua nimetulia na mpenzi wangu sara na alikua anasema
ananipenda kweli. Niliweka moyo wangu wote hapo huku nikiwa na soma sana lakini nilivyozama sana katika penzi
lake, nikakuta Sara anaanza kunibadilikia tena. Ghafla tu alianza tabia ya kutonitafuta mpaka nimtafute na hata
nikimtafuta anaweza sema atanitafuta lakini hafanyi hivyo. Hali hii iliniumiza sana maana nilikua najua kwamba ni
dalili ya kuwa Sara amepata mwanaume mwingine. Nilichanganyikiwa sana kipindi hicho mpaka masomo nilikua
naona hayaeleweki. Hakuniambia kwamba tuachane ila tabia yake ilionesha kuwa tayari ameishaniacha ila ni mmi
tu ndio sijui. Nilifuatilia nikakuta kumbe kapata Mwanaume mfanyakazi na anamiliki mpaka gari. Niliwahi shuhudia
kwa macho yangu Sara akiingia kwenye gari baada ya kutoka chuoni. Niliumia sana na nikaamua kukubaliana na
uhalisia kuwa nimeachwa ila moyoni nikajisemea “Siku nikipata ajira na kuwa na hela nitawakamata sana
wanawake… yani nitawala sana. Ntanunua gari na ntakuwa na wanawake kila kona… Siwezi mpa moyo wangu
mwanamke auchezee kama hivi, ntakuwa nao wengi ili niwachezee wao… Pesa nyingine nitakua natumia na
marafiki tu maana ni bora marafiki kuliko kuwa na mpenzi”.



Basi siku zilisonga hapo chuo mpaka tukamaliza na kurudi nyumbani Tabora. Nakumbuka mimi na Jimmy tulirudi
nyumbani na tulikua tunaishi kwa wazazi wetu. Kwetu na kwakina Jimmy ni karibu sana. Kwao ni nyumba ya tatu
kutoka kwetu. Tulivyokua wadogo hatukua pamoja, familia yake ilihamia hapo kipindi nipo sekondari na yeye
alikua sekondari na tulipokutana tukawa marafiki mpaka tulipoenda chuo pamoja na kurudi pamoja. Tulivyorudi
tulikua mabishoo sana na tunapendeza juu mpaka chini kila muda na masimu yetu makubwa ya kupalasa.
Baada ya miezi kadhaa ishu ya chuo tukawa tumeimaliza kabisa tukawa tunamawazo ya kupata Ajira kichwani
mwetu kutokana na vyeti tulivyopata. Lakini tulianza kuona kama neno “ajira” linaongelewa kwenye ma TV alafu
hatuzioni mtaani na hata wakiziongelea kwenye TV mara nyingi wanasema “changamoto ya upungufu wa ajira”.
Jambo hili lilinifanya nijiulize “Inamaana pamoja nakuwa na vyeti Ajira naweza kupata au nisipate? Duh!”. Siku moja
nikakuta tu ghafla jamaa yangu Jimmy kasafili. Na hakuniambia kwamba anasafiri mpaka nilipomcheki kwenye simu
“Wewe uko wapi mwanangu, mbona haujaonekana leo” ndio akaniambia amerudi Dar. Mimi nikamuliza “Mbona
hukuniambia rafiki yangu?” akasema “Hahaha ilikua ni ghafla mzee, Nitakucheki tutaongea vizuri”. Mh Mimi
nikajua atanicheki kweli lakini haikua hivyo, siku zilizidi kusongea tu hanicheki na hata nikimcheki ananiambia
“ntakucheki”. Baadae nikakata tamaa kabisa ya kumtafuta maana nilikua najua nimuongo hivyo ukimsikiliza
unapoteza muda nikakata mawasiliano nae. Kiukweli baada ya Jimmy kuniacha kule Tabora nilianza kuwa na
mtizamo tofauti kidogo juu ya Marafiki, nilikua kama nimegundua kuwa marafiki hawajashikana na maisha yangu,
wanaweza ondoka muda wowote.
Nikaendelea kukaa pale nyumbani bila mafanikio ya kupata ajira na wazazi nilikua naona hawaniwazi tena kwenye
mambo ya pesa, wao walikua wapo tayari walipie mamilioni sehemu nisome au nipate kazi kuliko kunipa mimi pesa
ya hivi hivi tu. Kadri siku zilivyo zidi kusonga nilianza kuchakaa kimuonekano kutokana na kukosa hela. Wakati
nakuja kutoka chuo nilikua napendeza kiasi kwamba nikikutana na mtu ananiuliza “Hiyo sendo uliovaa mguuni
shingapi?” nikimwambia bei anasifia “Dah nzuri sana hiyo sendo!” lakini mambo yalibadilika kiasi kwamba
nakutana na mtu ananiangalia juu mpaka chini alafu anauliza “Hiyo gundi ni supagruu?” namuuliza “Wapi? hapa
kwenye sendo?” Anajibu ” ndio, hapo mguuni” namwambia “Ndio ni yenyewe” ananijibu “Gundi nzuri sana
hiyo!”. Kiukweli nilichakaa sana na hali hiyo ilinifanya niwe na kiu ya kufanya chochote nipate ajira na ilikua kama
bahati hivi nilikutana na tangazo ambalo liliingia kwenye simu yangu kama ujumbe. Ujumbe huo niiliona kama fulsa
hivi kwasababu ulikua unaeleza kwamba kuna kampuni inaenda kuanzishwa na kabla ya kuanzishwa Dar inatoa
mafunzo kama miezi sita hivi na waliopata mafunzo ndio wataajiriwa. Kulikua kuna namba zao pale kwenye ujumbe
ili kupata maelezo zaidi…

