Jinsi ya kuondoa Lag unapocheza game la Warzone Mobile

Warzone Mobile ni game lililolalamikiwa sana na wachezaji wake wingi toka siku ya kwanza linatolewa rasimi. Wachezaji wake wamekua wakikumbana na changamoto nyingi sana na kupitia mitandao wamekua wakieleza matatizo yanayowakatua. Watengenezaji(Developers) wa game wamekua wakijaribu kutatua baadhi ya matatizo lakini kuna baadhi ya matatizo yanaweza kutatuliwa na wachezaji wenyewe tu. Moja ya matatizo yanayoweza tatutuliwa na mchezaji wa game mwenyewe ni hili la “Lag”.

Lag katika upande wa game, tunaweza sema ni uchelewaji au kusitasita kwa game wakati wa unacheza. Mara nyingi tatizo hili huonekana sana likiwa kwenye game za Online (zinazotumika internet) lakini hata game za Offline hukubwa na tatizo hili.
Haijalishi Lag zipo kwenye game la Offline au Online, huwa zinakera na kumuondoa mchezaji katika hali ya kufurahia kucheza game.

Katika Warzone Mobile unaweza kumbana na Lag mara nyingi sana usipozingatia baadhi ya mambo. Ikiwa unapata Lag unapolicheza unatakiwa kuzingatia mambo ya fuatayo ili kufurahia game lako bila tatizo hilo.

Magemu yenye muonekano mzuri ya battle Royale BONYEZA HAPA>>>

Zingatia haya kuondoa Lag unapocheza game la Warzone Mobile

Tumia kifaa au simu yenye uwezo mkubwa


Kuna vigezo rasmi vinavyoeleza ni kifaa au simu gani inauwezo wa kutumika kucheza game la Warzone Mobile. Lakini hii haina maana kila simu au kifaa kilicho kidhi vigezo kitaweza kucheza game hilo vizuri. Baadhi ya vifaa vinaweza tumika kucheza lakini katika kucheza, unakutana na tatizo la Lag. Hii inawezatokea kwasababu simu au kifaa hicho hakina uwezo ila sio wa kutosha kucheza bila matatizo. Kwaiyo unatakiwa kupata kifaa kizuri kwaajili Warzone Mobile hatakufanya utafiti kabla haujanunua.

Jiunge na internet nzuri yenye kasi


Warzone Mobile ni game la online. Hivyo unapolicheza, jambo la misngi kulizingatia ni mtandao/internet. Ukiwa unacheza game hili katika mtandao usio na kasi au ambao haujatulia, itakua ni ngumu kuondokana na Lag. Kwaiyo hakikisha unatumia internet ilio vizuri ili kufurahia game bila Lag.

Punguza ubora wa picha ikiwezekana

Wakati mwingine Lag hutokana na ubora wa hali ya juu wa picha unaosababisha kifaa chako kushindwa kuchakata vizuri. Unashauriwa unapokua unakumbana na Lag, upunguze ubora wa picha wa game lako katika kipengele cha “Graphics” kwenye “Settings”. Kufanya a hivyo kunaweza ondoa Lag katika uchezaji wako wa game.

Usicheza kifaa au simu ikiwa ya moto

Simu au kifaa unachotumia kucheza game, kinaweza kuwa kina pata moto unapocheza. Hali hii ya kifaa hicho kupata moto, inaweza pelekea game kuwa na Lag unapocheza.

Kwaiyo unapogundua simu yako ni yamoto na game lako lina Lag, basi huo ni muda wa kuliacha game hilo ili kifaa chako kupunguze joto.

Mwisho; Kuzima Voice chat ni kitu kidogo ambacho kinaweza kukupunguzia Lag lakini kwa kiasi kidogo sana. Pamoja na mambo yote hayo, Game la Warzone Mobile huwa linakua na matatizo yanayojitokeza mara kwenye updates zake. Hivyo kuna muda Lag zinaweza kutokea na tatizo likawa nje ya uwezo wako.

Leave a comment