Kurudiana na mpenzi wako wa zamani inaweza kuwa hatua kubwa inayohitaji fikra za kina na maandalizi mazuri. Watu wengi hupitia hali ya kutaka kurudiana baada ya uhusiano kuvunjika. Lakini sio jambo la kukurupuka tu; kuna masuala mengi ya kuzingatia kabla ya kuchukua hatua yoyote.
Katika makala hii, tutajadili hatua muhimu unazoweza kufuata ili kurudiana na mpenzi wako wa zamani kwa njia yenye mafanikio. Kila hatua imeundwa kukusaidia kufikiria kwa kina na kuimarisha uhusiano wenu unapofanikiwa kuurudisha kwenye uhai. Lengo ni kuhakikisha kuwa kurudiana kwenu kunaleta furaha na uimara badala ya maumivu ya zamani. Endelea kusoma ili uione njia bora ya kurudisha mahusiano kwenye hali nzuri.
Mambo ya kufanya kwa Mpenzi asieonesha kukupenda BONYEZA HAPA>>>
Jinsi ya kurudiana na mpenzi wako wa zamani
Fikilia maamuzi yako kabla ya hatua
Kwanza kabisa; Fikilia maamuzi unayotaka kufanya kama ni sahihi au si sahihi. Na tena ufikilie kuwa kama maamuzi ni sahihi kwasasa ila yataonekana kawa mabaya baadae, hautajilaumu sana.
Kwenye mapenzi, kuna baadhi ya watu huachana na mtu alafu hupata mtu alie sahihi, na pia kuna watu hurudiana na mtu alie sahihi. Sasa unahisi utakua ni yupi kati ya hawa watu? Hebu fikilia vizuri kwanza maamuzi yako.
Angalia kama kuna upendo kati yenu
Upendo ni kitu kigumu kukificha kikiwepo kati yenu hatakama mumeachana. Na kama mumeachana ila kuna upendo kati yenu, kunakua na uwezekano wa kurudiana. Kwaiyo kama unataka kurudiana na mpenzi wako, angalia kwanza kama kuna upendo kati yenu.
Unaweza utambua upendo kirahisi kwa kujaribu kuwa karibu nae. Angalia kama anawivu na wewe, angalia kama anakuwekea milango ya mumuingia, angalia kama uwepo wako karibu nae anautambua au kuukupenda kabisa.
Mfano mzuri; kwenye simu unaweza kuta alikublock lakini baada ya muda kaondoa block. Au kama sio kwenye simu basi anaweza hata kuwa mara nyingi anakuja katika sehemu unazoweza kumuona kirahisi na kuanza kuongea nae.
Jenga uaminifu upya
Kama mlitengana kwasababu iliopelekea asikuamini, basi unatakiwa kufanya kazi kubwa sana ya kujenga uaminifu. Mfano; Ikiwa ulimsaliti ndio mkaachana, utakua na kazi ya kumfanya aamini kuwa unajutia kosa lako, hautamsaliti tena na hauhitaji kumpoteza kwenye maisha yako. Tena kwa vitendo zaidi na sio maneno tu.
Kujenga uaminifu kunaweza kuchukua muda sana ila hakikisha unazingatia sana swala hilo maana asipokuamini, kunakua na uwezekano mkubwa wa kuvutiwa na wengine anaohisi wanamapenzi ya dhati kulio wewe. Hii ni kwasababu kosa lako limekua kama ishara ya kuwa hauna mapenzi ya dhati kwake.
Anzisha mahusiano ya mapenzi rasimi kwa uangalifu
Mwisho, fanya kuanzisha mahusiano ya mapenzi rasimi. Unaweza anza kufanya hivi kwa kumwambia bado unampenda na kuomba nafasi ya kuwa nae. Akikubari, utakua tayari umeingia nae kwenye mahusiano. Lakini usiishie kujiachia tu, jaribu kuwa muangalifu kwenye mambo mbalimbali kati yenu. Zingatia kuendelea kujenga uaminifu na kufanya mahusiano yenu yawe imara zaidi.
Wakati ukifanya yote hayo, epuka kulazimisha mpenzi au mtu ulieachananae kurudiana tena. Yani ukiona dalili za yeye kutotaka murudiane kivyovyote, acha kumfuatilia kabisa maana hata baada ya kurudiana unaweza kuteswa kihisa.