INAENDELEA….

Hii ni simulizi ya UTAMU WA JUMLA ilio katika maandishi. Ina uhusiano kidogo na Simulizi ya SUKARI YA DADA na MZIGO WA WAKUBWA. Inapatikana katika Sauti pia. Inavipande 11.

KUMBUKA: Hairuhusiwi kusomwa na mtu mwenye umri chini ya miaka 18.

Ukihitaji simulizi zote 3, Njoo WhatsApp

Jinsi ya kufanya video za TikTok ziwe na ubora/Quality

TikTok ni miongoni mwa platform maalufu sana ulimwengu, ambazo watu hutumia kuangalia video mbalimbali katika Internet. Mbali na kuangalia video, TikTok pia ni platform nzuri kwa Wafanyabiashara pamoja na watu wangine wanaojihusisha rasimi na uzalishaji wa video ( content creators).

Katika makala hii, tunaenda kuzungumzia jambo ambalo asilimia kubwa ya watu wanaotumia TikTok linawagusa. Jambo hilo linahusu ubora wa video za TikTok.

Unaweza ukawa unaweka video kwenye akaunti yako ya TikTok lakini video zako zinaingia TikTok zikiwa hazina ubora/Quality. Lakini pia unaweza kuwa unaangalia video za TikTok lakini video zinakua hazina ubora unaokufurahisha. Hayo mawilli yote ni matatizo na kama unayopitia, basi tambua yanaweza kuwekwa sawa na ukaanza kuweka au kuangalia video za TikTok zikiwa na ubora.


Hapa chini nimeeleza njia au dondoo zinazoweza kukusaidia kuongeza ubora wa video za TikTok ukiwa unaangalia au kuweka video zako. Katika kuelezea, tutakupa na mwanga kidogo juu sababu zinazoweza pelekea video za TikTok kutokua na ubora.

Jinsi ya kutengeneza Pesa katika TikTok BONYEZA HAPA>>>

Njia za kufanya video za TikTok ziwe na ubora/Quality

Tumia TikTok ya kawaida na sio TikTok Lite



Fahamu kuwa kuna app za aina mbili za TikTok unazoweza tumia kwenye simu. Kuna ya TikTok ya kawaida na pia Kuna app iitwatwayo “TikTok Lite”. TikTok Lite ni app rasimi ya TikTok isiotumia sana Data au bando lako.

App hii ni nzuri sana kuitumia unapohitaji kupunguza matumizi ya data au bando lako la internet. Lakini tatizo ni kwamba, unapotumia app hii unakua unaletewa video zisizo na ubora wa hali ya juu. Video huwa zinapunguzwa ubora unapozinangalia na hata unapoweka.

