Jinsi ya kutengeneza Pesa zaidi kwenye unachokifanya (Biashara au Huduma)

Tunafanya mambo mbalimbali ili kuingiza pesa kwenye maisha yetu. Karibu kila mtu ana Kazi, Biashara au Huduma ambayo humuwezesha kupata kipato cha kuendesha maisha yake. Kipato kinaweza kuwa kikubwa au kidogo lakini maisha huitaji pesa, hivyo watu hupambana sana katika vyanzo vya mapato yao ili kuishi. Katika kupambana huko, baadhi ya watu hupambana sio tu kupata mapato au pesa, bali kuongeza kiasi wanachopata. Na kupambana kupata kipato au pesa nyingi zaidi zaidi ya unachopata kwenye unachokifanya, sio jambo baya ila inaweza kuwa sio rahisi.

Ukitupa macho au kufanya utafiti katika biashara flani, utagundua watu hupata faida au kipato tofauti. Yani inaweza kuwa ni Huduma au Biashara moja lakini Baadhi ya Watu wakawa wanaoingiza pesa nyingi kuliko wengine. Hii ni hali ambayo ipo na itaendelea kuwepo maana waswalihi wanasema “Kila mtu na ridhiki yake”. Lakini kama hauridhika, kunauwezekano wa kupambana na kuongeza kiasi unachoingiza. Tumeona hii kwenye simulizi za watu mbalimbali wenye mafanikio makubwa ulimwenguni.

Kama ni mmoja ya watu wanaohitaji kutengeneza Pesa zaidi kwenye biashara au Huduma, hapa chini kuna mambo yanayoweza kusaidia kufanikisha hilo.

Ujuzi utakao kuwezesha kuingiza pesa mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Mambo ya kuzingatia ili kutengeneza Pesa zaidi kwenye unachokifanya (Biashara au Huduma)

Kujichanganya na waliofanikiwa.



Ukitaka kwa kama waliofanikiwa kwenye mambo yako, jaribu kujichanganga na watu waliofanikiwa kwenye mambo hayo. Watu wengi huwa wanajitenga na waliofanikiwa na kuanza kuwasema. Lakini wewe ili kufanikiwa kama wao, unatakiwa kuwa upande wao ili upate mitazamo kama yao. Kujichanga na walio fanikiwa kunaweza kukupatia mbinu mbalimbali za kufikia kwenye kipato unachohitaji. Mbali na mbinu, unaweza kupata hata fulsa toka kwao.

Utayari wa kujifunza na kubadilika.



Hiki kitu ni muhimu sana kwenye maisha ya mafanikio na kuongeza kipato. Ukiwa tayari kujifunza mambo na kubadilika, basi utakua na uwezo wa kujifunza mambo muhimu kwenye huduma au biashara yako. Alafu pia utakua na uwezo wa kuyafanyia kazi baadhi ya mambo ili kuongeza kipato.
Baadhi ya watu hauwana uwezo huo. Wanaweza ambiwa au kuona mbinu zote za kuongeza kipato lakini wasifanye chochote cha maana. Yani hufanya biashara au huduma kwa mazoea huku wakilalamika kuwa wanatamani kuongeza kipato. Na mbaya zaidi ni hawataki kubadilika.

Kuelewa Soko au wateja.


Chunguza mahitaji ya wateja na matatizo yao. Elewa tabia, wanachopenda, na uwezo wa kifedha wa wateja wako. Fikilia ni jinsi gani unaweza wasaidia kwenye mambo yao na ukapata pesa. Jaribu kutafuta pengo na litumie kama fursa kwenye kwenye biashara au huduma yako.


Usipoelewa vizuri unao wahudumia, utakua haujaielewa vizuri huduma yako pia. Na usipoielewa biashara au huduma yako, unaweza usipate hata faida ya unachofanya.

Kutambulisha kwa watu (Itangaze)



Ukiwa na Biashara au Huduma ambayo haitambuliki na wengi, inawezakua ni ngumu kupata watu wengi wanataokufanya upate hata faida. Lakini ikiwa inatambulika na unaitangaza, watu wataona unachofanya na kujihusisha nacho.

Hii itakusaidia kupata faida kuwa kwenye kitu unachofanya. Kwa sasa mtu unaweza tumia hata mitandao ya kijamii (kama Instagram, Facebook na TikTok) kutangaza bidhaa/huduma.

Jinsi ya kutangaza biashara yako Mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Leave a comment