Zingatia haya ili usichokwe na Mpenzi wako

Kuchokwa na mpenzi wako ni mojawapo ya changamoto kubwa ambazo watu wengi hukutana nazo katika mahusiano ya kimapenzi. Wakati mwingine, bila hata kugundua nini sababu ya kuchokwa, mtu anajikuta tu amechokwa. Hili si jambo la kushangaza, kwani mahusiano yanahitaji juhudi, uelewa, na ubunifu ili yaendelee kuwa yenye afya nzuri kwa pande zote mbili(Upande wa Mwanamke na Mwanaume).

Ni kawaida kwa watu kupuuza umuhimu wa mambo madogo yanayochangia uimara wa mahusiano alafu mahusiano yanayumba. Muda mwengine, mambo hayo tukiyafanya kwa kuzidi, yanafanya watu wachokwe kwenye mahusiano.
Kwa bahati nzuri, kuna mambo muhimu ya kuzingatia ili kufanya usichokwe kirahisi kwenye mahusiano. Baadhi ya mambo hayo ni yafuatayo;

Ujumbe wa mapenzi kwa umpendae BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kuzingatia ili usichokwe na mpenzi wako

Kuwa chanzo cha furaha na Amani kwake

Hapa Duniani tukiwa binadamu huwa tunapenda sana kuwa kwenye nyakati za Amani na furaha. Mara nyingi huwa tunapenda na kuwakumbuka sana watu wanaotupa Amani na furaha maishani. Na ni ngumu sana kumchoka mtu anaekupa furaha na Amani maishani, hivyo kuwa mtu huyo kwake. Kuwa mtu ambae anajua kabisa akiwa na wewe anapata amani na furaha.
Hakikisha kunamuda ukiwa nae unaweka lawama, kesi na matatizo pembeni alafu mnafanya mazungumzo ya furaha na Amani.

Mfanye akukose kwa muda flani (Akumiss)


Ni sawa kwa na mpenzi wako pamoja kwa muda mrefu lakini isiwe ni kila mara. Kuna muda inabidi ujiweke mbali nae kidogo ili akukumbuke na kujua umuhimu wako. Wataalam huwa wanasema kitu ambacho huonekana au kupatikana kirahisi hupunguza thamani. Na kwenye mahusiano hii inawezatokea pia.

Kuna muda jiweke busy na mambo yako, usipatikane kirahisi mpaka akutafute. Hii isiwe ni ugomvi, fanya kama kumkumbusha umuhimu wako kidogo kwa kuwa mbali nae alafu jirudi tena kwake kama kawaida. Kwa lugha nyingine tunaweza sema mfanye “Akumiss” kidogo kwa muda alafu kuwa nae karibu tena. Ukiwa unafanya hivi inaweza kuwa ngumu kwa mpenzi wako kukuchoka.

Kuwa na tabia ya kumfanyia asivyotarajia

Kama upo kwenye mahusiano alafu mambo yote unayomfanyia mpenzi wako ni yanayojirudia au yamezoeleka, basi kuna siku unaweza chokwa.
Ni vema ukawa na tabia ya kufanya baadhi ya vitu bila yeye kutarajia.

Usitabilike kwenye baadhi ya mambo katika Tendo au katika Maisha ya kuishi nae kawaida.

Kutengeneza nae mambo yajayo(future)

Mahusiano ya mapenzi bila future, yanawezekana ila huwa yanafika sehemu mnachokana. Yani kama ni Tendo tu ndio huwakutanisha pamoja na mpenzi wako, basi tambua tu kuna siku unaweza chokwa au wewe mwenyewe ukamchoka mwenzako.


Mahusiano ya mapenzi ni pamoja na kuwa pamoja au kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kimaisha. Na ili usichokwe, ni vema ukawa na tabia ya kupanga mambo mtayofanya pamoja mbali na tendo. Mfano, naweza panga na mpenzi wako kwenda kwenye sharehe pamoja, kuishi nyumba moja, kununua kitu flani pamoja na hata kukutana tu mupige stori.

Ukizingatia hayo yote, unaweza fanya iwe kungumu kwa mpenzi wako mwanamke au mwanaume kukuchoka. Anaweza kuwa anatamani kila siku uzidi kwa nae kwenye maisha yake.

Leave a comment