Kwaiyo ukihitaji kufurahia video zenye ubora, fanya kutumia app ya TikTok ya kawaida.

Zima Data saver



Kama unatumia app ya TikTok ya kawaida na bado ubora wa video sio mzuri, unaweza angalia kama kipengele cha “Data Saver” kama kimewashwa.

Kufanya hivyo utatakiwa kuingia kwenye “Settings” ya app ya TikTok alafu Chagua “Data Saver”. Ukifanya hivyo, utapelekwa kwenye ukurasa ambao utaangalia kama Data saver itakua imewashwa au haijawashwa.

Kama imewashwa, fanya kuizima maana ikiwa imewaka hupunguza ubora wa video ili kutunza Data.

Ruhusu “High-quality uploads”



Hii ni kwaajili ya watu wanahitaji kuziweka video zao kwenye TikTok zikiwa na ubora wa hali ya juu. Hapa Nazungumzia content creators au watu wanaorekodi video zikiwa kwenye ubora wa hali ya juu.

Katika TikTok Kuna kipengele unapotaka kupost video kinatakiwa kiwe kimewashwa ili video yako iliokatika ubora wa hali ya juu iingie kwenye TikTok ikiwa na ubora wa hali ya juu.

Kuwasha kipengele hicho, unapokua unapost video yako, bonyeza sehemu ilioandikwa “More Options” kisha Ruhusu “High-quality uploads”.
Baada ya kufanya hivyo, video zako zitakua hazipungui ubora unapoziiingiza katika TikTok.

Huu ni ushauri kwa mtu anaesema “Naipata pesa lakini siioni” katika Maisha

Ikiwa unapambana kupata pesa na unapata lakini hauioni, hii makala ni ya kwako.


Kwanza unatakiwa kujua kuwa watu wengi wapo kwenye hali hiyo kwa sasa. Yani unaweza kuwa na pesa ndogo au nyingi zinazoingia lakini zinapita mkononi mwako tu na hazituli.

Pamoja na kwamba watu husema “Pesa sio Kila kitu” lakini unatakiwa kuelewa kuwa maisha ya sasa yanahitaji pesa. Hii ni kwasababu asilimia kubwa ya vitu vilivyopo kwenye maisha yetu, vinatumia pesa na vinadai pesa kabisa Yani.

Mfano; ukiwa umepanga nyumba unayolipa elufu 50 kwa mwezi inamaana katika Maisha yako Kila baada ya siku 30 unalipia elufu 50. Sasa hapo Ukijumlasha na mambo ya chakula, umeme na mambo mengine yanayojitokeza kwenye mwezi unaweza jikuta Kila mwezi unatakiwa kwenye mikono yako utoe pesa nyingi sana. Na hizo pesa zote unazotumia kwa ujumla wanaita “Gharama za maisha”. Hii inamaana maisha yana “Gharama”.

Mbinu za kutimiza malengo yako ya Mwaka BONYEZA HAPA>>>

Gharama za maisha na kiasi cha pesa unachoingiza

Gharama za maisha yako zikiwa ni kubwa kuliko kiasi cha pesa unachoingiza, unawezakuwa ni mtu unaeshika pesa lakini huzioni na unaangukia kwenye madeni. Yani unakua ni mtu unaetumia pesa nyingi kuliko unazoingiza.

Kujitoa kwenye hali hiyo unatakiwa kwanza kumuomba mungu akusaidie badala ya kukimbilia kwenye vitu kama pombe ili kumpunguza Mawazo.


Hatua ya pili, unatakiwa kutulia na kuiweka akili yako kwenye matumizi yako ili kuelewa kiasi gani unatumia kwa siku, mwezi na hata mwaka. Hapa utatakiwa kujua pesa kiasi gani unatakiwa kuwa nayo kwa mwezi ili uwe na mahitaji muhumu yote(Kodi, chakula n.k). Na pia unatakiwa kujua pesa kiasi gani huwa zinatoka mikononi mwako na kwenda kwenye vitu visivyo vya muhimu. Kiufupi unatakiwa kuzingatia pesa zinatokaje mikononi mwako.

