Katika kipindi hiki wanaume huongea sana kuhusu wanawake na mahusiano lakini hii haimaanishi swala la “Kutongoza” linawezwa na kila mtu. Swala hili bado ni gumu kwa vijana wengi na ugumu wake huwa unawapelekea kupata wanamke wanaojitokeza kirahisi tu, na sio wanaowataka au kuwapenda.
Kwa wasio jua vizuri ulimwengu huu, Makala hii ina hatua ambazo mwanaume unaweza fuata kumpata kila mwanamke unaemuhitaji.
Kuna umuhimu mkubwa wa kijana kujua namna ya kutongoza mwanamke anaemtaka. Huwa kunasaidia hata kupata mwanamke sahihi maishani maana mtu usipojua kuwakamana, itakua ngumu kupata mwanamke unaemuona ni sahihi.
Maswali ya kumuuliza mpenzi wako mpya BONYEZA HAPA>>>
Hatua za kumpata Mwanamke yoyote unaempenda 2026
1. Mchunguze ni mtu wa namna gani na anapenda nini
- Kabla ya kuwa na ukaribu na mwanamke unaemtaka, hakikisha unamchunguza kwanza. Hapa nazunguzia kuangalia yeye ni mtu wa namna gani na anapenda nini katika mahusiano au maisha yake kwa ujumla.
- Hatua hii itakusaidia kujua unaingia vipi kwenye maisha yake. Kama anapenda pesa sana na unataka kuingia kwa namna hiyo, basi utajua hapa. Kama unaweza kukuelewa bila pesa, unona kwenye hatua hii pia.
2. Tengeneza ukaribu kupitia unachokijua kwake
- Ukishajua mambo flani kuhusu yeye, inaweza kuwa ni rahisi sasa kuanzisha ukaribu nae. Unaweza anza ukaribu kwa kuongea nae kidogo kuhusu mambo ambayo ni mbali kabisa na mahusiano. Hii inaweza kuwa ni kuongea vitu kuhusu biashara anayoifanya, kumuomba msaada kwenye kitu flani anachokiweza au onyesha kumjalia na hata ukimtania tu kwenye vitu vitakavyo mfurahisha sio mbaya.
- Kiufupi unakua ni kama unaingia kwenye maisha yake kiasi cha kuanza kumzingatia na kuwasilinana kwenye simu kuhusu jambo flani au kuongea nae tu pale mnapokutana. Lakini wakati unajisogeza kwake kutengeneza ukaribu, hakikisha haujengi mazoea nae sana. Fanya kila kitu unachokifanya ili kuwa karibu nae lakini mazoea yawe kwa kiasi tu.
3. Angalia muitikio wake juu ya ukaribu wako
- Ukishaweka ukaribu nae, anza kuangalia muitikio wake juu ya ukaribu wako. Yani angalia kama anafurahia au amekubali kirahisi wewe kuwa karibu yake.
- Unaweza ona mambo haya kwenye namna anavyo jibu ujumbe wa simu, namna anavyokuzingatia mkikutana na hata jinsi anavyoongea na wewe.
- Kupitia muitikio wake juu yako, unaweza hata kuona dalili za mapema za kufanikiwa kwenye jambo lako.
4. Tafuta muda mzuri wa kumwambia kuwa unampenda na umwambie
- Baada ya kujiweka karibu na akaonesha muelekeo wa kutambua ukaribu wako kwake, basi ni muda wa kumwambia ukweli. Kupitia ukaribu mulionao, tafuta wakati mzuri ambao utaanzisha mazungumzo ya kueleza hisia zako. Hii inaweza kuwa kwenye simu au kwa kuonanae kabisa.
- Kama ni kwenye simu, unaweza anzisha mazungumzo yako muda ambao unajua atakua ametulia(mfano; usiku, muda wa kulala). Kama ni ana kwa ana, unaweza muita au kukutananae mahali ili kumwambia hisia zako.
Wakati kufanya hayo yote, zingatia heshima. Baadhi ya wanawake unaweza kuwakosa kwasababu tu umewavunjia heshima. Wanawake huwa wanajali na kuangalia vitu vidogo vidogo alafu wanakuweka kwenye makundi. Kwaiyo unaweza kuwa na kila ushawishi lakini ukatupwa mbali au kuchezewa akili kwasababu ya mambo madogo kama dharau.



