Play Store inakataa kuingiza app na games kwenye simu (Can’t install)

Kama ni mtumiaji wa simu za Android na huwa unatumia Playstore kuingiza games au apps nyingie kwenye simu yako, kuna muda unaweza kumbana na matatizo katika kutumia playstore. Na moja ya matatizo unayoweza kukumbana nanaoyo ni hili la kushindwa kudownload au kupakua vitu na kuingiza kwenye simu.

Unaweza ukawa unatafuta app unayoitaka kwenye Playstore, unabonyeza kitufe cha “Install” ili kuipakua lakini badala ya kuanza kuingia kwenye simu, play store inazunguka kwa muda mrefu na app haiingi kwenye simu. Na ukiisubiri wa muda mrefu zaidi inakuja na ujumbe wenye neno “Can’t install”. Ikiwa unakumbana na tatizo hili, fuata maelezo hapa chini kutatua tatizo hili.

AI za kutengeneza Video kwa picha tu BONUS>>>

Jinsi ya kutatua tatizo la “Play store kukataa ku download app na games kwenye simu”

Unapopata tatizo hili kitu cha kwanza kufanya ni kuangalia kama Storage ya simu yako imebaki kidogo au ipo ya kutosha. Simu ikiwa imebakiza nafasi ndogo ya kuifadhi vitu, unaweza kumbana na tatizo hili. Hivyo utatakiwa kuwa na nafasi ya kutosha ili kuingia app au game unalohitaji.


Ukiona nafasi ya kuifadhi vitu ipo sawa, angalia kama muunganiko wa internet upo vizuri kwenye simu yako maana internet ikiwa inasumbua tatizo hili linaweza kukukumba pia.

Kama vyote viko sawa na bado tatizo linaendelea, Jaribu kuclear/kufuta data za app ya playstore kwa kufuata hatua zifuatazo:

  • Nenda kwenye orodha ya app za kwenye simu yako na utafute app ya Play store.
  • baada ya hapo, ishikilie app hiyo kwa sekude chache alafu kunachaguzi zitatokea.
  • kwenye hizo chaguzi zilizo tokea, chagua sehemu ilio andikwa “Application details” lakini inaweza kuwa imeandikwa “Application info” au “App info”.
  • Baada ya kufanya hvyo, utapelekwa kwenye ukurasa ambao utatakiwa kutafuta sehemu palipo andikwa “Storage” na kupabonyeza.
  • Ukisha fanya hivyo, utapelekwa kwenye ukurasa mwengine na kwenye kurasa huo, utatakiwa kubonyeza sehemu walipoandika “Clear Data” na kuchagua “Ok” kwenye swali utakalo ulizwa na simu yako baada ya kufanya hivyo. (Sehemu hiyo inaweza kuandika “Clear Storage” pia)

Baada ya kufanya hayo, utakua tayari umefuta data za playstore na utatakiwa kwenda playstore yako na kuanza kuitumia kama mwanzo… Itakua ipo vizuri na haina tatizo tena.

Ikiwa umefanya yote yaliopo hapa na haujafanikiwa, huenda kunaweza kuwa na tatizo katika app unayotaka kuingia kwenye simu. Baadhi ya app huwa zina matatizo yalionje ya uwezo wako. Ila unaweza njia mbadala ya ingiza app unayohitaji ikiwa kama Apk file.

Leave a comment