Baada kujua pesa zinatokaje mikononi mwako, utatakiwa kuanza kuzizuia baadhi ya pesa zinazokwenda kwenye mambo yasio ya muhimu. Ni ngumu sana maana pesa nyingine unaweza gundua zinatoka mikononi mwako ili kuifurahisha Roho na imekua ni kama Tabia tayari kufanya hivyo. Lakini pambana sana kuzuia kwa kubadilisha tabia na kuepuka utoaji wa pesa usio wa muhimu sana.

Wakati ukiendelea kupambana kuzuia pesa zisitoke mikononi mwako kizembe, unaweza kuwa na hasira sana kuhusu pesa maana utakua unaona baadhi ya pesa zinaendelea kutoka mikononi mwako bila umuhimu na unashindwa kuzizuia. Lakini usikate tamaa maana jambo hili litakukumbusha kujiuliza “Nitarudisha vipi pesa zilizotoka mikononi mwangu bila umuhimu?”, Pia utajiuliza “Nifanye nini ili hizi pesa zinazokuja zisiwe zinatoka mikononi mwangu?”.

Unarudisha vipi pesa zilizotoka mikononi mwako?

Ni ngumu kurudisha pesa zinazotoka mikononi mwako ila unaweza anza kuzingatia utengenezaji wa pesa nyingi nyingine zitakazokuja mikononi. Yani hapa naongelea kuongeza kipato chako.

Mfano: kama ni mfanya biashara, basi unatakiwa kufanya bashara yako ikuingizie pesa nyingi zaidi. Na njia rahisi ya kufungua ubongo wako kwenye upande wakuongeza kipato ni kujifunza toka kwenye vitabu au watu wengine wanaoingiza pesa zaidi. Au unaweza anza kujaribu vitu mbalimbali ili kuitanua biashara yako iweze kuingizia pesa zaidi.

Kiufupi ni unatakiwa kutafuta njia za kuongeza kipato au pesa zinazokuja mikononi mwako huku ukiendelea kuzuia matumizi yasio na maana. Na ukifanikiwa kuingiza pesa nyingi kuliko unazotumia, utakua ni kama umefanikiwa kuzirudisha pesa zinazotoka mikononi mwako huku ukipata na nyingine za juu kwaajili ya mambo mengine.

Nini cha kufanya ili pesa zisiwe zinatoka mikononi mwako?

Kufanikisha hilo unatakiwa uwe unaweka pesa yako kwenye sehemu isiopungua thamani yake au uwe unaiweka pesa yako kwenye sehemu inayofanya pesa yako izalishe pesa nyingine.

Kiufupi ni utanatakiwa uwe unatuza pesa yako kwa kuweka kwenye akaunti au michezo ya kutuziana pesa. Wengine huwa wananunua mpaka viwanja ili kuitunza pesa tu isishuke thamani. Na pia unaweza iweka pesa yako kwenye biashara inayozalisha pesa zaidi ya ulioiweka.

Katika safari ya kuelekea mafanikio. Usisahau kuwa mungu atakusaidia ukijituma, na pia karamu na daftari ni muhumu kuvitumia kwenye mahebu yako ya kimaisha.

Mbali na hayo; kujiweka katikati ya watu wanapenda mafanikio ni muhimu. Hakikisha unakua na watu wanaopenda mafanikio kwenye maisha na sio waliokata tamaa. Ukishindwa kabisa kupata watu, wafuate wanao hamasisha kujituma na mafanikio kwenye maisha waliopo mtandaoni. Kama wewe ni kijana wa kiume unapenda kutiwa hasira sana za kutoka ulipo, unaweza wafuata hata wakina Chiefgodlove au Chimakeke. Pamoja na mabaya yao, hiyo ni moja ya kazi yao.

Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy!

Kabla ya kumuacha Mpenzi kwa kukusaliti fikiria Mambo haya kwanza

Kila mtu anatamani kuwa na mpenzi mwaminifu na anayejali, kwani uaminifu ndio msingi wa mahusiano yenye furaha na utulivu. Si mwanaume wala mwanamke, wote wanapenda huwa na mahusiano na mtu asiewasaliti. Hisia za upendo na kuaminiana, hujenga mahusiano imara ambayo hutoa faraja na usalama wa moyo kwa wapenzi wote wawili. Hakuna anayependa kuwa na mashaka au wasiwasi kuhusu tabia za mwenzi wake, hasa linapokuja suala la kuwa na mpenzi mwingine. Hii ndio maana mwanzo wa mahusiano wapenzi husisitiza sana kutosalitiana kwa kuambiana maneno kama “Nitakupenda milele… Sina mwingine zaidi yako… Siwezi kukusaliti”.

