Wakati baadhi ya vijana Wakiume wanaongelea na hata kutafuta kabisa Majima au Mishangazi, hebu tunangalie athari zake. “Mishangazi” au “Majimama” ni majina ambayo kuna watu hutumia wakiwa na maana “Wanawake wakubwa wanaoingia kwenye mahusiano na vijana wadogo.” wanawake hawa wapo katika jamii zetu na kumekua na simulizi nyingi za vijana kujihusisha nao kimapenzi.
Mahusiano kati ya wanawake wakubwa na vijana yanaweza kuwa ni upendo toka moyoni kabisa. Yani wanaweza kuanza kwa mazoea ya kuwa karibu alafu mwisho, wakajikuta kwenye penzi zito. Ila kwakua wanasema, Mapenzi hayana umri, tunaweza sema ni jambo lisiloshangaza sana.
Lakini pia baadhi ya mahusiano ya namna hii huwa ni kama wanabadilishana pesa au maisha mzuri kwa mpenzi. Yani hapa Kijana wa kiume anawezakua anatoa mapenzi huku Mwanamke mkubwa akitoa pesa au maisha mzuri kwa Kijana. Kwaiyo Kuna namna Kijana wa kiume anaweza faidika hapa.
Pamoja na yote ambayo kijana wa kiume anaweza pata au kufaidika kwenye mahusiano ya namna hii, Bado sio Mahusiano salama. Kijana anaweza pata athari mbaya kubwa kwenye maisha yake anapokua na majimama au Mishangazi. Athari zinazo zungumziwa hapa ni zifuatazo:
Kijana hizi ni athari za Wanawake wakubwa sana (Majimama/Mishangazi)
Magonjwa
Kama tunavyo fahamu, magonjwa kama vile HIV huwa yanaweza ambukizwa kwa kushariki Ngono zembe. Ngono zembe ni kushiriki tendo la ndoa bila Kinga yoyote.
Kama upo kwenye mahusiano na mwanamke mkubwa, Tendo hili linaweza kuwa ni tendo la kawaida sana. Mnaweza zingatia kinga siku ya kwanza lakini ya pili mukazitupia mbali kwa kuamini haziwafurahishi kwenye tendo.
Sasa ikiwa mmeamua kutotumia Kinga Kuna hatari kubwa ya kuambukizana virusi ya ukimwi na magonjwa mengine.
Kuwachukulia poa wanawake wengine
Kijana wa kiume anapoingia kwenye mahusiano na mwanamke mkubwa anaweza jikuta anaanza kudharau mwanamke wa umri wake. Yani anaweza anza wachukulia poa sana mwanamke wa umri wake maana tayari anaoneshwa au kufanyiwa vitu vingi ambayo wanawake wengine hawafanyi.
Hali hii inaweza kumfanya huyo Kijana ajiamini sana anapokua na Mwanamke wengine. Lakini kujiamni huko ni matokeo ya kugundua kuwa mwanamke wengine hawajui mapenzi.
Kugeuka tegemezi
Kijana wa kiume akipata mwanamke mkubwa anaempa pesa kisa mapenzi, kuna hatari kubwa ya huyo Kijana kuwa tegemezi kwenye maisha yake. Anaweza fikia wakati hata akiachwa na jimama anaona maisha yake yameharibika.
Kwa kawaida mwanaume anatakiwa kubeba Majukumu, kujitegemea na kutegemewa. Huyo mwanaume akizoeshwa kutegemea mwanamke, inakua ni ngumu kwake kuchukua Majukumu, kujitegemea na kutegemewa tena. Huo kwake unakua ni mzigo mkubwa sana.
Kuingia kwenye migogoro
Baadhi ya wanawake wanaoitwa “Majimama” au “Mishangazi” ni wake za watu au Mama za watu. Kutokana na hili, pamoja na yote wanayofanya, Bado ni wanawake ambao wana ndungu na jamaa kwenye maisha yao.
Kijana anaweza ingia kwenye migogoro ya kifamilia bila kujua. Ukiwa kama kijana, unaweza kuwa chanzo cha mke na mume kukosana, unaweza chukiwa na watoto wake au ndungu. Mongogoro mingi inaweza kuibuka hapa.
