Sababu zinapelekea mtu kutodumu kwenye mahusiano

Kunazisha mahusiano ya mapenzi na mtu, kunaweza kuwa ndio safari ya kuishi mukiwa pamoja mpaka mwisho wenu. Lakini Safari hiyo, watu wengi hutengana na kuivuruga kabisa. Yani kwasasa sio kila mahusiano yanayoanza yanafika mbali, wengi huanzisha mahusiano ambayo hayadumu. Na asilimia kubwa ya mahusiano ambayo hayadumu ni mahusiano yanayohusha watu wenye umri wa 19-29. Watu wanaweza kuingia hata kwenye ndoa lakini Bado wasidumu.

Kwaiyo tatizo la kutodumu kwenye mahusiano ni jambo linalowagusa watu wengi sana. Hapa Duniani kuna wanawake na Wanaume wengi kwasasa wanajiuliza “Kwanini sidumu kwenye mahusiano” bila kupata majibu. Hivyo, ukiwa ni mmoja wa watu woanojiuliza kuhusu hili, basi tambua haukopekeako katika ulimwengu, kuna watu wengi sana.

Mahusiano yako yanaweza kuwa hayadumu kwasababu flani lakini ni gumu moja kwa moja kusema sababu hiyo. Ni ngumu maana kuna sababu nyingi zinazopeleake mtu kutodumu kwenye mahusiano. Hapa chini tumejaribu kuzungumzia sababu chache ili kusaidia mtu yoyote anaepitia tatizo hili kwasababu hizo. Kujua haya kunaweza kukusaidia katika Mahusiano utayopata au ulionayo.

Jinsi ya kupata Mpenzi mtandaoni BONYEZA HAPA>>>

Sababu zinapelekea mtu kutodumu kwenye Mahusiano

Woga wa kuumizwa

Kuna watu waliweka moyo katika Mahusiano ambayo yaliwaumiza sana. Na kama tunavyojua, Ukimpenda mtu sana au ukizama kwenye mahusiano nae sana, basi hata kuumizwa utaumizwa sana. Jambo hili likitokea kwa mtu, linaweza mfanya asidumu kwenye mahusiano mengine mapya tena kwasababu anakua anaogopa kuumizwa. Anaweza jitahidi kupenda lakini akikumbua maumivu au akiona dalili za kuumizwa, anajikuta anajiweka mbali na mahusiano.

Ikiwa unaona unashindwa kudumu kwenye mahusiano kwasababu hii, basi unatakiwa kujipa nafasi ya kupenda tena. Amini kuwa yaliopota yalikuumiza kwakua haukua na mtu sahihi tu kisha mpende anaekupenda. Tengeneza nae malengo bila woga maana woga utakufanya upoteze hata mtu sahihi kwako.

Matarajio makubwa

Asilimia kubwa ya watu (hasa vijana) huwa na matarajio makubwa juu ya wapenzi wao. Baada ya kuona wanachotajia hakipo, wanaona kama hawapendwi au hawana bahati ya kupata mahusiano wanayohitaji. Yani unaweza kuta mwanaume au mwanamke anatamani apate mpenzi mwenyewe maisha kama ya kwenye TV au mambo anayowaza yeye tu kichwani mwake. Akikutana na mtu anaehisi anafanana na huyo anaemuhitaji, basi anategemea kwenye mahusiano au kwenye maisha halisia atakua hivyo hivyo, jambo ambalo ni gumu kutokea.


Mambo mengi unayotarajia kuyapata kwa mpenzi wako au mahusiano yako, unaweza kuyakosa au ukayapa alafu baada ya muda yakapotea. Hivyo, ni vema ukapunguza mambo unayotarajia kwenye mahusiano au kwa mtu unaeingia nae kwenye mahusiano ili udumu nae. Usitege mpenzi wako atakua sahihi Kila wakati, atakua na hela kila wakati, atakua anakuzingatia sana wewe tu kila wakati au kufanya mambo mengine kama hayo.

Kutokutana na mtu sahihi

Wakati mwingine unaweza pitia kwenye hali ya Kila mahusiano kuvunjika na tatizo lisiwe kwako moja kwamoja. Tatizo linaweza kwa ni bado haujakutana na mtu sahihi atakae weza kuunda muhusiano na wewe yasiovunjiaka. Sio Kila mahusiano yanayovunjiaka yanavunjia kwa bahati mbaya, mengine huwa ya Bahati nzuri inayokupeleka kwa mtu atakae kupenda na kukuthamini.
Ili upate mtu sahihi, ni vema ukawa mtu sahihi pia. Kuwa mtu ulietayati kwa mahusiano yasiovunjiaka ili ukikutana na mwanaume au mwanamke atakaekupenda kwa dhati, ujione anabahati kukutana kukupata wewe.

Kukosa uvumilivu

Ukiwafuta wazee waliofanikiwa kuishi wakiwa pamoja kama mke na mume, na kuwaliza Siri ya kudumu wakiwa pamoja, watakuambia mengi ikiwemo “Uvumilivu”.
Ni ngumu kudumu kwenye mahusiano na binadamu mwenzio bila kuwa mvumilivu. Hii ni kwasababu kuna mambo mengi hutokea kwenye mahusiano ili kuharibu mahusiano na hakuna njia ya kuyashinda zaidi ya kuvumilia.

Tabia yako

Tabia yako inaweza kuwa chanzo cha mahusiano yako ya mapenzi kutodumu. Kuna tabia ambazo unaweza kuwa nazo na hauzizingatii lakini ndio hufanya mahusiano yako kuvunjika. Mambo kama Kiburi, dharau, uchafu, uvivu, kutoaminika, kuwa na wapenzi wengi au mambo mengine kama hayo.

Kama ni mpenzi wa simulizi, unaweza fuatilia simulizi ya UTAMU WA JUMLA ili kupata mwanga kwenye tabia zinavyoweza haribu mahusiano. Kwenye sehemu ndogo simulizi hiyo, kuna mtu alikua hadumu kwenye mahusiano kwasababu ya tabia yake.

Ni hayo tu katika ukurasa huu, Endelea kuwa karibu na The bestgalaxy

Leave a comment