Lakini wakati mwingine, hali ya kusalitiwa hujitokeza, na hii inaweza kuwa ngumu sana kwa aliesalitiwa kukubaliana nayo. Watu wengi hujawa na maumivu makubwa wanapogundua kwamba wamechezewa au kudanganywa na mtu alieshika furaha ya moyo wao. Hupata hisia zinazovunja moyo na kuumiza, na mara nyingi hisia hizi humfanya mtu kujiuliza kama anapaswa kuendelea na uhusiano huo au kuachana nao kabisa.

Uamuzi wa kumwacha mpenzi kwa sababu ya usaliti ni jambo zito maana ni kuharibu kabisa uhusiano uliokuwepo bila kujali mmetoka wapi. Ni muhimu kufikiria kwa makini kabla ya kuchukua hatua yoyote ili kuhakikisha kuwa unafanya uamuzi sahihi maana sio kila kusalitiwa kunatakiwa kuwa mwisho wa Mahusiano. Katika makala hii, tutaangazia mambo ya kujiuliza au kufikiria kabla ya kuchukua uamuzi wa mwisho.

Jinsi ya kujua kama mpenzi ulienae anakupotezea Muda tu BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kufikiria kabla ya kumuacha mpenzi kwa kukusaliti

Ni kweli?

Kuna mambo au matukio yanaweza kukufanya uamini kuwa mpenzi wako anakusaliti au amekusaliti lakini ikawa sio kweli. Ni ngumu kuamini kuwa mpenzi wako hajakusaliti wakati umeyaona mazingira ya kukusaliti. Watu wengine huwa Wanaamini kuwa wamesalitiwa hata kwa kuambiwa tu au kusikia maneno ya watu. Unachotakiwa kujua ni kwamba kuna wakati inaweza kuwa sio kweli.


Ni vema kabla ya kufanya uamuzi wa kumuacha kipenzi cha Roho yako, ukathibitisha ni kweli amekusaliti au hajakusaliti. Usije muacha mpenzi wako sahihi kwa vitu vya kuhisi au kusikia. Ukiona mambo yanakuchanganya, unaweza kukaa nae mukaongea kuhusu unachohisi au ulioyasikia kisha ukaangalia anayachukuliaje hayo mambo na yeye.

Chazo ni wewe, yeye au mtu mwingine?

Wengi likitokea jambo la kusalitiwa huwa tunaona mbaya ni aliesaliti lakini kuna wakati mtu mbaya unaweza kuwa ni wewe uliesalitiwa au akawa mtu mwingine tu mbali na nyie.
Ukiwa na uwezo au moyo mkubwa, unaweza jiuliza nini chanzo cha usaliti uliofanyiwa. Kuna watu wengi tu huwa wanasalitiana kwenye mahusiano lakini baadae wanagundua nini chanzo, wanarekebisha walipokosea alafu wanaendelea na mahusiano. Unaweza gundua kuwa wewe ndio umesababisha yeye kufanya hivyo au Kuna mtu mwingine ameamua kuwavuruga.


Jambo hili limejitokeza kwenye simulizi fupi iitwayo “SIRI NA SHEMEJI” na inaweza kuwa vizuri sana kama utafuatilia simulizi hii.

Bado anakupenda na anajutia kukusaliti?

Kuna watu wanasema “Usimwamini au kuendelea na mwanamke au mwanaume aliekusaliti”. Lakini kiukweli kwenye jamii zetu mambo ya kusalitiwa hutokea kwasababu mbalimbali na watu husameheana na kuendelea kujenga mahusiano yao kama hakuna kilichotokea.
Kabla ya kumuacha au kumsaheme mpenzi aliekusaliti ni vema ukajiuliza “Bado anakupenda?” na pia usisahau kujiuliza kuwa “Anajutia kukusaliti?”. Kama unaona kabisa mtu bado anakupenda sana na hataki kukupeteza kwenye maisha yake, kumsamehe unaweza kuwa uamuzi mzuri. Ila inabindi ujilidhishe kabisa ili usijejutia uamuzi wa kumsaheme.

Pia Jambo limejitokeza kwenye simu fupi iitwayo “SIRI NA SHEMEJI” na inaweza kuwa vizuri sana kama utafuatilia simu hii ili kuelewa zaidi.

Unaweza kusahau na kumpenda bila kujali?

Baada ya mpenzi wako kukusaliti, angalia moyo wako kama unaweza sahau yote na kuendelea kumpenda. Kama unaona kabisa hauwezi kumsamehe au kusahau alichofanya, ni vema ukamuacha tu maana ulionayo moyoni yanaweza pelekea kufanya jambo baya kwake kama kisasi.

Kwaiyo ni vema ukajipima kwanza kama unaweza sahau yote na kuendelea kupendana nae kama hakufanya kitu kibaya kwako. Yani kama umemsaheme, usije waza mabaya yake tena.

Hautakua wakwanza kufanya hivo, watu wengi hufanya kwa wapenzi wao, waume zao au mwake zao. Lakini ukiona hauwezi, jiweke mbali nae maana kuna siku moyo unaweza kukusukuma kumfanyia mabaya.

Ni hayo tu katika ukurasa huu wa The bestgalaxy, lakini kama ni mtu anaependa kuelewa zaidi, unaweza soma Simulizi ya “SIRI NA SHEMEJI” ili kuburudika huku ukiongeza uelewa kuhusu swala hili.

Jinsi ya kupata Visa au Mastercard kirahisi kwaajili ya malipo ya mtandaoni

Kufanya malipo mtandaoni ni moja ya mambo ambayo ni vema kila mtu anaetumia mitandao akafahamu. Hii ni kwasababu kwasasa kuna mambo mengi katika mtandao huwa yanahitaji mtu afanye malipo ili kuyapata. Malipo ya mtandaoni yanaturahisishia kufanya manunuzi ya bidhaa mtandaoni na hata kulipia huduma nyingine.

Njia za kulipia au kufanya malipo mtandaoni kwasasa zipo nyingi sana. Kuna njia nyingine huwa ni salama na njia nyingine sio salama. Lakini watu wengi wanahitaji njia salama na rahisi ya kufanya miamala hii, hasa wanapotaka kutumia njia za kimataifa za kufanya malipo mtandaoni. Hapa ndipo kadi za malipo za Visa na Mastercard zinapokuja kuwa msaada mkubwa kwa watumiaji wa mtandao.

Kadi za malipo Visa na Mastercard zinazoweza kutumika mtandaoni zina faida nyingi, ikiwemo usalama na urahisi wa kufanikisha miamala kutoka sehemu yoyote duniani. Hii ni muhimu sana kwa wale wanaopendelea kufanya manunuzi ya bidhaa na huduma tovuti tofauti za kimataifa mtandaoni. Kwa kutumia kadi hizi, unapata fursa ya kulipia mambo mengi sana mtandaoni. Kati ya vitu unaweza fanyia ni kulipia huduma za movies kama Netflix, unaweza nunua bidhaa katika masoko ya mtandaoni kama AliExpress au kupitia matangazo katika Facebook.

Kwaiyo kuna umuhimu wa kuwa na kadi ya malipo mtandaoni. Lakini si kila mtu anajua jinsi ya kupata kadi hizi kirahisi. Mara nyingi, watu hukutana na changamoto katika mchakato wa kupata kadi. Katika makala hii, tutakuongoza hatua kwa hatua njia rahisi ya kupata kadi ya malipo inayoweza tumika mtandaoni. Kujua hili kutakusaidia pindi utakapokua kwenye uhitaji wa jambo flani linalohitaji ufanye malipo mtandaoni kwa Visa au Mastercard.

Usitafute mambo haya mtandaoni utaibiwa BONYEZA HAPA>>>

Njia ya kupata Visa au Mastercard kirahisi kwaajili ya mtandaoni

Unapohitaji Visa au Mastercard ya haraka kwaajili ya malipo ya mtandaoni, fahamu kuwa unaweza ipata ndani ya dakika chache tu hapo ulipo. Unaweza tengeneza Visa au Mastercard (virtual cards) kwenye huduma ya mtandao wako wa Voda,Tigo na Airtel. Mitandao hii inakupa nafasi ya kutengeneza kadi ya malipo ya mtandaoni ndani katika chache tu.


Ukihitaji kutengeneza kadi kirahisi kwenye mtandao wako wa Simu unaotumia, pakua app ya Tigo Pesa, My Airtel au Mpesa. Baada ya hapo utatakiwa kujisajili kwanza na hiyo app alafu nenda katika kipengele cha kadi. Katika kipengele hicho utaweza kutengeneza kadi yako na hata kuifuta pindi utakapo maliza matumizi. Unaweza tengeneza kadi za kutumia muda mfupi na mrefu pia.

Hiki ni kipengele cha kadi katika app ya Tigo Pesa



Ila nashauriwa kuifunga kadi yako pindi unapomaliza matumizi ili kulinda pesa zisije katwa bila na huduma zako mbali bila lidhaa yako au kuibiwa waalifu.

Wanasema “Ukitaka Kufanikiwa, Kuwa Kama Tai” kwasababu hizi

Tai au Eagle ni ndege maarufu kwa uwezo wake kwenye mambo mbalimbali na amekua akiongelewa sana. Baadhi ya watu hutumia ndege huyu kama alama za kuonesha ujasiri, nguvu na ubora. Lakini pia kunawatu humtumia ndege huyu kama mfano katika Maisha na mafanikio.


Kutumia mfano wa tai kama alama ya mafanikio ni njia bora ya kuelewa mambo muhimu yanayoweza kutusaidia kufikia sehemu flani maishani. Ili kufanikiwa, Kuna muda ni kweli tunahitaji kuiga tabia na sifa fulani za tai ambazo ni zenye thamani na zinazoweza kutupeleka mbali. Kati ya sifa hizo ni hizi hapa chini.

Jinsi ya kulinda ndoto zako zisife maishani BONYEZA HAPA>>>

Sifa za kumuiga Tai ili kufanikiwa kwenye maisha

Kuwa na Maono na Mtazamo wa Mbali

Tai ana uwezo wa kuona mbali sana, hadi kilomita 5! Hii inampa nafasi ya kuona mlo wake au adui akiwa mbali. Ili kufanikiwa, ni muhimu kuwa na maono ya mbali na kutazama mambo kwa upana. Jiulize: unataka kufikia nini maishani, na ni vikwazo gani vinaweza kujitokeza? Kama tai, kila mara angalia mbali zaidi ya hali ya sasa, na ujipange kulingana na unachokiona mbele.

Kuanza upya

Kuna wakati Tai hutenga muda kujibadilisha kwa kung’oa manyoya yake ili kufanya manyoya mengine mapya yaote. Hii ni muhimu kwetu pia; wakati mwingine ni lazima tuondoe tabia, mahusiano, au mawazo ambayo yanatuzuia kusonga mbele. Wakati mwingine, uamuzi wa kuacha kile kinachoturudisha nyuma, ndicho kinachoweza kutupeleka mbali zaidi. Hivyo tunapaswa kuishi kwa mfano huu katika mambo yetu ya kila siku.

Kukabiliana na Changamoto

Tai huwinda nyoka kwa kuruka chini na kuwashika kwa makucha yao, kisha kuruka juu huku nyoka akihangaika. Kisha tai wanaweza kuponda au kung’oa kichwa cha nyoka huyo na kukimeza kizima wakiwa bado wanaruka.

Tai huenda juu kwasababu ndio sehemu ambayo anaijua vizuri lakini nyoka hawezi kuhimiri. Tunawezasema Tai huwa anampeleka nyoka sehemu ambayo anaijua vizuri na ile inaruhusu yeye kushinda vita kirahisi.

Hii katika maisha inatukumbusha kuwa bora katika upande wetu na kutumia tulichonacho kuzishinda changamoto zinazokuja bila kuogopa. Tumia ulichonacho kuwa unapohitaji kuwa, au nenda katika sehemu inayoruhusu kupata unachohitaji. Na pia ondoka sehemu inayosababisha ushindwe.

Kwahivyo, ukitaka kufanikiwa, kuwa kama tai: mtazamaji wa mbali, mwenye moyo usiotetereka, na mwepesi wa kubadilika.

Mambo ya kufanya Mpenzi akiwa hakupigii simu au kukutafuta

Simu imekuwa sehemu muhimu sana katika mahusiano ya siku hizi. Kupitia simu, wapenzi wanaweza kuwasiliana kwa urahisi, kubadilishana mawazo, na kueleza hisia zao bila kujali umbali uliopo kati yao. Kutopokea simu au kutokutafutwa na mpenzi wako kwa muda mrefu kunaweza kuleta wasiwasi, hasa katika mahusiano yenye mawasiliano ya mara kwa mara.

Kwa kuwa mazungumzo kupitia simu ni njia rahisi ya kutunza uhusiano, ni jambo la kawaida kwa mpenzi kujisikia vibaya au kutokuwa na amani mpenzi wake anapokaa muda mrefu bila kupiga simu. Kutozungumza kwa muda mrefu kunaweza fanya mtu kujihisi kutothaminiwa kwenye mahusiano yake ya mapenzi au kuhisi jambo jingine baya limeingia kwenye mahusiano.

“Kutokupigiwa simu na mpenzi” hali inayoweza kuwa na sababu nyingi na pia inaweza ikatokea kwa namna nyingi. Lakini badala ya kuwa na wasiwasi au kuchukia, kuna mambo kadhaa unaweza kufanya ili kuiweka sawa.
Ikiwa mpenzi wako hakupigii simu kwa namna yoyote na haujui nini Cha kufanya, hapa chini kuna jinsi tumeeleza mambo unayoweza kufanya.

Mambo ya kufanya mpenzi akiwa kakupigii simu au kukutafuta

Tengeneza tabia ya kumpigia sana wewe alafu ghafla uiache kwa muda

Unaweza kufanya Jambo hili kama mpenzi wako mpya anatabia ya kutokukupigia simu lakini ukimpigia, mnaongea vizuri tu na mahusiano yenu yametulia.
Utachotakiwa kufanya hapa ni kuzidisha kumjali na kumpigia simu za mara kwa mara alafu unaamua kutulia bila kumpigia ghafla. Jambo hili linaweza mfanya akupigie kujua ni nini tatizo maana sio kawaida yako.
Akikupigia kwa mara ya kwanza, inaweza kuwa ndio tabia yake ya kukupigia imeanzia hapo.

Maswali ya kumuuliza Mpenzi wako Mpya BONYEZA HAPA>>>

Kuwa na mambo mazuri ya kuongelea kwenye simu

Kuna watu muda huu, hawakupigii kwasababu hakuna jambo la kuongelea. Inaweza kuwa hivyo pia kwenye mahusiano. Mpenzi wako anaweza kuwa hakupigii simu mara kwa mara kwasababu mnakosa vitu vizuri vya kuongelea.
Kuna watu wengi tu huwa wanashindwa kuongea vizuri na wapenzi wao kwenye simu. Na baadhi ya wanaoongea, huwa hawaongei mambo mazuri ya kuvutia kiasi kwamba mpenzi awe anatamani kupiga simu na kuongea tena.

Kama unapitia jambo la kutopigiwa simu kwa namna hii, basi fanya kutengeneza uwezo wa kuongea na mpenzi wako kwenye simu mpaka awe anatamani kukupigia ili muongee.

Onana nae mzungumzie mahusiano yenu vizuri

Ikiwa hakupigii simu na hataki kuongea na wewe kwa namna yoyote ile kama mtu aliepandwa na hasira, basi hakikisha unamtafuta muonane ana kwa ana. Unaweza kumfuata mahari alipo na ukaongea nae kuhusu mahusiano yenu vizuri ili kujua nini tatizo. Kama utakua mbali nae, unaweza watumia ndungu au marafiki kumuuliza kuhusu tatizo linalomfanya asitake kuwasiliana na wewe.

La kumaliza ni kwamba, Kuna muda mtu anaweza kuwa hakupigii simu wala kupokea simu yako kwasababu ana matatizo yaliomkuta au yupo mazingira yasiomrusu. Hivyo uwe unafikilia upande huu pia kwa mwanamke au Mwanaume wako. Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy.